Title 2026

Ipi tofauti ya “Majibu” ya Maombi na “Majaribu”.

Swali: Je nikiomba kazi kwa mwaka mmoja na ikatokea fursa ambayo inanitaka nitoe rushwa kidogo ili niingie kazini, je hilo ni Jibu la Maombi yangu, au ni jaribu?


Jibu: Hilo si jibu la Maombi, bali ni “Jaribu” linaloletwa na ibilisi mbele yako. Majibu ya Maombi hayana njia za mkato, yanakuwa yamenyooka na yenye kibali.

Lakini inapotokea tunaomba jambo kwa Mungu atutendee, halafu inatokea fursa nyingine iliyo kinyume na Neno la MUNGU, hilo ni jaribu na tunapaswa tulishindwe.

Mfano mwingine ni pale mtu ameomba hitaji fulani kwa Mungu labda fedha ya kodi, halafu inatokea fursa ya wizi, utakaokamilisha kile kiasi.. sasa hiyo fursa si kutoka kwa MUNGU hata kama inakupa wepesi mkubwa wa kupata kile kiasi, bali ni Jaribu la maombi yako, na ni lazima kulishinda.

Au unaomba mume halafu anakuja Mume wa Mtu kutaka kukuoa, hayo sio majibu ya maombi bali ni majaribu..

Na yapo mambo mengine mengi,  yanayokuja kwa sura ya Majibu ya Maombi, lakini nyuma yake ni Majaribu ya maombi.

Sasa ni kwa namna gani tunaweza kutofautisha Majibu na Majaribu?.

Hakuna njia nyingine zaidi ya “KULIJUA NENO LA MUNGU”..Na hatulijui Neno la Mungu kwa kukariri mistari ya Biblia, au kuelezewa bali kwa “KUJIFUNZA BIBLIA”.

Huwezi kujua dhambi ni nini kama hauijui Biblia..

Warumi 7:7 “Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani”.

Pia hatutaweza kuyajua majaribu ya ibilisi kama hatutalijua Neno la MUNGU ndani ya Biblia takatifu.

Weka desturi za kusoma Biblia kwa kujifunza, usiwekeze tu peke yake katika Maombi na ukaliacha Neno la Mungu pembeni, ukiwa mtu wa namna hiyo, ibilisi atakuletea majaribu ukidhani ndio majibu ya maombi yako, na kufanya mfungo wako au maombi yako kuwa si bure.

Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

KISIMA BADO KINA MAJI, KIFUKUE TENA.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

Print this post

Upote ni nini kibiblia?

Kama ni msomaji wa biblia, Neno hilo utakutana nalo katika baadhi ya vifungu kwenye Zaburi..

Zaburi 11:2

[2]Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo. 

 

Zaburi 21:12

[12]Kwa maana utawafanya kukupa kisogo, Kwa upote wa uta wako ukiwaelekezea mishale. 

Upote ni ule uzi mwembamba unaofungwa kwenye uta, ambao mshale huwekwa pale kwa kuvutwa na kurushwa.

Upote hutengenezwa kwa ngozi na wakati mwingine kamba za mimea imara.. ni lazima utengenezwe kwa malighafi imara, ili isikatike pale unapovutwa.

Kwasababu hizi ni zana za kivita…kiroho hufunua pale mbili. Adui hutengeneza upote wake, ambao hurushia watu mishale ya moto ili kuwaua kiimani (Waefeso 6:16), ili kuweza kuishinda, biblia inatufundisha daima tuibebe ngao ya Imani.

Lakini pia Bwana Yesu anao upote wake ambao kwa huo hutupa silaha zake kwa adui zetu, sawasawa na hiyo Zaburi 21:12, Na silaha za Kristo zina nguvu sana sio tu kumlenga adui lakini pia kuangusha ngome.

Maboma na makao ya shetani.

2 Wakorintho 10:4-5

[4](maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 

[5]tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 

Lakini Nguvu ya silaha hizi hutegemea na hali ya mtu kiroho katika maeneo matatu; 

1) kimaombi, 

2)Utakatifu

3) Injili.

 Mwamini wa namna hii ambaye huchukia dhambi, huubiri injili na huzingatia kudumu katika maombi ya masafa,

Kiroho ni askari imara na mwenye silaha zenye nguvu sana, ziwezazo kumuharibu ibilisi.

Kuwa askari kamili wa Kristo

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mtambo/mitambo ni nini kibiblia?

Na kipenu ni nini (Isaya 1:8)

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Print this post

YAFAHAMU NA YATENDE MAPENZI YA MUNGU.

Jina la Mwokozi Mkuu YESU KRISTO, libarikiwe.

Kabla ya kusogea mbele kujifunza ujumbe huu, ni vizuri tukarejea sehemu ya kwanza ya ujumbe huu inayosema “FAHAMU JINSI YA KUPATA MAMLAKA YA DAMU YA YESU”

Katika ujumbe huo tuliona ni kwa namna gani tunaweza kuwa na uhalali wa kuitumia Damu ya YESU, ikiwa tutakuwa ndugu zake, fuatilia ujumbe huo hapa >>>FAHAMU JINSI YA KUPATA MAMLAKA YA DAMU WA YESU.

Sasa kuna umuhimu mkubwa sana wa “KUYAJUA” na “KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU”.. Kwani hiyo ndio tiketi ya ‘KUMWONA MUNGU’ siku ya mwisho.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.

Na tena Neno la Mungu linatusisitiza kutafuta kuyafanya mapenzi ya Mungu kwa bidii muda tuliobakiwa nao hapa duniani..

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali KATIKA MAPENZI YA MUNGU, WAKATI WENU ULIOBAKI WA KUKAA HAPA DUNIANI”.

Sasa Mapenzi ya MUNGU yamegawanyika katika sehemu kuu Mbili.. 1) Mapenzi ya Mungu kwa Mtu binafsi, na 2) Mapenzi ya Mungu kwa watu wote.

Ni lazima tufanya Mapenzi ya Mungu katika migawanyiko yote hii miwili.. ni kama sheria, zipo sheria ulizojiwekea wewe, na zile ulizowekewa na nchi, ni lazima zote iziishi. Hali kadhalika yapo mapenzi ya Mungu kwako wewe au mimi binafsi, na yale Mapenzi ya Mungu kwa watu wote.. hebu tutazame moja baada ya lingine.

    1. MAPENZI YA MUNGU KWA MTU BINAFSI.

Hili ni kusudi ambalo Mungu anataka ulifanya ukiwa hapa duniani kupitia karama, au nafasi uliyopewa na MUNGU. Ni lazima ufahamu duniani umeitiwa kufanya nini wewe kama wewe.. Kama umeitwa kuwa Askofu, au mwalimu, au mchungaji, au nabii, au mtume, au mwinjilisti, au mtu mwenye kukirimu, au mshauri, au mwingine yoyote katika nafasi yoyote ile kwa ajili ya ufalme wa MUNGU.

Usipojua mapenzi ya MUNGU ni yapi ni ngumu kuishi kwa kumpendeza MUNGU, kwasababu utafanya jambo lisilompendeza Mungu, utaishi mahali pasipopendeza Mungu, utaenda katika njia ambayo Mungu hajaikusudia juu yako.

Na mapenzi ya Mungu yanatofautiana  kwa mtu na mtu.. anavyotembea mwingine si sawa na utakavyotembea wewe,..lakini wewe umekusudiwa njia yako tofauti na mwingine, ni lazima uijue.

Sasa unajuaje kusudi/mapenzi ya Mungu kwako?

Njia ya kwanza ni ya kumpokea YESU na kutubu dhambi.. baada ya hapo, kuomba huku ukidumu katika kumpenda MUNGU, Roho Mtakatifu atakuongoza katika kusudi lake, na ukikaa katika kusudi/mapenzi ya MUNGU, utaona amani ya kiMungu ndani yako, na pia mafanikio katika utumishi huo.

Na utakapojaribu kuacha njia hiyo utaona mambo hayaendi kabisa..hapo utajua kuwa ulikuwa kwenye njia sahihi ya mapenzi ya MUNGU.

    2. MAPENZI YA MUNGU KWA WATU WOTE.

Baada ya kujua mapenzi ya MUNGU kwako ni yapo,  kwamba unapaswa ufanye nini, wakati mwingine uishi wapi, au utembee na nani safari bado haijaisha ni lazima pia uyajue mapenzi ya MUNGU kwa watu wote, aliyoyakusudia kila mtu ayaishi.

Sasa hayo mapenzi ya MUNGU kwa wote ni yapi?.. Tusome maandiko yafuatayo..

1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Kumbe mapenzi ya Mungu kwetu sote ni KUTAKASWA (Yaani utakatifu), na TUEPUKANE NA UASHERATI (wa mwilini na rohoni) na TUJUE KUIWEZA MIILI YETU KATIKA UTAKATIFU na HESHIMA.

Hapa ndipo shetani anapofumba macho wengi.. ni kweli tumejua mapenzi ya MUNGU kwetu ni kumtumikia, kumwimbia, kuhubiri, kufanya uinjilisti, lakini tumekosa kujua kuwa mapenzi ya MUNGU kwetu wote (kama watu wa Mungu) ni kuishi maisha matakatifu, yenye staha mwilini na rohoni.

Utakuta mkristo ameokoka anamwimbia Mungu, anahubiri na kweli wito wa MUNGU ndio uliomweka hapo, lakini tazama uvaaji wake, tazama maisha yake ya sirini, ni dhambi tupu imetawala.

Ni lazima kuyafanya mapenzi ya Mungu katika migawanyiko yote.

Bwana atusaidie sana kuliona hili, na yeye ni mwaminifu hajatuitia kwa hukumu bali tupate Baraka na faida, usiukimbie utakatifu ndugu mpendwa katika KRISTO, pasipo huo hatutaweza kumwona MUNGU (Waebrania 12:14).

Na kwa nguvu zetu hatutaweza kuishi maisha hayo ya usafi, lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu yote yanawezekana, tafuta ujazo wa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ipi tofauti ya utakatifu na utukufu?

CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.

JAWA SANA MOTO ULAO.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.

Print this post

DHAMBI HAIWEZI KUKAA NA MSHAHARA WAKO.

Warumi 6:23

[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Kwenye vifungu hivyo tunaonyeshwa kuwa Mungu hutoa zawadi(karama), lakini dhambi inalipa mshahara.. Na mpaka ilipe mshahara ni lazima kazi fulani ilifanyika..

Watu wengi hawajua kuwa kila tendo moja la dhambi, huhesabu mshahara fulani na mwishoni mtu huyo hulipwa wote, hata kama hakujua.

Unapokwenda kuzini leo, unarudia tena na kesho, na kesho kutwa hivyo hivyo, mshahara unajilimbikiza, siku isiyo na jina utashangaa tu ghafla mshahara wako huo hapo umekufikia…

Ndio hapo mauti ya kiroho au ya kimwili au ya jambo fulani humfikia mtu.

Sasa inapofikia wakati wa mshahara wengi hujifanya haiwahusu, lakini utaupokea tu.. upende usipende…wengi humdharau Yuda kwanini alijinyonga, si kwamba alipenda lakini ulikuwa ni wakati wa mashahara, ukiona leo watu wanakutana na madhara makubwa kwasababu ya dhambi zao, sio kwamba wana bahati mbaya, bali ni wakati wa mshahara.

Epuka dhambi, ikimbie dhambi.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

SHUGHULI MBOVU ZA UCHIMBAJI MABIRIKA.

Yeremia 2:13

[13]Kwa maana watu wangu hawa wametenda maovu mawili; wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji ya uzima, wamejichimbia mabirika, mabirika yavujayo, yasiyoweza kuweka maji. 

Ndugu Ipo tofauti kati ya chemchemi na birika, chemchemi ni chanzo cha asili ambacho hutoa maji yake yenyewe, haihitaji kuchimbwa, wala kukarabatiwa lakini birika ni hivi visima ambavyo mtu hutumia jasho lake kuchimba na hutegemea mvua ili kuwa na maji, lakini bado huvujisha maji yake chini ya ardhi ndio maana baadaye hukauka…maji ya visima kikawaida hayawagi masafi sana kwasababu hayatembei, ni rahisi kuona vyura, ngala, ruba, tofauti na ya chemchemi.

Sasa Bwana anasema watu wake wamefanya makosa MAWILI. Kwanza wamemuacha yeye aliye chemchemi ya maji ya uzima, Maana yake wana kiu, lakini hawataki maji yaondoayo kiu…hicho huitwa kiburi, au dharau na matokeo ya kiburi ni maangamizi. Ni sawa na mtu anajijua kabisa ni mgonjwa halafu analetewa tiba anasema sinywi dawa zako.

Lakini kama hilo halitoshi, wanaenda kufanya kazi ya kuunda chemchemi zao bandia, kwa kuchimba wenyewe ili wajihifadhie maji yao ambayo ni ya muda…hii ndio huitwa ibada ya sanamu..watu wanapoona fedha inaweza kusimama badala ya Mungu, hiyo ni sawa na kujichimbia birika ..wanapoona elimu, ushirikina, anasa, ulevi, ujuzi..vinatosha kuwa mbadala wa Mungu ni kujichimbia birika lako mwenyewe..

Ndio maana wanataabika, kutafuta ukweli wote ndani yake hawapati, wanapata raha za kitambo baada ya hapo ni majuto kurudi.

Ndugu tulia kwa Kristo ambaye alishamaliza kuunda chemchemi yake, kwake yeye huhitaji kutendea kazi, nenda tu unywe maji, kiu ya dhambi na mambo mengine maovu ya kidunia ife, uishi maisha ya amani na kustawi. Maji hayo ukinywa hata ukifa utakuwa unaishi, na kumpokea Yesu ndio kuyapokea maji. Ukimwamini Yesu na kumfanya Bwana na mwokozi wa maisha yako, na kumtii baada ya hapo ujue ndani ya roho ya maji yameshawasili.

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; 

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele. 

Achana na mabiriki.

Mungu atusaidie.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

FAHAMU JINSI YA KUPATA MAMLAKA YA DAMU WA YESU.

Matumizi ya damu ya YESU hayaishii tu katika kutamka, kwamba tukiwa na haja na jambo tunatamka “Kwa Damu ya YESU” na jambo lile linatokea au linatii… hapana ni zaidi ya hapo, kwasababu hata mashetani wanamjua Bwana YESU na Damu yake.

Hivyo hayatishiki na mtu wa kawaida kulitaja jina la YESU au Damu ya YESU na huku mtu huyo hana uhalali, au mamlaka ya kutumia Jina hilo, soma kilichowatokea Wana saba wa Skewa (Matendo 19:4) unaweza kuelewa zaidi.

Sasa Mamlaka ya kutumia DAMU YA YESU, tunapataje?

Tunapata mamlaka ya kutumia DAMU YA YESU kwa kanuni moja tu!, nayo ni ile ya kuwa na UNDUGU WA DAMU NA YESU?

Utauliza mtu anaweza kuwa na undugu wa Damu na YESU na mwingine asiwe nao?..

Ndio!, hiyo inawezekana kabisa na nitakuonyesha kimaandiko…Lakini tambua jambo moja kuwa ili mtu aitwe ndugu yako ni lazima muwe na mfanano wa damu, mnaweza msifanane sura, au mwonekano lakini bado damu ikaeleza undugu mlio nao (hiyo imethibitika kisayansi na wanadamu).

Na YESU KRISTO anao ndugu zake wa damu.. sasa tunawajuaje?.. tusome maandiko yafuatayo Mathayo 12:47

Mathayo 12:47 “Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.

48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani? 49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!

50 Kwa maana ye yote ATAKAYEYAFANYA MAPENZI  YA BABA YANGU aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu”.

Umeona? Ndugu za YESU wana sifa gani?… hawana sifa ya usomi, au uzuri, au ukuu au umaarufu… bali ni wale wote WANAOFANYA MAPENZI YA BABA ALIYE MBINGUNI.

Kumbe ili tuwe NDUGU WA DAMU WA YESU, ni lazima TUYAJUE na KUYAFANYA MAPENZI YA BABA MBINGUNI?.

Je unayajua mapenzi ya MUNGU kwako?.. Kama huyajui je unawezaje kuwa na ujasiri wa kuitumia DAMU YAKE, na ilihali huna muunganiko wowote na hiyo DAMU?

Ni lazima uyajue mapenzi ya MUNGU, na KUYAFANYA.. ili ile damu iweze kunena mema juu yako (Waebrania 12:24).

Je wewe  ni ndugu wa YESU?… Je unayajua Mapenzi ya MUNGU kwako?.. kama bado huyajui au huna uhakika kama unayafanya mapenzi yake au la!, basi usikose sehemu inayofuata ya somo hili inayozungumzia MAPENZI YA MUNGU.

Waebrania 2:11 “Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;

12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa.

13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu.

14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,

15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.

Bwana atusaidie..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.

SAFARI YA KUUONA USO WA MUNGU.

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

Nini tofauti ya kushuhudia na kuhubiri?

Print this post

PETE YA DHAHABU PUANI MWA NGURUWE.

Nini maana ya “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”


Jibu: Turejee..

Mithali 11:22 “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”

Kabla ya kujua kwa undani maana ya mstari huu, hebu tujifunze kidogo juu ya Nguruwe, na pete inayowekwa puani mwake.

Nguruwe ni mnyama mwenye sifa ya uchafu, na asiyekuwa na ustaarabu, anaweza kuoshwa na baada tu ya kumaliza kuoshwa akarudi kwenye matope..Biblia inatuthibitishia hilo..

2Petro 2:22 “Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”

Sasa pamoja na tabia hiyo ya uchafu na kukosa ustaarabu nguruwe waliyonayo, bado wana tabia nyingine ya kuchimba chimba chini ya ardhi, au kwenye mashamba na kwenye zio kwa kutumia “pua zao” kwa lengo la kutafuta chakula, au utofauti wa mazingira.

Tabia hiyo ya kuchimba chimba kwa kutumia pua, inawafanya kubeba tabia nyingine ya uharibifu usiokuwa wa kawaida,

Sasa wafugaji wa nguruwe ili kulidhibiti hilo, huwa wanaweka pete katika pua zao lengo ni ili wanapojaribu kuchimba chimba kwa kutumia pua zao, basi ile pete iliyowekwa puani iwaumize na waache au kupunguza tabia hiyo ya uharibifu.

Sasa hizi pete si za urembo, bali zinakuwa kama Hereni kwenye pua ya nguruwe, na zinakuwa ni za chuma..tazama picha juu..

Sasa inapotokea Mfugaji anamwekea nguruwe pete ya dhahabu badala ya chuma isiyo na thamani..itakuwa ni jambo la ajabu sana na la kushangaza..kwani nguruwe kamwe hajawahi kuthamini kitu cha thamani, na hata yeye mwenyewe hajithamini soma Mathayo 7:6

Sasa anapowekewa kitu cha thamani puani mwake, ni kitu cha ajabu na kinachoshangaza..

Kwa mantiki hiyo hiyo Biblia inajaribu kuufananisha uzuri wa mwanamke na PETE YA DHAHABU, na mwanamke asiye na busara inamfananisha na NGURUWE.

Kwamba Mwanamke aliye na uzuri wa uso halafu akakosa busara ni sawa na kitu cha thamani kilichowekwa mahali pasipostahili.

Mwanamke mzuri wa uso/wa nje halafu hana heshima kimwonekano ni sawa na pete puani mwa nguruwe,

“Uzuri” na “Busara” ni lazima viende pamoja, lakini ukiwa ni mzuri halafu huna busara ya kiMungu, unafananishwa na nguruwe.

Sasa swali ni je hii busara inapatikana wapi?

Chanzo cha Busara halisi ni YESU KRISTO, kwamba unapompokea YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, basi hapo tayari umeshafungua mlango wa busara kuumbika nakuanza kufanya kazi ndani yako.

Na kazi hiyo ya kujaza  busara ndani yako ni ya Roho wa Mungu atakayeingia ndani yako baada ya wewe kuokoka….Utaanza kuona  kiwango chako cha hekima kinaongezeka, na ueledi katika masuala ya kiroho na kimwili.. na hiyo busara itaulinda uzuri wako wa nje na ule wa ndani kama maandiko yanavyosema..

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;

11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Kwanini Mungu aliwazuia walemavu wasimtumikie madhabahuni kwake?(Walawi 21:16-24)

Print this post

WIMBO ULIOANDALIWA WAKATI WA USIKU.

Zaburi 42:8

[8]Mchana BWANA ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami,.. 

Biblia inataja nyakati mbili, ambazo mwamini anazipitia..nazo ni mchana na usiku.

Mchana ni nyakati za matumaini, nyakato za kuona njia, za kufanikiwa, za amani…hizi ni nyakati ambazo Bwana anasema ataagiza fadhili zake…maana ya fadhili ni kujitoa kwa upendo wa juu sana..Mungu huwafadhili watu wake hata katika nyakati za furaha, na amani.

Lakini pia anasema wakati wa usiku wimbo wake bado utakuwa nasi…usiku ni wakati wa huzuni, wakati wa upweke, wakati wa ukame wa kiroho, wakati wa majaribu, na mapito n.k.

Ni nyakati ambazo huoni chochote…kwasababu usiku sikuzote ni nyakati za ukimya na upofu..

Lakini pia huko Bwana anasema juu ya watu wake kuwa WIMBO WAKE, utakuwa pamoja nao.

Wimbo hufunua nini?

Wimbo humaanisha faraja, kicheko, shangwe, yaani hatawaacha wawe kama walio gizani wanyonge, wapweke, bali kama watu wafurahishwao na nyimbo nzuri sana..

Kama mwana wa Mungu, nyakati za majaribu, Bwana yupo pamoja na wewe, nyakati ambazo huzielewi upo wimbo wake ndani yako.

Wakristo wafikiapo hatua hii huukimbia wimbo wa Bwana na kutazama zaidi changamoto zao, shida zao, magumu yao, na mengineyo kana kwamba Mungu amewaacha, 

Lakini kama ukibakisha fikra zako kwake…utaona bubujiko kubwa sana likitiririka ndani yako, kwa jinsi ile ile ulivyokuwa katika nyakati za nuru..

Kwasababu hii ni ahadi yake. Na kamwe hawezi kudanganya. Unapojifunza kutulia uweponi mwa Mungu, kimaombi, kwa kutafakari, uwapo kwenye hizo nyakati hafifu..ghafla tu utaona furaha, amani, ushindi, kicheko, uwepo wa Bwana vinajaa ndani yako.

Kamwe usiukandamize wimbo huu?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.

JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.

MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.

Print this post

Maana ya Mithali 29:20 Je! umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?

Mithali 29:20

Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye

Mtu mwenye kuhamaki.

Ni mtu anayezungumza maneno kwa haraka, yaani anayezungumza bila kufikiri, au kujizuia.

Vitu kama mizaha, ugomvi, hasira, uongo, na mafarakano, huzaliwa na tabia kama hii ya watu kunena bila kufiriki.

Kwamfano, mtu anaweza kukutukana, na wakati huo huo hasira ikawaka ndani, sasa kwasababu huwezi kujizuia, unajikuta unarudisha majibizano, hatimaye na wewe unafungua kinywa chako unatukana.

Au labda unatambua jambo Fulani ambalo si jema, na pengine ukilisema linaweza lisiwe na maana yoyote, kinyume chake likazua ugomvi, au kumuabisha mwingine, au sintofahamu, lakini wewe kwasababu huwezi jizuia unalisema, mwishowe matatizo yanazuka makubwa yasiyokuwa na lazima.

Watu wanaoapa, ni matokeo ya kunena bila kufikiri, mafarisayo ambao walitenda dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni kwasababu ya maneno ambayo hayana hekima nyuma yake.

Mathayo 12:36  Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.

Mpaka hapo unaweza kuona ni kwanini mpumbavu anaweza kuonekana ana afadhali kuliko mtu mwenye kuhamaki.

Mstari huu unatukumbusha nguvu iliyopo katika maneno, biblia inasema ulimi ni kama moto ni kiungo kidogo lakini kinawasha misitu, hivyo hatuna budi kuwa wazito katika kunena,  tukifiri kwanza ndipo tuseme. Yakobo 1:19

19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Maneno yana nguvu, kila siku yatupaswa tujifunze kudhibiti vinywa vyetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

 

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

 

 

 

 

Print this post

Je wana wa Israeli waliofia jangwani, walienda mbinguni au jehanamu?

JIBU: Wakiwa jangwani wana wa Israeli walitenda  makosa  ya aina mbili.

  1. Makosa yaliyopoteza Ahadi
  2. Makosa yaliyopoteza Uzima wa milele.

Makosa yaliyopoteza Ahadi ndio yalikuwa yale ya kutokuamini. Mfano Mungu alipowatoa jangwani, na kuwavusha, mara nyingi walionyesha hali ya kutoamini, Kosa ambalo liliwafanya Mungu aghahiri kuwafikisha kule alipowaahidia, ambapo ni nchi ya Kaanani ibubujikayo maziwa na asali, Na kilele cha kosa hilo kilikuja  pale wale wapelelezi waliporudi katika kuichunguza nchi, na kutoa ripoti za kule, kwamba wao wanaonekana kama mapanzi, hivyo wote wakaanza kulia na kutaka kurudi Misri, Ndipo Mungu akakasirika sana na kuapa kuwa wote  hawataiona hiyo nchi ya Kaanani isipokuwa Kalebu na Yoshua, kwasababu wao hawakuonyesha kutokuamini.

Hesabu 14:21-24

21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana;
22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;
23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona;
24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki

Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hawatakwenda mbinguni, kwasababu wapo waliotubu,hata wakati ule ule

Kwahiyo kusema adhabu ile ndio iliwapelekea moja kwa moja kupoteza mbingu si sahihi.

Kwasababu Mungu aliendelea kutembea nao kwa wingu lake, baadaye akawainua viongozi, wa kuwaaamua na Pamoja na wazee, akawamwagia  Roho wake, (Hesabu 11:25). Hivyo kama Mungu kasingekuwa nao, basi hayo yote yasingefanyika, kwasababu Mungu hawezi kuwaongoza wafu.

Lakini yapo makosa ambayo yaliwagharimu adhabu ya kupoteza kabisa uzima wa milele. Na makosa kama hayo ndio yale ya makusudi kabisa, mfano wa hayo ni yale ya kuvunja amri za Mungu, kama vile kutengeneza sanamu ya ndama  na kuiabudu, Kuzini, kuwa na miungu mingine, na kuhalifu sabato za Mungu .

Makosa kama hayo ndio yaliyopelekea  kupoteza uzima wa milele, ndio maana ukichunguza utaona watu kama hawa walipokea adhabu za moja kwa moja.     Hivyo ni kuwa makini sana na neema ya Mungu.

Hata sasa, zipo dhambi za aina mbili zinazozungumziwa kwenye maandiko, dhambi za mauti, na dhambi zisizo za mauti.

Kwa urefu wa maelezo yake, pitia hapa>>> DHAMBI YA MAUTI

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?

Kwanini Roho Mtakatifu amzuie Paulo kuipeleka injili Asia? (Matendo 16:6-7).

Print this post