Maswali ya hivi karibuni ni ya kwanza katika orodha, ili kusoma bofya somo husika uingie.Pia ukiwa na maswali/ unahitaji maombezi/ piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312
Unaweza pia kuyapata mafundisho yetu ya kila siku Whatsapp. Jiunge kwa kubofya hapa chini>
Utapata Majibu ya Maswali mengi kupitia page hii. Karibu sana!
1. Kuota Mtu aliyekufa maana yake nini
2. Je apandacho mtu ndicho atakachovuna?
3. Je Kuota unakimbizwa ina maana gani?
4. Je Kuota unafanya mtihani kuna maanisha nini?
5. Kuota Nyoka maana yake nini?
6. Kuota Unasafiri maana yake nini?
7. Kuona una mimba maana yake nini?
8. Nini maana ya Asiyefanya kazi na asile?
9. Namna bora ya kuomba ni ipi?
12. Je Wakatoliki wanaabudu sanamu?
13. Kwanini Wakristo wengi ni maskini?
14. Kuota unapewa Pesa maana yake ni nini?
15. Je! Mungu anaweza kumsahau mtu?
16. Kuota Umebeba Mtoto maana yake nini?
[faqs]
Swali 1: Ni nani aliyemshawishi Daudi kuwahesabu Israeli ni Mungu au shetani?..Maana 2Samweli 24:1 inasema ni Mungu lakini 1Nyakati 21:1 inasema ni shetani.
Jibu: Ni shetani ndiye aliyemshawishi Daudi kwa ruhusa ya Mungu. Ayubu alijaribiwa na shetani kwa ruksa maalumu kutoka kwa Mungu. Hivyo ni sawa na kusema Mungu ndiye alimjaribu Ayubu..ni hivyo hivyo kwa Daudi pia.
Swali 02: Mungu anadanganya?maana Ezekieli 14:9 inasema anadanganya.
Jibu: Mungu hadanganyi shetani ndiye anayedanganya, mtu mwovu anapoikataa njia ya haki, Mungu anaweza kuruhusu shetani amwingie na kumdanganya, hivyo inaweza kutafsirika kwamba kadanganywa na Mungu lakini si Mungu bali ni shetani (Soma 1Wafalme 22:20-23).
Swali 03: Nabii aliyetabiriwa na Musa kuwa atatokea si Yesu bali ni nabii mwingine kutoka Arabia, Mohamedi (Kumbukumbu 18:15).
Jibu:
Kumbukumbu la Torati 18:15 “BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”
Musa alikuwa mwisraeli na si Mwarabu kutoka Saudi Arabia, na ndugu zake hawakuwa waarabu bali wayahudi..Na Mohamedi hakuwa Mwisraeli bali Mwarabu.
Lakini Bwana Yesu alikuwa Myahudi na alizaliwa Israeli. Na zaidi ya yote alifanya miujiza zaidi haya ya Musa. Kwahiyo Bwana Yesu ndiye aliyetabiriwa pale na yeye ndiye Mwanzo na Mwisho hakuna mwingine. (Matendo 7:37).
Swali 04: Biblia inasema tukifika peponi tutapewa wake mara 100 ya tulionao sasa, mabikira.(Marko 10:30). Kwanini mnasema hakuna kuoa peponi?
Jibu:
Marko 10:28 “Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”
Ndugu wake na ndugu waume, sio wake au waume au wachumba, bali ni ndugu wenye jinsia za kiume na za kike, na zaidi ya yote thawabu hizo ni katika ulimwengu huu huu, na sio peponi. Mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.(Marko 12:25)
Swali 05: Yesu alisema “kila mtu atabeba msalaba wake” iweje yeye achukue dhambi za wengine?
Jibu: Alisema “Mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake anifuate”. Marko 8:34.
Kinyozi akikwambia “ukitaka kuja kwangu kunyoa beba viwembe vyako unifuate na pia uwe tayari kupata maumivu endapo ikitokea hitilafu”.. Je! Kwa kusema hivyo atakuwa amekataa kuchukua mzigo wako wa kukunyoa?.
Na wokovu wa Yesu ni hivyo hivyo, ukitaka kupona, sharti ukubali gharama za wokovu. Ukikwepa gharama utakufa na dhambi zako.(Yohana 8:24).
Swali 06: Paulo kamtabiri Mohamed kupaa mpaka mbingu ya tatu 2Wakorintho 12:2, Mohamed ndiye pekee aliyefika mbingu ya tatu, Yesu hakufika huko.
Jibu: Si Mohamed aliyenyakuliwa mpaka mbingu ya tatu bali ni Paulo mwenyewe. Na Paulo aliishia hiyo mbingu ya tatu tu! Na si zaidi, lakini Bwana Yesu alifika mpaka mbingu za mbingu..ambazo hakuna aliyefika hata mmoja.
Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.
Waefeso 1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa…”
Swali 07: Je Bwana Yesu alikuwa ni Mungu au Mwanadamu? Maana biblia inasema alikuwa ni mtu! (Matendo 2:23)
Jibu: Bwana Yesu alikuwa ni Mungu kamili katika mwili wa kibinadamu, kutimiza kusudi Fulani maalumu,
Ukivaa vazi la kiaskari na kwenda kutimiza majukumu yako ya kiaskari, utaitwa askari na vile vile utafungwa na sheria za kiaskari, lakini hiyo haikufanyi wewe usiendelee kuwa mkurugenzi katika kampuni lako uliloliacha huko nyumbani, Au haikufanyi wewe usiendelee kuwa kiongozi katika Mtaa wako au mji wako.
Na Mungu alipouvaa mwili wa kibinadamu ulioitwa Yesu, ilikuwa ni lazima aitwe mtu! kwa kitambo lakini hiyo bado bado haimfanyi asiendelee kuwa Mungu.
Tito 2:13 ”tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”
Mada Nyinginezo:
Jibu: Tusome,
Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
36 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye
37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
38 Naye mwenyewe alikuwapo katika SHETRI, amelala JUU YA MTO; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?”.
Katika kisa hicho tunaona Wanafunzi walimchukua Bwana Yesu kama alivyo (yaani bila ya kitu chochote cha njiani kama vile chakula, au mavazi). Walimchukua kama alivyo..Na kumchukua kunakozungumziwa hapo ni kumchukua, kama vile mtu anavyomchukua mwenzake na kumpa lifti ya gari, ndivyo wanafunzi walivyomchukua Bwana Yesu..
Lakini tunaona walipokuwa njiani ndani ya ile Merikebu, Bwana Yesu alienda kulala katika Shetri ya Merikebu.
Sasa “SHETRI” au kwa lugha nyingine “TEZI”, ni sehemu ya Nyuma ya Meli au Merikebu, ambayo ni pana, na ndiyo iliyotumika katika kuwekea mizigo, na pia ndipo palipotengenezewa vyumba vya kulala watu. Sehemu ya mbele ya Meli au Merikebu inaitwa “OMO”, ambayo ni nyembamba ili kuisiaidia meli kukata mawimbi.
Sasa Bwana Yesu alienda kulala kwenye Shetri, mahali ambapo kulikuwa na nafasi ya kulala, na akawa amelala juu ya mto! (Mto unaozungumziwa hapa sio mto wa kutiririsha maji, bali ni ule mto wa kulalia kitandani, kuupatia shingo egemeo bora). Na akiwa Dhoruba ikaanza, na chombo kikakaribia kuzama..na Baadaye wanafunzi wakamwamsha Bwana na Bwana Yesu akaikemea ile Dhoruba ikatulia.
Sasa kikubwa tunachoweza kujifunza katika tukio hilo ni kuwa, Bwana Yesu anaweza kuwa yupo ndani yetu lakini amelala!. Tusipopaza sauti zetu kwa nguvu kwa maombi, basi tutahangaika na Dhoruba zilizopo nje, na wala yeye hatasema chochote.
Hii inatukumbusha kuwa waombaji, na si waombaji tu, bali waombaji wenye bidii, wenye kupaza sauti mpaka majibu ya maombi yatokee.
Bwana atusaidie katika hayo.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Bustani ya Edeni ipo nchi gani?
MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.
NI NINI TUNAJIFUNZA KWA DEMA NA MARKO?
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maneno ya Uzima wa Mungu wetu..
Yapo maswali kadhaa ambayo tunaweza kujiuliza, juu ya tukio la Bwana Yesu kutokewa na Musa na Eliya siku ile alipopanda mlimani kuomba pamoja na wale wanafunzi wake watatu (Petro, Yohana na Yakobo)..
Na maswali yenyewe ni haya..
1) Iweje Bwana Yesu atokewe na Musa ambaye tayari alishakufa miaka mingi?, na Zaidi ya yote maandiko yanasema alizikwa, tena na Mungu mwenyewe?..
2) Kwanini Musa na Eliya wamtokee?.. kulikuwa na umuhimu gani wa wao kumtokea Bwana?
Sasa ili tupate majibu ya maswali hayo vizuri, Labda tusome habari yenyewe kwa ufupi kisha tuendelee
Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.
29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.
30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni MUSA NA ELIYA;
31 walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”
Kiini cha majibu ya maswali yetu tutakipata katika huu mstari wa 31.. “walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”
Kumbe Sababu ya Musa na Eliya kumtokea Bwana, ilikuwa ni kuzungumza kuhusu Kufa kwake Bwana Yesu, ambako atakutimiza Yerusalemu.
Sasa swali linakuja?, je ni kwamba Bwana Yesu alikuwa hajui kwamba atakwenda kufa mpaka atokewe na watu hao wawili, wamweleze kuhusu kufa kwake?.. Jibu ni la!.. alikuwa anajua, lakini zipo siri nyingine zihusuzo kufa kwake na kufufuka kwake na kupaa kwake, ambazo hizo Baba alimfunulia siku hiyo kupitia manabii hao wawili.
Kumbuka kabla ya Kristo kufa, roho za watakatifu zilikuwa chini, na shetani alikuwa na uwezo wa kuzileta juu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka lile tukio la Samweli kuletwa juu ya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi, na baada ya kuletwa juu, Samweli aliweza kutoa unabii wa mambo yajayo, ijapokuwa alikuwa ameshakufa na kuzikwa, kwani tunasoma, alimtolewa Unabii Mfalme Sauli kuhusu KUFA KWAKWE, AMBAKO KUTAKWENDA KUTIMIA KIPINDI SI KIREFU KUTOKA PALE. Unaweza kusoma Habari hiyo kwa urefu katika kitabu cha 1Samweli 28:1-19.
Sasa Biblia haijaeleza Musa alikuwa anamweleza nini Bwana Yesu, lakini tunajua kabisa ni kuhusu Habari za kufunguliwa kwao wafu, na kwamba Bwana Yesu atakwenda kusulibiwa na kushuka sehemu ya wafu wao (akina Musa na wengine walipo na kuwaweka huru, na kwamba siku ya tatu atafufuka).
Kwahiyo kumbe kabla ya Bwana Yesu kufa, Wafu waliendelea kuishi, na pia iliwezekana kuwaleta baadhi yao juu na kutoa unabii, kwa njia yoyote ile!..
Kwasababu hiyo basi tumeshapata jibu ni kwanini MUSA, aliletwa juu na Mungu, ili kutoa unabii (Habari za kufa kwake Bwana Yesu, ijapokuwa Musa alikuwa ameshakufa kitambo na kuzikwa)…Ni kama tu vile, Nabii Samweli alivyoletwa juu na yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi. (Kumbuka jambo hilo liliwezekana tu kipindi kabla ya Bwana Yesu kufa, lakini baada ya Bwana Yesu kufa na kufufuka, hakuna mchawi yeyote anayeweza kumleta juu mtu aliyekufa, kwasababu Kristo alizichukua funguo za Mauti na kuzimu).
Hapo tumepata jibu kuhusu Musa, sasa vipi kuhusu ELIYA?
Tunajua kabisa Eliya hakufa, bali alipaa..Maana yake Eliya anayajua yaliyo ya Mbinguni.. kama Nabii, Bwana alimtoa huko na kuja kumpasha Habari Bwana Yesu, kuhusu kupaa kwake, na enzi na mamlaka zinazomngojea Mbinguni (labda na siku hiyo alimpa na tarehe ya kupaa kwake, hatujui).
Kwasababu ijapokuwa Eliya alikuwa amepaa mbinguni, lakini bado alikuwa ni Nabii. Kwahiyo ujio wa Eliya ulikuwa ni wa muhimu sana kwa Bwana, kupata taarifa kuhusu kupaa kwake.
Kwahiyo kwaufupi ni kwamba Mungu aliwatumia manabii hawa wawili kama Manabii wa Ushahidi. Na Ushahidi huo ni wa KUFA kupitia Musa, na Kupaa kupitia ELIYA. Kwasababu Kristo naye atakufa kama Musa aliye nabii mkuu, na vile vile atapaa mbinguni kama ELIYA.
Kwahiyo baada ya tukio lile, Bwana Yesu alipokea Ufunuo mkuu kuhusu Mauti yake na kufufuka kwake, na kupaa kwake.. Zaidi sana na kurudi kwake kutakavyokuwa..ndio maana tunaona pia Uso wake uling’aa kama jua, kuashiria siku ya kurudi kwake kutakavyokuwa.
Na wakati ulipofika kweli Bwana Yesu, alikufa, akafufuka, na akapaa mbinguni.. imesalia hatua moja tu!.. nayo ni KURUDI KWAKE KUTUCHUKUA!..
Je! Umejiandaaje?.. Kama Nabii hizo mbili za kufa na kufufuka kwake na kupaa kwake zilitimia.. Basi hata kurudi kwake kutatimia. Na tupo katika majira ya kurudi kwake, dalili zote zimeshaonekana, muda wowote mambo yanakwisha, Kristo anakuja kuwachukua watakatifu wake, na kitakachokuwa kimesalia kwa wale watakaobaki ni majuto na dhiki kuu.
Je umejiandaaje? Je umemwamini Yesu na kutubu dhambi zako? Je umebatizwa katika ubatizo sahihi?…kama bado unangoja nini?.. Ukiikataa leo injili siku hiyo hutakuwa na la kujitetea. Mpokee Yesu leo, na ukabatizwe na kujazwa Roho Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?
Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;
Ngome ni nini? Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?
SWALI: Isaya 59:5 ina maana gani?
Isaya 59:5 Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.
JIBU: Ni mstari unaoeleza asili ya watu waovu.
Anasema huangua mayai ya fira. Fira ni aina ya nyoka wenye sumu kali sana, ambao kwa kawaida mtu akikutana nao, ni lazima awaue, au akikuta mayai yao ni lazima ayakanyage, kwasababu, asipofanya hivyo yakitotolewa wataleta madhara, Lakini mtu mwovu biblia inasema ni kinyume chake huyatotoa. Ikiwa na maana ni mtu ambaye anaona madhara Fulani yanakuja mbele kwa wengine badala ayaangamize, yeye ndio anayekuwa wa kwanza kuyakumbatia.
Mfano mmojawapo wa hawa ni manabii wa uongo, wanaojua kabisa, dhambi ina madhara, na mtu asipoishi katika utakatifu hawezi kumwona Mungu (Waebrania 12:14), lakini kwasababu hawataki kupoteza watu, kwa tamaa za pesa, hawawaonyi juu ya mambo kama hayo, kinyume chake ndio wanawasogeza kabisa kwenye mambo ya mwilini, biashara na mali, wanamsahau Mungu. Halafu wanakufa katika dhambi zao na kwenda kuzimu.
Vilevile anasema husuka wavu wa buibui. Kama vile tunavyojua buibui anaposuka wavu wake, ni kwa lengo la kunasa wadudu awale. Halikadhalika asili ya watu wa waovu ndivyo ilivyo, huandaa mazingira yote, ya wenzao kunaswa katika mambo maovu na kuangamia.
Kwamfano unapomwombea adui yako afe, ni sawa na mtu anayeunda wavu wa uangamivu. Bwana alisema tuwaombee, lakini sisi tunawatakia mauti, tena katika maombi.
Kwa ufupi, hii ni tabia ya kutengeneza kama sio kufurahia anguko la wengine.
Hivyo biblia inatuonyesha pia tukiwa na tabia kama hizo, zinatufanya na sisi Mungu asitutee na kutupa haki zetu kwa vile tumwombavyo, nasi majibu yanakuja kinyume chake.. Pale tunapotazamia jema linakuja ovu,na tunapotazamia nuru linakuja giza, tunalithitibitisha hilo katika vifungu vinavyofuata..
Isaya 59:6-9
6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao.
7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.
8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.
9 KWA SABABU HIYO HUKUMU YA HAKI I MBALI NASI, WALA HAKI HAITUFIKILII; TWATAZAMIA NURU, NA KUMBE! LATOKEA GIZA; TWATAZAMIA MWANGA, LAKINI TWAENDA KATIKA GIZA KUU.
Hivyo tupambane, kwa bidii zote tusiwe vyombo vya shetani vya kuunda mabaya kwa wengine.
Bwana atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Ipo tofauti ya “Uzima” na “Uzima wa milele”.
Uzima, kila mwanadamu anao, na si wanadamu tu peke yao wenye uzima, bali hata Wanyama wanao uzima, na hata ndege na mimea. Lakini Pamoja na kwamba Uzima upo kwa viumbe vingi, lakini Uzima wa milele haupo kwa wote.
Uzima wa Milele ni kitu kingine kabisa…ambacho Mtu hana budi kukitafuta.. Na asipokitafuta na kukipata ataishia kuwa na uzima tu wa kitambo, ambao hautadumu sana, kwasababu wote wasio na uzima wa milele ndani yao, wakishakufa hawatafufuliwa na kuendelea kuishi, badala yake wataangamizwa katika ziwa la moto.
Na Uzima wa milele (ambao kwa lugha nyingine unaitwa “UZIMA TELE”), Unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni Yesu.
Yohana 10:10 “…mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, KISHA WAWE NAO TELE”.
Umeona?..Bwana Yesu amekuja ili tuwe na UZIMA, yaani tuwe na Afya, tuishi Maisha ya heri katika mwili, lakini hajaishia hapo, bali pia tuwe na UZIMA TELE, (Yaani tuwe Uzima wa Milele).
SASA SWALI NI JE TUTAUPATAJE UZIMA WA MILELE?
Jambo moja linalowachanganya wengi, ni kudhani kuwa kuwa na maadili mazuri au kuwa na dini nzuri, au KUSHIKA AMRI 10, ndio kupata Uzima wa milele, pasipo kujua kuwa kuzishika amri 10, au kuwa na dini nzuri, au dhehebu zuri, kama mtu “hajaamua kujikana nafsi ya kumfuata Bwana Yesu” ni kazi bure.. Dini yake nzuri huyo mtu, au maadili yake mazuri, au sifa yake nzuri bado, hakutampa uzima wa milele.
Hebu tusome kisa kifuatacho.. (Zingatia vipengele vilivyoanishwa kwa herufi kubwa).
Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate UZIMA WA MILELE?
17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. LAKINI UKITAKA KUINGIA KATIKA UZIMA, zishike amri.
18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,
19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?
21 Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, ENENDA UKAUZE ULIVYO NAVYO, UWAPE MASKINI, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; KISHA NJOO UNIFUATE”.
Hapo nataka uone maswali, huyu mtu aliyomwuliza Bwana na Majibu Bwana aliyompa.. Swali la kwanza huyu mtu alitaka kujua jinsi ya kuupata UZIMA WA MILELE. Lakini utaona Bwana Yesu alimwambia akitaka KUUPATA UZIMA, (Zingatia; sio uzima wa milele, bali Uzima tu), azishike amri.
Ikiwa na maana kuwa Kuzishika amri 10 peke yake hazimpi mtu UZIMA WA MILELE, bali zinampa tu UZIMA. (aishi Maisha marefu hapa duniani na ya heri) Sawasawa na Walawi 18:5.
Walawi 18:5 “Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo MTU AKIZITUMIA ATAISHI KWA HIZO; mimi ndimi Bwana”.
Lakini swali la pili, huyu mtu alilomwuliza Bwana Yesu ni kwamba, tayari ameshazishika hizo amri, ni kitu gani alichopungukiwa Zaidi?.
Na Bwana Yesu alipoona kuwa anauhitaji UZIMA WA MILELE na si UZIMA TU!. Ndipo akamwambia “akauze kila kitu alichonacho kisha amfuate” kwa ufupi, ajikane nafsi yake ajitwike msalaba wake na kumfuata.
Lakini kwasababu yule mtu alikuwa anautaka Uzima na si Uzima wa milele, hakutaka kufanya vile, akaondoka!.. Na akaondoka akiwa na Uzima, na heri katika Maisha, lakini hana Uzima wa milele, jambo la kuhuzunisha sana.
Ndugu unayesoma ujumbe huu, maandiko yanasema kuwa Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele, habadiliki (kasome Waebrania 13:8), Maana yake ni kuwa vigezo vyake ni vile vile, kwa jinsi alivyomwambia huyu bwana, kwamba akauze vyote amfuate ndipo apate uzima wa milele, ndivyo anavyotuambia hata watu wa leo.
Sio kwamba huyu ndugu, alikuwa na bahati mbaya mpaka aambiwe vile na Bwana Yesu. Hapana!. Maneno hayo hayo aliwaambia pia wanafunzi wake kabla ya kumfuata..
Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Sasa kuacha vyote kunakozungumziwa hapo ni kukitoa kitu katika moyo wako moja kwa moja, kama ni mali, Rafiki, ndugu, au chochote kile, unakitoa moyoni mwako na kuwa tayari kuyafanya mapenzi ya Mungu..Kama kimeondoka kweli moyoni mwako, basi hata ukiwa nacho kimwili hakina madhara yoyote, kwasababu kiwepo au kisiwepo, hakikusumbui kwasababu huna muunganiko nacho kiroho.. Lakini kama umekiondoa kimwili lakini moyoni mwako bado kipo, bado utakuwa hujafanya chochote..
Hivyo hiyo ni kanuni KUU sana, ambayo sote tunapaswa tujifunze. Gharama za kuupata uzima wa milele si ndogo. Zinahitaji kujikana nafsi kweli kweli, na kubeba msalaba na kumfuata Yesu.
Hebu kwa kumalizia tuisome faida hiyo ya kujikana nafsi na kumfuata Yesu kwa kumalizia mistari ya chini..
Mathayo 19:22 “Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
25 Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?
26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.
27 Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.
Je! Umejikana nafsi na kumfuata Yesu? Au unajitumainia dini yako?, huyu kijana alikuwa na dini na ameshika amri zote lakini hakuwa na uzima wa milele ndani yake?, unadhani wewe na dhehebu lako utautolea wapi?..
Maadili yako yatakupa Uzima tu!, ni kweli utabarikiwa kwa kuishi vizuri duniani, kwa kuwa na moyo mzuri, lakini kama Yesu hajaingia ndani yako, huna uzima wa milele.
Ukitaka uzima wa milele weka dhehebu lako pembeni, weka dini yako pembeni, weka mali zako pembeni, weka uzuri wako pembeni, weka umaarufu wako pembeni, weka sifa zako pembeni, na kila kitu chako, weka kando nenda kama mshamba mbele zake Bwana Yesu, kama asiyejua chochote, kama mtu aliyezaliwa leo, kama vile kondoo aliyetayari kuchungwa…Bwana Yesu anataka moyo uliojiachia kwake, moyo wa unyenyekevu..hapo ndipo atakapokuonyesha njia na kukupa uzima wa milele?.
Kama hujaokoka basi hakikisha siku ya leo haipiti bila kuokoka, kwasababu hujui ni nini kitatokea kesho, tafuta mtu aliye mkristo, aombe Pamoja na wewe katika sala fupi ya kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, au wasaliana nasi kwa namba zilizopo chini ya somo, tutakusaidia kwa hilo.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
Ufunuo 19:11-13
[11]Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
[12]Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
[13]Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
Ulishawahi kujiuliza ni kwanini mahali hapo Yesu hajitambulishi kwa jina lake la asili tulilolizoea, bali anajiita Neno la Mungu,?.
Ipo maana kubwa sana nyuma yake ambayo wakristo wengi hatuijui.
Ni muhimu tufahamu kuwa pale Tunapomtaja YESU, tunamlenga Yesu wa pande mbili.
Wakristo wengi tunaishia kumtambua Yesu kama mtu, jinsi alivyokuwa na mamlaka, na uweza, na maajabu, jinsi alivyosulubiwa na kuzikwa na kufufuka na kupaa juu, na sasa hivi anatawala na kumiliki viumbe vyote vya mbinguni na vya duniani ..jambo ambalo ni zuri sana, kwasababu kwa kumtambua hivyo ndivyo tunavyomwamini na kupokea wokovu na kuponywa shida zetu.
Lakini kosa ni pale tunapoishia kumtambia Yesu-mtu tu, hatutaki kumtambua Yesu kama Yesu-Neno.
Utajiuliza huyu YESU-NENO ni yupi?
Ni Yesu katika maneno yake aliyokuwa anayafundisha. Leo hii ukiweza kuyaishi maneno hayo kikamilifu 100%, basi na wewe unabadilika na kuwa Yesu, mwenyewe.
Kiasi kwamba, wakati mwingine hutahitaji Yesu aje kukusaidia, bali wewe mwenyewe utaweza kufanya, kila kitu.
Wakristo wengi tunampenda Yesu tunapomsoma au kumsikia, lakini hatutaki kuwa kama yeye. Kwasababu tunaona ugumu kuyaishi maneno yake.
Tunafanana na mwanafunzi anayetegemea tu kikokoteo (calculator) kupigia mahesabu yake, lakini kichwani asiwe na maarifa yoyote ya kinachofanyika nyuma ya kikokoteo kile
lakini mtu ambaye anajua kanuni ya kikokoteo, huyo huwa anakuwa ni bora zaidi..kwasababu hata pasipo kuwa nacho anaweza tu kupiga mahesabu yake na kupata majibu. Atakihitaji kwa kurahisisha tu kazi zake, lakini pasipo hicho bado anaweza kufanya.
Lakini hiyo itamgharimu aende shule, ajifunze misingi yote ya hisabati..tofauti na yule mwingine ambaye kazi yake ni kubofya tu. “Jibu hilo hapo!”
Ndivyo ilivyo kwa wakristo wanaomtegemea Yesu-mtu tu, na sio Yesu-Neno. Wanamgeuza Bwana Yesu kama calculator wanamwita awasaidie, lakini hawataki kuyaishi maneno yake..
Sio kila wakati tutamwitaji Yesu atusaidie, wakati mwingine anataka sisi wenyewe tufanye, ndivyo alivyowazoeza pia mitume wake ambao hapo mwanzo walizoelea kumtegemea tu yeye ilihali hawazingatii maneno yake
Mathayo 17:17
[17]Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu.
Wakati mwingine tunamwita Yesu, atusaidie, na anakaa kimya hafanyi chochote..tunaita usiku kucha hajibu lolote. Ni kwasababu gani? Ni kwasababu hatutaki kuliishi Neno lake.
Kwamfano: mmoja anaweza akawa anafunga na kukesha kumlilia Yesu ampe mali (kwasababu anamjua Yesu-mtu anaweza yote)..lakini huku anaendelea na mambo yake ya kidunia.. Na mwingine akalizingatia lile Neno la Yesu linalosema;
Mathayo 6:32-33
[32]Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
[33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
Huyu wa pili, anaweza asimtaje Yesu wala mali mahali popote, lakini akapokea hitaji lake, kwasababu tu kajua kanuni ya roho.. Lakini yule wa kwanza kupewa/kutokupewa ni juu ya Yesu mwenyewe..sio juu yake.
Hivyo tujifunze kuyaishi maneno ya Yesu, kwamfano tunapoambiwa tusamehe huyo ndio Yesu-Neno., tunapoambiwa tusizini ndiye Yesu Neno.
Na Yesu mwenyewe alitusisitizia kwamba maneno yake yakiwa ndani yetu, basi tukiomba lolote yeye atatupa.
Yohana 15:7
[7]Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
“Yodi” ni nini kama tunavyoisoma katika Mathayo 5:18?
BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.
UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?
HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.
Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?.
Wapo wanatofautisha maneno haya mawili, na wapo wanayoyaona kama ni kitu kimoja..
Ni kweli Bwana Yesu alituonyesha kuwa “maandiko na Neno” la Mungu ni kitu kilekile kimoja, na ndivyo ilivyo..
Soma Yohana 10:35
Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);
Isipokuwa tofauti yao ndogo ni kwamba maandiko yanajifunga tu katika maandishi.. lakini Neno la Mungu, ni aidha katika maandishi au kuzungumzwa.
Bwana anaweza kutoa ujumbe wake kwa sauti kinabii, vilevile anaweza kuzungumza kwa biblia (maandiko). Na zote zikawa sauti zake zenye majibu.
Lakini tulichopewa, na tunapaswa tukitegemee sana ni Neno la Mungu katika maandiko, alisema, “maandiko hayawezi kutanguka”, yaani kilichoandikwa kimeandikwa. Lakini Neno lake katika sauti anaweza kulitangua mwenyewe, au akaghahiri, au likawa la muda tu, tofauti na Neno katika maandishi.
Hivyo ukiishi kwa hilo, utakuwa salama. Lakini tukiwa wavivu wa kujifunza biblia. Tuwe na uhakika kuwa tunapoteza maisha yetu.
Marko 12:24
[24]Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?
Tupende Biblia zaidi ya chakula, tuone kuwa hatuwezi kuishi bila hilo; Daudi alisema.
Zaburi 119:140
[140]Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.
Tuyapende maandiko, kwani ndio uhai wetu.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Yeshuruni ni nani katika biblia?
URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?
Jibu: Tuisome Habari nyenyewe…
Yohana 8:3 “Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.
4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.
5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?
6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, AKAANDIKA KWA KIDOLE CHAKE KATIKA NCHI.
7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.
8 Akainama tena, AKAANDIKA KWA KIDOLE CHAKE KATIKA NCHI.
9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.
10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?
11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]”.
Katika tukio hilo maandiko, hayajasema wala kutaja ni kitu gani Bwana Yesu alichokuwa anakiandika ardhini, ikifunua kuwa SIO KITU CHA MUHIMU SANA SISI KUKIJUA, maana ingekuwa ni cha muhimu sana kukijua basi Mtume Yohana asingeacha kukiandika kwa faida yake na yetu pia, au Marko au Mathayo, wangeviandika… Lakini hakikuwa kitu cha muhimu sana kwetu kukijua…Ni sawa tutafute ni aina gani ya udongo, Bwana aliyoitengenezea tope, kwaajili ya kumponya yule kipofu.
Yohana 9:6 “Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho”.
Unaona?..kujua ni aina gani ya udongo iliyotumika hapo kutengenezea tope, haitusaidii sana, vile vile kujua ni aina gani ya Mti ulitumika kumsulubisha Bwana pale msalabani, pia haitusaidii chochote, kwamba tujue ule mti ulikuwa ni Mkoko, au Mtini, au Mpingo, au Mwerezi au Mwaloni haitusaidii chochote kiroho.. Ndio maana maandiko hayaeleza aina ya mti huo.
Vile vile ni maneno gani Bwana Yesu aliyokuwa anayaandika ardhini sio jambo la muhimu kulijua.. Wengi wanasema Bwana Yesu alikuwa anaandika dhambi za wale Mafarisayo na Masadukayo ardhini, kufuatia andiko la Yeremia 17:13..
Yeremia 17:13 “Ee Bwana, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. WAO WATAKAOJITENGA NAMI WATAANDIKWA KATIKA MCHANGA, kwa sababu wamemwacha Bwana, kisima cha maji yaliyo hai”.
Lakini bado hoja hii haina nguvu, kwasababu Bwana Yesu angekuwa kutwa kuchwa anashinda kuandika tu dhambi za watu mchangani, kwasababu waliokuwa wanamkataa ni wengi.
Hivyo alichokuwa anakiandika sio cha Muhimu kukifaham, lakini kilicho cha muhimu kujua ni KWANINI ALIKUWA ANAANDIKA ARDHINI, WAKATI WATU WANAMWONGELESHWA!. Hicho ndio cha muhimu kujua..
Sababu kuu ya Bwana Yesu kushuka na kuanza kuandika chini, ilikuwa ni kwa “LENGO LA KUWAPA NAFASI YA KUJITAFAKARI na YA KUCHUKUA MAAMUZI THABITI”.
Ili tuelewe vizuri, tuutafakari huu mfano mrahisi.
“Mtu Fulani unayemjua amekuja kwako kukuuliza swali la mtego, au swali ambalo anayo majibu yake..na wewe ukajua anayo majibu yake…Hivyo ukaamua kukaa kimya, usimjibu swali lile, huku ukianza kuchezea chezea shilingi iliyopo mezani, pako mbele yako, au ukaendelea kuchezea simu…Na baadaye akazidi kukuhimiza umjibu… wewe ukamjibu, jibu fupi, la kumtafakarisha..na baada ya kumjibu ukaendelea kuchezea chezea ile shilingi iliyopo mezani au ukaendelea kuchezea simu yako”.
Je kwa tukio hilo kuna lolote la kujifunza katika hiyo shilingi au hiyo simu?.. kwamba tuanze kutafuta kujua ni shilingi ngapi uliyokuwa unaichezea, au ni mizunguko mingapi uliyokuwa unaizungusha au tuanze kutafuta kujua ni nini ulikuwa unakitazama kwenye simu wakati unaongeleshwa?.
Jibu ni la!.. wewe ulikuwa unarusha rusha ile shilingi, au unachezea simu ile kwa lengo la kumpa yule mtu nafasi ya kujitafakari swali alilouliza, hali kadhalika baada ya kumjibu kwa ufupi na kuendelea kuchezea simu yako ni ili kumpa nafasi ya nafasi ya kuondoka, na kutafakari ulichomwambia.. asiendelee kukuuliza maswali ambayo anayo majibu yake. (Na kwa njama hiyo fupi, basi utafanikiwa kumwondoa huyo mtu mbele yako, bila kutumia nguvu nyingi).
Ndicho Bwana Yesu alichowafanyia Mafarisayo, lengo lake ni kuwapa muda wa kujitafakari na kuacha kuuliza maswali ambayo wanayo majibu yake, na vile vile kuondoka pale. Lakini si kuandika dhambi zao ardhini.
Hivyo hiyo ni Hekima Bwana aliyoitumia kufupisha majadiliano marefu, na hoja zisizokuwa na Msingi.
Na sisi tunachoweza kujifunza hapo ni kuwa, sio kila hoja ni za kushiriki, nyingine ni kuzikatisha kwa Hekima.. Si kila swali ni la kujibu kwa urefu, na si kila mazungumzo ni ya kuyakumbatia kwa muda mrefu. Mazungumzo ambayo ni ya mashindano ya dini, hayo Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho alimwonya Timotheo na makanisa yote Kristo, kwamba wajiepushe nayo..
1Timotheo 6:20 “Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo”
2Timotheo 2:14 “Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao”
Bwana Yesu alipopelekwa mbele ya Makuhani na mbele ya Pilato, hakuwa mtu wa maneno mengi, mara zote alipoulizwa maswali ambayo hayana maana yoyote alikaa kimya!!..
Marko 15:4 “Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.
4 Pilato akamwuliza tena akisema, HUJIBU NENO? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!
5 Wala Yesu HAKUJIBU NENO TENA, hata Pilato akastaajabu”.
Nasi pia pia hatuna budi kuwa watu wa maneno machache na watu wa kujiepusha na mashindano, ya dini.. Umeona, kwa matendo hayo mawili tu ya Bwana kuacha kuwazungumza na wale mafarisayo na kuendelea kuandika chini, ilitosha kuwaondoa Mafarisayo wale, Zaidi hata angetumia maneno mengi, lakini kwa maneno yale machache na tendo lile moja, alivifunga vyinywa vyao.
Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?
Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?