Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.
Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.
Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.
Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….
Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.
Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi kumwona Baba (Yohana 14:6).
Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.
Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.
Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.
Lifananishe kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Swali: Tunajua watoto wachanga hawana dhambi sasa kwanini ile gharika ya Nuhu ilizomba mpaka vichnga?..kwanini Mungu aangamize mpaka watoto wasio na hatia?..napata utata na gharika ile ya Nuhu, na kwenye ile miji ya Sodoma na Gomora je na watoto nao walifanya dhambi ya kustahili kuchomwa na kugharikishwa vile?
Jibu: Ni kweli Biblia inaonyesha ile gharika iliua wote wenye roho ya uhai puani, ikiwemo watoto wachanga na wanyama… na waliosalia ni watu nane tu! Kati ya Dunia iliyokuwa imejaa mabilioni ya watu.
Mwanzo 7:22 “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu”
Sasa kwanini Mungu aangamize hadi watoto wadogo, na ilihali tunajua kuwa watoto hawana dhambi.
Jibu la swali hili ni kwamba, “mtu anaweza kubeba adhabu ya dhambi ya mwingine lakini asibebe ile dhambi” ili tuelewe vizuri tutafakari huu mfano.. “Mama mjamzito kafanya kosa likamsababishia kifo, ni wazi kuwa na mtoto aliyeko tumboni naye atakufa” kwahiyo adhabu wameshiriki wawili lakini aliyefanya kosa ni mmoja.
Ni hivyo hivyo kipindi cha gharika na kipindi cha Sodoma na Gomora, Watoto walibeba adhabu za wazazi wao ingawa si dhambi!..(wao hawakufanya dhambi yoyote), lakini kutokana na maasi kuwa mengi ikawasababisha nao kushirikishwa katika adhabu hiyo, lakini hiyo haimaanishi kuwa hawataokolewa siku ya mwisho.. huwenda watakaokolewa katika ufufuo wa mwisho kwasababu Mungu ni Mungu wa haki hawezi kumhukumu mtu asiye na kosa.
Lakini kwa wengine (watu wazima) waliosalia ambao ndio waliowasababisha watoto wao kuangamizwa na maovu yao, hao biblia imesema kuwa ipo hukumu nyingine itawapata ya kuhukumiwa kwa mara nyingine na kutupwa katika lile ziwa la moto.
Mathayo 10:15 “Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.
Hapo anasema itakuwa rahisi Sodoma na Gomora kustahimili, maana yake ipo adhabu nyingine kwa watu wa Sodoma na Gomora zaidi ya hiyo iliyowapata ya kuteketezwa kwa moto kutoka mbinguni..
Ndio maana Biblia inasema tumwogope yeye awezaye kuuua mwili, na akiisha kuua mwili (kwa moto au maji au kitu kingine) bado anauwezo wa kushughulika na roho tena na kuihukumu katika ziwa la Moto.
Luka 12:5 “Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”
Watu wa Sodoma na Gomora, pamoja na watu wa gharika ya Nuhu waliuawa katika mwili, lakini bado tena ipo adhabu nyingine inakuja juu yao, jambo linalotisha sana..
Kwahiyo jambo kuu la kujifunza ni kuwa adhabu inaweza kurithiwa au kushirikishwa na mwingine hata pasipo kufanya kosa, na kinyume chake ni kweli Baraka zinaweza kurithiwa hata pasipo mwingine kufanya mema.. Mzazi unaweza kuwa chanzo cha Baraka au matatizo kwa mtoto wako.
Fahamu kuwa Kama utakuwa mwovu kupindukia basi fahamu pia watoto wako hawatakuwa salama kwa uovu wako, ndicho kilichomtokea Mfalme Daudi baada ya kwenda kulala na mke wa Uria, Biblia inasema mtoto aliyezaliwa alikufa, ijapokuwa mtoto hakufanya kosa lolote… lakini alilazimika kubeba adhabu ya baba yake.
Vile vile kuna mambo mema unaweza kuyafanya yakawa akiba njema kwa watoto wako, au watu wanaokuzunguka wakati wa sasa au wa baadaye.. Kwahiyo ni lazima kumcha Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je gharika ya Nuhu iliangamiza hadi samaki wa baharini na nyangumi?.
JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?
Je! Adamu na Hawa walizikiwa wapi?
Righteousness is a concept that goes beyond just doing what is morally right. In everyday terms, it includes qualities like integrity, honesty, self-discipline, and doing what is expected by society. But in the Bible, righteousness refers to living in right relationship with God, based on His standards—not just human ones.
Righteousness involves obedience to God’s law, a heart aligned with His will, and a lifestyle that reflects His holiness. It’s not just about actions, but also about the condition of the heart (Proverbs 4:23).
In the Bible, righteousness is portrayed as a way of life that flows from faith in God. It’s not earned by good deeds but credited by faith—just as it was for Abraham:
“Abram believed the Lord, and He credited it to him as righteousness.” — Genesis 15:6
The Apostle Paul refers to this same principle when he explains that true righteousness comes through faith in Jesus Christ, not from following the law alone:
“This righteousness is given through faith in Jesus Christ to all who believe.” — Romans 3:22
Scripture gives us examples of individuals who lived righteously—not perfectly, but faithfully:
These people walked with God in obedience, even in the face of trials and temptations.
Righteousness is often connected with blessing in Scripture. It brings stability, favor, and light even in dark times:
“The righteous will rejoice in the Lord and take refuge in him; all the upright in heart will glory in him!” — Psalm 64:10
“Even in darkness light dawns for the upright, for those who are gracious and compassionate and righteous.” — Psalm 112:4
These verses teach that righteousness not only pleases God but also leads to flourishing—spiritually and often practically.
Jesus warned religious leaders not to focus only on external acts like tithing while neglecting deeper matters like justice and love. He said:
“Woe to you Pharisees, because you give God a tenth of your mint, rue and all other kinds of garden herbs, but you neglect justice and the love of God. You should have practiced the latter without leaving the former undone.” — Luke 11:42
This means that righteousness includes both personal holiness and social justice. A righteous person cares about truth, mercy, and fairness—both in their walk with God and in how they treat others.
No one can truly be righteous by their own efforts. The Bible says:
“There is no one righteous, not even one.” — Romans 3:10
“All our righteous acts are like filthy rags.” — Isaiah 64:6
But the good news is that Jesus offers His righteousness to us. Through faith in Him, we are made right with God:
“God made him who had no sin to be sin for us, so that in him we might become the righteousness of God.” — 2 Corinthians 5:21
That means the starting point for a righteous life is not moral effort, but a relationship with Jesus. When we accept Him as Lord and Savior, He forgives our sins and gives us the Holy Spirit to empower us to live righteously.
You can’t live a righteous life if you’re separated from Christ. It begins with receiving Him:
“Yet to all who did receive him, to those who believed in his name, he gave the right to become children of God.” — John 1:12
Once you believe and receive Christ, God begins to transform your heart. You’ll find new strength to obey Him, new desires to live for Him, and a new identity as His child.
Righteousness is not about being perfect—it’s about being aligned with God. It’s shown through holiness, integrity, love, and obedience. And it starts with faith in Jesus.
Have you received the righteousness of Christ?
If not, today is the day to turn to Him. Let Him forgive your sins and fill your life with His Spirit.
“Blessed are those who hunger and thirst for righteousness, for they will be filled.” — Matthew 5:6
May the Lord bless you as you seek to live a righteous life in Christ.
Haya ndio mambo ambayo baada ya kuokoka, wokovu hufanya juu ya maisha ya mtu
Yohana 3:3
[3]Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
Maana yake ni kwamba pindi tu unapookoka, ni lazima ufahamu si kwamba unarekebisha yale maisha yako ya kale, na kuwa mtu mwema hapana bali unakuwa mtu mwingine kabisa. Kama mtoto mchana aliyekuja duniani, katika mazingira mapya kabisa.
Kwasababu ukristo sio nembo, au kikundi, au mtindo fulani au aina fulani ya dini hapana bali ni ulimwengu mwingine kabisa ambao mtu anaanza kuuishi.
2 Wakorintho 5:17
[17]Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
Wakolosai 1:13
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
Maana yake ni kuwa tunakuwa tayari kutoka chini ya utawala wote wa shetani, yaani kufuatisha mambo Ya kidunia, na anasa, wizi, tunaacha, Kama tulikuwa na vikoba vya kiganga, hirizi, mazindiko Yote hayo tunayaondoa, na kuanza kumtumikia Kristo, mfalme mpya.
Wafilipi 2:12-13
[12]Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
[13]Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Maana yake ni lazima Tujue wokovu ni mwendelezo ijapokuwa tunaokolewa pindi tu tunapookoka, lakini hatuupokei tu, na kusema tayari imekwisha hapana bali unapaswa udumu Moyoni mwetu, na kuhakikisha kila siku tunaweka umakini kwa kuuzalia matunda, kwa kufanya bidii kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Hivyo kwa ufupi wokovu sio tu, kipawa cha Mungu Kwetu, lakini pia kukubali maisha mapya, mfalme mpya, na njia mpya.
Maana yake ni nini?
Tangu siku hii ya leo wewe uliyookoka hakikisha unayaweka kando mambo yote ya kale ambayo ulikuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, kwasababu hiyo ndio TOBA pekee, kama ulikuwa mzinzi acha mara moja, ulikuwa mlevi, ulikuwa mwizi, ulikuwa mlanguzi acha, kama alivyofanya Zakayo alipokutana na Kristo. Kisha endelea kuishi maisha ya utakaso kila siku, ili Wokovu wako uzidi kuwa thabiti.
Bofya hapa kurudi kwenye mwongozo mkuu wa mafundisho ya mwongofu mpya. >>
Nini kinafuata? bofya hapa. >>>
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mungu ana makusudi makubwa na wewe, kwanza kukuokoa, na pili kukudhihirishia wema wake wote maishani mwako. Maamuzi haya ya kumpokea Bwana Yesu ni ya busara sana ambayo utayafurahia milele yote.
Ili kuupokea wokovu basi hapo ulipo unaweza kuchukua hatua ya imani, kwa kupiga magoti, kisha utafuatisha sala hii kwa imani. Na hakika wakati huu huu utaupokea wokovu bure.
Sema maneno haya kwa sauti:
“Bwana Yesu ninaamini kuwa wewe ni mwana wa Mungu, ninaamini kuwa ulikufa kwa ajili ya dhambi zangu, ukafufuka tena, na sasa unaishi milele. Ninakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi, nimestahili hukumu na kifo. Lakini leo ninaungama makosa yangu na dhambi zangu zote, na kuyasalimisha maisha yangu kwako. Ninaomba msamaha wako Bwana Yesu, liandike sasa jina langu katika kitabu cha uzima. Nakukaribisha moyoni mwangu, uwe na Bwana na mwokozi wangu tangu sasa. Nimeamua kukutii na kukufuata wewe sikuzote za maisha yangu. Asante Bwana Yesu kwa kunisamehe na kuniokoa. Amen”
Kwa sala hiyo fupi, tayari Bwana Yesu ameshakusamehe dhambi zako, kumbuka kusamehewa sio kumlilia Mungu sana kwa wingi wa dhambi zako ulizomtenda..Kana kwamba unamshawishi Mungu akusamehe. Hapana.
Mungu tayari alishawasemehe wanadamu kwa kifo cha Yesu Kristo pale msalabani. Hivyo ni jukumu tu la wanadamu kuukubali msamaha wa dhambi mioyoni mwao kwa kuamini Kile ambacho Mungu alikifanya Kupitia Yesu Kristo.
Ndicho ambacho Mungu alikisema hapa
Warumi 10:9-10
[9]Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. [10]Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kuamini kunakozungumziwa hapo ndio huko kukubali kwenyewe kazi ya Yesu aliyoifanya ya kuondoa dhambi za watu, kwa kufa kwake pale msalabani.
Ni sawa na mtu anakuja kukwambia nakupa hii almasi, ukiipokea basi umaskini wako wote umeondoka.
Sasa wewe kwa upande wako sio tena kukililia, hapana bali unawajibu tu wa kuamini kile kitu anachokupa, kwamba kinauwezo wa kuondoa umaskini..Ambapo sasa hudhuhihirishwa kwa kukipokea.
Ukishapokea sasa ndio matunda yake unayaona, kinyume chake ni kwamba bila kuamini kamwe huwezi kupokea, na umaskini utaendelea kubali kwako daima.
Ndicho Yesu alichokileta Kwetu. Ambacho ni msamaha wa dhambi. Akasema ukiamini Kuwa nimekufa kwa ajili ya dhambi zako, ili zifutwe kabisa kabisa basi utaokoka. Hivyo pale unapoamini kwa kukubali kumfanya Yesu kuwa ndio Bwana na mwokozi wako tangu huo wakati na kuendelea, na kwamba alikufa kwa ajili yako..Basi dhambi zako zinakuwa zimeondolewa kuanzia huo wakati, haijalishi zilikuwa ni nyingi Kiasi gani.
Hilo tu, ndio maana sala hiyo fupi, ikiwa umeisema kwa dhati yatosha, kukufanya wewe kuwa mwana wa Mungu. Kwasababu tayari Umemkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wako. Hilo ni hakikisho lake.
Bwana akubariki.
Nini kinafuata? bofya hapa. >>>
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo?
Bofya hapa kurudi kwenye mwongozo mkuu wa mafundisho ya mwongofu mpya. >>
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jina la Mkuu wa Uzima na Mfalme wa haki na pekee, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na Mwanga wa Njia yetu (Zab.119:105).
Kama Mkristo ni lazima uzijue alama hizi kuu nne (04), zitakazothibitisha kuwa unaye KRISTO maishani mwako, na alama hizo ni HEKIMA, HAKI, UTAKATIFU na UKOMBOZI.
1Wakorintho 1:30 “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi”
Maana yake kupitia Yesu Kristo tunapata Hekima, Haki, Utakatifu na Ukombozi.
1. HEKIMA YA MUNGU.
Kama Yesu ni hekima ya Mungu kwetu, je hii hekima ni nini na tunaipataje..
Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, Na kujitenga na uovu ndio ufahamu”.
Kumbe kumcha Bwana ndio hekima, maana yake kumpata Yesu ni kupata kumcha Bwana, na ndio hekima ya Mungu, na pasipo Yesu hakuna kumcha Mungu.
2. HAKI.
Na kama Yesu ni haki ya Mungu, je hii haki inapatikanaje..
Warumi 3:21 “Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii;
22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu”
Tunapomwamini Yesu tunakuwa tumeipata haki ya Mungu, haki ya kupokea kila tuombacho, haki ya kuishi milele, haki ya kumkaribia Mungu, haki ya kuwa na afya, haki ya kuwa amani, haki ya kuwa na furaha n.k
3. UTAKATIFU.
Na kama pia Bwana Yesu ni Utakatifu wa Mungu.. Je huu utakatifu tunaupataje?
Hiki ni kipengele muhimu sana, ambacho kinakwepwa na wengi, kumbuka huwezi kumtenganisha Yesu na UTAKATIFU, Ikiwa umemwamini Yesu ni lazima uishi maisha ya Utakatifu, hiyo ni kanuni. Na utakatifu sio ule wa rohoni tu, bali pia wa mwilini..
2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku TUKITIMIZA UTAKATIFU katika kumcha Mungu”.
Utakatifu unakuja kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, ambavyo vyanzo vyake ni tamaa ya macho na mwili, mfano wa hizo ni maudhui yote machafu yanayopatikana kwenye luninga, Mitandao na Magazeti, vile vile mazungumzo mabaya na makundi mabaya..
4. UKOMBOZI.
Yesu Kristo amefanyika pia ukombozi kwetu, kupitia kifo chake.. Na hii ndio alama ya mwisho inayomtambulisha Yesu, ambayo kimsingi hii ndio inayojulikana sana na wengi!
Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.
14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi”
Ndugu ukimjua Yesu kama mkombozi tu! (yaani anayesamehe dhambi), pasipo kumjua kwamba yeye pia ni “Mtakatifu” na anataka tuwe watakatifu kuna shida katika kuaminini kwako, vile vile ukimjua tu kama ni mtakatifu pasipo kumjua kama ni Hekima ya Mungu na Haki ya Mungu, bado pia kuna kitu kitakuwa hakijakamilika.. Lakini tukimjua katika sifa hizo Nne na kuziishi basi tutakuwa tumemjua hasa, na kufikia ule utimilifu.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”
Bwana atusaidie tuweze kufikia cheo cha kimo cha utimilifu wake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maana ya Mithali 10:1 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)
Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;
Huyu Imanueli tunayemsoma katika Isaya ni nani?
Swali: Tukisoma kitabu cha Isaya 7:14 tunamsoma Imanueli ambaye kimsingi ni Bwana YESU lakini tukiruka sura moja mbele (ile ya 8:8), tunamsoma Imanueli mwingine, juu huyu naye ni YESU au?
Jibu: Awali turejee mistari hiyo..
Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli”.
Ni wazi kuwa huyu si mwingine zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO.
Lakini hebu tuendelee na Isaya 8:8..
Isaya 8:8 “naye atapita, atapita kwa kasi na kuingia Yuda; atafurika na kupita katikati, atafika hata shingoni; na kule kuyanyosha mabawa yake kutaujaza upana wa nchi yako, Ee IMANUELI”.
Na hapa tunamwona Imanueli, sasa swali huyu naye ni Bwana YESU?.
Jibu ni la huyu si Bwana YESU.. awali ya yote ni vizuri kujua maana ya Imanueli..
Maana ya Imanueli ni “Mungu pamoja nasi”… hiyo ndio maana ya Imanueli, na ndio maana si ajabu neno hilo kuonekana katika biblia zaidi ya mara moja.
Sasa huyu Imanueli katika Isaya 8:8 ni Taifa la YUDA. Na hapa ametajwa kama Imanueli, kumaanisha uwepo wa Mungu kati ya Taifa hilo.
Ikiisoma habari hiyo kwa undani utaona kuwa ni kipindi ambacho mataifa mawili (Israeli na Shamu), yaliungana kutaka kupigana na Taifa la Ashuru, na kwasababu hiyo mataifa hayo mawili yalitaka kulishurutisha pia Taifa la Yuda liungane nao ili kwa pamoja wakampige Ashuru.
Lakini mfalme wa Yuda aliyeitwa Ahazi ushirika huo, na mataifa hayo mawili yakapanga njama kuvamia Yuda ili yamwue Ahazi na kumweka mfalme mwingine atakayekubaliana na wazo lao hilo la muungano…
Na matokeo yake mfalme Ahazi akataka msaada kwa waashuri, dhidi ya hayo mataifa mawili yaliyoungana..
ndipo Isaya nabii kwa ujumbe wa Bwana akawaambia Ahazi na Yuda yote kuwa wasimtegemee huyo mfalme wa Ashuru katika kutafuta msaada, wala wasiogope hayo mataifa mawili yaliyoungana (yaani Israeli na Yuda) kwani wao ni IMANUELU yaani MUNGU yu pamoja nao.
Kwahiyo yeyote mwenye MUNGU ni Imanueli (iwe mtu au Taifa)..ni Imanueli, wote walio okoka ni Imanueli kwasababu MUNGU yu pamoja nao.
Je upo ndani ya YESU?.
Kumbuka Mungu hawezi kuwa pamoja nawe kama wewe hujafungua mlango wa kuwa pamoja naye
Yohana 15:4 “Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu”
Fungua mlango leo wa kumkaribisha YESU maishani mwako, nawe utamwona MUNGU katika viwango vingine vya kiroho.
Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je unaujua uhusiano wa JIWE na MKATE kibiblia?.. Hebu leo tujifunze…
Mathayo 7:8 “ kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, MWANAWE AKIMWOMBA MKATE, ATAMPA JIWE?”
Ni hakika, hakuna mzazi yoyote mwenye akili timamu, ambaye mtoto wake akimwomba MKATE atampa JIWE. Hayupo mzazi wa namna hiyo, wala wanyama hawawezi kufanya mambo ya mfano huo wa watoto wao.
Lakini tunaona wakati fulani shetani alijaribu kumchonganisha Bwana YESU na Baba yake wa mbinguni kwa kumwambia, AGEUZE JIWE LIWE MKATE, kana kwamba Baba wa mbinguni alikuwa amemwekea yale mawe kule jangwani kuwa chakula chake (uvunjifu mkubwa wa heshima)!
Luka 4:2 “akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.
3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, LIAMBIE JIWE HILI LIWE MKATE”.
Hili lilikuwa ni jaribu kubwa la shetani kwa Bwana YESU kutaka kumwingizia roho ya kumwona Baba wa mbinguni kama ni mkatili, ambaye anampa mwanae mawe badala ya mkate kupindi cha njaa, na hivyo adui sasa anamfundisha ayageuze yale mawe kuwa mkate.
Na adui alijua kuwa endapo KRISTO angefanya vile (kwaasababu huo uwezo wa kugeuza jiwe kuwa mkate alikuwa nao) angempokonya uhusiano wake mwema aliokuwa nao na Baba yake, na tangu ule wakati angejua Baba anatoa mawe kwa watoto wake badala ya mkate.
Lakini Kristo kwasababu alikuwa amejaa Roho Mtakatifu aliyajua mafumbo yote ya shetani, hivyo hakudanganyika, na ndio maana hapo baadae katika Mathayo 7:9 akawaambia wanafunzi wake kuwa Baba mwema hawezi kumpa mtoto wake JIWE badala ya MKATE, sasa kwanini alisema vile?..kwasababu alishakutana na jaribu la namna hiyo hiyo jangwani.
Hali kadhalika unapopitia hali Fulani ya majaribu, usianze kutanga tanga na kuruhusu hofu, na kuona kama kila kitu kilichoko mbele yako hata kisicho na uhai ni fursa kutoka kwa MUNGU, sio kila kitu ni fursa kwako wakati wa majaribu!…vingi ni mitego ya ibilisi kwasababu anajua upo katika hali ya uhitaji wa hali ya juuu….hiyo ndiyo kawaida ya shetani.. alitaka pia kumwaminisha Bwana YESU kuwa yale mawe ni fursa ya kuondoa njaa yake.
Si kila kazi inayokuja mbele yako wakati wa vipindi vigumu ni fursa kutoka kwa MUNGU, kazi nyingine ni za Ibilisi (ni mawe). Mungu hawezi kukupa hayo kama riziki, ziache zipite!.. kazi za Bar ni mawe!, kazi ya Saloni za kiduni ni mawe!, kazi inayohusisha rushwa ni jiwe!, kazi inayohusisha kuuza utu wako ni jiwe!, kazi inayohusisha kuabudu miungu mingine ni jiwe!.. usizigeuze MAWE hayo kuwa MKATE!, hata kama una njaa ya kukaribia kufa!..ziache zipite, si majibu kutoka kwa MUNGU, bali ni majaribu kutoka kwa shetani, kwani huwezi kumwomba Baba wa mbinguni MKATE akakupa JIWE.
Huwezi kumwomba akupe kazi nzuri halafu akakuletea kazi ya kujiuza mwili wako!.. huyo sio MUNGU, bali ni ibilisi…Njaa yako, udhaifu wako, changamoto zako ambazo ni za muda tu!, zisikufanye ukaharibu mahusiano yako na MUNGU moja kwa moja.
Je tayari umeshampokea YESU?.. Kama bado fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho, na YESU amekaribia kurudi, na dunia inaenda kuisha, ni heri leo ukayasalimisha maisha yako kwake, ili usamehewe dhambi zako na jina lako liandikwe kwenye kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.
Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.
Ikiwa utahitaji Account yako nzima ifutwe moja kwa moja kwasababu zozote zile, pamoja na maudhui yake yote, basi wasiliana basi tutumie maombi hayo kupitia email yetu hii watakatifuwasikuzamwisho@gmail.com au namba zetu tajwa hapo chini na tutafanya hivyo mara moja.
+255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Ifuatayao ni Sera ya Faragha ya Tovuti/App ya Nuru ya Upendo (wingulamashahidi.org)
Tarehe ya Mwisho wa Marekebisho: [21/05/2025]
Tunapenda kukushukuru kwa kuchagua kutumia kituo cha Wingulamashahidi, jukwaa la injili ya YESU KRISTO, mafundisho ya Biblia, maombi, na jumbe za wokovu kupitia tovuti yetu na app yetu rasmi. Tunathamini faragha yako na tunajitahidi kuhakikisha taarifa zako zinalindwa kikamilifu.
Lengo la kukusanya taarifa zako ni kukuletea huduma ya kiroho iliyo bora zaidi. Na taarifa tuzikusanyazo ni:
Taarifa Binafsi (kama utazijaza): ambazo ni Jina lako, barua pepe, namba yako ya simu.
Taarifa za Kiufundi: Aina ya kifaa unachotumia, anwani ya IP, aina ya kivinjari, lugha, na mfumo wa uendeshaji.
Taarifa za Matumizi: Maudhui unayoyasoma, au kupakua, au kushiriki. Hii inatusaidia kujua aina gani ya masomo yanayopendelewa zaidi na watu.
Taarifa hizi zinahitajika kwa:
Kukurushia masomo mapya kwenye barua pepe yako.
Kuboresha muundo na mwonekano wa tovuti pamoja na app
Kujibu maswali yako, maombi ya maombi, au mawasiliano mengine ya kiroho..
Hatua za kiusalama tunazizingatia (kama SSL, uthibitisho wa watumiaji, na encryption) kuhakikisha taarifa zako hazidukuliwi na yoyote, wala kupotea, wala kutumiwa bila idhini ya mhusika. Pia tunazingatia kanuni za kimaadili kulingana na ukristo.
Hatutashiriki wala kuziuza, kusambaza, au kugawa taarifa zako binafsi kwa mtu mwingine yoyote bila idhini yako isipokuwa:
Kwa mujibu wa sheria au maelekezo ya mamlaka husika.
Kwa watoa huduma wanaotusaidia kutoa huduma hizi (mfano: huduma ya kutuma barua pepe), kwa masharti ya usiri.
Ikiwa kama utachagua kushiriki jumbe kwenye mitandao ya kijamii.
Hatukusanyi taarifa za watoto walio chini ya miaka 12 bila idhini ya wazazi au walezi. Ikiwa mzazi ataona kuwa kuwa mtoto wake ametoa taarifa binafsi bila idhini yao, basi tunaomba awasiliane nasi ili tuchukue hatua za kuondoa taarifa hizo mara moja.
Unayo haki ya:
Kufahamu ni taarifa gani tulizonazo kuhusu wewe.
Kuomba taarifa zako zifutwe au kurekebishwa inapohitajika.
Kujiondoa kwenye orodha ya wanaopokea pokea mafundisho kwa njia ya barua pepe au yoyote ile.
Kuhoji matumizi ya taarifa zako kwa ajili ya tafiti, chunguzi au matangazo (kama yatakuwepo).
Tovuti yetu hutumia cookies ili kuboresha matumizi yako. Unaweza kuchagua kuzima kama haitakuwa ni mapendekezo yako, lakini hii yaweza kuathiri usomaji wako wa tovuti.
Patakapotokea mabadiliko ya Sera hizi, tutakujuza mabadiliko hayo kupitia tovuti z. Mabadiliko huanza kutumika mara moja baada ya kuchapishwa.
Kwa maswali kuhusiana na sera hizi za faragha, tafadhali wasiliana nasi kupitia:
Barua pepe: wingulamashahidi@gmail.com
Tovuti: https://wingulamashahidi.org
Mungu akubariki sana kwa kuwa sehemu ya huduma hii. Tunakuombea baraka za Bwana YESU ziende nawe
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Shalom