Je kuna pepo wazuri kulingana na Waefeso 6:12?

Je kuna pepo wazuri kulingana na Waefeso 6:12?

Swali: Biblia inasema kushindana kwetu ni dhidi ya pepo wachafu, je kulingana na mstari huo, wapo pepo wazuri?


Jibu: Turejee…

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”

Biblia iliposema kuwa kushindana kwetu ni dhidi ya “pepo wabaya” haijamaanisha kuwa wapo pepo wazuri, bali inaelezea tu sifa ya hizo roho (mapepo) kwamba ni mbaya na chafu.

Ni sawa na biblia inapotaja Malaika watakatifu, (soma Mathayo 25:31, Marko 8:38 na Ufunuo 14:10) haimaanishi kuwa wapo Malaika wasio watakatifu, na kama wapo wasio watakatifu basi hawaitwi tena Malaika bali ni mapepo, vile vile hakuna mapepo wasafi na kama zipo hizo roho safi basi haziwezi kuitwa tena mapepo, bali zitaitwa Malaika.

Hivyo uzuri na usafi unaotajwa juu ya Malaika au Mapepo, ni kuelezea tu sifa zao na kazi zao, kwamba Malaika wote walioko mbinguni ni wasafi na watakatifu, na mapepo yote yaliyotupwa ulimwenguni ni machafu na mabaya.

Na kumbuka pia “Pepo na jini” ni kitu kimoja, isipokuwa ni lugha mbili tofuati tu!… Na hakuna jini wala pepo mzuri, wote ni wabaya na wachafu. Zipo dini zinazofundisha kuwa wapo majini (mapepo) wazuri, na kwamba watu wanaweza kuwa nao na wakawaletea mafanikio na hata kuwalinda.

Huo ni uongo wa shetani asilimia mia, kwani shetani ndiye baba wa uongo..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.

Shetani hajawahi kuwa na urafiki wa kweli na mwanadamu, wala hajawahi kuwa na mapenzi na mwanadamu, kitu anachokipenda kutoka kwa mwanadamu ni utukufu tu!.. lakini hajawahi kumpenda mwanadamu, na hakuna unabii ya kwamba atakuja siku moja kumpenda mwanadamu, yeye ni adui wa mwanadamu wa milele.

Na Kama tu shetani asivyopendwa kuitwa shetani, bali anapendwa aitwe mungu, kadhalika hawezi kuruhusu mapepo yake yaitwe vibaya, kwa sifa mbaya?..atawatakasa tu!.. na anawatakasaje?..si kwa njia nyingine bali kwa njia za dini za uongo, zinazohubiri na kufundisha kuwa wapo mapepo wazuri.

Kwa urefu kuhusiana na pepo wachafu(majini) fungua hapa >>

MAJINI WAZURI WAPO?

Je umempokea YESU?.. kama bado ni nini kinakungojesha?

Bwana anarudi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Naliupata wenyeji huu kwa mali nyingi, maana yake nini (Matendo 22:28)

Jibu: Habari hii inamhusu Mtume Paulo, kipindi aliposhikwa na kufungwa akiwa Yerusalemu.. sasa ili tuelewe vizuri tuanze kusoma ule mstari wa 25

Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?

26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi

27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.

28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.

Wenyeji unaozungumziwa hapo ni “URAIA”.. Kwahiyo hapo kiswahili kingine cha andiko hili ni hiki .. “Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA URAIA HUU KWA MALI NYINGI”.

Zamani za kanisa la karne ya kwanza, ufalme uliokuwa na nguvu duniani, ulikuwa ni ufalme wa Rumi, na ndio uliokuwa unatawala dunia chini ya Kaisari. Hivyo kutokana na nguvu ya ufalme huo, basi hata raia wake walikuwa na nguvu, na heshima.

Raia wa kirumi (yaani Mrumi) alikuwa hawezi kuadhibiwa bila kushitakiwa, na haki zake zilikuwa zinalindwa sana kuliko raia wa Taifa lingine lolote duniani,..ilikuwa ni kosa kubwa kumhukumu Mrumi kabla ya kumsikiliza.

Sasa hapa Paulo alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa lakini kwaasili ni Mwebrania (yaani muisraeli), na hapa alikuwa amevunjiwa haki yake kama raia wa kirumi, na hivyo akida pamoja na jemedari wakaogopa, kwasababu ni kosa kumhukumu Mrumi kabla ya kumpandisha kizimbani na kumsikiliza.

Sasa swali la Msingi kwanini, Jemedari aseme Uraia wake kaupata kwa mali nyingi?

Zamani ili uwe Raia wa kirumi ni aidha uwe mzawa (yaani umezaliwa katika Taifa la Rumi) au Umeununua uraia.

Sasa kitendo cha kuununua Uraia hakikuwa rasmi, bali kilikuwa ni kwa njia ya rushwa, na waliopata uraia huo waliupata wakati wa sense, ambapo majina yako yaliongezwa katika orodha ya warumi kinyume cha sheria, baada ya kulipa pesa nyingi,

Na hapa huyu Jemedari aliyeitwa Klaudio Lisia (Matendo 23:26) anaonekana kumwambia Paulo kuwa Uraia wake “Aliununua” maana yake kwa asili hakuwa mrumi, bali alikuwa kuwa mtu wa Taifa lingine, huenda Ugiriki, kwasababu hilo jina la Pili la LISIA ni jina la kigiriki, lakini Paulo yeye alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa na si kwa kununua uraia.

Upo uraia mwingine ambao ni wa Mbinguni…huo haupatikani kwa fedha, wala mtu haupati kwa rushwa bali bali kwa kuzaliwa mara ya pili.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”

Je umeupata uraia huu wa mbinguni kwa kuzaliwa mara ya pili?.. kama bado ni nini kinachokusubirisha??

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

USIVAE HERENI

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa PETE MASIKIONI MWAKE, na kwa vito asema Bwana”.

Kabla ya kuvaa kitu, au kuiga mtindo fulani, hebu tenga muda kwanza kufuatilia asili ya kitu hiko kibiblia, kwasababu kuna vitu vingine asili yake ni mbaya, na isiyo na baraka kwa Mungu.

Hebu jiulize swali hili.. Mungu akuumbe na masikio yaliyo kamili, halafu akwambie au akuruhusu ukayatoboe masikio hayo, eti ili tu upendeze?..hivi jambo hilo ni kweli Mungu kaliagiza au kaliruhusu??.. au ni ujanja tu wa akili za watu! (walionyanyuliwa na ibilisi, Waefeso 4:14).

Sasa sikuhukumu wewe uliyetobolewa masikio, huenda si wewe kwa hiari ulifanya hivyo, bali walikutoboa tu ukiwa mchanga..na pia waliokutoboa huenda nao pia walipokea tu kwa waliotangulia, hivyo huenda kosa si lako wala la wazazi, bali la yule wa kwanza kuanzisha makosa hayo..

Lakini sasa baada ya kuelewa, si sawa kuendeleza hayo makosa kwa vizazi vyako, vile vile si sawa kuweka chuma au dhahabu katika matundu ya masikio yaliyotobolewa, kwani kwa kufanya hivyo bado utakuwa unaendeleza desturi hiyo.

Hebu tusome tena…

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa pete masikioni mwake, na kwa vito asema Bwana”.

Asili ya kujipamba kwa pete za masikioni (yaani kuweka hereni) ilikuwa NI KUJIWEKA TAYARI KWA KUVUKIZA UVUMBA KWA MABAALI… na baali si mwingine zaidi ya shetani mwenyewe/kusifa katika kinyago chake kingine.

Kwahiyo zamani mtu akijipamba kwa kutoboa masikio na kuweka hereni alikuwa aidha ametoka kuvukiza uvumba kwa baali au ndio anaenda kuvukiza uvumba kwa baali, na hereni zamani hazikuwa zinavaliwa tu na wanawake, bali hata na wanaume, na lengo lilikuwa ni hilo hilo kumvukizia uvumba baali.

Labda utauliza ni wapi tena pengine panapoonyesha hereni, zinahusishwa na ibada za miungu..

Mwanzo 35:2 “Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, ONDOENI MIUNGU MIGENI ILIYOKO KWENU, mjisafishe mkabadili nguo zenu. .

4 NAO WAKAMPA YAKOBO MIUNGU MIGENI YOTE ILIYOKUWA MIKONONI MWAO, NA PETE ZILIZOKUWA MASIKIONI MWAO, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu”.

Sasa shetani ni yule yule, na ibada zake ni zile zile, hazijabadilika……kama bado yupo kwenye makafara ya mang’ombe mpaka leo, na mambuzi, na bado waganga wake ni wale wale, na mavazi yao ni yale yale, na uchawi wake ni ule ule, unadhani uchawi wake katika HERENI (pete za masikioni) utakuwa umebadilika??.. Jibu ni la! Utakuwa ni ule ule tu.

Tafakari, tafakari mama, tafakari dada, tafakari kaka unayevaa hereni, kuambiwa usivae hereni sio kwamba unawekwa chini ya sheria, hapana!.. bali kinyume chake ndio UNAKUWA HURU… Lakini kuvaa hereni ndio sheria, kwani itakulazimu kila siku kuivaa kabla ya kutoka nje, na kubadilisha aina ya hereni leo hii kesho ile, sasa huoni kama hiyo ndio SHERIA???, na kutokuvaa hereni ndio uhuru??.

Ni kweli ukiacha kuzivaa utaonekana si mrembo kwa baadhi ya watu, lakini utakuwa umejiepusha na ibada za sanamu, ambazo zitakuzalia madhara mengine makubwa kiroho.

Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, sawasawa na 1Wakorintho 3:16, na 1Wakorintho 6:19.

Kwa jinsi tunavyozidi kuiweka kuwa mitakatifu, ndivyo Roho Mtakatifu anavyokaa ndani yetu, na ndivyo tunavyomfaidi Roho Mtakatifu kwa matunda yake yaliyotajwa katika Wagalatia 5:22.

Bwana akubariki sana.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

                          Rudi Nyumbani.

Print this post

Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?

Swali: Kulikuwa na sababu gani ya Bwana MUNGU kuuweka mti wa mema na mabaya katikati ya bustani ili hali anajua kuwa mti huo ndio utakaowakosesha Adamu na Hawa, kwanini Mungu asingeondoa, na kuubakisha tu ule mmoja wa uzima katikati ya bustani?


Jibu: Ni kweli inaweza kuonekana ni busara mti mmoja tu kuwepo pale bustanini lakini ukweli ni kwamba endapo Mti mmoja tu ungekuwepo pale bado MTI WA UZIMA, usingeeleweka na wala maana yake isingekuwepo..

Kwani ili kuuthibitisha wema lazima uwepo ubaya mahali fulani… kwasababu wema hauwezi kujilikana kama ubaya haujadhihirishwa, vinginevyo ule wema utaonekana ni kitu cha kawaida, lakini ukifunuliwa ubaya ndipo wema unapopata kujulikana na kueleweka.

Nuru haiwezi kujulikana kama ni njema na kitu kizuri, kama giza halipo.. lakini ili Nuru ipate sifa, na kuheshimika ni lazima giza liwepo mahali ili nuru ilishinde giza.

Vile vile Mungu aliuweka ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambao matunda yake ni MAUTI, ili kuuthibitsha MTI WA UZIMA ambao matunda yake ni UZIMA.

Adamu na Hawa wasingeweza kuelewa nini maana ya UZIMA kama kisingekuwepo kingine kinachoelezea/kuhubiri MAUTI, vile vile hata sisi leo tusingejua Uzima ni nini kama MAUTI isingekuwepo, vile vile hatuwezi kujua Amani ni nini, kama hatujawahi kusikia kuhusu vita, au kupitia vita..

Hatuwezi kujua umaskini ni nini kama hatujawahi kuona utajiri, vile vile hatuwezi kujua utajiri ni nini kama hatuwahi kuona au kupitia umasikini,.. hatuwezi kujua kuwa tuna afya kama hatujawahi kuona wagonjwa, wala hatuwezi kujijua kuwa tuna ugonjwa kama hatujawahi kuona wenye afya, au sisi wenyewe kuwa na afya, huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakipo, wala huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakijawekwa mahali kama mfano.

Hivyo utaona kuwa uwepo wa vibaya au vyenye kasoro ni ili kuvithibithisha vile vilivyo vizuri na visivyo na kasoro.. Na lengo la Mungu kuuweka mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya lilikuwa ni kuwapa kuelewa Adamu na Hawa Uzima ni nini, na thamani yake, na ili wauthamini na kuushika… na wala lengo lake si kuwatega!.

Hebu pia tengeneza picha miili yetu isingekuwa na maumivu, je unadhani ni nini kingetokea?…bila shaka hakuna mtu ambaye angehangaika kuutunza… hakuna mtu angeogopa kujikata na kisu, au kutembea peku kwenye miiba, au kunywa maji ya moto yale yanayotokota… lakini maumivu yamewekwa ili tujue na kutamani kuwa katika hali ya kutokuwa na maumivu na vile vile kuitunza miili yetu na kuushikilia uzima vizuri .

Hali kadhalika uwepo wa mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya ni ili kuuthaminisha mti wa UZIMA. Ili mtu ajue umuhimu wa UZIMA, na RAHA ya Uzima, faida za uzima.

Je wewe umempokea YESU, na kuoshwa dhambi zako? Kumbuka YESU ndiye njia ya Mti wa UZIMA, na yeyote anayempokea humpa matunda hayo na kuishi milele, ndani yake.

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.

Ufunuo 2:7 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu”

Bwana akubariki.

Kujua kwanini BWANA MUNGU awazuie wasile matunda ya Mti wa Uzima baada ya kula ya ujuzi wa mema na mabaya fungua hapa >>>

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je unaijua anwani ya msalaba?…na je unajua nguvu yake? Kama bado hujaifahamu basi leo ifahamu na anza kuitumia katika maombi yako, badala ya vitendea kazi vingine kama maji, chumvi na mafuta.

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.

20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”

Jina la YESU WA NAZARETI ndio ANWANI ya maombi ya kila Mkristo.

Umewahi kujiuliza kwanini haijaandikwa YESU MGALILAYA, au YESU MBETHLEHEMU mji ule aliozaliwa, badala yake imeandikwa YESU MNAZARETI?..na tena kwa lugha zote tatu (3), zilizokuu za dunia.

Kuna nini katika Nazareti?

Nazareti ndio mji uliotabiriwa na manabii kubeba utambulisho wa Masihi Mkuu ajaye… hivyo huo ni mji wa UTAMBULISHO KIBIBLIA.

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Kwahiyo tunapotaja jina la YESU na kuelekeza yule wa NAZARETI tumelenga kwenye shabaha yenyewe hivyo mashetani yanaondoka, magonjwa yanaondoka, dhambi inaisha nguvu, kwasababu ndiye Masihi halisi aliyetajwa.

Hebu tulione hili zaidi…

Wakati Bwana YESU anamtokea Sauli alipokuwa anaenda Dameski kwa ajili ya kuwaua wakristo, utaona hakujitambulisha kama YESU wa Galilaya, au YESU aliye mbinguni, badala yake alijitambulisha kama YESU Mnazaeti ijapokuwa yupo mbinguni.

Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.

7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?

8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, MIMI NI YESU MNAZARETI, ambaye wewe unaniudhi”.

Utaona pia Mitume wa Bwana YESU waliitumia hii anwani popote walipokwenda katika huduma zao.

Petro aliitumia alipokutana na yule kiwete aliyezaliwa katika hali ile..

Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.

7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.

8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.

9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu”.

Soma pia Matendo 2:22, Matendo 3:6, Matendo 4:10, Matendo 10:38, Matendo 26:9, Marko 1:24, Marko 16:6, Marko 10:47, Luka 24:9, Yohana 1:45, utazidi kuona jambo hilo.

Na hiyo pia ndio sababu Mungu aliruhusu Pilato aandike anwani ile juu ya msalaba… “YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”. Kwa lugha zote kuu, ikimaanisha kuwa anwani ya wokovu wa msalaba kwa mataifa yote na lugha zote ni jina la YESU WA NAZARETI.

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

Maana yake njili inayohubiri msalaba pasipo kuhusisha anwani ya jina la YESU ni uchawi, maombi yoyote yasiyohusisha anwani ya jina la YESU ni unashiri na ibada za sanamu.

Kama anwani hiyo ya jina la YESU WA NAZARETI hata baada ya Bwana kupaa bado anaitumia akiwa mbinguni, sisi ni akina nani tuifanye iieshe matumizi katika zama zetu?, na kuweka mafuta, chumvi, maji au majina yetu kama mbadala??.

Tumia jina la YESU, liamini jina la YESU WA NAZARETI epuka matapeli, na jina la YESU HALIUZWI, EPUKA MATAPELI!.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inaposema ndugu wa kunyonya inamaanisha nini (Matendo 13:1)?

Swali: Katika kitabu cha Matendo 13:1, tunamsoma mtu mmoja akitajwa kama ndugu wa kunyonya wa Herode, je maana yake nini?.


Jibu: Maana ya “Ndugu wa kunyonya” ni “mtu aliyelelewa katika familia fulani, tangu utotoni, alipokuwa akinyonya” kwa lugha nyingine amekuwa “adopted” tangu utotoni, (katika umri wa kunyonya).

Hivyo mtu kama huyu anahesabika kuwa kama mwanafamilia, na watoto wa familia hiyo watamhesabu kama ndugu yao wa kunyonya, kwani amekulia katika familia yao.

Hivyo huyu Manaeni alilelewa pamoja na Mfalme Herode, katika familia moja, ingawa hawakuwa ndugu wa damu, lakini tangu utoto walikuwa pamoja.

Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na MANAENI ALIYEKUWA NDUGU WA KUNYONYA WA MFALME HERODE, na Sauli”.

Lakini kulikuwa na kusudi kwanini habari zake ziandikwe katika biblia, ukizingatia ya kuwa ndugu yake, ambaye alikuwa ni Herode pamoja na maherode wote walikuwa ni wakatili sana, waliwaua wakristo na kuwapiga vita vikali, lakini huyu Manaeni ambaye ni ndugu ya Herode, yeye alikuwa wa tofauti, kwani alikuwa ni miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kugeuka na kuifuata Imani ya Kikristo, na kuwa miongoni mwa wasimamizi wa Imani katika kanisa la kwanza la watu wa mataifa, huko Antiokia.

Na kumbuka Antiokia ndiko jina la Ukristo lilikozaliwa, kwani hapo kabla waliomfuata YESU walikuwa wanaitwa wanafunzi tu.

Matendo 11: 26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia”

Sasa kufahamu kwa urefu ushuhuda alilolibeba Mtumishi huyu wa Mungu (Manaeni) na ujumbe tuupatao watu wa sasa katika Kanisa, fuatilia somo linalofuata…

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Uzao wa Ibrahimu unamilikije mlango wa adui? (Mwanzo 22:17)

Swali: Katika Mwanzo 22:17, MUNGU anasema kuwa uzao wa Ibrahimu utamiliki malango ya adui, sasa unamiliki vipi huo mlango wa adui?.


Jibu: Turejee…

Mwanzo 22:17 “katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”.

Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa Mzao wa Ibrahimu aliyebeba ahadi kamili za Ibrahimu ni BWANA YESU KRISTO.

Wagalatia 3:16 “Basi ahadi zilinenwa kwa Ibrahimu na kwa mzao wake. Hasemi, Kwa wazao, kana kwamba ni wengi, bali kana kwamba ni mmoja, Kwa mzao wako, yaani, Kristo”.

Wengine wote, akina Isaka na Yakobo,(yaani Israeli katika mwili). walibeba sehemu za baraka hizo lakini si zote.. Iliweza kumiliki baadhi ya milango ya adui katika mwili lakini si yote.

Sasa kwa namna gani Israeli ya mwilini ilimiliki malango ya adui?

Kwa njia ya vita: kumbuka zamani miji ilikuwa inazungukwa na kuta, na mageti makubwa, hivyo nguvu na udhaifu wa mji ulikuwa katika mageti ya mji, hivyo lango la mji likitekwa na kumilikiwa basi tayari ule mji umeshatekwa,

Na Mungu aliwapa ahadi wana wa Israeli kwa jinsi ya mwili, kumiliki mlango/malango ya adui, ndio maana waliweza kuangusha miji ya kanaani iliyo mikubwa na yenye nguvu, na hatimaye kuiteka nyara miji hiyo.

Lakini mbali na hayo, lipo Lango ambalo Israeli ya mwilini asingeweza kumiliki, na mlango huo si mwingine zaidi ya ule wa MAUTI na KUZIMU.

Na kawaida mtu mwenye miliki ya mlango, ni yule mwenye FUNGUO ZA HUO MLANGO.

Mtu akikosa funguo hawezi kuwa na milki ya mlango wowote ule.

Hivyo Israeli ya mwilini alikuwa na Funguo za kufungua Mageti ya Wakaanani na Yeriko na mageti ya Wafilisti na kuwapiga na kuwatoa katika ardhi yao, lakini hakuwa na FUNGUO za MAUTI na KUZIMU,

Hakuweza kuzuia watu wasiingie kuzimu wala kuwatoa huko na kuwarudisha tena juu sawasawa na Ayubu 7:9.

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa”

Hivyo Israeli ya mwilini haikuweza kumiliki malango yote…. alikwama hapo kwenye Mauti na Kuzimu, sawasawa na maneno ya Bwana Mungu katika Ayubu 38:17.

Ayubu 38:17 “Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?”

Sasa swali la msingi, kama Israeli ya mwilini imeshindwa kumiliki milango hiyo, ni nani basi mwenye uwezo huo sawasawa na Mwanzo 22:17?.

Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu kile cha Ufunuo 1:17-18.

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU”

Huyo mwenye hizo funguo za Mauti na kuzimu, ndiye mwenye milki ya Mlango wa Adui.

Maana adui wa kwanza na wa mwisho wa mwanadamu ni MAUTI ambaye analetwa na dhambi, huyu ndiye aliyeanza na Adamu pale Edeni na atamalizwa na Mwana wa Adamu siku ya mwisho.

1 Wakorintho 15:26 “Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti”.

Na matokeo ya Mauti katika dhambi ni KUZIMU.

Kwahiyo YESU KRISTO ndiye mwenye funguo za Mauti na Kuzimu.

Wafu wote wanamilikiwa na Bwana YESU, na KUZIMU ipo chini ya mamlaka ya Bwana YESU, utauliza kivipi?..Mtu anayekufa sasa katika dhambi si shetani anayemtupa katika lile shimo la kuzimu, bali mamlaka ya YESU kupitia malaika wake ndio wanaowatupa watu katika lile shimo la kuzimu.

Kwasasa shetani hana mamlaka yoyote na wafu, hizo milki alishapokonywa na Bwana siku ile aliposhuka kuzimu, na hayo malango sasa yanamilikiwa na YESU KRISTO (Mkuu wa Uzima).

Warumi 14:9 “Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki waliokufa na walio hai pia”.

Nguvu za Bwana YESU kwasasa ni KUU SANA!!!, ukitaka kufahamu kwa sehemu kiwango cha nguvu alizonazo juu ya Mauti, ikumbuke ile kauli aliyosema..

Yohana 10:17 “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18 Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu”.

Tafakari mtu anakuambia anao uwezo wa kuitoa roho yake na kuirudisha tena,…yaani kama vile mtu anavyozima taa na kuiwasha….na tena anasema “hakuna mtu aniondoleaye”..Maana yake Bwana YESU hakuuawa, bali yeye mwenyewe ndiye aliyeitoa roho ndani ya mwili wake.

Ndio maana akasema yale maneno…

Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”

Sasa mtu aliyeuawa hawezi kusema maneno hayo…lakini Bwana YESU hakuuawa bali yeye mwenyewe aliiondoa roho yake katika ule mwili, na ndio maana hata wale askari walishangaa imekuwaje amekufa mapema vile kabla ya kuvunjwa miguu.

Sasa ni kweli yapo maandiko yanayosema kuwa Bwana YESU aliuawa, lakini fahamu kuwa popote yanapotaja hivyo ni kuitia nguvu mada iliyoanza, lakini ukweli ni kwamba Bwana hakuuawa na mtu bali aliitoa roho yake mwenyewe.

Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Mlango wa Adui wa Mauti, Bwana anao funguo zake.

Hivyo basi tukitaka mauti na kuzimu zisiwe na nguvu juu yetu, hatuna budi kumwendea yeye mwenye funguo hizo, na hatimaye atupe wokovu.

Lakini tukimkataa yeye mwenye funguo hizo, tujue kuwa hatutaokoka hata kidogo.

Malango ya adui, ni malango ya kuzimu, na ni malango ya mauti na yote chanzo chake ni dhambi.

Je umempokea Bwana YESU na kuoshwa dhambi zako?.

Kama bado unasubiri nini?.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Adamu na Hawa waliokoka?

Je mtu anaweza kupoteza wokovu?

USIWE ADUI WA BWANA

ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni msiba gani unazungumziwa katika 1Petro 4:12?.

Jibu: Turejee…

1Petro 4:12 “Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho”.

Neno “Msiba” kama linavyozungumziwa hapo halimaanishi ule Msiba wa mtu kufa. La! Bali neno hilo limetumika hapo kuwakilisha “jaribu zito”.

Kama tu lile lililompata yule mwanamke aliyetokwa na damu mda wa miaka 12.

Marko 5:27 “aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake;

28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.

29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule…………………

33 Na yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka, akijua lililompata, akaja akamwangukia, akamweleza kweli yote.

34 Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, enenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena”

Hivyo tukirejea andiko hilo la 1Petro 4:12 msiba unaozungumziwa hapo “Ni jaribu zito”.

Kwahiyo kwa kiswahili kingine mstari huo unaweza kusomeka hivi…

“Wapenzi, msione kuwa ni ajabu lile jaribu zito lililo kati yenu, linalowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho”

Na msiba huo (au jaribu hilo)…Ni “Kuteswa kwaajili ya Kristo”…tunalithibitisha hilo katika mstari unaofuata wa 13.

1 Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia”.

Soma pia 1Wathesalonike 3:7 unataja msiba wa dhiki katika Kristo.

Na hata leo wote watakaotaka kuishi maisha ya kumpendeza MUNGU na utauwa, watakutana na misiba ya Kuudhiwa kwaajili ya imani.

2 Timotheo 3:12 “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa”.

Lakini ukiishi maisha ya kuupenda ulimwengu, basi ulimwengu nao utakupenda kwasababu ulimwengu unawapenda walio wake.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

PIGO LA KUFA KWA WAZALIWA WA KWANZA

NYWELE ZAKO ZIKUFUNDISHE, SAUTI YA MUNGU.

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

MTAKENI BWANA NA NGUVU ZAKE.

HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

MRUDI MWANAO NAYE ATAKUSTAREHESHA

Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha”.

Kumrudi mtoto sio “kumwadhibu tu”. Bali pia kumrekebisha (Kauli zake na njia zake).

Ni kweli maandiko yanaruhusu kumwadhibu mtoto kwa kiboko pale anapokosea, lakini hiyo iwe hatua ya mwisho baada ya kuona harekebishiki kwa maneno..

Katika hatua hiyo maandiko yameruhusu kutumia mapigo kwa huyo mtoto, ili kuiokoa roho yake na kuzimu.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Soma pia Mithali 22:15.

Wengi wanaogopa kuwaadhibu watoto wao kwa mapigo wakiamini kuwa watapata madhara ya kisaikolojia na hata kiafya.. pasipo kujua kuwa hapo biblia imesema ukimpiga “hatakufa”..maana yake Mungu atazuia madhara yote ya kiafya, ikiwa lengo lako si lingine zaidi ya kumjenga.

Lakini kabla ya kufikia hatua hiyo ya matumizi ya fimbo, ni muhimu kuanza na maonyo, na makemeo.

Maana yake kama mtoto amekosea kusema ni lazima arekebishwe kusema kwake mapema, kwasababu watoto wanasikia mambo mengi na kuyachukua tu pasipo kupambanua.

Tuliwahi kufanya maombi sehemu fulani, tukakuta mtoto wa miaka 5 anatukana matusi makubwa na anarudia tusi hilo hilo moja, mara ya kwanza tulidhani ni mtoto ana mapepo, lakini baadae tuligundua kuwa hana mapepo na hata matusi aliyokuwa anayatamka alikuwa hajui maana yake, alitamka tu akidhani kuwa ni maneno ya kawaida, pasipo kujua kuwa alikuwa anatukana.

Sasa mtoto ni kwamba alisikia hayo matusi pengine kwa watoto wenzake anaocheza nao, wasio na maadili na yeye akidhani ni neno la kawaida akalichukua na kulitumia popote alipoona mazingira hayampendezi.

Sasa mzazi hakuchukua jukumu sahihi la kumrekebisha, badala yake tu alianza kumpiga kila alipotaja hilo neno akidhani kuwa anafanya makusudi, na hata sisi tulipofika alitukana na mamaye alimfinya, lakini alipolia bado aliendelea kutukana.

Mama alidhani mtoto anakiburi na mkorofi, kumbe mtoto alilia akijitetea kwa kudhani kuwa lile neno ni sahihi kutamka mahali pale.

Sasa laiti kama mzazi angepata wasaa wa kumketisha na kumwonya na kumwambia anachokisema si sahihi na hakifai, kabla ya mapigo… mtoto angeelewa na kubadilika.

Kwahiyo ni muhimu kuwasikiliza watoto wanasema nini na kuzirekebisha kauli zao mapema,

Ni vizuri kuangalia watoto wako wanachokiangalia na kukikosoa mbele yao kama hakifai…

Pia ni muhimu kufuatilia michezo yao wanayoicheza na kuikemea mapema mbele yao,…..kwani wao ni kuiga tu siku zote…ni vichache wanabuni wenyewe..

Vingi wanaiga kutoka kwa watu pasipo kupambanua, na wanajifunza kutoka kwa watu wanaowazunguka, ikiwemo wanafunzi wenzao mashuleni na pia kupitia Tv.

Kwahiyo kagua maisha ya watoto wako, na “warudi mapema”..wala hawatakuchukia, au kuwashusha kisaikolojia bali utawajenga kwa maisha yao ya baadae..

usipowarudi mapema na wakikua katika misingi hiyo itakuwa ni ngumu kubadilika ukubwani, kwani ile dhambi wameanza kuifanya tangu utotoni na hivyo hawawezi kushawishika kuona madhara yake ukubwani, na ili hali hawakuona madhara yake utotoni.

Mtoto akiwa na kiburi au mtukutu basi mkanye kila wakati, na panapobidi basi tumia kiboko ila usimwache akakua na hiyo tabia.

Na pia akiwa hasikii, tafuta kila namna awe anasikia, usiache na kusema huyu karithi hiyo tabia kwa watu fulani waliotangulia..

Na pia mfundishe kauli za kibiblia, na kuomba, mfundishe

salamu za kibiblia, na misemo ya kibiblia…akue katika hiyo hata kama bado hajaweza kuipambanua lakini mfanye akariri hivyo hivyo kwani itakuja kumsaidia mbeleni kwasababu itakuwa moyoni mwake.

Kwa kumlea hivyo biblia inasema baadaye atakustarehesha..

Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha”.

Kustarehesha maana yake “hatakuja kukusumbua huko mbeleni”…

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIOGOPE KUMWADHIBU MWANAO.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Lango la samaki lilikuwaje? (Sefania 1:10)

Swali: Hili lango la samaki linalotajwa katika Sefania 1:10 lilikuwaje na lilikuwa linahusika na nini?.


Jibu: Yalikuwepo malango kadhaa ya Kulikuwa mji wa Yerusalemu nyakati za zamani, ambayo yalizunguka pande zote za mji.

Baadhi ya malango hayo ni  “Lango la samaki”,  “Lango la kale”, “Lango jipya”Lango la Efraimu” na “Lango la kondoo”, ambalo liitumika kupitishia kondoo katika mji, kwa maelezo marefu juu ya lango hilo fungua hapa >>>

Mlango la kondoo ulikuwaje?(Yohana 5:2)

Lakini kuhusu “Lango la Samaki” turejee maandiko.

Sefania 1:10 “Na katika siku ile, asema BWANA kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani”.

Hili “Lango la Samaki” halikuwa na matumizi kama lile “Lango la Kondoo”…kwamba linatumika kupitisha samaki ndani ya mji.

La! Bali ni lango la mji wa Yerusalemu ambalo lilikuwa upande Kaskazini-magaribi, karibu na “Soko la Samaki”..Hivyo liliitwa jina hilo kufuatia soko la samaki lililokuwa karibu na lango hilo.

Ingawa pia kwasababu lilikuwa upande wa kaskazini, wafanya biashara kutoka Galilaya walilitumia hili, na wengi waliotoka Galilaya walikuwa ni Wavuvi..

Hivyo lilitumika pia na wafanya biashara wa samaki, lakini halikuitwa kwasababu hiyo bali kutokana na soko hilo la samaki lilikokuwa karibu na lango hilo.

Lango la samaki kwanza limeanza kuonekana kipindi cha Mfalme Manase ambaye alikuja kuujenga ukuta wa nje wa mji wa Daudi (Yerusalemu), aliujenga upande wa magharibi mpaka kufikia mlango huo wa samaki.

2 Nyakati 33:12-14 “Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi BWANA, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.

13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba BWANA ndiye Mungu.

14 Hata baada ya hayo akaujengea mji wa Daudi ukuta wa nje, upande wa magharibi wa Gihoni, bondeni, hata kufika maingilio ya LANGO LA SAMAKI; akauzungusha Ofeli, akauinua juu sana; akaweka maakida mashujaa katika miji yote ya Yuda yenye maboma”.

Baada ya miaka mingi kupita, tunakuja kusoma, kipindi ambacho mji wa Yerusalemu umebomolewa na Nehemia amerudi kuujenga ukuta, tunaona biblia inataja kuwa sehemu ya ukuta ya upande wa “Lango la samaki” ulijengwa na wana wa Senaa..

Nehemia 3:3 “Na lango la samaki wakalijenga wana wa Senaa; wakazitia boriti zake, wakaisimamisha milango yake, na vyuma vyake, na makomeo yake”.

Utaona tena lango hilo linatajwa kipindi cha mji kuwekwa wakfu (Nehemia 12:39).

Je umempokea Bwana YESU?..Je unafahamu kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU kwa pili?.

Je akija leo na kukukuta hivyo ulivyo utakwenda naye??

Bwana atusaidie sote.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post