Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Karibu tujifunze Neno la Mungu…Taa iongozayo miguu yetu na Mwanga wa njia zetu (Zab.119:105).
Karibia kila tukio linalotokea duniani baya au jema huwa linameruhusiwa na Mungu, hakuna kitu hata kimoja kinaweza kuendelea chini ya mbingu kama hakijaruhusiwa na Mamlaka iliyo kuu (yaani ya mbinguni). Utauliza hata zile ajali tunazoziona zimeruhusiwa zitokee?..jibu ni ndio…utauliza tena hata vifo vyote vya kikatili pamoja na shida na magonjwa ni Mungu kayaruhusu yatokee…jibu ni Ndio!…Mungu muumba wa Mbingu na nchi, aliyeumba vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana dunia haijamshinda kiasi kwamba jambo Fulani linaweza kutokea pasipo ridhaa yake…Tukilifahamu vizuri jambo hili litatufanya tumtazame Mungu kwa jicho lingine.
Sasa kwanini anaruhusu vimbunga juu ya watu wasiomjua yeye…ni kwasababu ya maasi na maovu ya watu… na kwanini anaruhusu vimbunga juu ya watu wake wanaomjua yeye?…ni kwasababu ile ile kama alivyovileta kwa mtumishi wake Ayubu.
Siku zote shetani hawezi kujiamulia kufanya jambo lolote kabla halijamfikia kwanza Mungu, lipitishwe, Tunaweza kuona jambo hilo katika kitabu cha Ayubu.
Ayubu 1:7 ‘Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. 8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. 9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? 10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. 11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako. 12 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana’.
Ayubu 1:7 ‘Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.
12 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana’.
Unaona shetani hafanyi jambo lolote pasipo idhini ya Mungu..
Shetani anapompiga mtu kwa magonjwa na dhiki na tabu…cha kuangalia hapo sio kwenda kupambana na shetani..hapana! cha kufanya hapo ni kwenda kutafuta chanzo cha mambo hayo yote ni nini? Na ukishagundua kuwa ni Mungu karuhusu ndipo unapotakiwa kupoteza muda mwingi kumtafuta yeye kuliko kupambana na shetani…ili ujue sababu ya yeye kuyaruhusu hayo ni nini…kwasababu ukiacha kumwangalia Mungu na kupambana na shetani hutamweza hata kidogo…kwasababu yeye anafanya kazi kwa kibali maalumu kutoka juu na ana nguvu kuliko wewe..
Leo utaona mtu anaumwa na ugonjwa usiojulikana pengine kalogwa anatafuta kwenda kuombewa na kutafuta mchawi wake ni nani…anahangaika kwenda kukemea huo ugonjwa umtoke au huo uchawi umrudie mbaya wake na kupambana na shetani…lakini pasipo kujua kuwa mpaka ule ugonjwa umempata tayari Mungu mwenyewe alisharuhusu jambo hilo juu ya mwili wake…hivyo pa kwenda kutafuta suluhisho sio pengine zaidi ya kwa Mungu…
Ndio hapo itakubidi uende kwa Mungu kwa unnyenyekevu na magoti..Na kumwuliza Bwana sababu ya mambo haya yote ni nini? Ndipo Bwana atakufunulia…pengine Maisha yako si masafi mbele zake hivyo ameyaruhusu hayo shetani akupige ili wewe umrudie yeye na utakapotubu na kuyasafisha Maisha yako hilo tatizo linaondoka pasipo hata kuwekewa mkono na mtu yeyote…Au kama Maisha yako yapo sawa basi ameruhusu tu upitie hayo ili kukupeleka kwenye kiwango kingine cha kiroho kama alivyofanya kwa mtumishi wake Ayubu..nk zipo sababu nyingi.
Hebu fikiria endapo Ayubu angeacha kumfikiria Mungu na kuanza kukemea wachawi na mapepo yaliyowaua wanawe, au angeanza kutanga tanga huku na huko kusaka watumishi wamfanyie maombi ya kufunguliwa kwenye vifungo vya mikosi na laana na kupakwa mafuta angefikia wapi? Bila shaka angepoteza dira kabisa ya kujua sababu ya yeye kuyapitia hayo ni nini.
Kwahiyo kila kitu hata kama tunauhakika ni shetani katekeleza, tujue kuwa ni Mungu karuhusu shetani afanye hayo kwa namna ya kawaida hawezi kufanya kama kuna ulinzi wa kiMungu juu yako…Ukijifunza kufikiri hivyo hutakaa umwogope shetani kamwe! Wala hutakaa ujishughulishe kuijua elimu yake..utajikita katika kumjua Mungu Zaidi.
Tatizo la wakristo wengi wanaijua Zaidi elimu ya shetani Zaidi ya kumjua Mungu, mtu atakuelezea kwa mapana na marefu namna wachawi wanavyofanya kazi na namna wanavyologa na aina za majini na mapepo..na dawa za kienyeji, lakini mwambie akufafanulie hata mstari mmoja wa kwenye biblia kama anafahamu. Anamjua shetani Zaidi ya Mungu na hivyo linapotokea tatizo hawezi kujua chanzo chake.
Hivyo inatupasa tujizoeze kumtazama Mungu Zaidi badala ya shetani, biblia inasema Mjue sana Mungu ili upate kuwa na Amani, na sio tumjue sana shetani.
Bwana akubariki jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
MJUE SANA YESU KRISTO.
MAFUNDISHO YA MASHETANI
NITAZIJARIBUJE HIZI ROHO?
LULU YA THAMANI.
Rudi Nyumbani
Print this post
Hili Neno Aba kwa mara ya kwanza katika biblia lilisikika likitamkwa na Bwana wetu Yesu, Hili ni Neno la Kiaremi(Aramiac), moja ya lugha ambayo Bwana Yesu alionekana akiizungumza mara kwa mara, maneno mengine yaliyorekodiwa ambayo Yesu alionekana akiyatamka yanayotokana na lugha hii hii ni pamoja na “Talitha kumi (Marko 5:41), Efatha (Marko 7:34), Eloi Eloi lama sabakthani (Mathayo 27:46) na hili Neno Aba lenyewe.”. Hivyo hii Lugha ya kiaremi ni lugha iliyokuwa imekaribiana sana na lugha ya kiyahudi isipokuwa hii ilikuwa imetohoa maneno mengi kutoka katika lugha za tamaduni nyingine kama vile Babeli n.k.. Hivyo kwa ujumla lugha hizi tatu yaani kiyahudi, kiaremi na kigiriki, Ni lugha ambazo Bwana Yesu alionekana akiziongea..
Sasa hili Neno Aba lina maana ya Baba katika lugha hiyo, Ni neno lenye uzito zaidi ya kusema Baba tu peke yake, Tukitumia mfano wa lugha ya kiingereza tunaweza kuelezea hali hiyo ikoje..kwamfano mtu anayemwita Baba yake, Father na yule anayemwita baba yake “Daddy”,kuna tofauti kubwa sana hapo. Utagundua huyu anayemwita Baba yake daddy anamahusiano ya karibu sana kuliko Yule anayemwita father,. Father anaweza akawa ni baba anayekupenda, anayekujali, anayehakikisha unapata mahitaji yako yote ya muhimu, chakula, nguo, shule, anakujengea nyumba, na n.k..lakini mtoto ambaye anamwona baba yake kama Daddy, licha tu ya kutimiziwa mahitaji yake muhimu, lakini juu ya hilo utamwona mtoto anamfurahia baba yake na anaoujasiri mwingi kwake, akimwona anaweza hata akaenda kumrukia, anaweza akamshirikisha mambo yake yote kama vile rafiki yake, hata wakitembea barabarani mtu anaweza asijue kama ni mtu na Baba yake wanatembea lakini kiuhalisi ni Baba yake tena anayemuheshimu sana. Hiyo ndio Daddy.
Sasa ndivyo hili Neno Aba lilivyomaanisha, Aba ni bonus+ ya BABA.. Kwa ule uhusiano ambao Bwana Yesu aliokuwa nao kwa Baba yake, hakukuwahi kutokea mtu yoyote duniani kuwa na uhusiano mkuu wa namna ile, utaona mpaka dakika ya mwisho anapitia majaribu mazito namna ile, akijua kabisa na Baba yake ndiye aliyempitisha katika hali ile mbaya ya dhiki, lakini bado utaona anamwita ABA..
Embu leo hii Mungu ayakorofishe mambo yetu yasiende vizuri, au tupungukiwe kidogo tu, utaona kila aina ya malalamiko na manung’uniko yatakayotoka katika vinywa vyetu kana kwamba Mungu anafurahia wewe uwe hivyo.
Marko 14:36 “Akasema, ABA, BABA, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
Hivyo unaweza pia ukaona lengo kuu la Yesu kuja duniani na kuishi maisha ya dizaini ile lilikuwa ni kututhibitishia sisi ni kwa jinsi gani Mungu anaweza akawa karibu na wanadamu kama mtoto na Daddy wake kwa viwango vya hali ya juu sana lakini ikiwa atukuwa tayari kutii.. Mambo ambayo hapo nyuma yalikuwa hayawezekani, na ndio maana hata wayahudi walimwona kama anakufuru kumuita Mungu Baba yake mpaka wakataka kumuua kwasababu hiyo (soma Yohana 5:18).
Mambo ambayo hata sasa bado yanawakera watu wengi hususani wale wa upande wa pili ( dini ya kiislamu), wanasema ni kufuru kumwita Mungu Baba kwani Mungu hajazaa, wala hana mshirika, sisi ni viumbe vyake basi, mengine zaidi ya hapo ni kufuru…Ni kweli kabisa wanachokisema ni sahihi, kwasababu mtu kufanywa kuwa mwana wa Mungu si jambo jepesi jepesi na la kujiamulia tu kwamba na mimi leo ni mwana wa Mungu, hiyo haipo hivyo huo ni UWEZO unatoka kwa Mungu mwenyewe..Na uwezo huo wanapewa wale tu wanampokea YESU kwa kumaanisha kabisa kumgeukia yeye. Sio kwa kukiri tu katika vinywa vyao, hapana bali ni kwa kukiri na kuamua kumfuata yeye.
1Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; 13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”
1Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”
Na ndio maana sisi tuliookolewa tuna ujasiri mwingi wa kumwendea Mungu, kwasababu yeye kwetu sio baba tu bali ni “ABA Baba”. Na Roho Yule Mtakatifu tuliyepewa anatushuhudia kuwa sisi tu watoto wa Mungu.Hivyo ujasiri wetu katika hilo ni mwingi.
Warumi 8:15 “Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. 16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 17 na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.”
Warumi 8:15 “Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
17 na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.”
Unaona, ukiwa mtoto wa Mungu huna hofu yoyote, Ni wazi kuwa ujasiri utakuja wenyewe tu kwasababu Daddy yupo!!. Hii ni neema kubwa ambayo hatukustahili kuipata, ni neema ambayo mpaka kwa wengine inaonekana ni kufuru, kwanini tusiithamini.?
Wagalatia 4:6 “Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, ABA, YAANI, BABA.
7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.”
Pengine na wewe tangu zamani umekuwa mkristo-jina tu, Na ndio maana Huuoni u-baba wowote wa Mungu ndani yako, hiyo yote ni kwasababu umekuwa mtu wa nia mbili, huku unataka dunia huku na bado unamtaka Mungu..Na Bwana amesema huwezi kutumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja, ikiwa na maana huwezi kuwa na MA-BABA wawili kwa wakati mmoja. Ikiwa leo utachukua uamuzi wa kusimama upenda wa Kristo moja kwa moja nataka nikuambie ukweli Mungu hutamwona kama BABA tu, bali kama ABA…Kama Daddy ndani yako. Hilo ndio lengo Yesu lililomleta duniani ni ili akufanye wewe kuwa hivyo.
Tubu dhambi zako leo, kama hujaanya hivyo..na chukua uamuzi wa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na katika jina la YESU KRISTO, kama hukubatizwa, kisha baada ya kutii maagizo hayo Mungu atakushushia mwenyewe Roho wake ndani yako atakaye lia Aba, Hiyo ni kukushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu, kweli kweli kuanzia huo wakati na kuendelea.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?
JE! WEWE NI MBEGU HALISI?
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe.
Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu, Taa ya miguu yetu na mwanga wa njia zetu.
Moja ya masomo mapana sana ni ‘Namna ya kusikia sauti ya Mungu na kuielewa’..Mungu huwa anazungumza na sisi kila siku, lakini ugumu unakuwa ni namna ya kuielewa sauti ya Mungu..Ni kweli sio kila kitu Mungu atakachozungumza na sisi tutakielewa..sio kila kitu kwasababu tuna mipaka Fulani ya kiufahamu kutokana na hii miili tuliyonayo ya kidunia…lakini tutakapoivaa ile miili mipya ya utukufu basi tutamsikia na kumwelewa Mungu kwa mapana Zaidi. Lakini ni muhimu kutafuta kuisikia na kuielewa sauti ya Mungu kwa kadri tuwezavyo sasa, kwasababu Mungu kila siku anazungumza na sisi.
Zipo sababu nyingi zinazofanya tusisikie sauti ya Mungu kabisa..mojawapo ni maovu yetu (Isaya 59:1-2) na kingine ni kusongwa na mambo mengi…masumbufu ya Maisha haya…hizo ni kama kelele masikioni mwetu zinazozuia tusisikie sauti ya Mungu…Unapokuwa unasongwa na sauti nyingi nyingi za mambo ya ulimwengu huu inakuwa ni ngumu sana kuisikia sauti ya Mungu, mtu anayejihusisha na utazamaji wa movies muda mrefu, anakuwa anajisikilizisha sauti nyingine ambazo zinazuia masikio yake kusikia sauti ya Mungu…ni sawa na Mtu aliyeweka earphones kwenye masikio yake…hawezi kusikia sauti ya mtu anayezungumza naye akiwa nje…au kama ataisikia ataisikia kwa mbali sana…au anaweza akasikia isivyopaswa.
Kadhalika mtu anayekuwa katika shughuli nyingi za utafutaji wa mali kuanzia asubuhi, mpaka jioni anafanya hivyo siku saba katika wiki na miezi 12 katika mwaka..ni ngumu sana kuisikia sauti ya Mungu ikizungumza naye..purukushani za huku na kule za Maisha, anakutana na watu hawa, wale..anakumbana na tatizo hili au lile, watu hawa wanamweleza hivi au vile n.k hiyo inazuia sana kuisikia sauti ya Mungu.
Lakini leo hatutaingia sana huko. Leo tutajifunza ni kwa namna gani tunaweza tukaitikia vyema wito wa Mungu..yaani wakati Mungu anapotuita.
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa, Mungu anapozungumza sio kama wengi wetu tunavyotazamia..kwamba atazungumza nasi kwa radi mbinguni au mingurumo, au tutasikia sauti Fulani ya kipekee ya ajabu ikitunong’oneza masikioni. Inaweza ikatokea hivyo lakini hiyo sio njia ambayo Mungu anaitumia kusema na watu siku zote…wengi wanaitafuta hiyo njia lakini Mungu hatumii njia hiyo, sauti ya Mungu inapokuja ni kama ‘’mawazo Fulani yanaingia ndani yako ambayo yanakuwa yanakupa ufunuo fulani’’..Mawazo Fulani yanayokufumbua macho ya kuelewa jambo Fulani ambalo ulikuwa hulielewi au ulikuwa hulijui. Na hayo mawazo yanakuwa ni kama vile wewe umeyatengeneza…unaweza ukadhani ni wewe unajiambia mambo hayo, lakini sio wewe ni Bwana anazungumza na wewe…Sauti yake wakati mwingine inafanana na sauti yako kabisa, isipokuwa ya Mungu inakuja na ufunuo Fulani wa kimaandiko, ambao huo ukiupata unasikia kusisimka katika roho, unajisikia furaha kulijua hilo jambo, unajisikia amani, unajisikia kumgeukia Mungu Zaidi na kumpenda…unajisikia kutolewa sehemu moja hadi nyingine kiimani…Hiyo ni sauti ya Mungu imezungumza na wewe. Na mara nyingi hii inakuja ukiwa sehemu ya utulivu sana ukimtafakari Mungu, au ukiwa katika kulisoma Neno lake. Kwa jinsi unavyokuwa mtulivu zaidi na kulitafakari Neno la Mungu zaidi ndivyo wigo mpana wa kuisikia sauti ya Mungu unavyokuja.
Pia licha ya sauti ya Mungu kufanana sana na sauti yako, lakini pia inafanana na sauti ya Mtu mwingine ambaye yupo karibu na wewe kiimani..Mtu anaweza kuzungumza na wewe Neno Fulani la kiMungu ukaona limekupa msisimko fulani ndani yako ya kutaka kumjua Mungu Zaidi, au kumpenda Mungu, au kumtafuta..Huyo ni Mungu anazungumza na wewe, ingawa unaweza kudhani ni yule mtu kazungumza na wewe, lakini kiuhalisia si Yule mtu bali ni Mungu.
Unaweza pia kuwa katika utulivu..Bwana akaanza kuzungumza na wewe kupitia mahubiri ambayo ulishawahi kuyasikia huko nyuma, ukasikia kabisa kama vile yule mtu anakuhubiria masikioni mwako saa hiyo…ukapata kufunguliwa macho na kuona kitu kipya ambacho ulikuwa hukijui…Sasa huyo ni Mungu anazungumza ndani yako kupitia sauti ya yule Mtumishi uliyemsikia. Na kwasababu bado hujaijua sauti ya Mungu wewe utadhani ni yule mtumishi anazungumza na wewe na hivyo utatafuta njia yoyote ya kwenda kukutana naye au kujiunga katika dhehebu lake au kanisa lake..
Lakini nataka nikuambie hapo utakuwa hujaitikia vyema wito wa Mungu. Ingawa uliisikia kweli sauti ya Mungu. Lakini huko uendako unakwenda kupotea….Hebu tujifunze kidogo katika maandiko juu ya jambo hilo.
1 Samweli 3: 1 ‘Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri. 2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), 3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu; 4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa. 5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena. 6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena. 7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake. 8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto. 9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. 10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. 11 Bwana akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha. 12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho. 13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia. 14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.’’
1 Samweli 3: 1 ‘Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.
2 Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona),
3 na taa ya Mungu ilikuwa haijazimika bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;
4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.
5 Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6 Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
7 Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8 Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
9 Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.
10 Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
11 Bwana akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha.
12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho.
13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia.
14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.’’
Katika habari hiyo tunamwona kijana Samweli…Na siku moja Mungu alipotaka kujifunua kwake, hakuzungumza naye na sauti mpya ya ajabu ya kipekee…bali alizungumza naye moyoni mwake na sauti inayofanana kabisa na ile ya Eli…’yaani kwa ufupi aliisikia sauti ya Eli ikimwita’..Na yeye kwasababu alijua Eli ni Mtumishi mteule wa Mungu, aliyechaguliwa na Mungu atumike katika nyumba ya Mungu…aliitikia wito isivyopaswa akamfuata Eli kwasababu tu ile sauti aliyoisikia ilikuwa kama ya Eli..akaenda kwa Eli lakini hakukipata kile alichokuwa anakitafuta kwa maana alitegemea aambiwe sababu ya kuitwa kwake lakini hakuambiwa..Akarudi kulala tena…akaisikia ile ile sauti kama ya Eli ikimwita mara tatu, bado akarudia kosa lile lile la kwenda kumfuata Eli mpaka Eli alipomsaidia kupata ufahamu kuwa Sauti aliyoisikia sio ya Eli ni ya Mungu, japokuwa inafanana na ya Eli mtumishi wa Mungu.
Na alipotulia kwa makini, na kuitikia vyema wito wa Mungu, ndipo Mungu akaanza kumwambia kusudi la wito wake…Samweli akaja kugundua kuwa kumbe huko kwa Eli alikokuwa anakwenda ndipo Mungu alipopachukia na ndiko Mungu anapotaka kumtuma akawaambie makosa yao.
Na sauti hiyo hiyo inawaita wengi leo hii…Lakini inapoita sio wakati wa kuitikia na kwenda kumfuata huyo mtumishi au dhehebu la huyo mtumishi unayesikia ujumbe kutoka kwake..Bwana ametumia tu sauti ya huyo mtumishi au sauti ya hilo dhehebu kukuita wewe…Lakini Bwana hayupo huko hata kidogo..Yupo hapo hapo ulipo?. Anapokuita ndugu usiende kujiunga na madhehebu utapofuka macho. Hutamsikia Mungu huko hata kidogo. Ndicho kilichomtokea Samweli mpaka alipoelewa somo.
Ndugu udhehebu ni mnyororo mbaya sana, ambao unawakosesha wengi na kuwapeleka kuzimu..Samweli hakujua uovu uliokuwa unaendelea kwenye nyumba ya Mungu ambao ulikuwa unaongozwa na Eli pamoja na wanawe..mpaka siku alipotoka na kuisikia sauti ya Mungu, akagundua kuwa kumbe Mungu ametukasirikia, kumbe japo watu kwa nje wanaona kila kitu kipo sawa lakini kumbe Mungu katukasirikia sisi tuliopo ndani…na hata huyu Eli ambaye Mungu alitumia sauti yake kuzungumza nami..kumbe hata yeye tayari kashaharibu mambo siku nyingi…hayo yote Samweli aliyajua baada ya kutoka kwenye udini na udhehebu wa Eli.
Hivi unajua chapa ya mnyama inauhusiano mkubwa sana na dini na madhehebu…Roho ya Mpinga-Kristo sasa inatenda kazi katikati ya madhehebu, kuhakikisha inawafunga matita matita watu na kuwapeleka watu jehanamu..sawasawa na Mathayo 13:30. Ndio maana unaona madhehebu yanaongezeka kila kukicha…Huo sio mpango wa Mungu kabisa…. Itafika siku moja baada ya unyakuo kupita, madhehebu yote yatasajiliwa katika umoja wa madhehebu duniani..na watu hawataweza kununua wala kuuza wala kuajiriwa wasipokuwa washirika wa mojawapo ya madhehebu yaliyosajiliwa katika umoja huo wa dini na madhehebu duniani…Siku hiyo mamilioni ya watu wataipokea chapa pasipo kujua kuwa wameipokea. Maelezo yake juu ya hayo ni marefu kidogo lakini..Kama hujafahamu kuhusu hayo basi yafuatilie na uyajue au unaweza ukanitext inbox nikutumie somo juu ya hayo.
Lakini huu sio wakati wa kujisifia dhehebu wala dini, ni wakati wa kutoka huko na kurudi kwenye Neno,(Ufunuo 18:4) huu sio wakati wa kusema mimi ni Muanglikana, Mlutheri, Mkatoliki, Mlokole, Msabato, Mbaptist, Mbranhamite, Mmennonites n.k Huu ni wakati wa Kuwa Mkristo wa kweli wa kimaandiko, Bibi arusi safi, aliyeisikia sauti ya Mungu kweli na kuitikia wito inavyopaswa kwa kuzaliwa mara ya pili na kuishi kulingana na Neno la kwenye biblia(Maisha ya utakatifu na yanayompendeza Mungu).
Mungu anapokuita itikia wito ipasavyo, Rudi kwenye Neno lake ndipo mahali salama, ujifunze ukue kiroho, Ona fahari juu ya Roho Mtakatifu anakushuhudia kila siku kuwa wewe ni mwana wa Mungu kuliko dini au dhehebu hivyo havitakufikisha popote.
Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Zinazoendana:
WITO WA MUNGU
JE! UMECHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU?
IELEWE SAUTI YA MUNGU.
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
SADAKA ILIYOKUBALIKA.
Watu wengi wanadhani makao ya watakatifu yatakuwa ni mbinguni milele, yani siku ile ya mwisho dunia itakunjwa kunjwa na kutupwa motoni, halafu sisi tutakwenda kuishi na Mungu mbinguni milele, Ni wazi kuwa jambo hilo sio la kimaandiko kabisa, Biblia inatufundisha kuwa tutakaa mbinguni miaka saba tu! Kisha tutarudi kutawala na KRISTO hapa duniani Milele.
Mungu alivyotuumba sisi wanadamu ni tofauti kabisa na alivyowaumba malaika, Utukufu Mungu aliouweka kwetu sisi, haufanani na ule wa malaika zake, Sisi tumeumbiwa miili, sisi tumeumbiwa kumiliki, sisi tumeumbiwa kutawala, na hivyo tutamwabudu Mungu katika njia hiyo hiyo. tofauti na malaika, Ndio maana Adamu mtu wa kwanza alishushwa hapa duniani, ili kutimiliza hayo makusudi. Alishushiwa mbingu yake hapa chini.
Lakini alipoasi ndipo alipofanya dunia ionekane kuwa sio sehemu ya kutamaniwa tena kuishi kwa watu, lakini ashukuriwe Mungu, vitu vyote vitakuja kurejeshwa katika uhalisia wake moja ya hizi siku.
Biblia inaposema Dunia inapita na tamaa zake zote (1Yohana 2:17), Haimaanishi kuwa Dunia itateketezwa na kuondolewa kabisa hapana bali Inaamisha kuwa Ulimwengu huu uliopo ndio unaopita na ndio utakaoteketezwa, mambo yote tunayoyaona, falme zote unazoziona, shughuli zote unazoziona na tunazozifanya, ustaarabu wote uliopo duniani leo hii, serikali zote na mamlaka yote hakuna hata mmoja kitakachosalia, vyote hivi vitaondoshwa kupisha majira mengine kuanza. Na ndio maana tunaambiwa tuishi kama wapitaji, kwasababu vitu tunavyovisumbukia havituwekei kumbukumbu la milele.
Leo hii unaipenda dunia, unapenda kuwa na maisha mazuri, unapenda kufanikiwa na kuwa tajiri na ndio maana unatafuta mali kwa nguvu zote, Unafanya hivyo ni ili uishi maisha mazuri na ya raha hapa duniani. Ni wazi kuwa hakuna mtu ambaye anaufurahia umaskini, kila mmoja anatamani awe na mafanikio makubwa, na hiyo ndiyo inayombidiisha afanye kazi kwa bidii. Lakini jifunze pia kukaa chini kutafakari nini kusudi la maisha, usiishi tu kama mnyama, hutaki kujua umetokea wapi na unakwenda wapi, badala yake unajitaabisha sana kujitashirisha.. mwisho wa siku unakuwa kama Yule mtu Bwana aliyemtolea mfano baada ya kufanikiwa sana kwa shughuli zake, sasa anatulia ili aiburudishe nafsi yake, lakini usiku ule ule waliitaka nafsi yake.
Ndipo Bwana akasema na zile mali alizozisumbukia zitakuwa za nani?(Luka 12:16) Unaona, ni muhimu kujua maisha unayopitia leo iwe ni katika vingi au katika vichache je! inafunua nini katika ulimwengu wa roho?.
Sasa Mungu karuhusu tuyaonje hayo, kama kivuli cha huo ufalme mwingine mkuu sana utakaokuja huko mbeleni. Kwamba watu hawatakuwa sawasawa kutakuwa na matajiri sana na vilevile kutakuwa na watu wa kawaida sana. Ufalme huo ambao utashuka hapa mara baada ya siku ile kuu ya Bwana kupita duniani, Yesu atakapotokea katika mawingu pamoja na watakatifu wake aliokuwa amewanyakua zamani, sasa wakati huo dunia itakuwa imeshasafishwa, na shetani ameshafungwa kwenye lile shimo la kuzimu kwa muda wa miaka 1000, dunia kuanzia huo wakati itakuwa Paradiso kama hapo mwanzo, Ustaarabu mpya wa kimbinguni utaanza kutenda kazi duniani, YESU KRISTO akiwa kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa Mabwana, ikimaanisha kuwa atakuwa na wafalme wengi sana chini yake na mabwana wengi sana chini yake, na makuhani wengi sana chini yake, ili kutumiza pamoja nao kazi ya ufalme wa Mungu Baba.(Ufunuo 1:6)
Nafasi hizo hazitakuwa za kila mtakatifu, hapana bali kila mmoja atalipiwa kulingana na matendo yake na taabu yake hapa duniani, kama wewe maisha yako yote yalikuwa ni ya ulevi, mpaka uzee wako ndio unamrudia Bwana, ukifika kule hutakuwa sawa na Mtume Paulo. Maisha tunayoishi sasa kwa Kristo ndio yanayotuleza kule tutakuwa nani.
Wakati huo ukifika kutakuwa na majuto mengi sio tu kwa watu waliokufa katika dhambi, hapana bali pia kwa watakatifu wakijutia kwanini hawakufanya zaidi kwa kujiwekea hazina katika huo ufalme wa milele wa Yesu Kristo utakaoshuka duniani.
Sasa kutakuwa na shughuli nyingi sana, na mambo mengi sana yatakayokuwa yanaendelea kule, na tunasoma baadaye hizi bahari zote zitakuja kuondolewa, leo hii ni 21% tu ya dunia inakaliwa na wanadamu sehemu nyingine zote ni maji na pamoja na hayo bado haijajazwa, sasa wakati huo habari hazitakuwepo Eneo la makazi ya watu litaongeza na haya mabara basi yatakuwa si chini ya 30, leo hii yapo 7 tu,na kote huko kutakuwa ni miji mikubwa, na makazi yaliyobuniwa mbinguni. kutakuwa hakuna magonjwa wala laana, wala wachawi, wala ajali, tutumwabudu Mungu katika makazi hayo milele na milele.
Kwa mambo makuu yote hayo utajisikiaje unakuwa mtu wa kawaida kule milele?, Ukitaka kufahamu vizuri utakuwa katika hali gani jijengee picha sasahivi, katika hali uliyopo, ujifananishe labda na Raisi, au Waziri, au mtu Fulani aliye na mali nyingi, uone tofauti yake na yako jinsi ilivyo kubwa, mambo mengi unavyoyakosa ndivyo itakavyokuwa kule, tofauti tu ya huku na kule, ni kwamba huku unaishi bado katikati ya hatari na shida na bado ni kwa kipindi kifupi tu, lakini kule Ukiwa umepewa mamlaka na YESU ni mamlaka ya milele na milele isiyokuwa na mwisho, hakutakuwa na kupandishwa cheo wala kushushwa cheo,Karama za Mungu hazina majuto…Ni afadhali tukose kila kitu hapa, lakini kule tukapate kila kitu.
Na ndio maana tunashauriwa tukiwa hapa duniani tuukomboe wakati, kwa kutafuta kujua mapenzi ya Mungu hasa ni nini kwetu. kwa jinsi ile ile tunavyohangaika kutafuta mambo ya ulimwengu huu, ni wakati sasa wa kupeleka nguvu zetu nyingi zaidi kutafuta mambo ya ufalme wa mbinguni unaokuja wa milele wa Yesu Kristo Bwana wetu …Kwasababu huko ndiko ndio kuna maisha. Haleluya.
Kumpa Yesu maisha yetu tu haitoshi, ni lazima tufanye na kitu cha ziada, safari ndio inaanza…tujiwekee hazina kule, kwa kufanya mapenzi ya Mungu na kuitenda kazi yake kwa uaminifu. Bwana anasema hivi.
Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia. 11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa. 12 TAZAMA, NAJA UPESI, NA UJIRA WANGU U PAMOJA NAMI, KUMLIPA KILA MTU KAMA KAZI YAKE ILIVYO. 13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
Ufunuo 22:10 “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.
12 TAZAMA, NAJA UPESI, NA UJIRA WANGU U PAMOJA NAMI, KUMLIPA KILA MTU KAMA KAZI YAKE ILIVYO.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
Napenda umalizie kwa kusoma habari hii, kisha sasa uanze kuchukua hatua kuanzia leo….
Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi. 13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja. 14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale. 15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake. 16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi. 17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida. 19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano. 20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho.”
Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.
13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.
14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.
15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho.”
Mfalme anakuja.
Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
SIKU ZA MAPATILIZO.
MFANO ULE YESU ALIOUTOA WA KABAILA ALIYESAFIRI KATIKA NCHI YA MBALI, UNA MAANA GANI (LUKA 19:12-27)?
UTAWALA WA MIAKA 1000.
NI KWELI MTU ANAWEZA AKAFA LAKINI ROHO YAKE IKAWA INATUMIKA KAMA MSUKULE (KUMILIKIWA NA MTU FULANI KWA WAKATI) MAHALI PENGINE?
Shalom, mtu wa Mungu karibu tujifunze Neno la Mungu, Taa iongozayo miguu yetu..na mwangaza wa njia zetu…
Leo tutajifunza juu ya Kumshukuru Mungu kwa kila jambo…
Kwanini tunapaswa tumshukuru Mungu kwa kila jambo? Jibu ni rahisi kwasababu hatukukaa naye kikao cha yeye kutuumba sisi…tumejikuta tumetokea tu ulimwenguni, kwahiyo lolote lijalo mbele yetu sio sisi tulilolitengeneza bali ni yeye, na hatukumpa yeye kitu hata atakapokitwaa tumwulize kwanini anafanya hivyo (Ayubu 41:11)…kwahiyo tuna sababu zote za kumshukuru kwa mambo yoyote yatakayotokea mbele yetu yawe ni mazuri au mabaya…
Wakati mwingine Mungu anaruhusu maovu yaje juu yetu kama gharika… kama ilivyokuwa kwa Ayubu, wakati mwingine Mungu anaruhusu mambo hayo kwasababu zake yeye ambazo sio lazima wakati mwingine akuambie ni kwanini…Lakini unapaswa ushukuru.
Kama Biblia inavyotuambia katika 1 Wathesalonike 5:16 “ Furahini siku zote; ombeni bila kukoma; SHUKURUNI KWA KILA JAMBO; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.
Hata tukipitia misiba tushukuru? ndio..hata tukifilisika tushukuru? jibu ni NDIO?..Hata tukiwa katika magonjwa tushukuru? jibu ni NDIO…Kwasababu hayo ndio mapenzi ya Mungu.
Kitu ambacho wengi wetu hatujui ni kuwa…Mungu anaweza kuleta pia UOVU au UBAYA juu ya watu wake…haijalishi huo ubaya utatekelezwa na shetani, au malaika au mwanadamu…lakini Ana uwezo wa kuleta Ubaya juu ya mtu ambaye hata anayeupendeza moyo wake kabisa kwa kusudi Fulani…
Biblia inasema katika…Maombolezo 3:37 “Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza? 38 Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki MAOVU NA MEMA?”
Unaona? Sio mema tu yanatoka kwake hata maovu…lakini Maovu anayoyaleta juu ya watu wake sio ya kuwaangusha bali kuwapa tumaini katika siku zao za mwisho(Yeremia 29:11)..Haleluya!..Bwana atajeruhi lakini ataponya! Ataangusha chini lakini atanyanyua! Ataua lakini atahuisha, Atafukarisha lakini atatajirisha N.k
1 Samweli 2:6 “Bwana huua, naye hufanya kuwa hai; Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu. Bwana hufukarisha mtu, naye hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu.”
Hosea 6:1 “Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. 2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.”
Hosea 6:1 “Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.
2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.”
Kwahiyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kutomnung’unikia Mungu pale jambo Fulani baya linapokuja juu yako…kinyume chake mshukuru kwasababu anakuwazia yaliyo mema katika siku zako za mwisho..Na pia kumbuka kuwa hakuna mwanadamu awezaye kumwuliza Mungu kwanini unafanya hivi au kwanini unafanya vile, au kwanini unaruhusu hili, au kwanini unaruhusu lile,…Kila kitu anafanya kama apendavyo. Na pia hatukuja na chochote hivyo hata vikichukuliwa vyote hatuna sababu ya kulaumu kwasababu hatukuja na kitu duniani..
Ayubu alizungumza sentensi moja ambayo ni muhimu sana kwetu sisi kuielewa…alisema …Ayubu 1:21 “ akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe”.
Maana ya kutoka kwa mama yake uchi, alimaanisha hakuja na kitu duniani, hata nguo, wala watoto, wala mashamba, wala wale ng’ombe aliowapoteza, wala wale mbuzi na ngamia…bali alikuja bila chochote…kwahiyo hata siku atakapokufa atarudi huko alikotokea bila kitu…kwa ufunuo huo basi akahitimisha kwa kusema Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake libarikiwe!!.
Ni ufunuo mkubwa sana aliupata…na sisi tunapaswa tuwe hivyo..tulikuja duniani bila ya kitu chochote na hivyo tutaondoka bila chochote…kwahiyo tukipata misiba,misiba, tukifilisika, tukipungukiwa tujue kuwa hatukuja na kitu..tukiyajua hayo tutaishi kwa Amani na kama wapitaji tu hapa duniani. Na hiyo itatufanya kuweka tumaini letu lote kwake, wakati Fulani mtume Paulo na wenzake walisongwa na taabu nzito mpaka wakakata tamaa ya kuishi..Lakini hiyo iliwafanya wazidi kumtumainie Mungu awaokoaye watu wote.
2Wakorintho1:8 “Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. 9 Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu, 10 aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa;” Kwahiyo tunapaswa tushukuru kwa kila jambo, na kuridhika kwa vile Mungu alivyotukiria, kwasababu hatukuja na kitu vile vile tutaona bila kitu chochote. 1 Timotheo 6:6 “Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu.”
2Wakorintho1:8 “Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi.
9 Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu,
10 aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa;”
Kwahiyo tunapaswa tushukuru kwa kila jambo, na kuridhika kwa vile Mungu alivyotukiria, kwasababu hatukuja na kitu vile vile tutaona bila kitu chochote.
1 Timotheo 6:6 “Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu.”
SWALI LA KUJIULIZA!
KUNA TOFAUTI GANI KATI YA SALA NA DUA?
FAIDA ZA MAOMBI.
Biblia inatueleza kuwa kuna aina mbili za dhambi, zipo dhambi zinazomtangulia mtu kwenda hukumuni na zipo dhambi zinazomfuata mtu hukumuni. Na leo tutaona hizi dhambi ni zipi:
1Timotheo 5:24 ‘Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata’.
Unajua ni heri kitu kinachokutangulia kuliko kile kinachokufuata, kwasababu kinachokutangulia siku zote kipo mbele yako unakiona, na hivyo kuona madhara yake na kutafuta njia ya kukikwepa ni rahisi, lakini kile kinachokufuata kipo nyuma yako, na wakati mwingine unaweza hata usijue kama kuna hatari nyuma yako mpaka pale kitakapokuletea madhara ndipo utakapojua. Mfano leo hii ukaenda porini kwa bahati mbaya ukakutana na mnyama DUBU, ikatokea ukafanikiwa kumponyoka na kukimbia mbali kidogo kwenda kupumzika labda tuseme umbali wa kilometa moja, Ni rahisi kudhani kuwa umempoteza, ni kweli kwa wakati huo utakuwa umempoteza hayupo pamoja na wewe, lakini Dubu ni mnyama mwenye uwezo mkubwa wa kunusa kuliko wanyama wote porini, anao uwezo wa kunusa chakula chake mahali kilipo zaidi ya kilometa 30 na kukifuata. Huo ni umbali kutoka Daresalaam mpaka Kibaha.. Hivyo haijalishi atachukua siku ngapi kukufikia, atakuwa anakufuatilia taratibu mpaka mwisho wa siku atafika pale ulipo na madhara yatakukuta.
Ndivyo ilivyo asili ya dhambi, zipo dhambi ambazo ni dhahiri kabisa zipo mbele ya mtu zinaonekana, hizo tayari zimeshafika hukumuni na kumurudishia majibu yake kuwa anastahili jehanamu. Kwamfano mtu anapokuwa msagaji au shoga, hana haja ya kujihakiki mara mbili kama yeye ataenda motoni au la! Ni dhahiri kuwa anachofanya si Mungu tu kakitaa bali hata jamii imekikataa, vivyo hivyo na anayezini, anayeua, anayefanya kazi ya ujambazi,anayetoa mimba, mchawi, mshirikina, n.k. hizi ni dhambi zilizodhahiri kabisa haihitaji mtu kusubiri kupandishwa kizimbani achunguzwe ndio ahukumiwe, akiwa hapa hapa duniani ameshajua yeye ni wa motoni tu moja kwa moja. Na hizi ni rahisi kuziepuka ikiwa unafanya mfano wa vitu kama hivyo, nakushauri utubu haraka sana ndugu umgeukie Mungu.
Lakini zile zinazomfauta mtu, ni dhambi za siri, ambazo kwa macho ya kawaida ni ngumu kuziona na dhambi hizi huwa mtu ni rahisi sana kuzifanya na rahisi pia kuzisahau, kwamfano mtu anapozungumza maneno yasiyokuwa na maana, mizaha kumuhusu Mungu, kama vile Yesu alivyosema katika Mathayo 12:36 “Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. 37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
Sasa Siku ile ya hukumu anaweza kudhani atahukumiwa kwa mambo yaliyodhahiri tu, lakini mazungumzo yote yatawekwa wazi Hizo ndio dhambi zinazokufuata.. Vitu vingine ni kama vinyongo, kutokusamehe, visasi, usengenyaji,uzishi, n.k.Yote haya mtu anaweza akawa navyo watu wasijue, au pengine yeye mwenyewe asijue kuwa ni makosa, siku ile ya hukumu ndipo atakaposhangaa ni nini hiki.?..Mfano dhambi ya kutokusamehe hii ndio itakayowashitusha wengi sana siku ile…watasema mbona mimi niliomba toba zote kwa Mungu, iweje Mungu hakunisamehe dhambi zangu..Lakini hakujua kuwa Bwana alisema ‘msipowasamehe watu makossa yao na Baba yenu wa mbinguni hatawasamehe nyinyi makosa yenu’.
Lakini vile vile Kumbuka “kifungu hicho hicho” kinatuambia yapo MATENDO MEMA yanayomtangulia mtu hukumu na yale yatakayomfuata.
1Timotheo 5:24 ‘Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata. 25 VIVYO HIVYO MATENDO YALIYO MAZURI YA DHAHIRI; WALA YALE YASIYO DHAHIRI HAYAWEZI KUSITIRIKA’.
1Timotheo 5:24 ‘Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata.
25 VIVYO HIVYO MATENDO YALIYO MAZURI YA DHAHIRI; WALA YALE YASIYO DHAHIRI HAYAWEZI KUSITIRIKA’.
Unaona, mtu pia akitenda matendo mema iwe ni kwa siri au kwa dhahiri hakuna lolote litakalosahaulika, kama tu vile dhambi ya siri na isiyo ya siri isivyosahaulika.
Mhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, LIKIWA JEMA AU LIKIWA BAYA.”
Sasa Matendo yaliyo dhahiri ni kama yapi?, mfano kama kufanya kazi ya Mungu, kusaidia ndugu,na kusaidia yatima, kuwa mtetezi wa watu, kupatanisha, n.k…
Lakini pia yapo matendo mema yaliyositirika, ambayo kwa macho ya kawaida mtu yeyote hawezi kuyaona, na rahisi pia kuyatenda na kuyasahau, mfano wa hayo ni kama vile kuombea wengine na kubariki, kuwaombea watakatifu na kanisa la Mungu kwa ujumla, kumtetea mtu Fulani aliyeonewa, kumsamehe mtu Fulani n.k..
Hivi ni vitu ambavyo siku ile ya hukumu huyu mtu aliyekuwa anavitenda atasimama akidhani hakuna lolote alilolifanya kwa Mungu..Lakini atashangaa siku hiyo thawabu zake zinakuja mahali asipojua atauliza hizi zinatoka wapi? ndio hapo Bwana atamkumbusha, kwa yale maombi yako ya kila siku aliyokuwa analiombea kanisa na watakatifu wote, Fulani na Fulani aliokoka kwa hayo…Fulani na Fulani alisimama kwa kupitia hayo..Fulani na Fulani aliponywa kupitia hayo.(Yakobo 5:16). Ipo faida kubwa sana kutenda mema bila kutarajia malipo au kuonekana na watu kwasababu siku ile matendo yako mema yatakufuata.
Ufunuo 14.13 ‘Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao’.
Hivyo ndugu kila mmoja wetu atasimama hukumuni, lakini lipo tumaini zuri kwa wewe ambaye bado upo kwenye dhambi, njia pekee ya kufutiwa hilo deni la mzizi wa dhambi zako, iwe ni zile zilizokutangulia au zinazokufuata dawa ni moja tu, Ni kumkabidhi leo Bwana YESU maisha yako. Huo ndio mwanzo wa Uzima.
Yeye atakusamehe kabisa, na siku ile, hakutakuwa na shitaka lolote juu yako. Wala hakutakuwa na harufu yoyote ya dhambi itakayokufuata, kwasababu sasahivi jambo atakalolifanya ikiwa utamruhusu aje ndani ya maisha yako ni kuhakikisha anaweka dhambi zako zote mbali na wewe kama vile Mashariki ilivyo mbali na Magharibi. Kwasababu anakuhurumia na kukupenda. Hapo ndipo tunaopoona faida ya DAMU ya YESU isiyoweza kuharibika.Haleluya!!
Zaburi 103: 11 “Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao. 12 Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. 13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi”. Hiyo yote ni ukiwa tayari kutii. Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Zaburi 103: 11 “Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao.
12 Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.
13 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.
14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi”.
Hiyo yote ni ukiwa tayari kutii.
DHAMBI YA MAUTI
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
JE! KUBET NI DHAMBI?
MSHAHARA WA DHAMBI:
DHAMBI YA ULIMWENGU.
NGUVU YA UPOTEVU.
Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO lisifiwe daima, Nakukaribisha ndugu mpendwa tujifunze maandiko, Leo tutangazia kwa sehemu kitabu cha waraka wa kwanza wa Petro tutaona Neno kuu la msingi ambalo mtume Petro aliwasihi ndugu wote katika Bwana ambao walikuwa wanaishi kama wageni katika mataifa mengi, Ikumbukwe kuwa wakati ule dhiki kuu ilipotokea Yerusalemu, wakristo wakiyahudi walipokuwa wakitafutwa wafungwe na kuuawa, wengi wao waliondoka Yerusalemu, na kukimbilia katika mataifa mengine ya mbali, vile vile na kule katika mataifa wale wakristo waliopokea injili nao pia hawakuwa katika hali ya usalama, nao pia shetani alikuwa anawawinda na hivyo walikuwa wanahama hama. Na ndio maana ukisoma nyaraka zote za mitume utaona wakristo wote walikuwa wanajulikana kama wasafiri, wageni na wapitaji katika dunia.
Na ndio maana tunaona waraka huu wa kwanza wa Petro, anauandika kwa watu wote (wakristo wa-kimataifa na wa-kiyahudi). Walio katika UTAWANYIKO, yaani kwenye mataifa mengine ya kigeni, Tunasoma hayo katika :
1Petro 1:1 “Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia; 2 kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.”
1Petro 1:1 “Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia;
2 kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.”
Unaona sasa ukisoma waraka huu utaona Petro akiwasihi wawaheshimu watu wote, wawe na mwenendo mzuri, watii mamlaka, waheshimiane wao kwa wao, wasaidiane, wapendane, na wasishitakiwe kwa jambo lolote ovu, ili kusudi kwamba watu wa mataifa wasiomjua Mungu wao wasipate Neno la kuwashitaki. Aliwasihi pia wakristo wote waliopo huko wavumilie, na zaidi ya yote wafurahie pale wanapoteswa kwa ajili ya Kristo.
1Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe. 14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia. 15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine. 16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.”
1Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.
15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.
16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.”
Unaona?, Huko katika mataifa ya ugenini, walikuwa ni kama kioo, na matamasha,watu wote wanawaangalia..Lakini mwisho wa siku Mtume Petro akawaambia maneno haya:
“Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.” (1Petro 3:15)
Hii ikiwa na maana kuwa itafika wakati wale watu wanaowazunguka watavutiwa kujua nini hasa sababu ya wao kuwa hivyo.Japo kuwa ni wageni, japokuwa wanapitia dhiki na mateso na shida lakini bado wapo na msimamo wao..Nini hasaa hawa watu wanakitazamia?.. Ndio hapo mtume Petro anawaasa sasa wawe tayari kuwaeleza habari za TUMAINI lililo ndani yao..
Kwamba ule uzuri waliowekewa mbele yao, na ufalme ambao upo karibuni kufunuliwa na wao wakiwa kama wafalme na makuhani,Taifa takatifu la Mungu pamoja na kiongozi wao mkuu Yesu KRISTO,kama MFALME wa Wafalme, ndio sababu inayowafanya waishi kama walivyo, wakae mbali na dhambi na matendo yote ya giza, wasione kama hizo dhiki na mateso ni kitu kikubwa katika maisha yao kulinganisha na tumaini lilipo mbele yao.(1Petro 2:9)
Embu jaribu kufikiria huyo mtu akisikia hivyo ataachaje kubadilika. Na sisi vivyo hivyo tunapaswa tuishi kama wapitaji, kama wageni wasafiriji, huku tukiwa na TUMAINI la amani na furaha, ili siku moja nasi tuulizwe na watu wasiomjua Mungu, watu wenye mahangaiko, wenye hofu ya maisha na mizigo ya dhambih watuulize je! Mbona nyinyi mpo hivi na bado maisha yenu ni ya amani.. Nasi ndipo tuwaeleze TUMAINI lililo ndani yetu habari za YESU KRISTO…kwa upole na hofu, sio kwa kuwatisha hapana bali kwa upole na hofu biblia inatuambia hivyo. Na mwisho tutajikuta wengi wanavutiwa na TUMAINI hilo..Lililo la kweli.
Wafilipi 3:1 “Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana….” 4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini. 5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. BWANA YU KARIBU. 6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. 7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.(Wafilipi 4:4-7)
Wafilipi 3:1 “Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana….”
4 Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. BWANA YU KARIBU.
6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.(Wafilipi 4:4-7)
Amen. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?
BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!
UPUMBAVU WA MUNGU.
MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.
Luka 10: 25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje? 27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. 28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi. 29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani? 30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa. 31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando. 32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando. 33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia, 34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza. 35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa. 36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi? 37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Luka 10: 25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?
30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?
37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Kuna kitu kidogo cha kujifunza katika hichi kisa…Mwanasheria mmoja alisimama kumwuliza swali la kumjaribu Bwana Yesu…kumwangalia atajibuje! Lakini Bwana alimjibu kwa kumrudisha kwenye Torati na kumwuliza imeandikwaje! Akamjibu “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako”.
Bwana akampongeza akamwambia afanye hivyo naye utaupata huo uzima wa milele. Lakini Yule mwanasheria hakuishia hapo…akataka kuendelea kumpima ufahamu Bwana Yesu kwa kumwuliza jirani yake ni nani??.
Sasa kumbuka huyu mtu hakuwa na lengo la kutaka kujifunza bali kwa lugha ya sasa hivi tunaweza kusema ni mtu aliyekuwa anajifanya mjuaji…Kwasababu alikuwa anajua kabisa vigezo vya kuupata uzima wa milele ni kumpenda Mungu kwa moyo wote na akili zote na pia kumpenda jirani kama nafsi yake, lakini bado alikuwa anamwuliza Bwana kwa kumjaribu…Na hapa anamwuliza tena Bwana jirani yangu ni nani…Na wakati Bwana ameshamjibu kuwa anapaswa ampende jirani yake kama nafsi yake..Kwahiyo alikuwa anajua kabisa jirani yake ni nani lakini alitaka kumwonyesha Bwana yeye ni mjuaji zaidi….
Na hicho kiburi alikipata kutokana na kusoma kwingi, alifahamu mambo mengi ya torati na dini yake kwasababu hapo juu biblia inasema alikuwa ni mwanasheria…Sasa hakuwa mwanasheria kama hawa wanasheria tunaowajua sasahivi wanaotumia katika ya nchi kuhukumu…Hapana bali yeye alikuwa ni mwanasheria aliyesoma sheria zote za Mungu kupitia Torati za Musa…Kwahiyo alikuwa anajua kufumbua maswali yote yanayohusiana na torati…kukitokea jambo Fulani anaweza kukupatia ufumbuzi kamili kwa kurejea kwenye Torati…atakwambia Aya Fulani ya torati, kipengele Fulani kinasema hivi na hivi…Kwahiyo ni watu ambao ulikuwa huwezi kuwadanganya kitu chochote kinachotoka kwenye Torati, walikuwa wanaijua yote.
Ndio maana alikuja kwa ujasiri kumjaribu Bwana akiwa tayari na majibu sahihi ya maswali yake kichwani.
Wakati yeye anadhani anajua kumbe mbele za Mungu alikuwa anaonekana hajui chochote.
Sasa katika mfano huo hapo juu Bwana Yesu alioutoa, alikuwa anataka kumwonyesha Yule mwanasheria kuwa “dhana ya kufikiri kuwa wayahudi ndio majirani zao pekee ni uongo”..Kama Torati ilivyowafundisha kuwa… “jirani yako ni Mwisraeli mwenzako”..Mtu mwingine tofauti na mwisraeli (Myahudi) sio jirani yako. Hivyo mtu unayepaswa kumpenda kama nafsi yako ni mwisraeli mwenzako tu!…Ndivyo huyu mwanasheria alivyokuwa anajua kichwani mwake na ndivyo torati ilivyokuwa inasema. Lakini ashukuriwe Mungu Bwana Yesu ndiye ukamilifu wa Torati Haleluya!!. Ndio maana Biblia inatuonya tutoke katika kamba za madhehebu kwasababu zinatufungia mlango wa kumjua Mungu…kamba za madhehebu zinatufanya tusimwelewe Mungu wala tusimsikie Mungu kwa kisingizio tu! Dini yetu inasema hivi, dhehebu letu linasema hivi. Zinatufanya tujione tunajua kila kitu kumbe hatujui chochote kama huyu mwanasheria hapa!.
Sasa tukirudi kwenye Torati ya Musa, Baada ya Mungu kuwatoa wana wa Israeli Misri na kuwaingiza nchi ya Kaanani aliwaambia…wapendane wao kwa wao, yaani wayahudi kwa wayahudi kama nafsi zao, pia walionywa wasichangamane na watu wa mataifa, hata wasioe watu wa mataifa. Na waliambiwa pia wasitozane riba wao kwa wao, wanaweza kuwatoza riba watu wa mataifa lakini sio wao kwa wao. Hivyo ilikuwa inaaminika na kufahamika kuwa sheria hiyo Musa aliyoitoa ya kumpenda jirani yako kama nafsi yako, inawahusu tu wayahudi kwa wayahudi, kwamba wao tu watapendana kama nafsi zao, kwamba mtu mwingine tofauti na Taifa lao ni ruksa kutokumjali..ni ruksa kutojishughulisha naye. Lakini mwisraeli mwenzako ndio unapaswa umpende kama nafsi yako. Ukisoma kitabu cha Mambo ya Walawi utaweza kuelewa jambo hilo vizuri kwa undani, lakini moja ya mstari unaozungumzia upendo kwa wayahudi tu ni huu..
Walawi 19:18 “Usifanye kisasi, WALA KUWA NA KINYONGO JUU YA WANA WA WATU WAKO; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi Bwana”.
Umeona?..Biblia inasema hapo “juu ya watu wako”..ikiwa na maana watu wengine (yaani watu wa mataifa) ni ruksa kuwawekea kinyongo endapo wamefanya jambo la kukwaza.
Kwahiyo ndivyo ilivyokuwa inaeleweka miaka na miaka…Na huyu mwanasheria ndivyo alivyokuwa anajua…Lakini tunaona Bwana alimwambia kitu kipya..kuhusu JIRANI YAKE KUWA NI NANI?…Alitegemea aambiwe kuwa jirani yake ni myahudi mwenzake, (aidha mlawi au kuhani au mwisraeli wa kawaida tu)..lakini Bwana alimwonyesha Msamaria ndiye ndugu yake.
Sasa WASAMARIA wakati huo hawakuwa watu wa Taifa la Israeli, walikuwa ni watu wa mchanganyiko na watu wa mataifa…Kwahiyo hawakuwa uzao wa Ibrahimu hata kidogo..Lakini Bwana alitoa mfano huo kuonyesha kuwa watu wa mataifa wanaweza kuwa majirani wa kweli kuliko hata hao waisraeli wanaojiona wamestahili kupendana wao kwa wao tu!.
Katika mfano ule tunaona…Alikuja kwanza kuhani ambaye alikuwa myahudi lakini alipita kando hakutaka kumsaidia myahudi mwenzake mtu wa Taifa moja na yeye…Baadaye kidogo alipita Mlawi ambaye alikuwa myahudi pia lakini hakutaka kumsaidia myahudi mwenzake aliyekuwa amepatwa na matatizo…Lakini alipopita Msamaria ambaye hakuwa hata myahudi wala hamjui Mungu wa Israeli, alimsaidia kwa msaada mkubwa Myahudi ambaye alikuwa hata hamjui..Na hivyo huyo Bwana ndiye akasema ni JIRANI mwema anayepaswa kupendwa kama nafsi yake.
Bila shaka baada ya mfano huo, Yule mwanasheria aliondoka kwa hasira kwasababu ni kama aliambiwa amri mpya awapende pia watu wa mataifa aliokuwa anaishi nao, (makafiri) kama nafsi yake.
Na sisi kuna jambo tunaweza kujifunza hapo….Udini na Udhehebu ni mbaya sana, unaweza kutufanya tudhani tunampendeza Mungu kumbe hatumpendezi hata kidogo…Ni mara ngapi umeona watu wanaojiita wakristo wakiwachukia watu wasio wa Imani yao?…Utaona wanatoa mpaka maneno ya laana kwasababu tu sio wakristo kama wao…Wakati hao wanaowashutumu ndio Mungu anawaona ni MAJIRANI ZAO WAZURI kuliko hata wakristo wenzao..
Kama umefanya utafiti, utagundua kuwa fursa nyingi au msaada mwingi, Mungu anawatumia watu wasio wa Kristo au watu wa kiulimwengu kutusaidia kuliko watu wa ki-Mungu, Utaona watu ambao ni wakidunia wakati mwingine ni wakarimu na wanaojali kuliko hata watu wanaomjua Mungu. Hao Bwana anatuambia tuwapende kama nafsi zetu..hao ndio wasamaria wema..ndio majirani zetu, sio wakuwachukia na kuwasema bali kuwapenda kama nafsi zetu….
Sio kwasababu hamjui Mungu wako basi ndio awe sababu ya kuwa adui yako na kusema watu wa imani yangu tu ndio marafiki zangu, wakati mwingine Bwana anawatumia hao watu wasiomjua Mungu wako kukuletea wewe msaada kama ilivyokuwa kwa huyu myahudi aliyeangukia katikati ya wanyanganyi badala asaidiwe na watu wa dini yake na imani yake anakwenda kusaidiwa na watu hata wasioijua Torati..
Biblia imetuonya tu tusichangamane kufuata njia zao zisizofaa, kama ni walevi hatuenendi katika njia zao, kama ni waasherati vivyo hivyo, kama ni wacheza dansi, kama ni waabudu sanamu tusishirikiane nao hata kidogo…lakini sio tusiwapende na kuwachukia, wakitaka kukopa kwako usiwape kisogo, wakikuaribisha kwao usikatae, wakikupa zawadi pokea, wakiumwa uwatembelee… ili kwa matendo yetu mazuri na upendo wetu tuwavute waje upande wetu, na tuonekane tumeweza kuyafanya mapenzi ya Baba yetu aliye mbinguni.
Hivyo jawabu la mambo yote ni upendo, kwetu sisi kwa sisi na kwa wale walio nje.
Bwana atusaidie sote .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
UPENDO
UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?
BIBLIA ITUAMBIA TUSALIMIANE KWA BUSU TAKATIFU. HILI BUSU NDIO LIPI?
HAWA ALIPOLAANIWA ALIAMBIWA “TAMAA YAKO ITAKUWA KWA MUMEO”.NI TAMAA IPI INAYOZUNGUMZIWA HAPO?
Hapo nyuma, kabla sijampa Kristo maisha yangu, na wakati ambao bado ni mchanga kabisa wa masuala ya wokovu, niliaminishwa kuwa kigezo kikuu kinachomtambulisha mtu huyu kuwa anazo nguvu nyingi za rohoni ni kiwango chake cha UPAKO, pengine na wewe ulifahamu hivyo au unafahamu hivyo, yaani mtu kuwa na uwezo wa kufanya miujiza,au kuona vitu katika ulimwengu wa roho kama vile mapepo, wachawi,majini, kuona maono, kuota ndoto, kunena sana kwa lugha, au kufanya sana ishara.n.k. Kwamba mtu kama huyo ni mtu mwenye nguvu nyingi sana rohoni na hivyo shetani anamwogopa sana. Jambo hili lilinifanya nione shauku kutatufa Upako kuliko kitu kingine chochote.
Lakini je! Kwa mujibu wa biblia hizo ndizo nguvu za rohoni?. Leo tutajifunza juu ya hilo, na ni kitu gani tufanye ili nguvu zetu za rohoni ziongezeke. Sasa Ili kuelewa nini maana ya nguvu za rohoni, ni vizuri tujifunze kwanza juu ya nguvu nyingine, Tunajua siku zote kitu chochote chenye nguvu huwa kinakuwa na uwezo wa “kuteka na kutawala”, Simba ni mnyama mwenye nguvu na ndio maana ameteka pori lote, hivyo nguvu ya aina yoyote ile huwa inateka na kutawala, tunafahamu pia mtu mwenye nguvu ya kiuchumi huwa anatawala, mwenye nguvu ya kisiasa huwa anateka na kutawala, mwenye nguvu ya kiteknolojia huwa na uwezo pia wa kuteka na kutawala, na ndio maana tunaona mataifa kama Marekani na Ulaya, yanatawala dunia sio kwasababu ni makubwa hapana, bali kwasababu yana nguvu Fulani zinazowazidi wengine.
Vivyo hivyo na kwa mwenye nguvu za Rohoni, ni lazima mtu awe na uwezo wa kuteka na kutawala, na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya.
Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.”,
Unaona nguvu anazozizungumzia sasa hapo ni NGUVU ZA ROHONI. Ikiwa na maana kuwa mtu mwenye nguvu nyingi za Rohoni ndiye atakayeweza kuuteka ufalme wa mbinguni, ukiwa na nguvu chache utakuwa mnyonge tu. Na leo nataka ujue hizi nguvu za Rohoni zinapatikana wapi.
Sasa tukirudi kwenye huo huo mstari hapo juu, lazima tujiulize swali moja, ni kwanini Bwana alisema “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa”, kwanini hakusema tangu siku za Ibrahimu au za Musa hadi sasa? Badala yake anasema “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa”, . Utagundua kuwa Bwana alitaka tujifunze kitu Fulani kwa Yohana mbatizaji katika masuala ya kupata nguvu za rohoni. Hivyo embu tumwangalie kidogo Yohana alikuwa ni mtu na namna gani tangu utoto wake.
Maandiko yanatuambia:
Luka 1:80 “Yule mtoto akakua, AKAONGEZEKA NGUVU ROHONI, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli”.
Unaona kumbe Yohana tangu utoto wake alikuwa akiongeza nguvu rohoni kwa kasi sana, mpaka alipokuwa mtu mzima alipoanza huduma yake. Lakini hakuwahi kufanya muujiza hata mmoja, wala kutoa ishara yoyote kutoka mbinguni kama vile Eliya, Biblia inasema hivyo (Yohana 10:41), Na ndio maana tunasema Upako wowote kulingana na maandiko sio kitambulisho kuwa mtu huyo anazo nguvu za rohoni. Mtu unaweza akawa na uwezo wa kuona maono yote duniani lakini rohoni ukawa mdhaifu kuliko hata mtu aliyempa Kristo maisha yake leo.
Sasa tunaona Yohana alipoteza muda wake mwingi kukaa mbali na makazi ya watu ili tu kuongeza nguvu zake rohoni tangu utoto wake,(baadaye kidogo tutaona ni kitu gani alichokuwa anakifanya alipokuwa anakwenda kule jangwani) mpaka kufikia kilele cha nguvu za rohoni mpaka Bwana Yesu Kumshuhudia vile katika:
Mathayo 11:11 “Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; 12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.”.
Mathayo 11:11 “Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji;
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.”.
Kwa Nguvu alizokuwa nazo rohoni, hakukuwahi kutokea nabii au mtu yoyote katika agano la kale aliyeweza kumfikia, sio Ibrahimu, sio Musa, sio Eliya, sio Daudi sio mtu yoyote Yule aliyefanya mambo makubwa unayemsoma katika agano la kale aliyeweza kuwa na nguvu zaidi yake (Yohana) kuuteka ule ufalme. Lakini Leo utafahamu SIRI imelala wapi nawe uanze kujishughulisha nayo.
Sasa kumbuka Yohana tangu utoto wake hakuwahi kujishughulisha na jambo lingine zaidi ya kutafuta kumjua huyu MASIHI ALIYETABIRIWA NI NANI?. Ambaye ndiye kiini cha dini yao kiyahudi, ndiye kiini cha wokovu uliokuwa unatarajiwa wa ulimwengu mzima, wakati wengine wanang’ang’ania kukariri torati huyu aling’ang’ania kumtafuta Kristo ambaye Mungu alimshuhudia tangu enzi za kale za manabii. Na hiyo ndiyo iliyomfanya mbinguni aonekane kila siku nguvu zake za rohoni kuongezeka kwa kasi sana.
Alianza kutafuta kwa bidii katika torati habari zake, tangu mwanzo mpaka mwisho, kwa jinsi alivyokuwa anamtafuta kwa bidii akachunguza akaona kuwa kumbe kwa mfano ule ule wa wana wa Israeli walivyookolewa utumwani Misri ndivyo mwokozi atakavyouokoa ulimwengu wote kwa jinsi hiyo hiyo..
Kwa hatua zile tatu, ambapo hatua ya kwanza, ilikuwa ni Yule mwanakondoo kuchinjwa, ili damu ipatikane kwa pigo la mzaliwa wa Kwanza Misri, akajua kumbe damu ilihitajika kufungua vifungo. Na pigo lile lililegeza kweli vifungo vya maadui zao kuwapa ruhusu wa kutoka Misri, lakini lile halikutosha kuwafanya maadui zao wasiwafuatilie, hivyo ilihitajika hatua nyingine ya pili na ndio ile ya nguzo ya moto, ambayo ilikuwa inawatangulia mbele yao sasa ilibidi irudi nyuma yao kuweka wigo wasiwafuate.. Yohana akagundua kumbe moto ulipitia juu yao kuwatakasa pasipo wao kujijua.
Lakini moto ule haukutosha kumaliza kabisa adui yao ulipoondolewa, bado walitaka kuwafuata na ndipo tunaona maji yalifuata kuwatakasa tena, nako ndiko kule kuvuka bahari ya shamu Kubatizwa, na hapo ndipo maadui zao walipomalizwa moja kwa moja walipotoswa na yale maji.
Hatua hizo tatu (yaani damu ya mwana-kondoo, moto-wa-Roho Mtakatifu, na Maji), ndizo Yohana alitambua kuwa Masihi ajaye atazitumia kumkamilisha mwanadamu kwa wokovu wake.
Sasa hapo ndipo Yohana alipopatia ufunuo wa ubatizo wa Maji akaanza kuufundisha na kuwaambia watu wabatizwe, huku akitazamia kuwa mwanakondoo atakajua ambaye atakamilisha yaliyobakia yaani maji na moto wa Roho Mtakatifu,
Yohana 1:26 “Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi. 27 Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake. 28 Hayo yalifanyika huko Bethania ng’ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza. 29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, MWANA-KONDOO WA MUNGU, AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU! 30 HUYU NDIYE NILIYENENA HABARI ZAKE YA KWAMBA, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu. 31 Wala mimi sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nalikuja nikibatiza kwa maji. 32 Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake. 33 Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu. 34 Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu. 35 Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake. 36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu! 37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu”.
Yohana 1:26 “Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi.
27 Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.
28 Hayo yalifanyika huko Bethania ng’ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza.
29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, MWANA-KONDOO WA MUNGU, AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU!
30 HUYU NDIYE NILIYENENA HABARI ZAKE YA KWAMBA, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.
31 Wala mimi sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nalikuja nikibatiza kwa maji.
32 Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake.
33 Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.
34 Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.
35 Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.
36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!
37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu”.
(Soma pia Mathayo 3:11)..
Unaona hapo Yohana alimtambua YESU na Kazi yake atakayokuja kuifanya kabla hata hajawasili, alimtengenezea njia, Hivyo mbinguni akaonekana mtu mkuu sana, mwenye nguvu nyingi za rohoni japo duniani watu walimwona maskini amerukwa na akili.
Leo hii nataka nikuambie ndugu usifurahie tu kuwa YESU ameyaokoa maisha yako, halafu ukaridhika, mahali ulipo, unaendelea na mambo yako, YESU KRISTO ni zaidi ya unavyomfikiria, Mungu kaweka Heshima yake yote pale, ndio hekima ya Mungu na NGUVU YA MUNGU (1Wakorintho 1:24), na ndipo utajiri wote, na hazina zote za maarifa zilipolala. Hapo ndipo Yohana alipopatia heshima yake na ukuu wake.
Wakolosai 2:2 “….wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo; 3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.”
Wakolosai 2:2 “….wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo;
3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.”
Kwa mtu Yule leo hii anayejishughulisha kutafuta kumjua YESU usiku na mchana, mtu huyo nguvu zake za rohoni zinaongezeka kwa kasi sana pasipo hata yeye kujijua. Na mwisho wa siku anajikuta anauteka ufalme wa Mbinguni kirahisi kabisa kwasababu amefahamu mahali lulu ya thamani ilipo.
Itafute hii LULU ndugu. Nataka nikuambie vita kubwa ya shetani ipo hapo, watu wasimjue Kristo ni nani hasaa na uweza wake, yeye anataka watu wamwone kama mtu wa kawaida tu, kwasababu anafahamu mtu akishamwelewa vizuri Bwana Yesu ni nani, basi atajijengea daraja zuri mbinguni na atamsababishia madhara makubwa sana katika ufalme wake.
Anza leo mwanzo mpya, maanisha kumfauta Kristo…usitafute upako wala miujiza..Bwana akikujalia hizo ni vizuri lakini sio jawabu la kuwa na nguvu za rohoni…Ikiwa unapenda kuwa mkuu hata zaidi ya Yohana, machoni pa Mungu,wala usijishughulishe na jambo lingine lolote, JISHUGHULISHE KATIKA KUMTAFUTA KRISTO, acha kuzisumbukia karama, acha kutafuta maombezi, acha kukesha kwa ajili ya upako, kesha kwa ajili ya KUMSOMA KRISTO. Sisemi usizitumie hizo karama, hapana zitumie maadamu Mungu kakupa, lakini huku nyuma usisahau kuwa ufalme wa mbinguni unatekwa na wenye nguvu za mafunuo ya YESU Kristo. Tumeaswa tumjua sana Yesu Kristo, Mwana wa Mungu mpaka tufikie kimo cha utimilifu wake.
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”
Unapoyatafakari maandiko, jenga mtazamo wa Kristo ndani yake, wengi wakifungua maandiko wanayatazama kwa sura ya mafanikio ya kidunia, hivyo wanapata ufunuo kulingana na walichokitazamia, lakini ukimsoma Kristo kwa lengo la kutaka kumjua zaidi…atakujaza maarifa na nguvu za rohoni, atajifunua kwako na kuanza kukufundisha kanuni zake zote kwa namna ya ajabu sana.