Title 2025

Theofania ni nini?

Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”

Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu  aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.

Mfano wa njia hizo,

> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)

> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)

> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)

> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)

> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)

> Mungu kumtokea Samweli  (1Samweli 3:10)

> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)

Je! theofania ipo hadi sasa?

Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.

Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.

Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)

Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.

Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Theolojia ni nini?. Na je ni sahihi kuisoma?

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Print this post

Wanethini ni watu gani kwenye biblia?

Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’  kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;

Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.

Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.

Soma pia, (Ezra  2:43, 2:58, 7:24)

Asili yao:

Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.

Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua

Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.

Kazi yao:

Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe  wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.

Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)

Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea

Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.

Kwanini Bwana aruhusu jambo hili?

Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na  kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.

Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?

Swali: Je ni vema sisi tuliookoka kushika matawi siku ya jumapili na kuingia nayo kanisani au kutembea nayo?


Jibu:  Jumapili ya mitende ni jumapili moja kabla ya jumapili ya pasaka, ambapo katika historia ni siku ambayo KRISTO aliingia YERUSALEMU, na watu wakakata matawi ya mitende na kuyatandaza njiani ili Bwana YESU apite. (kumbuka, mtende ni mti unaozaa matunda ya tende).

Mathayo 21:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,

2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana punda pamoja naye; wafungueni mniletee.

3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.

4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,

5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.

6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,

7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.

8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; NA WENGINE WAKAKATA MATAWI YA MITI, WAKAYATANDAZA NJIANI.

9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.

10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?

11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya”.

Sasa swali ni je! Na sisi ni sahihi/ruksa kuisheherekea/kuiadhimisha hii siku?

Jibu: Hatujapewa agizo lolote kwenye Biblia la kuiadhimisha jumapili ya mitende, wala jumapili ya pasaka. Isipokuwa kutokana na umuhimu wa hizo siku katika historia ya Ukristo, si vibaya kuzifanya hizo siku/tarehe kuwa za ibada ya kutafakari mambo yaliyotokea wakati huo.

Kwamfano katika jumapili ya mitende, ni wakati ambao watu walimsifu YESU kwa kumwimbia Hosana Hosana (yaani Okoa). Nasi kwa kutafakari jambo hilo twaweza kutengeneza kama igizo la wakati huo, na kumwimbia Bwana kwa furaha tukisema Hosana amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la BWANA, kwa kufanya hivyo huku tumeshika matawi ya mitende sio kosa wala dhambi kwani ni sehemu ya sifa tu kama sifa nyingine zinazohusisha shangwe za kurusha rusha leso juu au matawi ya miti.

Lakini matawi yale yakifanyika kama ni vitu vitakatifu, (kwamba vimebeba nguvu Fulani ya kiungu, kama vile sanamu zinazowekwa kwenye baadhi ya makanisa) hilo ni kosa, kwani tayari hizo ni ibada za sanamu, na si tena kwa lengo la sifa za kumtukuza MUNGU.

Utakuta mtu anatembea na tawi lile si kwa lengo la sifa, wala tafakari ya mambo yaliyotokea miaka elfu mbili iliyopita, bali kama kisaidizi cha kuondoa mikosi, au matatizo, au cha kufukuzia wachawi n.k Huyu mtu anakuwa anafanya ibada za sanamu, na inaweza isiwe ni kosa lake bali la waliomfundisha.

Kwahiyo jumapili ya mitende si vibaya kuadhimishwa ikiwa itafanyika kwa ufunuo na maarifa namna hiyo, lakini kama itafanyika kidini na kidesturi, inageuka kuwa ibada ya sanamu, jambo ambalo ni machukizo kwa BWANA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini Maana ya Hosana?

AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.

MUNGU AKETIYE MAHALI PA JUU PALIPOINUKA.

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

Print this post

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

SWALI: Kwanini Yesu akubali ombi la mapepo, na si kuyaamulia adhabu yake mwenyewe, au kuyafukuza kabla hata hayajaongea?

Luka 8:31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. 32 Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.

JIBU: Maneno hayo aliyasema baada ya kukutana na mtu yule aliyekuwa amevamiwa na jeshi la mapepo, yaliyomfanya akae makaburini  muda mrefu, bila nguo. Hivyo kama tunavyosoma yale mapepo yalipomwona tu Yesu, kabla ya tamko lolote yenyewe yakamfuata na kuwasilisha ombi lao kwa kusihi sana. Kwamba yawaingie wale nguruwe waliokuwa jirani wakichungwa. Yesu akasiliza ombi lao, akayapa ruhusa. Yakamtoka Yule mtu, na kuwaelekea wale nguruwe, na saa ile ile Yule mtu akawa mzima.

Lakini swali linakuja ni kwanini Yesu ayasikilize mapepo.. Kwanini ayapate nafasi ya kujichagulia pa kwenda?

Zipo sababu mbili.

Sababu ya kwanza ni kutimiza pia kusudi la Mungu:

Ni wazi kuwa Bwana alilitafakari wazo lao, na kuona kama lingeweza kuleta madhara yoyote au uharibifu wowote wa  mpango wa Mungu. Na akaona kinyume chake ni kuwa kusudi la Mungu litaendelea kuthibitika hata katika ombi lao, kwasababu kutoka kwao na kuwaingia wale nguruwe kisha kwenda kujitupa ziwani. Ilikuwa ni udhihirisho wa wazi kwa watu kuwa mapepo ni halisi, lakini pia yanatabia ya uuaji. Kwamfano kama angemponya tu, bila ishara yoyote, pengine wengine wangesema “aah huyu akili zilimruka tu!” alikuwa na stress zake, au maisha yalimtinga sana, akachizika, hivyo amekutana na mwanasaikolojia mzuri amemweka sawa… Lakini kuona mapepo yale yameruhuisiwa kwenda kuingia viumbe vingine, halafu yakawaendesha ziwani kuwaua, ilikuwa ni ishara bora zaidi ya kazi za Mungu.

Sababu ya pili: Ni kuto-harakisha hukumu ya Mungu

Utakumbuka mapepo yenyewe yalimwambia Yesu ‘tuna nini nawe, je umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?’

Mathayo 8:29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?

Maana yake ni kuwa mapepo yalijua kuwa walishawekewa wakati wao wa mateso baadaye kule shimboni na atakayekuja kuwapeleka huko ni Kristo. Hivyo hapa yanamkumbusha Bwana asibatilishe mpango huo, na kuwaadhibu mapema.

Pengine hiyo ndio sababu nyingine ya Bwana kutotoa adhabu kali kwao, ni kuwa mpango wa hukumu ungebatilika.

Ni jambo gani tunafundishwa hapo?

Kitendo cha mapepo kujisalimisha yenyewe kuomba kupunguziwa adhabu, ni kuonyesha mamlaka kuu iliyo ndani ya Kristo. Ambayo hata sasa ipo ndani yetu. Hatufundishwi kuongea na mapepo, bali kuyakemea kwa mamlaka yote. Ambayo yaweza tokea mengine hata kabla ya kukemewa yakaomba yenyewe nafasi ya kupunguziwa adhabu. Hilo linawezekana!

Tumia mamlaka uliyopewa ndani yako. Fukuza pepo wote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Gengeni ni wapi, wale nguruwe walipoteremkia? (Marko 5:13)

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

Print this post

Wakamchukua vile vile alivyo katika chombo.

Marko 4:35-36

[35]Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.

[36]Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.

Vifungu hivi vinazidi kutueleza tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo na huduma yake jinsi ilivyokuwa ya kitofauti sana hapa dunia.

Kujitoa kwake kulikuwa ni kwa gharama sana tofauti na sisi tunavyoweza kufikiri, embu fikiria kisa kile cha pale kisimani alipokutana na yule mwanamke msamaria, na kuanza kumshuhudia habari zake mpaka kupelekea wimbi kubwa la watu Samaria kumfuata.

Kwa jicho la kawaida unaweza kudhani ilikuwa ni huduma ya kawaida lakini kiuhalisia haikuwa ni jambo lililomruhusu sana kimwili. Kwani maandiko yanatuambia alichoka sana kwasababu alikuwa katika safari ndefu kutoka uyahudi Kwenye Galilaya.

Tunasoma akiwa na njaa na kuchoka ‘alijibwaga’ hivyo hivyo pale kisimani, akawaruhusu wanafunzi wake kwenda mjini kutafuta chakula..

Lakini Mwanamke yule alipokuja kisimani hakusema ngoja nipumzike kwanza, nivute pumzi, kinyume chake alianza muda ule ule kusema naye..hata baadaye alipoletewa chakula ale hamu yake ya kula ilikatwa na ile kazi ya Mungu Aliyokuwa anaifanya.

Yohana 4:6-8,30-33

[6]Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

[7]Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

[8]Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula…..

[30]Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

[31]Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.

[32]Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

[33]Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

Vivyo Hivyo tena wakati mwingine alikuwa anawahubiria Makutano mchana kutwa, mpaka ilipofika jioni ambapo alipaswa aende kupumzika kidogo, ili kesho aendelee na huduma. Maandiko yanatuambia akawaambia wanafunzi wake “Tuvuke Ng’ambo”.

Kibinadamu jambo kama hilo la safari Nyingine mpya lingetemea kwanza maandalizi fulani labda ya chakula, au mavazi, au kushughulikia mahitaji mengine…lakini kwakua kusudi la Mungu lilimsukuma kwa nguvu wakamchukua Vilevile alivyo katika chombo Mpaka ng’ambo..hakuna kuoga, wala kupumzika, wala kuwatembelea marafiki na ndugu, ni kuunganisha ziara nyingine, sio kwamba alikuwa hachoki hapana alichoka sana, kuthibitisha hilo utaona akiwa katikati Ya safari ile alipitiwa na usingizi kwa sababu ya uchovu (4:38)

Hii inatuonyesha wazi utayari wa Kristo ambao uliathiri mpaka hali zake za kimwili.

Ni kutufundisha nini?

Kwasababu yeye ni yule yule jana na leo na hata Milele, utayari ule ule aliokuwa nao zamani anao hata leo.

Kristo haitaji maandalizi wala hali ya kimazingira, katika kutumika Na sisi. Ni rahisi Kudhani mpaka Bwana atende miujiza tunahitaji kwanza maandalizi ya Maombi na mifungo na mikesha, au mpaka Bwana amwokoe mtu tunahitaji tuwe na elimu nyingi ya biblia, au uzoefu kumbe si lazima..

Ni kweli mambo hayo ni muhimu katika baadhi ya mazingira lakini si yote. Anataka tuwe wepesi wa kumchukua yeye vilevile kama alivyo katika mazingira yoyote?

Yupo tayari kwenda na sisi popote, maadamu tu sisi tunakuwa tayari kumchukua katika safari zetu kwa imani. Hatupaswi kujali tutatolea Wapi fedha za huduma kumuhubiri Kristo.

Ikiwa umeokoka, ni nini unasubiri Usimtumikie Mungu wako?. Unataka uwe kama Martha ambaye alijisumbua na maandalizi mengi wakati lililohitajika ni moja tu, kumsikiliza Kristo? Kumchukua vilevile kama alivyo.

Yesu alipowaacha mitume hakuwapa mitaji ya maspika, au vyuo vya kusoma au majengo ya kuabudia…aliwaambia enendeni nami nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari. Msibebe fimbo wala mkoba, wala pesa kibindoni, wala kanzu mbili.(Mathayo 10:5-10)

Kwa tafsiri nyingine anasema nichukueni hivi hivi nilivyo, msijali hali yangu, nanyi mtaona Maajabu mbeleni.

Bwana atujalie kujua matamanio yake, ili tusizuiliwe kuhudumu naye popote, kwenye mazingira yoyote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Masomo mengine:

RABI, UNAKAA WAPI?

Yesu alipopanda kuomba kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine?

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

Print this post

Nini maana ya “mtu atachukua dhambi zake” (Walawi 5:17).

Swali: Neno la MUNGU linamaanisha nini linaposema “mtu atachukua dhambi yake au uovu wake”?

Jibu: Turejee andiko hilo..

Walawi 5:17 “Na kama mtu akifanya dhambi, na kutenda mambo hayo mojawapo ambayo Bwana alizuilia yasifanywe, ajapokuwa hakuyajua, ni mwenye hatia vivyo, NAYE ATACHUKUA UOVU WAKE”

Tusome tena..

Walawi 24:5 “Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake ATACHUKUA DHAMBI YAKE”.

Utalisoma tena neno kama hilo katika Walawi 7:18, Hesabu 9:13, Ezekieli 44:10-12..

Katika  Agano la kale Bwana MUNGU aliruhusu mtu kulipizwa kisasi endapo amefanya jambo la kusudi lililo baya.. kwamba UHAI kwa UHAI.. jino kwa jino..jicho kwa jicho..

Maana yake kama mtu amemkata mwenzake mkono naye pia ni lazima akatwe mkono, kama mtu amemwua mwenzake sharti naye pia auawe..

Walawi 24:17 “Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;

18 na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.

19 Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;

20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo”.

Lakini yapo matukio ambayo yalikuwa yakifanyika yanakuwa HAYANA KISASI!, kwamfano mtu aliyesikika kamtukana MUNGU au kulilaani jina la MUNGU, mtu huyo sheria ilikuwa ni kuuawa kwa kupigwa mawe, sasa wale watu waliomwua kwa kumpiga mawe baada ya kuthibitika uasi wa Yule mtu, hao hawawezi kulipwa kisasi kwamba nao wauawe kwasababu sheria imesema uhai kwa uhai.

La! Bali wataachwa hai,.. sasa hiko kitendo cha hawa wauaji kuachwa Hai na kutokulipwa kisasi ndio tafsiri yake kwamba “Yule aliyekufa kauchukua uovu/dhambi yake mwenyewe”.. maana yake hajaacha dhambi kwa waliomwua!.

Lakini laiti kama atauawa pasipo hatia na ikathibitika hivyo, basi wauaji wale watabeba dhambi ya mauaji hivyo nao pia watauawa, kama sheria isemavyo kwamba uhai kwa uhai na jino kwa jino. Sasa kitendo hiko cha kuuawa kwa kosa la mauaji yasiyo na hatia, ndicho kinachoitwa kubeba dhambi ya aliyekufa.

(kumbuka si kwamba watabeba makosa ya Yule mtu, la!, Yule mtu atabaki na dhambi zake alizozifanya.. bali hawa wauaji watabeba lile kosa moja tu la mauaji ya mtu asiye na hatia), hivyo watahukumiwa tu kama wauaji waliomwua mtu asiye na hatia.

Na lugha nyingine ya kubeba dhambi ya mtu ni kubeba damu ya mtu. Hivyo mahali popote katika biblia Bwana MUNGU anaposema kuwa “nitaitaka damu mikononi mwa mtu” maana yake ni hiyohiyo kwamba “kwamba atamhukumu muuaji kwa kosa la kumwua asiye na hatia”.. na anaposema damu yake itakuwa juu yake mwenyewe aliyefanya kosa, maana yake ni kwamba aliyeuawa hatalipiwa kisasi kwa waliomwua.

Zifuatazo ni baadhi ya dhambi ambazo mtu akizitenda basi alibeba dhambi zake mwenyewe, wala waliomwua hawakuwa na hatia ya kulipwa kisasi wala kushtakiwa.

  1. Kulikufuru jina la MUNGU (Soma Walawi 24:5).
  2. Ibada za sanamu/miungu (soma Kumbukumbu 13:6-12).
  3. Kutoishika pasaka (Hesabu 9:13).
  4. Kufumaniwa katika uzinzi.
  5. Kulala na mnyama wa aina yoyote au ndugu yoyote wa karibu.(Kutoka 22:19)
  6. Kumlaani mzazi (Kutoka 20:9)

Je hata sasa (Agano jipya) sheria hizi zipo?.

Katika Agano jipya hatuna sheria yoyote ya kisasi, Bwana YESU alitufundisha hilo katika Mathayo 5:38-41, ikiwa na maana kuwa hatujapewa ruhusa ya kumwua mtu au kulipiza kisasi bali kisasi ni juu ya Bwana (soma Warumi 12:19).

Kwahiyo kama hatujapewa ruhusa ya kulipa kisasi, au kutoa hukumu ya aina yoyote  kama katika kipindi cha agano la kwanza, basi maana yake ni kwamba mtu yoyote Yule alipaye kisasi atakuwa na hatia pasipo kujalisha makosa aliyoyafanya ndugu yake!..

Muuaji wa aina yoyote ile, atabeba kosa la mauaji, (Bwana ataitaka damu ya aliyemwua mikononi mwake).. hata kama amemwua mtu aliyemlaani MUNGU, bado ni kosa!..katika agano la kale haikuwa makosa lakini agano jipya ni kosa!.

Kwahiyo hatujapewa ruhusa ya kuua kwa kosa lolote lile, tukifanya hivyo tutakuwa na hatia na Bwana ataitaka damu ya aliyekufa mikononi mwetu.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa

Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)

VUNJA AGANO LA MAUTI.

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Print this post

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

Jibu: Turejee maandiko machache..

“Uhai” ni hali ya kuwa “HAI” (yaani kuishi) ili kiumbe kiwe kinaishi ni lazima kipumue, kile, kikue na hata kijongee. Hizo ndizo tabia chache za viumbe HAI,  Wanadamu, wanyama na mimea vyote vina uhai kwasababu vinapumua, vinaongezeka na pia kujongea.

Lakini “UZIMA” Umeenda mbali zaidi kuelezea UHAI wa kiroho ambao unapatikana kwa mtu kuwa na mahusiano na MUNGU.

Uhai unaelezea mwili lakini Uzima unaelezea roho. Mimea haina UZIMA bali ina UHAI.. wanyama hawana UZIMA bali wana UHAI maandiko yanaonyesha hivyo…

Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri UHAI WA MNYAMA WAKE; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Na UZIMA unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO,

Yohana 10:10 “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, kisha wawe nao tele”.

ikiwa na maana kuwa wanadamu yoyote aliye nje ya YESU KRISTO anao “Uhai” tu kama wanyama lakini hawana “Uzima”… anapumua, anakula, anatembea lakini akisha kufa hana UZIMA tena.. Lakini aliye ndani ya KRISTO, hata akiwa amekufa ataendelea kwasababu anao  UZIMA wa MILELE alioupokea kutoka kwa YESU.

Je unao uzima wa milele ndani yako?…Je YESU ni sehemu ya maisha yako?

Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape UZIMA WA MILELE.

3 Na UZIMA WA MILELE ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Uzao wa Ibrahimu unamilikije mlango wa adui? (Mwanzo 22:17)

Print this post

Utakuwa Kichwa na si Mkia maana yake nini? (Kumbukumbu 28:13).

Jibu: Turejee..

Kumbukumbu 28:13 “Bwana atakufanya kuwa KICHWA, WALA SI MKIA; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;

14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia”.

Unaweza kutafakari kwanini hajasema Utakuwa KICHWA na wala si MGUU!.. kwasababu kichwa kipo juu na miguu ipo chini, na ndio sehemu ya mwisho ya mwili wa mtu… lakini badala yake anasema Utakuwa “kichwa”na si ”mkia”. Je kuna sifa gani mbaya katika mkia?

Sasa sote tunajua kuwa mwanadamu hajaumbwa na Mkia, bali kichwa tu peke yake, hivyo bila shaka hapo biblia imejaribu kutumia umbile la wanyama badala ya la mtu kufunua hali  ya mtu atakayemcha MUNGU na yule ambaye hatataka kumcha MUNGU, kwasababu wanyama ndio wenye kichwa na mkia na si mwanadamu.

Sasa kichwa cha mnyama yoyote ndicho kinachoongoza mwili wote, na ndio sehemu ya kwanza ya mwili wa mnyama. Lakini Mkia ni sehemu ya mwisho kabisa ya mwili wa mnyama, na sehemu hii imeungana na sehemu ya haja  kubwa ya mnyama. Kwahiyo wakati kichwa kinapokea chakula fresh, mkia unapokea uchafu (kinyesi).

Ikiwa na maana kuwa watu wanaomcha MUNGU, watapokea vilivyo  visafi na vya kwanza na vizuri, na wasiomcha MUNGU ni kinyume chake, watapokea vile vya mwisho na visivyo na heshima vilivyo haribika.

Pia watu wanaomcha MUNGU watakuwa wa kwanza, kulingana na sifa ya kichwa, lakini wasiomcha MUNGU watakuwa wa mwisho kama ilivyo nafasi ya mkia katika mwili wa mnyama, sasa hebu tafakari unakuwa wa mwisho na bado unapokea vilivyo vichafu (mfano wa vinyesi)..ni jambo baya sana..

Ni tahadhari kwetu tunaoishi, kwamba tuwekeze nguvu kubwa katika kumtafuta MUNGU ikiwa tutataka tuwe vichwa, lakini tusipotaka kufanya hivyo, maandiko yanasema tutakuwa mkia na maadui zetu MUNGU atawaweka juu yetu na sisi tutakuwa wa mwisho.

Kumbukumbu 28:43 “Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.

44 Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; YEYE ATAKUWA NI KICHWA, WEWE UTAKUWA MKIA.

45 Na laana hizi zote zitakujilia juu yako, zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza”

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

LAANA NI NINI KIBIBLIA?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

NI SAHIHI KABISA, HUU SI WAKATI WA TINI!

Maana ya Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao

Print this post

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

Ndio Maandiko yanatuonyesha kuwa tutatambuana tukifika mbinguni. Ifahamike kuwa fahamu zetu au kumbukumbu zetu za hapa ulimwenguni hazitaondolewa kabisa, tufikapo mbinguni, kila pito tulipitialo, na kila jambo lililowekwa na Mungu sasa hapa duniani, lina sehemu kubwa ya fundisho la maisha yajayo. Hivyo maisha ya duniani yana thamani kama yalivyo tu maisha yatakayokuja. Ndio maana kabla ya kuingia kule ilitupaswa kwanza tupitie hapa.

Zipo sehemu kadha wa kadha katika maandiko zinatuthibitishia kuwa  tutatambuana kule mbinguni.

1). Kufufuka kwa Yesu.

Tunaona Bwana wetu Yesu Kristo alipofufuka na mwili mpya wa utukufu, aliweza kutambuliwa . Kwamfano siku ile ya kwanza ya juma Mariamu Magdalena, akiwa pale kaburini alimtambua Bwana Yesu alipozungumza naye.

Yohana 20: 16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).

2) Mlima wa Mageuzi

Halikadhalika wakati ule Bwana Yesu anawachukua mitume wake watatu Petro, Yohana na Yakobo na kuwapeleka juu ya mlima ule mrefu, na kuwabadilikia sura, kama tunavyosoma watu wawili walitokea ambao ni Musa na Eliya.

Mitume waliweza kuwatambua ijapokuwa hawakuwahi  kuwaona uso kwa uso hapo kabla.

Mathayo 17:3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.

3) Fundisho la Paulo juu ya ufufuo

1Wakorintho 15:42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; 43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko

Mstari huo unatuonyesha  kuwa hatutaondolewa uhalisia wetu Tutabakia kuwa sisi sisi., isipokuwa tutavikwa utukufu wa juu zaidi. Maana yake ni kuwa tutatambuana.

4) Ahadi ya kukutanishwa tena

1Wathesalonike 4:16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana

hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

Tutarejeshwa, na kuonana. Hivyo kwa mujibu wa vifungu hivyo katika ulimwengu ujao sote tutajuana na kufahamiana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.

Sheria ni agizo la shuruti linalotolewa na mamlaka kuu…, na KANUNI ni mwongozo au utaratibu maalumu unaotolewa kuhusiana na utekelezaji wa sheria iliyowekwa au agizo lililotolewa..

Kwamfano katika biblia kulikuwa na Sheria ya “kuishika  Pasaka” lakini ilikuwepo pia kanuni (ambayo ni mwongozo wa namna ya kuiadhimisha hiyo siku), kwamba ni lazima kwanza iwe siku  ya 14 ya mwezi wa kwanza wa kalenda ya kiyahudi, na pia siku hiyo ni lazima achinjwe mwana kondoo na kumwoka motoni na aliwe pamoja na mboga zenye uchungu n.k (Soma Kutoka 12:1-12).

Sasa huo mwongozo wote wa jinsi ya kuiadhimisha hiyo siku ndio unaoitwa Kanuni, lakini sheria ni hiyo moja tu kwamba Waishike Pasaka..

Hesabu 9:14 “Na kama mgeni akiketi kati yenu ugenini, naye ataka kuishika Pasaka kwa Bwana; kama HIYO SHERIA YA PASAKA ILIVYO, na kama amri yake ilivyo, ndivyo atakavyofanya; MTAKUWA NA SHERIA MOJA, kwa huyo aliye mgeni, na kwa huyo aliyezaliwa katika nchi”.

Katika biblia kila Amri au sheria ilikuwa na Kanuni zake na hukumu zake.

Tunayo sheria na amri ya Kristo pia ambayo ni UPENDO, lakini huu upendo unao kanunini…ni lazima tuzitafutae kanuni za upendo  na tuzijue.

Isaya 28:13 “Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?

PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?

Nini tofauti kati ya kileo na divai?

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?

 

Print this post