Turejee..
Yohana 13:1 “Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo”.
“Upeo” ni kiwango cha mwisho cha Jambo… Kwamfano ukitazama juu, upeo wa macho yako unaishia kuona nyota zaidi ya hapo huoni kingine.. kwahiyo tunaweza kusema upeo wa kuona kwetu angani ni nyota..
Vile vile tunapofikiri kumhusu MUNGU, (kwa namna gani hana mwanzo wala mwisho) tunafikia kikomo cha kufikiri, tunafika mwisho wa Upeo wetu wa kufikiri (hatuwezi kufikiri zaidi ya hapo na kupata majibu).. na mambo mengine yote yana upeo wake..
Sasa hapa Bwana YESU aliposema kuwa “aliwapenda watu wake Upeo”.. maana yake alitupenda kiwango cha juu kabisa cha UPENDO, ambacho baada ya hicho hakuna kingine…
Upendo wa YESU kwetu ni MKUU mno, kina cha upendo wake, urefu wa upendo wake, mapana mapana ya upendo wake na kimo cha upendo wake hakielekezeki..
Waefeso 3:18 “ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina; 19 na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu”.
Waefeso 3:18 “ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;
19 na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu”.
Mahali pengine anasema hivi..
Yohana 5:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake”.
Ni rahisi mtu kuutoa uhai wake kwaajili ya mtoto wake, au mzazi wake au ndugu yake yoyote wa damu, lakini ni ngumu mtu kuutoa uhai wake kwaajili ya Rafiki.. Kwasababu marafiki hawatabiriki, leo anaweza kuwa rafiki yako kesho msaliti wako, na adui..
Mtu anaweza kutoa msaada kwa rafiki yake lakini si UHAI, na mtu kama huyo akitokea basi upendo wake ni mkubwa sana!… na hapa Bwana YESU anajitaja yeye, kwamba anautoa uhai wake kwaajili ya rafiki zake, na tena si rafiki mmoja, bali wengi, ijapokuwa anajua kuwa katikati ya marafiki wapo wanafiki na wasaliti, lakini anautoa uhai wake kwaajili yao wote.. hakika huo ni UPEO wa mwisho kabisa wa Upendo.
Biblia inasema mtu ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe..lakini YESU ametufanya sisi kuwa rafiki zake na ametupenda kuliko ndugu.
Mithali 18:24 “Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; LAKINI YUKO RAFIKI AAMBATANAYE NA MTU KULIKO NDUGU”.
Neno la Mungu linazidi kutufundisha juu ya huu UPEO WA UPENDO WA YESU, kuwa hakuna chochote kilichopo duniani, wala kilichopo mbinguni, wala mahali pengine popote kitakachoweza kutuondolea Upendo wa YESU kwetu,.. YESU mwokozi ataendelea kutupenda na hakuna mtu atakayetuchonganisha naye..
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. 34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. 35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? 36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. 37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. 38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.
37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Sasa kama tunapendwa kwa upendo mkuu namna hii kwanini na sisi TUSIPENDEKEE??…Kwanini tusiitikie vyema huu upendo kwa kumpa yeye maisha yetu, na muda wetu na mioyo yetu?..
Utajibu nini siku ile, utajiteteaje siku ile, kama leo ukiudharau upendo huu mkuu?.. Ni heri ukampokea YESU leo kama bado hujafanya hivyo, kwa kutubu na kupokea Roho Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.
JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA?
UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;
JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?
NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?
Print this post
Yohana 11:44
[44]Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.
Nakusalimu Katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Nataka tujifunze jambo moja Kwa Lazaro aliyefufuliwa…
Kama tunavyojua mtu huyu alikufa, akazikwa na akaoza pia..lakini Bwana Yesu alipofika kaburini Alifanya muujiza mkubwa wa kumfufua.
Na kweli Lazaro alitoka kaburini akiwa mzima kabisa bila shida yoyote…Lakini wengi wetu tunaishia hapo, na kusema Bwana Ametenda muujiza…Lakini Yesu alipomwangalia aliona bado akatoa agizo akisema mfungueni mkamwache aende zake.. Maana yake ni kuwa ufufuo, ulimpa uzima kweli lakini sio uhuru..
Ilihitaji afunguliwe, maana kaburi lilimfunga mikono yake, miguu yake pamoja na uso wake…hata alipofufuka bado liliacha mizizi yake kwa mtu.
Ufufuo unafananishwa na wokovu, Mtu anapomwamini Yesu anakuwa tayari amefufuka kutoka katika wafu…lakini hilo peke yake halitoshi, bado Anakuwa na kamba za makaburini (maisha ya kale), hivyo anapaswa afunguliwe…
Ukiokoka haimaanishi, tabia za kale zote zitaondoka siku hiyo hiyo, unahitaji kukubali kufunguliwa, ili uwe huru kwelikweli..
Sanda, zilizomzinga Lazaro, uso wake, miguu, mikono, kama wavu wa bui-bui, hutembei, Hushiki wala huoni…ndio maisha Ya wakristo wengi baada ya kuokoka yalivyo..
Zile tabia za kale wanaendelea nazo, uchungu, wivu, hasira, uadui, maumivu, vinyongo, hofu, wasiwasi, wanashindwa kuendelea mbele kwasababu hawatoi nafasi ya kufunguliwa…
Angalia hapo Bwana Yesu anasema..”Mfungueni, mkamwache aende zake…”
Hasemi jifungue…bali mfungueni…yapo mambo huna budi kukubali kusaidiwa ili upone..
Ndio hapo Mungu akaweka…Kanisa.
Ambapo..
Utakutana na wachungaji.. kukusimamia na kukulisha mpaka utakapokomaa Na kukua vizuri kiroho…kuishi bila kanisa yaani mwenyewe mwenyewe tu, ni sawa na kutembea na sanda lako,
Kumbuka Bwana anatarajia umzalie matunda mara baada ya wokovu wako…yapo majukumu ya kufanya baada ya kuokoka..lakini ikiwa miguu na mikono na uso umefungwa unatarajia nini hapo?
Kubali kufundishika, Kubali kuchungwa, kubali mashauri na kuonywa, kubali kuombewa, kubali kuishi na ndugu (katika Bwana), kubali kusoma Neno, kuomba na wenzako utafunguliwa sana.. zaidi ya kuridhika tu na wokovu ulioupokea ukidhani utazalisha chochote katika hali hiyo hiyo ya kiroho ambayo upo peke yako peke yako.
Mara nyingine hata maono yako huwezi kuyafikia kwasababu umefungwa miguu yako. usisonge mbele.. Ogopa sanda, kama vile unavyoogopa mauti.
Ukijiona una tabia ambazo haziendani Na hali mpya ya wokovu ulioupokea basi ndio wakati wa kushughulika na sanda lako, kwa kutii na kufuata hayo maagizo. Jiwajibishe, tendea kazi wokovu Wako, kwasababu kila mtu anawajibu wa kufanya hivyo.
Hofu ya Bwana ni nini? (2Wakorintho 5:11)
Sheria ya uhuru ni ipi? (Yakobo 2:12)
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
WhatsApp
Jibu: Turejee..
1Wakorintho 9:27 “BALI NAUTESA MWILI WANGU na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.
Kuutesa mwili kunakozungumziwa hapa si kujiumiza kwa viboko na mapigo… bali ni kuuzuia mwili kupata vitu viupendavyo, ili makusudi kutimiza mapenzi ya MUNGU.
Mfano wa vitu ambavyo vikizidi sana kufanyika katika mwili vinaathiri mbio za kiroho ni pamoja na VYAKULA NA USINGIZI vipo na vingine vingi lakini hivi ndio vikuu..
1. VYAKULA
Kula kila wakati kwa kipindi kirefu bila kuwa na vipindi vya KUFUNGA kunaathiri ukuaji wa kiroho na kuna mambo ambayo hayatatokea, kwani Biblia imesema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba..
Mathayo 17:19 “Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa? 20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. 21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA.]”
Mathayo 17:19 “Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [LAKINI NAMNA HII HAITOKI ILA KWA KUSALI NA KUFUNGA.]”
Kwahiyo Mtu mwenye desturi ya kufunga mara kwa mara na kuomba anakuwa anautesa mwili wake lakini anakuwa anapata faida kubwa rohoni
2. USINGIZI.
Mtu anayejizuia kulala kwa lengo la kuutafuta uso wa Mungu kwa Maombi, pia anahesabika kuwa anautesa mwili, na faida yake pia ni kubwa..
Marko 14:37 “Akaja akawakuta wamelala usingizi, akamwambia Petro, Je! Simoni, umelala? Hukuweza kukesha saa moja? 38 Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu”.
Marko 14:37 “Akaja akawakuta wamelala usingizi, akamwambia Petro, Je! Simoni, umelala? Hukuweza kukesha saa moja?
38 Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu”.
Na mwisho kumbuka, kujizua kufanya dhambi kama uzinzi, ulevi, sio kuutesa mwili, bali ndio kuupa mwili pumziko..kwasababu dhambi ni sumu ya mwili pia, dhambi inauharibu mwili… Mtu anapojizuia kutenda dhambi katika mwili, mwili wake hauteseki badala yake ndio unajengeka zaidi, kwahiyo usichanganye kutotenda dhambi na kuutesa mwili.
Ukiona dhambi kama Ulevi au Uzinzi au nyingine yoyote inakufanya mateka, kiasi kwamba usipoifanya mwili wako unateseka basi ni dalili ya kuwa bado utakaso kamili haujaingia maishani mwako, hivyo ni wakati wa kumgeukia Bwana kwa moyo wote kwa kutubu, kubatizwa kwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU na kisha kupokea Roho Mtakatifu,
Na ile sheria ya Roho wa uzima itakuweka huru mbali na dhambi, BUREEEEE kabisa..
Warumi 8:2 “Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti”.
Bwana atusaidie tuitese miili yetu kwa kufunga na kuzuia usingizi, ili tupate muda wa kukesha na kuomba kwa faida ya roho zetu.
TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!
Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)
SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.
Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?
Swali: Hofu ya Bwana inayotajwa katika kitabu cha 2Wakorintho 5:11, ni hofu ya namna gani?
2Wakorintho 5:11 “Basi tukiijua HOFU YA BWANA, twawavuta wanadamu; lakini tumedhihirishwa mbele za Mungu. Nami natumaini ya kuwa tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia”.
“Hofu ya Bwana” au “Hofu ya Mungu”.. Ni hali ya kuhofia Hukumu ya Mungu ijayo..
Tukianzia mstari wa juu kidogo katika maandiko hayo tunasoma kuwa kila mtu itampasa kusimama mbele ya kiti cha hukumu na kupokea malipo ya kazi yake.
2Wakorintho 5:9 “Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye. 10 Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”.
2Wakorintho 5:9 “Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye.
10 Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”.
Na mahali pengine Biblia inasema kila atatoa habari zake mwenyewe..
Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”.
Hivyo hiyo hali na kutafakari mambo yajayo, kwamba tutasimama mbele ya kiti cha hukumu, inazaa hofu, na hofu hiyo ndio ijulikanayo kama “Hofu ya Bwana” au “Hofu ya Mungu”.. Na wakati mwingine hofu hii haimpeleki mtu kuogopa hukumu ijayo baada ya kifo, bali hata akiwa hai, kwasababu pia Mungu anaweza kumhukumu mtu bado akiwa hai, kwa kuruhusu madhara yampate.
Mfano wa watu katika maandiko walioonekana kuwa na Hofu ya Mungu, ni Yule mnyang’anyi aliyeangikwa msalabani pamoja na Bwana.
Luka 3:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. 40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, WEWE HUMWOGOPI HATA MUNGU, nawe u katika hukumu iyo hiyo? 41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. 42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako”.
Luka 3:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, WEWE HUMWOGOPI HATA MUNGU, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako”.
Na mfano wa Mtu/Watu katika maandiko waliotajwa kukosa Hofu ya Mungu kabisa ni wale watu wa Sodoma na Gomora na wenyeji wa nchi ya Gerari..
Mwanzo 20:10 “Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili? 11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu”.
Mwanzo 20:10 “Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?
11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu”.
Na sisi ni lazima tuwe na “Hofu ya Mungu” siku zote, ili tuikwepe huku ya Mungu..kwani madhara ya kukosa hofu ya Mungu ni makubwa.. Tukiwa na hofu ya Mungu ndani yetu, tutajitenga na dhambi kwa namna yoyote ile.
Bwana atusaidie.
Nyakati za Mwisho na Tumaini la Utukufu kwa Mwamini Mpya
IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?
SWALI: Sheria ya uhuru ni ipi inayozungumziwa na mtume Yakobo kulingana na maandiko?
Yakobo 2:11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. 12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.
Neno hili pia utaliona likitajwa na mtume Yakobo katika vifungu vingine vya juu.
Yakobo 1:25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.
Katika biblia zipo sheria kuu mbili
Sheria ya dhambi na mauti ndio ile ya torati, ambayo kazi yake kubwa ni kufichua uovu, kushtaki makosa, lakini haimfanyi mtu kuwa huru, kwa mfano sheria inasema usizini, mtu atakataa kuzini, sio kwasababu hapendi uzinzi, lakini kwasababu sheria imesema tu hivyo, anaogopa adhabu atakapotenda hiyo dhambi atauawa.
Lakini sheria ya Roho wa uzima, ni sheria ya Mungu, isipokuwa hii mtu anavuviwa na Roho Mtakatifu, nguvu ya kuishi sawasawa na matwaka ya Mungu, bila shuruti Fulani, ni ya uhuru. Mfano labda sheria inasema usiue, mtu haui sio kwasababu sheria imesema, lakini kwasababu moyoni mwake hiyo nia, tamaa, au kiu ya kuua haipo, hivyo hata kama sheria isingesema hilo jambo lisingekubalika ndani yake, Hivyo mtu kama huyu tunasema ni huru na sheria, hayupo ki-sheria, sheria haimtawali ijapokuwa sheria yenyewe ipo.
Mtu akishaokoka, anakutana na sheria mpya ya Mungu, ambayo hiyo ni lazima ifuatwe na ishikwe, lakini inakuwa ya uhuru, sio tena ya kifungo, kwasababu Roho Mtakatifu anamsaidia huyo mtu kuiishi..
Ndio hiyo inayoitwa sheria ya uhuru, kwenye kitabu cha Yakobo.
Maana yake ni nini? Sisi kama waamini, Mungu anatarajia tuonyeshe matunda ya Imani yetu katika upendo, huruma, na matendo mema, kwasababu tunaye Roho.
Hivyo inapotokea, hayo hayaonekani, sheria itatuwajibisha, kutuhukumu, au vinginevyo hatukupokea sheria hiyo ya uhuru.. Ni sawa, na mtu aende kuua watu ovyo bila sababu yoyote,
Mtu huyu atahukumiwa, sawa tu na yule ambaye amesukumwa na sababu fulani, labda kisasi, hasira, wivu, chuki n.k.,
Hivyo sisi waamini, tulipokuwa huru na dhambi, hatupaswi kufikiri kuwa ndio tuna uhalali wa Kutenda dhambi. Kinyume chake, tujue kuwa ipo sheria yetu ya uhuru, itakayotuhukumu, kama tu vile wale wengine walivyohukumiwa kwa sheria ya dhambi na mauti (torati).
Ndicho alichokisema mtume Yakobo..
Kwa hitimisho ni kuwa sheria ya uhuru, ni sheria tunayoitimiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Ambayo hiyo pia itatuhukumu. Hivyo wewe kama mwamini, hakikisha wokovu wako unathibitika kwa kazi zake njema, chini ya upendo
Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29)
Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?
Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)
Kitabu cha Waraka wa kwanza wa Yohana ni kitabu ambacho kilielekezwa mahususi kwa makundi matatu (3) ya watu, Watoto, vijana, na Wababa. Sasa sio Watoto au vijana au wababa kimwili, Hapana, bali alikuwa anazungumzia ngazi hizo katika roho, yaani Kundi la Watoto kiroho, vijana kiroho na wababa kiroho.
1Yohana 2:12-14
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Na kila mmoja wao ameelezwa sifa zao, zinazowafanya wawe vile. Kwamfano Watoto kiroho, anasema ni kwasababu wamesahewa dhambi, lakini pia wamemjua Baba, tafsiri yake ni nini? Kwa mtu ambaye ni mchanga kiroho, anapokuja kwa Kristo, jambo la kwanza, ambalo atalipitia kwenye maisha yake, ni kutuliwa mizigo, mizito ambayo alikuwa anasumbuka nayo, ambayo asili yake ni dhambi. Ndio hapo ataanza kujiona mwepesi, anapokuja kwa Kristo, anajiona huru, katika kifungoni, anajiona na amani ambayo hajui chanzo chake ni nini, anajiona anapendwa,..Na ndivyo ilivyo upendo wa Mungu kwa huyu mtu unakuwa wa kipekee sana, ndio sababu kwanini anasema nimewaandikia nyinyi Watoto wadogo kwasababu mmesamehewa dhambi zenu, na mmemjua Baba. Hayo ni mambo mawili ambayo walio wa changa kiroho huyapitia.
Lakini kwa vijana, anasema nimewaandikia kwasababu mmemshinda yule mwovu. Hatua hii ya ujana ni ya kipindi cha ukuaji kiroho, hapa mara nyingi mwamini hukutana sana na majaribu ya shetani, mapingamizi makubwa, vita vya kiimani, misukosuko kwa sababu ya Kristo. Kiroho mtu kama huyu huitwa kijana, kwasababu wakati huu, ijapokuwa atasongwa lakini huwa haachi kumng’ang’ania Mungu, moto wake hauzimiki, hata kidogo, kama ni maombi, kasi huwa ni ile ile, usomaji Neno haupungui, hata akiumwa haiwi vyepesi kumwacha Mungu, kwasababu ni wakati wa Nguvu za Mungu nyingi Kutenda kazi ndani yake, na kumshinda mwovu kotekote.
Lakini Wababa kiroho, sifa yao pia ni tofauti na hao wengine, Sifa yao ni kuwa “ wamemjua yeye aliye tangu mwanzo”.
Maana yake ni nini? Kwanini hasemi kwasababu mmehubiri sana?, au kwasababu mmedumu sana ndani ya Kristo? Bali kwasababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo?
Kumfahamu Mungu, tangu mbali, ni kigezo kikuu sana cha ukomavu rohoni. Mpaka mitume kuitwa baba zetu, ni kwasababu walipewa kumwona Mungu kutokea mbali, tofauti na waandishi na makuhani..Ndio maana waraka tu huu ulipoanza anasema..
1Yohana 1:1 Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;
Hili lilikuja kudhihirika pale Yesu alipoanza kuwaeleza mambo yake mwenyewe aliyoandikiwa tangu, Torati ya Musa, Zaburi na Manabii, jinsi alivyokuwepo na watu wake, jangwani, kupitia ule mwamba, Mana, nyoka wa shaba, jinsi alivyo mtokea Ibrahimu kama Melkizedeki, jinsi alivyojidhihirisha kwao kwa namna mbalimbali kupitia tumbo la Samaki kwa Yona n.k. lakini hawakumwelewa.
Luka 24:44
44 Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. 45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
Sasa, mtu akishamwona Mungu kwa namna hiyo, basi Mungu kwake hawi wa “matukio” bali wa wakati wote. Yaani alikuwa nasi jana, yupo nasi leo, na atakuwa nasi hata milele.. Watoto wachanga kiroho, hawawezi kumwona Mungu jana, wenyewe Mungu wao, ni wa matukio ya leo.
Maeneo matatu ambayo macho yako yanapaswa yafunguke kuhusu, kumjua Mungu tangu mwanzo.
Hivyo ile uwe Baba, ni lazima umjue Mungu aliyekuwepo tangu Mwanzo, usiwe mtu wa matukio ya leo leo, kama mtu uliyeokoka jana, Kaa chini, tafakari sana, hatua moja baada ya nyingine ya maisha yako, anzia kwenye maandiko uone jinsi Mungu alivyokuwa na watu wake tangu zamani, ambao wengine kwa kukosa kumjua wakawa wanalalamika tu, wanaishi kiwepesi wepesi, na hatimaye kumsulubisha, lakini wale waliomjua waligeuzwa na kuwa mitume wake,
Kuwa baba rohoni.
Mungu akubariki.
Shalom.
Je umewaonea utungu watoto wako?
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.
SWALI:Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.mfano “We kenge njoo hapa”, kama YESU alivyo tumia mbweha katika
luka 13:32.
JIBU: Katika biblia tunaona watu wakiitwa kwa majina mbalimbali ya wanyama mfano mbwa mwitu (Mathayo 7:15), kondoo(Yohana10:27), nyoka(Mathayo 13:34). Lakini pia mbweha, Njiwa, nguruwe, Simba, mbuzi.
Sasa ni vema kufahamu makusudio ya watu/jamii kuitwa hivyo yalikuwa ni nini, hayakuwa kwa lengo la kutukana, au kukejeli, au kudharau..
Hapana Bali kwa lengo la kuonyesha tabia ya mtu, jinsi ilivyo hilo tu.
Kwamfano Yesu alipomuitwa Herode Mbweha, hakuwa na kusudi la kumtukana, au kumdharau, bali alikuwa Anaeleza tabia zake zilizo mfano wa mbweha, ambaye anatabia ya kuvizia na kurarua wanyama wadogo na kuwaua. Maana hivyo ndivyo Herode alivyokuwa, jambo lililoonekana Hata kwa baba zake Kipindi Yesu anazaliwa walimwinda ili wamuue.
Sasa Ikiwa mtu atajulikana kwa namna kama hiyo, kibiblia sio tusi.
Lakini kinyume chake watu hutumia Majina ya wanyama kuwatukana Wengine, au kuwaabisha, au kuonyesha dharau kinyume chao, chuki au hasira, hayo biblia imekataza…na ni dhambi
Kusema “wewe kenge njoo hapa”..Moja kwa moja kauli hiyo inaonyesha chanzo chake ni hasira, dharau au chuki.
Waefeso 4:29
[29]Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.
Wakolosai 3:8
[8]Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.
Mathayo 5:22
[22]Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.
Hivyo chunga kinywa chako. Kila Neno ulisemalo pima makusudi yaliyo nyuma yake.
VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.
JAWA SANA MOTO ULAO
USIWAOGOPE WAZAMZUMI
SWALI: Naomba kufahamu tunaposema Bwana Yesu asifiwe tunamaanisha nini? Na ni nani anayepaswa kuisema hiyo salamu, na kwanini wengine wanasema ‘shalom’ badala yake?
JIBU
‘Bwana Yesu asifiwe’ ni kauli inayotangaza kustahili kwa Yesu sifa kwa ile kazi njema aliyoifanya Hapa duniani.
Yesu ndiye Mtu pekee ambaye alikubali kuingia gharama ya kuacha enzi na mamlaka Mbinguni, na kuja kuishi hapa duniani kwa kusudi moja tu la kutukomboa sisi,katika dhambi zetu, akateswa na kujaribiwa sana, akafa baadaye akafufuka na hata sasa yupo hai ameketi kama mpatanishi wa sisi na Mungu,..
Kiasi kwamba kwa kupitia Yeye tunapokea msamaha wa dhambi, tunaponywa magojwa, tunamseta shetani, tunabarikiwa, tunawasiliana na Mungu moja kwa moja bila vikwazo vyovyote kwa damu yake.
Mtu Kama huyu ni lazima astahili kusifiwa..ndio maana inakuwa ni salamu ya Wakati wote BWANA YESU ASIFIWE..
Kwasababu ya nuru tuliyo ipata kwa kazi yake njema ya ukombozi.
Je ni nani anayepaswa kuisema?
Hakuna mtu anayekatazwa kuisema, lakini mtu asipojua kwanini Yesu asifiwe basi anaisema kwa unafki, Na Mungu hapendi unafiki. Kwamfano mtu ambaye hajaokoka, halafu anasema Bwana Yesu asifiwe, ni sharti ajiulize asifiwe kwa lipi wakati hakuna chochote kilichofanya na yeye katika maisha yake..
Ni sawa na mtu aliyeokoka aseme shetani asifiwe.. atasifiwa kwa jambo gani hapo wakati hakuna ushirika wowote alio nao na shetani. Lakini mganga wa kienyeji Akisema hivyo hiyo ni kweli kwasababu kuna faida amezipata Kwa shetani.
Salamu hii pia, au kauli hii, ni sahihi kutumika katika matamshi ya kiibada..mfano kwenye mahubiri, mafundisho, nyimbo, maombezi N.k. kwasababu katika Maeneo haya kazi za Yesu hudhihirishwa.
Lakini shalom Ni neno la kiyahudi linalomaanisha ‘Amani’. Ni Neno ambalo mtu yeyote anaweza kulitumia awe ameokoka au hajaokoka kwasababu ni Neno la kilugha zaidi kuliko kiimani. Ni sawasawa na sisi tunavyosema, ‘habari yako’. Mtu yeyote anaweza kutumia hilo neno. Lakini Bwana Yesu asifiwe ni Neno la kiimani ambalo anayestahili kulitamka ni mtu aliyemwamini Yesu tu.
Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.
Sasa Makosa kama haya, (ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.
Tutakwenda kuona aina tano (5) vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. [2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. [3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. [4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. [6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’
Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).
Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…
Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.
Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.
Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.
Mwanzo 4:10-13
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. [11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; [12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. [13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia
Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao
Kutoka 3:7-9
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; [8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. [9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.
Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.
Ufunuo 6:9-10
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. [10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.
Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.
5) Kilio (Shangwe) cha waovu.
Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kumbe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.
Mwanzo 18:20-21
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, [21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.
Je! Umemwamini Yesu?
Je una uhakika kuwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.
Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)
ENDELEZA UPONDAJI.
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
Swali: Tunasoma katika Yohana 1:29 kuwa Yohana anamshuhudia Bwana YESU kuwa yeye “mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu”.. Lakini tukirudi katika Mathayo11:3 tunasoma tofauti, Yohana anawatuma wanafunzi wake wamwulize kama yeye ndiye Kristo au wamtazamie mwingine, sasa swali ni je Yohana alimtilia shaka Bwana Yesu au hakumwamini tangu mwazo?.
Jibu: Ni ngumu imani ya Yohana kutikisika kirahisi lakini hebu kwanza turejee kitabu cha Mathayo…
Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza, 3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine? 4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; 5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 6 Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami”.
Ni kweli Masihi ajaye alikuwa ametabiriwa kuwa atakuja na nguvu kuwaokoa Israeli na utumwa wa maadui zao, na Israeli wote walitazamia kabisa kuwa Kristo atakayekuja atawafungua na utumwa mgumu wa warumi.. lakini haikuwa hivyo kwa YESU KRISTO, kwani alianza kushughulika na dhambi za wana wa Israeli, zaidi ya Taifa.. Hiyo ikawafanya baadhi ya watu kumtilia mashaka YESU kama yeye ndiye KRISTO (Yaani Masihi).
Na bila shaka Yohana hakuwa na wasiwasi wa YESU kuwa Masihi, kwani tayari alishaonyeshwa wakati anambatiza YESU kuwa Yule atakayembatiza na ishara ya hua ikionekana juu yake basi huyo ndiye Masihi, na ni wazi kabisa Yohana alijua kuwa wakati wake aliokuwa anaishi duniani, Kristo naye alikuwa anaishi, ila hakumjua ni nani mpaka wakati wa ubatizo, Roho kama Hua aliposhuka juu ya Bwana, na mbingu kufunguka. (Mathayo 3:16-17).
Sasa kama ni hivyo ni kitu gani kilichomfanya Yohana Mbatizaji atume wanafunzi wake kwa YESU na kumwuliza swali ambalo tayari alikuwa na jibu lake?.
Jibu ni kwamba baadhi ya watu ikiwemo wanafunzi wake Yohana bado hawakuwa na uhakika wa moja kwa moja kama YESU ndiye KRISTO, kwahivyo kwa kusikia Neno linalotoka moja kwa moja kinywani mwa YESU, ingeweza kuwafanya waamini zaidi, hivyo Yohana lengo lake huu ni wanafunzi wakasikie na kujihakikishia wenyewe, kwamaana muda wake wa kuishi ulikuwa umekaribia kuisha na watakayebaki naye ni YESU. Na walipokwenda walipata majibu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Yohana hakuwa na mashaka na Bwana YESU, bali wanafunzi wake na baadhi ya watu, na hiyo ni kutokana na kwamba Bwana YESU hakuwa anajitangaza hadharani kuwa yeye ni KRISTO.
Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi”.
Soma pia Luka 22:77..
Je umempokea YESU?.. Una uhakika kwamba YESU akirudi leo utakwenda naye?.. kama bado upo nje ya Imani fahamu kuwa upo hatarini sana, hivyo mkaribie YESU leo usamehewe dhambi zako na upokee ujazo wa Roho Mtakatifu. Shalom.
Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)
NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?
“Hakuna aniulizaye unakwenda wapi”, maana yake nini? (Yohana 16:5).
Nini maana ya “manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana” (Mathayo 11:13)
Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?