Kwamfano uchawi unapotumwa kwa mtu ambaye ni MZAO WA YESU KRISTO, labda tuseme ni ugonjwa fulani..na unakuta yule mtu wa Mungu hana habari yoyote, sasa kwasababu yeye ni mzao wa Mungu, Mungu hataruhusu ule ugonjwa umpate, atamkingia pasipo hata yeye kujijua kama katumiwa ugonjwa, Au hata kama Mungu akiruhusu ule ugonjwa umfikie, lile Neno la Mungu lipo ndani yake lile Neno linalosema Mathayo 8: “.. Mwenyewe [Yesu Kristo] aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.” ….
Basi atalitumia hilo Neno na kuanzia huo wakati anakuwa na amani akijua kuwa kwanza yeye ni mzao wa Mungu, na hakuna kilichopo juu yake,…Hivyo kule kuzimu wakitazama juu na kuona imani ya yule mtu imesimama, watajaribu kutupa ugonjwa tena na tena na wataona hakuna mafanikio hivyo wataacha kushughulika naye, na baadaye yule mtu anarudia katika hali yake ya kawaida.