Na kama vile kila mjumbe alikuwa anamulika NURU ya wakati ule kwa kila kanisa, vivyo hivyo baada ya Mungu kuamishia INJILI Israeli kuna watu ambao Mungu atawanyanyua kuwahubiria INJILI ambayo itawafanya wao wamwamini YESU KRISTO waliyemkataa miaka 2000 iliyopita, Kumbuka leo hii Wayahudi hawamwamini YESU kuwa ndiye masia aliyetabiriwa juu yao atakayewakomboa wanasema “Kama huyu YESU ndiye Masia, na leo hii afanye zile ishara walizozifanya manabii nasi tutamwamini”, wakiwa na maana ishara kama vile za MUSA na ELIYA, Kushusha moto, bahari kuwa damu, n.k.