Tunaishi katika ulimwengu ambao, ukisimama tu kuhubiri, au kukemea dhambi, moja kwa moja utaambiwa UNAHUKUMU, Ukimweleza mtu madhara ya dhambi ya uzinzi kuwa mwisho wake, ni motoni, atakuambia, wewe ni nani mpaka utoe hukumu hiyo.
Wakati Fulani nilizungumza na watu Fulani ambao walikuwa wanatetea dhambi ya ushoga, nikawaambia watu wanaofanya matendo kama hayo, mwisho wao ni jehanamu walinishambulia, kisha wakanipa andiko, lile, ambalo linamzungumzia yule mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, ambapo mafarisayo walimpeleka kwa Yesu, kwa lengo la kumjaribu, kama na yeye ataridhia kupigwa mawe, lakini mambo yakawa tofauti badala ya kuwaruhusu wampige mawe akawaambia, “Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe”. Basi wote wakatawanyika wakamwacha yule mwanamke akiwa na Bwana peke yake.( Yohana 8:1-11)
Hivyo kwa Habari hiyo hawa watu nao wakaniambia, kama wale watu hawakumtupia yule mwanamke mawe, wewe ni nani utuhukumu sisi kwa tunachokifanya, humwogopi Yesu?.
Nikawaambia mimi siwezi kuwatupia ninyi mawe, lakini Yesu mwenyewe atawatupia ninyi mawe, wakati wenu ukifika.
Watu wanadhani Kristo atakuwa katika kiti chake cha rehema milele, kuchukuliana na dhambi zetu,, hawajui kuwa atasimama kama hakimu siku moja kuwahukumu na kuwaadhibu waovu wote,..Wanadhani, Bwana anafurahia uasherati wa mtu, au uzinzi wa mtu, wanadhani alifurahia pia Uzinzi wa yule mwanamke, ndio maana hakufanya chochote.
Nataka nikuambie ikiwa yule mwanamke angeendelea katika uzinzi wake, ni kweli angekwepa mawe ya wanadamu kwa wakati ule, lakini angekutana na mawe ya Kristo siku ile ya hukumu.
Wakati huo hakutakuwa na huruma yoyote katika macho ya Bwana Yesu, haijalishi wewe ni mtoto au mlemavu, au mzee, kama ulikufa katika dhambi, utahukumiwa na kutupwa motoni milele.
Hata kabla ya siku ya hukumu yenyewe kufika, siku ile ambayo atakuwa anarudi katika mawingu kuja kutawala kama mfalme, biblia inasema, ulimwengu mzima utamwombolezea (Ufunuo 1:7).. Na utamwombolezea kwasababu gani, kwasababu ya hayo mapigo atakayokuwa anawamwagia waasi wote katika huuu ulimwengu.
Inatisha sana kwasababu, Bwana Yesu atawaua watu wengi sana, wasiokuwa na idadi. Soma hapa;
Isaya 66:15 “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.
16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI”.
Siku hiyo Wazinzi, mashoga, wafiraji, walevi, washirikina, watatamani milima iwaangukie, ili tu waiepuke hiyo ghadhabu ya Bwana Yesu, lakini haitakuwa hivyo; watashiriki tu mapigo yake.
Ufunuo 6:15 “Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,
16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.
17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama”?
Ndugu, yangu, huu wakati usitamani ukukute, kwasababu hata baada ya kupokea mapigo hayo makali kutoka kwa Bwana Yesu, bado utasimama katika kiti chake cha hukumu na kutoa hesabu ya mambo yote uliyokuwa unayafanya hapa duniani yasiyompendeza Mungu, na baada ya hapo utatupwa katika lile ziwa la moto uangamie milele na milele.
Tukiyatafakari haya kwa umakini, ndio tutajua ni kwa namna gani Bwana Yesu hapendezwi na dhambi hata kidogo, Kuona leo hii unatoa mimba hafanyi chochote, unatazama picha za ngono, hachukui hatua yoyote, unaiba hakuadhibu, unazini, unalewa, unaabudu sanamu, bado hajishughulishi na wewe..usipumbazike ukadhani, hali hiyo itaendelea hivyo hivyo milele, hata baada ya kufa.
Waebrania 10:31 “Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.
Ni heri ukayasalimisha Maisha yako leo kwa Bwana Yesu maadamu neema ipo, Wakati umekaribia, mambo yatabadilika ghafla, parapanda italia, kisha watakatifu wataondoka..Wewe ambaye utabakia katika huu ulimwengu, ndio utakayekutana na huo upande wa pili wa shilingi wa Bwana Yesu, ni kilio na kusaga meno!. Hutaamini kama huyu ndio yule Bwana aliyekuwa ananililia kila siku niache dhambi kwa sura ya upole, nikawa namdharau. Atakuuwa mwili na roho.
Mathayo 10:28b “… afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”.
Bwana atusaidie sana, ikiwa hujaokoka, embu anza Maisha yako upya na Kristo leo. Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe katika jina la Bwana Yesu Kristo, ili upokee ondoleo la dhambi zako, na baada ya hapo Bwana atakusaidia. Hatuna muda tena, Yesu anarudi wakati wowote.
Kwa msaada ya kumpokea Yesu, basi wasiliana nasi kwa namba hizi; +255789001312 /+255693036618
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
“Nikolai” ni neno la kigiriki lenye maana ya “Kuteka madhabahu”.
Katika kanisa la kwanza kulikuwa na kundi dogo la watu lililonyanyuka, ambalo lilikuwa linateka madhabahu.
Na kuteka madhabahu kunakozungumziwa sio kuteka nyara vitu vya madhabahuni au watu wanaosimama madhabahuni, hapana!.
Bali kuteka kunakozungumziwa hapo, ni kusimamisha mfumo ambao unaondoa uongozi wa Roho Mtakatifu ndani ya kanisa, na kusimamisha uongozi wa wanadamu.
Kikawaida kanisa linapaswa liongozwekwa karama za Roho Mtakatifu, yaani Uinjilisti, uchungaji, unabii, aualimu, karama za lugha, miujiza, imani n.k (1Wakorintho 12).
Hizo ndizo zinazoliongoza kanisa, na ndizo zinazojenga mwili wa Kristo,lakini enzi za kanisa la kwanza liliinuka kundi la watu wasio na Roho, na kutaka kuliongoza kanisa kibinadamu.
Maana yake badala Roho Mtakatifu anene, apange, afundishe, aamue, na afanye jambo kupitia karama alizoziweka ndani ya watu wake..kinyume chake wakainuka watu wakawa wao ndio wanapanga, wananena, wanafundisha na wanaamua kupitia falsafa zao, hekima zao, vyeo vyao, heshima zao katika jamii, umaarufu wao, elimu zao, ujuzi wao, mwonekano wao, na si tena kupitia karama za Roho.
Ratiba za masomo ya kufundisha zikawa zinapangwa na wanadamu, inaweza kutolewa kalenda hata ya mwaka mzima, masomo ya kufundisha tayari yameshaandaliwa.
Hivyo ubinadamu ukawa umeteka madhabahu ya Bwana badala ya Roho Mtakatifu. Huo ndio “Unikolai”.
Na katika kanisa la kwanza maandiko yanasema unikolai ulianza kama Matendo tu, Yaani watu hao ambao yalikuwa ni mapando ya adui shetani, walikuwa wanafanya hayo lakini sio kuwafundisha watu.
Ufunuo 2:6 “Lakini unalo neno hili, kwamba wayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo na mimi nayachukia”.
Lakinibaadaye unikolai ulikuja kubadilika na kuwa “Mafundisho”, yaani watu wakawa sio tu wanatenda unikolai, bali wakawa wanafundisha wengine kuutenda unikolai, (yaani kuunyanyua uongozi wa kibinadamu na kuushusha chini uongozi wa Roho Mtakatifu).
Ufunuo 2:15 “Vivyo hivyo wewe nawe unao watu wayashikao mafundisho ya Wanikolai vile vile.
16 Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu”.
Matendo na mafundisho ya Wanikolai katika nyakati hizi za mwisho ndio yameshika hatamu.
Leo hii hakuna tena uongozo wa Roho mtakatifu ndani ya kanisa, ni Liturjia, na malokeo ndio yanayoongoza… kiasi kwamba hata ikitokea mtu kafunuliwa jambo jipya na Roho Mtakatifu la kwenda kufundisha, hawezi kupata nafasi kwasababu tayari kalenda ya nini cha kufundisha mwaka mzima imeshawekwa, na lazima aifuate hiyo!.
Leo hii ili uaminike kuwa wewe mchungaji au mtumishi wa Mungu ni lazima uwe umepitia chuo cha biblia na theolojia, ukisema unao wito wa Roho Mtakatifu bila kupitia mambo hayo huwezi kueleweka. (Huo ni unikolai), ambao Bwana Yesu kasema anauchukia!!!.
Unikolai hautaki kabisa Uongozo wa Roho Mtakatifu, unampinga Roho Mtakatifu siku zote.
Na shetani anajua kanisa linaloongozwa na Roho Mtakatifu ni hatari sana katika ufalme wake. Na yeye hataki watu waende mbinguni.
Hivyo atafanya juu chini kumzimisha Roho ndani ya kanisa, lakini ashukuriwe Mungu, katikati ya giza nene ipo Nuru mahali.
Bwana anao watu wake mahali fulani katika kila Taifa, ambao hawajamzimisha Roho.
Bwana atusaidie na sisi tuwe miongoni mwa hao ambao hawajamzimisha Roho.
1 Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho”
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Tusome,
1 Yohana 2:16 “Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.
Kiburi cha Uzima ni kiburi mtu anachokipata kutokana na vitu alivyonavyo vya kidunia (hususani mali).
Watu ambao hawajamjua Mungu, uzima wao wameuweka kwenye mali, wanapokuwa na mali nyingi ndipo wanapojiona waoni watu (wanao uzima), wakikosa wanajiona wao si kitu.. hivyo inapotokea wanapata mali hizo zinawapa kiburi na kuwafanya wabadilike tabia mbele za Mungu na wanadamu.
Lakini Bwana Yesu alisema maneno haya..
Luka 12:15 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.
16 Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu”.
Je na wewe uzima wako umeuweka wapi?
Je ni kwenye nyumba ulizozijenga? Je ni hizo ndizo zinazokupa kiburi hata kumdharau Mungu na kuwadharau wengine?, Je ni fedha ulizonazo?, au Magari?, au Vyeo? Inazokufanya uone injili ni habari zilizopitwa na wakati?..kama ndio basi unacho kiburi cha uzima pasipo kujijua, ambacho maandiko yanasema hakitokani na Mungu, kwasababu mali ni kama maua leo ipo kesho haipo, hivyo si ya kujitumainisha nayo, kamwe isituletee kiburi.
Je umejitajirisha wapi leo? Mbinguni au duniani, umejiwekea hazina yako wapi?, Mbinguni au duniani?
Bwana atusaidie tusiwe na kiburi cha uzima.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo: