Je Imani yako imefifia?, je upendo wako umepoa?, je Amani yako imepungua?, na haki yako imepoa?.. Na hujui cha kufanya na ndani bado una haja sana ya kuwa na mambo hayo?.. Basi suluhisho lipo ndani ya biblia.
Ifuatayo ni kanuni moja nyepesi ya kurejesha joto la ROHO MTAKATIFU ndani yako. Kumbuka mtu aliyejaa Roho Mtakatifu ataonyesha matunda yafuatayo…
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi;…”.
Ikiwa mambo haya yalikuwa ndani yako lakini sasa huyaoni tena, au ikiwa hauna kabisa, basi tumia kanuni ifuatayo kuyarejesha/kuyajenga ndani yako.
KAA KARIBU NA WATU WATU WANAOMWITA BWANA.
Watu wanaomwita Bwana, kwa lugha nyingine ni watu waliookoka kikweli kweli,…Utauliza kwa namna gani?…Tusome maandiko yafuatayo..
2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.
Hapo mwisho anasema, ukatafute haki, Imani na upendo na amani “pamoja na wale wote wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Kumbe! Haki inapatikana kwa watu wanaomwita Bwana kwa dhamiri safi, kumbe tukikaa na watu waliomaanisha kumwita Bwana na kumtafuta basi Amani tutaipata, na upendo na Imani.
Kama maandiko yasemavyo kwamba “chuma hunoa chuma, Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake” (Mithali 27:17). Vivyo hivyo na sisi tunapokaa na watu wenye kumaanisha kumtafuta Mungu basi ule moto ulio ndani yao atahamia na kwetu pia.
Lakini tukijitenga na kubaki wenyewe, au tukijumuika na watu wengine wasio na nia ya dhati kumtafuta Bwana, ni ngumu kuuwasha ule moto wa Roho ndani yetu!, tutabaki kama tulivyo!.. Kanuni ni kukaa pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi!…Vile vile tunapojitenga na kuamua kukaa peke yetu kwa muda mrefu ni pia ni hatari!!.. Imani, amani, upendo na haki yako vinaweza kuathirika pakubwa.
Sasa tunawapatia wapi watu wamwitao Bwana kwa moyo safi?.
1.Katika kanisa lililo hai.
Hii ni sehemu pekee ambayo utawapata watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, jiunge na kanisa la kiroho lililo karibu nawe, au hata lililo mbali ikiwa lililo karibu nawe halina utakatifu. Jumuika na watu hao, katika utii na unyenyekevu, na katika ibada zote, na hapo Roho Mtakatifu atakujenga ndani yako na kukujaza nguvu zake, utaona Imani yako inapata nguvu, upendo wako uliopoa unawaka tena, haki yako iliyopotea inarudi na Amani yako pia inahuika upya, na ifanye hiyo iwe desturi yako daima.
Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine;..”.
Na utajuaje kanisa hilo, ni la kiroho?.
Kigezo cha kwanza ni mwonekano wa nje wa waabuduo wa mahali hapo!, ukiona mwonekano na mazungumzo ya waabuduo si ya kiMungu, kwamba wanazungumza kidunia na wanavaa kidunia, kiasi kwamba hauoni tofauti na mtu anayeenda disko na anayeshiriki mahali hapo, basi tuchukua tahadhari hapo si sehemu salama!.
Vile vile mafundisho yanayofundishwa mahali pale kama hayalengi TOBA, na UJIO wa PILI wa BWANA YESU, na UTAKATIFU wa MWILINI na ROHONI, pia hapo si sehemu salama, lakini kama kanisa lina vigezo hivyo vya Utakatifu wa kimafundisho na kimwonekano, basi ndani yake watakuwepo watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, kaa hapo na utaona mabadiliko makubwa ya kiroho ndani yako.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.
Ikiwa wewe ni kijana basi fahamu basi fahamu mambo yafuatayo.
1.MAWAZO MABAYA YANAANZIA UJANANI.
Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya”.
Mawazo ya kuidharau injili, mawazo ya ukaidi wa moyo na kiburi cha uzima yanaanzia ujanani.
Yeremia 22: 21 “Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako TANGU UJANA WAKO, KUTOKUITII SAUTI YANGU”.
2. MUNGU ANATAFUTWA UJANANI NA SI UZEENI!.
Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.
Maana yake katika uzee “haitawezekana kabisa” kumtafuta Mungu kama utapuuzia wito wa Mungu katika ujana wako!!!. Wakati wa Ujana ndio wakati wa kujifunga NIRA YA MUNGU iliyotajwa na BWANA YESU katika Mathayo 11:29.
Maombolezo 3:27 “Ni vema mwanadamu aichukue NIRA WAKATI WA UJANA WAKE.
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake”.
3. KAMA UTACHAGUA ANASA, BASI FAHAMU KUWA SIKU YA MWISHO UTASIMAMA HUKUMUNI.
Mhubiri 11:9 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya KWAMBA KWA AJILI YA HAYO YOTE MUNGU ATAKULETA HUKUMUNI”
Maana yake kama utachagua uzinzi katika ujana wako, au ulevi, au anasa nyingine yeyote basi pia jiweke tayari kusimama mbele ya kiti cha hukumu siku ile ya mwisho, ambapo maandiko yanasema kila mtu atatoa habari zake mwenyewe (Warumi 14:12), na tena kila neno la upuuzi litatolewa hesabu yake siku ile ya hukumu (Mathayo 12:36).
4. NEEMA YA WOKOVU HAIKUBEMBELEZI.
Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 MWENYE KUDHULUMU NA AZIDI KUDHULUMU; NA MWENYE UCHAFU NA AZIDI KUWA MCHAFU; NA MWENYE HAKI NA AZIDI KUFANYA HAKI; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”.
Ikiwa umechagua uchafu!, basi usiufanye kidogo!..ufanya sana, lakini kama umechagua USAFI, basi JITAKASE SANA, usiwe hapo katikati (vuguvugu!)..
5. UTAKAPOKUWA MZEE UTAPELEKWA USIKOTAKA.
Yohana 21:18 “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”.
Uhuru ulionao si wa Daima, ipo siku utaisha, na wengine watakuwa na mamlaka juu yako…….
Je wewe kama kijana sasa umejipangaje?..je unawaza nini katika ujana wako huu? au unafikiri nini?…Kwanini usiamua kumgeukia Muumba wako leo!, na kuachana na udunia, na tamaa za ujanani, ambazo hazina faida yoyote Zaidi sana zina hasara nyingi?
2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.
Bwana Yesu akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Ikiwa unahitaji msaada wa kuokoka na ubatizo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapo chini.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
Je! Mke wa ujana wako ni yupi kibiblia?
ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?
Jibu: Turejee,
Yohana 4:19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 Lakini SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.
Maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli, ni KUMFANYIA MUNGU IBADA, KATIKA ROHO MTAKATIFU NA KATIKA KWELI YA NENO LAKE.
Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE…”
Sasa BWANA YESU aliposema kuwa “SAA INAKUJA”, alimaanisha kuwa kuna kipindi kinakuja mbeleni, ambacho waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, na wakati huo si mwingine Zaidi ya ule wa Pentekoste. Kipindi ambacho Roho Mtakatifu atamwagwa juu ya kanisa kwa mara ya kwanza, baada ya BWANA YESU kuondoka!.
Huo ndio uliokuwa mwanzo wa watu kumwabudu Baba katika roho na kweli. (Matendo 2:1-15)
Lakini pia aliposema kuwa..“NA SASA IPO”…. maana yake hata huo wakati tayari Baba ameshaanza kuabudiwa katika roho na kweli. Na aliyekuwa anamwabudu baba katika ROHO NA KWELI ni yeye mwenyewe BWANA YESU KRISTO. Kwasababu tayari alikuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, ambaye alipoondoka ndipo akammwaga juu ya kanisa.
Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.
Na hata sasa tupo kipindi ambacho Neema ya Roho Mtakatifu bado ipo duniani kwa kila anayemwitaji sawasawa na Matendo 2:38, Na kumbuka Roho Mtakatifu pekee ndiye funguo za mtu kumwabudu Mungu katika roho na kweli, na pasipo yeye haiwezekani kumwabudu Mungu katika roho.
Kwa somo refu lihusuyo jinsi ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”
Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
Kama mwanamke uliyeokoka. Fahamu kuwa una wajibu wa kujiombea wewe, kuombea jinsia yako, na kuliombea Kanisa la Kristo kwa ujumla. Huu ni mwongozo wa kipengele muhimu vitakavyokusaidia katika maombi yako. ambavyo kama utakuwa ni mwombaji wa mara kwa mara katika maeneo hayo, basi unajijengea mazingira ya kuwa mwanamke bora, mama bora, na zaidi sana mtumishi bora wa Bwana katika mwili wa Kristo.
Mwongozo huu unaweza kuutumia pia muwapo wanawake wawili au watatu katika kikundi chenu cha maombi, au kanisani. Na hivyo kila kipengele tenga muda wa kutosha kuomba.
NANGA: Zaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;”
Mfano wa wanawake hawa alikuwa ni Loisi.
NANGA: 2Timotheo 1:5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo
NANGA: Yeremia 9:17 Bwana wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje; 18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji. 19 Maana sauti ya maombolezo imesikiwa toka Sayuni, Jinsi tulivyotekwa! tulivyofadhaika sana! Kwa sababu tumeiacha nchi, kwa kuwa wameangusha makao yetu.
NANGA: Luka 10:39 Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.
NANGA: 1Petro 3:4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
NANGA: 1Petro 3:6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote
NANGA: 1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani
NANGA: Luka 8:3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao
NANGA: Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye
NANGA: Luka 1:6 Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiendelea katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama. 7 Nao walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili ni wazee sana
NANGA: Kutoka 15:20 Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza. 21 Miriamu akawaitikia,Mwimbieni Bwana ,kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini
NANGA: Soma – 2Samweli 21, yote
NANGA: Luka 24:22 tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, 23 wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai
PIA OMBA…
NANGA: 2Yohana 1:1 Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli;
NANGA: (Soma Kutoka 1:15-19)
NANGA: Ruthu 1:16 Naye Ruthuu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; 17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe name
NANGA: Luka 2:36 Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. 2.37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba
NANGA: Luka 2:51 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. 51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake
NANGA: Luka 10:40 “Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi;..”
NANGA: Waamuzi 4:4 Basi Debora, nabii mke, mkewe Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule. 5 Naye alikaa chini ya mtende wa Debora, kati ya Rama na Betheli, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu; wana wa Israeli wakakwea kwake, awaamue
NANGA: Luka 15:8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? 15.9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.
NANGA: Soma (Marko 12:42, 1Wafalme 17:12, Luka 7:11)
OMBA PIA…
PIA OMBA HIZI TABIA ZIONDOKE NDANI YAKO NA WANAWAKE WOTE…
Kwa ushauri/ Msaada/ Maombezi /Ratiba za ibada, wasiliana nasi kwa mawasiliano haya;
Na, Mwl Denis & Devis Julius
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?
SWALI: Nini maana ya Mithali 21:1
“Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo”.
JIBU: Kuna mithali inayosema “maji hufuata mkondo”. Ikiwa na maana, palipo na mfereji kule kule unapoelekea ndipo maji nayo huelekea. Mfano ukielekeza mrefeji shambani mwako, basi maji yale yataelekea huko si kwingineko, ukielekezea mfereji nyumbani mwako, basi maji yatakuja ndani mwako. Kamwe maji hayajiamulii pa kuririkia.
Vivyo hivyo na Mungu, ndivyo anavyofananisha mamlaka yake juu ya wafalme na wakuu wa dunia hii. Kwamba mashauri yao, hawajiamulii tu peke yao kwa kujitakia. Kwamfano utakumbuka kuna wakati Mungu alimnyanyua Moyo Koreshi mtawala wa Uajemi ili awape ruhusu wayahudi warudi katika nchi yao wakamjengee nyumba.
Ezra 1:1 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema, 2 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; 3 Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu. 4 Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu
Mungu huyo huyo ndiye aliyemfanya mfalme Nebukadreza kuwa na moyo mkatili ili awachukue watu wake utumwani kwasababu ya makosa yao.(Yeremia 27:6, 43:10)
Mungu anaweza kuwatumia watawala kuadhibu taifa, au kuwabariki watu wake. Hii ni kuonyesha kuwa hakuna tawala yoyote katika hii dunia inamilikiwa na fikra za mwanadamu asilimia 100, bali mengi ya mashauri ya wakuu hutoka juu mbinguni, au yameruhusiwa na Mungu. Wao ni kama maji tu yanayofuata mkondo wa kusudi la Mungu.
Ndio jambo ambalo Mungu alimwambia Mfalme Nebukadreza kwamba “aliye juu ndiye anayetawala”(Danieli 5:21) lakini yeye alidhani ni uongo, mpaka siku alipoondolewa kwenye ufalme wake kwa miaka 7, na kurudishwa baadaye.
Hivyo, jambo hili, sio tu la viongozi wa kidunia, lakini pia hata wa kanisani. Ikiwa kanisa ulilopo linasimamia kweli na utakatifu na Kristo Yesu ndio kiini cha fundisho lao, basi waheshimu sana viongozi wako, kwasababu si kila shauri linalotoka kwenye vinywa vyao, ni wao wamefikiria. Wao ni kama maji tu yaliyomwagwa kwenye mfereji, ili kukuongoza wewe. ukishandana nao, au ukipuuzia kuongozwa nao, wakati mwingine unapingana na maamuzi ya Mungu wako bila kujijua.
Waheshimu viongozi wako wanaokulea kiroho, kama vile unavyowaheshimu watawala ya kidunia.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.