Search Archive maswali na majibu

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Shalom

Hii ni sehemu ya pili ya maswali na majibu yahusuyo ndoa.. Sehemu ya Kwanza unaweza kuisoma kupitia  link hii >> MASWALI-NDOA

SWALI 01: Je Mkristo anaruhusiwa kuoa mtu wa Imani nyingine? Yaani akafunga naye ndoa tu, na kila mmoja akaendelea na imani yake.

Jibu: Ndoa ya kikristo ni ndio inayohusisha Imani moja, Bwana mmoja, Roho mmoja, tumaini moja, Ubatizo mmoja na Mungu mmoja..

Waefeso 4:3  “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.

4  Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

5  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.

6  Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”

Kwahiyo kabla ya Ndoa ni lazima wawili hao wafikie kuwa na imani moja, na ubatizo mmoja na Roho Mmoja na Mungu mmoja, wasipofikia huo umoja basi hiyo sio ndoa ya kikristo.

Sasa nini cha kufanya endapo ikitokea mmoja si wa imani ya  kikristo?, Jibu: Huyo ambaye tayari kashaokoka anapaswa amhubirie mwenzake habari za Wokovu kwanza, na aamini na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu (kwaufupi awe mkristo aliyesimama kweli kweli) na baada ya hapo ndipo wafunge ndoa, lakini kumbuka, si abadilike kwasababu tu anataka kuoa au kuolewa!, hapana bali anapaswa apate badiliko la kweli kiasi kwamba hata kama asipoolewa na huyo basi bado Kristo atabaki kuwa Mwokozi wake siku zote za maisha yake.

SWALI 02: Je kuna umuhimu wowote wa kupima afya kabla ya kufunga Ndoa?

Jibu: Ndio upo umuhimu wa kufanya hivyo kama kuna huo ulazima. Kuhakikisha afya zenu zipo sawa kabla ya kufanya lolote, maandiko hayajakataza kufanya hivyo. Na endapo ikitokea mmoja kakutwa na maradhi ambayo yatawafanya wawili hao wasiweze kukutana kimwili!.. Basi hapo ni uchaguzi wa Yule aliye salama, kama upendo wake ni mwingi kama ule wa Kristo, anaweza kuishi na huyo anayemchagua, lakini kamba si hawezi basi yupo huru kutafuta mwingine aliye chaguo lake hafanyi dhambi.

Lakini kama tayari wameshafunga ndoa na mmoja akapata maambukizi ya maradhi hayo basi Yule aliye salama hapaswi kumwacha huyo aliye na maradhi, wataendelea kubaki pamoja siku zote. Vile vile kama mmojawapo kapata ulemavu ambao utamfanya asiweze kabisa kukutana na mwenzake basi Yule aliye mzima pia hapaswi kumwacha mwenzake aliye na udhaifu, siku zote za maisha yake.

SWALI 03: Je wakristo wanaruhusiwa kutoa Ujauzito (Mimba)?

Jibu: Mkristo haruhusiwi kutoa ujauzito (mimba), kwasababu yoyote ile isipokuwa ya kiafya kwa maelezo ya madaktari:

Kwamfano  Ikitokea mtoto kafia tumboni hapo ni lazima ile mimba changa iondolewe ili kuokoa maisha ya mama, vile vile ikitokea itilafu katika tumbo la mama, ambayo ili mama awe salama (asipoteze maisha) na kama mama huyo hana imani ya kutosha ya kuamini kuwa anaweza kuishi bila kuitoa na akawa salama, na hivyo akakubali itolewe kufuatia maelezo hayo ya daktari, mama huyo hafanyi dhambi!, kwasababu ya usalama wake mwenyewe.

Lakini sababu nyingine yoyote ya kutoa mimba tofauti na hiyo ya kiafya, ni dhambi!..Kwamfano mwanamke kapata ujauzito bahati mbaya na alikuwa hana mpango wa kuipata hiyo, hapo hapaswi kuutoa huo ujauzito, au kapata ujauzito kwa njia ya ukahaba, hapo hapaswi kuitoa hiyo mimba, atabaki nao mpaka hatua ya kujifungua.

SWALI 04: Ni nani mtu sahihi wa kumpelekea matatizo ya ndoa? Endapo kukitokea kutokuelewana?

Jibu: Endapo kukitokea kutoelewana, ni vizuri kuomba kwa Bwana suluhisho na kurejea biblia kujua ni nini biblia inasema kuhusu hali hiyo, lakini kama bado mwanandoa anahisi anahitaji msaada zaidi basi anapaswa ayafuate makundi yafuatayo.

1: MCHUNGAJI WA KWELI WA BWANA:

Si wachungaji wote ni waaminifu, lakini pia wapo walio wa kweli na waaminifu, watu hao ni kituo bora cha kupata ushauri wa kiMungu na maombezi.

2. MZAZI:

Kama unaye mzazi aliyeokoka basi hicho pia ni kituo bora sana cha kupokea mashauri bora..na yenye msingi mkubwa.

Kamwe usitafute ushauri kwa marafiki, majirani, ndugu wa mbali, au watu usiowajua kuhusiana na mambo ya kindoa.

SWALI 05: Endapo nikagundua baada ya kufunga ndoa Mwenzangu ana matatizo katika uzazi wake (hana uwezo wa kuzaa au kuzalisha)..Je naweza kwenda kupata mtoto nje na kuendelea kuwa naye?

Jibu: Kama mwanandoa mmoja anamatatizo ya uzazi yanayomfanya asiweze kuwa na mtoto, hapo mwanandoa mwingine asiyekuwa na matatizo hayo hapaswi kumwacha Yule mwenye matatizo, wala kuondoka na kwenda kupata mtoto wa kando, atabaki naye huyo huyo siku zote za maisha yake, huku wakimwomba Bwana awafungue!.

Na kama ni mapenzi ya Bwana wao kuwa na watoto, basi Bwana atawapa mtoto haijalishi ni miaka mingapi itapita (Ibrahimu na Sara walipata watoto katika uzee), na Mungu ni Yule Yule hajabadilika.

Lakini pia kama wanaona ahadi za Mungu bado zipo mbali wanaweza ku-adopt  mtoto/watoto na kuwalea kama watoto wao.. Vipo vichanga vingi visivyo na wazazi, na mtu akiwalea hao mbele za Mungu ni zaidi hata ya Yule mwenye watoto 100 waliotoka katika uzazi wake.

SWALI 06: Je mkristo anaruhusiwa kupanga uzazi?

Jibu: Ndio wakristo wanaweza kupanga idadi ya watoto wanaotaka kuwa nao!. Biblia haijatoa amri ya kuzaa idadi ya watoto 10 au 50, ni kila mtu atakavyotaka yeye. Lakini imetoa tu angalizo kuwa tuwe watu wenye uwezo wa kuwatunza wakwetu (1Timotheo 5:8  Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.)

Kwahiyo ni lazima Mkristo awe na uwezo wa kuwatunza watoto wake, hivyo ni lazima awe na uzazi wa mpango.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA-1

MAFUNDISHO YA NDOA.

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

Rudi nyumbani

Print this post

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA

SWALI 01: Je wakristo tunaruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja?

Jibu: Kwa mujibu wa biblia, Ndoa ya kikristo ni ya mke mmoja na mume mmoja.

Marko 10:6 “Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.

7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;

8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja”.

SWALI 02: Je kama mtu alifunga ndoa ya kiserikali, au kimila ndoa hiyo inatambulika mbinguni?..Yaani Mungu anawatambua kama ni mume na mke kihalali?.

Jibu: Ndio! Mbinguni watu hao wanatambulika kama ni mke na mume, ingawa ndoa yao haitakuwa ndoa takatifu ya kikristo..maana yake kuna mambo hawataweza kuyafanya wakiwa katika hiyo hali, mfano wa mambo hayo ni Uchungaji wa kundi, au Uaskofu au Ushemasi. Kwasababu nafasi hizo ni za kuhubiria wengine njia sahihi, hivyo haiwezekani mtu awahubirie wengine wafunge ndoa takatifu ya kikristo wakati yeye mwenyewe hayupo katika ndoa kama hiyo. (Atakuwa mnafiki).(Tito 1:6-7).

Hivyo ni sharti aibariki ndoa yake hiyo na kuwa ndoa takatifu ya kikristo ili asifungwe na baadhi ya mambo.

Mfano wa ndio hizi ambazo ni za kipagani lakini Mungu alikuwa anazitazama ni kama ile ya Herode ambayo Yohana mbatizaji aliikemea.

Marko 6:17 “Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;

18 kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo”.

Herode hakuwa mkristo lakini alipomwacha tu mke wake na kwenda kumchukua wa ndugu yake ikawa ni chukizo mbele za Bwana, na vivyo hivyo ndio zote zilizofungwa ambazo zimehusisha mahari pamoja na makubaliano pande zote, basi ndio hizo Mungu anazitazama na zinapaswa pia ziheshimiwe.

SWALI 03: Je Wakristo tunaruhusiwa kutoa talaka?

Jibu: Wakristo hawaruhusiwi kuachana baada ya kuoana. Kwahiyo talaka hairuhusiwi katika ndoa ya kikristo wala mwanaume haruhusiwi kumwacha mke wake katika hali yoyote ile ya udhaifu wa kimwili.

Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”

SWALI 04: Je! Kama Mwanamke alikuwa ameolewa na mwanaume ambaye tayari alikuwa na Mke, je anapookoka anapaswa amwache huyo mume wake au aendelee naye?.

Jibu: Kulingana na maandiko anapaswa amwache kwasababu tayari huyo alikuwa ni mume wa mtu, hivyo ili maisha yake yawe na ushuhuda na aishi kulingana na Neno ni lazima amwache huyo na akaolewe na mwanaume mwingine ambaye hajaoa (lakini katika Bwana tu), au akae kama alivyo.

SWALI 05: Kama mwanaume alikuwa ameoa wanawake wawili na kashaishi nao muda mrefu na kuzaa nao watoto, lakini ukafika wakati akaokoka je anapaswa amwache mmoja na kuendelea na mwingine au?

Jibu: Kama mwanaume alikuwa amemwoa mwanamke wa kwanza katika ndoa ya kikristo (yaani iliyofungishwa kanisani), na baada ya ndoa hiyo akaongeza mwingine wa pili…Na baadaye akatubu na kuokoka upya!. Hapo hana budi kumwacha huyo wa pili kwasababu alikuwa anafanya uzinzi kulingana na biblia, haijalishi ameishi na huyo mwanamke kwa miaka mingapi, na amepata naye watoto wangapi..anapaswa amwache na kubaki na mke wake wa kwanza.

Lakini kama alimwoa mke wa kwanza kipagani na kulingana na sheria za kipagani akaongeza wa pili, na  akaishi nao muda mrefu na wanawake hao wote wawili bado wanahitaji kukaa naye, hapaswi kuwaacha labda mmoja wapo wa wanawake hao aridhie mwenyewe kumwacha kwa hiari yake..

Lakini kama ataendelea kubaki nao mtu huyo ndoa yake hiyo ya wake wawili haitawezi kubarikiwa kanisani, na pia yeye mwenyewe hataweza kuwa Mchungaji, askofu au Mwinjilisti au shemasi bali atakuwa muumini wa kawaida tu, kwasababu biblia inasema ni lazima Askofu awe mume wa mke mmoja..

Tito 1:6 “ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.

7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu; asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu”.

SWALI 06: Je?.Kujifungua kwa operation au kuzalishwa na wakunga wakiume ni halali kwa mwanandoa wa kikristo?.

Jibu: Operesheni ni njia mbadala ya kukiondoa kiumbe tumboni ili kusalimisha maisha ya mama na mtoto..Hivyo kibibla sio dhambi, kwasababu lengo lake ni kuokoa maisha na si lengo lingine.

Vile vile kuzalishwa na mkunga wa jinsia ya kiume si dhambi, kwasababu lengo ni lile lile kusaidia kuokoa maisha,..Katika eneo la uokozi ni eneo ambalo haliangalii jinsia..

Kwasababu pia zipo operesheni kubwa zaidi hata za kuzalisha ambazo zinahusisha kuondoa au kurekebusha viungo vya ndani kabisa vya uzazi wa mwanamke au mwanaume, ambazo operesheni hizo madaktari wake bingwa wanakuwa ni wa jinsia tofauti na wanaofanyiwa, hivyo hapo kama mtu anataka kupona kwa njia hiyo ya matibabu basi hana uchaguzi, wa atakayemfanyia hiyo operesheni.

Kwahiyo katika mazingira kama hayo, jinsia yoyote itakayotumika kumfanyia matibabu huyo mgonjwa wa kikristo, itakuwa si dhambi kwa mkristo huyo anauefanyiwa hiyo operesheni wala kwa yule anayemfanyia.

Shalom.

Usikose sehemu ya pili…

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

MAFUNDISHO YA NDOA.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Maswali na Majibu

Maswali ya hivi karibuni ni ya kwanza katika orodha, ili kusoma bofya somo husika uingie.Pia ukiwa na maswali/ unahitaji maombezi/ piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Unaweza pia kuyapata mafundisho yetu ya kila siku Whatsapp. Jiunge  kwa kubofya  hapa chini>

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ
https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

Print this post

MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA NA WASIO WAKRISTO (Sehemu ya kwanza).

Swali 1: Ni nani aliyemshawishi Daudi kuwahesabu Israeli ni Mungu au shetani?..Maana 2Samweli 24:1 inasema ni Mungu lakini 1Nyakati 21:1 inasema ni shetani.

Jibu: Ni shetani ndiye aliyemshawishi Daudi kwa ruhusa ya Mungu. Ayubu alijaribiwa na shetani kwa ruksa maalumu kutoka kwa Mungu. Hivyo ni sawa na kusema Mungu ndiye alimjaribu Ayubu..ni hivyo hivyo kwa Daudi pia.

Swali 02: Mungu anadanganya?maana  Ezekieli 14:9 inasema anadanganya.

Jibu: Mungu hadanganyi shetani ndiye anayedanganya, mtu mwovu anapoikataa njia ya haki, Mungu anaweza kuruhusu shetani amwingie na kumdanganya, hivyo inaweza kutafsirika kwamba kadanganywa na Mungu lakini si Mungu bali ni shetani (Soma 1Wafalme 22:20-23).

Swali 03: Nabii aliyetabiriwa na Musa kuwa atatokea si Yesu bali ni nabii mwingine kutoka Arabia,  Mohamedi (Kumbukumbu 18:15).

Jibu:

Kumbukumbu la Torati 18:15 “BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”

Musa alikuwa mwisraeli na si Mwarabu kutoka Saudi Arabia, na ndugu zake hawakuwa waarabu bali wayahudi..Na Mohamedi hakuwa Mwisraeli bali Mwarabu.

Lakini Bwana Yesu alikuwa Myahudi na alizaliwa Israeli. Na zaidi ya yote alifanya miujiza zaidi haya ya Musa. Kwahiyo Bwana Yesu ndiye aliyetabiriwa pale na yeye ndiye Mwanzo na Mwisho hakuna mwingine. (Matendo 7:37).

Swali 04: Biblia inasema tukifika peponi tutapewa wake mara 100 ya tulionao sasa, mabikira.(Marko 10:30). Kwanini mnasema hakuna kuoa peponi?

Jibu:

Marko 10:28 “Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.

29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,

30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”

Ndugu wake na ndugu waume, sio wake au waume au wachumba, bali ni ndugu wenye jinsia za kiume na za kike, na zaidi ya yote thawabu hizo ni katika ulimwengu huu huu, na sio peponi. Mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.(Marko 12:25)

Swali 05: Yesu alisema “kila mtu atabeba msalaba wake” iweje yeye achukue dhambi za wengine?

Jibu: Alisema “Mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake anifuate”. Marko 8:34.

Kinyozi akikwambia “ukitaka kuja kwangu kunyoa beba viwembe vyako unifuate na pia uwe tayari  kupata maumivu endapo ikitokea hitilafu”.. Je! Kwa kusema hivyo atakuwa amekataa kuchukua mzigo wako wa kukunyoa?.

Na wokovu wa Yesu ni hivyo hivyo, ukitaka  kupona, sharti ukubali gharama za wokovu. Ukikwepa gharama utakufa na dhambi zako.(Yohana 8:24).

Swali 06: Paulo kamtabiri Mohamed kupaa mpaka mbingu ya tatu 2Wakorintho 12:2, Mohamed ndiye pekee aliyefika mbingu ya tatu, Yesu hakufika huko.

Jibu: Si Mohamed aliyenyakuliwa mpaka mbingu ya tatu bali ni Paulo mwenyewe. Na Paulo aliishia hiyo mbingu ya tatu tu! Na si zaidi, lakini Bwana Yesu alifika mpaka mbingu za mbingu..ambazo hakuna aliyefika hata mmoja.

Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.

Waefeso 1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;

21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

 22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa…”

Swali 07: Je Bwana Yesu alikuwa ni Mungu au Mwanadamu? Maana biblia inasema alikuwa ni mtu! (Matendo 2:23)

Jibu: Bwana Yesu alikuwa ni Mungu kamili katika mwili wa kibinadamu, kutimiza kusudi Fulani maalumu,

Ukivaa vazi la kiaskari na kwenda kutimiza majukumu yako ya kiaskari, utaitwa askari na vile vile utafungwa na sheria za kiaskari, lakini hiyo haikufanyi wewe usiendelee kuwa mkurugenzi katika kampuni lako uliloliacha huko nyumbani, Au haikufanyi wewe usiendelee kuwa kiongozi katika Mtaa wako au mji wako.

Na Mungu alipouvaa mwili wa kibinadamu ulioitwa Yesu, ilikuwa ni lazima aitwe mtu!  kwa kitambo lakini hiyo bado bado haimfanyi asiendelee kuwa  Mungu.

Tito 2:13 ”tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”


Mada Nyinginezo:

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

Ni yupi aliyekuwa mkwe wa Musa kati ya Reueli na Yethro?

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.

Maelezo ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,  Ni upumbavu na aibu kwake.


Hekima inatufundisha tusiwe watu wa kujibu au kuzungumza kabla hatujasikia habari yote au taaarifa yote na kuitafakari kwanza..Kwamfano mwenzako anazungumza jambo Kisha wewe ukaingilia kati na kutaka kujibu, hoja ambayo haijakamilika..Matokeo yake hapo ni Nini kama sio kutoa majibu yasiyosahihi?. Au ambayo hayajakamilika?

Ndio hapo anasema ni upumbavu na aibu kwake. 

Hii imeathiri hata kusambaa Kwa taaarifa za uongo. Mtu atasikia jambo, kwasababu Hana taaarifa nalo vizuri, atatoka muda huo huo na kwenda kumpasha mwingine, na yule mwingine atampasha mwingine..Hivyo taaarifa za uongo huzagaa Kwa upesi sana. Ndivyo ambavyo hata waandishi wa habari ambao hawawi makini wanavyosambaza habari ambazo bado hawajazifanyia uchambuzi yakinifu. Na matokeo yake husababisha matatizo makubwa katika jamii. 

Mafarisayo na wayahudi walimpinga Yesu kwasababu walikuwa ni watu wa kupokea tu taaarifa ambazo hawazitafiti, walisikia Yesu anatokea Nazareti, wakahitimisha amezaliwa Nazareti, wengine wakamwita Msamaria. Lakini kama wangesubiri kutuatilia Kwa ukaribu mawazo Yao yangebadilika, na wasingekuwa wapumbavu kama tunavyowasoma kwenye biblia.

Hata wakati alipokuwa anazungumza nao, hawakutaka kusikiliza mpaka mwisho ni Nini Bwana anataka kuwaambia, kwamfano Kuna wakati aliwaambia, mtu akilishika Neno lake hataonja mauti milele. Lakini wao Hawakutaka ufafanuzi alimaanisha Nini.. hapo hapo wakarukia na kumwita ana Pepo;Kwa kauli Ile.

Yohana 8:52-53

[52]Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

[53]Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

Wakati mwingine aliwaambia livunjeni hili hekalu,nami nitalisimamisha baada ya siku tatu. Wakairukia hiyo kauli bila kusubiria maelezo  yake , ndio ikawa habari ya mji mzima Kuna mtu kasema anaweza kulijenga Kwa siku 3 hekalu lililojengwa Kwa miaka 46. Kumbe hawakujua Kristo anazungumzia habari ya mwili wake.(Yohana 2:20)

Biblia inatuasa tuwe wepesi wa kusikia, na si wa kusema; Ina faida nyingi.

Yakobo 1:19

[19]Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

HAUWEZI KURUKA MADARASA YA MUNGU!

KUOTA UPO UCHI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Maana ya Mithali 19:15 ‘Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;

Rudi nyumbani

Print this post

Hii ni Maana ya Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;

Fahamu Maana ya;

Mithali 18:18 Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.


Kupiga kura ni Moja ya njia ambayo ilitumika kuleta suluhisho lenye utata, na wakati mwingine kuchagua viongozi/wamiliki. Pitia hapa ujue zaidi kuhusu kura zilivyopigwa zamani za biblia…>> Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo;

Na Mungu wakati mwingine aliingilia kati na kuleta majibu yake sahihi kwa kupitia njia hiyo. Kwamfano wakati ule Yona anamkimbia Mungu, Hali ilipochafuka kule baharini, utaona wale watu walipiga kura, ili kujua sababu ya mambo yale ni nani na Ile kura ikamwangukia Yona.

Mitume wa Bwana baada ya kuomba, kuhusu mrithi wa nafasi ya Yuda wakapiga kura katika ya wale wanafunzi wawili, nayo ikamwangukia Mathiya, na likawa kweli ni chaguo la Mungu.(Matendo 1:15-19),

Hata wakati wa nchi ya Israeli kugawanywa . Kura zilitumika kuamua nani akae wapi, na nani arithi wapi (Hesabu 26:55).

Hivyo kupiga kura ilikuwa ni mojawapo ya njia kuleta jibu lisilokuwa na upendeleo. Au lililoegemea upande Fulani mmoja. Na kwa kufanya hivyo malalamiko mengii yalikomeshwa kwasababu maamuzi hayakuamuliwa na upande wowote ule.

Ndio maana ya hili andiko

Mithali 18:18

[18]Kura hukomesha mashindano;  Hukata maneno ya wakuu.

Hata kipindi Cha sasa njia ambayo hutumiwa kuchagua viongozi wengi ulimwenguni Huwa ni ya  kura.  Isipokuwa hii siyo ya kurusha SHILINGI, au kete angani  inayomwangukia mmojawapo ndio anakuwa kiongozi..hapana Bali ni kuruhusu Kila mmoja kutia maoni yake..Kisha zinahesabiwa na yule mwenye nyingi hupewa. Na hivyo hakuna malalamiko. 

Tofauti na Ile mtu atawadhwe tu Moja Kwa moja kuwa kiongozi, Hiyo huleta ukakasi mwingi.

Hivyo ni kutufundisha kua Bwana anaouwezo wa kuingilia kura zipigwazo na kuleta majibu yake sahihi..hususani pale anaposhirikwa Kwa maombi, na kama hakusema Kwa njia nyingine ya Moja Kwa moja.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

MKUU WA ANGA.

Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Biblia inakataza kuapa kabisa, lakini kwanini watu wanaapa mahakamani na katika vifungo vya ndoa?

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Rudi nyumbani

Print this post

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Ni muhimu kujua kanuni kadhaa za kuomba ili maombi yetu yawe na majibu.

Tumewahi kujifunza kanuni kadhaa huko nyuma na leo imempendeza Bwana tujifunze kanuni nyingine.

Neno la Mungu linasema yafuatayo katika kitabu cha Yakobo 4:2-3.

Yakobo 4:2 “ Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Kumbe sababu ya kutopata yale tunayoyaomba ni jinsi tunavyoomba!.. (kwamba tunaomba vibaya!).

Na kuomba vibaya kunakozungumziwa hapo si kukosea kupangilia maneno wakati wa kuomba, bali ni kuomba kusikompendeza Bwana, ambako ni nje na mapenzi ya Mungu, mfano wa maombi hayo ni yale mtu anaomba Bwana ampatie fedha ili awe nazo awakomeshe wanaomdharau. (Maombi ya namna hii ni maombi mabaya, na mara nyingi hayana majibu)

Hivyo unapoomba zingatia mambo yafuatayo.

1.Kuwa na Nia Njema:

Nia njema, maana yake ni kusudi jema… Kama unahitaji Bwana akupe mafanikio Fulani ya kiroho au ya kimwili, hakikisha Nia yako ni njema, kwamba utokane tu na ugumu unaoupitia, na pia upate kitu cha kuwasaidia wengine, na si kwa lengo la kuwakomesha wanaokudharau. Ukiwa na Nia ya kupata vitu ili wengine waone, maombi hayo yanaweza yasijibiwe kabisa.

2. Mwombe Mungu mahitaji na si Fedha.

Wengi wetu tunapenda kupeleka maombi ya kupata fedha kutoka kwa Mungu.. Lakini kiuhalisia hayo si maombi bora. Tunasahau kuwa tunachokihitaji sana ni mahitaji yetu kama chakula, mavazi, makazi, afya na mengineyo, ambayo hayo Mungu anaweza kukutimizia pasipo fedha.

Ukiwa na haja ya chakula, mwambie Bwana naomba chakula na yeye anajua namna ya kukupatia hicho chakula kama kwa njia ya kukupatia fedha ukanunue, au kwa kukuletea mtu atakayekupa hicho chakula, (usikimbilie moja kwa moja kumwambia Bwana akupe fedha ya chakula), kwani yeye anazo njia nyingi za kukulisha wewe, si lazima kwa kutumia fedha.

Vile vile ukitaka mavazi, makazi, biashara, afya n.k  Mwambie Bwana akupe vitu hivyo, na wala usiombe fedha za kupata mavazi, au za kupata makazi, au za kufanya biashara.. wewe mwambie naomba mavazi, yeye anajua jinsi ya kukupatia kama kupitia mlango huo wa fedha au kupitia watu yeye anajua, vile vile usiombe mtaji kwa Mungu, badala yake iombe ile kazi kwasababu wakati wewe unawaza kupata mtaji kwanza kumbe pengine Mungu amekuandalia mahali utakapoanza kufanya kazi pasipo mtaji.

Ukihataji Bwana akupe kifaa cha kazi au chombo za kukurahisishia usafiri, usimwambie Bwana akupe Pesa za kununua chombo hicho, badala yake mwombe Bwana akupe hicho chombo, kwa njia anayoijua yeye.

Ukitaka kusafiri usimwombe Bwana fedha za kusafiri, wewe mwombe akusafirishe, yeye atajua njia atakayotumia kukufikisha kule unakotaka kwenda, kama amtanyanyua mtu na kukusafirisha kwa gharama zake au bure, au atafungua mlango wa wewe kupata fedha hizo, ila usijifunge kwa kanuni ya fedha.

Vile vile unapoumwa usimwombe Mungu pesa za matibabu, mwombe afya, yeye anajua njia atakayotumia kukupa hiyo afya, na mambo mengine yote, epuka Kutaja “Pesa” mbele za Mungu!!.. bali taja lile hitaji!.

Kwanini maombi mengi ya kuomba Pesa hayajibiwi?

Kwasababu kuna roho nyuma ya pesa, inayowasukuma watu katika tamaa mbaya za kidunia, na kuwatoa wengi kwenye Imani, ndivyo maandiko yanavyosema.

1Timotheo 6:10  “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”

Ndio maana utaona asilimia kubwa ya watu waliopata pesa wanakuwa na kiburi!. Lakini waliopewa na Bwana ni wanyenyekevu. Mtu aliyezawadiwa baiskeli na yule aliyenunua baiskeli kwa fedha, utaona yule aliyenunua anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyepewa. Ingawa wote wana baiskeli!.

Yule aliyezawadiwa nyumba na yule aliyejenga kwa fedha yake, utaona yule aliyejenga anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyezawadiwa. Na mapenzi ya Mungu ni sisi tuwe wanyenyekevu na si watu wenye viburi, hivyo kamwe hawezi kukupa kitu ambacho baadaye kitakuja kukupa kiburi.

Ni wachache sana ambao Mungu anawabariki kwa fedha, kwasababu anajua tayari ameshawatengeneza mioyo yao, hawawezi kuwa na kiburi hata wawe na kiasi gani cha fedha, na hiyo naweza kusema ni asilimia 1% lakini wengi Mungu hawapi hizo fedha wanazozihitaji kwasababu anajua tamaa tulizo nazo. Na ukiona mtu ana fedha nyingi na ana kiburi (hizo fedha hajapewa na Mungu!!).

Kama mkristo biblia inatufundisha tusiwe watu wa kupenda fedha, wala kuzisifia wala kuzitukuza, badala yake tumtukuze Mungu na tumfanye Mungu siku zote kuwa MPAJI WETU (YEHOVA YIRE)!!. Kwamba fedha ziwepo au zisiwepo bado tutaishi, bado tutavaa, bado tutakula, bado tutamiliki vitu.. Tuliookoka tuna uwezo wa kuishi bila fedha wala vitu vilivyotukuzwa na wanadamu na bado tukawa na maisha bora kuliko watu wenye mambo hayo.

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Daudi achukue mawe matano, na malaini na sio vinginevyo?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya mawe matano ya kombeo na jiwe la kwanza maana yake nini na la pili hata la tano, na kwa nini mawe laini asingeokota jiwe ni jiwe tu?


JIBU: Daudi alipokutana na Goloathi maandiko yanatuambia akashuka katika kijito Cha maji akayaokota mawe matano malaini, kama silaha yake ya kumwangusha Goliathi.

1 Samweli 17:40

[40]Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.

Lakini Swali linakuja, Kwanini yawe matano, na je yanafunua Nini rohoni? Na pia Kwanini yawe malaini?

Baadhi ya watu wanaamini pengine Daudi hakuwa na Imani ya kutosha Kwa Mungu ya kuamini kuwa jiwe Moja tu lingetosha kumwangusha Goloathi, ndio maana akachukua matano. Lakini uhalisia ni kwamba Daudi alikuwa na Imani, hata kitendo tu Cha kukataa kubeba silaha za vita alizopewa na mfalme ilikuwa ni Imani kubwa.

Wengine wanaamini mawe Yale matano, yanafunua mambo matano ambayo Daudi alikuwa nayo yaani  1) Imani, 2) utiifu, 3)utumishi, 4)maombi na 5) Roho Mtakatifu.

Wengine wanaamini kuwa yanasimama kuwawakilisha wale watoto 5 wa Yule jitu aliyeitwa Refai, ambapo, Goliathi akiwa mmojawapo.(2Samweli 21:15-22). Hivyo Daudi alionyesha kuwa wote atawaangamiza.

Wengine wanaamini kuwa mawe yale matano yanafunua zile huduma tano (5), Waefeso 4:11. Ambazo hizo zinasimama kama msingi wa kumuangusha shetani  katika kanisa.

Lakini tukirudi  katika muktadha wa habari yenyewe, kiuhalisia ni kuwa Daudi alichukua mawe matano, akiamini kuwa la kwanza likimkosa bado la pili lipo atarusha tena, na kama la pili likimkosa basi bado lipo la tatu atarusha tena..Kufunua jinsi gani alivyokuwa na akiba ya imani. Bwana Yesu alisema, Imetupasa kuomba sikuzote bila kukata tamaa,  (Soma Luka 18:1-8), Upo wakati utaomba jambo kwa Bwana, halafu usijibiwe muda huo huo, je! Utakata tamaa kesho tena usiombe? Yesu anatuambia tuombe bila kukoma. Daudi aliamini hata ikitokea jiwe la kwanza limegonga dirii ya chuma, sio wakati wa kuvunjika moyo, ni kuvuta lingine, na kuendelea na mapambano. Vivyo hivyo na sisi yatupasa tuwe watu wenye akiba nyingi ya imani ndani yetu. Tunaomba tena na tena na tena, kwasababu hatujui ni jiwe lipi litaleta majibu, kama ni la kwanza au la katikati au la mwisho.

Lakini pia utaona hekima nyingine Daudi aliyoitumia ni kwenda kuyachukua mawe yake kwenye kijito cha maji. Jiulize ni kwanini iwe kwenye maji na sio penginepo? Kwasababu kimsingi mawe yapo kila mahali. angeweza kuokota tu ardhini.

Ni kufunua nini? Daudi alitambua VIJITO VYA MAJI YA UZIMA, ndipo wokovu ulipo. Ambavyo ni Yesu Kristo (Yohana 7:28). Usalama wa imani yake uliegemea kwa Mungu.  Hata sasa Bwana anataka imani yetu iegemee kwa Yesu Kristo, huko ndiko asili ya nguvu zetu ilipo, Kama mkristo usipolitambua hili ukawekeza imani yako kwenye elimu, au mali, au vitu vya ulimwengu huu, tambua kuwa huwezi mpiga adui yako ibilisi, kwa lolote.

Na mwisho kabisa Daudi aliyatwaa mawe laini kwanini yawe malaini.  Hata katika maji, yapo mawe ya maumbile mbalimbali, yapo makubwa yapo madogo, yapo yenye ncha, yapo malaini. Lakini alitambua kuwa jiwe litakalokaa katika kombeo lake, na litakalopaa vizuri na kumwangusha adui yake, sio kubwa, wala lenye ncha, wala zito sana. Bali laini, la mviringo. Kufunua nini.. Hauhitaji imani kubwa ya kuhamisha milima ili kumwangusha ibilisi. Bali kipimo cha imani yako, ukikitumia vema kinatosha kabisa kumdondosha Shetani.

Warumi 12:3  Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani. 4  Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; 5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

Ukitumia vema nafasi yako uliyopewa na Mungu. Katika udogo wako, unyonge wako, umaskini wako, utamwangusha adui. Kila mmoja wetu amepewa nguvu hizo na Mungu. Hivyo usisubiri uwe Fulani ndio udhani utauangusha ufalme wa shetani. Hapo hapo ulipo ikiwa umeokoka, jiwe lako Kristo amekutolea. Litumie vizuri, lirushe vema, Goliathi atalala chini.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

LIONDOE JIWE.

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

JIWE LILILO HAI.

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mhubiri 10:20 inaposema Usimlaani mfalme, la, hata katika wazo lako?

Mhubiri 10:20 Usimlaani mfalme, la, hata katika wazo lako; Wala usiwalaani wakwasi chumbani mwako; Kwa kuwa ndege wa anga ataichukua sauti, Na mwenye mabawa ataitoa habari

JIBU: Ni vema kutambua kuwa aliyeandika habari hii alikuwa ni mfalme, hivyo alitambua vema alichokiandika,  na kwa hekima ya Ki-Mungu akazinakili ili ziwe onyo na angalizo kwetu . Ni wazi kuwa aliwahi kukutana na taarifa nyingi za uasi zilizowahi kupangwa  kinyume chake kwa siri, au  maneno ya unafiki, au ya dhihaka zilizosemwa kwa siri kinyume chake. Na yote hayo yakamfikia kwa haraka sana, kinyume na matarajio ya wale waliyoyapanga. Na huwenda wakawa wanabakiwa na maswali mengi, ni nani anayetoboa siri zao?.Wakakosa majibu

Sasa ni kwanini iwe hivyo?

Ni kwasababu Utawala wowote wa wakuu, unaundwa pia na ulinzi wake maalumu, (unaojulikana na ule wa siri usiojulikana). Kiasi kwamba chochote utakachokipanga kinyume chake kwa siri , tambua tu kitamfikia. Ndio maana hapo anasema usiwalaani katika wazo, au katika chumba chako cha siri.. Akiwa na maana hata wazo lako usiliruhusu kufanya hivyo, kwasababu mtu anayanena yaujazayo moyo wake. Kabla uasi haujatokea nje, unaanzia kwanza rohoni.

Halikadhalika wakwasi wanaozungumziwa hapo, ni watumishi wa wafalme, aidha mawaziri, au maakida, au maliwali ambao kikawaida huwa ni matajiri, vivyo hivyo na wao usijaribu kufanya hivyo ukidhani taarifa hazitawafikia. Zitawafikia, Mhubiri anatumia mfano wa ndege anasema.. ‘Kwa kuwa ndege wa anga ataichukua sauti, Na mwenye mabawa ataitoa habari’. Yaani kwa jinsi ndege wanavyoweza kusafiri kwa haraka, sehemu moja hadi nyingine, kwa wepesi wao na safari yao ya anga isivyo na vikwazo, ndivyo watu usiowajua watakavyoifikisha habari kwa wakuu wao, kinyume na matazamio yako.

Ndivyo ilivyokuwa kipindi cha mfalme Ahasuero, kulitoka watu wawili waliopanga mikakati kwa siri kumuua, lakini taarifa zilimfikia haraka mfalme kwa kinywa cha Mordakai mlinzi wa mlangoni, na wale watu wakagundulikana wakauliwa mara moja. (Esta 2:21-23)

Kufunua nini?

Hakuna jambo lolote la siri ambalo halitajulikana kwa wakuu.

Tunaye Mfalme wa Wafalme, YESU KRISTO ambaye ndiye anayepaswa kuogopwa na watu wote ulimwenguni. Na kwamba hatupaswi kufanya jambo lolote kinafki, au kwa-siri mbele zake, linalokinzana na ufalme wake duniani. Kwasababu yote yatakuja kufichuliwa na kuwekwa wazi siku ile ya mwisho ya hukumu.

Yeye mwenyewe  alisema;

Luka 12:2  “Lakini hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa ambalo halitajulikana. 3  Basi, yo yote mliyosema gizani yatasikiwa mwangani; na mliyonena sikioni mwa mtu katika vyumba vya ndani, yatahubiriwa juu ya dari”

Hivyo uonapo kazi ya Mungu ya kweli inatendeka, kuwa makini sana na kinywa chako, uyapinge hata hayo mawazo yanayotaka kukwambia utukane, au ukufuru, au upinge. Vilevile wewe kama mhudumu wa kazi ya Bwana, tumika kwa uaminifu na kwa hofu ukijua kabisa mambo yako yote yanaonekana wazi mbele za Mungu, hakuna maficho.

Tuwe makini sana na ufalme wa Yesu Kristo duniani.

Je! Upo ndani ya Kristo? Je! Unatambua kuwa hizi ni nyakati za hatari, Yesu yupo mlangoni sana kurudi kulichukua kanisa lake? Unaishi maisha ya namna gani, ukifa leo huko uendako utakuwa mgeni wa nani? Embu tubu dhambi zako mgeukie Bwana akutakase, umtumikie yeye katika kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho, itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima kisha ukapata hasara ya nafsi yako?. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya toba >>>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

JINA LAKO NI LA NANI?

Rudi nyumbani

Print this post