Title January 2019

DHAMBI YA ULIMWENGU.

Dhambi ipo moja tu! nayo ni kutomwamini BWANA YESU KRISTO, hayo mengine ni matokeo ya dhambi, uwizi, usengenyaji, rushwa, uasherati, utukanaji, uuaji n.k si dhambi bali ni matokeo ya dhambi iliyo moja tu! nayo ni KUTOKUMWAMINI BWANA YESU KRISTO.

Na kumbuka kumwamini Yesu Kristo, sio kumsoma na kuamua kumwamini, hapana! Bali ni kupata ufunuo wa yeye ni nani, alitoka wapi, alikuja kufanya nini, na umuhimu wake kwa ulimwengu ni upi?.…ukishamwelewa kwa namna hiyo, basi ndani yako kutawaka shauku ya kutaka kujishughulisha na mambo yake (hapo utakuwa tayari umeshamwamini).

Kwahiyo kama dhambi ni moja tu! ambayo ni kutokumwamini Kristo Yesu Kristo, hayo mengine ni matokeo ya hiyo dhambi, Hivyo siku ya hukumu Bwana hatamuhukumu mtu kwasababu alikuwa mvuta bangi, au kwasababu alikuwa mwasherati, au kwa sababu alikuwa mwongo…hapana atamuhukumu mtu kwanza kwa sababu hakumwamini YESU KRISTO, MWANA WA MUNGU. Hiyo ndiyo dhambi ya msingi kabisa..

Yohana 3: 17 “Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.

18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; ASIYEAMINI AMEKWISHA KUHUKUMIWA; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.

Tuchukue mfano mwepesi, kuna kichaa mahali Fulani, kaonekana akivunja vioo vya magari ya watu, na kupiga watu barabarani, na kaharibu mali, na kisha wakamkamata na kumfunga kamba! Je! wale waliomfunga kamba watamhukumu kwanza kwa kuanza kumuuliza kwanini amevunja vioo vya magari?, au kwanini anapiga watu, au kwanini ni mwaribifu…utagundua kwamba! Hawataweza kufanya hivyo…watajua tatizo halipo katika matendo anayoyafanya, bali tatizo lipo katika akili zake nalo ni ile hali ya ukichaa iliyondani yake!!…Hivyo wakitaka wapate ufumbuzi wa tatizo lao, watashughulika kwanza na tiba ya akili yake, zaidi ya tiba ya mambo anayoyafanya, hawawezi kumshauri aache uaribifu, au aache kupiga watu katika hali yake ya ukichaa aliyokuwepo, ni sawa na kupaka rangi upepo.. sharti wamtibu kwanza tatizo lake hilo moja!..Na mengine yatatibika yenyewe.

Ndivyo ilivyo kwa mtenda dhambi yoyote yule aliye mwasherati, mwizi, muuaji, mla rushwa, msengenyaji n.k….tatizo lake ni moja tu HAJAMWAMINI YESU KRISTO. Hajapata ufunuo utakaoweza kumfanya aache vitendo viovu. Na njia pekee ya kuviacha hivyo haitaokani na bidii au nguvu za mtu binafsi, anaweza akajitahidi kufanya hivyo leo na kesho lakini kesho kutwa akarudia uchafu wake ule ule wa kale, bali hiyo inakuja kwa kumwamini yule awezaye kuondoa mambo hayo ndani ya mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Biblia inasema “ Yohana 1:29 “Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU!”

Ukisoma hapo kwa makini utaona hakusema “AZICHUKUAYE DHAMBI ZA ULIMWENGU” bali imesema “AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU”..ikimaanisha kuwa hiyo dhambi NI MOJA TU! sio nyingi nayo ni KUTOKUAMINI. Ndugu Yesu pekee ndiye anayeweza kuwa tiba ya hofu unayopitia sasa hivi, yeye pekee ndiye anayeweza kuwa kimbilio lako yeye pekee ndiye nguvu zako na faraja yako, yeye pekee ndiye kila kitu kwako, wewe peke yako hutaweza kuondoa dhambi yoyote ndani yako, kadhalika mwingine yoyote hakuna. Hivyo Ndivyo ilivyo, na ndivyo itakavyokuwa daima. Na huo ndio ukweli. Hakuna mwingine, na mtu akimpinga huyo basi amethibitisha kwamba yeye mwenyewe anaweza kujiokoa na kusimama kwa nguvu zake kumshinda shetani na dhambi…Lakini fahamu kuwa hakuna ambaye alishawahi kuwa mkamilifu kwa nguvu zake mwenyewe tangu dunia kuumbwa isipokuwa YESU pekee.

Kwa yeyote atakayemwamini na kumpokea HATI hiyo ya dhambi itaondolewa juu yake. Na kutakaswa kila siku wa Roho wake. Lakini kwa atakapuuzia hukumu hatoikwepa kwa namna yoyote.

Bwana alisema sharti injili ikahubiriwe kwa kila kiumbe, ndipo ule mwisho uje!! Na ni kwasababu Neno lake huwa halipiti! Ni lazima kila mtu atasikia habari za Yesu Kristo, wengine mara moja tu! wengine mara mbili mbili, wengine mara tatu tatu..Lakini mwisho injili itasikika kwa kila mtu, Roho Mtakatifu atanyanyua watu wake popote pale, iwe mijini, iwe vijijini, iwe shuleni, iwe mtaani, iwe gerezani iwe ikulu..Injili itafika..Na wewe unayesoma ujumbe huu, leo imekufikia kwa njia hii, sijui kwako hii ni mara ya ngapi?..labda ni mara ya kwanza, au mara ya 20..jibu unalo wewe… Lakini umesikia habari za Huyu Yesu Mkombozi wa ulimwengu na Madhara ya kutomwamini. Ni heri ukamtafuta leo kabla nyakati za hatari hazijafika…Ukimpokea na kumwamini atausafisha uovu wako wote, na kukufanya wewe kiumbe kipya.

1 Yohana 5.3 “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.

5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, ISIPOKUWA NI YEYE AAMINIYE YA KWAMBA YESU NI MWANA WA MUNGU?

6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu.

7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli”.

Tafadhali “share” na pia wahubirie wengine habari njema za msalaba kwa kadri uwezavyo popote ulipo.Na pia tembelea website yetu /www wingulamashahidi org/ kwa mafundisho ya ziada.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

BIBLIA INASEMA “HAMJUI YA KUWA MTAWAHUKUMU MALAIKA? (1WAKORINTHO 6:2-3) ” TUTAWAHUKUMUJE?.

NADHIRI.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.


Rudi Nyumbani

Print this post

NADHIRI.

Kumbukumbu 23: 21 “Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.

22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.

23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako”.

Nadhiri, ni kitu chochote unachoweza kukiahidi kumtolea Mungu kwa ihari yako mwenyewe. Na kitu hicho kinaweza kuwa sadaka mfano mali, fedha, shamba n.k..Lakini pia nadhiri ni ahadi mtu anayoweza kuiahidi ya maisha Fulani mbele za Bwana mfano mtu anaweza akaahidi mbele za Bwana kumtumikia yeye endapo atafanyiwa kitu Fulani na Mungu..Mfano tunamwona Yakobo wa kwenye maandiko.. wakati ambapo anamkimbia Esau Ndugu yake kwasababu aliuchukua mbaraka wake maana Esau alimkasirikia kwa hilo…Hivyo ikamlazimu Yakobo aende nchi ya mbali katika ukoo wa baba yake na mama yake huku akiwa mikono mitupu hana kitu kabisa… Na wakati akiwa njiani akamwekea Mungu nadhiri kwamba endapo Mungu atamlinda njia aiendayo na kumfanikisha katika chakula na mavazi ndipo Yehova atakuwa Mungu wake na atamtolea yeye fungu la kumi la kwa kila alichopewa.. Tunasoma hayo katika..

Mwanzo 28: 18 “Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.

19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.

20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae;

21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu. 22 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi”.

Na tunaona baada ya kumwekea Mungu hiyo nadhiri, Bwana Mungu kweli alimfanikisha Yakobo alimpa utajiri mwingi katika mifugo na mali na wakati anamrudia ndugu yake Esau kutoka kwa Labani mjomba yake, aliikuwa amepata mali nyingi sana na utajiri , na ndipo Yakobo akaitoa nadhiri ile, akamtumikia Mungu siku zake zote na kumtolea fungu la kumi.

Mwanzo 31: 13 “Mimi ni Mungu wa Betheli, huko ulikotia mafuta nguzo, na kuniwekea nadhiri. Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile uliyozaliwa”.

Kwahiyo hiyo ni moja wapo ya nadhiri, nadhiri ya kumtumikia Mungu, endapo atakufanyia kitu Fulani. Na kama tunavyoona hapo Mungu anakumbuka kila nadhiri mtu anayoiweka mbele zake, alikumbuka ya Yakobo siku aliyomwekea na mahali alipomwekea..hivyo anamkumbusha.

Kuna usemi unaosema kwamba AHADI ni DENI, lakini NADHIRI ni ZAIDI YA DENI..ni kifungo, biblia inatuonya kabla hatujaweka nadhiri, tujitafakari kwanza mara mbili mbili mbele za Mungu kabla ya kuchukua uamuzi huo.. Inasema

Hesabu 30: 1 “Kisha Musa akanena na wale vichwa vya kabila za wana wa Israeli, na kuwaambia, Neno hili ndilo aliloliagiza Bwana.

2 Mtu atakapomwekea Bwana NADHIRI, au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake”.

Na pia inarudia kusema kitu hicho hicho katika kitabu cha… 

Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu NADHIRI, usikawie kuiondoa; KWA KUWA YEYE HAWI RADHI NA WAPUMBAVU; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.

5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe”.

Mistari yote hiyo inaonyesha jinsi gani Mungu anafuatiliza kila Neno linalotoka katika kinywa cha mtu, Neno lolote linalotoka vinywani mwetu mbele za Bwana.

Kitu kimoja wengi wasichojua ni kwamba, NDOA NI NADHIRI. Na kwanini Mungu anachukia kuachana sio kwasababu tu Mungu anachukia uasherati! Hapana zaidi ya hilo anachukia sana mtu anapoivunja nadhiri aliyoitoa kwa kinywa chake. Wakati wa ndoa kufungwa mtu anaahidi mbele za Mungu kuishi kwa upendo, na mwenzake na kwa uvumilivu, kutoachana katika hali yoyote ile watakayoipitia katika maisha, aidha katika umaskini au katika utajiri, katika uzima au ulemavu, katika huzuni au furaha n.k..Na wanaahidi kuwa Kifo ndicho kitakachowatenganisha…

Sasa kwa wanandoa kama hawa pasipo kufikiri wanaweza wakadhani kuwa wameahidiana wao hizo ahadi, kumbe hawajui na nadhiri wamemwekea Mungu..kwasababu wamekwenda kuziweka mbele zake..Na endapo ikitokea wameachana kwasababu yoyote mojawapo ya hizo hapo juu, Biblia inasema “Bwana hawi radhi na wapumbavu”..inasema ni afadhali mtu kutokuiweka kabisa kuliko kuiweka asiiondoe..Hicho ni kifungo cha maisha.

Kumuacha mke wako au mume wako kwasababu tu amekuwa maskini, au mlemavu…ni tiketi kamili ya kwenda katika lile ziwa la moto hakuna msamaha juu ya hiyo dhambi, ukimwacha mume wako au mke wako kwasababu tu mmegombana siku moja au kwasababu amekuwa mnene, au kwasababu amekuwa mzee au havutii tena..hakuna neema juu ya hilo, suluhisho pekee ni kumrudia tu!!.

Bwana anasema katika

Hesabu 30:2 “ Mtu atakapomwekea Bwana NADHIRI, au, ATAKAPOAPA KIAPO ILI KUFUNGA NAFSI YAKE KWA KIFUNGO, ASILITANGUE NENO LAKE; ATAFANYA SAWASAWA NA HAYO YOTE YAMTOKAYO KINYWANI MWAKE”.

Hii ina maana kuwa kabla ya kuamua kuoa, au kuolewa..yatafakari hayo yote kwanza na upige gharama kabisa..endapo ikitokea atakayekuja kuwa mume wako/ mke wako kafilisika utaendelea kumpenda na kuishi naye…endapo ikatokea kawa mlemavu utaendelea kumheshimu na kumpenda,..endapo mmegombana utakuwa tayari kumsamehe n.k, utakuwa tayari kumtunza kama mwili wako mwenyewe?? Kama hayo yatakushinda ni afadhali USIWEKE HIYO NADHIRI KABISA. Ni afadhali usioe wala kuolewa kabisa.

Mhubiri mmoja wa kimarekani anaitwa William Branham, wakati Fulani Alienda kumwombea mtu mmoja aliyekuwa anaumwa sana karibia na kufa…na kwasababu Bwana amemkirimia karama ya kinabii, wakati akiwa katika hatua ya kumwekea mikono Yule mgonjwa ili amwombee…Ono likamjia kutoka kwa Mungu, akamwona Yule mtu akiwa katika hali ya Kuzama maji, na wakati akiwa katika kuzama…akamlilia Mungu amwokoe asife maji, akiwa katika ile hali akamwekea Mungu nadhiri na kumwambia endapo, atamwokoa na MAUTI ILE YA KUZAMA MAJI basi atamtumikia yeye siku zote za maisha yake..na Bwana akamsikia akamwokoa na mauti ile ya kufa maji..Lakini Yule mtu alipotoka pale akaisahau ile nadhiri aliyomwekea Mungu..akaendelea na maisha yake ya kawaida…Na Bwana akamwambia katika ono ndugu William Branham kwamba huyo mtu hatapona ugonjwa uliompata bali atakufa..kwasababu alimwekea Mungu nadhiri na hakuitimiza…Na alipomwambia Yule mtu, mambo hayo Bwana aliyomwonyesha Yule akakiri ni kweli alimwekea Mungu nadhiri wakati anakaribia kuzama maji..Lakini alilolisema Bwana amelisema, baada ya siku kadhaa Yule mtu alifariki.

Ipo mifano kadha kadha katika maandiko, ambayo watu walifanya mchezo na nadhiri, Mmojawapo wa watu hao tunamwona ni Anania na Safira mkewe. Hawa wakiwa katika vyumba vyao vya siri waliahidi kuuza shamba lao na kiasi chote cha fedha kitakachopatikana basi watakipeleka madhabahuni kwa Bwana…ndivyo walivyoahidi mbele za Bwana na Bwana akasikia, akawajalia kufanikisha haja ya mioyo yao, lakini walipoona Bwana amewafanikisha na wameuza lile shamba kwa kiwango kizuri walichokitarajia tamaa ikawaingia wakasahau kuwa walimwahidi Mungu kiasi chote, lakini wao wakaficha sehemu ya fedha, na kumpelekea Mungu kiasi kidogo…Biblia inasema kwa kosa hilo hawakudanganyana wao bali walimdanganya Mungu mwenyewe na walikufa wote wawili ndani ya siku moja.

 Matendo ya Mitume 5 : 1-42

“1 Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe, aliuza mali,

2 akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume.

3 Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?

4 Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.

5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.

6 Vijana wakaondoka, wakamtia katika sanda, wakamchukua nje, wakamzika.

7 Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia, naye hana habari ya hayo yaliyotokea.

8 Petro akamjibu, Niambie, Mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? Akasema, Ndiyo, kwa thamani hiyo.

9 Petro akamwambia, Imekuwaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu yao waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe.

10 Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.

11 Hofu nyingi ikawapata kanisa lote na watu wote walioyasikia haya”.

Ndio maana Zamani katika agano la kale, Bwana aliwakataza kabisa watu waliomwekea Mungu nadhiri, wasinywe mvinyo wa aina yoyote, wala divai,wala hata mzao wa mzabibu usifike vinywani mwao, unajua ni kwasababu gani?..Ni kwasababu mtu aliyemwekea Mungu nadhiri kila wakati anapaswa awe katika akili yake timamu, ili asiisahau ile nadhiri aliyomwekea Mungu…Mvinyo unamfanya mtu ajisahau, unamfanya mtu atoke katika akili yake ya kawaida.. Na pia Bwana alitoa maagizo mtu yoyote aliyejiweka kuwa mnadhiri wa Bwana asikate nywele zake sharti ataziacha ziwe ndefu mpaka siku atakapoitimiza nadhiri yake? Unajua ni kwasababu gani?..Ni kwasababu kila atakapoziona nywele zake kichwani nyingi akumbuke kuwa alimwekea Mungu nadhiri, inakuwa ni kama kitu cha kumkumbusha kuwa ana deni sehemu Fulani katika maisha yake. Ndio maana Samsoni alionywa asikate nywele zake,wala wazazi wake wakati wa ujauzito wake alionywa asinywe divai. Kwasababu yeye alikuwa ni mnadhiri wa Bwana biblia inasema hivyo.

Hesabu 6: 1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na watu wa Israeli, uwaambie, Mtu mume au mtu mke atakapoweka nadhiri kubwa, nadhiri ya Mnadhiri, ili ajiweke wakfu kwa Bwana;

3 ATAJITENGA NA DIVAI NA VILEO; hatakunywa siki ya divai, wala siki ya kileo, wala asinywe maji yo yote ya zabibu, wala asile zabibu, mbichi wala zilizokauka.

4 Siku zote za kujitenga kwake asile kitu cho chote kilichoandaliwa kwa mzabibu, tangu kokwa hata maganda.

5 Siku zote za nadhiri yake ya kujitenga, wembe usimfikilie kichwani mwake; hata hizo siku zitakapotimia, ambazo alijiweka wakfu kwa Bwana, atakuwa mtakatifu, ataziacha nywele za kichwani mwake zikue ziwe ndefu”.

Ni hatari sana kuweka nadhiri na kutoitimiza..Katika maandiko matakatifu nyakati za Waamuzi kulikuwa na mwamuzi mmoja anayeitwa YEFTHA, huyu alimwekea Mungu nadhiri kwamba endapo ataenda vitani na kushinda, basi Yule atakayetokea wa kwanza mbele yake kumpokea basi atamfanya sadaka ya kuteketezwa, lakini kwa bahati mbaya alitegemea kije kitu kingine, pengine ng’ombe zake lakini alikuja binti wake wa pekee na alikuwa hana mwingine…lakini kwasababu anajua madhara ya kuahidi nadhiri na kutoitimiliza, akamteketeza binti wake kwa moto, ili kuiondoa ile nadhiri, na Mungu hakumhesabia makosa.

Waamuzi 11: 29 “Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni.

30 Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli,

31 ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa.

32 Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake.

33 Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli.

34 Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na machezo; naye alikuwa ni mwanawe pekee; hakuwa na mwingine, mwana wala binti, ila yeye.

35 Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwahao wanisumbuao; KWA KUWA MIMI NIMEMFUNULIA BWANA KINYWA CHANGU, NAMI SIWEZI KUREJEA NYUMA”.

Kumbuka Bwana hajawahi kuagiza watu wamtolee yeye sadaka ya kuteketezwa, na yeyote afanyaye hayo alikuwa anakwenda kinyume na maagizo yake, lakini kwasababu ya NADHIRI Bwana hakumhesabia YEFTHA makosa. Na Yefha alitambua kabisa endapo asingetimiza maneno aliyoyazungumza kwa kinywa chake basi yangeweza kumtokea mambo mabaya sana..mfano wa Anania na Safira.

Ndugu unayesoma haya, ulimwahidi Mungu nini alipokuponya? Ulimwahidi Mungu nini alipokufanikisha katika mambo yako? Ulimwahidi nini siku alipokuokoa?…Ulimwekea Nadhiri gani, kama ipo je! Unaikumbuka bado? Au umeisahau? Kama wewe umeisahau kumbuka Mungu hajaisahau?..uliahidi kumtolea fungu la kumi je unafanya hivyo?..uliahidi kutoa kitu Fulani kwa ajili yake..je! ulifanya hivyo?? Uliahidi endapo akikuponya, au akikufanikisha, au akikufaulisha au akikufikisha salama utamtumikia? Je! Umefanya hivyo?..Wakati mwingine upo katika hatari nyingi na unapitia mambo magumu ni kwasababu uliweka nadhiri na haukuitoa.

Bwana akujalie kuyaona hayo!. Ili uukwepe mkono wa Mungu.

Tafadhali “share” kwa wengine na Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MSHIKE SANA ELIMU.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

JINA LAKO NI LA NANI?

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.


Rudi Nyumbani

Print this post

MCHE MWORORO.


Kuja kwa Bwana duniani kulikuwa kwa kitofauti sana, wakati ambapo Israeli ilimtazamia aje kipindi ambacho uzao wa Daudi unaonekana wazi kwa wafalme waliokuwa wanatawala Yuda zamani za wafalme. Lakini yeye hakutokea hicho kipindi, walipotazamia labda pengine angetokea wakati ambapo wamerudishwa kutoka Babeli lakini hakuonekana hata katika hicho kipindi, wengine walizani utawala wa Umedi hautaisha hata ajapo lakini hakutokea pia ndani ya utawala ule mpaka ulipoisha, Wengine walitazamia labda ingekuwa ni katika utawala wa Uyunani, lakini hata huo nao hakutokea, mpaka ulipoanza utawala mwingine mpya uliojulikana kama Rumi ya kipagani, na ndipo akaja kuzaliwa mwokozi wa ulimwengu Bwana Yesu Kristo, Ni siku ambazo Israeli tayari imeshapoa sana, siku ambazo Israeli tayari imeathiriwa na tamaduni za kigeni za kipagani , siku ambazo Israeli imeshasahau hata kama kuna masihi mkombozi wao anayetakiwa kuja isipokuwa kwa wayahudi wachache tu ndio waliokuwa wanamtazamani, lakini taifa lote lilishalala na ndio maana hata siku ile Mamajusi kutoka mashariki walipoleta taarifa za kuzaliwa mfalme wa wayahudi, biblia inasema habari zile sio tu zilimfadhaisha Herode peke yake bali na Yerusalemu yote pia. Alishuka wakati viwango vya maovu katika Israeli na dunia nzima vipo juu, Bwana alikiita kizazi kile, kizazi cha zinaa na uzinzi , Lakini huo ndio wakati Mungu aliouchagua kumleta mwanae duniani.

Biblia inasema alikuwa kama mche mwororo kwenye nchi kavu, alikuwa kama mzizi mbichi katika nchi kame, siku ambazo watu hawakuwa na habari na Mungu, siku ambazo viongozi wa kidini walikuwa ni wapenda fedha kupindukia, kuliko kumpenda Mungu (Luka 16:14) tofauti na ilivyokuwa hapo zamani, ambapo walawi waliokuwa wanahudumu katika nyumba ya Bwana, hawakujiuhusisha na mambo ya kidunia, bali fungu lao lilitengwa kwa ajili yao, lakini wahudumu wa kipindi cha Yesu, sio tu walikuwa ni wapenda fedha, bali pia walikuwa wafanyaji wa biashara katika sehemu takatifu hekaluni mwa Mungu. alikuja kipindi ambacho unafki umejaa katikati ya viongozi wa kidini (Mathayo 23:13-15), kipindi ambacho viongozi wa kidini wamejaa kutokuwa na kiasi na dhihaka biblia inasema hivyo (Mathayyo 23:25). kipindi ambacho watu wote wenye haki na manabii pindi walipojaribu kusema ukweli walikuwa wanapigwa hadharani kwenye masinagogi yao na kuuliwa na hao hao viongozi wa kidini. Na tunaona ndivyo walivyokuja kufanya hata kwa Bwana(Mathayo 23:33).

Lakini huo ndio uliokuwa wakati wa Mungu aliouchagua kuleta wokovu duniani. Bwana Yesu Alikuwa kama jani bichi jangwani, alikuwa kama mizizi mibichi kwenye ardhi ya ukame, alikuja wakati usiostahili wa yeye kuja, kipindi ambacho Israeli haijawahi kuona nabii kwa muda wa miaka 300 kwa maana nabii wa mwisho alikuwa ni Malaki…Kipindi ambacho watu wa mataifa wanalimiliki taifa la Israeli, wakiamrishwa kana kwamba wapo nchi ya ugenini. Kipindi ambacho kila mtu anajiamulia mambo yake. Lakini ndio wakati wa Masihi kutokea, kutengeneza tena upya mambo yote.

Isaya 53: 1 “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

2 Maana alikua mbele zake kama MCHE MWORORO, NA KAMA MZIZI KATIKA NCHI KAVU; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.

3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.

4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA“.

Maandiko yanasema ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta?. Inaamanisha kuwa kuzaliwa kwa Kristo duniani lilikuwa ni jambo lisilosadika kwa yeyote Yule aliyelisikia, eti katikati ya ouvu atokee masihi?..afadhali ingekuwa wakati wa kipindi cha waamuzi au kipindi cha wafalme wa Israeli. Lakini sio kwa wakati ule aliokuja..

Hivyo pamoja na ukame wote huo wa kiroho uliokuwa Israeli kwa wakati ule. Hapo ndipo Kristo alipotokea, Hapo ndipo wale wenye nguvu wachache ambao hawakukata tamaa walitambuka kuja kwa Kristo, walisadiki habari za kuja kwake, Mkono wa Mungu ulifunuliwa kwao..Mfano wa hao kwenye biblia tunamwona HANA, mwanamke aliyekuwa amejitoka kikamilifu kwa Mungu, Licha ya kufiwa na mume wake katika siku za ujana wake, lakini hakuona sababu ya kwenda kuolewa tena bali alichagua kudumu hekaluni usiku na mchana akimwomba Mungu, auharakishe wokovu aliowaahidia wayahudi tangu zamani, wakati wayahudi wengine wameshakata tamaa na kuendelea na mambo yao, na kusahau kitu kinachoitwa mwokozi duniani, lakini Hana hakuwa hivyo yeye alidumu hekuluni kwa miaka 84. usiku na mchana akimtafakari Mungu na wokovu uliokuwa unatarajiwa Israeli tangu zamani. Mpaka siku moja wakati Yesu anaenda kuwekwa wakfu Hekaluni na wazazi wake ndipo Mungu akamwonyesha huyu ndiye aliyekuwa anamtazamia…

Kadhalika alikuwepo mzee mwingine naye vivyo hivyo alikuwa anatazamia faraja ya Israeli yaani kuja kwa mwokozi kwa muda mrefu, mpaka ikafikia wakati Mungu akamshuhudia kwamba hatakufa mpaka atakapomwona mwokozi duniani.

Habari hizo tunazisoma katika Luka 2:25-38

“25 Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.

26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,

28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;

30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

33 Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.

34 Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa.

35 Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

36 Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.

37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.

38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, NA WOTE WALIOKUWA WAKIUTARAJIA UKOMBOZI KATIKA YERUSALEMU AKAWATOLEA HABARI ZAKE”.

Embu leo hii jaribu kufikiria ungekuwa na wewe upo katika kipindi kile je! Ungeweza kutambua kuzaliwa kwa Bwana duniani? Je! Hata ungehadhithiwa ungeweza kusadiki habari hizo?, kati ya mamilioni waliokuwa Yerusalemu ni watu wachache sana walioweza kufunuliwa tukio hilo la kuja kwa mwokozi duniani. Alikuja kama MWIVI, hakuja kwa kujionyesha onyesha, au kwa kupigwa parapanda angani ili dunia nzima itazame, bali alikuja kama mwivi. Alizaliwa zizini.

Na ndivyo itakavyokuwa kuja kwake mara ya pili. Kama ilivyokuwa katika kuja mara ya kwanza, wakati ambao watu wameshakata tamaa ya kuja Masihi duniani ndipo alipokuja na kujifunua kwa wale wachache ambao hawakuzimia mioyo yao katika kumsubiria mfano wa ANA na SIMEONI. Wakati ambao unafki mwingi na upendaji fedha umekithiri katika kanisa la Kristo na kwa watu wanaojiita watumishi wake,kama ilivyokuwa kipindi kile, ndipo Kristo atakaposhuka. Wakati ambapo manabii wengi wa uongo wamezagaa kila mahali na wale wa ukweli wanatengwa na kanisa ndipo Kristo anaposhuka 

Hivyo ndugu mambo tunayoyaona sasahivi ni dalili madhubuti inayotutambulisha kuwa tunaishi katika majira ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Siku hiyo itakapofika siku ile ya UNYAKUO, dunia haitajua chochote, wakristo vuguvugu wanaodai wanamngojea Bwana na huku mguu mmoja upo nje, mambo ya kidunia yakiwasonga siku hiyo hawatajua chochote, bali atakuja kwa watu wachache sana, mfano wa Ana na Simeoni watu waliojazwa Roho Mtakatifu, watu ambao usiku na mchana wanautazamia wokovu na macho yao yapo mbinguni siku zote ndio watakajua, watu ambao ni wacha Mungu kama Simeoni, watu ambao wanadumu madhabahuni pa Mungu, hawataki kutoka katika mstari wa Neno ndio watakaojua lakini wengine wote watabaki wakisubiria hukumu ya Mungu mwenyezi.

Bwana atatokea kwao kama mche mwororo, kama jani bichi katika dunia chafu, katika jamii ya watu wenye dhihaka wanaosema huyo Yesu mnayengojea kwa miaka 2000 sasa yuko wapi, tulidhani angekuja wakati wa mitume hakutokea, tulidhani angekuja wakati wa kipindi cha matengenezo ya kanisa mbona hakutokea, wakati wa kipindi cha upentekoste hakutokea mpaka millennium mpya imeanza hajaja bado, huyo sio wa kuja leo wala kesho. Nyie mnapoteza mida yenu, badala ya kufikiria mambo ya muhimu mnawaza juu ya kuja kwa YESU hichi ni kizazi kipya…

Unaona? Hao watu wa kudhihaki biblia inasema watatokea katika siku za mwisho. Lakini wewe kaka/dada, unayemngojea Bwana sasa. Usikatishwe tamaa, siku ya wokovu wetu ipo karibu kushinda hata sisi tunavyodhani. Usiache kumtazama Kristo, majira haya dunia inayoona kuwa hakuna uwezekano wa kuja kwa Bwana, lakini ndio haya haya atakayokujia kama mwivi. Ndio haya Mungu aliyoyachagua. Siku yoyote hatutakuwepo hapa duniani.

Ni matumaini yangu utaufanya uteule wako na wito wako imara sasa kabla siku ile haijafika.

Amen.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine. Na Mungu akubariki!

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MWAMBA WETU.

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

NI JAMBO LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?


Rudi Nyumbani

Print this post

TUKAZE MWENDO KWA TULIYOANDALIWA.

Luka 10:22 “Akasema, NIMEKABIDHIWA VYOTE NA BABA YANGU, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.”


Yohana 13:3 “Yesu, hali akijua ya kuwa Baba amempa vyote mikononi mwake, na ya kuwa alitoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu”


Ufunuo wa Yohana 5 : 1-14 

1 Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba. 

2 Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, N’nani astahiliye kukifungua kitabu, na kuzivunja muhuri zake? 

3 Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. 

4 Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. 

5 Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba. 

6 Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote. 

7 Akaja, akakitwaa kile kitabu katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi. 

8 Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu. 

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 

10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi. 

11 Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu, 

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”

Shalom! Umewahi kujiuliza wafu leo wapo wapi?, je! mtu akifa leo katika dhambi au katika haki anakwenda wapi?…Ni wazi kuwa mtu akifa katika haki, roho yake inakwenda mahali panapojulikana kama Paradiso au peponi, ni mahali pa zuri na pa raha, ambapo roho ya mtu huyo itapumzishwa huko kwa kitambo kidogo pamoja na wenzake wa imani moja naye ambao nao walikufa katika haki..Huko wanakusanyika pamoja, mpaka siku Kristo atakapokuja mawinguni ambapo wataamshwa(au kufufuliwa) na kuvaa miili ya utukufu, na kisha kwenda mbinguni kwa Baba.


Kumbuka mbinguni Bwana Yesu alipo hakuna mtu aliyefika sasa, ni mahali pa zuri ambapo hapana mfano huko hata Eliya hayupo, wala Musa, wala Henoko, wala Ibrahimu, huko ni sehemu mpya kabisa ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia mambo yaliyopo kule…Eliya na Henoko ambao hawakuonja mauti hawakupelekwa huko mbinguni Bwana aliko sasa,bali walipelekwa Paradiso.


Yohana 3: 13 WALA HAKUNA MTU ALIYEPAA MBINGUNI, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.


Bwana Yesu alisema “Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Yohana (14:2-3)


Umeona Bwana anasema anakweda kutuandalia makao, ikiwa na maana kuwa, ni mahali kupya kabisa panapokwenda kuandaliwa…na akishamaliza atatukaribisha kwake, ili alipo nasi tuwepo.


Kwahiyo kwa muhtasari huo unaweza ukaona kwamba Kristo Yesu pekee ndiye aliyeko mbinguni sasa, akituandalia sisi makao, na Makao hayo si mengine zaidi ya nafasi zetu sisi tutakazukuwa nazo kule, pamoja na miili yetu ya utukufu tutakayoivaa siku atakayokuja kutuchukua.


Sasa unaweza ukauliza mbona kuna watu wengi wanasema wamepelekwa mbinguni wakaona hiki na kile?..Jibu rahisi ya swali hilo ni kwamba hawakupelekwa mbinguni bali walionyeshwa maono ya mbinguni..Na kumbuka maono ni lugha ya picha…Mtu anaweza akapewa maono ya mbinguni, katika maono yale akaona barabara za dhahabu, akaona na milima na mabonde mazuri, akaona na maua mazuri na chemchemi nzuri, lakini mtu huyo hajapelekwa mbinguni…bali amepewa tu maono ya mahali ambapo pangeweza pakafananishwa na Mbinguni…Ni sawa leo, mtu aoneshwe clip ya Taifa la Urusi akiwa hapa Tanzania, je! mtu huyo atakuwa amefika Urusi? Ni dhahiri kuwa bado hajafika, ni kaonyeshwa tu kipande cha video ya Urusi, Ndivyo ilivyo kwa watu wengi wanaopewa maono ya Mbinguni, wanakuwa tu wanapewa vipengele vidogo vidogo vya jinsi mbingu ilivyo uzuri wake kwa lugha ya kibinadamu. Lakini kiuhalisia kabisa ni mambo ambayo hayatamkiki kibinadamu.


mbinguni Bwana Yesu alipo hakuna mtu yoyote anayejua yanayoendelea huko..Ni siri, mpaka siku Kanisa litakaponyakuliwa ndipo watakatifu watakapoenda kuona mambo mazuri na mapya walioandaliwa. Ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.


Biblia inasema..

Waebrania 11: 36 “wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;  

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;  

38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.  

39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;  

40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ILI WAO WASIKAMILISHWE PASIPO SISI.


Unaona hapo, watakatifu wote waliotutangulia, ukisoma Waebrania 11&12 yote utaona wingu kubwa la mashahidi linazungumziwa pale, utaona akina Ibrahimu, Henoko, Musa, Gideoni, n.k. fahamu tu wote hao mpaka sasa hawajaipokea ile ahadi walioahidiwa kwasababu yetu sisi, na ndio maana hapo biblia inasema ILI WAO WASIKAMILISHWE PASIPO SISI. Hii ikiwa na maana wingu hilo la mashahidi waaminifu wa Kristo waliojitoa maisha yao kikamilifu kwa ajili ya Bwana wote bado hawajakamilishwa wote wapo mahali wamehifadhiwa wakitusubiria sisi nasi tukamilishe ili kwa pamoja siku ile ya Bwana wote tuende mbinguni YESU wetu alipo kwenye makao aliyokwenda kutuandalia.


Ni raha iliyoje tukifahamu hilo. Hivyo mimi na wewe tukazane tufike sehemu hiyo, ambayo imeandaliwa kwa ajili yetu. Kwasababu itakuwa ni majuto makubwa sana na vilio kwa wale ambao watakosa unyakuo,.Wakati huo ukifiria wenzako wapo mbinguni wanang’aa kama jua na wewe unasubiria ziwa la moto, itakuwa ni majuto kiasi gani, kibaya zaidi ukijua kabisa ulikuwa na muda wa kutubu lakini uliupuuzia..Fanya uamuzi leo, yatengeneze maisha yako upya tena, naye Bwana atakurehemu.


Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

KANUNI JUU YA KANUNI.

Isaya 28:13 “Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.”

Yapo madhara makubwa sana ya kufungwa katika vifungo vya kidini kwa muda mrefu, au kanuni Fulani za kidhehebu kwa muda mrefu kwasababu hiyo inapelekea kuridhika na kubakia katika hali hiyo hiyo, na mwisho wa siku Roho Mtakatifu anakuwa hana nafasi tena ya kumwongoza mtu wa namna hiyo kwasababu tayari kanuni za dini yake zimeshamfunga, na hivyo haoni haja tena ya kumtaka Roho Mtakatifu awe kiongozi wake. Na hilo ndilo lililokuwa pia katika kipindi cha Bwana wetu YESU.

Wakati ule wayahudi walikuwa chini ya dini zao kongwe (Mafarisayo na Masadukayo), ni kweli baadhi ya mambo waliyokuwa wanaamini chanzo chake ni Mungu lakini hawakuweza kuufikia utimilifu wote wa kukubaliwa na Mungu kwasababu tayari walishajifunga, walikwama sehemu Fulani kwa muda mrefu.

Lakini wakati ulipofika wa Mungu kuona sasa kuna haja ya kuleta utimilifu wote duniani ndipo alipomtuma mwanae mpendwa YESU aje duniani kutueleza yote. Lakini wale watu kwa kuwa kanuni za dini zao zilikuwa zimewakaa sana walijiona tayari ni wakamilifu, hivyo hawakuona kuna haja ya mtu kuwaletea ukamilifu mwingine zaidi ya huo walionao, waliona kuwa sheria ya Musa inatosha tu! mtu akiishika hiyo inamtosha kumfanya awe mkamilifu.

Torati inasema usizini, hivyo mtu akishiishi bila kuzini hata kama anawakata tamaa kila siku ndani ya moyo wake basi inatosha yeye kuonekana kuwa mkamilifu maadamu hajawahi kuzini katika maisha yake, na ndio maana hata Bwana Yesu alipokuja kutilia mkazo amri hiyo hiyo pale alipowaambia mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha zini naye, wakaona kuwa kama huyu anavunja maagizo ya Mungu. Hawakujua kuwa ni kile kile Bwana anakisisitiza isipokuwa katika ukamilifu wote,..Ni amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni. Lakini wao kwakuwa walikariri maandiko walimpinga vikali.

Kadhalika na mambo mengine yote Yesu aliyokuwa anayasema wao walidhani kuwa wanaletewa mambo mapya, walipoombiwa mtu amwoneaye ndugu yake hasira ni sawa na muaji, walidhani Kristo kajitungia mwenyewe maneno yale, lakini Kristo alikuwa anawafanya kuwa wakamilifu zaidi katika sheria zao. Ni sawa mwalimu amwambie mwanafunzi wake kuwa licha tu ya kuandika majibu ya mtihani wake, apange kazi yake vizuri na aandike vizuri pia… Lakini kwa kuwa walijizoelea kuenenda hivyo katika kanuni zao kwa muda mrefu, basi hata kutafari tena ni kwanini yale maneno yalisemwa vile kukafa ndani yao.

Wanakuwa wanayafuata tu kama desturi au mila, na sio kama vile Roho anawaongoza, au anawataka wao wawe watakatifu.

Kumbuka mpango wa Mungu juu ya maisha yetu sio tu kuokolewa halafu basi, hapana, Mungu anataka tufikie ukamilifu wote alioukusudia mwanadamu aufikie, ingekuwa tu ndio hivyo halafu basi siku ile ulipoyasalimisha maisha yako kwa Bwana basi ungepaswa ufe uende kwa Baba. Lakini haiko hivyo ni lazima tufikie ukamilifu wote Mungu anaoutaka ndio tuondoke, sasa basi ikiwa ndio hivyo ni wajibu wa Bwana kila siku kutupa amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, huku kidogo na huku kidogo,.,na ndio maana biblia haina kitabu kimoja, bali 66, imekuwa hivyo ili tuweze kuvumbua utimilifu wote wa Mungu.

Ikiwa mtu ni mwamini wa kweli utakuta hapo mwanzoni alipomwamini Kristo, hakuona kuwa kuvaa vimini ni dhambi, lakini kwa kuwa Roho wa Mungu yupo ndani yake, anamfundisha na kumpa kanuni juu ya kanuni kila siku ili kumfanya kuwa mkamilifu, utaona baadaye anaona si sawa kuwa na zile nguo hivyo anachoma vile vimini, alivyokuwa anavaa kadhalika hapo mwanzo alikuwa anaona ni sawa tu kwa mwanamke wa kikristo kuvaa suruali lakini kwa kuwa Roho wa Mungu yupo ndani yake, Neno la Mungu likimjia kumwambia atupe hizo suruali, kwamba haimpasi mwanamke kuvaa mavazi yampasayao mwanamume, hatashangaa kwasababu atajua kuwa maagizo hayo yanalandana na utakatifu ambao ndio Mungu anautaka. Lakini utakuwa mtu mwingine ambaye yeye yupo chini ya kanuni za kidhehebu au za kidini, sasa kwa kuwa dini yake haisemi kuwa mwanamke kuvaa vimini na suruali pamoja na wanja na hereni ni machukizo mbele za Mungu, siku ambapo atasikia kwa mara ya kwanza Neno hilo utamwona anaanza kupinga pasipo hata kutafakari, atadai kwamba maadamu sizini mimi sina hatia, lakini hajui kuwa anaambiwa hivyo kwa faida yake mwenyewe ili aukamilishe utakatifu wake wa kutokuzini, kwasababu biblia inasema amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha zini naye, sasa ni kweli yeye anaweza akawa hajatamani wala hajazini, lakini yupo mwingine kazini juu yake, kwasababu ya mavazi yake ya uchi uchi, Na Bwana Yesu alishasema mtu yeyote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake kisha akatupwe baharini. Je! hapo mtu kama huyo atakuwa na la kujitetea siku ile ya Hukumu?.

Kuna hatari kubwa sana ya kuongozwa na mapokeo yale yale tu yaliyo kwenye dini zetu, na kusahau Roho Mtakatifu anataka nini kwa mwaminio katika wakati anaoishi. Mungu hafanyi kazi ya kuokoa tu watu, anafanya kazi pia ya kuwafanya wawe wakamilifu. “Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”

Umebatizwa ukiwa mchanga, na sasa unajua kabisa hakuna ubatizo wa watoto wachanga, wala wa kunyunyiziwa bali wa kuzamwishwa kwenye maji tele na kwa jina la YESU, lakini hapo kabla ulifanya kimakosa na hivyo haukukamilishwa, lakini sasa Bwana anakupa kanuni sawasawa na Neno lake katika (Mdo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5) kwamba ukabatizwe tena kwa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako. Usifanye moyo wako mgumu, ukadhani kuwa ni dini mpya au mtu anataka kukutoa kwenye dhehebu lako. Tii tu kwasababu ni maagizo ya YESU BWANA WAKO.

Hapo mwanzo ulikuwa unadhani kuna mpatanishi zaidi ya mmoja, kwamba hata bikira Maria anaweza akawa mpatanishi wa dhambi zako, na kukuombea,..haukuwa na nia mbaya kufahamu hivyo..Lakini sasa umejua ukweli kuwa mpatanishi wa dhambi zetu ni mmoja tu! biblia inasema “hakuna wokovu kwa mwingine awaye yote zaidi ya YESU (matendo 4:12)”. Hiyo ni kanuni ambayo ulikuwa hauijui, Bwana amekupa tena leo, usiipinge wala kuikataa kwasababu lengo lake Bwana ni kukufanya wewe uwe mkamilifu ili siku ile uweze kusimama mbele yake. Hakuna maagizo ya kwenda toharani kwenye biblia. Mtu ameandikiwa kufa mara moja baada ya kifo ni hukumu…elimu nyingine inayosema kuna nafasi ya pili baada ya kufa ni kutoka kwa Yule adui, akitaka ujitumainisha ya kwamba hata ukiendelea katika dhambi ipo nafasi ya pili huko unakokwenda…Biblia inasema mkumbuke Muumba wako kabla roho haijamrudia yeye aliyeiumba (Mhubiri 12:1-7).

Hivyo ndugu ikiwa ulishamwamini Bwana, ni wakati wa wewe kukua kutoka hatua moja ya utakatifu hadi nyingine, na hiyo lazima iendane na kanuni za Mungu pamoja na amri zake, kutoka kanuni moja hadi nyingine.. Angalia maisha yako ya leo je! ni sawa na ulivyokuwa jana na juzi?, je! kuna kitu chochote kimeongezeka ndani yako?. Umekaa ndani ya wokovu kwa miezi sasa, kwa miaka sasa, je! kuna mabadiliko ,mambo unayoyatenda unataka yafanane na mtu aliyemkabidhi Bwana maisha yake leo?. Kama hakuna badiliko basi fahamu kuwa uongozo wa Roho Mtakatifu ulishakufa ndani yako siku siku nyingi, ulishamzimisha Roho ndani yake asiendelee kukufundisha. Hivyo geuka urudi..naye Roho atarudi ndani yako kukuongoza.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, HATA KUWA MTU MKAMILIFU, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”.

Hivyo ni maombi yangu Bwana atakujalia kukua na kutii maagizo yote Mungu anayokupa leo na kuyatendea kazi Na Maneno haya yawe akiba katika moyo wako, Mungu akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa ndugu zako na rafiki zako.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MUNGU MWENYE HAKI.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.


Rudi Nyumbani

Print this post

YESU MPONYAJI.

Zamani nilipokuwa mdogo nilikuwa ninasikia Yesu ni mponyaji! Yesu ni mponyaji! Lakini sikuwahi kufikiria kama angeweza kuja kuniponya mtu kama mimi. Nakumbuka ilikuwa ni mwaka 2004, siku moja nilipokaa na kufungua redio mida ya usiku mtumishi mmoja alikuwa anahubiri, na baada ya kumaliza mahubiri yake alisema ikiwa unaumwa na unataka uponyaji shika sehemu unayoumwa nami nitakuombea. Basi mimi kwa wakati huo nilikuwa ninasumbuliwa na sikio kwa muda mrefu, sikio lilikuwa linajaa mawimbi kama upepo unaovuma hivyo lilikuwa linanifanya nihisi maumivu mara kwa mara na kukosa raha. Lakini niliposikia yule mtumishi anasema shika mahali unapoumwa, ndipo na mimi nikashika sikio langu, nilifanya kama najaribu tu hivi nione kama nitaponywa sikuwahi kujua kama Yesu anaweza akawa karibu na mtu kiasi hicho.

Lakini cha ajabu alipomaliza kuomba, nilihisi kitu kama moto kimeshuka kwenye sikio, ukadumu kama kwa sekunde chache tu, kisha ukaisha, nikadhani labda utakuwa ni upepo wa joto umepitia tu, lakini niliposhika na kuweka kidole changu kwenye tundu la sikio na kutoa sikuhisi wimbi lolote wala maumivu yoyote kitu ambacho hapo kabla nilikuwa nikifanya hivyo ninahisi maumivu makali, nilipofanya kwa nguvu tena sikusikia chochote lilikuwa zima kama tu sikio lingine lilivyo kana kwamba halikuwahi kuwa na matatizo. Mpaka sasa ni miaka 14 imeshapita sifahamu tatizo lolote la masikio.Ndipo kuanzia huo wakati nikaanza kumtazama Kristo kwa jicho lingine sikujua kwamba kumbe anaweza kuwa karibu na mimi kiasi hicho..Na sio hilo tu alishawahi kuniponya namna hiyo hiyo mara kadhaa mbele.

Nimeandika huu ushuhuda wangu mwenyewe kukutia moyo wewe ambaye unayepitia katika hali za magonjwa na umekata tamaa kuona kuwa hakuna mtu yoyote anayeweza akaijali hali yako unayopitia sasa. Ndugu unaweza ukawa unaumwa kiasi cha kufa, unaweza ukawa sasahivi upo na ugonjwa uliokusumbua kwa muda mrefu, ambao umekugharimu pesa nyingi kutibiwa lakini haikuwezekana, bado tu unazidi kuwa katika hali ya kukosa matumaini, Unaweza ukasema Yesu hayajui matatizo yako, ni jinsi gani unavyopitia maumivu. Lakini nataka nikuambie Kama kuwa mgonjwa basi Kristo ilimgharimu awe mgonjwa zaidi yako ili wewe uwe mzima, kama ni kuwa mauti uti, basi Kristo alikuwa mauti uti mara nyingi zaidi yako kwa ajili yako ili kusudi kwamba aweze kuirudisha afya yako.

Kama ulikuwa na huzuni, Kristo alikuwa na huzuni kiasi cha kufa, Pengine Unasikia maumivu makali kutokana na majeraha makubwa yaliyo katika mwili wako, basi jua tu Kristo alipata maumivu ya namna yake mfano wake hakuna mwanadamu anayeweza akayapatia leo, ili kusudi kwamba wewe uwe mzima.

Hivyo usidhani kuwa YESU hajui unachokipitia, anafahamu sana kwasababu na yeye pia alishayapitia embu fikiria yale mapigo aliyokuwa anayapata siku ile, makovu, miiba kupenyezwa kwenye kichwa chake na kupondwa kwa fimbo, mijeledi ya visu 39, misumari mikononi na miguuni, na bado misumari hiyo hiyo ndiyo aliyoitegemea imning’inize msalabani, ni taabu kiasi gani mtu anaweza kupata, unategemea vipi mtu kama huyo asipatwe na mchanganyiko wa maumivu ya magonjwa unayoyajua wewe leo, alipata HOMA kali zaidi ya mtu yeyote aliyepata hapa duniani, aliugua, alikuwa mauti uti kwasasa tunaweza kusema hali aliyokuwepo Bwana Yesu ni zaidi ya mtu aliyeko ICU leo, mwili wote ulivimba hata usiweze kumtambua tena kwa ajili ya mapigo yale, wewe leo ugonjwa ulionao hauwezi kufikia hatua ya kuteseka kaisi hicho, lakini yeye alipata ugonjwa huo mkuu kwa ajili yako. Hivyo ndugu usiwe na hofu yeye BWANA anafahamu vizuri hali unayopitia, hauhitaji kumwadithia anaijua hali yako.

Sehemu mojawapo ya huduma iliyomleta Bwana duniani na aliyotiwa mafuta kwayo ndio hiyo ya kushughulika na madhaifu yetu.

Mathayo 8:14 “Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.

15 Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.

16 Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya WOTE waliokuwa hawawezi,

17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, MWENYEWE ALIUTWAA UDHAIFU WETU, NA KUYACHUKUA MAGONJWA YETU.”

Unaona hapo?, YESU hakumponya mmoja au wawili, au watatu tu basi, hapana biblia inasema aliwaponya WOTE waliomwendea.Hivyo usiogope ikiwa ugonjwa ulionao hauponyeki, iwe ni cancer, iwe ni kisukari, iwe ni ukimwi, wowote ule, Usiogope unachopaswa kufanya ni kumkabidhi tu Kristo huo ugonjwa aushughulikie, wala hauhitaji mtumishi aje kukuwekea mikono, hata sauti hii unayoisikia inatosha kuinyanyua Imani yako na kupokea uponyaji wako. Unachopaswa kufanya ni mwamini tu YESU, na kama hujamkabidhi maisha yako, mkabidhi leo. kisha wewe mwenyewe zungumza naye mwambie unataka UPONE. Kisha kuanzia huo wakati anza kumshukuru kwasababu alishakusikia..usirudie rudie kumwambia wewe mshukuru tu! kwasababu yeye sio kama sisi wanadamu, jambo moja lazima tuambiwe mara sita sita ndipo tuelewe.

Anza pia kupenda kulitafakari Neno la Mungu kuanzia huo wakai, soma biblia shuhuda zote za matendo makuu ya Yesu aliyokuwa anawafanyia watu, pitia injili zote nne, hiyo itakusaidia kuiimarisha imani yako kwa YESU, tatizo linakuja ni pale mtu anamwomba leo Bwana YESU amponye, halafu anaendelea na mambo yake mengine, hana muda tena na habari za Mungu.

Unajua tatizo linakuja wapi kwa mtu wa namna hiyo?. Ni pale hata mfano Mungu akimponya ugonjwa wake, hatajua kuwa ni Mungu ndiye aliyemponya, hivyo hata uponyaji wake atakuwa na mashaka nao akidhani pengine ni Mungu au pengine kapona tu yeye mwenyewe, ataendelea kuwa hivyo kwasababu hakuwa na muda wala na Imani kwa aliyemtarajia amponye. Hivyo watu wa namna hiyo kupokea uponyaji wao inakuwa ni ngumu sana kwasababu ni rahisi sana kuingiwa na mashaka, na Imani ikishaingiwa na mashaka huwa haizai.

Lakini ukiwa ni mtafakariji mzuri wa Neno la Mungu, inakuwa ni ulinzi kwako, pale IMANI yako inapotaka kuyumba kidogo unakumbuka maandiko, au unayatafakari maandiko. Na mwisho wa siku Uponyaji wako unakufika.

Hivyo ndugu, YESU ni muweza mtwike yeye fadhaa zako kwasababu yeye anajishughulisha sana na mambo yako na kama haujamkabidhi maisha yako, fanya hivyo leo maadamu muda upo, kwasababu yeye anahitaji kuiponya roho yako zaidi ya mwili. Kwasababu anaweza akakuponya ukimwi leo ukawa mzima, lakini kesho ukaishia katika ziwa la moto, sasa hiyo inayo faida gani. Ni heri uponywe vyote, na ndicho anachokitaka yeye, Kwahiyo tubu ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ili ufanyike mtoto wa Mungu kwanza, Kisha hayo mengine atakuzidishia.

Ubarikiwe sana.

Pia washirikishe wengine habari za Uzima ulio katika damu ya YESU popote pale ulipo.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UMEFUNULIWA AKILI?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

TUSIFUNGWE NIRA PAMOJA NA WASIOAMINI.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

DHAMBI YA ULIMWENGU.


Rudi Nyumbani

Print this post

MWANA WA MUNGU.

Biblia inasema katika

Waefeso 4: 13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.

15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, KRISTO.”

Hapo anasema NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, ikiwa na maana kuwa, kuna uwezekano tukamfahamu kidogo, hivyo inahitajika kumfahamu sana MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO) Na kusudi lenyewe la kumfahamu sana Yesu Kristo, sababu zimeshatolewa hapo mbele nazo ni “ili tusiwe tena watoto wachanga tukichukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja,na kuzifuata njia za udanganyifu”.

Moja ya jukumu la muhimu sana kwa mkristo yoyote aliyezaliwa mara ya pili ni KUJIFUNZA KUMJUA YESU KRISTO NI NANI??…Kwa maana neno lenyewe Mkristo, limetokana na neno KRISTO yaani yeye aliyetiwa mafuta na Mungu, kwa hiyo kama Yesu ndiye Kristo moja kwa moja wafuasi wake wataitwa Wakristo. Taifa la Tanzania lina watu wake wanaoitwa watanzania, kadhalika na taifa la Marekani, watu wake wanajulikana kama wamarekani, vivyo hivyo Taifa la Yesu Kristo, watu wake wataitwa Wakristo..

Kwahiyo ni wajibu wetu na haki yetu kumjua Yesu Kristo kwa undani kuwa yeye ni nani? Katoka wapi? Je! Ni Mungu au ni mwanadamu wa kawaida tu? Anaokoaje okoaje watu!, alikuwa wapi kabla ya ulimwengu kuumbwa, yupo wapi sasahivi, na atakuwa wapi baadaye,? Na kama yupo ana mamlaka gani sasa na anafanya nini sasahivi, na atakuwa na mamlaka gani baadaye?, je! kuna umuhimu wowote kumfuata na kumwamini? Je! kuna sababu yoyote ya kujitumainisha kwake au la!? Kwanini afe? Na kisha azikwe na kisha afufuke? Je! kulikuwa na umuhimu wowote wa yeye kufanya hivyo? Na kwanini aondoke na asingeendelea kubaki duniani? Na kwanini apae kurudi alikotoka sababu kuu ya kufanya hivyo ni nini?..Kwanini alikuwa anajiita mwana wa Adamu, hilo neno mwana wa Adamu maana yake ni nini? na lina mahusiano gani kati yake na sisi? Kwanini anajiita yeye ni mwana wa Daudi? Ana uhusiano gani na Daudi? Na kwanini sehemu nyingine anasema yeye ndiye aliye na ufunguo wa Daudi? Huo ufunguo wa Daudi ndio upi? Na unafungua nini (Ufu 3:7)?

Na kwanini sehemu nyingine anajiita mwana wa Mungu,.. kwanini wanamwita simba wa Yuda kwanini sio simba wa mwituni?,… na kwanini anajiita yeye ni Jiwe kuu la pembeni?, hilo jiwe kuu la pembeni ndio kitu gani? Kwanini anajiita yeye ni mwana kondoo? na wala si ng’ombe?… Kwanini anajiita yeye ndiye ile nyota ya asubuhi,… Kwanini anasema yeye ndio njia na kweli na uzima? Mtu anawezaje kuwa njia?…. Kwanini anajiita shahidi mwaminifu? ….Kwanini anasema yeye ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa? Je! wafu wana wazaliwa wa kwanza na wa mwisho? Nk..nk…nk

Sasa kama huna majibu ya maswali hayo kwa angalau asilimia themanini (80%) na bado unasema wewe ni mkristo, unahudhuria kanisani na kuwa mshirika mwema…Basi jua kuwa HUMFAHAMU YESU KRISTO NI NANI. Na kwasababu hiyo basi utabakia kuwa mtoto mchanga na utachukuliwa na kila aina ya upepo wa Elimu unaokuja mbele yako, mtu Fulani akitokea akikwambia Yesu yuko hivi, utafuata tu! mwingine akitokea akikuambia yuko vile…utafuata tu! hata mganga wa kienyeji akivua hirizi zake na kuvaa suti na kuanza kukuhubiria habari za Yesu kwa jinsi anavyojua yeye, UTAMWAMINI TU! kwa kwasababu HUMJUI YESU KRISTO, Kwasababu wewe ni kama mshabiki wake tu YESU! sio mtu wa Taifa lake, hustahili kuitwa Mkristo, ni Mkristo jina tu!…

Swali maarufu na la kipekee Bwana Yesu alilowahi kuwauliza mitume wake ni hili “Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?”… Unaona swali hilo? Mitume hawakuwa na bahati mbaya sana kuulizwa hilo swali na Bwana Yesu, hata leo Roho Mtakatifu anakuuliza wewe unayesoma ujumbe huu moyoni mwako “Nawe wasema kuwa mwana wa Adamu ni nani?”…je! ni Bwana na mwokozi tu? au ni nani zaidi?..

Nataka nikwambie tu ndugu wa thamani? Unayesoma ujumbe huu…Tafuta sana kumjua Yesu Kristo kuliko kitu kingine chochote! Kuliko hata hizo mali unazozihangaikia, kwasababu uzima, mauti, tumaini, hatima, na mambo yote yanatoka kwake…Dunia yote sasahivi imewekwa chini yake, hakuna chochote kinachotokea kiwe kibaya au kizuri ambacho hajakiruhusu yeye?… Hakuna mtu yeyote ambayo anaweza kutenda jambo lolote liwe baya au zuri kabla yeye hajalipitisha..

Maombolezo 3: 37 “Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?

38 Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema?”

Unaona hapo? Bwana ndiye muhasisi wa kila kitu! Kwaufupi tu hatuwezi kumwelezea hapa jinsi alivyo lakini yeye ndiye aliyetiwa mafuta na Mungu mwenyewe, nyota iliyosahihi kabisa ya kufuata! Isiyoelekeza upotevuni.

Matokeo ya watu kuzombwa na mafundisho mengi ya uongo yaliyopo duniani sasa ni kutokana na kwamba watu hawamjui Yesu waliyempokea, kwasababu biblia inasema yupo yesu mwingine anayehubiriwa duniani.

(2Wakoritho 11.4 Maana yeye ajaye akihubiri YESU MWINGINE ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!).

Tukiyajua hayo, tutakuwa makini na tutatia bidii kutaka kumjua YESU KRISTO mwokozi wetu kwa undani kila iitwapo leo ili tusimame upande ulio salama, vinginevyo hatuwezi kwepa kuchukuliwa na wimbi hili la upotevu lilipo duniani pasipo hata sisi kujua. Maana biblia inasema watawadanganya yamkini hata walio wateule.

Ni maombi yangu kuwa kuanzia leo,utamtafuta kumjua Huyu Yesu Kristo kwa undani wake?, uweza wake Kumbuka Biblia pia inamtaja yeye kuwa ni SIRI YA MUNGU, hivyo kama ni siri inahitajika bidii kuijua, hivyo basi tumepewa jukumu la kuzidi kumjua Yesu Kristo kwa undani kwa kadri siku zinavyozidi kwenda hata tutakapoufikia umoja wa Imani unaozungumziwa hapo..

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NAMNA GANI NITAPOKEA NGUVU ZA BWANA YESU?

UAMSHO WA ROHO.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

KARAMA ILIYO KUU.

MOYO ULIOELEKEA KWA MUNGU


Rudi Nyumbani

Print this post

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

Bwana Yesu alitufundisha SALA iliyo ya kipekee sana, ambayo tunaweza kusema ni sala mama iliyobeba vipengele vyote muhimu vitakavyotuongoza sisi katika kumwomba Mungu daima. Na katika sala hiyo kuna mahali tukifika tunasema UFALME WAKO UJE.

Ulishawahi kujiuliza au kutafakari kwa karibu kidogo ni kwanini ufalme wake uje?. Hiyo inatupa picha kuwa Upo ufalme ambao bado hujafika, nao si mwingine zaidi ya ule wa mbinguni. Mambo yanayoonekana mwilini siku zote yanafunua mambo ya rohoni, katika mwili tunaona falme nyingi tofauti tofauti na kila falme inatafuta kuwa kubwa na yenye nguvu zaidi ya nyingine ili imiliki.. Lakini pia unapaswa kujiuliza ikiwa wanadamu wote ni sawa, ikiwa wanadamu wote walitoka kwa mtu mmoja Adamu, ni kwanini basi wasingekuwa na ufalme mmoja imara, unaomiliki dunia yote?. Ni kwanini basi tunaona falme nyingi tofauti tofauti duniani na kila moja inataka kuwa zaidi ya nyingine?. Ipo sababu inayoifanya dunia kuwa hivyo,

Tunafahamu siku zote ili familia isimame haiwezi kuwa na mababa wawili, ni lazima awepo mmoja tu atakayetawala na kuongoza kila kitu kwenye nyumba vinginevyo kama ingekuwa hivyo basi migongano lazima ingejitokeza na hivyo familia isingeweza kusimama, kadhalika na hii dunia ili isimame haiwezi ikawa na FALME zaidi ya moja inayotawala kote. Vinginevyo siku zote kutaendelea kutokea uharibifu kama tunaouna leo hii duniani.

Sasa ili tufahamu hatma ya falme hizi zote za dunia zilizopo sasa ni vizuri kujifunza kwanza hatma ya falme zilizotutangulia huko nyuma hata kabla ulimwengu kuumbwa, zilitokeaje tokeaje na kusimamaje mpaka leo hii Tunaona kuna ufalme mmoja tu usioasika wa MUNGU ambao ndio huo tunautazamia uje hivi karibuni Kwasababu biblia inasema,

Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani(1Wakorintho 10:11)”.

Embu sasa tujifunze jinsi ule ufalme wa mbinguni ulivyoweza kusimama, Kama tunavyosoma biblia inatuambia hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi..Ikiwa na maana ya MBINGU makao ya malaika na NCHI makao ya wanadamu. Lakini haituambii kuwa mbingu ilikuwa ukiwa, bali nchi ndio iliyokuwa ukiwa na ukiwa huo uliendelea kwa kipindi Fulani biblia isichokitaja mpaka hapo Mungu aliposhuka tena kuiunda dunia na kumuumba mwanadamu ndani yake na baadaye kuja kumpa ufalme.

Sasa tukirudi kule mbinguni baada ya malaika kuumbwa aliunda mfumo wa ufalme, utakaoweza kutawala mambo yote ya kule. Na kama tunavyofahamu ni kawaida ya Mungu kuvitawaza viumbe vyake ili visimamie kazi zake zote za umiliki. Na ndio hapo tunakuja kuwaona malaika wa juu kabisa wakina Michaeli, Gabrieli, na Lusifa,(ambaye ndio shetani) wanatokea ili waongoze vyote katika upana wa mbingu ile, waongoze jamii kubwa sana ya malaika watakatifu waliokuwa mbinguni, wasimamie kazi zote za Mungu zilizokuwa zinaendelea mbinguni. Wauendeshe ule ufalme Mungu aliouweka chini yao katika kanuni zote na utaratibu wote ambao Mungu alikusudia ufanyike. Waende sawasawa na mapenzi ya Mungu.

Ni ufalme uliokuwa wa amani kwa muda mrefu,Mungu aliufurahia akiona jinsi malaika zake wanavyokwenda kwa hekima zake lakini ilifika wakati mambo yakabadilika, Shetani kwa kuona ujuzi uliokuwa ndani yake kuwa ni mwingi, kwa kuona uzuri na hekima aliyokuwa nayo katika bustani ya Mungu ya mbinguni akatamani kuwa kama Mungu, akatamani ule ufalme ungekuwa wake ajitawale mwenyewe, sasa ameshajua kila kitu hana haja tena ya kutembea chini ya kanuni za Mungu, anataka na yeye akawe na ufalme wake ajitegemee, na mawazo yake yalikuwa siku moja amwangushe muumba wake chini ili amiliki vyote(Isaya 14). Hivyo alianza kidogo kidogo kubudi njia zake mwenyewe za udanganyifu huku akisapotiwa na baadhi ya malaika wengine waliokuwepo mbinguni ambao nao pia hawakutaka kutawaliwa. Ikaendelea hivyo hivyo mpaka mapambano yalipozuka mbinguni.

Lakini shetani kwa akili zake chache alifahamu kuwa utaleta upinzani mkubwa sana kwenye ufalme ule kiasi cha kutetemesha mbingu. Alijua hata kama vita itatokea na akashinda basi ufalme ule utagawanyika na kuwa falme mbili. Yeye ataondoka na vyake, na wale kubakiwa na vyao, Hakujua kuwa kama kuna yeyote mbinguni anaouwezo wa kumshusha chini kiasi ambacho tunamwona sasahivi..

Embu jaribu kufikiria mpaka shetani anafikia hatua hiyo ya kuonyesha kiburi kikubwa namna hiyo, Mungu alikuwepo wapi asimpoteze kabisa?. Hii inatuonyesha kuwa Mungu ni Mungu wa uhuru, ikiwa mtu utauchagua uovu uwe sehemu ya maisha yako, Mungu hatakuja kukuondolea kama apendavyo japo anao uwezo huo, bali atamshauri lakini akikataa atamwacha uende kumwangamiza, kwasababu sisi hakutuumba kama maroboti tusiokuwa na uwezo wa kufanya maamuzi.

Hivyo kiburi cha shetani kilivyozidi kunyanyuka, alivyojiona kuwa ndio anazidi kupata nguvu mbinguni, anaamua sasa atakalo.. Biblia inatuambia ALIANGUKA GHAFLA KAMA UMEME KUTOKA MBINGUNI.

Siku yalipomtokea hayo hakuamini kama ingekuwa ni kiwepesi namna hiyo jinsi alivyoanguka kwa ghafla dizaini ile…Yaani kitendo cha kufumba na kufumbua yeye na malaika zake walijikuta wametupwa chini kwenye dunia ambayo hapo mwanzo ilikuwa haijakawaliwa na wanadamu.

Na ndio maana Bwana Yesu anasema Luka 10:8 “..NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI KAMA UMEME.”

Unaona hapo?. Hakuna kitu kinachosafiri haraka hapa duniani kama Umeme, Hivyo Bwana Yesu kusema hivyo alitaka kuonyesha ni jinsi gani kuanguka kwa shetani kulivyokuwa kwepesi kushinda alivyoweza kufikiria na kwa haraka, yaani wakati alipoanza kujiundia ufalme wake bandia ambao ulionekana kama ni mkubwa kule mbinguni, ulivunjwa mara moja, na kujikuta yeye pamoja na malaika zake hawapo tena mbinguni. Ni tendo la haraka sana kama vile UMEME.

Embu tusome kidogo baadhi ya unabii uliomuhusu Shetani na ufalme wake aliokuwa amejiundia.:

Ezekieli 28: 12 “Mwanadamu, umfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, umwambie, Bwana MUNGU asema hivi; Wewe wakitia muhuri kipimo, umejaa hekima, na ukamilifu wa uzuri.

13 Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari.

14 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.

15 ULIKUWA MKAMILIFU KATIKA NJIA ZAKO TANGU SIKU ILE ULIPOUMBWA, HATA UOVU ULIPOONEKANA NDANI YAKO.

16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto.

17 Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.

18 Kwa wingi wa maovu yako, katika uovu wa uchuuzi wako, umepatia unajisi patakatifu pako; basi nimetokeza moto kutoka ndani yako, nao umekuteketeza, nami nimekufanya kuwa majivu juu ya nchi, machoni pa watu wote wakutazamao.

19 Wote wakujuao kati ya kabila za watu watakustaajabia; umekuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwapo tena hata milele”.

Isaya 4: 11 “Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika.

12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.

14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.

15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.

16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;

17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?

18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;

19 Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako, Kama chipukizi lililochukiza kabisa; Kama vazi la wale waliouawa, Wale waliochomwa kwa upanga, Wale washukao mpaka misingi ya shimo; Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu.

20 Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi, Kwa maana umeiharibu nchi yako, Umewaua watu wako; Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele”.

Hivyo ndivyo Shetani na ufalme wake ulivyo sasa. 

SASA MAMBO HAYO YANATUFUNDISHA NINI?.

Kama Mungu aliziumba Mbingu na nchi, na kule mbinguni aliweka ufalme, kadhalika na katika nchi aliweka ufalme wake. Na ufalme huo Ulianzia Edeni katika bustani ya Mungu. Akamweka mwanadamu wa kwanza katika bustani hiyo, naye ndiye Adamu kama tu vile Mungu Mungu alivyomweka shetani katika Edeni ya mbinguni bustani ya Mungu (kama tulivyosoma hapo juu kwenye Ezekieli 28:13). Lakini mwanadamu hakutaka kutawaliwa na Mungu ndipo naye akausikiliza ule uongo wa shetani akaasi, na kuanzia hapo ndipo ukawa mwanzo wa ufalme mbovu huko huko zikatokea na nyingine nyingi duniani na kila moja ya hizo falme zipo chini ya malaika wa shetani sasa. Na shetani akiwa kama mfalme wa wafalme wa ulimwengu huu sasa.

Kumbuka shetani alishashindwa mbinguni akijua kuwa lile anguko lake lilikuwa kuu sana. Hivyo alipotupwa huku duniani anawavaa wanadamu wawe na tabia kama za kwake ili nao siku ya uharibifu wao ufike kwa ghafla na haraka sana kama UMEME. Ili wote kwa pamoja wajikute katika lile ziwa la Moto.

Na ndio maana biblia ilishasema katika..

1Wathesalonike 5: 2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, NDIPO UHARIBIFU UWAJIAPO KWA GHAFULA, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.”

Ndugu, anguko la ufalme huu mbovu wa shetani unaoendelea sasa duniani utakuja kwa ghafla sana na haraka, mahali ambapo wanadamu wanasema sasa sayansi yetu imetufikisha mbali, ustaarabu wetu wa umoja wa mataifa na haki za kibinadamu sasa zinazuia uvunjifu wa amani duniani, hivyo dunia inaweza kuendelea kuwepo kwa muda wa mabilioni ya miaka, Kumbuka hapo hapo ndipo shetani alipofikia kabla hajaanguka aliwaza kule mbinguni. lakini siku yalipompata ndipo alipojua kuwa aliye juu ndiye anayetawala. Kadhalika ndivyo itakavyokuwa kwa dunia hii ambayo ipo karibuni kutoweshwa, Ni lazima iwe hivyo ili kuupisha ufalme wa Mungu kuchukua nafasi yake kwa kupitia YESU KRISTO BWANA WETU.

Mji wa Babeli, uliotukuka sana duniani zamani hizo na uliohusika kuwachukua wana wa Israeli mateka, ulikuwa ni ufalme ambao hakuna mtu angeweza kutegemea kama ungeanguka, kwa jinsi ulivyokuwa na ulinzi mkubwa, na kuta imara, na ustaarabu mkubwa..lakini ulipofika siku yake ya maangamizi, Viganja vilitokea ukutani mwa mfalme wa ufalme huo na kuandika MENE MENE, TEKELI na PERESI..Usiku huo huo ndio ulikuwa mwisho wa mji unaoitwa Babeli. Ndivyo itakavyokuwa kwa falme zote za duniani zilizopo leo, uharibifu utakuja gafla na UFALME WA YESU KRISTO, UTAKUJA.

Ufunuo 11:15  “Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, UFALME WA DUNIA umekwisha kuwa UFALME WA BWANA WETU NA WA KRISTO WAKE, naye atamiliki hata milele na milele”.

Hivyo ndugu, usifuate upepo wa huu ulimwengu unavyoelekea, ukapumbazika kwa jinsi unavyozidi kunawiri ukadhani kuwa bado muda mrefu Kristo kurudi mara ya pili na kuangusha huu ufalme wa giza uliopo sasa. Jua tu uharibifu wake utakuja saa watu wasioweza kuutazama. Utaanguka kama umeme. Ni maombi yangu kuanzia sasa utajiweka tayari na kuanza kutazama mambo ya ufalme wa mbinguni unaokuja usiohasika zaidi ya mambo ya ulimwengu huu ambayo ni kitambo tu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USIMWABUDU SHETANI!

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?.

MARIAMU

UHURU WA ROHO.

HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

NYOTA YA ASUBUHI.


Rudi Nyumbani

Print this post

JIWE LA KUSAGIA


Marko 9.41 “Kwa kuwa ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake.
42 Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini. “Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini”.

Bwana Yesu alisema Ishara hizi zitafuatana na hao waaminio? kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya (Luka 1:17-18).

Lakini pamoja na ishara hizo, zipo ishara nyingine zinazofuatana na hao waaminio..Na ishara hizo ni thawabu zinazoambatana nao, kadhalika na laana zitakazoambana nao kama wasipotii.

Mtu aliyemwamini Kristo, akatubu na kuacha dhambi zake kabisa, na kupokea Roho Mtakatifu, Bwana huwa anampa thawabu mkononi mwake katika ulimwengu wa roho na huwa hiyo thawabu inatembea naye…Inapotokea kafika mahali kakaribishwa na watu na kuhudumiwa vizuri hata nafsi yake ikafurahi na kuburudika, wale watu waliomhudumia mtu huyo kwakuwa ni mtu wa Kristo, huwa biblia inasema haimpiti kamwe thawabu yake. Kumbuka kumtendea wema Mkristo ni tofauti na kumtendea mema maskini ambaye sio Mkristo.

Ukimtendea mema Mkristo ni sawa umemtendea mema Kristo mwenyewe kwasababu ndani ya yule mtu, yupo Kristo mwenyewe. Ukimkaribisha umemkaribisha Kristo mwenyewe, ukimbariki ni sawa umembariki Kristo mwenyewe..Hivyo thawabu yake ni kubwa zaidi kuliko thawabu ya kumsaidia mtu mwingine yoyote ambaye sio mkristo.

Lakini pamoja na kwamba kuna Baraka zinazoambatana na watoto wa Kristo, wote waliozaliwa mara ya pili, zipo pia Laana zinazofuatana na hawa watoto wa Mungu. Biblia inasema “amlaaniye Israeli atalaaniwa na ambarikiye Israeli atabarikiwa…Sasa licha ya wale wa Israeli tunaowaona kule mashariki ya kati, wapo pia waisraeli ambao ni waisraeli hasa,.. na hawa sio wengine zaidi ya watoto wote wa Mungu,waliompokea Bwana Yesu Kristo na kumwamini na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake. Hawa ndio waisraeli hasa biblia inayowataja.

Hivyo kumlaani mtu yoyote ambaye ni milki ya Bwana Yesu, mtu aliyeamua kuyasalimisha maisha yake kwake ni sawa na kumlaani Kristo mwenyewe na ni sawa na kujilaani wewe mwenyewe… Kwahiyo ni muhimu sana kuchunga midomo yetu, mbele za watoto wa Mungu. Usimwone ni Mpole ukamdharau wala usimwone ni wa huruma ukamtamkia maneno yasiyofaa utajitafutia matatizo ambayo chanzo chake hutakijua.

Sasa laana nyingine iliyo mbaya, ambayo inatembea na hili kundi la watoto wa Mungu, ni ile itokanayo na KUWAKOSESHA.

Ni heri umlaani mtu aliyempa Kristo maisha yake, kwasababu mtu huyo anaweza kukusamehe na pengine Mungu akaepusha ghadhabu yake juu yako, lakini kosa lolote mtu atakalofanya litakalomfanya yule mtoto wa Mungu aliyekuwa amesimama kiimani KUANGUKA…Hilo ni kosa ambalo halina msamaha ni baya kuliko kosa la kumlaani.
Sasa nini maana ya KUKOSESHA.

Kukosesha ni jambo lolote ambalo mtu anaweza kumfanyia mtoto wa Mungu kwa makusudi aliyesimama kiimani kuanguka na kurudi nyuma au kutenda dhambi, au kosa lolote litakalomfanya mtoto wa Mungu amkosee Mungu wake.

Kwamfano imetokea Binti kampa Kristo maisha yake kweli na kakusudia kuacha dhambi kabisa, na kabatizwa, Na akaanza kuishi maisha ya ukristo kulingana na maandiko, lakini kijana mmoja pale pale kanisani anayejua kabisa maandiko anatokea na kuanza kumsumbua na kumtaka, na hatimaye kumdanganya, na kwasababu ya ule uchanga wa kiroho wa yule binti akanaswa na mtego wa Shetani na kuanguka katika dhambi ya uasherati na kumkosea Bwana Mungu wake, sasa yule binti Bwana atamwadhibu … Lakini yule kijana aliyemkosesha ana adhabu kubwa zaidi kuliko ya yule binti.. Au binti anayejua kabisa kijana Fulani kaokoka na anamtumikia Bwana kwa moyo,lakini kwa tama yake ya macho anaanza kumtafuta kijana yule na kumshawishi, kwa kujipendekeza hata akamwangusha yule kijana kwenye dhambi ya uasherati wake hapo Ndio biblia inasema… “Ingemfaa zaidi mtu huyo JIWE LA KUSAGIA LIFUNGWE SHINGONI MWAKE, akatupwe baharini, KULIKO KUMKOSESHA MMOJAWAPO WA WADOGO HAWA.”

JIWE LA KUSAGIA NI NINI BASI?.

Zamani watu walikuwa hawasagi nafaka kwa mashine kama tulizonazo sasa, walikuwa wanasaga kwa kutumia mawe mawili, lile kubwa linakaa chini na lile dogo linakuwa juu ndio linalotumika kusagia…mawe haya yanakuwa ni mazito sana ili kusudi kusaidia nafaka ile iweze kusagika na kuwa unga…Sehemu chache sana katika nyakati hizi ndio bado zinatumia huo ustaarabu wa usagaji wa nafaka. Lakini zamani ilikuwa ni lazima kila nyumba iwe na hilo jiwe, hata kama hiyo nyumba ni maskini vipi, ilikuwa ni kitu cha muhimu sana, ni kama tu kinu kwa sasa..usipokuwa na jiwe hilo ilikuwa huwezi kula kwasababu ndio kifaa cha msingi kabisa cha riziki kilichokuwa kinahitajika katika nyumba kwa wakati huo.

Sasa Bwana Yesu alitumia mfano wa jiwe la kusagia, kufunua kwamba mtu yoyote atakayemkosesha “mmojawapo wa wadogo wamwaminio yeye” ingelimfaa zaidi mtu huyo jiwe hilo la kusagia lifungwe shingoni mwake na kwenda kutupwa baharini…Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba INGEMFAA ZAIDI MTU HUYO RIZIKI YAKE YOTE ANAYOIPATA IONDOLEWE, NA IWE KITANZI KWAKE CHA KUMWUA KATIKA MAANGAMIZI AMBAYO YANATOKANA NA HIYO RIZIKI. na pale anaposema akatupwe katika bahari alimaanisha mtu huyo, ATUPWE KATIKA ZIWA LA MOTO”

Unaona hiyo laana jinsi ilivyo mbaya?? Ina maana kuwa katika mahali popote unapopatia riziki, hiyo sehemu inakuwa kitanzi kwako cha kukufanya wewe uangamie kwa kuzama kama mtu anavyozama katika maji akiwa na jiwe shingoni, na hatimaye hiyo sehemu yako ya kujipatia riziki (kazi yako) inakuua na kuwa sababu ya kukupeleka katika ziwa la Moto.

Ulikuwa unafanya kazi nzuri, na kupata kipato kizuri, hiyo kazi inageuka kuwa kitanzi kwako inaanza kukushusha chini, inakuzamisha kwenye matatizo ambayo hayajawahi kutokea, inakutafuna na mwisho wa siku inakuua, na baada ya kifo inakupeleka katika ziwa la moto. Hata kama bado hujafikia hatua ya kujitafutia mwenyewe lakini ikiwa unafanya dhambi hizo za makusudi, itafika tu wakati utatatufa kitu kwa ajili ya maisha yako. Na ndiko huko huko utakapokwenda kujimalizia mpaka kuzimu.

Ndugu yangu unayesoma haya, jiepushe na watoto wa Mungu, wewe binti kaa mbali na walioamua kumfuata Bwana Yesu, usijaribu kuwashawishi wawe kama wewe ulivyo, usijaribu kuwashawishi watoke katika mstari ili kumkosea Bwana wao wawe kama wewe. Kama wewe umeamua kuwa vuguvugu basi kuwa kwa nafsi yako mwenyewe, usiwafanye watoto wengine wa Mungu wajikwae kwasababu yako, ni kujitafutia matatizo yasiyokuwa na utatuzi.

Usiwashawishi wengine, kuvaa vimini, kuvaa suruali, kupaka wanja, kwenda disco, na ndani ya dhamira yako unajua kabisa, mambo hayo ni makosa kuyafanya kwa watumishi wa Mungu…Usijaribu kuyafanya hayo, kwasababu ni sawa na unamfanyia Kristo mwenyewe.

1Wakoritho 8: 12 “Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo”.

Kwa nje utamwona katika hali ya udhaifu, lakini ndani yake yupo Kristo, Siku ile ya Mwisho Bwana Yesu alisema atawatenga kondoo na mbuzi, mbuzi ni wale wote waliolikwaza na kulihuzunisha na kulikosesha kundi hili la watoto wa Mungu, wale wote ambao waliwalaani, na kuwatesa na kuwakosesha watoto wa Mungu hao wote watakaa mkono wa kushoto wa YESU Kristo siku ile, watahukumiwa na kisha watatupa katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti.

Mathayo 25: 41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

Kama ulikuwa unafanya hayo pasipo kujua, Bwana ni mwenye Rehema, anachotaka kwako ni ukiri tu ulifanya hayo pasipo kujua na kwamba unahitaji kugeuka na kuwa kiumbe kipya, kwa kudhamiria kabisa kumuishia Mungu, na kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza yeye.. Na kuwa katika kundi lake lililobarikiwa la kondoo na sio mbuzi. Baada ya kutubu Bwana alitupa maagizo ya kwenda kubatizwa, hivyo katafute haraka mahali panapobatiza ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa JINA LA YESU KRISTO na baada ya kufanya hivyo Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kukuongoza katika kweli yote. Baada ya hapo utakuwa na uhakika wa uzima wa milele, na umekamilisha hatua za muhimu za wokovu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JINA LAKO NI LA NANI?

TUNAYE MWOMBEZI.

MJUE SANA YESU KRISTO.

DALILI ZIPI ZITAMTAMBULISHA MTU KUWA AMEFANYIKA KIUMBE KIPYA?


Rudi Nyumbani

Print this post

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

Biblia inatuambia kuwa malaika ni roho watumikao, kuwahudumia wale watakaourithi wokovu. (Waebrania 1:14). Biblia inatuambia pia shetani naye ni mshitaki wetu, yeye na jeshi lake la mapepo wakitushita sisi mbele za Mungu wetu mchana na usiku tunaona kama walivyofanya kwa Ayubu (Ufunuo 12:7), vivyo hivyo malaika watakatifu wa Mungu ambao hao Mungu aliwaweka kwa lengo la kutuhudumia sisi (yaani wakristo), wanasimama mbele za Mungu wetu usiku na mchana wakipeleka habari zetu njema mbele zake.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba MALAIKA WAO MBINGUNI SIKU ZOTE HUUTAZAMA USO WA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI.” (Mathayo 18.10).

Hii ni huduma kuu ya malaika walio nayo sasa.

Lakini japo malaika hawa wamepewa uwezo mkubwa zaidi yetu sisi, japo ni watakatifu sana kuliko sisi, japo ni wakamilifu kuliko sisi lakini tunasoma wanaposimama mbele za Mungu ili kupeleka habari zetu mbaya wanatetemeka na kuogopa, Embu fikiria leo hii unajiita mkisto, na siku ile ulipofanyika kuwa mwana Mungu, ulifahamu kuwa Kristo alilituma jeshi lake la malaika kukulinda pamoja na kuhusukia kuchukua dua zako na matendo yako mema mbele za MUNGU. Lakini jaribu kifikira wewe unayejiita mkristo halafu leo hii unakwenda kuzini, na huku unajua kabisa wapo malaika watakatifu walitumwa kutembea na wewe, halafu wanakuona unafanya kitendo hicho cha aibu na cha kichafu ambacho mtu anayejiita Mkristo hastahili kukifanya. Wewe unadhani malaika watakatifu watapeleka repoti gani nzuri ya kwako mbele za Mungu.?

Kwasababu kumbuka unapoomba maombi yako yanachukuliwa na malaika na kufikishwa mbele ya kiti cha enzi, unapofanya wema, wema wako unachukuliwa na malaika moja kwa moja na kuwasilishwa mbele ya kiti cha enzi, anapofanya tendo lolote jema linachukuliwa na kupelekwa katika kumbukumbu za kimbinguni zikingojea kusomwa mbele ya kiti cha enzi mbinguni, kadhalika yule malaika husika naye huwa anajisikia fahari kupeleka habari njema kama hizo mbele za Mungu. Hata akifika pale atakusifia kwa maneno mazuri na kumkumbusha Mungu na mambo mengine ya kwako mazuri unayoyafanya hata kama hujawahi kumwomba Mungu. Malaika wanakuwaanapanda j na kushuka juu yako kupeleka mema yako na kukuhudumia sawasawa na maono aliyoyaona Yakobo (aliona malaika wakipanda juu na kushuka) Mwanzo 28:12 “Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake”.

Lakini unapokuwa ni mwovu halafu unasema umeokoka, umebatizwa, umepokea Roho Mtakatifu, hataweza kupeleka habari yoyote njema mbele za Mungu kwa ajili yako?. Kumbuka yeye ni mtakatifu lakini matendo yako yanamfanya ajione mchafu na asiyestahili kupeleka habari zako mbaya mbele zake. Na hii ni mbaya sana kwasababu wakati Mungu atakapopokea ripoti za wana wake wengine duniani, za kwako zitakuwa hazifiki, na hapo atakapomuuliza malaika husika aliyepewa jukumu la kutembea na wewe, vipi habari za huyu mtu kwanini hazinifikii, lakini kwa kuwa malaika wa Bwana ni wenye hekima nyingi, watajaribu kuzungumza tu yale mema ya nyuma uliyokuwa anayafanya na kusitiri ubaya wako. Lakini jicho la Mungu linaloona mbali, litatazama lenyewe. Na yeye na kuuangalia mwenendo wako yeye mwenyewe. Hapo ndugu usitamani ufikie hatua hiyo kwasababu hakuna msamaha tena ghadhabu ya Mungu ni kali, hatua hiyo ukishafikia ni nani atakayekutetea?.

2Petro 2:10 “Na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka.

11 Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; IJAPOKUWA MALAIKA AMBAO NI WAKUU ZAIDI KWA UWEZO NA NGUVU, HAWALETI MASHITAKA MABAYA JUU YAO MBELE ZA BWANA.

12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao;

13 Wakipatikana na madhara, ambayo ni ujira wa udhalimu wao, wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa; wamekuwa ni mawaa na aibu wakifuata anasa zisizo kiasi katika karamu zao za upendo, wafanyapo karamu pamoja nanyi;

14 wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

15 wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;”.

Unaona hapo biblia inasema “; IJAPOKUWA MALAIKA AMBAO NI WAKUU ZAIDI KWA UWEZO NA NGUVU, HAWALETI MASHITAKA MABAYA JUU YAO MBELE ZA BWANA”.

.. Unasema wewe ni mkristo lakini unapojisikia tu kutenda dhambi unakwenda kufanya bila kuogopa kuwa Mungu juu anakutazama. Unakuwa mlevi wa chini chini, hutaki ujulikane kwa wakristo wenzako, hujui kuwa malaika wa Bwana wanaona mambo unayoyafanya, wanakosa jambo jema la kwenda kuzungumza juu yake mbele ya kile kiti kitakatifu cha Enzi mbinguni. Unakula rushwa, unakuwa mwizi, unaabudu sanamu, unatazama pornography na unafanya mustarbation kisirisiri ni kweli mwanadamu hakuona lakini wapo wengine wanaokuona, na hao si wengine zaidi ya malaika wa Bwana na mashetani.

Ikiwa sifa zako njema hazipelekwi na malaika basi uwe na uhakika kuwa mambo yako maovu yanachukuliwa na mapepo na kuimbwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu usiku na mchana.

Sasa baada ya Mungu mwenyewe kushuka na kuangalia matendo yako, kwa dua za hayo mashetani ambazo ziliwasilishwa mbele zake, akiona jinsi uliyoonywa mara nyingi ugeuke hutaki ndipo hapo Bwana anatoa tamko. HUYU SI WANGU TENA!. Unakabidhiwa shetani, kuanzia huo wakati unakuwa milki halali ya shetani, hali yako inakuwa mbaya kuliko ulivyokuwa mwanzoni wale malaika waliotumwa kukulinda wanaondoka, habari zako zinasitishwa kutajwa mbinguni wema wako wote unasahauliwa.

Tafsiri ya jina shetani au Ibilisi ni MCHONGEZI au MSHITAKI. Kazi ya shetani kubwa ni kutushitaki mbele za Mungu usiku na mchana…Malaika wao wanapeleka habari zetu njema mbele za Mungu lakini shetani na majeshi yake wao wanapeleka habari mbaya mbele za Mungu. Hiyo ndiyo vita kubwa inayoendelea katika ulimwengu wa Roho, kati ya malaika na mapepo.

Hawapigani kwa kukatana na mapanga, hapana bali wanashindana kwa hoja.

Tuchukue mfano mwepesi..mkristo mmoja anayeitwa Rodgers anayesema ameokoka leo kafunga na kusali lisaa limoja, katoa zaka kanisani, na kamsaidia ndugu mmoja aliyekuwa na uhitaji mtaani kwake, sasa kinachotokea katika ulimwengu wa Roho yule malaika wake anayetembea naye anapeleka habari za wema wake huo mbele za Mungu, na kumwambia Mungu kuwa Mtumishi wako Rodgers kafanya hichi na kile leo, hivyo anastahili thawabu Fulani kulingana na Neno lako hili na lile, Lakini bahati mbaya wakati malaika hao wanamsifia Rodgers mbele za Baba, Rodgers pasipo kulijua hilo kesho yake anakwenda kuzini..kinachotokea sasa ni shetani na malaika zake wanakwenda kumchongea Rodgers mbele za Mungu, kwamba yule mtu mnayesema ameokoka na anastahili kupata hichi na kile leo hii tumemwona anazini hivyo kulingana na Neno hastahili kuitwa mtoto wa Mungu kwasababu maandiko yanasema aziniye na mwanamke hana akili kabisa(Mithali 6:32) na zaidi ya yote maandiko “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu 1Yohana 3:9 ” …na kumbuka haya mapepo yanatoa kabisa mistari mbele za Mungu kumshtaki Rodgers na kwasababu yametoa hoja za nguvu mbele za Mungu, wanakuwa wamewashinda wale malaika wanaomsifia Rodgers na hivyo Rodgers anakabidhiwa shetani. Hivyo ndivyo shetani anavyowashitaki watu.

Unakumbuka maandiko yanasema wana wa Mungu (Malaika) siku moja walipokwenda kujihudhurisha mbele za Mungu shetani naye alikwenda katikati yao kumshitaki Ayubu? (Hiyo inapatikana katika kitabu cha Ayubu 1:6-12).

Kwahiyo Mtu anayeishi maisha ya uvuguvugu na bado anasema ni Mkristo, anafanyika kuwa chombo cha shetani kikamilifu, kama ulikuwa mzinzi kidogo hapo ndipo unajikuta nguvu mbaya ya uasherati unakuvaa unakuwa unakuwa zaidi ya hapo, pombe ulikuwa unakunywa kidogo, unafikia hatua ya kumaliza hata kreti, tabia yako inabadilika ghafla na kibaya zaidi hata kumrudia Mungu hutaweza tena kwasababu Bwana Yesu alishasema hakuna mtu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa kwanza kavutwa na Baba yangu aliye mbinguni. Sasa kama ni Mungu mwenyewe kakukataa unadhani ile nguvu ya kutubu wakati huo utaitolea wapi?. Haiwezekani.Na mwisho wake ni Mauti, kwasababu biblia inasema mshahara wa dhambi ni MAUTI, Na ndio maana malaika watakatifu wanaogopa kupeleka mashitaka yako mabaya juu mbele za Mungu, kwasababu wanafahamu madhara yatakayomkuta mtu huyo mara baada ya kukataliwa.

Ni jambo la kuogopesha sana. Leo hii Bwana anapotuambia tuwe moto, anaamisha kweli kweli, maana tukiwa vuguvugu ndio huko kutapikwa kunafuata. Inasikitisha kuona kwamba mtu anasema ameokolewa na Bwana lakini mambo ya kidunia hajayaacha,.bado anavaa kidunia, anavaa vimini, anavaa suruali, anakwenda Disko, anasikiliza nyimbo za kidunia, anaipenda dunia kuliko kumpenda Mungu, anatazama pornography, anakwenda kwa waganga,ni mtukanaji. Biblia inasema ni heri mtu huyo asingookoka kabisa, kwasababu hata wale malaika watakatifu wasingeletwa kumtazama, Lakini kuwa vile halafu unaishia kuwatia visirani, na kuwafedhehesha unadhani mwisho wake utakuwa ni nini?.

Wana wa Israeli walipokuwa wanatoka Misri Bwana aliwaagizia malaika wake aende mbele yao, na akawaonya wasimtie kisirani kwa mienendo yao mibovu kwa kuwa hatawasamehe,(kutoka 23:20) Unaona tunasema tumekuwa wakristo tujue kuwa hatupo wenyewe. Bali Roho wa Kristo yupo pamoja nasi kadhalika na jeshi la kifalme la malaika wa mbinguni lipo pembeni yetu kutuhudumia. Hivyo tunapaswa tuwe makini sana na mienendo yetu.

Ni maombi yangu, leo hii utaulinda wokovu wako, kila wakati. Ikiwa malaika tu wenyewe wanaogopa kupeleka habari zetu mbaya, japo wao ni watakatifu, unadhani sisi tunapaswa tuishije. Malaika japo wokovu hauwahusu wao lakini wanasita kuizungumza mienendo yetu mibaya mbele za Mungu, si zaidi sisi ambao tupo duniani ambao wokovu unatuhusu? Tunapaswa tujilinde sana mienendo yetu ya kikisto.

Ikiwa bado hujampokea Kristo katika maisha yako huu ndio muda, unachopaswa kufanya ni kutubu mwenyewe kwa kumaanisha kuacha dhambi zako na maisha yako ya kale, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo upate ondoleo la dhambi zako, (Matendo 2:37-38)na baada ya hapo utafanyika mwana wa Mungu kwa Roho wa Kristo atakayekuja ndani yako.. Nawe pia jeshi hili la kimbinguni la malaika watakatifu litatumwa kwako kukulinda, kukutetea na kupelekea habari zako njema mbele za kiti cha Enzi usiku na mchana.

Bwana akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

VITA BADO VINAENDELEA


Rudi Nyumbani

Print this post