Title 2025

Nini maana ya ..“huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino (mwanzo 3:15)”

Swali: Uzao wa mwanamke utampondaye kichwa nyoka, na nyoka ataupondanye mguu uzao wa mwanamke?


Jibu: Turejee..

Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;

15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; HUO UTAKUPONDA KICHWA, NA WEWE UTAMPONDA KISIGINO”.

Andiko hili lina maana mbili (02) ya mwilini na rohoni.. tuzitazame zote.

      1. MWILINI

Kiumbe cha kwanza kinachoogopeka zaidi na mwanadamu ni nyoka vingine ni simba na mamba, lakini nyoka ndiye anayeshika namba moja..

Na mwanadamu anapokutana na nyoka mara nyingi anakimbilia kuponda kichwa!… hata pasipo kufundishwa na mtu, kichwa cha nyoka ni shabaha ya kwanza ya mtu, na hiyo haiji tu kwa bahati mbaya bali ni kwasababu tayari tangu mwanzo Mungu alishasema hayo.. “HUO UTAKUPONDA KICHWA”.

Lakini pia sehemu ya kwanza sehemu ya kwanza ya nyoka kuuma/kugonga ni mguu wa mtu/kisigino, kwasababu ndio sehemu ya chini kabisa ya mwili wa mwanadamu na ndio sehemu rahisi nyoka kuifikia kwasababu yeye mwenyewe anatambaa kwa tumbo..

Ni ngumu nyoka kukimbilia kung’ata mkono wa mtu au goti la mtu, lakini ni rahisi sana kisigino kwasababu ndio kipo chini na karibu sana na yeye.. Sasa hiyo ni maana ya kimwili, yenye uhalisia hebu tutazame maana ya pili ya kiroho.

    2. ROHONI.

Kiroho “Uzao wa mwanamke” ni  “Uzao wa YESU KRISTO”.. sasa si kwamba Yesu ni mwanamke la!. Bali kwasababu alizaliwa na mwanamke pasipo mbegu ya mwanaume kuhusika… Kwahiyo Yesu alikuwa na mama wa kibinadamu, lakini hakuwa na Baba wa kibinadamu (Isaya 7:14)..ndio maana anajulikana kama Uzao wa mwanamke.

Na wote wanaomwamini Yesu wanaingia katika uzao huo, (wa mwanamke).. Na uzao wa mwanamke una nguvu kwasababu ndio uzao wa MUNGU.

Sasa kama uzao wa mwanamke ni Yesu pamoja na wote wanaomwamini, vipi kuhusu uzao wa nyoka. Uzao wa nyoka ni wote ambao hawaitaki kweli, lakini wanamwabudu ibilisi.. kwanini wote wanaomwabudu ibilisi wanaitwa uzao wa nyoka?.

Ni kwasababu Biblia inamtaja “Nyoka” kama Ibilisi (Soma Ufunuo 20:2).. Na tena Bwana Yesu akasema “ninyi ni wa baba yenu ibilisi”.

Yohana  8:43 “Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu.

44 Ninyi ni wa BABA YENU, IBILISI, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.

Hapo anasema “Ninyi ni wa BABA YENU, IBILISI” sasa badala ya kusema “ibilisi” weka “nyoka” kulingana na Ufunuo 20:2, kwahiyo ni sahihi kabisa kusema “nyinyi ni wa baba yenu joka/nyoka” hivyo wao ni uzao wa nyoka.

Ndio maana Yohana akawataja kama wazao wa nyoka..

Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?”

Soma tena Mathayo 12:34, Bwana Yesu anautaja uzao wa nyoka.. Kwahiyo kumbe tumejua! Mtu yeyote anayeikataa kweli na kumwabudu ibilisi ni uzao wa nyoka!..

Sasa hebu turejee pale maandiko yanaposema “uzao wa mwanamke utamponda kichwa uzao wa nyoka, na uzao wa nyoka utaponda kisigino uzao wa mwanamke.”

Hapa anazungumzia uwezo wa kimamlaka.. Kwamba uzao wa mwanamke (yaani watu walio ndani ya Imani ya Yesu Kristo) watakuwa na mamlaka juu ya uzao wa ibilisi, na hawa watakuwa na uadui, ndio maana utaona ijapokuwa watu wa MUNGU siku zote ni washindi lakini bado wanakutana na majaribu ya watu wanaomwabudu ibilisi, na wakati mwingine wanaumizwa nao.

Kwahiyo upo uadui wa asili kati ya watu wa Mungu (walio na imani ya YESU) na wale wanaomwabudu ibilisi.. Watu wa Mungu wanaponda vichwa (yaani Uongozi na mamlaka) za falme za watu wa ibilisi, ndivyo maandiko yanavyosema..

Habakuki 3:13 “Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako, Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako; UKAKIPONDA KICHWA CHA NYUMBA YA WAOVU, Ukiuweka wazi msingi hata mwambani”.

Na kinyume chake, watu wa ufalme wa giza (wa ibilisi) wanasumbua miguu (sehemu za mwisho mwisho) za watu wa Mungu… ndio maana utaona ijapokuwa Kristo aliziponda mamlaka za giza pale Kalvari kupitia kifo chake lakini miguu yake ilikuwa na alama za misumari, kutimiza unabii wa uzao wa nyoka kuponda miguu uzao wa mwanamke.

Na Ukitaka kuthibitisha zaidi kuwa “Uzao wa Nyoka” unaweza kuwakilisha watu Fulani.. rejea maandiko yafuatayo..

Mwanzo 49:17  “Dani atakuwa NYOKA barabarani, BAFE katika njia, Aumaye VISIGINO vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali”.

Kwahiyo tunaona kuna faida kubwa ya kuwa upande wa Bwana zaidi ya ule wa ibilisi.. kwasababu upande wa ibilisi utapondwa kichwa na uzao wa mwanamke..Na hata sasa matukio ya nyoka kuuawa na mwanadamu ni mengi kuliko nyoka kuua wanadamu.. kiroho inatakangaza jambo hilo hilo, kuwa uzao wa Mungu una nguvu nyingi.

Je upo upande gani?.. je wewe ni uzao wa nyoka au wa mwanamke??.. Kama hujaokoka huna haja ya kutafuta kujua upo upande gani, ni moja kwa moja upo ule wa nyoka, “wa kupondwa kichwa” kwasababu ibilisi ni nyoka.. Mpokee leo YESU na ugeuzwe asili yako, kama bado hujampokea, na uwe mtu mwenye mamlaka ya kuponda vichwa vya majoka..

1Samweli 2:10 “Washindanao na Bwana watapondwa kabisa; Toka mbinguni yeye atawapigia radi; Bwana ataihukumu miisho ya dunia; Naye atampa mfalme wake nguvu, Na kuitukuza pembe ya masihi wake”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

KUOTA NYOKA.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

Print this post

MAOMBI YA KAMBI

Huu ni mwongozo wa maombi yetu ya kambi July 30 – Aug 2.

Kanisa la Nuru ya Upendo

Daresalaam Tegeta.  Bofya hapa

👇 📥 

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Miongozo mingine.

MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

MWONGOZO WA MAOMBI YA FAMILIA

Print this post

MWILI NI KWA BWANA na BWANA NI KWA MWILI.

Je Mungu anaangalia mwili na kuihitaji?.. jibu ni Ndio!.. maandiko yanathibitisha hilo wazi kabisa..

1Wakorintho 6:13 “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. LAKINI MWILI SI kwa zinaa, BALI NI KWA BWANA, NAYE BWANA NI KWA MWILI”.

Nataka uone hayo maneno ya mwisho yanayosema “…mwili si kwa zinaa, BALI NI KWA BWANA, NAYE BWANA NI KWA MWILI” Kumbe “miili yetu” ipo mahususi kwaajili ya “Bwana” na Bwana yupo mahususi kwaajili ya “miili yetu”.. Si ajabu tunapomwomba mahitaji ya mwilini anatujibu haraka sana kama tu vile ya rohoni.

Si ajabu tunapoteseka katika mwili hapendi, kwasababu miili yetu ni ya thamani sana kwake, kwaufupi ili tuwe wanadamu ni lazima tuwe na miili..

Sasa je! huu usemi ya kwamba Mungu haangalii mwili unatoka wapi?.. bila shaka ni kwa ibilisi!.

Maandiko yanazidi kusema kuwa  “sisi si mali yetu wenyewe”

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe”.

Tuzidi kusogea mbele katika andiko hilo… tujifunze ni kwa namna gani MWILI ni Kwa BWANA na BWANA ni kwa MWILI.

Muunganiko wa Miili yetu na Kristo ni mpana sana kiasi kwamba Biblia inatafsiri “viungo vyetu vya mwili ni viungo vya Kristo pia”.. maana yake huo mkono unaouona kama ni wako, kibiblia ni mkono wa Kristo, hayo macho si yako bali ni ya Kristo, kwahiyo kama umemwamini Yesu halafu ukaenda kufanya zinaa, maana yake umechukua kiungo cha Kristo na kukifanyisha zinaa..ndivyo Biblia inavyosema..

1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!”

Huo mguu unaoona ni wako kiuhalisia kama umeokoka si wako tena bali ni wa Kristo… ndio maana Bwana Yesu alisema mahali watakapowakaribisha basi wamemkaribisha yeye Kristo..na wakiwakataa wamemkataa yeye Kristo… kwanini?.. ni kwasababu miili yetu si mali yetu wenyewe baada ya kuokoka!, bali viungo vyetu vyote vinakuwa ni vya Kristo na vina mhubiri Kristo.

Luka 10:16 “Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma”.

Umeona??.. maana yake mtu aliyeokoka ni “Kristo anayetembea”.. ukiendelea kujifunza zaidi katika habari ile ya hukumu ya kondoo na mbuzi katika Mathayo 25:31-46… utaona wale watu waliuliza “ni lini Bwana tulipokuona  una njaa, upo uchi tukakulisha na kukuvisha” ndipo Yesu atawaambia “kwa kadri mlivyowatendea wadogo wale basi walimtendea yeye”… wadogo wanaozungumziwa pale ni “watu wa Mungu wanaohubiri habari njema”.

Kwahiyo kumbe matumbo yenye njaa ya watu wa kweli wa Mungu ni matumbo ya Kristo, kumbe miguu yenye vumbi ya watu wa Mungu wa kweli ni miguu ya Kristo.. kwaujumla kumbe miili ya watu wa Mungu ni miili ya YESU mwenyewe!… si ajabu pale alisema “…nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!”

Sasa kama ni hivyo kwanini unauvika mwili wako mavazi ya jinsia nyingine…je ni Kristo yupi unayemhubiri kwa uvaaji wako?..kwanini unafanya zinaa?, kwanini unachora mwili wako?, kwanini unauvutisha sigara na kuunywesha pombe?

Yachukulie haya kwa uzito mtu wa Mungu, wala si usipuuzie!, na kusema Mungu haangalii mwili?.. jihadharia na mafundisho ya uongo! Yanayokuambia kuutunza mwisho ni mafundisho ya sheria na vifungo!.. Tunapookoka hatujapewa uhuru wa kufanya dhambi!, La! Hatujafunguliwa kufanya dhambi!.

Siku ya mwisho hatutafufuliwa roho bali miili ndio itakayofufuliwa, na Kristo hakutoa roho yake kwa ukombozi wetu, bali mwili wake wenye damu, mifupa, mishipa, nyama, moyo, miguu, mikono, ngozi !.. vyote Kristo alivitoa kwaajili ya ukombozi wetu..

Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.

Biblia inazidi kutufundisha kuitoa miili yetu kwa Bwana..

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

Je Bwana YESU alimjibu Pilato au hakumjibu? Je biblia inajichanganya?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.

Print this post

NAKUJUA JINA LAKO!

Kutoka 33:17 “Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, NAMI NAKUJUA JINA LAKO

Jina la Mtu limebeba siri kubwa sana,  lakini kabla ya kutazama jina la MUNGU.

Kitu pekee kilichomtambulisha na kinachomtambulisha MUNGU kwetu sasahivi ni JINA LAKE!.. Kamwe hajawahi kutuonyesha Sura yake, wala kuitangaza mahali popote pale!, bali jina lake.. bali jina lake amelitangaza na kulitukuza sana..

Sasa si kwamba anapenda kujificha kwetu!.. La bali ametuchagulia kilicho bora kwake tukijue!.. Kwahiyo kulicho bora kwake kwetu ni jina lake zaidi ya sura yake.

Na kilicho bora kwa MUNGU kwetu kukijua ni MAJINA YETU zaidi ya SURA ZETU… Utauliza kivipi?..

Kitu pekee kinachoko sasa mbinguni kinachotutambulisha sisi sio SURA ZETU bali ni MAJINA YETU.. Mbinguni hakuna picha zetu!, bali majina!..

Ufunuo 13:8 “Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye JINA LAKE HALIKUANDIKWA katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia”.

Soma pia Ufunuo 17:8,  Ufunuo 3:5,  Wafilipi 4:3 utaona hakuna sura kule za watu kule mbinguni… hivyo uzuri wako wa sura, weupe wako, weusi wako, urefu wako, ufupi wako, unene wako, ubounsa wako na wangu unaishia hapa!!!..

Hiyo pia ndio sababu ya Bwana YESU kuwaambia wanafunzi wake wasifurahia pepo wanavyowatii bali wafurahie majina yao yameandikwa mbinguni…

Luka 10:20 “Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni”.

Na unajua, Mungu anatujua kwa majina zaidi ya Sura na rangi?…ndivyo alivyomwambia hata nabii Musa.

Kutoka 33:17 “Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, NAMI NAKUJUA JINA LAKO”.

Umeona hapo?.. Mungu anamwambia Musa anamjua jina lake, sio sura yake…. Kwahiyo ni muhimu sana kuaangalia MAJINA YETU na kuyatengeneza…. Maandiko yanasema ni heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi..

Mithali 22:1 “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi…”

Sasa tunachaguaje majina??.. je tubadilishe majina tuliyonayo?.. jibu ni La!.. tutaendelea kuwa na majina yetu haya haya ikiwa kama yana maana njema.. Lakini majina yetu haya haya yanaweza kubadilika na kuwa BORA..

Kwa jinsi jina lako linavyozidi kuwa Bora mbele za Mungu, ndivyo nafasi yako mbinguni inavyozidi kuwa kubwa, na kwa kadiri linavyozidi kufifia mbele za Mungu ndivyo mbinguni linavyofutika kumbukumbu lako..

Sasa tunafanyaje majina yetu kuwa Bora?.. Si kwa kwenda kuyatolea sadaka ya ukombozi, au kuyaombea kwenye mkesha.. La!.. unaweza kutoa sadaka za aina zote duniani na jina lako lisiwe mbinguni, lakini bado likaendelea kuwa kubwa mbele za watu, na unaweza kuwa na jina la heshima kwa mbele za watu lakini mbele za Mungu ukawa huna jina.

Ifuatayo ni njia pekee ya kulitakasa jina lako, na hivyo heshima yako, na hadhi yako.. na njia hiyo si nyingine zaidi ya KUMCHA MUNGU, na KUJITENGA NA DHAMBI.. Utauliza kivipi, tusome maandiko yafuatayo?.

Kutoka 32:31 “Musa akarejea kwa Bwana akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.

32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao — na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.

33 Bwana akamwambia Musa, MTU YE YOTE ALIYENITENDA DHAMBI NDIYE NITAKAYEMFUTA KATIKA KITABU CHANGU”.

Umeona kitu kinachochafua jina la Mtu?… ni DHAMBI, Hiko ndicho kinachomwondoa mtu kwenye kumbukumbu za MUNGU, na si tu mbinguni na hata duniani pia..

Kumbukumbu 29:20 “Bwana hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya Bwana na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA ATALIFUTA JINA LAKE CHINI YA MBINGU”.

Huenda dhambi imechafua jina lako!.. suluhisho ni moja tu, kutubu na kuacha dhambi!.. jina lako hilo litasomeka kwenye kitabu cha mwanakondoo mbinguni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

FUNDISHA KILE UNACHOKITENDA NA KUKIISHI

Print this post

Je umewaonea utungu watoto wako?

Ulishawahi kuona mwanamke anajifungua mtoto bila kusikia utungu wowote? Hilo jambo bila shaka Litakuwa ni la ajabu… kwasababu haliendani kabisa na kanuni za asili …

hata maandiko yanasema hivyo..

Isaya 66:7-8

[7]Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume.

[8]Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara?..

Ni kanuni ya asili ili kiumbe kipya kizaliwe, mzaaji ni lazima apate utungu tu kama malipo ya kile akizaacho ..kila mwanadamu unayemwona chini ya jua, kuna mtu alipata maumivu kwa ajili yake..

Kanuni hii ipo rohoni pia…Kila mtakatifu unayemwona (aliyesimama), haikuwa bure bure…au kirahisi rahisi tu kama unavyodhani, kuna Waliopitia utungu juu yao…

Utauliza hili lipo wapi Kwenye maandiko?.

Paulo kwa Wagalatia,aliandika maneno haya;

Wagalatia 4:19

[19]Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu;

Paulo anawalilia wagalatia, kwa jinsi walivyoiacha neema ya Kristo, na kurudia mafundisho ya kiyahudi..anasema nawaonea utungu tena….tafsiri yake ni kuwa hapo nyuma alishawahi kuwaonea utungu…akawazaa…lakini sasa ni kama vile wanahitaji kuzaliwa tena….

Hivyo watu wote waliozaliwa mara ya pili wapo Waliowanea utungu.

Siku za Utungu mwanamke hupitia mambo haya:

1). Hulia na kuugua: 

Maana yake hiki ni kipindi cha machozi na kuomba juu ya wale wote unaotamani wampokee Kristo..ndiyo tabia waliokuwa nayo mitume.

Matendo ya Mitume 20:31

[31]Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi.

Watu wengi wanatamani kuona geuko la dhati kwa jamii zao, rafiki zao, waume zao, watoto wao lakini hawana muda wa kuwaombea kwa kuzama sana kwa kipindi kirefu na wakati mwingine kufunga huku wakiwahubiria…wanaikwepa Kanuni hii ya kiumbe kipya kuzaliwa.

2) Mwanamke hupitia hatari mbalimbali zinazohatarisha maisha; 

Hichi kipindi wanawake wengi huchungulia kifo, kwa sababu ya maumivu, au shinikizo au kutokwa na damu nyingi sana.

Ndivyo ilivyo pale unapojaribu, Kumvuta mwenye dhambi aifikie toba ya kweli, adui huanza kuinua vita, dhidi yako wewe na huyo unayemzaa.. lile joka litataka kufanya vita na wewe.

Ufunuo wa Yohana 12:1-4

[1]Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.

[2]Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa.

[3]Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

[4]Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake.

Ukijikuta katika wakati huu fahamu ni kung’ang’ana kumfuatilia kondoo huyo bila kujali hali au vipingamizi…unaweza kuona visababu sababu visivyoeleweka, mara hataki tena kukusikiliza, mara anaumwa, mara ndugu zake wanampinga, mara anakuwa mzito.hapa hupaswi kukata tamaa..endelea kumfuatilia kwasababu hizo ni hila za adui kumzuia asikate shauri kwa Bwana Yesu..

Fahamu tu kazi yako si bure upo wakati ataamini na kugeuka kabisa kabisa kwasababu Nguvu uliyonayo na kuu kuliko ya ibilisi..na furaha yako itakuwa ni pamoja na malaika mbinguni. (Luka 15:10).

Pia Biblia inasema…

Yohana 16:21

[21]Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

Upo wakati utayafurahia matunda yako. Siku utakapoona kupitia hao makumi, mamia, maelfu ya watu wanaokoka..na siku ile Bwana anakupa thawabu kwa tunda hilo ulilomzalia.

Swali ni je utungu wako upo wapi?.. ni wapi unaweza kusema yule ni mwana wangu nimemzaa mimi katika Kristo?..

Kwenda tu kusema Yesu anakupenda okoka, halafu ukamwongoza Sala ya toba na kumwacha…hili halimaanishi huyo ni mtoto wako. Ndio maana wapo watu wengi wanaosema leo wamemkiri Yesu, lakini ukiwaangalia sio viumbe vipya..kwasababu hawakuzaliwa, bali waliaminishwa tu.

Tukubali kuzaa kwa kuwafundisha, kuwaombea sana, na kuwafuatilia mpaka watakapokata shauri la kweli kumpokea Yesu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

Print this post

Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)

SWALI: Sulemani ana maana gani kusema..Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,  Hata yatakapoona vema yenyewe.? 

Wimbo Ulio Bora 2:7

[7]Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, 

Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,  Hata yatakapoona vema yenyewe.


 

JIBU: Mwandishi anaeleza hekima ya kweli juu ya mapenzi halisi yanavyoundwa.. na hivyo anawaasa wale wote wanayoyatafuta…wajue kanuni hizo ili wasiingie katika hasara kama sio majuto.

Andiko hilo linalenga nyanja zote mbili;

  1. Mahusiano ya mwilini (mwanaume na mwanamke)
  2. Mahusiano ya rohoni.(Kristo na Kanisa lake)

Anaposema nawasihi enyi binti za Yerusalemu..

Anawakilisha kanisa, au watu wote wanaotaka kuingia katika mahusiano ya kindoa..

Anasema;

 Kwa paa na kwa Ayala wa porini… Anaapa Kwa wanyama hawa, lakini tunajua mara nyingi kwenye agano la kale watu walikuwa wanaapa kwa jina la Mungu…lakini hapa anatumia wanyama hawa ambapo ni Paa na Ayala.

Ni aina ya swala, ambao kwa eneo la Mashariki ya kati ilikuwa ni kawaida sana kuwaona kwenye mapori tulivu..

Wanyama hawa wana sifa ya:

  1. Upole na umakini
  2. Wanaaibu na kutishika kwa haraka, 
  3. Wana wepesi kwenye kukimbia.
  4. Na wakipotelea porini, si rahisi kuwapata tena.

Hivyo mwandishi anawasihi watu wanapotaka kuingia katika mapenzi wayaone Kama ni kuwawinda Ayala na Paa… Ambao hawahitaji pupa…

Ndio maana anasema; 

“Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.”

Akiwa na maana kuwa unapochochea mapenzi kwa haraka utayapoteza…mfano tu unapomvamia Ayala kwa pupa, hutampata atapotelea mbali…

Bali unapokuwa mtulivu na kumsogelea kidogo kidogo, ni rahisi kumnasa…

Hivyo Katika mahusiano ya mwilini anatuasa kuwa mahusiano ya kweli, yanajengwa katika muda…sio kwa kuyapaparikia…vijana wengi, wanang’ang’ania kuingia katika mahusiano kabla ya umri sahihi, au nyakati sahihi au wengine wakikutana hata wiki haijakwisha, ndani ya muda mfupi sana, utaona wameshaahidiana kuoana, na hatimaye kujikuta, wapo kwenye mahusiano hayo, kipindi kinapopita na kugundua uhalisia wao, na kasoro nyingi wanaanza kujuta kulitokea nini? Ni kwasababu walikurupukia mapenzi wala hawakuruhusu yaamke yenyewe katika wakati wake.

Lakini katika Roho, Bwana anaeleza mahusiano kati ya yeye na mtakatifu wake..Upendo kwa Kristo thabiti, hujengwa kwa jinsi tunavyokaa na kudumu ndani yake, na kujua sifa zake, tabia zake, na uweza wake, Na hiyo inakuja kwa kusoma Neno, maombi, na ibada…watu wanaotembea katika mambo hayo kwa kipindi kirefu ndio wanaozama katika mapenzi ya kweli na Kristo.

 

Lakini mtu anayempenda Yesu kwasababu kaponywa ugonjwa, au kwasababu kasaidiwa Biashara yake kustawi, au Bwana amemwonekani mahali fulani kipekee, mwingine anamtumikia Mungu kwasababu ya shinikizo fulani la watu…Hapo ni sawa na kumrukia Ayala kwa pupa…hatimaye utamkosa..

 

Watu hawa wanakuwa ni upendo wa kitambo tu, mambo yakishabadilika waanza kusema mioyoni mwao, kama Yesu mwenyewe ndio huyu ni heri nirudie tu maisha yangu ya nyuma…

 

Hiyo yote ni kwasababu alikurupuka…bila kujua sifa na tabia za ampendaye.

 

Usikubali upendo wako kwa Kristo ujengwe kwa matukio ya ghafla…ujenge upendo katika mahusiano ya muda.. ndipo yatakapokuwa thabiti.

 

Wimbo Ulio Bora 2:7

[7]Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,  Kwa paa na kwa ayala wa porini, 

Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,  Hata yatakapoona vema yenyewe. 

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

 

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

Maombi Maalumu ya Kuombea Ndoa.

Print this post

TUTAFUTE KWA BIDII KUKAA NDANI YA YESU.

Kwa haraka ni rahisi kutafsiri maana ya kukaa ndani ya Yesu ni “kumpokea Yesu”  au “kuishi maisha ya wokovu”..sio makosa kufikiri hivyo kwani ni sahihi kabisa..

lakini leo nitaka tuone maana ya ndani ya “kukaa ndani ya Yesu”.

Awali ya yote hebu kwanza turejee maandiko.

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Je umeshawahi kumweka mtu moyoni kwa tendo zuri alilokufanyia?..

Au je umeshawahi kumtoa mtu moyoni kwa tendo baya alilokufanyia?.

Kama umeshawahi kupitia mojawapo ya hizo hali basi utakuwa umeshaanza kuelewa maana ya maneno hayo Bwana YESU aliyoyasema kwamba “kaeni ndani yangu nami ndani yenu…(Yohana 15:4).

Maana yake kuna mambo unaweza kuyafanya ukawa umeingia moyoni mwa Kristo, akavutiwa nawe zaidi, ukawa upo moyoni mwake..

Wapo watu ambao Yesu yupo mioyoni mwao (ndani yao) lakini wenyewe hawapo ndani ya YESU.

Hebu tujifunze zaidi kwa mifano…

Unaweza kuwa na marafiki wawili mmoja yupo moyoni mwako sana (aidha kutokana na jambo zuri alilowahi kufanya kwako) na mwingine ni rafiki tu wa kawaida kwako hayupo ndani yako,

Na kuna watu yawekana ukawa mioyoni mwao, lakini wewe usiwe mioyoni mwao..

Na ni hivyo kwa Bwana, kuna watu wapo ndani ya Yesu na kuna ambao hawapo ndani ya Yesu ingawa wamemwamini Yesu.

Sasa swali la msingi, ni kitu gani tunachoweza kufanya kikatuingiza ndani ya moyo wa Bwana YESU, (yaani tukamvutia sana hata kutuingiza ndani yake?).

Majibu ameyatoa yeye mwenyewe Bwana Yesu.

Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.

57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.

Meza ya Bwana  ni tendo moja linalougusa moyo wa Bwana Yesu kuliko tunavyodhani kamwe usipuuzie ushirika mtakatifu.

Jambo la pili linalotuingiza ndani ya YESU, ni Kuzishika amri zake..

1 Yohana 3:24 “Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa”

Na amri kuu ni Upendo..

2 Yohana 1:5 “Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.

6 Na huu ndio upendo tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo”.

Kwahiyo kwa kufanya mambo mawili makuu, yaani Ushirika wa meza ya Bwana na tukipendana sisi kwa sisi, tutaugusa pakubwa sana moyo wa Kristo.

Na matokeo ya kuwa ndani ya Yesu kwa kufanya mambo hayo mawili, na kupewa chochote tunachokiomba..

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.

 Mwisho: hatua za kukaa ndani ya Yesu kwanza zinaanza kwa wewe kumpokea Yesu, na ndipo mambo hayo mawili yanafuata.

Je umempokea Yesu kweli kweli?, kama bado unasubiri nini?…mpokee Yesu leo, ufanyike kiumbe kipya na kuoshwa dhambi zako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je Sulemani alifuga nyani? (2Nyakati 9:21)

Jibu:  Turejee maandiko hayo..

2Nyakati 9:21 “Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu zilizokwenda Tarshishi pamoja na watumishi wa Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na NYANI, na tausi.

22 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima”.

Sasa swali, je Sulemani alifuga NYANI?..

Jibu ni ndio alikuwa anao NYANI, lakini hakuwa anawatumia kwa kitoweo, kwani kulingana na sheria za torati, Nyani alikuwa miongoni mwa wanyama najisi (wasiofaa kuliwa M/Walawi 11:27).

Lakini kama hakuwa anawatumia kama kitoweo alikuwa na anawatumia kwa shughuli gani?.. Jibu ni wazi kuwa kwa MAONESHO au michezo! (Ingawa Biblia haijaweka wazi kuwa ni kwa michezo).. lakini asilimia kubwa ni wazi kuwa Nyani na Tausi walitumika kwa kazi hizo katika majumba ya wafalme.

Hata sasa si ajabu ukiingia Ikulu utakuta nyani na Tausi na wanyama wengine, sasa uwepo wa wanyama wale Ikulu, si kwaajili ya kitoweo kwa Raisi, bali kwa maonyesho tu. Na Sulemani ni hivyo hivyo alikuwa ni mtu anayepokea zawadi nyingi kutoka mataifa mengi, na zawadi hizo ni za kila aina, hivyo si ajabu kuona akipewa zawadi za wanyama, au akifanya  biashara za wanyama.

Je na sisi wakristo tunaruhusiwa kufuga wanyama pori hao katika nyumba zetu au wanyama hao wamebeba roho?..

Jibu ni Ndio tunaruhusiwa ikiwa sheria juu ya wanyama hao hazijavunjwa.. kama mtu ana kibali cha serikali kumiliki wanyama hao wa pori, basi kibiblia si kosa kuwamiliki pia, lakini iwe tu kwa dhamira kama hizo za maonyesho, lakini ikiwa kwa shughuli nyingine kama za kiibada au kijangili, ni kosa kibiblia.

Je umempokea YESU?.. Je unajua kuwa tunaishi majira ya kurudi kwa pili kwa YESU?, na parapanda imekaribia sana kulia?..Mwamini Yesu, na tubu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je wanyama wote waliwezaje kuenea kwenye safina ya Nuhu?

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.

Swali: Je Kula nyama mbichi ni dhambi?.

Kwanini MUNGU aangamize watoto kwenye gharika ya Nuhu?

Print this post

Tafsiri ya Mhubiri 4:13-16,  isemayo ‘Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki’

SWALI: Naomba kufahamu Tafsiri vifungu hivi Mhubiri 4:13-16,  isemayo ‘Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki’ Nini maana ya habari ile?

Mhubiri 4:13 Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu. ambaye hajui tena kupokea maonyo.
14 Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki; naam, hata katika ufalme wake alizaliwa hali ya umaskini.
15 Nikawaona wote walio hai waendao chini ya jua, ya kwamba walishikamana na huyo kijana, huyo wa pili aliyesimama badala ya yule.
16 Hawakuwa na kikomo hao watu wote, hao wote ambao alikuwa juu yao; lakini hata hivyo wale wafuatao baada yake hawatamfurahia. Hakika hayo pia ni ubatili, na kujilisha upepo.

JIBU:

Mstari wa 13. Unazungumzia jinsi hekima, ilivyo bora kuliko cheo, au umri wa mtu. Yawezekana mtu akawa na vyote, lakini akipungukiwa na hekima, ni hatari kubwa sana, Na dalili moja wapo ya kupungukiwa hekima kama anavyofafanua mhubiri ni kukataa kupokea maonyo.

Mfano wa viongozi wa namna hii kwenye biblia ni Rehoboamu(mtoto wa Sulemani), Nebukadreza (nyakati za mwanzoni), Belshaza, Ahabu, Herode. Unaweza kuona jinsi utawala wao ulivyokuwa mwiba mkubwa kwa taifa, na wengine hata kwa vizazi vya mbeleni, kwasababu hawakukubali maonyo ya ki-Mungu..

Ni lazima tukubali kufundishika, kwasababu huo ndio msingi wa hekima (Mithali 13:1, 13:18, 15:5)

Lakini mstari wa 14

Anaeleza, jambo lingine, linalohusiana na ubatili… anazungumzia habari ya kijana aliyetoka katika umaskini, mpaka kuwa mfalme, aliyetoka vifungoni mpaka kuwa mfalme..

Kufunua kuwa mafanikio ya mwanadamu hayatabiriki, sio tu walio na cheo, au waliozaliwa katika familia ya kifalme,  ndio wanaofanikiwa, Bwana anaweza kumwinua maskini, mtu asife faa, na kumfanya mtawala na mkuu, mfano wa Yusufu, na Daudi.

Pia Mstari 15,

Unaeleza kuinuka kwa mtawala mwingine, baada ya huyo kijana. Halafu watu wakashikamana naye huyo..Kuonyesha kuwa sifa za kibinadamu, huwa hauzidumu, maana yake kuwa hata uweje shujaa, ufanye mambo mazuri kiasi gani, utafurahiwa kwa kitambo tu, baadaye utachokwa, siku atakaponyanyuka mwingine, atapendwa, na kufuatawa..na wewe utasahaulika..

Mstari 16

Unaendelea kusema, bado watu waliendelea kumfauta huyo mfalme mpya, yaani walimfurahia pia sawa tu na walivyofurahiwa wafalme wengine nyuma waliopita, lakini ghafla baada ya muda wakamchoka naye pia..Mzunguko ukawa ni huo huo..

Ndipo mhubiri anahitimisha kwa kusema ni ubatili mtupu..Maana yake heshima, sifa, na  mapokeo ya kibinadamu hayana umilele nyuma nyake, ni sawa tu na kufuata, upepo, ambapo unaweza kukupa matumaini ya muda, kukupelekea mbali, lakini katikati ya safari, ukayeyukia mbali na usijue unapokupeleka.

Haya ndio mambo tunayoyaona hata sasa katika ulimwengu, ni rahisi sana kuona watu wakimfurahia kiongozi mpya, tena yule mpambanaji, lakini baada ya muda wanaanza kupoteza furaha naye, na hatimaye kumpinga, wakitaka mwingine, na yule mwingine ajapo, huwa vivyo hivyo, wanamfurahia kwa muda, baadaye wanamchoka, mzunguko huo umekuwepo ulimwenguni wakati wote..

Lengo lao ni  wakitumainia, kumpata kiongozi bora, lakini hajawahi kutokea..

Hawajui kuwa yupo kiongozi bora, mwema, asiyechokwa, asiye na hila, asitafuta vya kwake, aliyejitoa nafsi yake yeye mwenyewe, anayedumu milele, ambaye huyo mwanadamu akimkubali basi matarajio yake yanafikiwa, kwasababu ankuwa naye wakati wote moyoni mwake.. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Amwaminiye, anapokea uzima wa milele. Wengine wote unafuata upepo..

Je! Upo tayari kumpokea leo, Kama ni ndio, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba  >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

Print this post

Vyusa ni nini? (Ayubu 41:7)

Ayubu 41:7 Je! Waweza kuijaza ngozi yake na vyuma vyenye ncha, Au kichwa chake kwa vyusa?

Vyusa ni mikuki maalumu iliyoundwa kwa ajili ya kunasia samaki, ambayo wavuvi hutembea nayo, kuvizia samaki, hususani wale waliokaribia na kilele, kisha huwachoma kwa nguvu, na kuwavuta nje ya maji, na kwasababu ya ukali na mvuvi, na wepesi wa ngozi zao, mara nyingi mkuki ule hauwezi kunasuka mwilini mwao.

Sasa katika habari hiyo, ukianzia mistari ya juu hata katika sura nzima na zile zilizotangulia, ni Ni mahojiano kati ya Ayubu na Mungu, ambapo Mungu anamuuliza maswali Ayubu ayajibu, ni maswali ambayo mpaka sasa hayana majibu, mambo makuu ya Mungu na uweza wake usiofafanulika kwa ufahamu wa kibinadamu. Sasa moja ya mambo aliyokuwa anamuuliza Ayubu ni kuhusu, mnyama “Mamba”, kwa jinsi alivyomuumba kwa namna ya kipekee, tofauti na samaki wengine, Anamweleza  jinsi alivyo jasiri, asiye na woga, anamuuliza Ayubu je unaweza kutupa ndoano yako ukamvua kama vile ufanyavyo kwa samaki wengine?(Ay 41:1).

Kwa jinsi magamba yake yalivyo magumu, anasema hata upanga ukipita juu yake haumwingii..

41:26 Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.

Ndio hapo sasa mbeleni anasema tena, je! Je unaweza kukitoba kichwa chake kwa vyusa, kama vile ufanyavyo kwa sangara, na perege? Si itakuwa sawa na unautoboa ukuta na chelewa.

Mungu kwa urefu ameeleza sifa zake mnyama huyu katika sura yote ya 41 (japo kimsingi alikuwa anamwelezea Kristo Yesu, kwa mfano wa wanyama), akimfananisha na mnyama huyu jinsi alivyokuwa thabiti kiasi kwamba hakukuwa silaha yoyote ya adui iliyompata, na jinsi alivyotisha na kuwa na nguvu za kushinda hata mauti..

Kwa uerfu wa habari hiyo fungua hapa usome>>>> SIFA ZA MAMBA YULE MKUBWA WA AYUBU.

Je! Umempokea mfalme huyu moyoni, mwenye nguvu za kutisha, asiyetikiswa na kitu chochote?. Kumbuka wokovu ni kwa faida yako mwenyewe, hakuna njia unaweza ukamshinda adui, kama Kristo hajakuficha ndani yake. Utavuliwa tu na adui kama samaki dhaifu, lakini uwapo ndani ya Kristo hakuna awezaye kukuvua. Ikiwa upo tayari kuyasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu..wasiliana na sisi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.

Pia kwa maana za maneno mengine ya kwenye biblia fungua hapa >>>> Maana ya Maneno Kwenye Biblia

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Madongoa ni nini? (Ayubu 7:5)

Nini maana ya Selahamalekothi?

Ayubu alimaanisha nini kusema ‘nami nitarudi tena huko uchi vilevile;?

Print this post