Uele ni nini katika biblia? (Zaburi 91:6)

Uele ni nini katika biblia? (Zaburi 91:6)

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 5..

Zaburi 91:5 “Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,

6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri”.

“Uele” ni janga linaloleta mauti linaloweza kumpata mtu.. ajali ya gari ni mfano wa Uele, Ajali ya kuzama kwenye maji ni mfano wa “Uele”, janga la kuungua moto mpaka kufa ni mfano wa “Uele”.

Maandiko yanatufundisha kuwa wote wamtumainio Bwana, na kumkimbilia na kumfanya kuwa ngome na msaada, hawatakuwa na hofu na majanga hayo, kwani Mungu ni ngome ya wote wanaomcha, naye ndiye awaokoaye na majanga.

Zaburi 121:4 “Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5 BWANA ndiye mlinzi wako; BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele”.

Je una hofu na UELE?..Mpokee Yesu kwa kutubu dhambi na kujazwa Roho Mtakatifu, naye atakupa furaha nawe utaishi maisha ya raha na ya utulivu.

Zaburi 127:2 “……Yeye humpa mpenzi wake usingizi”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA AJALI, KUNAMAANISHA NINI?

Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments