Jina la YESU KRISTO libarikiwe. Karibu katika kuyatafakari maneno ya Uzima,
Si kila sauti inayokujia kwa faraja, ina lengo la kukupa faraja.. si kila sauti inayokujia kwa kukupa matumaini ina lengo la kukupa matumaini mwisho wake. Hebu tujifunze juu ya Bwana wetu YESU KRISTO, alivyoweza kuzipambanua roho..
Mathayo 16:12 “ Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka. 22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. 23 Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, Shetani; u kikwazo kwangu; MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU.”
Mathayo 16:12 “ Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.
22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
23 Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, Shetani; u kikwazo kwangu; MAANA
HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU.”
Nataka tuone hilo neno “MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU.”.. Kumbe mawazo ya shetani siku zote sio ya mapepo, wala ya mashetani yake bali ya wanadamu!.. Maana yake shetani anaangalia ni nini wanadamu wanakipenda zaidi na kuvitamani na kupitia vitu wanadamu wanavyovipenda na kuvitamani na kuvitafuta ndio vitu hivyo hivyo anatumia kuwaangusha chini katika hatua za mwanzo.
Hapa anajua mwanadamu anapenda “faraja na kutiwa moyo” anakuja kwa gia hiyo hiyo kwa Bwana YESU, akitaka kumfariji kwamba “hatapata mateso, hatakwenda msalabani”.. kwsababu anajua hayo ndio mawazo ya wanadamu siku zote, kutafuta faraja, kutiwa moyo n.k.
Lakini kwasababu YESU KRISTO ni “MWAMBA MGUMU”.. anayajua mawazo ya kila mtu kabla hata hajaambiwa, pale pale alimwona shetani ndani ya Petro, na kumkemea..
Ni kanuni hiyo hiyo shetani anaiendeleza hadi leo, hajabadilika, shetani anayasoma mawazo ya wanadamu wanataka nini na kupenda nini, anajua wanadamu , wanapenda kutiwa moyo, hawapendi kukemewa kemewa, hawapendi kukatishwa tamaa..
Sasa ili baadaye afanikiwe kumkatisha mtu tamaa kikweli kweli, ni lazima aanze kama na kwa kumfariji sasahivi, ili baadaye amvunje moyo kweli kweli, na asiweze kusimama tena, ni lazima aanze sasa hivi kama kwa kumtia moyo..ndicho alichokuwa anataka kujaribu kukifanya kwa Bwana YESU lakini alishindwa.
>Biblia imesema imetupasa “Kuokoka” lakini shetani atakuambia “Bado wakati ngoja kwanza utafute maisha”
>Biblia imesema imetupasa “Kuwa waombaji” lakini shetani atakuambia “wewe upo bize sana, unachoka na kazi”
>Biblia imesema imetupasa “Kuhudhuria kanisani kila jumapili na hata katikati ya wiki (Waebrania 10:25)” lakini shetani atakuambia “kazi zimekuwa nyingi, Mungu atakuelewa tu”.. Ni kama neno la faraja lakini mwisho wake ni huzuni kubwa.
>Biblia imesema imetupasa “Kumtumikia Mungu (Yohana 9:4)” lakini shetani atakuambia “bado wakati, wapo wanaokuombea”
> Biblia imesema imetupasa “kujikana nafsi na kubeba msalaba tunapookoka”.. Lakini shetani atakuambia “usiogope siku moja utajikana tu, ila sasahivi endelea tu kuwa hivo hivo vuguvugu, hakuna mtakatifu duniani”
> Biblia inasema “usiwe mzinzi, na ukizini utakufa” lakini shetani anakuambia hutapata madhara wala hutakufa wapo wanaofanya na wanaishi mpaka leo..
Hayo yote ni mawazo ya shetani ndugu, ambayo ni ya wanadamu!.. Ni lazima tuwe makini katika hili, si kila sauti au wazo linalokuja kwa faraja na matumaini ni la MUNGU, angalia na pima je! Hilo wazo linakubaliana na wazo la MUNGU, kama linakinzana na Neno la MUNGU basi hata kama linakuja kwa sauti ya faraja kiasi gani usisikilize!.. bali sema “NENDA NYUMA YANGU SHETANI KWANI HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU BALI WANADAMU”..
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je wakati Bwana YESU anazaliwa shetani alikuwa amefungwa?
SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.
Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?
Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?
Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)
Print this post
1 Petro 1:23-25
[23]Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. [24]Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka; [25]Bali Neno la Bwana hudumu hata milele. Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
[23]Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.
[24]Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka;
[25]Bali Neno la Bwana hudumu hata milele.
Na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
Neno la Mungu linatuonyesha mtu aliyeokoka, anatambulika kuwa amezaliwa mara ya pili kwa mbegu isiyo haribika…lakini wengi hawajui makusudi ya kuzaliwa kwa mbegu hiyo ni nini?
Kabla ya kuona mbegu isiyo haribika, ifahamu kwanza mbegu iharibikayo ni ipi..
Katika habari hiyo tunaonyeshwa mbegu iharibikayo mfano wake ni ile ya mwanadamu .maana yake ni kuwa wewe ulizaliwa kwa mbegu ambayo inaanza katika mtoto, kisha ujana wenye nguvu, lakini baadaye utaishia na kuchakaa, na kuchoka kwa kuishiwa nguvu na hatimaye kufa…ndio hapo anasema mwili wote ni kama nyasi hukauka na kuanguka…kwasababu asili ya mbegu hii si ya kudumu daima.
Vivyo hivyo na mbegu nyingine zote za hapa duniani mfano, za wanyama, samaki, mimea zote ni mbegu ziharibikazo huisha ubora kulingana na wakati.
Lakini ukizaliwa kwa mbegu isiyo haribika maana yake ni kuwa ubora wako haupungui wala hauishi kulingana na wakati ..
Mtu aliyezaliwa kwa mbegu hii ambayo ni Neno la Mungu…huwa hazeeki rohoni, haishiwi nguvu wala hafi kiroho..
Lakini utashangaa mtu anasema kazaliwa mara ya pili, hapo mwanzoni alianza vizuri sana na Bwana, anaomba, anasoma Neno, amesimama, anamtumikia Bwana kwa bidii na uaminifu, lakini baada ya muda anaanza kupoa, hatimaye anaacha hata kuabudu na mwisho anakufa kiroho….miaka miwili nyuma alikuwa ameokoka lakini leo ni mtu mwingine kabisa…hapo ni lazima ujiulize je huyu mtu alizaliwa kwa mbegu ipi?
Kama ni mbegu isiyoharibika mbona wokovu wake unaharibika kulingana na wakati ..kikawaida mwamini kwenye maisha ya kiroho hufanyika upya siku baada ya siku, huama kutoka utukufu mmoja hata mwingine imani moja hata nyingine…lakini wewe unaharibika siku baada ya siku, je wewe ni mbegu gani?
2 Wakorintho 3:18
[18]Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho.
2 Wakorintho 4:16
[16]Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Ikiwa unajiona wewe umezaliwa kwa mbegu isiyoharibika, basi onyesha hivyo kwa ubora wako wa kiroho na kiiamani kila siku…ikiwa ni mchungaji onyesha mwendelezo wa kulisimamia kundi la Mungu katika nyakati zote iwe ni ngumu na nyepesi, ikiwa ni mwinjilisti, hupaswi kuacha kuhubiri maisha yako yote, ikiwa ni mhudumu wa kanisani, simama katika nafasi yako kwa ubora wote…usiseme yatosha, usiseme nimechoka,.kwasababu hukuzaliwa kwa mbegu ichokayo, isinyaayo, bali kwa Neno la Mungu lidumulo milele. Ikiwa ni mwombaji, usianze kusema hapo zamani mimi nilikuwa nina uimara kimaombi, kinyume chake onyesha vitendo, hata sasa moto wako ni ule ule tena na zaidi.
Unyesha ubora huo na amani ya Bwana iwe pamoja nawe.
Maran Atha.
Shuhuda za Mungu ni zipi?
Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?
TIA MIZIZI CHINI, ILI UZAE MATUNDA JUU.
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lilo njia na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).
Je! Umeokoka na kuna dhambi ambayo bado hujaiacha na hujui ufanye nini?.. Twende pamoja katika ujumbe huu utapata kitu au suluhisho la tatizo ulilo nalo.
Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa, mtu anapoamua kwa dhati kabisa kutoka moyoni mwake kumfuata YESU, basi zile dhambi zote zilizokuwa zinamtesa ni lazima zife ndani yake!, lakini inapotokea mtu kaokoka lakini bado mambo ya kale yanamsumbua kuna SHIDA!
Fanya hivi ili upone hilo tatizo… ACHA HIYO DHAMBI!..ACHA KUITUMIA HIYO DHAMBI!. Huenda bado hujaelewa.. ni hivi.. ACHA HIYO DHAMBI.
Kitu chochote ukiacha kukitumia kinaisha nguvu na hatimaye kinakufa kabisa/kinapotea…hata chuma kisipotumika kinapata kutu na hatimaye kuharibika kabisa..Moto usipochochowa unakufa (Soma Mithali 26:20) na Dhambi isipotumika inakufa…Hiyo ndio tabia ya dhambi wengi tusiyoijua.. kuwa dhambi ina tabia ya KUFA.
Warumi 6:11 “Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa WAFU KWA DHAMBI na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu”.
Ukitaka kushinda dhambi ya “Kujichua”.. “Acha Kujichua”… Ukitaka kuacha dhambi ya Uzinzi acha uzinzi, ukitaka kuacha dhambi ya ulevi, acha ulevi, ukitaka kuacha matusi, acha kutukana, ukitaka kuacha hasira acha hasira..
Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye NA KUZIACHA atapata rehema”.
Utauliza.. “nitaachaje”.. Wazo linapokuja kichwani la kwenda kufanya hivyo, unaanza kulikataa likiwa huko huko kichwani, na kukubaliana na matokeo ya maumivu, kwasababu inakuhitaji kuingia gharama kushindani na dhambi….lakini ukijilegeza na kuitii dhambi itazidi kustawi ndani yako.
Ukishaikataa kichwani, ni wakati wa kuutiisha mwili wako, na kusema utafanya unachokisema wewe na unachokitaka na sio mwili unachokitaka!… nakuhakikishia ukimaanisha kufanya hivyo, dhambi itakosa nguvu ndani yako!.. Kwani unapoamka kila siku asubuhi na kukatisha usingizi wako ili uwahi kwenye majukumu yako, mwili huwa unapenda??..
Huwa haupendi katika siku za mwanzo lakini unakuwa unajilazimisha tu…mpaka ile ratiba inapokaa akilini kiasi kwamba unafika wakati ukifika tu ule muda wa kuamka usingizi wenyewe unakata..kwanini!..ni kwasababu tayari umeshauua usingizi majira yale uliyozoea kuamka.. kwahiyo ukifika tu huo wakati hauhitaji kengele, tayari kengele ipo kwenye ubongo wako na usingizi unakuwa haupo huo muda..
Na dhambi ni hivyo hivyo, unaiacha na kuilazimisha isikae maishani mwako, na mwisho itakufa tu… mahali pale ulipozoa kukutana ili kulewa, zikifika zile saa hata kiu haipo, mitaa ambayo ulikuwa ukikatiza ni lazima utamani kulewa, sasa utaikatiza bila shida yoyote.
Aina ya watu ambao ulikuwa ukiwaona huwezi kuvumilia, unawaka tamaa…utafika wakati utawaona ni watu wa kawaida sana, tena utajishangaa ulikuwa ni mtu wa namna gani?
Rushwa ulizokuwa unakula, ambazo huwezi kufanya jambo bila kuhonga, utajishangaa hutamani tena kuchukua/kutoa rushwa..
Lakini ni lazima uingie gharama katika hatua za awali, usikubali kujilegeza.. na kusubiri muujiza wa wewe kuacha hayo…amua kubadilika kwa KUACHA DHAMBI.. ACHA DHAMBI, ACHA DHAMBI..Hakuna dawa nyingine zaidi ya hii ACHA!, na MUNGU atakusaidia..
Shalom.
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?
Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?
NITAACHAJE DHAMBI?.
Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.
SWALI: Mara nyingi biblia inataja “shuhuda za Mungu” Je hizi shuhuda ni zipi?
Mfano katika vifungu vifuatavyo Neno hilo utaliona;
Zaburi 119:2
[2]Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.
Zaburi 119:22
[22]Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
Zaburi 119: 24
[24]Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.
Zaburi 119:99
[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
Soma pia…Zab 119:119, 144, 132:12
Hizi shuhuda ni zipi?
Shuhuda ni neno linalozaa ushuhuda au kushuhudia.
Ni kitendo cha kuthibitisha ukweli wa jambo.
Kwamfano nikisema yule “mtu ni mkarimu”. Hapo nimemshuhudia kwasababu nimeona kitu hicho ndani yake, aidha amenitendea mimi ukarimu au kamtendea mwingine..
Tofauti na kama angejisemea mwenyewe..
Hivyo Mungu naye ana vitu amevihakiki kuwa ni kweli, na hizo ndizo zinazoitwa shuhuda zake..
Mpaka jambo Mungu amelihakiki mwenyewe ni kutuhakikishia kuwa hatupotei tukilifuata, tofauti na kama tungeshuhudiwa na wanadamu…kwasababu shuhuda za wanadamu zina udanganyifu mwingi nyuma yake.
Yesu Kristo ni mwana wa Mungu na ndiye uzima wetu.
1 Yohana 5:7-12
[7]Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 9… Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. [10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. [11]Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. [12]Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
[7]Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
9… Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe.
[10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.
[11]Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.
[12]Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
Huu ndio ushuhuda mkuu wa Mungu, na huu ndio tuliopewa tuuhubiri kwa ulimwengu pia kwamba kwa Yesu kuna ukombozi, na uzima..
Matendo ya Mitume 4:33
[33]Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote.
Sisi (tulioamini) ni wana wa Mungu Huu ni ushuhuda mwingine wa Mungu mwenyewe ndani yetu kupitia Roho wake Mtakatifu.
Warumi 8:16-17
[16]Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; [17]na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
[16]Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
[17]na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
Si Kristo tu peke yake ni mwana wa Mungu, na sisi pia tunapomwamini tunafanyika watoto wake (Yohana 1:12 )watoto wa Mungu mfano wa Kristo.
Hivyo tunapopitia mateso kama yeye, hatupaswi kuwa na hofu au manung’uniko, kinyume chake ndio tujipige vifua vyetu kushangilia, kwani hata yule wa pekee(Yesu), aliyapitia hayo…kwasababu kama vile alivyopata mateso na alivyorithi utukufu vivyo hivyo na sisi tutarithi utukufu wake.
Mungu anataka tutembee kwa ujasiri hapa duniani, tusiishi kama yatima, tuishi tukijua kuwa tunaye Baba mbinguni anayetutazama na kujishughulisha sana na mambo yetu yote, kwasababu yeye mwenye ametuthibitisha kuwa sisi ni wana wake…Kama yeye ametuthibitisha nafsi yako kwanini ipinge? Wanadamu kwanini wapinge, ulimwengu kwanini upinge?
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa tunaposema tumezishika shuhuda zake maana yake ni kuwa tumeamini wokovu na uzima utokao kwa Kristo Yesu, lakini pia tumekubali kuwa wana wa Mungu, yaani tukubali dhiki kwa ajili ya jina lake, tuishipo maisha ya kumpendeza yeye, lakini pia kupokea tumaini la utukufu lililo mbele yetu.
DHAMBI HAIWEZI KUKAA NA MSHAHARA WAKO.
USHUHUDA WA RICKY:
FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.
WhatsApp
Jibu: Turejee..
Kumbukumbu la Torati 11:15 “Nami nitakupa nyasi katika MAVUE yako kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
“Mavue” ni kiswahili kingine cha “mashamba”….shamba likiwa moja linaitwa “VUE” yakiwa mengi “MAVUE”.
Kwahiyo hapo anaposema “Nitakupa nyasi katika mavue yako”.…maana yake nitakupa nyasi katika mashamba yako.
Hii ni ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli, na ni ahadi ya MUNGU kwetu pia, ikiwa tutayashinda
Tuanzie ule mstari wa 13..
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote, 14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako. 15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Kumbukumbu 11:13-15 “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote,
14 ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.
15 Nami nitakupa nyasi katika MAVUE YAKO kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba”.
Neno hili pia tunalisoma katika
Maandiko yafuatayo…
1Samweli 25:15 na 1Samweli 30:11.
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?..
Kama bado unasubiri nini mpendwa?..Fahamu ya kuwa kwa jinsi unavyozidi kuendelea kuishi maisha ya dhambi
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Neno utakaso mara nyingi, tunalitazama katika jicho la Mungu kututakasa sisi(1Thes 5:23), lakini pia sisi kujitakasa wenyewe (1Petro 1:22), lakini tunasahau kuwa Kristo naye tunamtakasa… maandiko yanasema hivyo katika,
1 Petro 3:14
[14]Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.
Kama Kristo anatakaswa? Swali ni je! Anatakaswaje wakati yeye ni mkamilifu?
Hapo anasema;
‘mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu’.
Kumbe ni mioyoni mwetu, sio kwamba yeye mwenyewe tumtakase mahali alipo(hawezi kutakaswa kwasababu yeye ni msafi). Mioyo yetu ndio humfanya aonekane kivingine.
Kutakasa ni kukifanya kitu kiwe kisafi au kiwe kikamilifu tena, kurejee katika hadhi yake iliyopotezwa.
Sasa kumtakasa Yesu moyoni, ni sawa na kumfanya Yesu awe jasiri tena, ajae utukufu wake, ajawe na raha na fahari yote ndani ya mtu.
Haya ni mambo ambayo ukiyatenda/ kuyakubali basi unamtakasa sana Yesu moyoni mwako
Sawasawa na hilo andiko hapo juu anasema..
Zipo nyakati ambazo utachukiwa bure kwasababu umekataa uongo, au utafukuzwa kazi kwasababu umekataa rushwa, au utafungwa kwasababu unahubiri injili ,au utapigwa kwasababu unakemea dhambi..
Nyakati kama hizi wengine huzikwepa, na kuamua kusimama na maovu ili tu kuepusha madhara yatakawapata… hawajui kuwa wanamweka Kristo kando.
Matokeo yake Yesu anakosa kutukuzwa ndani yetu, kwasababu yeye naye alikubali kuteswa kwa kusimamia ukweli na haki, akapigwa, akasulubiwa kwa kifo cha aibu.. Hivyo atakapoona watu pia wanafuata Nyayo zake, hutakasika sana, hujitukuza sana ndani ya huyo mtu, hujithibitisha kuwa kazi yake kamilifu huendelea kumulika gizani.
Hivyo usikwepe mapito yenye gharama, wala usihuzunishwe nayo maadamu ni haki unayoisimamia. Mtakase Kristo.
Lakini pia..
Waefeso 1:6-7
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. [7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.
[7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
Kwa jinsi unavyoitambua kazi ya Kristo aliyoitenda kwa ajili yako pale msalabani kwamba kwa kupigwa kwake umepokea neema na ukombozi kupitia msamaha wa dhambi ndivyo unavyomtakasa Kristo moyoni mwako.
Tumia muda mwingi kutafakari juu ya neema ya wokovu, kisha msifu na kumtukuza na kumshukuru juu ya hilo. Kristo anapoona umeithamini kazi yake, huinuka sana moyoni mwako.
Utakumbuka yule mwanamke kahaba na Miriamu ndugu yake Martha walivunja vibweta vya marhamu vyenye thamani nyingi, wakampaka Yesu kichwani na miguuni, mpaka wengine wakasema ni upotevu mkubwa sana..lakini Yesu alipoona alisema wametenda kazi njema juu yake, (Marko 14:3-9, Luka 7:36-50).
Jifunze kumtolea Kristo sadaka zaidi hata kipimo chako cha sikuzote, sio kwamba unamshawishi Yesu kwa vitu, (yeye hashawishi na hivyo)..Lakini anapendezwa sana, na watoaji, anatakasika sana pale unapofanya kitu cha ziada kwa ajili ya Mungu wako. Jifunze kutoa sana sadaka.
Yesu anajaa utukufu na waombaji…utakumbuka alikuwa na mitume kumi na wawili…lakini waliokuwa tayari kudumu naye katika masafa ya ndani ya kimaombi walikuwa ni watatu; yaani Petro Yohana na Yakobo.
Na wakati ule alipopanda juu ya ule mlima mrefu(Mathayo 17), ghafla walimwona katika utukufu mwingine wa ajabu, nguo zake zilikuwa zikimeta-meta kwa weupe mkuu.. wakashangaa na kuingiwa na hofu..
Lakini Yesu asingeweza kubadilika mbele yao, kama wangekuwa mbali na yeye katika maombi.
Hivyo unapozama sana katika uombaji, ndivyo unavyomtakasa Kristo ndani yako. Anajiona safi na mkamilifu.
Kwa hitimisho ni kuwa, unapokubali mateso pamoja na Yesu, unapo msifu sana kwa kazi yake ya msalaba, unapotoa sadaka zako nyingi na unapokuwa mwombaji.
Moyoni unahesabika kuwa unamtakasa Bwana wako sana.
Shalom, Mungu akubariki.
WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.
Kanisa kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.
SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI
Swali: Je nikiomba kazi kwa mwaka mmoja na ikatokea fursa ambayo inanitaka nitoe rushwa kidogo ili niingie kazini, je hilo ni Jibu la Maombi yangu, au ni jaribu?
Jibu: Hilo si jibu la Maombi, bali ni “Jaribu” linaloletwa na ibilisi mbele yako. Majibu ya Maombi hayana njia za mkato, yanakuwa yamenyooka na yenye kibali.
Lakini inapotokea tunaomba jambo kwa Mungu atutendee, halafu inatokea fursa nyingine iliyo kinyume na Neno la MUNGU, hilo ni jaribu na tunapaswa tulishindwe.
Mfano mwingine ni pale mtu ameomba hitaji fulani kwa Mungu labda fedha ya kodi, halafu inatokea fursa ya wizi, utakaokamilisha kile kiasi.. sasa hiyo fursa si kutoka kwa MUNGU hata kama inakupa wepesi mkubwa wa kupata kile kiasi, bali ni Jaribu la maombi yako, na ni lazima kulishinda.
Au unaomba mume halafu anakuja Mume wa Mtu kutaka kukuoa, hayo sio majibu ya maombi bali ni majaribu..
Na yapo mambo mengine mengi, yanayokuja kwa sura ya Majibu ya Maombi, lakini nyuma yake ni Majaribu ya maombi.
Sasa ni kwa namna gani tunaweza kutofautisha Majibu na Majaribu?.
Hakuna njia nyingine zaidi ya “KULIJUA NENO LA MUNGU”..Na hatulijui Neno la Mungu kwa kukariri mistari ya Biblia, au kuelezewa bali kwa “KUJIFUNZA BIBLIA”.
Huwezi kujua dhambi ni nini kama hauijui Biblia..
Warumi 7:7 “Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani”.
Pia hatutaweza kuyajua majaribu ya ibilisi kama hatutalijua Neno la MUNGU ndani ya Biblia takatifu.
Weka desturi za kusoma Biblia kwa kujifunza, usiwekeze tu peke yake katika Maombi na ukaliacha Neno la Mungu pembeni, ukiwa mtu wa namna hiyo, ibilisi atakuletea majaribu ukidhani ndio majibu ya maombi yako, na kufanya mfungo wako au maombi yako kuwa si bure.
Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.
NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.
NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?
KISIMA BADO KINA MAJI, KIFUKUE TENA.
FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.
Kama ni msomaji wa biblia, Neno hilo utakutana nalo katika baadhi ya vifungu kwenye Zaburi..
Zaburi 11:2
[2]Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Zaburi 21:12
[12]Kwa maana utawafanya kukupa kisogo, Kwa upote wa uta wako ukiwaelekezea mishale.
Upote ni ule uzi mwembamba unaofungwa kwenye uta, ambao mshale huwekwa pale kwa kuvutwa na kurushwa.
Upote hutengenezwa kwa ngozi na wakati mwingine kamba za mimea imara.. ni lazima utengenezwe kwa malighafi imara, ili isikatike pale unapovutwa.
Kwasababu hizi ni zana za kivita…kiroho hufunua pale mbili. Adui hutengeneza upote wake, ambao hurushia watu mishale ya moto ili kuwaua kiimani (Waefeso 6:16), ili kuweza kuishinda, biblia inatufundisha daima tuibebe ngao ya Imani.
Lakini pia Bwana Yesu anao upote wake ambao kwa huo hutupa silaha zake kwa adui zetu, sawasawa na hiyo Zaburi 21:12, Na silaha za Kristo zina nguvu sana sio tu kumlenga adui lakini pia kuangusha ngome.
Maboma na makao ya shetani.
2 Wakorintho 10:4-5
[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) [5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
[5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
Lakini Nguvu ya silaha hizi hutegemea na hali ya mtu kiroho katika maeneo matatu;
1) kimaombi,
2)Utakatifu
3) Injili.
Mwamini wa namna hii ambaye huchukia dhambi, huubiri injili na huzingatia kudumu katika maombi ya masafa,
Kiroho ni askari imara na mwenye silaha zenye nguvu sana, ziwezazo kumuharibu ibilisi.
Kuwa askari kamili wa Kristo
Mtambo/mitambo ni nini kibiblia?
Na kipenu ni nini (Isaya 1:8)
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24