Title May 2026

Huduma ya kuendelea kuwa mwaminifu pale wachache wanapokusikiliza.

Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu. 

Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.

Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo,  lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana,  injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..

Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.

Yeremia 7:27

[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. 

Ezekieli 2:3-7

[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. 

[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. 

[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. 

[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. 

[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana. 

Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.

Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.

Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao  sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.

Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.

Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni. 

Mungu akubariki sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

Print this post

MTU WA NNE, ANADHIHIRISHWA KWA MOTO

Shedraki, Meshaki, na Abednego, walipokataa kuisujudia sanamu ya mfalme, kama tusomavyo maandiko, walifungwa na kutupwa kwenye tanuru ya moto,  lakini wakiwa kule motoni, alionekana mtu wa nne, ambaye mfalme Nebukadreza alimwona kama mwana wa Mungu,  ndiye Yesu Kristo mwenyewe.

Danieli 3:24  Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.

Nachotaka ufahamu ni kwamba mtu wa nne, alikuwa Pamoja nao, siku zote, lakini kufunuliwa machoni pa watu, ilihitaji moto, ikiwa na maana nje ya moto, hakutambulika Dhahiri machoni pa wengi, bali kwa wale tu waliomwamini, tena mioyoni mwao.

Moto ni nini?

Moto, ni shinikizo lolote juu ya Imani ya mtu kwa Yesu Kristo, ambalo wakati mwingine  linahatarisha hata maisha yake. Huu moto wengi wanaukwepo lakini hawajui kuwa ndio unaompa Kristo nafasi ya kujifunua zaidi kwenye maisha yako.

Ukiona unataka kufukuzwa kazi kisa, siku za jumapili huwendi kazini unahudhuria ibadani, fahamu kuwa Kristo anaumbika Dhahiri kwenye maisha yako.

Ukiona unahatarisha biashara yako, kisa umegoma kula rushwa, ndivyo Kristo anakwenda kuonekana Dhahiri kwenye kazi zako, ni jambo tu la muda..

Ukiona, unafukuzwa, unapigwa, unafungwa, kwasababu ya msimamo wako mkali wa kimafundisho unaokemea dhambi, ujue kuwa, Kristo anakwenda kusimama na wewe kwa viwango vingine vya juu sana.

Moto kimsingi si mzuri, upitapo ni lazima utasikia maumuvi, lakini mbele ya Kristo, hauna nguvu, hivyo vitisho, mapigo, vifungo, dhihaka, havina nguvu yoyote, kwasababu yeye yupo Pamoja na wewe muda huo, ndivyo ilivyokuwa kwa Shedraki, Meshaki na Abednego, hawakuungua kwasababu ya ule moto.

Badili fikra zako, badala ya kuhuzunika kwa majaribu, Bwana anasema furahi, kwasababu huko ndipo viwango vyetu vya kumuona Kristo vipo.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Mungu azungumze na Ayubu kupitia upepo wa kisulisuli (Ayubu 38:1)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

USIYAKUBALI MARADHI YA MISRI

Print this post

Je ni kweli Mungu haangali utu wa nje katika kumpatia mtu haki au hukumu?.

Swali: Katika 1Samweli 16:7 tunasoma, MUNGU anamwambia nabii Samweli kuhusu mtu atakayempaka mafuta kama Mfalme katika nyumba ya Yese, kwamba yeye haangalii uso kama wanadamu wanavyoangalia.


Jibu: Turejee..

1Samweli 16:6 “Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.

7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, USIMTAZAME USO WAKE, WALA UREFU WA KIMO CHAKE; KWA MAANA MIMI NIMEMKATAA. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; MAANA WANADAMU HUITAZAMA SURA YA NJE, BALI BWANA HUUTAZAMA MOYO”.

Andiko hili linalenga MAUMBILE ya ASILI ya Mtu, kwamba hayo ndio MUNGU hayaangalii kama kipimo cha kumpatia mtu “haki” au “hukumu”, na mambo hayo ni kama rangi ya mtu, urefu, ufupi, ulemavu, au uzima..

Mambo hayo hayatutofautishi sisi kwa sisi mbele za MUNGU. Kwamba ukiwa mfupi au mrefu au mweupe au mweusi basi ndio unaweza kupata kibali mbele za MUNGU. La!, hayo ni mambo ambayo MUNGU hayaangalii kabisa..

Lakini jinsi tunavyoiweka miili yetu, na kuivisha na kuilisha na kuinywesha ni vitu ambavyo MUNGU anavitazama sana kwasababu vipo ndani ya uwezo wetu, lakini urefu na ufupi hakuna mtu anajipangia, ni maumbile ya asili ya MUNGU mwenyewe.

Kwahiyo mtu anapovaa mavazi ya jinsia nyingine, au yanayouchora mwili wake, hayo yanajalisha sana mbele za MUNGU (1Timotheo 2:9, Kumbukumbu 22:5), au mtu anapojichubua au kujichora mwili wake Mungu anatazama (Soma Walawi 19:28).

Kwahiyo Bwana MUNGU, aliposema Haangalii uso, maana yake hashawishwi na maumbile ya asili  ya mtu. Je umempokea YESU?. Una hakika YESU akirudi leo utakwenda naye?.

 Kama bado haujampokea YESU unasubiri nini? Mwamini leo na ubatizwe kwa maji na kwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Print this post

AU NATAKA KUWAPENDEZA WANADAMU?

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa   tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”

Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchikiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.

Ni kufanya jambo ili machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.

Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.

Mathayo 6:2,5

[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…

[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

Ni hali mbaya sana, Mahali  pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..

Yohana 12:42-43

[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.

Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kabisani.

Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana wa Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)

Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.

Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukwana, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.

Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.

Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.

Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

Print this post

KUWEKA MAMBO MOYONI, NI TABIA YA MARIAMU.

Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.

Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.

Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingi kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kawaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…

Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;

Luka 1:28-29

[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. 

[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? 

Luka 2:17-19

[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. 

[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. 

[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake. 

Luka 2:48-51

[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. 

[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 

[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. 

[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake. 

Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi mwake sio kwa akili zake…

Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.

Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…

Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.

Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.

Halidhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..

Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..

Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.

Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.

Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…

Hayo ndio mambo ya kubeba..

Geuka fikiri kama Mariamu.. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.

MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

Print this post

NI LAZIMA KUENDELEZA UTAKASO.

Utakaso wa ndani ni jambo endelevu.. hakuna hatua ambayo mtu amefika na kusema hapa sasa nimekamilika na sihitaji tena kujitakasa.. hakuna, lakini Biblia inatufundisha kuwa ni lazima tujitakase utu wetu wa ndani na kuwa wapya siku baada ya siku.

2Wakorintho 4:16 “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, LAKINI UTU WETU WA NDANI UNAFANYWA UPYA SIKU KWA SIKU”.

Na tena katika Ufunuo, maandiko yanasema “Mtakatifu na azidi kutakaswa (Ufunuo 22:11)”

Sasa tunahoji kama Mtakatifu ameshakamilika kuna haja gani tena ya kuendelea kutakaswa?..Umeona?.. maana yake mtakatifu ni lazima aendelee na utakaso, ijapokuwa anaitwa “Mtakatifu” hakuna mahali atafika na kusema sasa nimekamilika..

Kila hatua ya usafi tunayoifikia inatufungua macho kuona uchafu mwingine uliopo ndani, na tunashughulika na huo, na mwingine na mwingine..mpaka siku ya ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).

Sasa twende mbele zaidi kuangalia vitu gani vinavyomtakasa mtu.

    1. ROHO MTAKATIFU.

Roho Mtakatifu ndio sabuni ya kwanza ya kuondoa uchafu ndani ya Mtu ndio maana kuna umuhimu sana wa Mtu kupokea ujazo wa Roho Mtakatifu baada ya kuamini.

1Petro 1:2 “kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika KUTAKASWA NA ROHO, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu”.

Soma pia 1Wakorintho 6:11 na Warumi 15:16.

Kanuni ya Ujazo wa Roho Mtakatifu ni ile tunayoisoma katika Matendo 2:37-38, yaani kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na ubatizo wa maji mengi kwa jina la Bwana YESU.

    2. NENO LA MUNGU

Maneno ya MUNGU yaliyoandikwa ndani ya kitabu ya Biblia ndio sabuni ndio sabuni ya pili kumtakasa mtu maisha yake. Bwana YESU alisema, tunatakaswa na kweli ya Neno la MUNGU.

Yohana 17:17 “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli”.

Soma pia Waefeso 5:26..

Mtu mwenye desturi ya kusoma Neno la Mungu ni lazima kila siku atakuwa anayaona makosa yake, lakini mtu asiyesoma Neno la Mungu kila siku atajiona yupo sawa na hahitaji kujitakasa wala kurekebishwa. Kwanini? Kwasababu Neno la Mungu ni kama kioo, mtu huwezi kujua uso wako upoje kama hujitazami kwenye kioo (Yakobo 1:22-23).

   3. MAOMBI.

Maombi yanatakasa utu wa ndani katika kiwango kikubwa sana.. na si tu utu wa ndani bali vitu vyote pia..

1Timotheo 4:5 “kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba”.

Kiwango cha mtu kukua kiroho pia kinapimwa na kiwango cha Maombi, mtu anayeongeza viwango vyake vya maombi kila siku ni mtu pia anayekua kiroho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je ni kweli malipo ni hapa hapa duniani?

Swali: Je ni kweli malipo ya watu wote ni hapa hapa duniani?

Jibu: Turejee Mithali 11:31, tutapata mwanga wa swali letu..

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi zaidi?”

Ndio madhara ya makosa yote yanaanzia hapa hapa duniani, kabla ya kufa.. Kwamfano, Neno linasema “waheshimu baba yako na mama yako upate siku nyingi na za heri za kuishi duniani (Kutoka 20:12)”.

Sasa mtu ambaye hawaheshimu wazazi wake wala kuwatii, yeye ni kuwadharau na kuwatukana, mtu huyo ataanza kulipwa hapa hapa duniani kwa kupunguziwa miaka yake ya kuishi, na sio tu miaka ya kuishi, bali pia na ya Kheri, na sio hiyo tu bali na dhambi nyingine zote, kama wizi, au uzinzi hukumu yake inaanzia hapa hapa kama mtu haQtapigwa kwa maradhi basi atapigwa kwa roho za mapepo kwani uzinzi unaunganisha nafsi za watu.

Kwahiyo utaona ni kweli, adhabu ya waovu, inaanzia hapa hapa duniani, lakini hiyo bado haimaanishi kuwa baada ya kifo hakutakuwa tena na adhabu..La! Biblia inatufundisha kuwa hata baada ya kulipwa duniani bado kuna hukumu nyingine baada ya kifo ya ziwa liwakalo moto kwa mtu mwovu.

Kwa namna gani? Tusome maandiko yafuatayo..

Ufunuo 22:8 “Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo”.

Umeona?.. Kwahiyo kama mzinzi akipigwa na maradhi kutokana na uzinzi alioufanya na akafa bila kutubu, ijapokuwa kateseka duniani na maradhi, bado tena ataenda kuteseka na adhabu ya ziwa la moto, hata watu wa Sodoma na Gomora Biblia inatuonyesha kuwa watahukumiwa tena siku ya mwisho ingawa tayari walishachomwa duniani  (Soma Mathayo 10:145).

Ikifunua kuwa dhambi si ya kuchezea kabisa, ina madhara hapa duniani, na kule kwenye maisha ya baada ya kifo.

Upo usemi ya kwamba, Mungu atawapunguzia adhabu wale waliokufa katika dhambi ikiwa walidhurika wakiwa duniani, nataka nikuambia, dhambi ina matokeo makubwa kote kote, huku duniani na baada ya kifo.

Tunafundishwa kuikimbia dhambi, Sasa labda unajiuliza utaikimbiaje?.. Utaikimbia kwa kuanza kujitambua kuwa wewe ni mwenye dhambi na umemkosea MUNGU, baada ya hapo unachukua hatua ya kuungama, yaani kuomba toba kwa makosa yako yote, kwa kumaanisha kabisa.

Baada ya hapo, hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na Roho Mtakatifu atashuka juu yako kukutia muhuri wa milele. Kupitia Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako utaona mabadiliko ya kimaisha na kiutendaji ndani ikiwa kama hutamzimisha kwa kurudia dhambi kwa makusudi na kuacha kukusanyika na wengine.

Lakini kama utazingatia kuhudhuria vipindi vya Neno la Mungu na maombi ya pamoja, Roho Mtakatifu atakaa na wewe na hapo utakuwa umekamilisha hatua yako ya kuikimbia dhambi.

Bwana atusaidi.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

Ipi tofauti ya Hasira na Ghadhabu ya MUNGU?.

MALIPO YA UPOTEVU.

Ni kwa namna gani YESU KRISTO atawahukumu walio hai na waliokufa?

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Print this post

KUFAHAMU SIO KUJUA

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..

Ipo tofauti kati ya “kufahamu jambo” na “kulijua jambo”.. Unaweza kulifahamu jambo lakini usilijue kwa undani, vivyo hivyo kuna tofauti ya “kuyafahamu maandiko” na “kuyajua maandiko”.  Hivi ni vitu viwili vyenye tofauti kubwa sana, hebu tujifunze kidogo kwa namna gani.

Tusome habari ifuatayo kisha tufafanue..

Mathayo 22:23 “Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,

24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.

25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.

26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.

27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.

29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Nataka tuzingatia hilo neno “MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU”.

Kumbuka hawa watu waliokuja kumwuliza Bwana hilo swali ni MASADUKAYO, ni watu wa dini, wanayoyafahamu maandiko karibia yote ya kwenye torati, na hapa wanamjia YESU kwa swali linalotoka katika maandiko ya MUSA (torati), wakisema “Mtu akifa basi mke wake anaruhusa ya kuolewa na ndugu wa karibu”.. jambo ambalo ni kweli kabisa lipo kwenye Biblia.

Lakini pamoja na kwamba walikuwa wanayafahamu hayo maandiko, bado Bwana YESU anawaambia “Hawayajui maandiko” na tena wanapotea sana.

“29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU.

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.

Tuirudie tena habari hii katika Marko..

Marko 12:24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO wala uweza wa Mungu?

25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni.

26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?

27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana”.

Kumbe wakati ambao wanajidhania kuwa wanayajua maandiko kwa wingi wa mistari wanayoifahamu vichwani mwao, Kristo alikuwa anawaona hawajui chochote, na hiyo ndio sababu kuu ya kupotea kwao, hawayajui maandiko bali wanayafahamu tu.

Ndugu hatupaswi kuwa kama compyuta au simu ambao inaweza kuwa na vitu vingi pamoja na biblia nzima, lakini haiyajui maandiko, na wala yale maandiko hayaisaidii kwa chochote.

Hatupaswi kuwa na idadi kubwa ya mistari vichani ambayo haina ufunuo wowote. Mistari yenye nguvu na ibilisi anayoigopa ni ile iliyopo moyoni iliyobeba ufunuo, maana yake yenye uhai katika maisha ya mtu, na inayomwongoza, na yenye nguvu, na inayothibitisha imani.

Masadukayo walikuwa wanafahamu tu Musa kasema, na kujitamba katika hayo, pasipo kujua kuwa andiko bila ufunuo ni bure..

Sasa swali ni je!, tutayajuaje maandiko badala ya kuyafahamu tu?

Kinachotangulia ni kuyafahamu, ni lazima tuyafahamu na kufahamu kunakuja kwa kuyasoma au kuyasikia yanaposomwa.. baada ya kuyafahamu hatua inayofuata ni kuyajua. Na njia pekee ya kuyajua maandiko ni kwa kupitia Roho Mtakatifu..

Huyu peke yake ndiye anayeweza kutuhamisha kutoka katika kuyafahamu maandiko mpaka kuyajua, kwani anapoingia ndani ya Mtu, anakuwa ni Mwalimu mwingine wa ziada, kukufundisha maana za ndani ya maandiko uyasomayo, anakuchambulia na kukufundisha mambo ambayo hata ukirudia kusoma tena hilo andiko ulilolisoma utaona kama vile ni jingine kabisa, na huo ndio uhudumu wa agano jipya unaotajwa katika 2Wakorintho 3:6, ambao unatutosheleza.

2Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.

Je tayari umempokea Roho Mtakatifu?.. kama bado mwamini YESU na tubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO, baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukaa na wewe siku zote, kwani ahadi ya Roho Mtakatifu ni kwa kila mtu.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

Ipi tofauti ya “Majibu” ya Maombi na “Majaribu”.

Ipi Tofauti ya Agano jipya na Agano la Kale?.

TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?

Nini tofauti kati ya kileo na divai ?

Print this post

Je watu watu wasio haki hawatahukumiwa kabisa kulingana na Zaburi 1:5?.

Swali: Turejee…

Jibu: Zaburi 1:5 “Kwa hiyo wasio haki HAWATASIMAMA hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki”.

Andiko hili halimaanishi kwamba wasio haki (yaani watu waovu) hawatasimamishwa siku ya hukumu, La! haimaanishi hivyo, bali kinyume chake inamaanisha “watasimamishwa” lakini hawataweza kujitetea wala kushinda hukumu.

Neno “kusimama” linamaanisha “kushinda au kufanikiwa”… kwahiyo Wasio haki wote watahukumiwa, na sehemu nyingine nyingi katika maandiko zinathibitisha hilo..

2Petro 2:9 “basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, NA KUWAWEKA WASIO HAKI KATIKA HALI YA ADHABU HATA SIKU YA HUKUMU;

10  na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka”.

Ni njia moja tu mtu anaweza kuitumia kuepuka hukumu ya MUNGU, nayo ni Kumwamini Bwana YESU KRISTO na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu (Marko 16:16).

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; WALA HAINGII HUKUMUNI, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kwa namna gani YESU KRISTO atawahukumu walio hai na waliokufa?

Je biblia inajichanganya kwa habari ya hukumu ya Mungu (Yohana 12:47 na Yohana 5:22, 27).

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Nini maana ya Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma?

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Print this post

Je! Hayo Mambo ya duniani na ya mbinguni ni yapi?

Yohana 3:12

[12]Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni? 

SWALI: Je! Hayo Mambo ya duniani ni yapi? Na hayo mambo ya mbinguni pia ni yapi Yesu aliyoyamaanisha?


JIBU: Ukianza kusoma tokea vifungu vya juu utaona sababu ya Bwana Yesu kusema maneno hayo, ni baada ya yule Nikedemo mkuu wa mafarisayo kumfuata usiku ili kumuuliza maswali, lakini Yesu akamjibu kwa kumwambia kuhusu habari za kuzaliwa mara ya pili, lakini jambo hilo likawa gumu sana kwa nikodemu kulipokea…akamweleza Bwana yawezekanikaje mambo hayo? …Ndipo Yesu mwishowe akayasema maneno hayo;

12]Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni? 

Sasa hapo hamaanishi alikuwa anafundisha mambo ya duniani, hapana…bali alikuwa anatumia mifano ya duniani kueleza yale ya rohoni ili iwe rahisi watu kuelewa..kwamfano hapo alitumia mifano ya mtu kuzaliwa, vilevile akatumia mifano ya tabia ya upepo kumfafanulia Nikodemu aelewe mtu wa rohoni naye anavyopaswa awe…mahali pengine alitumia mifano ya wakulima, wafanyabiashara, maharusi, wavuvi, wafalme. wanyama n.k.

Ilikufundisha ufalme wa Mungu ulivyo na unavyofanya kazi..

Lakini mambo ya mbinguni ni yale ambayo hayana uhalisia na maisha yetu ya duniani kabisa…mambo hayo huwezi yaeleza kwa mifano ya kidunia..Hivyo ni kuyapokea tu kwa imani.

Kwamfano jinsi gani hekima ya Mungu isipopatikana popote isipokuwa ndani ya Yesu Kristo. Na jinsi gani Mungu aliumba ulimwengu kwa kupitia Kristo, ambaye alikuja kama mwana aliye Mungu yuleyule (Yohana 1:1-4).

Mambo hayo hayakuweza kusadikika kwa hekima za kibinadamu, ndio maana yalifichwa yakaja kufunuliwa baadaye kwa Roho Mtakatifu kwa mitume kuwa ndiye Mungu mwenyewe katika mwili( 1Timotheo 3:16)

Ndio maana wayahudi na hata watu wengine leo hii wa dini wanashindwa kuelewa iweje Mungu awe na mtoto, wakati hana mshirika…halafu huyo huyo mtoto awe ndio yeye tena.

Jambo kama hili halina mifano ya kibinadamu ya kujitosheleza kuelezea, ni kuamini tu!…lakini kwa imani waziona kazi zake na kujua hakika Kristo ndiye Mungu mwenyewe bila tashwishwi…Hivyo amini tu, uelewa kamili utaufahamu ufikapo mbinguni, ni sawa na Yesu alivyomwambia Nikodemu upepo huvuna upendako, hujui utokako vilevile hujui uendako, lakini sauti yake waisikia…ndivyo ilivyo katika asili ya uungu wa Mungu.. Tunamjua Kristo kuwa ni Mungu kwa kazi zake kuu na timilifu juu ya maisha yetu.. 

Ni nini Bwana anataka wewe ujue.

Sehemu kubwa ya mambo yanayotuzunguza yanahubiri habari za ufalme wa mbinguni. Kama hatutaelewa kwa kuitafakari mifano hii, kamwe tusidhani tutaelewa yale yasiyoingia maanani kabisa tuyasikiapo.

Je! Umempa Yesu maisha yako? Kumbuka hizi ni siku za mwisho na Yesu amekaribia kurudi, unasubiri nini usiokoke?

Tubu sasa upokee uzima wa milele. Ikiwa unahitaji msaada huo wa kuokoka basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba na ushauri.

+255789001312 / +255693036618

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.

Print this post