Category Archive Home

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

Habari za Elifazi, Sofari, na Bildadi tunazipata katika kitabu cha Ayubu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka kuwa  walikuwa ni marafiki wa Ayubu  wa karibu sana waliokuja kumlilia pale alipopatwa na yale matatizo ambayo tunayoyasoma kwenye biblia. Lakini kabla ya hao kuja tunasoma pia Ayubu alikuwa ni MWELEKEVU sana aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu wa kila namna, na baada ya shetani kuona wivu juu yake,ndipo akaamua kwenda kumshitaki kwa Mungu, ajaribiwe ili aiache Imani yake. Kama tunavyofahamu, baadaye Mungu alimruhusu shetani amjaribu Ayubu.  Na ndipo shetani akaenda kuzimu kuandaa MAJARIBU yake mazito MATATU(3), ambayo katika hayo alipata uhakika kabisa kwamba Ayubu hawezi kunusurika ni lazima amkane Mungu na kuachana na uelekevu wake. Embu tuyapitie kwa ufupi.

Jaribu la kwanza lilikuwa ni la nje ya mwili wake na nafsi yake: 

 Hili lilihusisha  vitu vyote vilivyomzunguka Ayubu, vitu kama mali zake, wanyama wake, biashara zake pamoja na watumwa wake, n.k. Hawa wote shetani aliwapiga kama tunavyosoma habari katika Ayubu sura ya 1,  lakini hakuishia hapo alizidi kupiga kufikia hatua  kuwaua mpaka na watoto wake, na kumfanya Ayubu abaki peke yake, Lakini shetani alipoona hayo majaribu  bado hayamtikisi  Ayubu kwa namna yoyote zaidi ya yote aliishia kulibariki jina la BWANA. ibilishi akakusudia kubadilisha kinyago na kuamia kwenye ngazi ya juu iliyo nzito  zaidi. (lile Neno linatimia mtu hujaribiwa kulingana na Imani yake.)

Jaribu la Pili lilikuwa ni katika mwili wake: 

Tunasoma shetani alianza kumpiga Ayubu kwa magonjwa ya ajabu, majipu yaliyozuka mwili mzima yalimfanya Ayubu kufikia hatua ya kukonda sana na kukaa kwenye majivu muda wote akijikunia vigae. Kumbuka hili ni jaribu baya zaidi kuliko lile la kwanza kwasababu hili lilimuhusu yeye moja kwa moja. Afya yake ilidorora ghafla hivyo aliona kama mlango wa mauti unamwita muda wowote. Lakini pamoja na hayo Ayubu aliushikilia uelekevu wake, hatua hii ndiyo iliyomfanya hata mke wake Ayubu amkufuru Mungu, kwa kuona kuwa huyo Mungu waliyekuwa wanamtumainia kwa hatua hiyo waliofikia sasa hana msaada wowote kwao, kwa mume wake na kwa familia yake, Hivyo hakuna sababu ya kumtumikia tena. Lakini alizidi kuvumilia kwa muda mrefu na shetani alipoona ameshindwa, akaamia kwenye hatua nyingine ya juu zaidi ambayo ndiyo ngumu na ya hatari kuliko zote kiasi kwamba ingekuwa ni rahisi Ayubu kuchukuliwa na shetani kama asingesimama kikamilifu na Mungu wake. Hii ndio silaha ya mwisho shetani anayoitumia kuwamaliza watu wa Mungu. Na hakuna nyingine iliyojuu ya hiyo.

Jaribu la Tatu lilikuwa la rohoni: 

Kule Ayubu alipokuwa anapashikilia ndipo, hapo hapo shetani alipopajia. Kumbuka kitabu cha Ayubu sehemu kubwa kinaeleza juu ya hili jaribu la tatu, ambalo ndio msingi na kila mtu anapaswa afahamu kwasababu hapo ndipo siri hii ilipokaa, (hivyo unaposoma biblia soma kwa kujifunza vinginevyo masomo makuu na ya msingi yaliyo ndani yake yatakupita kama utakuwa unasoma tu kama gazeti). Sasa hapa tunaona ni mapambano ya moja kwa moja kati ya Shetani na Ayubu. Sasa kama tunavyosoma mara baada ya Ayubu kuzidi kushikilia msimamo wake na Mungu wake licha ya kwamba ana magonjwa na kufiwa na watoto wake, lakini bado yupo na Mungu wake. Shetani ndipo sasa akaingia kazini kwa kawatia mafuta watumishi wake wa uongo, ili waende kumgeuza moyo Ayubu kwa mafundisho ya udanganyifu. Na hawa si wengine zaidi ya ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI.

Hawa walikuwa ni marafiki zake na Ayubu wa Karibu, ni watu pia waliomcha Mungu lakini sio kwa kiwango cha Ayubu. walikuwa ni Wazee wenzake, washauri wenzake, ambao pengine kwa wakati wakiwa pamoja waliweza kuwafundisha  hata watu wengine njia za haki, na ukamilifu. Walipata sifa nzuri kwa Ayubu na ndio maana Ayubu aliweza kuwachagua wao tu! kuwa kama marafiki zake na washauri wake wa karibu. Lakini katika hatua kama hii walionekana kama wapo kinyume na Ayubu. Hii inadhihirisha kuwa mtazamo wao juu ya UKAMILIFU ulikuwa ni tofauti na wa AYUBU. Sasa kama tukichunguza habari zao kwa karibu tunaona moja kwa  moja kwa kumtazama Ayubu katika hali aliyokuwa nayo wakaanza kumuhukumu kuwa, hakika kuna mahali amemkosea Mungu. Lakini sababu zao walizozitoa za Ayubu kumkosea Mungu hazikuwa za “rohoni” bali za nje tu, lakini wenyewe waliangalia vya “mwilini” wakilinganisha na vya rohoni (kwamba ndio kigezo cha kukubaliwa na Mungu). Na hii ndio sababu kubwa iliyowafanya wapishane na Ayubu.

Sasa ukitazama moyo wa Ayubu utaona yeye alijua kuwa ushahidi mkubwa wa kukubaliwa na Mungu upo katika moyo wake(uhusiano binafsi alionao na Mungu wake, na si vinginevyo.) pasipo kujali anapitia hali ya namna gani ya nje! iwe ni umaskini, shinda, njaa, uchi, magonjwa n.k. na ndio maana vilipotokea aliweza kustahimili kwasababu alijua ndani ya moyo wake hakijaharibika kitu, hajaona kama amefanya  jambo la kumkosea Mungu. Uwepo wa Mungu ndani yake ulikuwa upo pale pale. Lakini wale marafiki zake watatu ambao wao walitumiwa na shetani kutenda kazi ile, walitazama kwa jicho lingine lisilo la ki-Mungu, na kuhitimisha kwamba kigezo pekee cha Mtu kukubaliwa na Mungu, ni kufanikiwa katika mambo yote, afya, familia, mali,mifugo  umri, n.k.basiii!!! sasa ukiona umepungukiwa na hayo yote basi ni dhahiri kuwa Mungu amekukataa na hayupo na wewe hivyo unapaswa UTUBU.  ndio yalikuwa mahubiri yao kwa Ayubu kuanzia mwanzo mpaka mwisho (Pata muda taratibu mwenyewe upitie kitabu cha Ayubu chote), na kibaya zaidi waliyathibitisha hayo waliyokuwa wanayasema kwa kutumia maandiko matakatifu, na mengine kufunuliwa kupitia maono usiku. Kiasi kwamba unaweza ukadhani ni Mungu kweli anazungumza na wewe kupitia watumishi wake. Embu Tusome baadhi ya maneno yao waliokuwa wanamuhubiria Ayubu..

Elifazi alianza kwa kumwambia Ayubu tukisoma Ayubu 4:6-9..

“6 Je! Dini yako siyo mataraja yako, Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?

7 Kumbuka, tafadhali, NI NANI ALIYEANGAMIA AKIWA HANA HATIA? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.

9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika. “

Akiwa na maana kuwa kwamba Ayubu angekuwa ni mwelekevu kweli asingepatikana na shida zote hizo kwasababu walijua maandiko kwamba mwenye haki hawezi kukatiliwa mbali,(Na ni kweli ndivyo yanavyosema lakini yalitumika mahali pasipoyapasa)na pia  waliongezea “watu wapandao madhara huvuna hayo hayo” hivyo Ayubu kuwa vile ni kwasababu huko nyuma alikuwa ni mkaidi, hivyo kavuna alichokipanda.

Bildadi rafiki yake wa pili naye akaongezea na  kumwambia Ayubu:

Mlango 8

“1 Ndipo Bildadi huyo Mshuhi akajibu, na kusema,
2 Wewe utanena maneno haya hata lini? Maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo mkuu hata lini?
3 Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?
4 KWAMBA WATOTO WAKO WAMEMFANYIA DHAMBI, NAYE AMEWATIA MKONONI MWA KOSA LAO;
5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;
6 UKIWA WEWE U SAFI NA MWELEKEVU; HAKIKA YEYE SASA ANGEAMKA KWA AJILI YAKO, NA KUYAFANYA MAKAZI YA HAKI YAKO KUFANIKIWA.
7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
8 Basi, uwaulize, tafadhali, vizazi vya zamani, Ujitie kuyaangalia yale baba zao waliyoyatafuta;
9 (Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;)
10 Je! Hawatakufunza wao, na kukueleza, Na kutamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Je! Hayo mafunjo yamea pasipo matope Na makangaga kumea pasipo maji?
12 Yakiwa yakali mabichi bado, wala hayakukatwa, Hunyauka mbele ya majani mengine.
13 Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu; Na matumaini y
ake huyo mbaya huangamia;
14 Uthabiti wake utavunjika, Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.
15 Ataitegemea nyumba yake, isisimame; Atashikamana nayo, isidumu.
16 Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua, Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.
17 Mizizi yake huzonga-zonga chuguu, Huangalia mahali penye mawe.
18 Lakini, aking’olewa mahali pake, Ndipo patamkana, na kusema, Mimi sikukuona.
19 Tazama, furaha ya njia yake ni hii, Na wengine watachipuka kutoka katika nchi.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu mkamilifu, Wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Bado atakijaza kinywa chako kicheko, Na midomo yako ataijaza shangwe.
22 Hao wakuchukiao watavikwa aibu; Nayo hema yake mwovu haitakuwako tena”.

Unaona hapo tunaona Bildadi anamwambia Ayubu sababu pekee ya watoto wake kuangamizwa ni kwasababu watoto wake walikuwa ni waovu. Lakini tunasoma Ayubu alikuwa kila siku anaamka alfajiri kuwaombea watoto wake rehema na dua kwa Mungu. Yaani kwa ufupi Bildadi alimaanisha kuwa kifo, misiba, wakati wote ni matokeo ya kutokuwa mwelekevu mbele za Mungu. Bildadi aliendelea kumlaumu Ayubu kwamba kama kweli angekuwa ni mkamilifu mbele za Mungu, basi Mungu mwenyewe angenyanyuka amtete, lakini sasa mbona bado anaonekana hali yake iko vile vile tena ndio ikizidi kuwa mbaya zaidi. Kwahiyo matatizo yale ni ushahidi tosha kwamba maisha yake hayapendezi hata kidogo mbele za Mungu.

Na rafiki yake wa mwisho Sofari aliendelea kumvunja moyo Ayubu na kusema..

Mlango 20

“1 Ndipo Sofari, Mnaamathi, akajibu, na kusema,
2 Kwa hiyo mawazo yangu hunipa jawabu, Kwa ajili ya haraka niliyo nayo ndani yangu.
3 Nimesikia maonyo yanayonitahayarisha, Nayo roho ya ufahamu wangu hunijibu.
4 Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,
5 YA KUWA SHANGWE YA WAOVU NI KWA MUDA KIDOGO, NA FURAHA YA WAPOTOVU NI YA DAKIKA MOJA TU?.
6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni;
7 HATA HIVYO ATAANGAMIA MILELE KAMA MAVI YAKE MWENYEWE; HAO WALIOMWONA WATASEMA, YUKO WAPI?
8 Ataruka mfano wa ndoto, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; Wala mahali pake hapatamtazama tena.
10 Watoto wake watataka fadhili kwa maskini, Na mikono yake itarudisha mali yake.
11 Mifupa yake imejaa ujana wake, Lakini utalala nchi naye mavumbini.
12 Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
13 Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake. Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;
14 Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika, Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.
15 Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.
16 Ataamwa sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.
17 Hataiangalia hiyo mito ya maji, Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.
18 Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze; Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
19 Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini; Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
20 Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake, Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
21 Hakikusalia kitu asichokula; Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.
22 Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki; Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.
23 Hapo atakapo kulijaza tumbo lake, Mungu atamtupia ukali wa ghadhabu zake, Na kuunyesha juu yake akiwa anakula.
24 Ataikimbia silaha ya chuma, Na uta wa shaba utamchoma kwa pili.
25 Yeye autoa, nao watoka mwilini mwake; Naam, ncha ing’aayo yatoka katika nyongo yake; Vitisho viko juu yake.
26 Giza lote linawekwa kwa ajili ya hazina zake; Moto ambao haukuvuviwa na mtu utamla; Utayateketeza yaliyosalia hemani mwake.
27 Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo nchi itainuka kinyume chake.
28 Maongeo ya nyumba yake yataondoka, Yatamwagika mbali ka
tika siku ya ghadhabu zake.
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu itokayo kwa Mungu, Na urithi aliowekewa na Mungu”.

Kama tunavyosoma hapo, Sofari naye hakuona haya kumwambia Ayubu kwamba yeye alikuwa katika “shangwe za watu waovu ambazo hazidumu ni za muda tu”. Akiwa na maana kuwa Mali Ayubu alizokuwa nazo kwanza zilikuwa ni za muda tu! kwasababu hazikuwa ni za haki, akimaanisha kuwa uthibitisho pekee wa Mungu kuwa na Ayubu ni mali zidumuzo na kama hazidumu basi hizo ni shangwe za waovu. Hivyo hatuwezi kueleza habari zao zote lakini ukiwa na muda pitia kitabu cha Ayubu chote utaona Injili ya hawa watu ilivyokuwa kwa Ayubu na jinsi walivyoweza kutumia maandiko na maono kuthibitisha uongo wao ili tu wamfanye Ayubu auache uelekevu wake mbele za  Mungu. Hawa ndio walimfadhaisha Ayubu mara mia elfu zaidi hata ya kupotelewa na watoto na mali zake, kwasababu walikuwa wanataka kumfanya Ayubu atilie shaka uelekevu wake mbele za Mungu.  walifanyika kama vyombo vya shetani kumjaribu Ayubu.

Mambo hayo yameandikwa ili kutuonya sisi watu wa zamani hizi, Shetani anapomaliza kumjaribu mkristo kwa magonjwa, kwa dhiki, kwa misiba, kwa udhaifu, kwa kupungukiwa na mali, kwa vifungo, kwa mateso, kwa shida, kwa njaa, n.k na kuona kuwa mtu huyo bado kasimama katika imani yake na uelekevu wake kama Ayubu basi huwa  anabadilisha mfumo wake wa majaribu, na kuleta majaribu magumu zaidi, na ya hatari zaidi, anakuletea watu aliowatia yeye mafuta, mfano wa akina ELIFAZI,SOFARI, NA BILDADI ambao watatumia maandiko kukushawishi na kukuhakikishia kwamba njia unayoiendea sio sahihi, na kama hauna Roho wa Mungu ni rahisi sana kuchukuliwa na uongo wa watu hao, watakwambia KIGEZO PEKEE cha Mungu kukukubali ni wewe kuwa na MALI, kigezo pekee cha kuwa Mungu hajakutupa ni kutokupitia shida kabisa, watakwambia ukipitia misiba basi kuna tatizo kwenye imani yako, watakwambia ukipitia magonjwa basi kuna mahali umemuudhi Mungu, ukiwa na ulemavu fulani basi kuna laana fulani inakufuata kwasababu wenye haki lazima wawe na afya, watakuhakikishia kwa maandiko kabisa “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo. “

watu kama hawa hata siku moja hawataangalia AFYA YA ROHO YAKO, kwamba je! unaishi maisha matakatifu?, au unayo imani? au una upendo? au je! unamzalia Mungu matunda ya haki?? au unamfanyia Mungu ibada ya kweli? wao wataangalia AFYA YA MWILI wako tu! na siku ikitetereka kidogo tu, basi umekwisha chukuliwa nao utaishia kuudharau ukristo na kusema ni ulokole tu,

Ndugu jiepushe nao, wanaipotosha kweli ya Mungu, ni shetani kawainua kuwajaribu watu wa Mungu, na kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa ili waiache imani, kwasababu laana kubwa mbele za Mungu sio kupungukiwa mali, au kukosa afya,au kupitia misiba au dhiki, hapana bali laana kubwa mbele za Mungu ni kutomwamini yeye aliyetumwa na yeye (yaani Yesu Kristo),na  kukosa uhusiano binafsi na Mungu kwasababu biblia inasema..

Warumi 8: 35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.

37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.

38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Hivyo ndugu yatangeneze maisha yako kwa kumpenda Bwana Mungu wako pasipo kupelekwa na upepo huku na huku au  kundi hili la waalimu na manabii wa uongo,(Hao ndio manabii wa uongo wa siku za mwisho) Biblia inasema kila jambo na majira yake wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna, wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kujenga na wakati wa kubomoa, mkumbuke Ayubu baada ya yale majaribu Bwana alimrudishia mara mbili ya vile alivyovipoteza, lakini kama angewasikiliza wale rafiki zake leo hii angekuwa wapi?. Si angeishia kumwangalia Mungu katika kioo cha mafanikio tu??. lakini hakuruhusu imani yake ipotee na zile mali za kwanza alizokuwa nazo, alitunza uhusiano wake binafsi na Mungu katika hali yoyote aliyopo, nasisi vivyo hivyo tuwe matajiri, au maskini, tuwe na vitu au tusiwe na vitu, tuwe wazima au tuwe wagonjwa, uhusiano wetu na Mungu unapaswa uwe pale pale kama Ayubu, usiyumbishwe na mazingira ambayo shetani anayaleta kupitia watumishi wake wa uongo ambao ndio sasahivi wamezagaa kila mahali kuwarubuni watu na mafundisho yao ya kujigamba.

Bwana akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

AYUBU ALIJARIBIWA KWA MUDA GANI?.

KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?

KWANINI SAMWELI ALIRUHUSIWA KUHUDUMU HEKALUNI KAMA VILE WALAWI WAKATI YEYE NI MU-EFRAIMU?


Rudi Nyumbani

Print this post

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Licha ya kuwa na INJILI YA MSALABA,ambayo ndio kiini cha kila mwanadamu ipo injili nyingine pia ijulikanayo kama INJILI YA MILELE, hii ni tofauti na injili ya msalaba. Injili ya msalaba yenyewe inatangaza wokovu kwa mwanadamu tu, kwa kupitia mmoja naye ni YESU KRISTO BWANA wetu. Kwahiyo injili nyingine yeyote inayodai kumkomboa mwanadamu na haimweki Bwana Yesu kama kiini cha injili yenyewe, basi injili hiyo ni batili, kwasababu yeye pekee ndiye Njia, kweli na uzima, hakuna mtu yeyote atakayemwona Mungu, pasipo kupitia kwake yeye biblia inasema hivyo(Yohana 14:6).. Kwahiyo zipo injili nyingi zinazodai zinaweza kumkomboa mwanadamu lakini kati ya hizo ni moja tu itakayoweza kumkomboa mwananadamu! Nayo ni Kwa kupitia Yesu Kristo, na ndio maana Mtume Paulo alisema|:

2Wakoritho 11: 4 “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au INJILI NYINGINE msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”

Unaona hapo? Biblia inasema kuna Yesu mwingine, roho mwingine na injili nyingine tofauti na ile iliyohubiriwa na mitume. Kwahiyo injili yoyote inayohusishwa na ukombozi wa mwanadamu inapaswa imlenge YESU KRISTO ALIYESULIBIWA,akafa na kufufuka kama kiini cha Ukombozi wenyewe, kwa asilimia mia yeye peke yake na sio pamoja mtu mwingine.

Lakini leo kwa ufupi tutaitazama INJILI YA MILELE ambayo ipo na imezungumziwa katika biblia..kama tunavyosoma katika;

Ufunuo 14: 6 “Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye INJILI YA MILELE, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa,

7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji”.

Sasa hii injili ya milele ni ipi?

Kama jina lake lilivyo “Milele” inamaana kuwa ni injili ambayo Ipo milele yote, ilikuwepo kabla ya mwanadamu kuumbwa, ipo sasa, na itaendelea kuwepo milele na milele, Kumbuka INJILI YA MSALABA ilikuwa na mwanzo, na itakuwa na mwisho, mwanzo wake ilikuwa ni Kalvari, na mwisho wake itakuwa katika Unyakuo. Baada ya hapo hakutakuwa na nafasi tena ya ukombozi, kwasababu mlango wa neema utakuwa umefungwa. Kitakachokuwa kimebaki ni ile ile injili ambayo ilikuwepo milele na milele.

Na ndio maana ukisoma mstari huo hapo juu utaona kuwa yule malaika(mjumbe) anapita kuitangaza hiyo injili ambapo kwa wakati huo unyakuo wa kanisa utakuwa umeshapita na mlango wa neema ya kuokolewa utakuwa umefungwa kwa watu wa mataifa.

Kwahiyo injili hii ni tofauti na ya msalaba tuliyonayo sasa, hii ya msalaba tunaifahamu kwa “kuhubiriwa”. Hatuwezi kuifahamu pasipo kuhubiriwa ndio maana biblia inasema katika;

Warumi 10: 13 “kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana{YESU KRISTO} ataokoka.

14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? TENA WAMSIKIEJE PASIPO MHUBIRI?

15 Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!{INJILI YA MSALABA}”

Kwahiyo unaona hapo, ni lazima awepo mtu wa kuihubiri ndipo watu waokolewe.

Tofauti na ilivyo INJILI YA MILELE. Injili hii haisambazwi kwa kuhubiriwa na mtu yeyote, Ni Mungu mwenyewe anaiweka ndani ya mtu, katika eneo maalumu la moyo wa mwanadamu linaloitwa “DHAMIRA”..ambayo kila mtu anazaliwa nayo. Na inafanya kazi ya kuhukumu njia zote mbaya zinazokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu ndani ya mtu..Na Injili hii haipo tu kwa wanadamu, ilikuwepo hata kwa malaika, kwasababu ni ya milele, ilikuwepo huko enzi na enzi, ipo na itakuwepo.

Kwahiyo sasa kitendo tu cha mtu kuwa mwanadamu, tayari moja kwa moja kuna kitu ndani yake kitakuwa kinamshuhudia mambo yanayofaa na yasiyofaa, bila hata kuhubiriwa  na mtu yeyote, au kukumbushwa na mtu yeyote, kwamfano, kila mtu anafahamu kuwa uuaji sio sawa, iwe anayo hofu ya Mungu au hana hofu ya Mungu, kila mtu anafahamu kuwa dhuluma ni mbaya, hata kama sheria isingesema hivyo, ndani ya moyo wake dhamira inamuhubiria kuwa kitendo hicho ni kibaya, Kadhalika haihitaji kuifahamu biblia kujua kuwa uonevu ni makosawizi ni makosautukanajiubakajirushwa ni makosa hayo yote hata kama mtu hajawahi kumsikia Mungu, au chochote kinachoitwa Mungu anajua kabisa hayo mambo hayafai kufanya, pia haihitaji kwenda katika vyuo vya biblia kutambua kuwa kulala na ndugu yako wa damu ni makosa, kadhalika na ushoga au usagaji ni makosa, utajikuta tu wewe mwenyewe unachukia kufanya hivyo au unalipinga hilo wazo ndani yako pale linapokuja kwasababu unajua kabisa kuwa hayo ni makosa.

Sasa hiyo ndio inayoitwa INJILI YA MILELE, Mungu anayoihubiri ndani ya moyo wa mtu. Na ndiyo hiyo siku za mwisho itakuja kukumbushwa kwa watu, wamche Mungu.wakati huo unyakuo utakuwa umeshapita.

Kwahiyo usidhani kuwa wale watu ambao hawajasikia habari za YESU(Injili ya msalaba) mahali popote, hawatahukumiwa. Hapana Watahukumiwa tu kama wale wengine kwa injili hiyo. Watu wa kipindi cha Nuhu hawakuwa na sheria waliyopewa na Mungu kama watu wa Musa na kuendelea,Na ndio maana Mtume Paulo alieleza habari za watu hawa kama tunavyosoma katika…

Warumi 1: 17 Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.

18 Kwa maana GADHABU YA MUNGU imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

19 Kwa kuwa MAMBO YA MUNGU YANAYOJULIKANA YAMEKUWA DHAHIRI NDANI YAO, KWA MAANA MUNGU.

20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; YAANI, UWEZA WAKE WA MILELE NA UUNGU WAKE; hata wasiwe na UDHURU;

21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.

22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;

23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.

24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.

25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.

26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.

28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

29 Wamejawa na UDHALIMU, UOVU na TAMAA na UBAYA; wamejawa na HUSUDA, na UUAJI, na FITINA, na HADAA; watu wa NIA MBAYA, wenye KUSENGENYA,

30 wenye KUSINGIZIA, wenye KUMCHUKIA MUNGU, wenye JEURI, wenye KUTAKABARI, wenye MAJIVUNO, wenye KUTUNGA MABAYA, WASIOTII WAZAZI WAO,

31 wasio na UFAHAMU, wenye KUVUNJA MAAGANO, WASIOPENDA JAMAA ZAO, WASIO NA REHEMA;

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.

Umeona hapo ndugu, biblia inasema wakijua kabisa watendao mambo kama hayo wamestahili mauti lakini bado wanayatenda. Dhamira zao zikiwashuhudia ndani kuwa wanayoyafanya sio sahihi lakini wanaendelea kuyafanya, Na wewe je! Ambaye upo kwenye dhambi utahitaji mhubiri siku moja aje kukuthibitishia kwenye biblia kwamba, uvutaji sigara ni dhambi, au uasherati ni dhambi?? Angali ndani ya moyo wako dhamira inakushuhudia kabisa unachofanya ni makosa?..hakika unaweza usilione lakini fahamu kuwa hukumu inakungojea.!

Wewe unayevaa vimini, na kutembea nusu uchi barabarani unasema Mungu haangalii mavazi lakini moyo wako unakuambia kabisa hayo ni makosa unayoyafanya na bado unaweka moyo mgumu, wewe unayevaa suruali,unayepaka wanja, na kupaka lipstick, na kuvaa wig na hereni, Hukumu ipo mbeleni dada!, wewe unayesengenya, wewe ambaye ni shogawewe unayejisagawewe unayetoa mimba, wewe uliye mwasherati, wewe uliye mlevi, wewe unayetazama pornography, wewe unayefanya masturbation, wewe unayeabudu sanamu za watakatifu waliokufa zamani angalia biblia inavyokuambia hapo juu < wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu(sanamu), na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo >..Unaona unajua kabisa Mungu hawezi kufananishwa na mfano wowote wa kinyago cha kuchonga lakini wewe bado unakwenda kuvipiga magoti na kuviabudu..

2Wakorintho 6: 16 inasema “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu?”..

Lakini biblia inaendelea kusema kwa jinsi utakavyozidi kuweka moyo wako mgumu, kuna kipindi kitafika Mungu anakuacha uendelee hivyo hivyo kwasababu umekataa kuitii hiyo sauti inayosema ndani yako, mpaka ile siku ya hukumu ije na utaingia kuzimu!! Alisema “”28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa”. 

Kwahiyo dada/kaka hukumu ya Mungu haikwepeki hata uwe nje ya kanisa, njia pekee ni kujisalimisha maisha yako kwa BWANA YESU ambaye yeye ndiye aliyetoa uhai wake ili akuokoe, Tubu geuka, ukapewe uwezo wa kushinda dhambi. Muda umekwenda kuliko unavyodhani, na Injili ya msalaba sio ya milele utafika wakati utatamani uingie utakosa, muda ndio huu, mpe Bwana maisha yako tangu sasa.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

KITABU CHA UKUMBUSHO

Yapo maswali kadha wa kadha umekuwa ukijiuliza kama mkristo (tukisema mkristo tunamaanisha mtu aliyegeuka na kudhamiria kwa gharama zake zote kubeba msalaba wake na kumfuata Kristo). Wakati mwingine unajikuta aidha ndani ya moyo wako au nje na maswali unayokosea majibu!!.

Kwamfano pengine unasema tangu nilipompa Bwana maisha yangu ni kweli ndani ya moyo wangu nilipata amani kubwa ya ki-Mungu lakini nje! Naona mambo mengi hayapo sawa, nilipojaribu kuishi maisha matakatifu marafiki na ndugu wakanitenga , nilipojaribu kuacha usengenyaji ndipo nilipoanza kuonekana mbele ya marafiki zangu ninajidai,

Nilipoacha rusha ndipo visa vikainuka kazini na kupelekea kuongeza idadi ya watu wanichukiao, niliposaidia watu badala ya kupokea shukrani ndio napokea lawama, nilipoanza kufunga na kuomba badala ya matatizo kupungua ndio yaliendelea kuwa vile vile, nilipoanza kufanya kazi ya Mungu ndipo matatizo ya kiuchumi yakanyanyuka zaidi,

Mpaka unafikia hatua ya kusema mbona huku kuishi maisha ya kujinyima na mambo ya dunia hakuna faida yoyote ninayoipata, zaidi ya kuwa vile vile tu siku zote!, mbona wale wasiomcha Mungu wana raha siku zote, ni matajiri pamoja na kwamba wanamkana Mungu, wanazidi kufanikiwa katika mambo yao,mbona wazinzi ndio wanao afya nzuri?.

Mimi pamoja na utakatifu wangu wote na wema wangu wote, Mungu kama hanioni na kunipa raha kama hao wengine, japo ninafanya mema kushinda wao?, kwani ni laana gani ninayo hadi yanipate hayo yote, au wao wana kitu gani cha ziada cha kushinda mimi mpaka wao wayapate hayo yote?,..Kumbuka Hayo ni mawazo yaliyopo ndani ya watakatifu wengi wa Mungu, Hata Daudi naye pia alizungumza maneno kama hayo tusome katika:

Zaburi 69: 7 “Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.

8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.

9 Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.

10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.

11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao.

12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki”.

Zaburi 73:1 “Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.

2 Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.

3 MAANA NALIWAONEA WIVU WENYE KUJIVUNA, NILIPOIONA HALI YA AMANI YA WASIO.

4 Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu.

5 Katika TAABU YA WATU HAWAMO, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu. 

6 Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo.

7 Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.

8 Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.

9 Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani.

10 Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao.

11 Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu?

12 Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi”.

Zaburi 42: 3 “Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako”.

Kama tunavyosoma Daudi pamoja na wema wake wote wa kuwaombea watu wengine fadhili mbele za Mungu kwa kufunga na wakati mwingine kwa machozi lakini bado alionekana kuwa kama ni kituko na mgeni mbele zao. Mpaka kufikia hatua ya kuwaonea wivu watu waovu.

Kadhalika na mambo haya haya yanawazwa na watakatifu walioko leo duniani , Wanasema aidha kwa midomo yao au kwa mioyo yao: Mungu wetu yuko wapi? Mbona hatuoni faida yoyote ya kumtumikia, mbona hatuoni faida yoyote ya kuacha kuvaa vimini, hereni, suruali, kuacha kupaka lipstick na wigi, wale wanaoendelea kufanya hivyo hao ndio wanaolewa kwa harusi nzuri, wana watoto wazuri lakini mimi bado nipo vile vile tu!.

Utasema mbona sioni faida yoyote ya kuacha pombe na sigara, mbona sioni faida yoyote ya kuacha uasherati, disco, anasa,na kucheza kamari na ku-bet, wenzangu wanafanikiwa kirahisi mimi nipo vile vile tu, Mbona sioni faida yoyote ya kuacha kula rushwa, zile pesa nilizokuwa ninapata mwanzoni sizioni tena nikizipata sasahivi, wale wenzangu tuliokuwa tunakula nao rushwa zamani wanazidi kunawiri na kusomesha watoto wao na kujenga majumba makubwa na mimi nimebaki katika hali ile ya kawaida tu!.n.k.

Haya yote yamekuwa ni maswali ya WATAKATIFU tangu zamani, Lakini Bwana naye aliyasikia na kuyatolea majibu yake: Kama tunavyosoma katika Malaki 3 Bwana anasema.

Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

14 MMESEMA, KUMTUMIKIA MUNGU HAKUNA FAIDA; na, TUMEPATA FAIDA GANI KWA KUYASHIKA MAAGIZO YAKE, NA KWENDA KWA HUZUNI MBELE ZA BWANA WA MAJESHI?

15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. NAYE BWANA AKASIKILIZA, AKASIKIA; na KITABU CHA UKUMBUSHO KIKAANDIKWA MBELE ZAKE KWA AJILI YA HAO WAMCHAO BWANA, NA KULITAFAKARI JINA LAKE.

17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.

18 Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia”.

Unaweza ukaona hapo?. Hakuna wema wowote wa mtakatifu atakaoufanya ukapita bure bure tu! , mbinguni kuna KITABU CHA KUMBUKUMBU kimewekwa kwa watu maalumu, kinarekodi mambo yote mema watakatifu wanayoyafanya kila siku huku duniani.

Na kama ni kitabu basi inaamanisha ili kiwe kitabu kamili ni lazima kiwe na kurasa nyingi na sio chache, na kitabu hichi cha watakatifu, ni matendo mema tu ndio yanayoandikwa huko, na sio kingine. Kwahiyo wingi wako wa kumcha Mungu na matendo yako mema mbele za Mungu kila siku yanarekodiwa katika kitabu kile na ndio yatakayoelezea wingi wa thawabu utakazopewa mbinguni katika siku ile ya mwanakondoo.

Hivyo ndugu/dada ukiwa ni mkristo kweli kweli uliyedhamiria kusimama katika Imani huu sio wakati wa kudhani kumtumikia hakuna faida yoyote,Faida zipo nyingi sana utazijua kwa marefu na mapana utakapofika katika urithi uliowekewa na Mungu wako.

Mambo ya ulimwengu huu sio urithi wetu, wewe upate usipate, uwe tajiri uwe maskini, uwe una afya usiwe na afya, vyovyote wewe endelea kumcha Mungu bila kujali lolote lile ukijua siku ile ni Mungu wako aonaye taabu yako ndiye atakayekulipa, maadamu unajiona upo sawa na Mungu wako usikwamishwe na kitu kingine chochote,songa mbele! endelea kuliweka Kumbukumbu lako sawa mbinguni, usidanganyike na mafundisho ya watumishi bandia kwamba kuwafanikiwa au kutokufanikiwa kifedha ndio uthibitisho kwamba Mungu yupo na wewe au Mungu amekuacha, hapana uthibitisho pekee ni maisha unayoishi ya kumpendeza Mungu wako sikuzote, kwasababu kitabu cha kumbukumbu kipo mbinguni.

Ongeza bidii, ikiwa umekataa rushwa endelea kuipinga, ukiwa umekataa uasherati endelea kufanya hivyo kwa bidii zaidi, ikiwa umekataa kuenenda kama mfano wa watu wa ulimwengu huu kuvaa vimini, suruali endelea hivyo hivyo kumbukumbuku lako kila siku linawekwa na thawabu yako ya siku haitapita bure..Bwana aliyeumba macho anaona yote!.

Lakini ukisema nitafanya hivyo nikifika umri fulani au wakati fulani, hujui kesho yako itakuwaje, na utakosa kumbukumbuku bora siku ile wakati wenzako wanafarijiwa kwa mambo mazuri yasiyoelezeka ya umilele na wewe haupo.Usiwaige watu waovu katika njia zao?

Na ni kwasababu gani Mungu anaruhusu waovu wafanikiwe sasa? .

Ni kwasababu urithi wao upo katika dunia ya sasa iliyoharibika na hawana sehemu yoyote katika urithi katika ulimwengu unaokuja. Hivyo faraja yao ipo katika mambo ya ulimwengu wa sasa kule hawana sehemu ndio sababu Bwana karuhusu wapate faraja yao hapa.

Bwana alimwambia Daudi.

Zaburi 92:7 “WASIO HAKI WAKICHUPUKA KAMA MAJANI NA WOTE WATENDAO MAOVU WAKISTAWI. NI KWA KUSUDI WAANGAMIZWE MILELE”

Kwahiyo sababu pekee ya waovu kufanikiwa sio kwasababu wanampendeza Mungu, ni ili waangamizwe milele, je! Na wewe unapenda kuwa miongoni mwao?, unafanikiwa katika rushwa yako ili uje uangamizwe milele?, unafanikiwa katika uasherati wako,na ulevi wako, na biashara yako haramu ili uje uwe miongoni mwa hao watakaoangamizwa milele?

Unafanikiwa katika utapeli wako na kamari yako na betting yako, ili uje uangamie milele?? Biblia inasema ITAKUFAIDIA NINI UPATE ULIMWENGU MZIMA, NA KUPATA HASARA YA NAFSI YAKO?, itakufaidia nini uonekane ni wakisasa kuliko watu wote duniani, kwa kujichora, kwa kuvaa vimini, na suruali na mawigi na kisha upate hasara ya nafsi yako? Ndugu KUMBUKUMBU LA WENYE HAKI LINAANDIKWA MBINGUNI kamwe usitamani mambo yao wala njia zao, kama hujampa Kristo maisha yako ni vema ukafanya hivyo sasa angali wakati upo, kabla mlango wa Neema haujafungwa.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, na Mungu atakubariki.

Kwa msaada wa maombi/Ushauri/ubatizo/mafundisho/Whatsapp: Namba zetu ni hizi: +255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

KITABU CHA UZIMA

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

JE! NI SAHIHI MTU KUBATIZWA KWENYE MAJI YA KISIMANI?

KWANINI KUNA WATU WANAFANYIWA DELIVERANCE (MAOMBI YA KUFUNGULIWA), LAKINI BAADA YA MUDA WANARUDIWA TENA NA HALI ILE ILE SABABU NI NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

Mara nyingi sana Mungu huwa anazungumza na sisi kupitia maisha yetu ya kawaida tunayoishi kila siku, tunapokosa shabaha ni pale tunapotarajia Mungu aseme nasi kwa njia zile tunazozifahamu, kwamfano, kuona maono au ndoto, unabii au kutokewa na malaika, mambo ambayo sio muda wote Mungu anayatumia kuzungumza na watu wake.

Sehemu kubwa Mungu anayotumia kuzungumza na watu wake ni kupitia maisha, na ndio maana inatugharimu kuyasoma maisha ya BWANA wetu Yesu Kristo na maisha ya watakatifu waliotangulia nyuma ili kuichuja na kuitambua sauti ya Mungu nyuma ya maisha yao.Kwamfano tunasoma tunaposoma kitabu cha mwanzo, au wafalme au Esta au Ruthu, au Nehemia au Ezra au hata safari ya wana wa Israeli hivyo ni vitabu vinavyoelezea maisha ya watu, na huko huko tunajua kusudi la Mungu kwetu sisi ni lipi.

Siku zote Mungu anajifunua katika mambo madogo, ambayo inahitaji utulivu vinginevyo tutaishia kusema Mungu hajawahi kuzungumza na sisi kabisa kama watu wengine wanavyosema..na kumbe alishazungumza na sisi mara nyingi, lakini hutukutia mioyo yetu ufahamu na kuelewa.

Kuna wakati Fulani mahali tulipokuwa tumepanga tulipata nafasi ya kuwa pamoja na wachezaji wawili wanaochezea timu moja maarufu hapa Tanzania, kwetu sisi hatukuona ni kitu cha ajabu sana kukutana nao kwa mwanzoni (kwasababu sisi sio washabiki wa michezo,hata hivyo ni kinyume kwa mkristo kuwa mshabiki wa mambo kama hayo) lakini maisha yao kwa jinsi tulivyoendelea kukaa nao yalitustaajabisha kidogo, kwa jinsi yalivyokuwa ya kipekee sana. Kwasababu kama wachezaji wa kidunia tulitazamia watakuwa ni watu wasiokuwa na nidhamu katika jamii (yaani kuishi maisha kama tu ya wasanii wengine wa kidunia), lakini kwa hawa tuliona utofauti wa mbali wa ya tulivyodhania.

Ratiba yao ilikuwa ni hii ; Kila siku wanaamka asubuhi sana saa 12 kamili, na kwenda uwanjani kufanya mazoezi mpaka saa 3, wakisharudi kutoka huko wana pumzika kidogo mpaka saa 7 mchana wakati wa jua kali, wanarudi tena uwanjani (saa 7 na saa 8) peke yao kufanya mazoezi ya nguvu kuliko waliyoyafanya asubuhi kwenye jua kali, kisha wanarudi kupumzika tena mpaka saa 11 jioni ndio warudi tena uwanjani kujumuika na wengine katika mazoezi ya kawaida, na hayo ndiyo yalikuwa maisha yao asubuhi, jioni, kila siku.

Lakini hicho nacho hakikutushangaza sana, kilichotushawishi zaidi mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwauliza ni baada ya kuwatazama kwa muda mrefu, na kuwaona wakijiweka mbali na wanawake,na ulevi, uzururaji, na kuwa na idadi ndogo ya marafiki wanaokuwa nao..wao kazi yao ilikuwa ni mazoezi tu na kupumzika basi!!..hawakuwa wanafanya kitu kingine cha ziada.

Na ndio Siku hiyo moja tukawauliza ni kwanini nyie mnaishi maisha kama hayo tofauti na wengine, wakatujibu; Mambo yanayowakosesha wengi katika michezo na kuwafanya washuke viwango vyao kwa haraka, ni kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja,wakasema; unapokuwa mchezaji na unataka kiwango chako kisishuke ni lazima uzingatie mambo yafuatayo;

1) Kukaa mbali na uasherati.

2) kukaa mbali na pombe na sigara

3) kukaa mbali na uzuraraji (ANASA).

4) Na kuzingatia mazoezi kwa bidii hususani katika wakati mgumu..hivyo mtu akizingatia yeyote akizingatia mambo hayo michezo haitakuwa na ugumu wowot kwake .

Sasa baada ya watu hao wa kidunia(ambao sio wakristo) kutuambia maneno kama hayo, tulifahamu hiyo ni sauti ya Mungu inayosema na sisi moja kwa moja, na andiko la kwanza lililotujia kichwani ni hili..;

1Wakorintho 9: 24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 NA KILA ASHINDANAYE KATIKA MICHEZO HUJIZUIA KATIKA YOTE; BASI HAO HUFANYA HIVYO KUSUDI WAPOKEE TAJI IHARIBIKAYO; bali sisi tupokee TAJI isiyoharibika .26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

Ikiwa hao hawajapewa neema ya kuishinda dhambi kama tuliopewa sisi katika Bwana wetu Yesu Kristo pale tunapomwamini lakini wanao uwezo wa kuyakataa mambo ya kidunia ili tu wasipoteze mataji yao, Inatupasaje sisi tunaojiita wakristo?. Wao wanajua kabisa huko wanapokwenda watakutana na watu wenye ujuzi mkubwa kama wa kwao, hivyo wanagharimika sasa hivi kujitaabisha katika mazingira yote magumu ili watakapoenda kule kushindana na wale wengine iwe ni rahisi kwao kushinda na kupokea tuzo iliyobora ambayo inagombaniwa na wengi

Mtume Paulo aliandika ..

2Timotheo 2: 4 “Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.

5 HATA MTU AKISHINDANA KATIKA MACHEZO HAPEWI TAJI, ASIPOSHINDANA KWA HALALI”.

Katika Maneno hayo tunaona Mungu anatufundisha Neno lake katika maisha yanayotuzunguka, kumbuka ukiwa mkristo, haimaanishi kuwa ndio umefika, hivyo kuanzia huo wakati ustarehe tu hapana! ni lazima ujue kuwa huko unapokwenda pia kuna TUZO zimeandaliwa, tena tuzo zenyewe ni tuzo zisizoharibika..na ni watakatifu wengi wanaozigombania, na yeye aliyestahili ndiye atayeipokea Tuzo ya juu zaidi kuliko wengine.. Bwana Yesu alisema “12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”. (Ufunuo 22:12)

Lakini Tuzo hiyo hatuipati kama hatutaziingia gharama kama Paulo alizozisema ..”Ninautesa mwili wangu na kuutumikisha”… Ikiwa wachezaji wa ulimwengu huu wanaitesa miili yao na kuitaabisha (sio kana kwamba wenyewe wana madhaifu hapana! Bali Wanafahamu wanachokitafuta,) watawashinda wakristo kwa kujizuia na mambo mengi ili tu kupokea taji ambayo kesho inakwisha thamani yake..Unadhani inatupasa tuingie gharama kubwa kiasi gani sisi tunaojiita wakristo ili kupokea ile TUZO isiyoharibika (yaani inayodumu milele?)…Bila shaka ni kubwa zaidi ya wale, ni kujizuia zaidi ya wale, ni kujinga na mizigo ya dhambi mara nyingi zaidi ya wale.

Biblia inasema lipo WINGU kubwa la MASHAHIDI linalotuzunguka katika mashindano yaliyopo mbele yetu ukipata nafasi lisome hili wingu lote katika Waebrania sura ya 11, utaona ni jinsi gani walishinda mbio kwa saburi, na kama sisi tusipokuwa na juhudi katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu, basi zile tuzo nono kule zitachukuliwa na wengine waliostahili, ukisoma biblia inatuambia watu wale(wingu kubwa la mashahidi) ulimwengu haukustahili kuwa nao,

Walikuwa ni wasafiri duniani, watu ambao mawazo yao waliyaelekeza katika ulimwengu ujao mpaka kuhesabu maisha ya hapa duniani kuwa si kitu (mfano Ibrahimu), mpaka kufikia hatua Mungu mwenyewe anajivunia kuitwa Mungu wao kwa vile walivyoyaelekeza mawazo yao mbinguni, walikatwa na misumeno, walipigwa, walisulibiwa lakini hawakuikana imani yao,na sisi je! Tutapate kuwa kama hao kama tusipojikana na tusipojitesa na kuitumikisha miili yetu sasa hivi?..(soma waebrani 11 yote utaona jambo hilo)

Ukizidi kuisoma habari ya hilo Wingu la Mashahidi mpaka kufikia sura ya 12, ndio mtume Paulo anahitimisha kwa kusema…

Waebrania 12: 1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, NA TUWEKE KANDO KILA MZIGO MZITO, NA DHAMBI ILE ITUZINGAYO KWA UPESI; NA TUPIGE MBIO KWA SABURI KATIKA YALE “MASHINDANO” YALIYOWEKWA MBELE YETU,

2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

3 Maana mtafakarini sana yeye ALIYESTAHIMILI MAPINGAMIZI MAKUU NAMNA HII ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.

Dada/Kaka nawe pia hawa wanamichezo wanaokuzunguka wanakufundisha nini? siku ile utajisikiaje kuona waliokuwa warembo kuliko wewe, ambao wangeweza kuutumainia uzuri wao kupata kila kitu katika dunia hii lakini walijizuia na tamaa za kitambo na zaidi ya yote unawafahamu, utajisikiaje kuwaona siku ile wanang’aa kama nyota na wewe unakuwa sio kitu mbele yao milele?, siku ile wanapewa tuzo wewe utakua uko wapi?

Utajisikiaje kuona yupo ndugu unayemfahamu mwenye uwezo kuliko wewe ambaye angeweza kuutumainia uwezo wake kupata kila kitu katika hii dunia lakini alijizuia kwa ajili ya Kristo na kuhesabu dunia ya miaka 70 sio kitu kulinganisha na umilele unaokuja huko mbeleni na siku ile anakuwa mfalme na wewe si kitu..utajisikiaje? ??

Ndugu ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu na wenye nguvu ndio wanaouteka biblia inasema hivyo, Weka mbali mambo ya ulimwengu huu, kajiwekee hazina sasa mbinguni, Kama hujamkabidhi Bwana maisha yako huu ndio wakati, fanya hivyo sasa ili uanze kuiunda tuzo iliyo bora tutakapofika kule siku ile….

Swali ni lile lile ninakuuliza tena hawa wanamichezo wanaokuzunguka wanakufundisha nini katika mashindano ya aina yako ya kikristo?.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share ujumbe huu kwa wengine na Bwana atakubariki.

Kwa msaada wa maombi/Ushauri/ubatizo/mafundisho/Whatsapp: Namba zetu ni hizi: 

+255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

TUKAZE MWENDO KWA TULIYOANDALIWA.

KANUNI JUU YA KANUNI.

YESU MPONYAJI.

NAOMBA KUJUA UTOFAUTI KATI YA DHAMBI, UOVU NA KOSA KIBIBLIA.


Rudi Nyumbani

Print this post

DANIELI: Mlango wa 12.

Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO lihimidiwe milele na milele.

Huu ni mwendelezo wa kitabu cha Danieli leo tukiwa katika ile sura ya mwisho ya maono Danieli aliyoonyeshwa yahusuyo siku za mwisho. Katika sura hii tunaona Gabrieli akiendelea kumfunulia Danieli mfululizo wa mambo yaliyoanzia sura ile ya 10 na 11 ambapo tuliona jinsi Danieli akiambiwa kwa undani mambo yaliyojiri katika utawala wa Uajemi na Uyunani ambao uliishia na mtawala mkatili wa kiyunani aliyeitwa Antiokia IV Epifane aliyewatesa wayahudi. Lakini tukitazama katika sura hii ya mwisho ya 12 tunaona Danieli akionyeshwa picha (japo kwa sehemu) ya matukio yatakayokuja kutokea katika utawala wa mwisho (yaani RUMI).

Tukisoma ule mstari wa kwanza,..unasema

“Danieli 12:1 Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile.”

Kumbuka Mikaeli ni malaika anayesimama kwa ajili ya kulipigania taifa la Israeli (Ni malaika wa vita), hata ukitazama katika sura ya 10, utaona Mikaeli alikuja kumsaidia Gabrieli katika vile vita ili kuufikisha ujumbe wa Mungu, Na amekuwa akiwapigania Israeli dhidi ya wale wakuu (au mapepo) ya Falme zile zote zilizotangulia kuwapo. Hivyo ili Mikaeli na jeshi lake waipiganie Israeli vizuri na kushinda inategemea kiwango cha kumcha Mungu cha wayahudi, kikiwa chini inamaana wale wakuu wa giza wanapata wigo mkubwa zaidi ya kuwatesa watu wa Mungu(Wayahudi), vivyo hivyo kiwango cha kumcha Mungu kikiwa juu, ndivyo Mikaeli na jeshi lake linavyoweza kupata nguvu ya kuipigania Israeli na kushinda dhidi ya wale wafalme wa giza. Kwahiyo vita vya malaika vinatemea hali za kiroho za watu wa Mungu.

Na ndio maana utaona wakati wowote waisraeli wakimuacha Mungu maadui zao wanakuja kuwashambulia, lakini wanapomrudia Mungu na kuzishika sheria zake, Mungu anawaokoa na maadui zao kwa kuwapigania. Na ndivyo ilivyo hata kwa wakristo, Kuna malaika amesimama kwa ajili yetu, hakuna malango yoyote ya kuzimu yatakayosimama mbele ya kanisa la Kristo kama likienda katika hali ya utakatifu.

Tukiendelea katika mstari huu tunaona biblia inasema Mikaeli atasimama, na kutakuwa na wakati wa taabu ambayo haijawahi kutokea tangu Israeli iwe taifa, hii inafunua kuwa mambo hayo yatatokea katika siku za mwisho kwenye ule utawala wa RUMI, wakati wa dhiki kuu pale mpinga-kristo atakaponyanyuka na kuwaua wayahudi wengi, biblia imekiita hicho kipindi kama “wakati wa taabu ya Yakobo (Yeremia 30:7)”

Na ndio kipindi alichotabiri Bwana Yesu katika Mathayo 24: 21 “Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.”.

Na pia pale anasema.”wakati huo watu wako wataokolewa”. hii ikiwa na maana kuwa wayahudi wengi watapewa neema ya kumwamini Yesu Kristo kama ndiye Masihi wao aliyetabiriwa kumbuka kwasasa wayahudi wamefumbwa macho hawamwamini Yesu Kristo lakini watakuja kupewa neema hiyo baadaye.

(Ukisoma Warumi 11: 25 inasema..“Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu UGUMU umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.

27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.).

Jambo hili litatimia pale juma la 70 la Danieli litakapoanza ambapo wale wayahudi 144000 watatiwa muhuri kama tunavyosoma katika ufunuo 7.

Tukiendelea mistari inayofuata…

“Danieli 12:2 Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.

3 Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele.”

Hapa tunaweza kuona Danieli akifunuliwa siri zihusuzo ufufuo wa wafu, kwamba wakati utakuja ambapo wafu wote watafufuliwa. jambo ambalo Bwana Yesu alishalizungumzia katika Yohana 5:25” 

28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.

29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.”

Kadhalika alionyeshwa pia wenye hekima watang’aa kama mwangaza wa jua, pamoja na hao waongozao wengine kutenda haki. Kila mtu anayawafundisha watu katika njia za haki na utakatifu na kuwafanya watazame mambo ya mbinguni, biblia inasema siku ile atang’aa kama nyota za mbinguni.

Mstari wa 4 unasema..

“4 Lakini wewe, Ee Danielii, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.”

Danieli anaambiwa aufunge unabii huo mpaka wakati wa mwisho ulioamriwa ikiwa ikiashiria kuwa wakati wa mwisho(ambao ndio tuliopo sisi) mambo hayo yatafunuliwa, na watu wataelewa yaliyoandikwa humo ndani, na ndio maana ukienda mbele kidogo anasema MAARIFA yataongezeka.

(Maarifa yataongezeka):Kumbuka maarifa haya, ni maarifa ya kumjua Mungu, siku hizi za mwisho maarifa yameongezeka juu ya masuala ya kimungu, japo sio kwa watu wote bali kwa watu wachache wenye hekima, ilikuwa ni ngumu kwa wakati ule wa Danieli, kumuelewa mpinga-kristo atakuja kwa namna gani, au shetani anafanyaje kazi, lakini kwa wakati wetu kwa kupitia Bwana YESU, mambo hayo yapo wazi, na historia ikithibitisha hayo yote kuwa mpinga-kristo atatokea si pengine zaidi ya kanisa Katoliki la RUMI,.

Vivyo hivyo maarifa juu ya utawala wa amani wa YESU KRISTO wa miaka 1000 hayakujulikana kwa wakati ule, lakini sasahivi tunafahamu, n.k.; Na maarifa haya yanaendelea kuongezeka siku baada ya siku kwa msaada wa Roho wa Mungu mpaka tutakapofikia kilele cha utimilifu.

Kadhalika na maarifa katika mambo ya ulimwengu, yameongezeka, kama tunavyoona Jinsi Teknolojia inavyozidi kuongezeka, usafiri umekuwa wa haraka sana, watu wanaenda huku na huko dunia imekuwa kama kijiji. Na maarifa yataongezeka katika kila eneo.

Tukiendelea…

“Danieli 12:5 Ndipo mimi, Danielii, nikatazama, na kumbe, wamesimama wengine wawili, mmoja ukingoni mwa mto upande huu, na mmoja ukingoni mwa mto upande wa pili.

6 Na mmoja akamwuliza yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, Je! Itakuwa muda wa miaka mingapi hata mwisho wa mambo haya ya ajabu?

7 Nami nikamsikia yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, hapo alipoinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni; akaapa kwa yeye aliye hai milele na milele, ya kwamba itakuwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati; tena watakapokuwa wamekwisha kuvunja nguvu za hao watu watakatifu, ndipo mambo hayo yote yatakapotimizwa”. 

Tunaona baada ya Danieli kuelezwa juu ya dhiki kubwa itakayokuja huko mbeleni, Hapa tunaona malaika mmoja akimuuliza yule mtu aliyekuwa juu ya mto, kwamba hayo mambo yatadumu kwa miaka mingapi hadi yaishe, ndipo yule mtu akawaambia itakuwa ni kwa wakati na nyakati mbili na nusu wakati (ikiwa na maana ni MIAKA MITATU NA NUSU). Hii inaonyesha kuwa kipindi cha dhiki kuu kitadumu kwa muda wa miaka mitatu na nusu.

Danieli 12:8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?

9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa mwisho.”

Tunaona tena hapa Danieli kwa jinsi alivyokuwa “mtafutaji na mchunguzaji” alitaka kujua kwa undani tena juu ya matukio yatakayotokea katika utawala wa mwisho wa Rumi, kama alivyoelezewa na Gabrieli juu ya utawala wa Uajemi na Uyunani katika sura ya 11. Lakini aliambiwa Enenda zako Danieli, maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho ikiwa na maana kuwa asitafute kujua zaidi ya hapo, kwani yaliyosalia yamewekwa kwa ajili ya watu wa siku za mwisho yaani mimi na wewe.

Swali ni je! Na sisi tunatafuta kufahamu mambo hayo kama Danieli alivyotafuta kujua ya kwake?.

Danieli anaendelewa kuambiwa..

“Danieli 12:10 Wengi watajitakasa, na kujifanya weupe, na kusafika; bali wabaya watatenda mabaya; wala hataelewa mtu mbaya awaye yote; bali wao walio na hekima ndio watakaoelewa.”

Umeona hapo wakati wa mwisho dunia ikiwa katika kilele cha maovu, watu wamemsahau Mungu kwa mambo maovu kama anasa, ulevi, uasherati, matendo ya kikatili, fashion, udanganyifu wa mali n.k. wapo ambao watajitakasa na kujifanya kuwa watakatifu zaidi. Mfano dhahiri tunauona kwa Nabii Eliya wakati Israeli yote imegeukia kuabudu mabaali, na maovu yamezidi kila mahali, na pale Eliya alipojaribu kuwashitaki Israeli wote mbele za Mungu akidhani ya kuwa amebakia peke yake anayemcha Mungu. Lakini Mungu alimwambia kuwa amejisazia watu ELFU SABA wasiopigia goti baali.

Na vivyo hivyo kwa kizazi hichi kilichopotoka pale unapodhani hakuna tena watu wanaompendeza Mungu, hakuna tena wanawake wanaovaa vizuri, hakuna watu wanaomwabudu Mungu katika Roho na kweli , hakuna watakatifu n.k. fahamu kuwa Mungu amejisazia watu wake wachache kila mahali wanaoupendeza moyo wake na hao ndio watakaokuwa na hekima na kuzidi kujisafisha na kuelewa mambo hayo. Lakini kwa wale waovu biblia inasema wataendelea kuwa wabaya na hawatajua chochote na siku ile itawajilia kama mwivi, hivyo jiangalie na wewe upo kundi gani?. Usidanganyike na upepo wa huu ulimwengu kwamba wengi wanafanya hivi na mimi ngoja nifanye..Utaangamia.

Mwisho kabisa Danieli anaambiwa..

“Danieli 12:11 Na tangu wakati ule ambapo sadaka ya kuteketezwa ya daima itaondolewa, na hilo chukizo la uharibifu litakaposimamishwa, itapata siku elfu na mia mbili na tisini.

12 Heri angojaye, na kuzifikilia siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.

13 Lakini enenda zako hata utakapokuwa mwisho ule; maana wewe utastarehe, nawe utasimama katika kura yako mwisho wa siku hizo.”

Kuanzia kipindi kile mpinga-kristo atakapoingia katika HEKALU na kuwazuia wayahudi wasiendelee kutoa sadaka ya daima katika nyumba ya Mungu, ambayo itakuja kutengenezwa tena huko Yerusalemu (kumbuka maandalizi yote ya kujengwa sasa hivi yapo tayari), kwahiyo kuanzia hicho kipindi mpaka mwisho wa dhiki kutakuwa na siku 1290.

Sasa kumbuka biblia inasema kipindi cha dhiki kuu kitadumu kwa siku 1260 Yaani miaka mitatu na nusu ambapo mpinga-kristo atakuwa anafanya mauaji duniani kote, lakini hapa utaona zimeongezeka siku nyingine 30 za ziada yaani (1290-1260=30). Hizi siku 30 zilizoongezeka, ni kipindi kinachojulikana kama SIKU YA KUOGOFYA YA BWANA kwa kuajili ya kujilipizia kisasi kwa waovu wote wakaao juu ya nchi. Ni kipindi kitakachodumu katika hizi siku 30 ambacho kitahusisha mapigo ya vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu. (Ufunuo 16).

Ukiendelea mstari wa 13…utaona kuna siku nyingine tena 45 zimeongezea juu ya zile 1290 na kuwa siku 1335. Hichi kitakuwa ni kipindi cha matengenezo pamoja na hukumu ya mataifa,ambapo Bwana atakuja na mawingu na wafu watafufuliwa wahukumiwe (Ufunuo 20:14).

Hivyo kulingana na ukali wa hiyo dhiki yaani (dhiki ya mpinga-kristo pamoja na mateso ya SIKU YA BWANA) ni watu wachache sana watakaopona (wateule-wayahudi), Biblia inasema katika siku hiyo watu wataadimika kuliko DHAHABU (soma Isaya 13:9-13)

Na kama Bwana Yesu alivyosema katika Mathayo24:

22 “…..kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”..Na ndio maana utaona ni siku 1335 ambazo ni chache sana ukilinganisha na kama ingekuwa ni miaka 10 hakika asingepona mtu yeyote.

Mwisho wa yote Danieli anaambiwa “12 HERI ANGOJAYE, na kuzifikilia siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.”

Kumbuka ni wayahudi ndio wanaoambiwa HERI wakizifikia hizo siku, hivyo ni uvumilivu na kujificha, na saburi nyingi zinahitajika kwao, pamoja na hekima ya kuzihesabu hizo siku mpaka huo wakati utakapotimia wa Mungu kulipiza kisasi kwa mataifa yote yaliyoshirikiana na yule mnyama ambapo wakati huo Bwana atakapokuja hatarudi peke yake bali atarudi na Bibi-arusi wake(Kanisa) waliokwisha kunyakuliwa kabla ya dhiki kuanza..

Ndipo baada ya hayo utawala wa miaka 1000 utaanza ambapo BWANA atatawala kama MFALME WA WAFALME na BWANA WA MABWANA, na watakatifu wake watakuwa makuhani na wafalme milele na milele. Haleluya.

Je! Ndugu utakuwepo kwenye huo utawala? Je! umeokolewa?, angalia hatari iliyopo mbeleni, shetani anataka ubaki katika hali hiyo hiyo ili siku ile uijutee milele, anataka uzidi kupuuzia ivyo hivyo kila siku, usione kuwa Bwana anakaribia kuja, usipotaka kuacha ulevi,ushirikina, usengenyaji, uzinzi, vimini, suruali, fashion,pornography, kilichosalia mbele yako ni Hukumu tu.

Kumbuka Mungu hapendezwi na kufa kwake mwenye dhambi ..na ndio maana alisema.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”

Mpe Bwana maisha yako leo upate uzima wa milele…usiidharau damu ya thamani iliyomwagika kwa ajili yako pale Kalvari.

Na yeye alisema pale msalabani kwa wale waliompokea.. “IMEKWISHA!!”

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada Nyinginezo:

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.

UNYAKUO.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

BEI YA UFALME WA MBINGUNI.

MCHE MWORORO.

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

DANIELI: Mlango wa 11

Mungu wetu MKUU YESU KRISTO, asifiwe.

Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, kama tulivyoona katika mlango uliopita, Danieli akionyeshwa maono yale na Gabrieli, akiwa kando ya ule mto Hidekeli jambo hili tunalisoma katika ile sura ya 10, Lakini kwenye hii sura ya 11 na 12 tunaona ni mwendelezo ule ule wa mazungumzo kati ya Gabrieli na Danieli, Kumbuka baada ya Danieli kujinyenyekeza mbele za Mungu kwa kufunga na kuomba alionyeshwa mambo yatakayokuja kutokea katika kipindi chake na katika nyakati za mwisho, kwa undani zaidi.

Tukisoma…

Mlango 11:1 Tena mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario, Mmedi, mimi nalisimama nimthibitishe na kumtia nguvu.2 Nami sasa nitakuonyesha yaliyo kweli. Tazama, watasimama wafalme watatu katika Uajemi; naye mfalme wa nne atakuwa tajiri kuliko hao wote; naye atakapopata nguvu kwa utajiri wake, atawachochea wote juu ya ufalme wa Uyunani. 

Kumbuka sasa hapa ni Gabrieli anazungumza mazungumzo yaliyoanzia tokea sura ya 10, anamwambia Danieli, watasimama wafalme watatu katika ufalme wa Uajemi ambao aliyeko yeye, na watakapoondoka hao atakuja mfalme wa nne, ambaye atakuwa na nguvu kuliko hao wa kwanza. Historia inaonyesha walipita wafalme wanne katika utawala wa Uajemi baada ya Mfalme Koreshi, na inaonyesha huyo mfalme wa nne, alikuwa ni AHASUERO, yule wa malkia Esta, ambaye alikuwa na utajiri mwingi, ndio maana ukisoma kitabu cha Esta utaona aliweza kutawala kutoka bara Hindi mpaka Kushi majimbo 127, hivyo alikuwa ni mtawala mkuu sana, lakini mwisho wa utawala wake, alikuja kushindana na wafalme wa uyunani, lakini hakufanikiwa bali aliangamizwa na ufalme wake ukaanguka katika mikono ya wayunani.

Tukiendelea mstari wa 3-4..

“3 Na mfalme hodari atasimama, atakayetawala kwa mamlaka kubwa, na kutenda apendavyo.

4 Naye atakaposimama, ufalme wake utavunjika, na kugawanyika katika pepo nne za mbinguni; lakini hautakuwa wa uzao wake, wala hautakuwa kama mamlaka yake ambayo alitawala kwayo; kwa maana ufalme wake utang’olewa, hata kwa ajili ya wengine zaidi ya hao. “

Huyu Mfalme Hodari ni “Alexanda mkuu” ndiye aliyesimama na kuiangusha Uajemi, Na historia inaonyesha alikuwa na nguvu nyingi kila mahali alipokwenda kupigana alifanikiwa,hii ndio ile pembe moja mashuhuri ya yule beberu kama tulivyoiona katika ile sura ya 8, lakini kama hapo inavyosema ufalme wake utavunjika, ni kweli maana alikufa katika umri mdogo miaka 32, na uzao wake haukusimama na kuurithi ufalme wake, kinyume chake ufalme wake uligawanyika katika pande nne, zilizomilikiwa na majenerali waliokuwa chini yake ndio zile pepo nne za mbinguni. 

 Mstari wa 5.

” Na mfalme wa kusini atakuwa hodari; na mmoja wa wakuu wake atakuwa hodari kuliko yeye, naye atakuwa na mamlaka; mamlaka yake itakuwa mamlaka kubwa. “

Historia pia inaeleza baada ya huu Ufalme kugawanyika katika pande nne; kaskazini ilikuwa chini ya Lisimakusi, magharibi chini ya Kasanda, Mashariki chini ya Selekusi na kusini chini ya Ptolemi. Hivyo mmoja kati ya hawa majemedari wake (Alexanda) atakuwa hodari kuliko Ptolemi mfalme wa kusini na huyo sio mwingine zaidi ya SELEKUSI aliyekuwa mfalme wa Mashariki, ambaye historia inasema alifanikiwa kuwaangusha wafalme wale wawili yaani wa kaskazini na wa Magharibi na kumiliki mbili ya tatu ya ufalme wa Alexanda yaani mashariki, magharibi na Kaskazini, wakati Ptolemi alibakiwa na kusini tu.. Hivyo ufalme ukabakia katika pande mbili tu, kaskazini na Kusini.

Tukiendelea mstari wa 6.

“Na baada ya miaka kadha wa kadha watashirikiana; kwa kuwa binti wa mfalme wa kusini atakuja kwa mfalme wa kaskazini, ili kufanya mapatano naye; lakini hatakuwa na nguvu za mkono wake sikuzote; wala mfalme yule hatasimama, wala mkono wake; lakini yule binti atatolewa, na hao waliomleta, na yeye aliyemzaa, na yeye aliyemtia nguvu, zamani zile. “

Baada ya kipindi fulani kupita historia inarekodi Mfalme wa Pili wa Kaskazini (Antiokia Theo) na Mfalme wa tatu wa kusini (Ptolemi Filadelfia) walikuja kufanya mapatano, Mfalme wa kusini alimtoa Binti yake anayeitwa Berenisi, aolewe na mfalme wa kaskazini kwa mapatano kuwa mtoto atakayezaliwa amiliki falme zote mbili yaani ufalme wa Kaskazini na Ufalme wa kusini, Hivyo mfalme wa Kaskazini alimwacha mke wake wa kwanza(aitwaye Laodika) na kumuoa Berenisi na kuzaa naye mtoto.

Lakini biblia inasema hayo hayatawezekana, kwasababu baada ya baba yake Berenisi kufa, Mfalme wa kaskazini alimtalakia Berenisi na kurudiana na mke wake wa zamani Laodika, aliyeachiwa watoto wawili, Hivyo Laodika alipoona amerudishwa katika nafasi yake ya umalkia alimfanyia hila mfalme na kumpa sumu, Hivyo akafungua wigo wa watoto wake kuurithi ufalme, zaidi ya yote alikuja kumuua Berenisi pamoja na mtoto wake ili asipatikane wa kuchukua nafasi ya watoto wake, Hivyo mtoto wa Laodika aliyeitwa SELEKUSI KALINIKUSI akatangazwa kuwa mfalme mahali pa baba yake, ili kutimiza maono Danieli alioonyeshwa kwamba mfalme, wala yule binti wala mkono wake wala aliyemzaa hawatasimama.

 Tukiendelea…

“7 Lakini katika chipukizi la mizizi yake atasimama mmoja mahali pake atakayeliendesha jeshi la askari, naye ataingia katika ngome ya mfalme wa kaskazini, na kuwatenda mambo, na kuwashinda;

8 na miungu yao, pamoja na sanamu zao, na vyombo vyao vizuri vya fedha na dhahabu atavichukua mpaka Misri; kisha atajizuia miaka kadha wa kadha asimwendee mfalme wa kaskazini. “

Hili chipukizi la mizizi yake (yaani Berenisi) ambaye atasimama mahali pake, alikuwa ni Kaka yake Berenisi aliyeitwa PTOLEMI UGRETESI aliyerithi ufalme wa kusini baada ya Baba yake na dada yake kufa. Hivyo kwa hasira na ghadhabu ya kuuliwa kwa dada yake alipanga jeshi kubwa na kwenda kupambana na mfalme wa kaskazini, alifanikiwa kuingia kwenye ngome ya kaskazini akisaidiwa na mataifa ya kando kando yaliyokuwa yanamchukia mfalme wa kaskazini, hivyo aliweza kuteka nyara nyingi na kurudi nazo Misri, aliweza pia kuteka majimbo baadhi ya Asia ndogo na Siria yaliyokuwa yanamilikiwa na mfalme wa kaskazini na kuyafanya kuwa yake.

Mstari wa tisa unasema..

“9 Naye huyo ataingia katika ufalme wa mfalme wa kusini, lakini atarudi mpaka nchi yake mwenyewe.

10 Na wanawe watafanya vita, na kukusanya mkutano wa majeshi makuu; watakaokuja na kufurika na kupita katikati; nao watarudi na kufanya vita mpaka penye ngome yake.”

Mistari hii inaonyesha jinsi mfalme wa Kaskazini atakavyokwenda katika ufalme wa Kusini lakini alikuja kurudi katika nchi yake, lakini watoto wake wawili ambaye mmoja wao alikuja kufa baadaye walipanga majeshi kwenda kupigana na mfalme wa kusini ili kulipiza kisasi na kufanikiwa kurudisha majimbo yaliyochukuliwa na mfalme wa Kusini (Ptolemi ugretesi), Hivyo mmoja wa wale watoto aliyeitwa “ANTIOKIA MAGNUSI” alimpiga Ptolemi ugretesi na kufanikiwa kurejesha baadhi ya majimbo yaliyochukuliwa nayo ni Siria na Seleukia.

Tukiendelea..

“11 Na mfalme wa kusini ataingiliwa na ghadhabu, naye atatoka na kupigana naye, yaani, na mfalme wa kaskazini; naye atapanga jeshi kubwa; na jeshi hilo litawekwa mikononi mwake. “

Baada ya Ptolemi ugretesi kufa, “PTOLEMI FILOPATA” akamiliki badala yake, huyu ndiye aliyeingiliwa na ghadhabu kubwa kuona kwamba mfalme wa Kaskazini anamjia na jeshi kubwa, lakini kama biblia inavyotabiri jeshi hilo litawekwa mikononi mwake na ndivyo ilivyokuwa, Mfalme wa Kaskazini alikuja kupigwa na Mfalme wa Kusini katika vita vya Rafia pembezoni mwa Gaza mwaka 217 KK.

 Tukiendelea..

“12 Atakapokwisha kuchukua lile jeshi, moyo wake utatukuzwa; naye atawaangusha makumi elfu; lakini hataongezewa nguvu. “

Baada ya kushinda vita dhidi ya ufalme wa Kaskazini moyo wake ulijitukuza..

Tukiendelea..

“13 Kwa maana mfalme wa kaskazini atarudi, naye atapanga jeshi kubwa kuliko lile la kwanza; naye hakika atakuja mwisho wa zamani zile, yaani, baada ya miaka kadha wa kadha, pamoja na jeshi kubwa na mali nyingi.

14 Na zamani zile watu wengi watasimama ili kumpinga mfalme wa kusini; pia, wenye jeuri miongoni mwa watu wako watajiinua ili kuyathibitisha maono; lakini wataanguka.

15 Basi mfalme wa kaskazini atakuja, na kufanya kilima, na kuupiga mji wenye maboma; na silaha za kusini hazitaweza kumpinga, wala watu wake wateule, wala hapatakuwa na nguvu za kumpinga.

16 Maana ajaye kupigana naye atatenda kadiri apendavyo, wala hapana mtu atakayesimama mbele yake; naye atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi mwake. “

Hili lilikuja kutimia pale Mfalme wa Kaskazini (Antiokia III Magnus) alipopanga majeshi makubwa, na kwenda kupambana na mfalme wa Kusini, na kumshinda, na baadhi ya wayahudi wenye kiburi walimuunga mkono Antiokia kumpinga mfalme wa Kusini,ili kuyathibitisha maono, hivyo ilimsaidia Antiokia kupata nguvu, lakini hawakujua kama hayo yatawageukia kuwa mwiba kwao, kwasababu baada ya huyo atanyanyuka mfalme atakayewatesa na kuwaua. Hivyo aliposhinda akawa na nguvu juu ya NCHI YA UZURI (yaani Israeli) na hakuna taifa lililoweza kusimama dhidi yake.

“17 Naye atakaza uso wake ili aje pamoja na nguvu zote za ufalme wake, naye atafanya mapatano naye; naye atatenda kadiri apendavyo; naye atampa binti wa watu ili amharibu; lakini hilo halitasimama wala kumfaa. “

Zaidi ya yote Antiokia III, alitaka kumiliki mpaka ufalme wa kusini yaani Misri, hivyo alitumia hila kwa kumpa Binti yake (aitwaye Kleopatra) mfalme wa Kusini (Ptolemi) ili kwamba amsaliti na kisha baadaye auchukue ufalme wote lakini hilo halikufanikiwa kwasababu Kleopatra badala ya kumsaliti Ptolemi moyo wake uliambatana naye.

“18 Baada ya hayo atauelekeza uso wake kwenye visiwa, naye atavipiga visiwa vingi; lakini mkuu mmoja ataikomesha aibu iliyoletwa na yeye; naam, aibu yake hiyo atamrudishia mwenyewe.

19 Ndipo atauelekeza uso wake kwenye ngome za nchi yake mwenyewe; lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena”. 

Historia inaonyesha baada ya Antiokia III, kuona amelaghahiwa na binti yake, alimua kuhamishia jitihada zake katika nchi za visiwa vya mbali ambavyo ni Asia ndogo na Ugiriki ili kutanua milki yake, lakini Jenerali mmoja wa Kirumi aliyeitwa “LUKAS KORNELIO SKOPIO” alimpiga na kumshinda kabisa na kumnyang’anya alivyokuwa navyo alipojaribu kuivamia Ugiriki, Hivyo aibu yake ikamrudia mwenyewe kama biblia ilivyosema badala ya kushinda, alishindwa.

Na hata aliporudi kwake hakuwa salama baada ya muda mfupi aliuawa.

 Tukiendelea..

“20 Ndipo badala yake atasimama mmoja, atakayepitisha mwenye kutoza ushuru kati ya utukufu wa ufalme wake; lakini katika muda wa siku chache ataangamizwa, si kwa hasira, wala si katika vita. “

Baada ya Antiokia III mfalme wa kaskazini kufa mtoto wake aliyeitwa SELEUKIA FILOPATAalitawala mahali pake, huyu alikuja na sera ya kuongeza kodi katika ufalme wake ili kuzidisha mapato. Alijaribu kufanya hivyo hata katika Israeli na kufikia hatua ya kutaka kujaribu kuteka Hekalu la Mungu lililopo Yerusalemu kwa nguvu lakini hilo halikuwezekana, alikuja kufa baada ya muda mfupi hakufanikiwa kutawala kwa muda mrefu kama Baba zake. Kama ilivyotabiriwa.

 “21 Kisha badala yake atasimama mmoja, mtu astahiliye kudharauliwa, ambaye hawakumpa heshima ya ufalme; naye atakuja wakati wa amani, naye ataupata ufalme kwa kujipendekeza. “

Huyu alikuwa ni “ANTIOKIA IV EPIFANE”, ndugu yake Seleukia, alinyanyuka japo alishutumiwa kwa kumuua kaka yake hakupata ufalme kwa njia ya halali, bali alitumia njia za kujipendekeza za kutoa ahadi za kulaghai,kujinyanyua, na rushwa, ili kupata ufalme na jambo hilo lilifanikiwa mikononi mwake. Mfano dhahiri wa mpinga-kristo atakayekuja atatafuta ufalme kwa kujipendekeza.

Mstari wa..

“22 Na wale wenye silaha mfano wa gharika watagharikishwa mbele yake, na kuvunjika, naam, mkuu wa maagano pia.

23 Na baada ya maagano atatenda kwa hila; maana atapanda, naye atakuwa hodari pamoja na watu wadogo.

24 Wakati wa amani atapaingia mahali palipofanikiwa sana pa wilaya hiyo; naye atatenda mambo ambayo baba zake hawakuyatenda, wala babu zake; atatawanya kati yao mawindo, na mateka, na mali; naam, atatunga hila zake juu ya ngome, hata wakati ulioamriwa.

25 Naye atachochea nguvu zake na ushujaa wake juu ya huyo mfalme wa kusini kwa jeshi kubwa; na mfalme wa kusini atafanya vita kwa jeshi kubwa mno lenye nguvu nyingi; lakini hatasimama; maana watatunga hila juu yake.

26 Naam, walao sehemu ya chakula chake watamwangamiza, na jeshi lake litagharikishwa; na wengi wataanguka wameuawa. “

Tunasoma katika historia, Antiokia IV Epifane alishuka kupigana na Misri lakini hakushinda kwasababu Misri ilisaidiwa na Rumi, na zaidi ya yote washauri wake walimfanyia hila hivyo akapigwa katika vita.

 “27 Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa.

28 Ndipo atakaporudi mpaka nchi yake mwenye utajiri mwingi; na moyo wake utakuwa kinyume cha hilo agano takatifu; naye atafanya kama apendavyo, na kurudi mpaka nchi yake. “

Antiokia alipotoka Misri kwa hasira ya kushindwa vita, alifika Yerusalemu na kuwakasirikia wayahudi pamoja na Hekalu la Mungu, ndipo dhiki ya wayahudi ilipoanzia.

 Mstari wa..

“29 Kwa wakati ulioamriwa atarudi, na kuingia upande wa kusini; lakini wakati wa mwisho mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa wakati wa kwanza.

30 Maana merikebu za Kitimu zitakuja kupigana naye; basi atavunjika moyo, naye atarudi na kulighadhibikia hilo agano takatifu; na kutenda kadiri apendavyo; naam, atarudi, na kuwasikiliza walioacha hilo agano takatifu.”

Merikebu za Kitimu ni Warumi waliowasaidia wamisri kupigana naye..lakini aligeuza moyo wake ni kurudi Yerusalemu kupambana na hao walioonekana kwenda kinyume na yeye (wayahudi).

“31 Na wenye silaha watasimama upande wake, nao watapatia unajisi mahali patakatifu, ndiyo ngome, nao wataondoa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, nao watalisimamisha chukizo la uharibifu. “

Historia inasema Antiokia IV, aliingia kwenye hekalu la Mungu huko Yerusalemu na kuweka sanamu ya Mungu wake ZEU, na kuwazuia wayahudi wasitoe sadaka za kuteketezwa za daima katika hekalu la Mungu.

Tukiendelea..

“32 Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza; lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.

33 Na hao walio wenye hekima katika watu watafundisha wengi; hata hivyo wataanguka kwa upanga, na kwa moto, na kwa kufungwa, na kwa kutekwa nyara, siku nyingi.

34 Basi watakapoanguka, watasaidiwa kwa msaada kidogo; lakini wengi wataambatana nao kwa maneno ya kujipendekeza.

35 Na baadhi yao wenye hekima wataanguka, ili kuwatakasa, na kuwasafisha, na kuwafanya weupe, hata wakati wa mwisho; kwa maana ni kwa wakati ulioamriwa, ambao haujaja.

36 Naye mfalme atafanya kama apendavyo; naye atajitukuza na kujiadhimisha juu ya kila mungu, naye atanena maneno ya ajabu juu ya Mungu wa miungu, naye atafanikiwa mpaka ghadhabu itakapotimia; maana yaliyokusudiwa yatafanyika.”

Antiokia ni mfano dhahiri wa mpinga-kristo atakayekuja, kama tunavyosoma kwenye 2Wathesalonike 2:3-4, inasema…3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.

Hivyo unaona hapo Antiokia ni kivuli halisi cha mpinga-kristo (PAPA) atakayekuja.

 “37 Wala hataijali miungu ya baba zake; wala yeye aliyetamaniwa na wanawake; wala hatamjali mungu awaye yote; maana atajitukuza mwenyewe juu ya wote.

38 Lakini katika mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua atamheshimu, kwa dhahabu, na fedha, na vito vya thamani, na vitu vipendezavyo.

39 Naye ataziteka nyara ngome zenye nguvu kwa msaada wa mungu mgeni; na yeye atakayemkubali atamwongeza kwa utukufu; naye atawapa kumiliki wengi; naye ataigawa nchi kwa rushwa,

40 na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati.

41 Tena ataingia katika hiyo nchi ya uzuri, na nchi nyingi zitapinduliwa; lakini nchi hizi zitaokolewa na mkono wake, Edomu, na Moabu, na wakuu wa watu wa Amoni.”

Hizi nchi za Edomu, na Moabu pamoja na Edomu hakuzigusa kwasababu zilimsaidia kwenda kinyume na Israeli (Nchi ya Uzuri).

“42 Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka.

43 Lakini atakauwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibia na Wakushi watafuata nyayo zake.

Historia inaonyesha alifanikiwa kuwa na hazina nyingi za fedha na dhahabu mfano dhahiri wa mpinga-Kristo atakayekuja..(PAPA), Ukitazama utaona hazina kubwa ya dunia sasa ipo Roma.

 Mstari wa 44..

“44 Lakini habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi.

45 Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri; lakini ataifikilia ajali yake, wala hakuna atakayemsaidia. “

Antiokia IV Epifane alikuja kufa, Kifo chake kilikuja ghafla na hakuna aliyemsaidia pamoja na kujiiunua kwake kama mungu na kujitukuza vile alianguka ghafla,. Kuonyesha kuwa hakuna tumaini lolote kwa mpinga-kristo atakayekuja na kwa watu wake, Biblia inasema.Ufunuo 18:8″ Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika SIKU MOJA, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu. “

Kumbuka Dhumuni kubwa la Gabrieli kumuonyesha Danieli mambo haya yote moja baada ya lingine yatakayotokea katika utawala aliokuwa anaishi na kwa sehemu utawala utakaokuja, ni kumfanya Danieli aelewe mpango wa Mungu kwa kina. Kama tunavyosoma katika sura zilizopita Danieli hakuonyeshwa mambo haya kwa undani juu ya hizi falme kama alivyoonyeshwa katika Sura hii..

Vivyo hivyo na kipindi tunachoishi sasa, Bwana anayo AGENDA, kwa Kanisa lake, lilipotoka,lililopo na linapokwenda! swali ni je! Unafahamu AGENDA ya Mungu kwa wakati unaoishi??..je unajua kuwa kanisa unaloishi ni la mwisho kati ya yale saba ambayo Kristo aliyataja katika Ufunuo 2 na 3

Je! Unafahamu kuwa mihuri saba ilishafunuliwa?, Je unafahamu kuwa ile chapa ya mnyama imeshaanza kutenda kazi,? tena kibaya zaidi inatenda kazi ndani ya makanisa?..Kama huyafahamu hayo, ni vizuri ukatenga muda umuombe Mungu akufunulie kama Danieli alivyoomba ili siku ile isije ikakujia kama mwivi kwa kukosa kuwa na maarifa..Kumbuka tunaishi katika kizazi ambacho kitaweza kushuhudia kuja kwa pili kwa Kristo, je! umeokolewa?

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; “

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Katika sura ya 12 tutaona jinsi yule malaika(Gabrieli) akimfunulia Danieli mambo ambayo yatakuja kutokea katika ule ufalme wa mwisho wa RUMI.

Kwa mwendelezo >>> Mlango wa 12


Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 17

UFUNUO: MLANGO WA 18

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

ESTA: MLANGO WA 1 & 2

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

DANIELI: Mlango wa 10

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe.

Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, leo tukitazama ile sura ya 10, Kama tukiangalia kwa undani kitabu hichi tutaona kuwa sehemu kubwa ya Unabii Danieli aliopewa ulikuwa unahusu zile FALME 4 zitakazotawala mpaka mwisho wa dunia, ambazo ni 1) BABELI 2) UMEDI na UAJEMI 3) UYUNANI na 4) RUMI.

Lakini kama ukichunguza ile sura ya pili, utaona Danieli alifunuliwa kwa juu juu picha inayohusu falme hizo, kwa kupitia ndoto ya mfalme Nebukadneza aliyoiota juu ya ile sanamu, tunaona pale hakupewa maelezo yoyote marefu kuhusu hizo falme, alionyeshwa tu utaanza ufalme wa kwanza ambao ni wa dhahabu, kisha fedha, halafu shaba na mwisho chuma, hakupewa hata majina ya falme hizo zitakazokuja kutawala baadaye isipokuwa Babeli tu.

Lakini pamoja na hayo Danieli hakuridhika aliendelea kumsihi Mungu amfunulie undani wa mambo hayo na ndio maana tunaweza kuona katika sura ya 7, akionyeshwa maono yanayohusu jambo lilelile isipokuwa hapa yameingia kwa undani zaidi tofauti na alivyoonyeshwa kule kwanza.

Tunasoma aliona wanyama 4 wakitoka baharini ambao ndio zile zile falme 4 zenyewe. Mnyama wa kwanza ndio yule kama simba(Babeli), wa pili alikuwa kama dubu na mifupa mitatu ya mbavu mdomoni mwake ambayo tulishaona tafsiri yake ni nini, wa nne alikuwa mfano wa chui mwenye vichwa vinne, na tunaona Danieli alipewa tafsiri juu ya vichwa vile akaelezwa kuwa watakuwa ni wafalme 4 watakaonyanyuka katika huo utawala wa tatu ambao ni wa uyunani, pia akaonyeshwa mnyama mwingine wa mwisho wa 4 ambaye alikuwa mbali sana na wale wengine kimaumbile.

Pamoja na hayo Danieli katika maono haya alitajiwa na majina ya falme hizi 2 zitakazofuata, tofauti na maono yale ya kwanza hapa alifunuliwa kuwa ufalme wa pili utakuwa ni UMEDI NA UAJEMI, na watatu utakuwa ni ufalme wa UYUNANI. Kwa undani wa maelezo haya unaweza ukasoma mlango wa 7 tuliokwisha kuupitia.

Lakini bado tunaona Danieli baada ya kuona hayo picha bado haikuwa dhahiri kwake hivyo alikuwa na shauku ya kuzidi kufahamu juu ya mambo hayo yataishiaje, na ndio tunaona katika ile sura ya 8 Mungu aliendelea kumfunulia juu matukio yatakayokuwa yanatendeka ndani ya hizo falme, hapa tunaona akionyeshwa yule kondoo mwenye pembe mbili na Beberu, ambapo yule Beberu alikuja kumshambulia yule kondoo na kumuua kwa ile pembe moja aliyokuwa nayo, ambayo baadaye ilikuja ikavunjika na kuzuka pembe nyingine nne.

Sasa Danieli alizidi kuonyeshwa kwa ufafanuzi zaidi mambo yatakayokuja kutokea katikati ya hizi falme, kwamba yule kondoo mwenye pembe mbili ni ufalme wa Umedi na Uajemi, na yule beberu ni ufalme wa uyunani, na ile pembe moja ni mfalme wa kwanza wa uyunani ambaye atanyanyuka na kuuvunja ufalme wa Uajemi, kumbuka mambo hayo yote Danieli hakuonyeshwa katika maono mengine yaliyotangulia, hivyo unaweza ukaona ni mambo yale yale isipokuwa Danieli anafunuliwa kwa undani zaidi, ukiendelea kusoma utaona alionyeshwa pia kutakuwa na pembe nyingine ndogo itakayozuka katikati ya zile pembe 4, itakayojitukuza mbele za Mungu na huyu si mwingine zaidi ya ANTIOKIA EPIFANE 1V. wa uyunani kama historia inavyoonyesha.

Kumbuka Danieli wakati anaonyeshwa juu ya Falme hizi ukisoma katika ile sura ya 7 aliona pembe ndogo(mpinga-kristo) ikizuka katika ufalme wa mwisho wa 4 ambao tunafahamu ni Rumi, lakini hakuonyeshwa pembe nyingine ndogo itakayozuka katika Ufalme wa 3 wa uyunani, lakini hapa tunaona ameonyeshwa pembe hii katika sura hii ya 8. Hivyo tunaona ni mwendelezo wa maono yale yale isipokuwa kwa undani zaidi.

Vivyo hivyo ukiendelea sura ya 10, 11 na ya 12, utaona jinsi Danieli akifunuliwa maono yale yale kwa uchambuzi zaidi, tukio baada ya tukio, mpaka maono yale yakawa dhahiri kwake.

Kwenye Sura hii ya 10 tunaona Danieli akijisogeza mbele za Mungu kwa unyenyekevu akimsihi Mungu ampe ufahamu zaidi juu maono hayo aliyokuwa anafunuliwa na ndio maana utaona baada ya kufunuliwa biblia inasema “alifahamu na kuelewa maono yale”, ikiwa na maana hapo mwanzo mambo yale hayakuelewa vizuri kwake.

Tukisoma..

Mlango 10:1-21”

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni VITA VIKUBWA; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo.

2 Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.

3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia.

4 Na siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kando ya ule mto mkubwa, Hidekeli;

5 naliinua macho yangu, nikatazama, na kumbe, mtu aliyevikwa nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi;

6 mwili wake pia ulikuwa kama zabarajadi safi, na uso wake mfano wa umeme, na macho yake kama taa za moto, na mikono yake na miguu yake rangi yake kama shaba iliyosuguliwa sana, na sauti ya maneno yake kama sauti ya umati wa watu.

7 Nami, Danielii, nikaona maono haya peke yangu; maana wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona maono haya; lakini tetemeko kuu liliwashika, hata wakakimbia ili kujificha.

8 Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikusaziwa nguvu.

9 Walakini naliisikia sauti ya maneno yake; nami niliposikia sauti ya maneno yake, ndipo nikashikwa na usingizi mzito, na uso wangu umeielekea nchi.

10 Na tazama, mkono ukanigusa, ukaniweka juu ya magoti yangu, na vitanga vya mikono yangu.

11 Akaniambia, Ee Danieli, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka.

12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.

13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.umed

15 Na alipokwisha kusema nami maneno hayo, nikauelekeza uso wangu chini, nikawa bubu.

16 Na kumbe, mmoja mfano wa wanadamu akanigusa midomo yangu; ndipo nikafumbua kinywa changu, nikanena, nikamwambia yeye aliyesimama karibu nami, Ee Bwana wangu, kwa sababu ya maono haya huzuni zangu zimenipata tena; hata asikusaziwa nguvu.

17 Maana, mtumishi wa Bwana wangu huyu atawezaje kusema na Bwana wangu huyu? Kwa maana kwangu mimi, mara hazikusalia nguvu ndani yangu, wala pumzi haikusalia ndani yangu.

18 Kisha mmoja mfano wa mwanadamu akanigusa tena, akanitia nguvu.

19 Akasema, Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Aliposema nami nikapata nguvu, nikasema, Ee Bwana wangu, na aseme Bwana wangu; kwa maana umenitia nguvu.

20 Ndipo akasema, Je! Unajua sababu hata nikakujia? Na sasa nitarudi ili nipigane na mkuu wa Uajemi; nami nitakapotoka huku, tazama, mkuu wa Uyunani atakuja.

21 Lakini nitakuambia yaliyoandikwa katika maandiko ya kweli; wala hapana anisaidiaye juu ya hao ila huyo Mikaeli, mkuu wenu.

Kumbuka sura hii inaeleza jinsi Gabrieli alivyomtembelea Danieli, akimweleza sababu ya kukawia kwake, kwamaana hata baada ya Danieli kumaliza kufunga na kuomboleza majibu yalikuwa hayajafika bado, Lakini ujumbe kamili Gabrieli aliomletea ulikuwa unahusu maelezo ya ndani kabisa yahusuyo zile falme na sio kitu kingine, ambayo tutakuja kuona katika sura ya 11 na 12.

Lakini katika sura hii tutaona SIRI zilizopelekea Danieli kupokea mafunuo makubwa kama yale, Awali ya yote Danieli alisema NI VITA VIKUBWA, ikiwa na maana kuwa kuna upinzani mkubwa katika kuyapata mambo hayo, Tunaweza kusoma pale Gabrieli alimwambia “Tangu siku ile ya kwanza alipoutia moyo wake ufahamu maombi yake yalisikiwa Lakini mkuu wa ufalme wa uajemi alimpinga siku 21…”

Tunajifunza nini hapo? Mungu huwa hamjibu mtu maombi yake baada ya kufunga na kuomba, hapana bali huwa anamjibu mtu maombi yake pale tu anapotia moyo wake ufahamu, na ndipo maagizo yanatolewa papo hapo na ndio maana Bwana Yesu alisema (Mathayo 6:8) “Baba yetu anajua tunachohitaji kabla hata hatujamwomba” unaona?.. Lakini sasa adui yupo huyo ndiye anayehakikisha majibu hayafiki kwa muhusika, hivyo inahitaji kupigana vita kumshinda.

VITA KATIKA ANGA.

Kama ukisoma hapo juu utaona kuwa mkuu wa ufalme wa uajemi alimpinga Gabrieli, pia ukiendelea kusoma utaona alisema “atakapotoka huko kupigana na mkuu wa uajemi, mkuu mwingine w a Uyunani atakuja”. Sasa kumbuka hawa wakuu wa uajemi na uyunani sio wafalme wa dunia, bali ni roho za mashetani zilizokuwa zinaendesha hizo falme 4 za dunia, kumbuka wakati Danieli anafunuliwa maono haya alikuwa katika Ufalme wa Uajemi, Babeli ilikuwa imeshaanguka, Hivyo mkuu wa ufalme wa Babeli (PEPO) alikuwa ameshaondoka, lililopo hapo ni la uajemi, kisha litakuja PEPO la Uyunani na mwisho litakuja la RUMI, ambalo ndio lipo sasahivi likitenda kazi.

Lakini kumbuka kama biblia inavyosema Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na mamlaka, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. “

Neno hilo likiwa na maana kuwa hatutumia njia za kibinadamu kushinda na hizi FALME za giza, Kushindana kwetu sio kusema ninatuma kombora, au moto, kuzimu, au maombi ya kuteketeza anga na wakuu wa anga, hapana Danieli hakufanya hivyo, njia hiyo ni kwa namna ya damu na nyama na haiwezi kumshinda shetani hata kidogo, bali biblia inaendelea kusema..

Waefeso 6: 13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga KWELI viunoni, na kuvaa dirii ya HAKI kifuani,

15 na kufungiwa miguu UTAYARI tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya IMANI, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya WOKOVU, na upanga wa ROHO ambao ni NENO LA MUNGU;

Hivyo malaika kabla ya kuwasilisha maombi ya mtu kwanza huwa anakutana na MSHITAKI HAPO JUU (mkuu wa giza na mapepo yake), ambaye anatushitaki sisi mbele za Mungu (Ufunuo 12:10)kwa kuonyesha kwamba hatustahili kukipokea kitu tunachokiomba, na hoja yake ikiwa na nguvu, majibu hayatufikii anayazuia kwa kuwa ana hati miliki yako, (kwamfano, mtu anaomba jambo fulani kwa Mungu halafu bado anamashaka mashaka kama kweli atajibiwa maombi yake au la!. biblia inasema lolote muombalo aminini ya kwamba mmepokea nalo litakuwa lenu. Sasa mwovu, akikuangalia na kuona kuwa hauna Imani ya kupokea jambo hilo mitikisiko fulani inakutokea unakataa tamaa, yeye anatumia hiyo nafasi kukushitaki mbele za Mungu kuwa huyu mtu hana uhakika na anayemwomba hivyo hastahili kupokea hicho kitu, hapo shetani anakuwa ameshinda vita, hivi ndio vita vinavyopiganwa. Na ndio maana biblia inasema Imani ni ngao itakayoweza kuzima mishale yote ya moto ya yule mwovu.

Yakobo 1:5-8″ Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.

6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. “

Mfano mwingine mtu anaomba Neno fulani kwa Mungu, halafu hajakoloewa, tatizo sio kwamba maombi yake hayajasikiwa, hapana bali MKUU WA GIZA yupo hapo juu akipeleka hoja juu ya maisha yako mbele za Mungu, kwamba Neno linasema ” Mtu yeyote asiye na Roho wa Kristo huyo sio wake (Warumi 8:9)” Hivyo yule malaika aliyetumwa kukuletea majibu akikutana na hoja zenye nguvu kama hizo atakwama, maana yule mshitaki atamwambia, Mtu huyu ni mali yangu kwasababu hana Roho wa Mungu, hivyo haya majibu hayamuhusu. Sasa mtu wa namna hii kakosa CHEPEO YA WOKOVU na UPANGA WA ROHO. hivyo lazima vita hivi vimshinde tu na akose anachokitafuta.

Mfano mwingine mtu anayeabudu sanamu (sanamu za bikira Maria, na watakatifu, pamoja na kusali rozari), halafu bado unakwenda kumwomba Mungu, mkuu wa giza atapeleka hoja, za kimaandiko “Kutoka 20:4 inasema Mungu atawapatiliza maovu yao hao wote wanaoabudu sanamu kwa wivu wake”, Hivyo badala ya kupokea baraka, yanageuka kuwa laana kwa mtu huyo.

Neno la Bwana linasema..

Ezekieli 14: 3, & 7-8 “Mwanadamu, watu hawa wametwaa VINYAGO vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu NIULIZWE na wao katika neno lo lote?

…….7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na KULIWEKA KWAZO LA UOVU MBELE YA USO WAKE, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;

8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. “

Kwahiyo kwa Danieli mpaka majibu kama hayo kumfikia, aliweza kumshinda (mkuu wa uajemi) katika nyanja zote katika ulimwengu wa roho, hivyo shetani alishindwa kwasababu hakuwa na hoja yoyote ya kumshitaki mbele za Mungu yamfanye asipokee majibu yake.

Na faida aliyoipata Danieli baada ya kushinda tunaweza kuiona katika sura zinazofuata, Mungu aliweza kumfunulia agenda na mpango mzima wa mambo yanayokuja mbeleni juu ya ufalme aliokuwepo na unaokuja wa Uyunani pamoja na ule wa mwisho. hatua kwa hatua tofauti na maono aliyokuwa anayaona mwanzo, mambo hayo utayaona katika sura ya 11 na 12.

Kwahiyo kwa ujumla tunaweza kujifunza katika sura hii Danieli ni mtu aliyekuwa anahama kutoka utukutu hata utuktufu, ono moja halikumfanya aridhike na hali aliyopo aliendelea kutafuta kwa kusoma vitabu na kuomba mpaka mambo yote ya mbeleni yakawa wazi kwake, na sisi vivyo hivyo tunahitaji kusoma sana maandiko na kuomba, mpaka mambo yatakayotukabili huko mbeleni yawe wazi kwetu, hatupaswi kuridhika tu katika hali tulizopo angali tukijua hatufahamu yanayokuja mbeleni.

Biblia inasema Bwana Yesu alikuwa akiongezeka KIMO na HEKIMA, kumbuka sio KIMO cha urefu bali Kimo cha kumjua Mungu, na aliongezeka hekima pia ya kuyajua mapenzi ya Mungu, ikiwa na maana kuwa alipozaliwa sio kwamba alikuwa anajua kila kitu kama ndio hivyo alipokuwa na miaka 12 asingekuwa anawasikiliza na kuwauliza maswali marabi, Hii inaonyesha kuwa alikuwa anakua kwa hekima. Sasa kama yeye ambaye ni Bwana wetu alifanya hivyo inatupasaje sisi?. Tunapaswa tukue tufikie cheo cha kimo cha utimilifu wake (Waefeso 4:13).

Kumbuka pia mkuu wa giza tulilopo sio tena wa uyunani au uajemi bali ni RUMI, na ni roho inayowapofusha watu wasione mbele, wala wasitake kufahamu mambo ya mbele kama wale wengine walivyomzuia Danieli asione mambo ya mbeleni, kwahiyo fahamu kuwa vita vilivyopo sasahivi ni vikubwa kuliko vile vya Danieli. Si ajabu watu wamepoteza hamu ya kufahamu mambo ya mbeleni na mbinguni, injili wanazopenda kuzisikia ni za mafanikio tu, na mambo ya ulimwengu huu yanayopita, ni dhahiri kabisa mkuu wa giza hili amewapofusha macho.

Hivyo ndugu kama unaabudu sanamu, kama hujaokolewa, kama unaishi katika dhambi, kama Huliamini Neno la Mungu, una mashaka upo vuguvugu, fahamu upo chini ya mamlaka ya mkuu wa anga hili, na yeye ndiye mshitaki wako mbele za Mungu usiku na mchana ili usione mambo ya mbeleni au usipokee baraka za Mungu na mwisho kabisa usiione mbingu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa mwendelezo >>> Mlango wa 11

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada Nyinginezo:

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI.

MKUU WA GIZA.

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

VITA BADO VINAENDELEA.

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

DANIELI: Mlango wa 9

Jina la Bwana wetu na mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe;

Katika sura hii tunaona Danieli kwa shauku ya kutaka kujua hatma ya Taifa lake Israeli na watu wake,hata lini wataendelea kukaa katika nchi ya ugenini,aliazimu kutafuta kwa bidii, kwa njia nyingi ikiwemo kwa kusoma VITABU, na kufunga na kuomba juu ya jambo hilo mpaka akasikiwa. Kama tunavyosoma;

Danieli 9:1-2 ” Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo;

2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, KWA KUVISOMA VITABU, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, MIAKA SABINI.

Tukisoma habari hii (Danieli 9:–2) tunaona Danieli alikwenda kusoma VITABU, na sio KITABU, ikiwa na maana kuwa alisoma kitabu zaidi ya kimoja, na moja ya hicho kilikuwa ni kitabu cha Yeremia Nabii. Na katika kuchunguza kwake alikutana na maandiko yanayosema hivi.

Yeremia 29:1-10″ Maneno haya ndiyo maneno ya waraka, ambao nabii Yeremia aliupeleka toka Yerusalemu, kwa hao waliobaki wa wakuu waliochukuliwa mateka, na kwa makuhani, na kwa manabii, na kwa watu wote, ambao Nebukadreza aliwachukua mateka toka Yerusalemu hata Babeli.

2 (hapo walipokwisha kutoka Yerusalemu Yekonia mfalme, na mama yake mfalme, na matowashi, na wakuu wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi, na wahunzi;)

3 kwa mkono wa Elasa, mwana wa Shafani, na Gemaria, mwana wa Hilkia, (ambao Sedekia, mfalme wa Yuda, aliwatuma hata Babeli, kwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli), kusema,

4 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, AWAAMBIA HIVI WATU WOTE WALIOCHUKULIWA MATEKA, NILIOWAFANYA WACHUKULIWE TOKA YERUSALEMU MPAKA BABELI;

5 Jengeni nyumba, mkakae ndani yake, kapandeni bustani, mkale matunda yake;

6 oeni wake, mkazae wana na binti; kawaozeni wake wana wenu, mkawaoze waume binti zenu, wazae wana na binti; mkaongezeke huko wala msipungue.

7 Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani.

8 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Manabii walio kati yenu, na wabashiri wenu, wasiwadanganye ninyi, wala msisikilize ndoto zenu, mnazootesha.

9 Kwa maana kwa jina langu hutabiri maneno ya uongo kwenu; mimi sikuwatuma, asema Bwana.

10 Maana Bwana asema hivi, BABELI UTAKAPOTIMIZIWA MIAKA SABINI, NITAWAJILIA NINYI, NA KULITIMIZA NENO LANGU JEMA KWENU, KWA KUWARUDISHA MAHALI HAPA.”

Unabii huu Bwana aliwaambia watu wa Yuda kwa kinywa cha Yeremia kutokana na maasi yao na uovu wao kwamba watachukuliwa mateka na watu wa Babeli nao watakaa huko kwa muda wa miaka 70 kisha Bwana atawajilia tena na kuwarudisha katika nchi yao. Kumbuka wakati wayahudi wote wakiwa wamelala licha ya kuwa katika hali yao ya utumwa Danieli aliazimu binafsi kutafuta kufahamu majira na nyakati anazoishi, kwa maana Bwana Yesu alisema katika Mathayo 7, tafuteni nanyi mtaona, kwa maana kila atafutaye huona. Hivyo Danieli kwa kufanya hivyo kutafuta kwa bidii, Mungu alimjalia kuona kuwa imebakia miaka miwili tu, mpaka wao kutoka Babeli yaani walikuwa wameshamaliza miaka 68 kati ya ile 70 ya wao kukaa utumwani. Na ndio maana Biblia imemwita Danieli kama mtu mwenye Hekima, na mtu apendwaye sana.kwasababu ni mtu aliyependa kutafuta kujua majira na saa anayoishi.

Vivyo hivyo na kizazi chetu cha mwisho tulichopo, Mungu ameshaweka majira ya watoto wake kwenda kwenye unyakuo na siku ambayo hii Babeli ya rohoni itakapo hukumiwa, Kumbuka Mungu hana desturi ya kumlazimisha mtu kufahamu agenda yake ya ukombozi bali wale waliotayari na wanaotafuta kujifunza na kutuka kujua ndio watakaofahamu, na Mungu atawaongoza katika Kusoma, na ndio maana kuna umuhimu sana wa KUJIFUNZA na KUYACHUNGUZA MAANDIKO kila Siku, kwasababu SIRI nyingine hazitafahamika isipokuwa kwa kujifunza sana NENO LA MUNGU kwa mfano wa Danieli.

Hauoni hata katika majira tunayoishi, ile roho ya mpinga-kristo inatenda kazi, na inatenda kazi ndani ya kanisa lakini ni wachache tu ndio wanaweza kuliona ni kwasababu Biblia inasema ni wenye hekima tu, ndio watakaojua, na Hekima hii huja kwa kusoma, na kujifunza chini ya uongozo wa Roho Mtakatifu, Kumbuka hata jina la yule mnyama, inahitaji hekima kulijua, kwamba ukihesabu jina lake ndio ilete jumla ya 666. (VICARIVS FILII DEI).

Ufunuo 13:17 tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake. 18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na AIHESABU HESABU YA MNYAMA HUYO; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.

Vivyo hivyo Bwana Yesu alisema katika Luka 12:54 Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?”

Hivyo ni vema kufahamu MAJIRA unayoishi, kwamba dalili zote zinaonyesha unyakuo umekaribia, kwamfano kulingana na biblia, yale makanisa 7 yanayozungumziwa katika ufunuo 2&3, sita kati ya hayo yameshapita na wajumbe wake wameshapita na sasa ndio tupo katika kanisa la saba na la mwisho liitwalo LAODIKIA na mjumbe wake alishapita, hili ndio kanisa la mwisho litakaloshuhudia kuja kwa pili kwa Kristo, lakini cha kusikitisha watu wengi hawalijui hilo kwasababu hawataki kusoma na kujifunza NENO la Mungu kwa undani.

Ishara nyingine inayoonyesha kuwa tunaishi katika kizazi ambacho kinaweza kushuhudia kuja kwa pili kwa Kristo ni kunyanyuka kwa taifa la Israeli, kumbuka kwa muda wa miaka zaidi ya 2000 taifa la Israeli lilikuwa limetawanyika kwenye mataifa mbalimbali duniani, lakini mwaka 1948 Mungu alilirejesha tena na kuwa taifa huru, na sasa hivi limetimiza miaka 70, na Bwana alisema kwa MTINI jifunzeni mfano mtakapoanza kuona unachipua tena, basi mjue wakati wa mavuno umekaribia,” Kumbuka Mtini unafananishwa na Taifa la Israeli (Yeremia 24)

Hivyo tukiona Israeli inachipuka tena basi tujue wakati wa Bwana Kurudi umekaribia..Lakini Bwana alizidi kusema ..Amin! Amin! nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia”. Kwahiyo kizazi kinachozungumziwa hapo ni kizazi kilichoshuhudia Taifa la Israeli kuchipuka tena, na ndio hichi kizazi tunachoishi mimi na wewe. Hizi ni baadhi tu ya ishara nyeti ambazo zinatuonyesha kuwa hatuna muda mwingi tena hapa duniani. Ukombozi wetu upo karibu.

Tukirejea katika kitabu cha Danieli tunafahamu hakuishia tu kusoma kitabu cha Yeremia bali hata vingine kwamfano kitabu cha Isaya, kilishatabiri mambo kama hayo hayo (Soma Isaya 13 & 14).

Hivyo baada ya kuyajua hayo ndipo Danieli akamgeukia Mungu wake kumwomba dua na kumsihi sana juu ya dhambi zake na za watu wake Israeli.

MAOMBI YA DANIELI:

Tunasoma..

Danieli 9:2-23 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake;

5 tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako;

6 wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi.

7 Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa.

8 Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi.

9 Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi;

10 wala hatukuitii sauti ya Bwana, Mungu wetu, kwa kwenda katika sheria zake, alizoziweka mbele yetu kwa kinywa cha watumishi wake, manabii.

11 Naam, Israeli wote wameihalifu sheria yako, kwa kugeuka upande, wasiisikilize sauti yako; basi kwa hiyo laana imemwagwa juu yetu, na uapo ule ulioandikwa katika sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu; kwa sababu tumemtenda dhambi.

12 Naye ameyathibitisha maneno yake, aliyoyanena juu yetu, na juu ya waamuzi wetu waliotuamua, kwa kumletea mambo maovu makuu; maana chini ya mbingu zote halikutendeka jambo kama hili, lilivyotendeka juu ya Yerusalemu.

13 Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Musa, mabaya haya yote yametupata lakini hata hivyo hatukumwomba Bwana, Mungu wetu, atupe fadhili zake, ili tugeuke na kuyaacha maovu yetu, na kuitambua kweli yake.

14 Basi Bwana ameyavizia mabaya hayo, akatuletea; maana Bwana, Mungu wetu ni mwenye haki katika kazi zake zote azitendazo; na sisi hatukuitii sauti yake.

15 Na sasa, Ee Bwana Mungu wetu, uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama ilivyo leo; tumefanya dhambi, tumetenda maovu.

16 Ee Bwana sawasawa na haki yako yote, nakusihi, hasira yako na ghadhabu yako zigeuzwe na kuuacha mji wako Yerusalemu, mlima wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka.

17 Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana.

18 Ee Mungu wangu, tega sikio lako, ukasikie; fumbua macho yako ukautazame ukiwa wetu, na mji ule ulioitwa kwa jina lako; maana hatukutolei maombi yetu kwa sababu ya haki yetu, lakini kwa sababu ya rehema zako nyingi.

19 Ee Bwana, usikie; Ee Bwana, usamehe; Ee Bwana, usikilize, ukatende, usikawie; kwa ajili yako wewe, Ee Mungu wangu; kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako.

20 Basi hapo nilipokuwa nikisema, na kuomba, na kuiungama dhambi yangu, na dhambi ya watu wangu Israeli, na kuomba dua yangu mbele za Bwana, Mungu wangu, kwa ajili ya mlima mtakatifu wa Mungu wangu;

21 naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni.

22 Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danielii, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu.

23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya. “

Jambo la kujifunza hapo tunaweza kuuona unyenyekevu wa Danieli mbele za Mungu, ijapokuwa alikuwa ni mtu mkamilifu aliyependwa na Mungu lakini alijihesabia kuwa ni mwenye makosa pamoja na watu wake, alitubu kwa kufunga na kuugua, Vivyo hivyo na Bwana wetu YESU KRISTO, ingawa alikuwa ni mkamilifu hakutenda dhambi hata moja, lakini alitubu kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili yetu kwa kufunga na kuomba kwa dua nyingi pamoja na machozi.

Waebrania 5:7-10″ Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;

8 na, ingawa ni MWANA, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata;

9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki. “

Lakini wengi wetu inapotokea Bwana ametupa kibali fulani mbele zake, ndio wakati wa kujiinua na kujiona bora kuliko wengine wote, pengine kwasababu Mungu amekupa karama fulani aidha ya uchungaji, au unabii, au uponyaji, au lugha, au maono, au miujiza ukaanza kujiona bora mbele za Mungu kuliko wengine, lakini kwa Danieli haikuwa hivyo, licha ya kwamba alikuwa na vipawa vyote hivyo, lakini alijinyenyekeza.

Vivyo hivyo tunamwona na Bwana wetu YESU KRISTO pamoja na kwamba alikuwa ni Mungu mwenyewe katika mwili lakini alijishusha kiasi cha kufikia kuosha miguu ya wavuvi(mitume). Kama wao walifanya hivyo inatupasaje sisi tunaojiita watu wa Mungu, .??

Tukiendelea kusoma tunaona Malaika Gabrieli alimjia Danieli kumtia moyo na kumpa vitu vingine vya ziada kuliko hata vile alivyokuwa anavitazamia, licha tu ya kuonyeshwa mambo yahusuyo kutoka Babeli alioonyeshwa pia mambo yatakayokuja kutokea mpaka mwisho wa Dunia kwa watu wake.

MAJUMA 70:

Tukisoma..

Danieli 9:23-27″ Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya.

24 Muda wa majuma sabini umeamriwa juu ya watu wako, na juu ya mji wako mtakatifu, ili KUKOMESHA MAKOSA, na KUISHILIZA DHAMBI, na KUFANYA UPATANISHO KWA AJILI YA UOVU, na KULETA HAKI YA MILELE, na KUTIA MUHURI MAONO NA UNABII, na KUMTIA MAFUTA YEYE ALIYE MTAKATIFU.

25 Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu.

26 Na baada ya yale majuma sitini na mawili, masihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa.

27 Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu. “

Kama tunavyosoma hapo kutakuwa na majuma 70 yaliyoamuriwa juu ya watu wake Danieli (Yaani wayahudi pekee). Kibiblia juma moja, linasimama kama miaka 7, hivyo majuma 70, ni sawasawa na miaka (7×70 = 490), Hivyo kutakuwa na miaka 490 kwa wayahudi mpaka mwisho wa mambo yote utakapofika(yaani mwisho wa dunia).

Tukisoma pia tunaona “tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu”. kutakuwa na majuma 7 na 62 ambayo ni sawasawa na majuma 69, Kumbuka miaka hii ilianza kuhesabiwa pale tu amri ya kuujenga upya Yerusalemu ilipotolewa, na jambo hili lilitimizwa na Mfalme Koreshi wa Uajemi, aliyetabiriwa na Bwana tangu zamani za nabii Isaya kwamba ataujenga upya Yerusalemu.

Tukisoma Isaya 44:26-28 ” nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, UTAKALIWA NA WATU, nayo miji ya YUDA, ITAJENGWA, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;

27 niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako;

28 nimwambiaye KORESHI, MCHUNGAJI WANGU, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa. “

Pia ukisoma Isaya 45:1, 45:13, utaona jambo hilo, Kuwa Mungu alishamtabiri Koreshi amjengee nyumba kule Yerusalemu. Na amri ya kujenga tena Yerusalemu ilikuja kutoka mwaka 454 KK.

Hivyo ndani ya haya majuma 69 ya kwanza, yaani miaka 483 Jerusalemu ulijengwa tena na njia kuu zake na handaki zake katika nyakati za taabu kama biblia inavyosema.

Tukiendelea mstari wa 26 unasema “Na baada ya yale majuma sitini na mawili, masihi atakatiliwa mbali, naye atakuwa hana kitu(Danieli 9:26)”. Kwahiyo tunaona hapo mara baada ya yale majuma 69 kuisha (yaani 62+7) MASIHI atakatiliwa mbali. Jambo hili lilitimia mwaka 30WK, wakati Bwana YESU aliposulibiwa, hivyo kukamilisha miaka 483 tangu agizo kutolewa na Mfalme Koreshi kuujenga upya Yerusalemu.

Na kama tunavyoendelea kusoma “watu wa mkuu atakayekuja wataungamiza mji (Danieli 9:26)”. Huyu mkuu anayezungumziwa hapa ni Mpinga-kristo ambaye atakuja siku za mwisho, naye atatokea RUMI, kwasababu biblia inasema watu wake ndio watakaouteketeza mji, na hii ilitimia mwaka 70WK pale jeshi la Rumi lilipouzunguka mji wa Yerusalemu na kuuteketeza kwa moto ili kutimiza ule unabii wa Bwana Yesu aliousema juu ya mji wa Yerusalemu (ukisoma katika Luka 19:41-44).

Kwahiyo mpaka hapo litakuwa limesalia Juma moja yaani miaka 7 kutimiza yale majuma 70. Lakini ukitazama utaona wayahudi baada ya kumkataa MASIHI wao muda wao ulisimamishwa (Luka 13:34-35) na Mungu akaacha kushughulika nao, hivyo neema ikahamia kwa mataifa, na ndiyo iliyopo mpaka sasa hivi, takribani miaka zaidi ya 2000, lakini haitadumu huku siku zote, wakati utafika nao umeshakaribia na neema itarudi tena Isreali kwa muda mfupi kumalizia juma lao moja la mwisho yaani miaka 7, na kumbuka wakati wa mataifa utaisha pale tu kanisa litakaponyakuliwa.

(Warumi 11:25″ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UWASILI.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.

27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao. )

Tukiendelea mstari wa 27 tunasoma..” Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu (Danieli 9:27).”

Sasa kumbuka huyu anayezungumziwa hapa ni mpinga-kristo (ambaye ndie yule mkuu wa watu atakayekuja), atafanya agano thabiti na watu wengi kwa juma moja, na katika nusu ya juma, yaani miaka mitatu na nusu ya kwanza atalivunja,

Hii itatokea baada ya unyakuo kupita pale mpinga-kristo (PAPA) atakapoingia agano la amani na wayahudi kwa muda wa juma moja wakati huo Hekalu la tatu YERUSALEMU litakuwa limeshajengwa na sadaka za kuteketezwa za daima zitakuwa zinaendelea, lakini katikati ya Juma hilo moja atalivunja hilo Agano, na kuzuia sadaka zote na dhabihu zisitolewe katika nyumba ya Mungu. Zaidi ya yote atataka yeye aabudiwe kama Mungu (2Wathesalonike 2:2), hilo ndilo chukizo la uharibifu. Na katika hiyo miaka mitatu na nusu ya mwisho atawaua watu wote watakaokataa kumsujudia yule mnyama au kupokea chapa yake katika kipindi kinachojulikana kama kipindi cha DHIKI KUU.

Kumbuka dhiki hii ilikusudiwa kwa wayahudi tu lakini na kwa watakaobaki (watu wa mataifa ) wasiokwenda kwenye unyakuo nao pia wataipitia. Lakini mwisho wake(mpinga-kristo) utafika ghafla, na makao yake yataharibiwa na kuangamizwa kabisa.

Kisha baada ya hapo utakuja utawala mpya wa miaka 1000 usio na uharibifu wa BWANA wetu YESU KRISTO, naye atatawala na watakatifu wake MILELE na MILELE.

Tukiyajua haya kuwa wakati tulionao ni mfupi tunapaswa kila siku tuufanye imara WITO WETU, NA UTEULE WETU (2Petro 1:10). Kwa maana ..1Wakoritho 6:9-10″ Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.”

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Mwendelezo >>> Mlango wa 10

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


 

Mada Nyinginezo:

JUMA LA 70 LA DANIELI.

NGURUMO SABA.

MIHURI SABA

“WALA MSIMWITE MTU BABA DUNIANI”..HAPO BWANA WETU YESU ANAMAANISHA NINI KUSEMA HIVYO?

BIDII YA MFALME YOSIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

DANIELI: Mlango wa 8

Jina la YESU KRISTO, BWANA wetu libarikiwe.

Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, Kama tulivyoona katika sura iliyotangulia Danieli akionyeshwa wale wanyama 4 waliotoka baharini, wa kwanza mwenye mfano wa simba, wa pili kama Dubu, watatu kama Chui na wanne alionekana kuwa mbali sana na wale wengine kwa muonekano wake ikiashiria utendaji wake ulikuwa ni wa tofauti, na tuliona wanyama wale waliwakilisha zile FALME 4 zitakazotawala mpaka mwisho wa Dunia, wa kwanza ukiwa ni Babeli, wapili, Umedi & uajemi, watatu Uyunani na wanne ambao ni wa mwisho ni RUMI.

Lakini tukiendelea na mlango huu wa 8, tunaona Danieli akionyeshwa maono mengine ya kipekee yanayohusiana na mambo yatakayokuja kutokea huko mbeleni kuhusiana na hizo falme kama Danieli 8:19 inavyosema..” Akaniambia, Tazama, nitakujulisha yatakayokuwa wakati wa mwisho wa ghadhabu; maana, ni ya wakati wa mwisho ulioamriwa. “

Tusome.

Danieli 8:1-4″

1 Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza maono yalinitokea mimi, naam, mimi Danieli, baada ya hayo yaliyonitokea hapo kwanza.

2 Nami naliona katika maono; ilitukia, nilipoona, nalikuwako huko Shushani ngomeni, katika wilaya ya Elamu; nikaona katika maono, nami nalikuwa karibu na mto Ulai.

3 Ndipo nikainua macho yangu nikaona, na tazama, mbele ya mto alisimama kondoo mume, mwenye pembe mbili; na pembe zile mbili zilikuwa ndefu; lakini moja ilikuwa ndefu kuliko ya pili, na ile iliyokuwa ndefu zaidi ilizuka mwisho.

4 Nikamwona huyo kondoo mume akisukuma upande wa magharibi, na upande wa kaskazini, na upande wa kusini; wala hakuna mnyama ye yote awezaye kusimama mbele yake, wala hakuna mnyama ye yote awezaye kupokonya mkononi mwake; lakini alitenda kama alivyopenda mwenyewe, akajitukuza nafsi yake.

Danieli katika maono haya alimwona kondoo mume mwenye pembe mbili, kumbuka ukiendelea mbele kwenye mstari wa 20 utaona tafsiri yake kuwa huyo kondoo anawakilisha ufalme wa UMEDI & UAJEMI,..

“Danieli 8:20 Yule kondoo mume uliyemwona, mwenye pembe mbili, hizo ndizo wafalme wa Umedi na Uajemi.

Na kama tunavyosoma hapo pembe moja ilikuwa ndefu kuliko nyingine na ndio iliyozuka mwishoni hii ikiwa na maana kuwa mfalme mmoja atakuwa na nguvu kuliko mwingine na huyu sio mwingine zaidi ya Koreshi mfalme wa UAJEMI ambaye tunaona alinyanyuka mwishoni baada ya Dario ambaye alikuwa ndugu yake mfalme wa Umedi kufa, Hivyo Ufalme wa Uajemi chini ya Koreshi uliimarika sana, mpaka ulipofikia wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero aliyemtwaa Esta kuwa malkia.

Na pia tunaona kondoo huyu akisukumu pande zote nne za nchi ikiashiria kuwa alifanikiwa kuteka sehemu kubwa ya dunia na mataifa makubwa, kuanzia India mpaka Ethiopia, jambo hili tunaweza tukalisoma katika kitabu cha Esta 1:1…” Zamani za Ahasuero; naye huyu Ahasuero alimiliki toka Bara Hindi mpaka Kushi, juu ya majimbo mia na ishirini na saba; “

Alionekana pia akijitukuza nafsi yake, ni dhahiri kuwa milki kubwa aliyokuwa nayo ni rahisi kujinyanyua moyo hivyo pengine alifikiri kuwa hakuna taifa lolote lingeweza kumwangusha. lakini kama tunavyoendelea

Mstari wa 5-8″ unasema…

Danieli 8:5 Nami nilipokuwa nikifikiri, tazama, BEBERU akatoka upande wa magharibi, juu ya uso wa dunia nzima, bila kuigusa nchi; na beberu yule alikuwa na pembe mashuhuri kati ya macho yake.

6 Naye akamwendea huyo kondoo mume mwenye pembe mbili, niliyemwona akisimama karibu na mto, akamshambulia kwa ghadhabu za nguvu zake.

7 Nikamwona akimkaribia kondoo mume, akamwonea hasira kali, akampiga kondoo mume, akazivunja pembe zake mbili; na huyo kondoo mume alikuwa hana nguvu kusimama mbele yake; bali akamwangusha chini, akamkanyaga-kanyaga; wala hapakuwapo awezaye kumwokoa kondoo mume katika mkono wake.

8 Na yule beberu akajitukuza sana; na alipokuwa na nguvu, pembe ile kubwa ilivunjika; na badala yake zikazuka pembe nne mashuhuri zilizoelekea pepo nne za mbinguni.

Vivyo hivyo ukienda mbele kusoma mstari wa 21-22 utaona tafsiri ya yule beberu kuwa ni Ufalme wa UYUNANI, ambao ndio ulioungusha ufalme wa Umedi na Uajemi,…{“21 Na yule beberu, mwenye manyoya mengi, ni mfalme wa Uyunani; na ile pembe kubwa iliyo kati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.22 Tena katika habari ya pembe ile iliyovunjika, ambayo badala yake zilisimama pembe nne, falme nne zitasimama kutoka katika taifa lile, lakini si kwa nguvu kama zake. (Danieli 8:21-22)”}

Kumbuka kama tulivyosoma katika milango iliyopita, ufalme wa tatu uliokuja kutawala dunia ulikuwa ni UYUNANI na ndio unawakilishwa na yule chui mwenye vichwa 4 katika Danieli sura ya 7,

Hivyo Danieli anaonyeshwa tena jambo lile lile katika ono tofauti lakini kwa undani zaidi, na Beberu huyu anaonekana akija akiwa na PEMBE MOJA MASHUHURI katikati ya macho yake naye akaenda kumvamia yule kondoo mwenye pembe mbili na kumwangamiza kabisa.

“Alexanda Mkuu” ndio ile pembe mashuhuri iliyozuka, Historia inasema mtu huyu alifanikiwa kuteka falme nyingi kwa kipindi cha muda mfupi sana, ndani ya miaka 12 alikuwa ameshaitiisha sehemu kubwa ya dunia kuanzia makedonia, India, hadi Misri na ilipofika 331 KK aliidondosha ngome ya Umedi na Uajemi (ndio yule kondoo) na kuiangamiza kabisa.

Na kama tunavyosoma mstari wa 8, tunaona ile pembe ilipokuwa na nguvu ilivunjika ghafla, na badala yake zikazuka pembe nyingine 4 mashuhuri. Historia inaonyesha Alexandra Mkuu, ambaye ndio ile pembe, alikufa ghafla na ugonjwa akiwa bado kijana wa miaka 31, Hivyo baada ya kufa hakuonekana wa kumrithi, hivyo wale majenerali wake 36 waliokuwa chini yake walianza kuupigania ufalme, hakuonekana aliyekuwa na nguvu kama za Alexanda hivyo mwishoni walikuja kuishia wanne tu, na kuugawanya ufalme katika pande nne sawasawa na biblia ilivyotabiri. Na majenerali hao walikuwa ni:

1)CassanderAlitawala pande za magharibi ambazo ni Makedonia na Ugiriki

2)LysimachusAlitawala pande za kaskazini ambazo ni Bulgaria na maeneo ya Asia ndogo

3)PtolemyAlitawala pande za kusini ambayo ni Misri

4)SeleucusAlitawala pande za Mashariki ambazo zilikuwa Israeli, Syria na mashariki yake.

Kumbuka hizi Pembe NNE ndio vile Vichwa vinne Danieli alivyoonyeshwa katika yule mnyama wa tatu, aliyefanana na CHUI katika Danieli sura ya 7.

Lakini tukiendelea kusoma kuanzia ule mstari wa 9 hadi wa 14 tunaona PEMBE nyingine NDOGO, ikizuka katikati ya moja ya zile pembe nne.

Tusome..

“Danieli 8:9 Na katika moja ya pembe hizo ilitokea pembe ndogo, iliyokua sana, upande wa kusini, na upande wa magharibi, na upande wa nchi ya uzuri.

10 Nayo ikakua, kiasi cha kulifikilia jeshi la mbinguni; ikaangusha chini baadhi ya jeshi lile, na ya nyota, ikazikanyaga.

11 Naam, ikajitukuza hata juu yake aliye mkuu wa jeshi hilo, ikamwondolea sadaka ya kuteketezwa ya daima, na mahali pa patakatifu pake pakaangushwa chini.

12 Na jeshi likatolewa kwake pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya daima, kwa sababu ya makosa; nayo ikaiangusha kweli hata chini; ikatenda ilivyopenda, na kufanikiwa.

13 Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi?

14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa. “

PEMBE NDOGO

Hii Pembe ndogo iliyozuka kati ya zile nne, historia inaonyesha ni mtawala aliyezuka katika ufalme wa Seleucus mmoja wa wale watawala wanne ambaye alikuwa wa mashariki, na tunaona ilizidi kujiimarisha mpaka kufikia NCHI YA UZURI (AMBAYO NI ISRAELI), Na mtawala huyu si mwingine zaidi ya ANTIOKIA IV, EPIFANE. Aliyetawala kuanzia 175-164 KK ..alijiita EPIFANE, akiwa na maana kuwa yeye ni “MUNGU ALIYEDHIHIRIKA”, huu ni mfano wa kile kile cheo cha mpinga-kristo atakayenyanyuka siku za mwisho. Kumbuka mambo yanayoandikwa, au yaliyotokea katika historia ni kivuli cha mambo yatakayokuja kutokea siku za mwisho.

Lakini tukisoma mstari wa 10 tunaona “Nayo ikakua{PEMBE}, kiasi cha kulifikilia jeshi la mbinguni; ikaangusha chini baadhi ya jeshi lile, na ya nyota, ikazikanyaga.

Kumbuka nyota za mbinguni zinafananishwa na makuhani wa Mungu, au viongozi wa watakatifu wa Mungu, ukisoma (Danieli 12:3., na ufunuo 2 & 3)utaona hilo jambo. Hivyo historia inaeleza huyu mtawala katili ANTIOKIA alishuka Yerusalemu na kuanza kuua wakuhani wa Mungu walokuwa wanahudumu katika nyumba ya Mungu na kuzuia watu wasitoe dhabihu katika nyumba ya Mungu( Hekaluni) na ndio maana ukisoma mstari wa 11 unasema ” Naam, ikajitukuza{hiyo pembe} hata juu yake aliye mkuu wa jeshi hilo, IKAMWONDOLEA SADAKA YA KUTEKETEZWA YA DAIMA, na mahali pa patakatifu pake pakaangushwa chini”.

Hivyo kuanzia huo wakati wayahudi wote walikatazwa kufanya ibada yoyote katika nyumba ya Mungu, badala yake Antiokia akawalazimisha wayahudi wafuate tamaduni za kipagani za kigiriki badala ya sheria ya Musa.

Alizidi hata kufikia hatua ya kuiba vyombo vya hekaluni na kutengeneza madhabahu ya mungu wake wa kipagani-ZEU ndani ya HEKALU la Mungu, Hilo ni chukizo kubwa sana kwa Mungu na kwa Wayahudi, aliendelea kwa kuchinja vitu haramu kama nguruwe na kunyunyiza damu juu ya madhabahu ndani ya hekalu la Mungu. Na wayahudi walipojaribu kwenda kinyume naye juu ya kulichafua hekalu la Mungu aliwaua wengi kikatili na wengine kuwauza utumwani, alikataza wayahudi kutahiriwa, yeyote atakayekiuka adhabu yake ilikuwa ni kifo, wayahudi walilazimishwa kula nyama za nguruwe na kutolea dhabihu miungu migeni ya kigiriki mambo ambayo ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu. Lakini kumbuka haya yote yaliwapata wayahudi kwasababu ya MAKOSA YAO, kama mstari wa 12 unavyoeleza….”12 Na jeshi likatolewa kwake pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya daima, KWASABABU YA MAKOSA; nayo ikaiangusha kweli hata chini; ikatenda ilivyopenda, na kufanikiwa. “

Wayahudi walimsahau Mungu na kuacha kuzishika sheria zake hivyo Mungu akaruhusu kiongozi mbaya na mkatili kama huyu anyanyuke dhidi yao. Lakini baadaye Mungu alikuja kumuhukumu na kufa ghafla.

Kumbuka Antiokia ni kivuli cha mpinga-kristo atakayekuja, biblia inasema atajiinua nafsi yake na kutaka kuabudiwa kama Mungu tunasoma.1Wathesalonike 2:3 Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; 4 yule mpingamizi, AJIINUAYE NAFSI YAKE JUU YA KILA KIITWACHO MUNGU, AMA ; hata yeye mwenyewe KUKETI KATIKA HEKALU LA MUNGU, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu. “

Na kama vile Antiokia aliwalazimisha wayahudi waikane imani yao na kuabudu miungu ya kipagani, vivyo hivyo na mpinga-kristo (PAPA) atawalazimisha watu wa ulimwengu mzima kupokea dini yake inayotambulishwa na ile chapa, na yeyote atakayepinga adhabu yake itakuwa ni kifo cha mateso kama ilivyokuwa kwa Antiokia kumbuka wakati hayo yanatokea kanisa litakuwa limeshanyakuliwa.

Tukiendelea mstari wa 13-14 inasema..

Danieli 8:13 “Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi?

14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi ELFU MBILI NA MIA TATU (2300); ndipo patakatifu patakapotakaswa. “

Hizi siku 2300 ni sawa na miaka sita na theluthi moja hivi, ndipo uovu wote utaondolewa katika hekalu la Mungu, na Historia inaonyesha tangu kipindi Antiokia kuzuia sadaka za kuteketezwa mpaka siku ziliporejeshwa tena, ilikuwa ni siku 2300 kamili kama unabii ulivyotabiri.

Hii ilitokea pale baadhi ya wayahudi kutokuvumiliana na vitendo vya Antiokia na kuamua kuasi kwa kuingia vitani hivyo wakanyanyuka wana wa Matthatias mmoja wao akiwa YUDA MAKABAYO, na kwenda porini kumpinga Antiokia siku zote za utawala wake, walifanikiwa kumshinda na kuichukua tena YERUSALEMU na KULIWEKA TENA WAKFU Hekalu la Mungu baada ya kuchafuliwa kwa muda mrefu, hivyo wakatimiza unabii wa siku 2300 hii ilikuwa ni mwaka 164 KK. Siku hiyo wayahudi wakaanza tena kutoa sadaka za kuteketezwa, Na ndipo ile sikukuu ya KUTABARUKU ilianzia hapo {KUTABARUKU ni kuweka wakfu} (Yohana 10:22).

Kumbuka Danieli alionyeshwa mambo hayo kwa ajili ya SIKU ZA MWISHO, kwa sehemu yametimia kama KIVULI TU, lakini matukio halisi yenyewe yatakuja katika vizazi hivi vya siku za mwisho siku mpinga-kristo atakaposimama na kuwakosesha watu wengi.

Hivyo ndugu biblia inasema 2 Thesalonike 2:

7 Maana ILE SIRI YA KUASI HIVI SASA INATENDA KAZI; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

Biblia inasema ni SIRI, hivyo inahitaji hekima kuigundua, utendaji kazi wake ni katika SIRI, na JINA lake pia lipo katika SIRI, BABELI MKUU MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI! (Ufunuo 17:5). ni roho ile ile iliyokuwa kwa Antiokia, ndio ipo mpaka sasa hivi, IBADA ZA SANAMU katika nyumba ya Mungu(KANISA), pombe kanisani, uasherati kanisani, ushoga kanisani, vimini kanisani, burudani kanisani, sanaa & siasa kanisani, mizaha kanisani, biashara kanisani n.k. haya yote ni machukizo kama aliyofanya Antiokia na Belshaza juu ya nyumba ya Mungu. Ni roho ile ile.

2Wakoritho 6:15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?

16 Tena pana mapatano gani kati ya HEKALU LA MUNGU NA SANAMU? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, TOKENI KATI YAO, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike, “

EPUKA ROHO YA UDHEHEBU NA DINI ZA UONGO MGEUKIE KRISTO AYASAFISHE MAISHA YAKO KWA NENO LAKE NA UZALIWE MARA YA PILI ILI UWE MTAKATIFU. Kwasababu biblia inasema pasipo huo UTAKATIFU hakuna mtu atakayemwona Mungu(Waebrania 12:14).

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa Mwendelezo >>> Mlango wa 9

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 13

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

NGUVU YA UPOTEVU.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “HERI WALIOTASA, NA MATUMBO YASIYOZAA, NA MAZIWA YASIYONYONYESHA”?

MAFUMBO YA MUNGU.

JE! MTU ANAYETUNGISHA MIMBA KWENYE CHUPA MAHABARA, ANAHATIA MBELE ZA MUNGU?

KUJIPAMBA NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

DANIELI: Mlango wa 7

Jina la BWANA wetu YESU KRISTO lihimidiwe.

Katika sura zilizotangulia (yaani ya 1-6), tuliona zikielezea sana sana historia za maisha ya watakatifu waliyopitia zaidi kuliko unabii lakini kuanzia Mlango huu wa 7 na kuendelea tunaona Danieli akionyeshwa maono ya mambo yatakayokuja kutokea katika siku za mwisho. Tukisoma..

Danieli 7:1-8″ Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.

2 Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.

3 Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali.

4 Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.

5 Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.

6 Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.

7 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.

8 Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.

Tukirejea kwenye ile sura ya pili tunaona jinsi Mfalme Nebudreza akionyeshwa katika ndoto Falme nne zitakazotawala dunia mpaka hapo ALIYE JUU(YESU KRISTO) atakapochukua Falme zote za dunia, hivyo Danieli alimpa tafsiri yake, Ufalme wa kwanza ukiwa ni Babeli, wa pili ukiwa ni Umedi na uajemi, wa tatu ukiwa ni ufalme wa uyunani na wa nne ni Rumi. Jambo hili hili tunaona linajirudia tena katika sura hii ya 7, Danieli akifunuliwa zile zile Falme 4 zitakazotawala ulimwengu wote mpaka mwisho wa dunia isipokuwa hapa anaonyeshwa kwa undani zaidi.

Hapa aliona wanyama 4, wakitoka baharini, kumbuka bahari inawakilisha mikusanyiko ya watu wengi(makutano){ufunuo 17:15, } hivyo hizi falme zitanyanyuka kutoka katikakati ya watu.Kumbuka wanyama hawa 4 Danieli aliowaona ndio yule yule mnyama Yohana alioonyeshwa akitoka Baharini mwenye vichwa 7 na pembe 10, wa kwenye Ufunuo 13 isipokuwa hawa wameunganishwa wote pamoja..

“ufunuo 13:1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa MFANO WA CHUI, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya DUBU, na kinywa chake kama kinywa cha SIMBA, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi. “

Tutazame wanyama hawa.

MNYAMA WA KWANZA:

Kama tunavyosoma yule mnyama wa kwanza alionekana kama mfano wa SIMBA na akiwa na mabawa ya tai, kumbuka utawala wa kwanza Babeli ndio uliohusika kuwapeleka wana wa Israeli utumwani, ulifananishwa na simba ukisoma Yeremia 4:5-6 inaelezea kuwa watu walioichukua Israeli mateka na kuwapeleka Babeli walifananishwa na kama simba aangamizaye mataifa. Na pia kama anavyoonekana na mabawa ya tai hii inaashiria uharaka wake katika kuteka, kitu kinachopaa siku zote kina kasi kuliko vinavyokwenda kwa miguu hivyo Babeli ulikuwa mwepesi wa kuteka.

Habakuki 1:6″ Kwa maana, angalieni, nawaondokesha Wakaldayo {wakaldayo ni wa-babeli}, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao.”

7 Hao ni watu wa kutisha sana, wa kuogofya sana; hukumu yao na ukuu wao hutoka katika nafsi zao wenyewe.

8 Farasi zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi wao hujitapa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; HURUKA KAMA TAI AFANYAYE HARAKA ALE. “

Kwahiyo tunaona hapo yule mnyama wa kwanza ni ufalme wa Babeli ambao ulikuja kuanguka baadaye na kunyanyuka mwingine wenye nguvu kushinda huo.

MNYAMA WA PILI:

Mnyama huyu anaonekana akifanana na Dubu, na pia anaonekana kama ameinuliwa upande mmoja ikiwa na maana kuwa anazo pande mbili na upande mmoja imezidi mwingine, na tunafahamu utawala huu si mwingine zaidi ya ufalme wa UMEDI na UAJEMI, na historia inaonyesha ufalme wa Uajemi ulikuwa na nguvu zaidi kuliko Umedi , hivyo zilipoungana zikaja kuundoa ufalme wa Babeli katika mamlaka yake na kuimiliki dunia upya, na pia yule Dubu anaonekana akiwa na MIFUPA MITATU ya mbavu kinywani mwake hizi ni ngome tatu walizoziangusha hawa wafalme wa Umedi na Uajemi, nazo ni Lidya, Misri na Babeli.

Ukisoma Isaya 13:15 ilishatabiri ukatili wake hata kabla ya utawala huo kunyanyuka.inasema ..

“15 Kila mtu atakayeonekana atatumbuliwa, na kila mtu atakayepatikana ataanguka kwa upanga.

 16 Na watoto wao wachanga watavunjwa-vunjwa mbele ya macho yao, nyumba zao zitatekwa nyara, na wake zao watatendwa jeuri.

17 Tazama, nitawaamsha WAAMEDI juu yao, ambao hawaoni fedha kuwa kitu, wala hawafurahii dhahabu.

18 Na nyuta zao zitawaangusha vijana; wala hawatahurumia mazao ya tumbo; jicho lao halitawahurumia watoto.

19 Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.”

ukizidi kusoma utaona huyu mnyama anaambiwa “ainuke ale nyama tele” ikiwa na maana kuwa atapewa uwezo wa kuteka mataifa mengi, na ndivyo ilivyokuja kuwa, katika historia inaonyesha Umedi na Uajemi uliteka na kutawala mataifa mengi Kuanzia India mpaka Ethiopia majimbo 127 (Esta 1:1) inaelezea vizuri.

MNYAMA WA TATU:

Mnyama huyu wa tatu Danieli alimwona akiwa mfano wa chui mwenye vichwa vinne, tukisoma..“6 Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.”

Huu ni utawala wa UYUNANI (UGIRIKI) ambao ulikuja kunyanyuka baada ya mtawala wa Uyunani “Alexander the great” kuiangusha ngome ya Umedi na Uajemi, ni mtawala aliyekuwa na nguvu sana, kama chui alivyo mwepesi wa kushika mawindo yake, ndivyo ilivyokuwa kwa huyu mtawala mdogo, kila alipokwenda kupigana na maadui zake alifanikiwa, kwa muda wa miaka 12 tu alikuwa tayari amekwishafanikiwa kuiteka dunia nzima. Lakini naye pia hakudumu sana katika utawala wake, alipokuwa na miaka 31 alipata ugonjwa na kufa, hivyo hakuacha mtu wa kumrithi baada yake, Hivyo ikasabisha wale majemedari waliokuwa chini yake kupigania ufalme lakini hakufanikiwa kutokea mwenye nguvu kama za Alexander hivyo ufalme ule ukagawanyika katika pande NNE, Ambavyo ndio vile vichwa vinne vya yule mnyama; Cassander, Lysimachus ,Ptolemy na Seleucus

MNYAMA WA NNE:

 Danieli 7:7 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.

Mnyama huyu ni utawala wa RUMI, ndio ile miguu ya chuma kwenye yale maono aliyoyaona Mfalme Nebukadreza kwenye Danieli 2, na mnyama huyu hapa anaonekana akiwa na meno ya chuma, ikiashiria ana nguvu nyingi za kuharibu na kusagasaga, na pia hapa anaonekana na pembe 10, ambavyo ndio vile vidole 10 vya kwenye ile sanamu ya Nebukadreza. Kumbuka utawala huu ndio uliokuwa utawala katili kuliko yote iliyotangulia, na ndio unaotawala hata sasa katika roho,Lakini Katika historia, utawala wa Rumi ya magharibi ulikuja kugawanyika katika mataifa 10 yanayojitegemea AD 476, ambayo ni

1) Alemanni– kwa sasa ni Ujerumani

2) Franks – kwa sasa ni Ufaransa

3) Burgundians-Kwa sasa ni uswizi

4) Visigoths -Hispania

5) Lombards-Italia

6) Anglo-Saxons– Uingereza

7) Suevi- Ureno

8) Vandals -iling’ofolewa na ile pembe ndogo iliyozuka

9) Ostrogoths-ilingom’ofolewa na ile pembe ndogo iliyozuka

10) Heruli– iling’ofolewa na ile pembe ndogo iliyozuka

Lakini tukiendelea kusoma mstari wa 8 tunaona kuna PEMBE nyingine ndogo ikizuka

“Danieli 7:8 Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake PEMBE TATU katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.

Hivyo baada ya Danieli kuona haya alitamani kufahamu ile pembe ndogo maana yake ni nini??, Kama tunavyosoma Danieli 7:19 Kisha nalitaka kujua maana ya yule mnyama wa nne, aliyekuwa mbali na wenziwe wote, mwenye kutisha sana, ambaye meno yake yalikuwa ya chuma, na makucha yake ya shaba; aliyekula, na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake;

20 na habari za zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake, na ile pembe nyingine iliyozuka, ambayo mbele yake zilianguka pembe tatu; yaani, pembe ile yenye macho, na kanwa lililonena makuu, ambayo kuonekana kwake kulikuwa hodari kuliko wenzake.

Kumbuka Pembe zinawakilisha ufalme au mfalme, Hivyo zile pembe 10 zinasimama kama wafalme wenye falme, vivyo hivyo na ile pembe ndogo ya 11 iliyoonekana kuzuka na kung’oa pembe nyingine tatu ni mfalme atakayenyanyuka na kuangusha wafalme wengine watatu. Historia inaonyesha mara baada ya utawala wa RUMI kugawanyika katika zile Falme 10, utawala wa KIPAPA ulizuka na kungusha tatu ya hizo ngome 10, pale zilipotaka kushindana na utawala wa PAPA aliziharibu kabisa na kuzishinda na hizo si nyingine zaidi ya Vandals, Ostrogoths na Heruli.

Na kama tunavyosoma pembe hiyo ilijitukuza sana na kunena maneno makuu ya makufuru, tunafahamu cheo pekee kinachosimama kama Mungu duniani ni cheo cha UPAPA, leo hii katika enzi yake yeye anasimama kama ” badala ya Kristo duniani”, anao uwezo wa kusamehe dhambi, anafahamika kama mtawala wa mbinguni, duniani, na chini ya nchi, N.K. hayo yote ni maneno ya makufuru mbele za Mungu. watu wanamtazama duniani yeye kama Mungu.

Lakini Mstari wa 21 unasema. ” Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu, ikawashinda; “ hakuishia tu katika kujitukuza lakini aliendelea hata kufanya vita na watakatifu Hili ni jambo limekuwa likijirudia katika historia tangu utawala wa KIPAPA chini ya Kanisa Katoliki uanze, wakristo wengi wamekuwa wakiuliwa kikatili pindi tu pale walipoonekana wanaenda kinyume na Dini hiyo. Wakristo zaidi ya milioni 68 waliuawa kikatili walipoonekana tu wanalishika Neno na kupinga mafundisho ya uongo ya kanisa hilo. Kumbuka wakatoliki sio wapinga-kristo isipokuwa ule mfumo wa lile kanisa na kile cheo anachokikalia kiongozi wa lile kanisa ndio cha MPINGA-KRISTO MWENYEWE.

Mstari wa 25 unasema Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa WAKATI, NA NYAKATI MBILI, NA NUSU WAKATI (Danieli 7:25)”. Hii inafunua siku mpinga-Kristo yule PAPA wa mwisho atakaposimama kutenda kazi.

Kumbuka hawa PAPA waliopo sasa hivi na waliopita wamekaa katika viti vya mpinga-kristo lakini yupo MMOJA atakayesimama na kubadilisha majira, na sheria, biblia inasema

( 1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba MPINGA KRISTO YUAJA , hata sasa WAPINGA KRISTO WENGI wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho).

Na siku sio nyingi atasimama atawale na kuitesa dunia kwa nyakati na nyakati mbili na nusu wakati, ambayo ni miaka mitatu na nusu, kwasababu kibiblia nyakati moja ni mwaka mmoja.

Hivyo hiyo itakuwa ni miaka mitatu na nusu ya dhiki kuu,. labda anaweza akawa ndio huyu PAPA aliyepo sasa au mwingine muda utaeleza yote.. Huu ni wakati wa kujiweka tayari muda wowote mambo yanabadilika, Hauoni sasa hivi anavyozunguka kuleta DINI zote pamoja, akiwa kama mtu mwenye wafuasi wengi kuliko wote duniani. Kilio chake ni AMANI! AMANI! kwa kivuli hicho anatafuta ufalme ili baadaye aje kupambana na uzao wa Mungu.

Biblia inasema..1Wathesalonike 5:1-3″ Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.Wakati wasemapo, KUNA AMANI NA SALAMA, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. “

Ndugu wakati umeisha usidanganyike na watu wanaosema dunia haishi leo wala kesho, geuka weka mambo yako sawasawa yahusuyo wokovu.Huu ulimwengu unapita na mambo yake yote.

Mstari wa 9-10. unasema…” Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.10 Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na VITABU VIKAFUNULIWA.

Hapa tunaona mwisho wa yote vitabu vitafunguliwa vihusuvyo maisha yetu, kila mtu na kitabu chake na utahukumiwa katika hicho, je! kitabu chako unakiandikaje? Biblia inasema sisi ni barua, na kila siku tunafungua kurasa mpya wa vitabu vyetu, na siku ile utakapokufa kitafungwa kikingojea kufunguliwa tena katika siku ile ya HUKUMU.

Hivyo tukiona mambo haya tunajua kabisa ule mwisho umekaribia UTAWALA USIOWEZA KUHARIBIKA wa mwokozi wetu ,hivi karibuni utakuja hapa ulimwenguni,.BWANA wetu YESU KRISTO MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA, atamiliki pamoja na watakatifu wake milele tunasoma..

Danieli 7:27 Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; UFALME WAKE NI UFALME WA MILELE, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.

2Petro 1:10” Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”

AMEN!

Kwa Mwendelezo >>> Mlango wa 8


Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 13

UFUNUO: MLANGO WA 17

JE! KUSHIRIKI AU KUJIHUSISHA KWENYE MICHEZO NI DHAMBI?

   WAPUNGA PEPO WANAOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NI WATU WA NAMNA GANI?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?


Rudi Nyumbani:

Print this post