KUMBUKUMBU LA DHAMBI.

KUMBUKUMBU LA DHAMBI.

Wakolosai 3:12 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13 mkichukuliana, na KUSAMEHEANA, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi”.

Kwanini tunapaswa tuwasamehe wale waliotukosea?…Ni kwasababu na sisi kila siku tunahitaji rehema na msamaha kutoka kwa Mungu wetu..Wengi hatujui nguvu iliyopo katika msamaha…Biblia inasema “achilieni nanyi mtaachiliwa (Luka 6:37)”…Maana yake tusipowaachilia watu na sisi pia hatutaachiliwa…

Na msamaha sio wa masaa machache au siku chache…bali ni wa milele…mtu akikukosea huda budi kumsamehe moja kwa moja…maana yake haitatokea siku ukamwekea kinyongo tena..lakini endapo umemsamehe leo na ikapita mwezi ukayakumbuka makosa yake na kuanza kuyatia tena moyoni…Biblia inasema hapo na wewe dhambi zako ulizozitenda huko nyuma zitakumbukwa na Mungu.

Kwamfano ulishaomba rehema na kutubia wizi ulioufanya huko nyuma kabla hujampa Yesu maisha yako…au kuna siku ulimrusha mtu kiasi Fulani cha pesa, au kuna siku ulimwibia boss wako pesa, au kuna kipindi ulimchomolea mtu simu n.k Na siku moja ukakutana na injili na ukatubu na kulia..na kuacha wizi…na ukaishi hivyo kwa zaidi ya miaka 10 bila kuiba tena…Lakini siku moja ikatokea mtu kakuchomolea simu yako, ambayo ndio hiyo tu ulikuwa nayo na uliinunua kwa gharama…ikakusababishia mpaka ukapoteza mambo yako ya muhimu sana uliyokuwa umeyahifadhi katika simu ile…na moyoni ukaudhika sana, na baadaye ukamgundua yule mtu aliyekuibia, ukamwekea kinyongo moyoni pasipo hata kumwambia..

Sasa katika hali kama hiyo…kama usipomsamehe Yule mtu, ukaendelea kumchukia vile vile moyoni mwako…hata kama huibi sasa, hata kama bado unaendelea kusali na kufanya mambo mengine ya Imani…Tayari Mungu anakuona wewe nawe ni mwizi…ule wizi wote uliokuwa unaiba kule nyuma unakumbukwa wote, kama vile umeufanya jana tu!!…Haijalishi imepita miaka mingapi hujaiba…Mbele zake unarudishwa na kuonekana kama umeufanya masaa machache tu nyuma…na hivyo hata ikitokea umekufa utaenda kuulizwa kwanini uliiba ile simu, kwanini ulimwibia Yule boss wako, kwanini ulimtapeli Yule mtu n.k n.K.

Hebu soma habari hii kwa makini na utaratibu…

Mathayo 18:21 “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake”.

Ndugu achana na biashara za kupambana pambana na maadui zako, jifunze kusamehe ndivyo na wewe utakavyosamehewa na Mungu Baba…Aliyekufundisha kwamba mlaani anayekukosea…huoni kwamba anataka na wewe ulaaniwe na Mungu?…anayekuzuia kusamehe huoni kama anakutakia mabaya?..huoni anakufungulia mlango wa kwenda jehanamu ya moto??…hebu soma tena mstari wa 35 hapo juu….na wewe binafsi unapojizuia kuwasamehe wanaokukosea hata baada ya kuelewa haya..huoni unajishitaki mwenyewe na kumkumbusha Mungu dhambi zako?.

Bwana atujalie kuyaelewa hayo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments