Uradhi wa Mapenzi yake ni nini? (Waefeso 1:5)

Uradhi wa Mapenzi yake ni nini? (Waefeso 1:5)

Jibu: Tureje..

Waefeso 1:5 “Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe WANAWE kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na URADHI WA MAPENZI YAKE”.

Maana rahisi ya “Uradhi wa Mapenzi” ni “Mapenzi ya Hiari”..

Mtu anayefanya kazi fulani kwa Hiari yake mwenyewe na kwa mapenzi yake yote bila kusukumwa, kulazimishwa wala kuhamasishwa mtu huyo ni sahihi kusema amefanya kazi ile kwa “Uradhi wa Mapenzi”.

Na Mungu ametupenda alituchagua sisi tuwe “Watoto wake”.. Kwa mapenzi yake ya Hiari.. na kwa furaha ya Moyo wake, Maana yake ni jambo linalompa raha na furaha sisi kuwa watoto wake, sio uamuzi wa majuto kwake..

1Yohana 3:1 “Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, KWAMBA TUITWE WANA WA MUNGU; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye”.

Kwahiyo ni bahati na upendo mkubwa sana MUNGU kutufanya sisi kuwa watoto wake, na Kuwa Mtoto wa Mungu maana yake ni lazima utabeba tabia za Uungu, na ndio maana wana wa MUNGU wanaitwa miungu..

Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, NDINYI MIUNGU?

35 Ikiwa ALIWAITA MIUNGU wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.

Ni hii ni kweli kabisa mwana ni lazima afanane na Baba, hata mtoto wa Mtu ni Mtu, mtoto wa kondoo ni kondoo, na mtoto wa simba ni simba..vivyo hiyo ni mtoto/watoto wa MUNGU ni miungu.

Je umefanyika mtoto wa MUNGU?.. Na je unaijua kanuni ya kufanyika kuwa mtoto wa MUNGU?.. Si nyingine zaidi ya ile tunayoisoma katika Yohana 1:12..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”

Mpokee leo YESU nawe utapata uwezo huu mkuu wa kuwa mwana wa Mungu na mrithi wa ahadi za MUNGU… kwasababu ni Uradhi wa mapenzi yake tuwe hivyo.

Waefeso 1:9 “akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?

JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?

Siku ya kujiliwa inayozungumziwa katika  1Petro 1:12, ni ipi?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?

Print this post

 Buu/ Mabuu humaanisha nini kwenye biblia?

Kibiblia ni neno lenye maana ya wale funza, ambapo hutokea palipo na mzoga, au uozo. Hivyo popote ukutanapo na Neno hilo, huashiria/humaanisha, uharibifu au maiti, au kaburi,

Kwamfano ukisoma;

Ayubu 17:14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;

Buu kama lilivyotumika hapo ni kaburi, Ayubu akimaanisha katika hatua aliyofikia, kaburi, na uharibifu ni kama familia yake (baba yake, mama yake na dada yake), kama tunavyojua familia ni kitu cha karibu sana na mtu, ndivyo Ayubu alivyojiona katika hali aliyokuwa amepitia.

Maana yake, kifo kilikuwa karibu na yeye zaidi hata ya familia yake.

Sehemu nyingine inasema;

Ayubu 25:6 iuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!

Mwandishi akimaanisha mwanadamu ni sawa na mzoga, (yaani mwili wenye uharibifu usio na umilele).

Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;

Kutoka 16:20,24, Kumbukumbu 28:39, Ayubu 7:5.

Katika maeneo mengine kwenye biblia linatajwa moja kwa moja kama  funza. (Isaya 66:24)

Hii ni hatma ya kila mwanadamu asiye na Mungu, yeye ni buu, haijalishi atakuwa na afya leo, anapesa zote ulimwenguni, anacheo kikubwa au elimu, maisha yake bila Yesu Kristo kumwokoa, ni buu tu (maiti, kaburi, )..atakufa na kuishia jehanam ya moto. Lakini  akiokoka, hata ajapokufa, ataishi, siku ya ufufuo ikifika, atafufuliwa na kubadilishwa mwili wake na kupewa mwili mwingine wa utukufu, kisha Kwenda kuishi na Kristo milele na milele mbinguni.

Ikiwa haujaokoka, bado na upo tayari kufanya hivyo leo, basi basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba upokee msamaha wa dhambi leo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).

Jehanamu ni nini?

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

Print this post

IFAHAMU NGUVU YA DAMU YA YESU KABLA YA KUSULIBIWA.

Shalom, karibu katika kuyatafakari maandiko..

Inafahamika kuwa Kristo alimwaga Damu yake pale Golgotha, pale ambapo misumari ilipopita katikati ya mikono yake na miguu yake, pamoja na mapigo mengine mwili mzima. Kwa damu ile iliyomawagika tulipata ondoleo la dhambi na ukombozi wa Roho zetu,

Lakini Damu hiyo hiyo, tunasoma haikuanza kumwagika saa hiyo ya Mateso ya msalaba…Bali ilitangulia kumwagwa wakati Bwana akiwa anaomba pale kwenye mlima wa Mizeituni pamoja na wanafunzi wake,

Sasa ilimwagika kwa jinsi gani?.. si kwa jinsi nyingine bali kwa jinsi ya JASHO LAKE

Luka 22:44 “Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; HARI YAKE IKAWA KAMA MATONE YA DAMU YAKIDONDOKA NCHINI.]

Sasa swali la msingi ni kwanini, itoke wakati akiwa katika MAOMBI?..  Ni kwasababu maneno pekee hayatoshi kufikisha maombi kwa Baba, bali Damu inanena zaidi kuliko maneno, na Hivyo ile damu iliyokuwa inamwagika wakati wa maombi ilinena zaidi kuliko maneno tu.. Kwa namna gani tunalithibitisha hilo??..Turejee habari ya Habili.

Biblia inasema Damu ya Habili ilinena ardhini baada ya kuuawa kwake..ijapokuwa alikufa lakini ile damu ililia na kuomboleza mbele za Mungu.. (soma Mwanzo 4:10) na Mungu akaisikia, na ikaleta kisasi kwa Kaini aliyemwua..

Vile vile maombi ya Bwana YESU pamoja na Damu yake inayomwagika ardhini kabla ya mateso ya msalaba.. ilinena zaidi na ndio maana baada ya pale, walitumwa Malaika kumtia Nguvu..na tena Damu ya YESU inanena mema kuliko ile ya Habili..

Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Na wakati huu tunapoomba kwa kufahamu Ufunuo huo uliopo katika Damu ya YESU, tutapenda MAOMBI!.. tukijua na kuamini kuwa ipo damu ya YESU inayochuruzika sasa kwaajili yetu tunapoomba.. na hiyo damu inanena mema zaidi ya maneno yetu.

Lakini kama tupo nje ya Imani ya kumwamini Bwana YESU KRISTO, damu yake hiyo haiwezi kunena mema kwaajili yetu, ili iweze kunena mema na kumshinda Yule Mwovu, na hata kuvuta majibu ya maombi, ni sharti kwanza kumwamini Bwana YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kubatizwa ubatizo wa maji na Roho, kuanzia huo wakati na kuendelea ile damu inakuwa inanena mema kwaajili yako na utakuwa unazo nguvu za kumshinda shetani.

Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NA SISI TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.

Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?

Print this post

Ni umeme gani Bwana anaouzungumzia katika (Mathayo 24:27)?

Swali: Katika Mathayo 24:27, tunaona “UMEME” ukitajwa, Je kipindi cha Bwana YESU umeme ulikuwepo?


Jibu:  Turejee..

Mathayo 24:27 “Kwa maana kama vile UMEME utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu”.

Umeme unaozungumziwa hapo ni ule “MWANGA WA RADI” unaoonekana nyakati za Mvua… Kwaasili “Radi” ni “Umeme” na si Moto. Na tangu Uumbaji Radi zipo,

Ayubu 28:26 “Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa UMEME WA RADI”.

Soma pia Ayubu 37:15, Zaburi 77:18, Zaburi 135:7, Yeremia 10:13, Yeremia 51:6, Danieli 10:6 na Nahumu 2:4 na Luka 10:18.

kwahiyo hapo maandiko yamemaanisha kuwa kama vile Radi imulikavyo kutoka mashariki hata magharibi ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake mwana wa Adamu.

Na kwanini Umeme umetumika kufunua ujio wa YESU?.. Ni kwasababu ya Nguvu ya Umeme, na kasi ya Umeme.. Kikawaida Radi huwa inapiga sehemu ya juu iliyoinuka nan a inaweza kupasua mti wa Mbuyu ulio mkubwa vipande viwili chini ya dakika moja..

Na YESU KRISTO atarudi kwa nguvu hizo hizo, na kupakanyaga mahali pa juu pa dunia palipoinuka (Amosi 4:13)

Isaya 22:5 “Kwa maana siku ya kutaabika, SIKU YA KUKANYAGWA, SIKU YA FUJO INAKUJA, itokayo kwa Bwana, Bwana wa majeshi, katika bonde la Maono; inabomoa kuta; na kuililia milima”.

Je umempokea YESU?.. na kumfanya Bwana na Mwokozi wa maisha yako? Na kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza yeye?.. Kama bado unasubiri nini?.. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa YESU leo, kwamaana siku hizi tuishizo ni siku za hatari na dakika yoyote ule mwisho unafika.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Print this post

“MIMI NDIMI” SABA.

Biblia inatufundisha kumfahamu sana MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO)..

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”

Tukimjua vizuri mwana wa Mungu tutaweza kutembea naye vema, tutaweza kumpendeza vema na vile vile tutaweza kumheshimu zaidi.

Leo tutazame jinsi MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO) alivyojitambulisha mwenyewe mara saba (07) kama “MIMI NDIMI”.

    1. MIMI NDIMI MKATE WA UZIMA.

Yohana 6:35 “Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe”.

Maneno haya ameyarudia tena katika mstari wa 48 na 51 ya mlango huo huo wa sita (06).. Ikiwa na maana kuwa tukimpata YESU maishani ni zaidi ya chakula cha damu na nyama.. chakula cha damu na nyama kinatoa uzima wa masaa machache tu, au siku chache tu, na baadaye mtu atasikia tena njaa, na asipokula anakufa, lakini YESU ndiye chakula cha UZIMA, ambacho mtu akila hatasikia tena njaa.. bali atakuwa na uzima wa milele.

    2. MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU.

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.

Kwa kumwamini YESU na kuyaishi maneno yake, maisha yetu yatakuwa na Mwanga, kila mahali tutakapokwenda na kila tutakachofanya kitakuwa na mwelekeo kama vile mtu anavyotembea katika Nuru..

   3. MIMI NDIMI MLANGO WA KONDOO

Yohana 10:7 “Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo”.

Yeye ndiye mchungaji mwema, na kama vile Mchungaji anavyowahesabu kondoo wake wanaoingia na kutoka zizini, na kwamba hakuna hata mmoja atakayepotea mkononi mwake, kadhalika na YESU ndiye Mchungaji wetu, atulindaye na kutuongoza zizini, kuingia kwetu na kutoka kwetu, wala mkononi mwake hatutapote.

    4. MIMI NDIMI MCHUNGAJI MWEMA.

Yohana 10:11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo”.

Mchungaji mwema ni Yule anayejitoa hata uhai wake kwaajili ya kondoo, na Kristo aliutoa uhai wake kwaajili yetu, kuonesha upendo wake mkuu kwetu.

    5. MIMI NDIMI UFUFUO NA UZIMA.

Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”

Kwa kumwamini YESU tunalo tumaini la kufufuliwa siku ya mwisho, hakuna mwanadamu yoyote wala malaika aliyewahi kumwahidia mwanadamu yoyote ahadi kama hii inayotoa tumaini baada ya kifo.

   6. MIMI NDIMI NJIA, KWELI NA UZIMA.

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.

Hakuna njia ya mkato ya kufika mbinguni, isipokuwa kupitia YESU KRISTO, tukilijua hili tutamwangalia kwa bidii ili tuwe warithi wa uzima wa milele.

    7. MIMI NDIMI MZABIBU WA KWELI.

Yohana 15:1 “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima”.

Tunapokaa ndani ya YESU ni kama matawi katika shina la mzabibu, ambalo linazaa sana, na sisi tutazaa sana kama tukikaa ndani ya YESU KRISTO.

Je umemkaribisha huyu YESU (Mkuu wa Uzima) maishani mwako?.. au bado unatanga-tanga na dunia tu!.. badilisha uelekeo leo, anza kutembea na YESU aliyejaa heshima.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

ELOI ELOI LAMA SABAKTHANI?

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

ZIFAHAMU ALAMA KUU NNE ZA KRISTO NDANI YAKO.

JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.

Print this post

Nini maana ya “AMETUPENDA UPEO” (Yohana 13:1) ?

 Turejee..

Yohana 13:1 “Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo”.

“Upeo” ni kiwango cha mwisho cha Jambo… Kwamfano ukitazama juu, upeo wa macho yako unaishia kuona nyota zaidi ya hapo huoni kingine.. kwahiyo tunaweza kusema upeo wa kuona kwetu angani ni nyota..

Vile vile tunapofikiri kumhusu MUNGU, (kwa namna gani hana mwanzo wala mwisho) tunafikia kikomo cha kufikiri, tunafika mwisho wa Upeo wetu wa kufikiri (hatuwezi kufikiri zaidi ya hapo na kupata majibu).. na mambo mengine yote yana upeo wake..

Sasa hapa Bwana YESU aliposema kuwa “aliwapenda watu wake Upeo”.. maana yake alitupenda kiwango cha juu kabisa cha UPENDO, ambacho baada ya hicho hakuna kingine…

Upendo wa YESU kwetu ni MKUU mno, kina cha upendo wake,  urefu wa upendo wake, mapana mapana ya upendo wake na kimo cha upendo wake hakielekezeki..

Waefeso 3:18 “ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;

19 na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu”.

 Mahali pengine anasema hivi..

Yohana 5:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake”.

Ni rahisi mtu kuutoa uhai wake kwaajili ya mtoto wake, au mzazi wake au ndugu yake yoyote wa damu, lakini ni ngumu mtu kuutoa uhai wake kwaajili ya Rafiki..  Kwasababu marafiki hawatabiriki, leo anaweza kuwa rafiki yako kesho msaliti wako, na adui..

Mtu anaweza kutoa msaada kwa rafiki yake lakini  si UHAI, na mtu kama huyo akitokea basi upendo wake ni mkubwa sana!… na hapa Bwana YESU anajitaja yeye, kwamba anautoa uhai wake kwaajili ya rafiki zake, na tena si rafiki mmoja, bali wengi, ijapokuwa anajua kuwa katikati ya marafiki wapo wanafiki na wasaliti, lakini anautoa uhai wake kwaajili yao wote.. hakika  huo ni UPEO wa mwisho kabisa wa Upendo.

Biblia inasema mtu ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe..lakini YESU ametufanya sisi kuwa rafiki zake na ametupenda kuliko ndugu.

Mithali 18:24 “Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; LAKINI YUKO RAFIKI AAMBATANAYE NA MTU KULIKO NDUGU”.

Neno la Mungu linazidi kutufundisha juu ya huu UPEO WA UPENDO WA YESU, kuwa hakuna chochote kilichopo duniani, wala kilichopo mbinguni, wala mahali pengine popote kitakachoweza kutuondolea Upendo wa YESU kwetu,.. YESU mwokozi ataendelea kutupenda na hakuna mtu atakayetuchonganisha naye..

Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.

34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.

37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.

38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa kama tunapendwa kwa upendo mkuu namna hii kwanini na sisi TUSIPENDEKEE??…Kwanini tusiitikie vyema huu upendo kwa kumpa yeye maisha yetu, na muda wetu na mioyo yetu?..

Utajibu nini siku ile, utajiteteaje siku ile, kama leo ukiudharau upendo huu mkuu?.. Ni heri ukampokea YESU leo kama bado hujafanya hivyo, kwa kutubu na kupokea Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;

JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

 

Print this post

UNAJISIKIAJE, KUTEMBEA NA SANDA?

Yohana 11:44

[44]Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.

Nakusalimu Katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Nataka tujifunze jambo moja Kwa Lazaro aliyefufuliwa…

Kama tunavyojua mtu huyu alikufa, akazikwa na akaoza pia..lakini Bwana Yesu alipofika kaburini Alifanya muujiza mkubwa wa kumfufua.

Na kweli Lazaro alitoka kaburini akiwa mzima kabisa bila shida yoyote…Lakini wengi wetu tunaishia hapo, na kusema Bwana Ametenda muujiza…Lakini Yesu alipomwangalia aliona bado akatoa agizo akisema mfungueni mkamwache aende zake.. Maana yake ni kuwa ufufuo, ulimpa uzima kweli lakini sio uhuru..

Ilihitaji afunguliwe, maana kaburi lilimfunga mikono yake, miguu yake pamoja na uso wake…hata alipofufuka bado liliacha mizizi yake kwa mtu.

Maana yake ni nini..

Ufufuo unafananishwa na wokovu, Mtu anapomwamini Yesu anakuwa tayari amefufuka kutoka katika wafu…lakini hilo peke yake halitoshi, bado Anakuwa na kamba za makaburini (maisha ya kale), hivyo anapaswa afunguliwe…

Ukiokoka haimaanishi, tabia za kale zote zitaondoka siku hiyo hiyo, unahitaji kukubali kufunguliwa, ili uwe huru kwelikweli..

Sanda, zilizomzinga Lazaro, uso wake, miguu, mikono, kama wavu wa bui-bui, hutembei, Hushiki wala huoni…ndio maisha Ya wakristo wengi baada ya kuokoka yalivyo..

Zile tabia za kale wanaendelea nazo, uchungu, wivu, hasira, uadui, maumivu, vinyongo, hofu, wasiwasi, wanashindwa kuendelea mbele kwasababu hawatoi nafasi ya kufunguliwa…

Angalia hapo Bwana Yesu anasema..”Mfungueni, mkamwache aende zake…”

Hasemi jifungue…bali mfungueni…yapo mambo huna budi kukubali kusaidiwa ili upone..

Ndio hapo Mungu akaweka…Kanisa.

Ambapo..

Utakutana na wachungaji.. kukusimamia na kukulisha mpaka utakapokomaa Na kukua vizuri kiroho…kuishi bila kanisa yaani mwenyewe mwenyewe tu, ni sawa na kutembea na sanda lako,

Kumbuka Bwana anatarajia umzalie matunda mara baada ya wokovu wako…yapo majukumu ya kufanya baada ya kuokoka..lakini ikiwa miguu na mikono na uso umefungwa unatarajia nini hapo?

Kubali kufundishika, Kubali kuchungwa, kubali mashauri na kuonywa, kubali kuombewa, kubali kuishi na ndugu (katika Bwana), kubali kusoma Neno, kuomba na wenzako utafunguliwa sana.. zaidi ya kuridhika tu na wokovu ulioupokea ukidhani utazalisha chochote katika hali hiyo hiyo ya kiroho ambayo upo peke yako peke yako.

Mara nyingine hata maono yako huwezi kuyafikia kwasababu umefungwa miguu yako. usisonge mbele.. Ogopa sanda, kama vile unavyoogopa mauti.

Ukijiona  una tabia ambazo haziendani Na hali mpya ya wokovu ulioupokea basi ndio wakati wa kushughulika na sanda lako, kwa kutii na kufuata hayo maagizo. Jiwajibishe, tendea kazi wokovu Wako, kwasababu kila mtu anawajibu wa kufanya hivyo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Hofu ya Bwana ni nini? (2Wakorintho 5:11)

Sheria ya uhuru ni ipi? (Yakobo 2:12)

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Print this post

Nini maana ya “Ninautesa mwili” (1Wakorintho 9:27)?

Jibu: Turejee..

1Wakorintho 9:27 “BALI NAUTESA MWILI WANGU na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Kuutesa mwili kunakozungumziwa hapa si kujiumiza kwa viboko na mapigo… bali ni kuuzuia mwili kupata vitu viupendavyo, ili makusudi kutimiza mapenzi ya MUNGU.

Mfano wa vitu ambavyo vikizidi sana kufanyika katika mwili vinaathiri mbio za kiroho ni pamoja na VYAKULA NA USINGIZI vipo na vingine vingi lakini hivi ndio vikuu..

  1. VYAKULA

Kula kila wakati kwa kipindi kirefu bila kuwa na vipindi vya KUFUNGA kunaathiri ukuaji wa kiroho na kuna mambo ambayo hayatatokea, kwani Biblia imesema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba..

Mathayo 17:19 “Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?

20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA.]”

Kwahiyo Mtu mwenye desturi ya kufunga mara kwa mara na kuomba anakuwa anautesa mwili wake lakini anakuwa anapata faida kubwa rohoni

   2. USINGIZI.

Mtu anayejizuia kulala kwa lengo la kuutafuta uso wa Mungu kwa Maombi,  pia anahesabika kuwa anautesa mwili, na faida yake pia ni kubwa..

Marko 14:37 “Akaja akawakuta wamelala usingizi, akamwambia Petro, Je! Simoni, umelala? Hukuweza kukesha saa moja?

38 Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu”.

Na mwisho kumbuka, kujizuia kufanya dhambi kama uzinzi, ulevi, sio kuutesa mwili, bali ndio kuupa mwili pumziko..kwasababu dhambi ni sumu ya mwili pia, dhambi inauharibu mwili… Mtu anapojizuia kutenda dhambi katika mwili, mwili wake hauteseki badala yake ndio unajengeka zaidi, kwahiyo usichanganye kutotenda dhambi na kuutesa mwili.

Ukiona dhambi kama Ulevi au Uzinzi au nyingine yoyote inakufanya mateka, kiasi kwamba usipoifanya mwili wako unateseka basi ni dalili ya kuwa bado utakaso kamili haujaingia maishani mwako, hivyo ni wakati wa kumgeukia Bwana kwa moyo wote kwa kutubu, kubatizwa kwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU na kisha kupokea Roho Mtakatifu,

Na ile sheria ya Roho wa uzima itakuweka huru mbali na dhambi, BUREEEEE kabisa..

Warumi 8:2 “Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti”.

Bwana atusaidie tuitese miili yetu kwa kufunga na kuzuia usingizi, ili tupate muda wa kukesha na kuomba kwa faida ya roho zetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

Sheria ya uhuru ni ipi? (Yakobo 2:12)

Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?

Print this post

Hofu ya Bwana ni nini? (2Wakorintho 5:11)

Swali: Hofu ya Bwana inayotajwa katika kitabu cha 2Wakorintho 5:11, ni hofu ya namna gani?


Jibu: Turejee..

2Wakorintho 5:11 “Basi tukiijua HOFU YA BWANA, twawavuta wanadamu; lakini tumedhihirishwa mbele za Mungu. Nami natumaini ya kuwa tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia”.

“Hofu ya Bwana” au “Hofu ya Mungu”.. Ni hali ya kuhofia Hukumu ya Mungu ijayo..

Tukianzia mstari wa juu kidogo katika maandiko hayo tunasoma kuwa kila mtu itampasa kusimama mbele ya kiti cha hukumu na kupokea malipo ya kazi yake.

2Wakorintho 5:9 “Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye.

10 Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”.

Na mahali pengine Biblia inasema kila atatoa habari zake mwenyewe..

Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”.

Hivyo hiyo hali na kutafakari mambo yajayo, kwamba tutasimama mbele ya kiti cha hukumu, inazaa hofu, na hofu hiyo ndio ijulikanayo kama “Hofu ya Bwana” au “Hofu ya Mungu”.. Na wakati mwingine hofu hii haimpeleki mtu kuogopa hukumu ijayo baada ya kifo, bali hata akiwa hai, kwasababu pia Mungu anaweza kumhukumu mtu bado akiwa hai, kwa kuruhusu madhara yampate.

Mfano wa watu katika maandiko walioonekana kuwa na Hofu ya Mungu, ni Yule mnyang’anyi aliyeangikwa msalabani pamoja na Bwana.

Luka 3:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.

40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, WEWE HUMWOGOPI HATA MUNGU, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako”.

Na mfano wa Mtu/Watu katika maandiko waliotajwa kukosa Hofu ya Mungu kabisa ni wale watu wa Sodoma na Gomora na wenyeji wa nchi ya Gerari..

Mwanzo 20:10 “Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?

11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu”.

Na sisi ni lazima tuwe na “Hofu ya Mungu” siku zote, ili tuikwepe huku ya Mungu..kwani madhara ya kukosa hofu ya Mungu ni makubwa.. Tukiwa na hofu ya Mungu ndani yetu, tutajitenga na dhambi kwa namna yoyote ile.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nyakati za Mwisho na Tumaini la Utukufu kwa Mwamini Mpya

IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!

Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?

Print this post

Sheria ya uhuru ni ipi? (Yakobo 2:12)

SWALI: Sheria ya uhuru ni ipi inayozungumziwa na mtume Yakobo kulingana na maandiko?

Yakobo 2:11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.
12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.

Neno hili pia utaliona likitajwa na mtume Yakobo katika vifungu vingine vya juu.

Yakobo 1:25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.

Katika biblia zipo sheria kuu mbili

  1. Sheria ya kwanza ni sheria ya dhambi na Mauti (Warumi 8)
  2. Na sheria  ya pili ni sheria ya Roho wa uzima.

Sheria ya dhambi na mauti ndio ile ya torati, ambayo kazi yake kubwa ni kufichua uovu, kushtaki makosa, lakini haimfanyi  mtu kuwa huru, kwa mfano sheria inasema usizini, mtu atakataa kuzini, sio kwasababu hapendi uzinzi, lakini kwasababu sheria imesema tu hivyo, anaogopa adhabu atakapotenda hiyo dhambi atauawa.

Lakini sheria ya Roho wa uzima, ni sheria ya Mungu, isipokuwa hii mtu anavuviwa na Roho Mtakatifu, nguvu ya kuishi sawasawa na matwaka ya Mungu, bila shuruti Fulani, ni ya uhuru. Mfano labda sheria inasema usiue, mtu haui sio kwasababu sheria imesema, lakini kwasababu moyoni mwake hiyo nia, tamaa, au kiu ya kuua haipo, hivyo hata kama sheria isingesema hilo jambo lisingekubalika ndani yake, Hivyo mtu kama huyu tunasema ni huru na sheria, hayupo ki-sheria, sheria haimtawali  ijapokuwa sheria yenyewe ipo.

Mtu akishaokoka, anakutana na sheria mpya ya Mungu, ambayo hiyo ni lazima ifuatwe na ishikwe, lakini inakuwa ya uhuru, sio tena ya kifungo, kwasababu Roho Mtakatifu anamsaidia huyo mtu kuiishi..

Ndio hiyo inayoitwa sheria ya uhuru, kwenye kitabu cha Yakobo.

Maana yake ni nini? Sisi kama waamini, Mungu anatarajia tuonyeshe matunda ya Imani yetu katika upendo, huruma, na matendo mema, kwasababu tunaye Roho.

Hivyo inapotokea, hayo hayaonekani, sheria itatuwajibisha, kutuhukumu, au vinginevyo hatukupokea sheria hiyo ya uhuru.. Ni sawa, na mtu aende kuua watu ovyo bila sababu yoyote,

Mtu huyu atahukumiwa, sawa tu na yule ambaye amesukumwa na sababu fulani, labda kisasi, hasira, wivu, chuki n.k.,

Hivyo sisi waamini, tulipokuwa huru na dhambi, hatupaswi kufikiri kuwa ndio tuna uhalali wa Kutenda dhambi. Kinyume chake, tujue kuwa ipo sheria yetu ya uhuru, itakayotuhukumu, kama tu vile wale wengine walivyohukumiwa kwa sheria ya dhambi na mauti (torati).

Ndicho alichokisema mtume Yakobo..

Kwa hitimisho ni kuwa sheria ya uhuru, ni sheria tunayoitimiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Ambayo hiyo pia itatuhukumu. Hivyo wewe kama mwamini, hakikisha wokovu wako unathibitika kwa kazi zake njema, chini ya upendo

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29)

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)

Print this post