MIGUU ILIYO MYEPESI KUKIMBILIA MAOVU, NI CHUKIO KWA BWANA.

MIGUU ILIYO MYEPESI KUKIMBILIA MAOVU, NI CHUKIO KWA BWANA.

Zipo dhambi za maandalizi, na zipo dhambi zisizo na maandalizi..

Hizi dhambi za maandalizi ni rahisi sana kuzishinda, kwasababu sio za kushtukiza kwani huwa zinaanzia mbali na hivyo mtu ni rahisi kuziona na kuzikwepa, na akizifanya mbele za Mungu adhabu yake inakuwa ni kubwa kuliko zile ambazo zinakuja bila maandalizi,

Mfano wa dhambi zisizo na maandalizi, ni kama vile hasira, hofu, mawazo mabaya, na mara chache sana kuzungumza maneno yasiyofaa..

Lakini Mfano wa dhambi zenye maandalizi, ni kama vile Uzinzi/Uasherati wa aina yoyote ile ikiwepo punyeto, ushoga, usagaji, ulevi, utoaji mimba, utapeli, wizi, n.k.

Hizi ni dhambi ambazo mtu hawezi kuzifanya bila kuwa na maandalizi Fulani, au kupitia hatua Fulani(process). Huwezi kusema nimepitiwa kufanya uzinzi wakati kitendo chenyewe kabla ya kufanya mlikutana mahali Fulani, mkakubaliana, na kabla hujafanya kile kitendo ndani yako kabisa kulikuwa na kipenga chekundu kinalia kikikuambia kuwa hicho kitendo unachokwenda kukifanya sio sawa ni dhambi, lakini wewe unakwenda tu, bila kujali..na mwisho wa siku unakifanya..vile vile na wizi,..n.k.

Fahamu kuwa mbele za Mungu dhambi kama hizo usidhani gharama zake ni ndogo kuziondoa.. kamwe usije ukasema ah, si nitatubu tu?..Fahamu kuwa Toba sio tiba ya dhambi, kama vile Panadol kwamba ukiumwa kichwa unakwenda kumeza kisha unapona, kesho tena ukiumwa unakwenda kumeza nyingine..

Ukadhani pia katika kila aina ya dhambi ya namna hii dawa ni kutubu tubu. Ujue kuwa Zipo dhambi biblia imeziita dhambi za Mauti..Hizi ukitenda na huku unajua hupaswi kuzifanya, hakuna msamaha, ndio unaweza ukasemehewa baada ya kutubu kwa muda mrefu sana lakini adhabu ya kifo bado itabakia pale pale..

(Kwa urefu wa somo hili la dhambi ya mauti,  utalipata chini kabisa mwisho wa somo hili),

Dhambi hii Hata ulieje, hata utubuje, adhabu ya kifo haiondoki..kwasababu uliitenda kwa makusudi,

Inawezekana wewe nawe leo ni mmojawapo wa walio mbioni kukimbilia kutenda maovu hayo..Embu geuka ujiepusha na hatari hiyo iliyopo mbele yako…Na wewe mwingine ambaye umekuwa ukiishi katika kutenda dhambi kama hizo za makusudi ukidhania kuwa utatubu tu, na kwamba neema itakuwepo kila siku kukuokoa..Embu futa mawazo hayo na kwa moyo mmoja leo hii umgeukie muumba wako, utubu leo dhambi zako kwa kumaanisha nawe pia Mungu atakusikia..

Kumbuku miguu ikimbiliayo maovu na machukizo kwake Bwana, ni moja ya mambo sita yanayomuudhi Bwana (Mithali 6:18).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

DHAMBI YA MAUTI

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

MADHABAHU NI NINI?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

MAOMBI YA VITA

KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Buberwa Kitengule
Emmanuel Buberwa Kitengule
2 years ago

Barikiwa sana,masomo yenu kwani yamefungua ufahamu wangu kwa kiasi kikubwa.Naamini mafundisho haya yakiwafikia wengi nao pia yatakuwa msaada kwao.Kwa mfano mpaka sasa nimeelewa kuhusu ubatizo na ninatafuta ni wapi nikabatizwe kwa jina la la Yesu naamini Mungu ataniongoza manake ndio shauku yangu.