Answer: Let’s read
2 Corinthians 3:6 “Who also hath made us able ministers of the new testament; not of the letter, but of the spirit: for the letter killeth, but the spirit giveth life.
To revive means to “Give life” Only God who can give out life to us. So when it says the letter killeth but the spirit giveth life means scripture without revelation of the Holy Spirit it can lose or kills person’s spirit ( Either a person to die physically or spiritually).
But if the scriptures used with the guidance of the Holy Spirit it gives life to a person even if the person was dead can be alive again.
Let’s see how the scripture kills a person physical and later in spiritual death.
How scripture can physically kill a person:
Leviticus 24:19 “And if a man cause a blemish in his neighbour; as he hath done, so shall it be done to him;
20 Breach for breach, eye for eye, tooth for tooth: as he hath caused a blemish in a man, so shall it be done to him again”.
Deuteronomy 19:21 “And thine eye shall not pity; but life shall go for life, eye for eye, tooth for tooth, hand for hand, foot for foot”.
When he says LIFE FOR LIFE, means a man who gave up the life of another for purpose must his life also to be taken away from him, or breaking someone’s tooth and his tooth must taken away from him too, and if he beat or eye piercing and his eye must be pierced.
This scripture and other scriptures taken as it is they must kill a person, many people were dying because of this scriptures, at past when a women found committing adultery her judgement was to be stoned untill to death.
But when the Holy Spirit came, he put it right through the mouth of our Lord Jesus Christ and say..
In Matthew 5:38 “Ye have heard that it hath been said, An eye for an eye, and a tooth for a tooth:
39 But I say unto you, That ye resist not evil: but whosoever shall smite thee on thy right cheek, turn to him the other also.
40 And if any man will sue thee at the law, and take away thy coat, let him have thy cloke also.
41 And whosoever shall compel thee to go a mile, go with him twain.
42 Give to him that asketh thee, and from him that would borrow of thee turn not thou away.
43 Ye have heard that it hath been said, Thou shalt love thy neighbour, and hate thine enemy.
44 But I say unto you, Love your enemies, bless them that curse you, do good to them that hate you, and pray for them which despitefully use you, and persecute you;
45 That ye may be the children of your Father which is in heaven: for he maketh his sun to rise on the evil and on the good, and sendeth rain on the just and on the unjust.
Let’s see how scripture can kills someone spiritually
Lets see this scripture
1 Timothy 5:23 “Drink no longer water, but use a little wine for thy stomach’s sake and thine often infirmities.
This scripture has killed many people spiritually, and made them and up in alcoholics and careless life and the devil has nailed, his goal is to make people die without repentance so as people to go to hell of fire.
Let’s see other related scripture
Ecclesiastes 9:5 “For the living know that they shall die: but the dead know not any thing, neither have they any more a reward; for the memory of them is forgotten”.
This scripture has kill many people spiritually, and end up believing that there is no other life after death, no hell of fire. So according to this scripture made many people to live the life that please them in this world and careless life with this conception that there is nothing going on after death, even after committing adultery no one to judge.
Jesus Christ, the Giver of life said in..
Luke 16:19 “There was a certain rich man, which was clothed in purple and fine linen, and fared sumptuously every day”
20 And there was a certain beggar named Lazarus, which was laid at his gate, full of sores,
21 And desiring to be fed with the crumbs which fell from the rich man’s table: moreover the dogs came and licked his sores.
22 And it came to pass, that the beggar died, and was carried by the angels into Abraham’s bosom: the rich man also died, and was buried;
23 And in hell he lift up his eyes, being in torments, and seeth Abraham afar off, and Lazarus in his bosom.
24 And he cried and said, Father Abraham, have mercy on me, and send Lazarus, that he may dip the tip of his finger in water, and cool my tongue; for I am tormented in this flame.
25 But Abraham said, Son, remember that thou in thy lifetime receivedst thy good things, and likewise Lazarus evil things: but now he is comforted, and thou art tormented.
26 And beside all this, between us and you there is a great gulf fixed: so that they which would pass from hence to you cannot; neither can they pass to us, that would come from thence.
27 Then he said, I pray thee therefore, father, that thou wouldest send him to my father’s house:
28 For I have five brethren; that he may testify unto them, lest they also come into this place of torment.
29 Abraham saith unto him, They have Moses and the prophets; let them hear them.
30 And he said, Nay, father Abraham: but if one went unto them from the dead, they will repent.
31 And he said unto him, If they hear not Moses and the prophets, neither will they be persuaded, though one rose from the dead.
Here the Holy Spirit says there is judgement after death.
So it’s important to have the Holy Spirit as the helper or a teacher when reading scriptures for the better understanding, without the Holy Spirit it is very hard to understand the scriptures because you will end up giving yourself your own interpretations.
If you have not yet received Jesus , you will never understand scriptures, but once you decide to receive Jesus as your saviour and repent your sins and commit yourself never repeat them again and be baptized with the perfect baptism with many water as it is on this scripture (Yohane 3:23)and in the name of Jesus Christ , as the same day you receive Jesus the same day the Holy Spirit will begin to work in you and creat something new.
God bless you.
Related Articles:
What is the difference between flesh and spirit uncleanness?
Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)
Maneno hayo tunayasoma katika kile kitabu cha Mathayo 18:18,
Mathayo 18:18 “AMIN, NAWAAMBIENI, YO YOTE MTAKAYOYAFUNGA DUNIANI YATAKUWA YAMEFUNGWA MBINGUNI; NA YO YOTE MTAKAYOYAFUNGUA DUNIANI YATAKUWA YAMEFUNGULIWA MBINGUNI”
Sasa ili tuweze kuelewa vizuri tuanzie kusoma mistari ya juu kidogo, mstari wa 15
Mathayo 18:15 “Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.
16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.
17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.
18 AMIN, NAWAAMBIENI, YO YOTE MTAKAYOYAFUNGA DUNIANI YATAKUWA YAMEFUNGWA MBINGUNI; NA YO YOTE MTAKAYOYAFUNGUA DUNIANI YATAKUWA YAMEFUNGULIWA MBINGUNI ”.
Katika mazingira kama hayo Bwana alimaanisha kuwa, inapotokea mtu mmoja (aliyeokoka), kafanya kosa basi unapaswa ukamwonye ukiwa wewe na yeye peke yenu, akikusikia na kutubu basi utakuwa umemwokoa kutoka njia ya upotevu (yaani umempata), lakini kama hajakusikia wewe baada ya kumwonya kimaandiko, maandiko yanasema ukachukue watu wengine wawili au watatu urudie mmwonye tena kwa pamoja na kama hataki kusikia basi kanisa liambiwe na aonywe na wengi zaidi na kama pia hataki kusikia na kutubu kwa kosa lake hilo au makosa yake…, maandiko yameruhusu mtu huyo kuachwa kama alivyo.
Na madhara ya kuachwa na kanisa kama alivyo ni makubwa kwasababu hayaishii tu hapa duniani, bali hata mbinguni mtu huyo anakuwa ameachwa (ametengwa na uwepo wa Mungu)..Hakuna chochote atakachovuna katika roho baada ya hapo, mpaka yeye mwenyewe atakapotubu..
Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kuitii injili. Hususani tunapoisikia zaidi ya mara moja, pale inapotuonya, kwasababu tusipoitii, basi inageuka kwetu kuwa USHUHUDA, (yaani sababu ya kutuhukumu siku ile ya mwisho), na inakuwa inafungwa juu yetu, kwasababu tumeidharau, na inapofungwa juu yetu, maana yake imekuwa imetufungia na dhambi.
Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake maneno haya..
Marko 6:10 “Akawaambia, Mahali po pote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale.
11 Na mahali po pote wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia, MTOKAPO HUKO, YAKUNG’UTENI MAVUMBI YALIYO CHINI YA MIGUU YENU, KUWA USHUHUDA KWAO.
12 Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu.”
Utaona pia katika kanisa la kwanza, sehemu nyingi mitume walipokuwa wakifika, na kuhubiri injili, wenyeji wa miji ile walipowakataa walikung’uta mavumbi na kuondoka kwenda miji mingine, maana yake ni kwamba tayari watu wa huo mji, mbingu zimefungwa juu yao, hakuna chochote cha kiroho watakachonufaika nacho baada ya hapo, (wanakuwa wamefungiwa dhambi sawasawa na Yohana 20:23) kwasababu wameidharau injili iliyoletwa kwao zaidi ya mara moja, ikiwataka watubu wamgeukie Mungu.
Matendo 13:50 “Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.
51 NAO WAKAWAKUNG’UTIA MAVUMBI YA MIGUU YAO, WAKAENDA IKONIO”.
Hivyo Kaka/Dada, usidharau maonyo yoteyote ya Mungu yanayoletwa kwako, unapoonywa na kanisa juu ya uzinzi wako, juu ya huyo mwanamke/mwanaume wa kizinzi unayeishi naye, unapaswa uogope!, na kugeuka na kutubu haraka..Maana siku ile kanisa litakaposema basi!, na mbinguni kutakuwa ni BASI!!..Ni Mungu ndio kaamua iwe hivyo, si mwanadamu, ni Mungu ndio kaamua kanisa lake liwe na hayo mamlaka na si mwanadamu.. Na ni kwanini kaamua iwe hivyo, ni kwasababu kama hutaweza kumsikiliza ndugu mwenzako anayekuonya, au kulisikiliza kanisa, basi hata Kristo akikutokea hutaweza kumsikiliza, ndio maana kanisa litakaposeama basi, basi hata mbinguni nako ni Basi!
kwahiyo ni jambo la kuogopa sana!.. kadhalika usiidharau injili inayoletwa kwako, kwasababu siku ikiondolewa kwako, na ile nguvu ya kumrudia Bwana inakuwa haipo tena juu yako, hivyo itii injili yake leo, kwasababu anakupenda na anatupenda sote, hataki tuangamie, sawasawa na ahadi zake.
Luka 10:10 “Na mji wo wote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni,
11 Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yetu tunayakung’uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo
13 Ole wako Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu.
14 Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zake kuliko ninyi.
15 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa hata mbinguni? Utashushwa hata kuzimu.
16 Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze Neno la Mungu ili tupate maarifa sahihi ya kuishi hapa duniani.
Na leo tutaona mazingira ambayo ukikaa katika hayo basi Mungu atakujalia umwone mke/mume sahihi aliyekuchagulia toka mbali.
Tofauti na mazingira ya kiulimwengu ambayo yenyewe ili yakupe mke/mume wa kidunia ni sharti uwe katika mazingira ya kidunia..yaani uvae vimini, ujitembeze na suruali barabarani, unyoe viduku, uishi kama wasanii wa kidunia, uwepo disco na kwenye party party kila wakati n.k. ili uonekane.
Ukikaa katika mazingira kama hayo hakika dunia itakupatia unachokitafuta..
Lakini leo tutajifunza mazingira ya ki-Mungu… Ili Mungu akuonyeshe mke/mume sahihi tokea mbali je! Ukae katika mazingira gani.?
Tutamtazama Isaka mtoto wa Ibrahimu. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka mpaka wakati mama yake anakufa hakuwa na mke bado.
Lakini siku moja Baba yake alipoona ni wakati sasa wa Isaka kuwa na mke alimtuma Kijakazi wake mmoja kwenda kumtafutia mke kutoka katika nchi ya mbali nchi sana ya baba zake. ..kwani hakutaka kumpatia mke kutoka katika miji ile waliyokuwepo.
Kuonyesha kuwa haijalishi utazungukwa na vijana wengi wazuri mahali ulipo, hiyo bado haikufanyi udhani mke/mume Mungu aliyekuchagulia ni lazima atoke hapo.
Sasa utaona mara baada ya yule kijakazi kutumwa kwenda kumtafutia Isaka mke na kumpata alipokuwa anarudi..Huku nyuma kuna tabia na desturi ambayo Isaka alikuwa nayo ambayo nataka leo tuione kwasababu hapa ndipo kiini cha somo letu kilipo.. Tusome..
Mwanzo 24:62-66
[62]Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini.
[63]Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.
[64]Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia.
[65]Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.
[66]Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda.
Rudia tena Mstari wa 62 unasema…
‘Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni’.
Unaona, Pindi tu alipotoa mguu wake na kwenda kondeni kutafakari..alipojijengea desturi ya kwenda maporini mbali na makazi ya watu ili tu kupata utulivu na Mungu wake, kuutafakari ukuu wake na uweza wake na maajabu yake na ahadi zake..huko huko Mke wake alitokea..na akamwona tokea mbali..
Pengine yeye alidhani mjini alikoondoka ndipo wake wanapotokea lakini..alishangaa kule kule kondeni kwa mbali sana ngamia wanakuja wamembeba bibi arusi wake..
Hiyo ni kuonyesha Isaka haukuwa na hulka kama za vijana wengine walizokuwa nazo..alipendelea zaidi kumtafakari Mungu kuliko kuzurura zurura huko na huko.
Matokeo yake akampata Rebeka, mwanamke ambaye tunamsoma mpaka leo, licha ya kuwa alikuwa ni mwanamke anayemcha Mungu lakini bado alikuwa ni mzuri sana wa uso..Mwanzo 26:6-7
Ndugu, ikiwa unamuhitaji mke mzuri na anaye mcha Mungu basi kuwa kama Isaka..lakini ikiwa unamuhitaji Yezebeli basi ishi mfano wa hao vijana wa kidunia wanavyoishi leo hii..
Na hili pia lipo kwa upande wa pili wa mabinti..ikiwa unataka uolewe na mwanamume ilimradi tu mwanamume basi jiweke kama hao mabinti wa kidunia wanavyojiweka wanaotembea nusu uchi barabarani na kujipambapamba kama vile Yezebeli ili waonekane wanavutia..
Utampata unayemtafuta.
Lakini kinyume chake ni kuwa ukitulia katika kusudi la Mungu..unatumia muda mrefu kwa Mungu wako kuliko kutanga tanga..unamtakafakari tu yeye..nakwambia Mungu utakuongoza kwa Isaka wako tokea mbali..kama vile Rebeka alivyomwona Isaka akimfuta kutokea mbali..
Uhitaji kujionyesha onyesha ovyo..kwasababu anayekuletea mke/mume ni Mungu, si mwanadamu..wewe kaa katika kumtakafakari yeye maisha yako yote.
Kuoa utaoa, kuolewa utaolewa tu!..ukiishi maisha yanayopendeza Mungu si uongo utakutendea tu.
Daudi alisema..
Zaburi 37:25
[25]Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,
Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa
Wala mzao wake akiomba chakula.
Mungu hawezi kuacha kumpa mteule wake kitu kilicho chema, na kizuri.. Hawezi kuruhusu mke/mume pasua kichwa atokee mbele ya njia yake, mtu anayemcha yeye. Hilo haliwezekani..
Hivyo kama bado hujaokoka. Tubu leo anza maisha yako upya na Bwana Yesu kwa kumaanisha kabisa..Toba ya kweli inaambatana na kuucha ulimwenguni, mkatae shetani na kazi zake zote na vimini vyake vyote, na suruali zote na viduku vyote..kamtafakari Mungu huko makondeni, hata kama utaonekana mshamba..
Ishi maisha ya kumlingana Bwana..Na bila shaka wakati utafika atamtuma malaika wake kwenda kukuletea mwenzi sahihi..Kama Ibrahimu alivyomtuma kijakazi wake, kumletea Isaka Rebeka.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Tuwasome,
Walawi 11:13 “Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;
14 na mwewe, na kozi kwa aina zake,
15 na kila kunguru kwa aina zake;
16 na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
17 na bundi, na mnandi, na bundi mkubwa;
18 na mumbi, na mwari, na mderi;
19 na korongo, na koikoi kwa aina zake, na hudihudi, na popo”.
Tai ni ndege maarufu anayejulikana kwa uwezo wake wa kuona mbali, na vile vile mwenye uwezo wa kuruka juu zaidi ya ndege wengine wote, Mvua inaponyesha na mawingu kutanda, Tai hupaa juu ya mawingu, na baadaye kushuka chini mvua inapoisha, tofauti na ndege wengine wote ambao mawingu yanapotanda tu!, wanakimbilia viota vyao kujisitiri.(Tazama picha chini).
Furukombe au kwa kiingereza “Vulture” ni aina nyingine ya ndege ambao kimwonekano wanakaribia kufanana na Tai, isipokuwa hawa wana midomo mirefu kidogo, na pia wanakula Mizoga ya wanyama waliokufa maporini (Tazama picha chini), rangi yao ni rangi ya kahawia.
Kipungu ni aina iyo hiyo ya Furukombe, isipokuwa kipungu ni mweusi, tabia zake ni kama za Furukombe wa kahawia, anakula mizoga, tofauti na Furukombe, kipungu yeye anapatikana nchi za ukanda wa baridi.(Tazama picha chini)
Mwewe ni jamii ya Tai, na ni ndege maarufu wenye rangi ya kahawia na wanapatikana na kuonekana sana maziringira wanayoishi wanadamu. Mwewe naye huruka juu sana, lakini si kama Tai, anapatikana sana sehemu za joto, na chakula chake kikuu ni ndege wengine wadogo wadogo, kama mashomoro pamoja na vifaranga vya kuku. (Tazama picha chini).
Kozi ni Mwewe mweusi, Huyu hana tofauti na Mwewe wa kahawia kitabia, kilichowatofautisha ni rangi tu!, na ukubwa. Kozi yeye kiumbile ni mdogo kuliko Mwewe, na mkia wake ni mfupi. (Tazama picha chini).
Kirukanjia ni aina ya “Bundi” wenye manyoya kama mapembe kwenye vichwa vyao, (Tazama picha chini).
Dudumizi ni aina ya ndege weupe wanaoishi kwenye fukwe za bahari, ambao wana miguu iliyofungamana kama bata, chakula chao kikubwa ni samaki. (Tazama picha chini).
Kipanga ni ndege anayekaribia kufanana sana na Mwewe, isipikuwa yeye kimwonekano ni mdogo, tabia za kipanga ni kama za mwewe, chakula chake ni kama cha mwewe,(yaani kula ndege wengine wadogo ikiwemo vifaranga vya kuku).
Mnandi ni aina ya ndege wanakaribia kufanana na Dudumizi, isipokuwa Mnandi wanaishi kando kando ya maziwa na mito, na chakula chao kikubwa ni samaki kama walivyo dudumizi, na kimwonekano ni wausi.
Mumbi ni bundi mweupe, (Tazama picha chini).
Mwari ni bundi wa jangwani. (Tazama picha chini).
Mderi ni jamii ya Mwewe wanaokula samaki. . (Tazama picha chini)
Korongo ni jamii ya ndege weupe wenye midomo mirefu na miguu mirefu iliyo membamba, wanaishi kando kando ya mito na mabwawa, chakula chao kikubwa ni samaki na nyoka. (Tazama picha chini).
Koikoi ni jamii ya ndege wadogo, wenye sifa ya kusafiri umbali mrefu >Kwa maelezo marefu juu ya ndege hawa koikoi na somo gani wamebeba kiroho fungua hapa>> Koi koi.
Hudi hudi ni aina ya ndege, wenye kichwa kilichochongoka na wenye rangi mbali mbali kwenye manyoa yao..
Hiyo ndiyo orodha ya ndege ambayo Bwana Mungu aliwakata wana wa Israeli wasiwale. Kulikuwepo na wanyama wengine kama Nguruwe, Sungura, ngamia na wengine baadhi, ambao pia wana wa Israeli hawakuruhusiwa kuwala..
Bwana Mungu alitumia tabia za wanyama hao kutaka kufundisha jambo fulani la kiroho, ambalo sisi watu wa agano jipya tumeweza kulielewa, hivyo kwasasa hakuna tena kilicho najisi, vyote vimetakaswa.
Sasa kuelewa ni somo gani lilikuwa nyuma ya viumbe hao, mpaka kufikia Bwana Mungu kuwakataza Israeli wasiwale, unaweza kufungua hapa >>> Je tunaruhisiwa kula nyama ya Nguruwe?
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?
Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?
Hema ya kukutania kama jina lake lilivyo, ni hema iliyotengenezwa mahususi kwaajili ya “kukutania”.
Katika biblia, Musa aliongozwa na Bwana Mungu kutengeneza Hema ndogo maalumu, ambayo kupitia hiyo, Mungu ataweza kukutana na watu wake na kuzungumza nao.
Hema hiyo Musa aliambiwa aitengeneze nje ya kambi, Na haikuwa ya kudumu, bali ya kuhama hama, kwasababu wana wa Israeli walikuwa bado wapo katika safari ya kwenda Kaanani, hivyo ilikuwa ni ya kutengenezwa na kuvunjwa. (Tazama picha juu).
Na mtu yeyote alipokuwa na jambo ambalo anataka kuuliza kwa Bwana, basi alimfuata Musa, na kisha Musa huingia ndani ya hiyo hema kusikia kutoka kwa Bwana.
Hapo awali ni Musa tu, ndiye aliyekuwa na ruhusa ya kuingia ndani ya Hema, baadaye Haruni naye alikuja kupata nafasi ya kuingia, baada ya sheria za kikuhani kuongezwa.
Na Ishara itakayoonesha kuwa Bwana ameshuka juu ya Hema hiyo tayari kuzungumza na watu wake, ni ile Nguzo ya wingu ambayo iliyokuwa inawaongoza wana wa Israeli mchana.
Nguzo hiyo iliposhuka na kukaa juu ya hema basi wana wa Israeli wote walijua Bwana ameshuka na kuna jambo au ujumbe anataka kuutoa. Nguzo hiyo kwa jina lingine iliitwa “utukufu wa Bwana”.
Hivyo uliposhuka huo utukufu basi Musa aliingia ndani ya hiyo hema kusikia Bwana anasema nini.
Mfano utaona wakati Haruni na Miriamu walipomnung’unikia Musa juu ya mke wake wakiMisri , jambo ambalo halikumpendeza Mungu…utaona “Utukufu wa Mungu”, yaani ile nguzo ya wingu ilionekana juu ya hema.
Hesabu 12:1 “Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.
2 Wakasema, Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao.
3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.
4 BWANA akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia,
Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.5 BWANA akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.
6 Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto.
7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?.
9 Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake.
10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.
11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi”.
Pia unaweza kusoma juu ya habari ya Dathani na Kora walipoinuka na kutaka wao ndio wawe viongozi wa mkutano badala ya Musa.
Hesabu 16:19 “ Kisha Kora akutanisha mkutano wote kinyume chao mlangoni pa hema ya kukutania; na utukufu wa BWANA ukatokea mbele ya mkutano wote.
20 Kisha BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja.
22 Nao wakapomoka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?
23 BWANA akasema na Musa, na kumwambia,
24 Nena na mkutano, na kuwaambia, Ondokeni ninyi hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani, na Abiramu”.
Mistari mingine inayozungumzia juu ya hema ya Bwana na utukufu wake huo ni pamoja na Kutoka 40:34, Walawi 1:1, na Hesabu 2:17.
Lakini je hiyo Hema ya kukutania sasa ni wapi?
Hema yetu ya kukutania sasa ni kwenye Neno la Mungu (Biblia), hapo ndipo tutakapoonana na Mungu, tutakaposikia kutoka kwa Mungu,tutakapopata maonyo na faraja. Hapo ndipo penye utukufu wa Mungu.
Hakuna mahali pengine tutakapopata kusikia Sauti ya Mungu, isipokuwa katika Neno lake.
Hivyo hatuna budi kujifunza biblia kila siku.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SWALI: Nini maana ya huu mstari,
Mithali 31:6 “Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake”.
Je tunaruhusiwa kunywa pombe, tunapokuwa katika shida?
JIBU: Kumbuka agano la kale lilikuwa ni agano la mwilini, hivyo walitafuta kila mbinu za mwilini ili kutatua matatizo ya mtu, kwamfano utaona ilikuwa ili kutatua tatizo la zinaa na migororo katika ndoa, waliruhusiwa kutoa talaka, au kuoa wake wengi. Lakini jambo kama hili haukuwa mpango wa Mungu tangu mwanzo.
Mathayo 19:7 “Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi”.
Na ndio maana utaona, japokuwa waliruhusiwa kufanya hivyo, lakini bado tatizo la uzinzi halikutatuliwa lote, kwamfano Daudi alikuwa na wake wengi, pamoja na Masuria wengi, lakini bado hakuacha kwenda kutafuta wake za watu, na kuzini nao (Mke wa Uria). 2Samweli 11&12..Kwasababu kiu ya uzinzi haizimwi kwa kuoa wake wengi.
Vivyo hivyo, Na katika masuala ya kuondoa huzuni, au uchungu moyoni, walikuwa na desturi, kwamba mtu aliye katika hali hiyo, mfano kama kafiwa na watoto wake wote, au mke n.k. kama vile Ayubu Walikuwa wanawapa pombe, wanywe kwa kipindi hicho iwasahaulishe matatizo yao. Lakini hilo halikufanikiwa kwa wakati wote, kwasababu pombe ikiisha tu kichwani, huzuni yake inarudia tena pale pale..kwasababu kiu ya huzuni haiwezi kukatwa kwa pombe..Mungu aliruhusu tu iwe hivyo kwa muda, kwasababu ya mazingira waliyokuwa nayo kwa wakati ule, lakini halikuwa kusudi lake tangu mwanzo.
Na ndio maana sasa katika wakati wa agano jipya Mungu alileta suluhisho la moja kwa moja la mambo yote rohoni na suluhisho lenyewe ni ROHO MTAKATIFU.
Bwana Yesu alisema..
Yohana 7:37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”
Roho Mtakatifu akishaingia ndani ya mtu, anafanya kazi ambayo pombe imeshindwa, madawa ya kulevya yameshindwa, anamwondolea mtu hofu yote, uchungu wote, tamaa yote, wasiwasi wote na mashaka yote, na kiu yote ya uovu milele. Na ndio maana mtu aliyejazwa na Roho Mtakatifu vizuri huwa anaonekana kama mlevi, mtu asiyejali ni nini anakipitia saa hiyo..Kama tunavyoona siku ile ya Pentekoste.
Matendo 2:15 “Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;
16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto”.
Hivyo, sisi hatuna ruhusu ya kunywa pombe, kwasababu ndani ya pombe, biblia inasema upo UZINZI, na matendo mabaya, lakini katika Roho Mtakatifu upo uhuru. Ukinywa pombe unatenda dhambi.
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”
Kwahiyo mstari huo hauhalalishi ulevi, kama tu vile uoaji wa wake wengi usivyokuwa halali sasa, japokuwa uliruhusiwa katika agano la kale.
Tutambue ujumbe wa saa tunayoishi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
JE! ULEVI NI DHAMBI?.
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?
USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.
Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)
Rudi nyumbani
Jibu: Tusome,
Mathayo 11:19 “Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”.
Kabla ya kujua kama Bwana Yesu alikuwa ni mlevi au la!..tujiulize kwanza kama alikuwa kweli Mlafi?.
Kama Bwana hakuwa mlafi basi ni wazi kuwa pia hakuwa mlevi.
Lakini swali la kujiuliza ni kwanini walimwona kama mlafi na Mlevi?
Jibu ni kwasababu muda mwingi alikuwa anashinda na wenye dhambi akiwafundisha.
Kikawaida ukionekana mara kwa mara unazungumza na walevi, au unashinda na walevi, ni rahisi na wewe kuzushiwa ni Mlevi hata kama si mlevi, vile vile unapoonekana mara kwa mara unaingia kwenye nyumba za watu, na wakati mwingine kula nao ni rahisi kuzushiwa ni mlafi.
Sasa Bwana Yesu naye alikuwa ni mtu wa kuzunguka mara nyingi kwenye nyumba za watu, hususani wenye dhambi pale walipomwalika, hivyo hiyo ikamfanya wale wasiomwelewa kufikiri ni mlafi, kufikiri kwamba anazunguka kwenye hizo nyumba kutafuta kula, kumbe Bwana hakuwa anaingia kwenye nyumba za watu kutafuta chakula bali kutafuta roho zao.
Utalithibitisha hilo siku alipokwenda kwa Zakayo mtoza ushuru katika Luka 19:2-8, na alipokwenda kwa Simoni mkoma katika Mathayo 26: 6-13, Na sehemu nyingine zote.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana hakuwa mlevi, kama vile jinsi ambavyo hakuwa mlafi.. Ila alionekana na baadhi ya watu kama mlevi kutokana na jinsi alivyokaa muda mwingi na wenye dhambi, ambao ndani yake wamo walevi…
Lakini hekima yake ilikuwa na nguvu kuliko yao, kwasababu aliwaambia maneno yafuatayo..
Marko 2:16 “Na waandishi na Mafarisayo walipomwona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.
Na sisi hatuna budi, kuiiga hekima ya Bwana Yesu, ya kuwapelekea injili wale wasio na afya, watu walio katika vifungo vya giza walio katika manyumba, walio katika masoko yao ya kujiuza miili yao, walio mahospitalini, mitaani n.k na sio muda wote kudumu kanisani tu!..mahali ambapo tayati kuna nuru, tayari kuna watu wenye afya.
Bwana atusaidie.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?
SWALI:Tunasema Yesu karejesha kila kitu Adamu alichopoteza pale Edeni, Lakini kiuhalisia mbona hajarejesha kila kila kitu, mbona tunaona kifo bado kipo, mbona waovu ndio wanaotawala dunia, mbona magonjwa na ajali vinakithiri duniani?
JIBU: Ni kweli kabisa Bwana wetu Yesu Kristo, amekabidhiwa umiliki wa vitu vyote, Kuanzia juu mbinguni, mpaka huku duniani, vyote vipo chini yake. Na kazi kuu aliyokuja kuifanya ni kuvirejesha vyote vilivyoharibiwa na adui, katika nafasi yake, na hata Zaidi yah apo.
Mathayo 11: 27a Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu;..
Soma pia,
Waefeso 1:20 “…. akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo
23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote”.
Basi kama ni hivyo, utauliza ni kwanini basi, hatuoni mamlaka yake yote yakitimia ulimwenguni?
Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa, Huduma ya Bwana wetu Yesu Kristo haijaishia pale tu alipopaa kwenda mbinguni..bali aliondoka kwa muda tu, akaahidi kurudi, Na ndio maana ujio wake,aliugawanya mara mbili, ambapo mara ya kwanza alikuja kwa lengo la kuokoa roho za watu na mauti, ndipo hapo akalazimika kufa msalabani, ili damu ipatikane kwa ajili ya ondoleo la dhambi. Hivyo kipindi chote hicho hakuhangaika, na mambo yoyote ya mwilini, au ya kiutawala, au ya kijeografia japokuwa alikuwa amekabidhishwa vyote.
Lakini ujio wake wa pili, hautakuwa tena kama ule wa kwanza, wenye lengo la wokovu wa roho za watu..Hapana, bali atakuja mahususi kwa lengo la kuukomboa huu ulimwengu na mifumo yake yote mibovu, Hapo ndipo atakapokuja kama mtawala, yaani MFALME WA WAFALME na BWANA WA MABWANA. Katika ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 19:16)
Sasa atakapokuja katika awamu hii,
1) jambo la kwanza atakalofanya ataleta Amani duniani. Kutimiza lile andiko kwamba siku ile Mbwa-mwitu atalala Pamoja na mwana-kondoo, mtoto anyonyaje atacheka kwenye tundu la nyoka. (Isaya 11:5-9, 65:25)
2) Pili atadhibiti uchungu; Watu hawatazaa t tena kwa uchungu (Isaya 65:23)
3) Tatu atabidhibiti, magonjwa na maajali: Hilo ndilo litakalowafanya watu waweze kuishi miaka mingi hata karibia na 1000. (Isaya 65:20). Biblia inasema kipindi hicho, mtu atayekufa na miaka mia ataitwa mtoto mchanga.
4) Nne atadhibiti uharibifu: Yaani Hutajenga, akakaa mwingine, wala hutapanda akala mwingine..(Isaya 65:22)
5) Tano atadhibiti dhambi: Kumbuka wakati huo shetani atakuwa amefungiwa, na mtu yeyote atakayeonyesha dalili za uvunjifu wa amani, fimbo ya chuma, itamlalia.(Ufunuo 12:5)
6) Na mwisho kabisa atamalizana na MAUTI, huyu ndiye adui wa mwisho.
Kiasi kwamba hakutakuwa na kifo tena ulimwenguni, wala machozi, wala maombolezo.
Hapo ndipo atakamporejeshea Baba mamlaka yote. Na kazi yake itakuwa imekwisha ya ukombozi. Na ndio hapo tutaingia katika ile mbingu mpya na nchi mpya, ambayo Jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.
1Wakorintho 15:24 “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26 ADUI WA MWISHO ATAKAYEBATILISHWA NI MAUTI”.
Hivyo, kwa kipindi hichi tulichopewa hapa katikati, tangu siku alipopaa hadi sasa, ni kuhakikisha kila mmoja, anaupokeo huo ukombozi wa roho yake, kwa gharama yoyote ile. Na hiyo inakuja tu kwa kumwamini Yesu Kristo, na kumpokea Roho wake.
Lakini kama mtu atakutwa katika hali ya dhambi hadi siku anayorudi mara ya pili, ajue kuwa hakuna neema tena ya ukombozi juu yake kwasababu Kristo ameshabadili ofisi. Wakati huo, atawaangamiza waovu wote kwa kuwaua kwa pumzi yake (Ufunuo 19:21). Kisha kwenda kuwatupa katika ziwa la moto.
Hivyo, uovu unaouna leo hii duniani ni wa kitambo tu, vita unavyoviona, uchungu, magonjwa na vifo, vyote vina muda mfupi. Hivi karibu Bwana anarudi, kuja kutawala na sisi kwa muda wa miaka 1000. Ndani ya hichi kipindi kila kitu kitarejeshwa katika hali yake.
Na ndio maana huna sababu ya kukimbizana na huu ulimwengu mbovu, ambao tumezungukwa na hatari ya kila namna, ndugu jiwekee hazina mbinguni, kwenye huo ulimwengu ujao wa amani unaokuja.
Lakini kwa bahati mbaya si wote watapokea neema hii ya kutawala na Kristo. Ikiwa utakufa leo katika hali yako ya dhambi. Utabakia huko huko makaburini hadi siku ile ya ufufuo, kisha uhukumiwe na kutupwa motoni.
Je! Bado unaendelea katika dhambi zako? Bado unaichezea tu hii neema? Kisa Kristo ni mpole sasa kwako unadhani atakuvumilia hivyo katika hali yako ya dhambi milele ? Ndugu yangu. Bwana Yesu Kristo ni mkuu kuliko unavyoweza kufikiri, utalithibitisha hilo, siku ile atakaporudi mara ya pili. Ambapo biblia inasema kila kinywa kitakiri, na kila goti litapigwa. Na mataifa watamwombolezea.
Heri ukampa Yesu Kristo Maisha yako angali bado una muda mchache, hivi karibuni Parapanda italia, Na Kristo atabadili ofisi yake.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
SWALI; Naomba kuuliza katika ufunuo 21:27 kwamba hakitaingia kilicho kinyonge hili neno kinyonge linamaanisha nini? Je ni watu dhaifu mfano vilema?
Ufunuo wa Yohana 21:27
[27]Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
JIBU: “Kinyonge” kinachozungumziwa hapo si mtu mlemavu, kama ingekuwa hivyo Bwana Yesu asingesema..kiungo chako kimoja kikikukosea king’oe ni heri uingie mbinguni mlemavu kuliko kuwa viungo vyako vyote na kuishia kuzimu.(Mathayo 5:29-30)
Lakini kinyonge kinachozungumziwa hapo ni kipi?
Kitu kinyonge sikuzote ni kitu kisichokuwa na nguvu ya kustahimili mtikisiko fulani aidha mapigano,ugonjwa,Dhoruba, mateso n.k.
Vivyo hivyo katika roho mtu asiyekuwa na nguvu ya kuushinda ulimwengu huyo ni sawa na mnyonge. Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya..
Mathayo 11:12
[12]Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Utajiuliza ni kwanini Bwana arejee siku za Yohana mbatizaji, na sio siku za labda, Isaya, au Musa, au Samweli? Bali Yohana Mbatizaji?
Alisema hivyo, ili kutupa picha na sisi tunapaswa tuishi Maisha ya kuukana ulimwengu, mfano wa Yohana mbatizaji..Ambaye biblia inasema Maisha yake yote, aliishi majangwani mbali na ulimwengu, na matokeo yake akawa akiongezeka nguvu rohoni kila siku (Luka 1:80).
Hivyo na sisi tunapaswa tuushinde ulimwengu, ili tuweza kuuteka ufalme wa Mungu, ikiwa uzinzi utatushinda, ikiwa anasa na tamaa za ujanani zitatushinda, basi sisi ni wanyonge, na hivyo, kamwe hatutakaa tuuingie ule mji mpya wa Yerusalemu, utakaoshuka kutoka mbinguni. Kwasababu watakaoingia kule ni watakatifu tu walioushinda ulimwengu, na si vinginevyo.
Huu si wakati wa kuikumbatia dhambi..na kusema kwamba mimi siwezi kuushinda ulimwengu, ni wajibu wako kushindana mpaka ushinde…hupaswi kuwa mnyonge. Kumbuka wewe ukishindwa haimaanishi kuwa mwingine kashindwa.
Lakini tutawezaje kufikia hapo?
Tutafika kwa njia moja tu nayo ni kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi, na kujitwika misalaba yetu na kumfuata Yesu kwa gharama zozote zile.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jibu: Tusome,
Warumi 8:29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza”.
Ni kweli maandiko hapo yanasema Bwana anawajua walio wake tangu asili.
Ili Mungu awe Mungu ni lazima ajue mambo yote, ni lazima aujue mwisho katika mwanzo. Vinginevyo asipojua hivyo, huyo sio Mungu.
Lakini pamoja na kujua hatima zetu wote, bado hajatuambia ni nani ataokolewa na nani hataokolewa. Nafasi ya kuokolewa ipo kwa wote, kadhalika nafasi ya kupotea ipo kwa wote, ni jukumu letu sisi kupambana ili tusijikute tumeingia katika hilo kundi la ambao hawataokoka na kuingia katika ziwa la moto.
Bwana Yesu alijua tangu mwanzo ni Nani atakayemsaliti, na akawaambia mapema wanafunzi wake kwamba mmoja wenu atanisaliti, Lakini hakutaja jina kwamba ni Yuda!. Aliachia hapo katikati, kila mtu ajihisi kama ni yeye, ili lengo kila mtu ajitathmini mienendo yake na ajihadhari na roho ya usaliti.
Lakini Bwana kwa kusema hivyo, hakuacha kuendelea kuwahubiria wanafunzi wake, au hata Yuda na wanafunzi pia waliendelea kuhubiri, kwasababu siri ya atakayemsaliti alikuwa nayo Bwana na sio wao..Hivyo kazi waliyokuwa nayo ni kuendelea na kuhubiri injili, na kujitahidi wasitimize huo unabii…
Marko 14:18 “Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti.
19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi?
20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe”.
Na hata sasa Mungu anatuambia lipo kundi litakalomsaliti, lipo litakaloingia katika ziwa la moto, lakini hajataja majina, hivyo ni wajibu wetu sisi kupambana tusiwe mojawapo ya hao.
Sasa swali tunalopaswa tujiulize kila mmoja wetu ni hili:
Utajuaje kama wewe utaangukia katika kundi la watu ambao wataingia jehanamu ya moto?..
Hautajua kwa tafsiri ya jina lako, wala kwa rangi ya uso wako, wala kwa kimo chako, wala kwa jinsia yako wala kwa kabila ulilotokea au familia uliyotokea.
Bali utajijua kwa tabia zako!. Kama maisha yako bado ni ya dhambi, ya anasa, ya kiulimwengu na uzinzi na uasherati, ya kuabudu sanamu, ya kutokujali mambo ya Ki-Mungu kama Yuda, ingawa unaonywa mara nyingi..basi fahamu kuwa upo miongoni mwa lile kundi lililotabiriwa kutourithi uzima wa milele.
Kadhalika kama upo ndani ya Kristo, na umepokea Roho Mtakatifu, na unayafanya mapenzi yake basi fahamu kuwa upo katika kundi la watu waliotabiriwa uzima wa milele.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba injili tunapaswa tuendelee kuihubiri kama mitume walivyoendelea na kazi hata baada ya kujua kuwa miongoni mwao yupo atakayemsaliti Bwana..zaidi sana tujihadhari na dhambi ili tusiwe miongoni mwa watakaotupwa katika ziwa la moto.
2 Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii,
Bwana awajua walio wake.
Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu“
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo: