Shalom
Hii ni sehemu ya pili ya maswali na majibu yahusuyo ndoa.. Sehemu ya Kwanza unaweza kuisoma kupitia link hii >> MASWALI-NDOA
SWALI 01: Je Mkristo anaruhusiwa kuoa mtu wa Imani nyingine? Yaani akafunga naye ndoa tu, na kila mmoja akaendelea na imani yake.
Jibu: Ndoa ya kikristo ni ndio inayohusisha Imani moja, Bwana mmoja, Roho mmoja, tumaini moja, Ubatizo mmoja na Mungu mmoja..
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. 5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. 6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”
Kwahiyo kabla ya Ndoa ni lazima wawili hao wafikie kuwa na imani moja, na ubatizo mmoja na Roho Mmoja na Mungu mmoja, wasipofikia huo umoja basi hiyo sio ndoa ya kikristo.
Sasa nini cha kufanya endapo ikitokea mmoja si wa imani ya kikristo?, Jibu: Huyo ambaye tayari kashaokoka anapaswa amhubirie mwenzake habari za Wokovu kwanza, na aamini na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu (kwaufupi awe mkristo aliyesimama kweli kweli) na baada ya hapo ndipo wafunge ndoa, lakini kumbuka, si abadilike kwasababu tu anataka kuoa au kuolewa!, hapana bali anapaswa apate badiliko la kweli kiasi kwamba hata kama asipoolewa na huyo basi bado Kristo atabaki kuwa Mwokozi wake siku zote za maisha yake.
SWALI 02: Je kuna umuhimu wowote wa kupima afya kabla ya kufunga Ndoa?
Jibu: Ndio upo umuhimu wa kufanya hivyo kama kuna huo ulazima. Kuhakikisha afya zenu zipo sawa kabla ya kufanya lolote, maandiko hayajakataza kufanya hivyo. Na endapo ikitokea mmoja kakutwa na maradhi ambayo yatawafanya wawili hao wasiweze kukutana kimwili!.. Basi hapo ni uchaguzi wa Yule aliye salama, kama upendo wake ni mwingi kama ule wa Kristo, anaweza kuishi na huyo anayemchagua, lakini kamba si hawezi basi yupo huru kutafuta mwingine aliye chaguo lake hafanyi dhambi.
Lakini kama tayari wameshafunga ndoa na mmoja akapata maambukizi ya maradhi hayo basi Yule aliye salama hapaswi kumwacha huyo aliye na maradhi, wataendelea kubaki pamoja siku zote. Vile vile kama mmojawapo kapata ulemavu ambao utamfanya asiweze kabisa kukutana na mwenzake basi Yule aliye mzima pia hapaswi kumwacha mwenzake aliye na udhaifu, siku zote za maisha yake.
SWALI 03: Je wakristo wanaruhusiwa kutoa Ujauzito (Mimba)?
Jibu: Mkristo haruhusiwi kutoa ujauzito (mimba), kwasababu yoyote ile isipokuwa ya kiafya kwa maelezo ya madaktari:
Kwamfano Ikitokea mtoto kafia tumboni hapo ni lazima ile mimba changa iondolewe ili kuokoa maisha ya mama, vile vile ikitokea itilafu katika tumbo la mama, ambayo ili mama awe salama (asipoteze maisha) na kama mama huyo hana imani ya kutosha ya kuamini kuwa anaweza kuishi bila kuitoa na akawa salama, na hivyo akakubali itolewe kufuatia maelezo hayo ya daktari, mama huyo hafanyi dhambi!, kwasababu ya usalama wake mwenyewe.
Lakini sababu nyingine yoyote ya kutoa mimba tofauti na hiyo ya kiafya, ni dhambi!..Kwamfano mwanamke kapata ujauzito bahati mbaya na alikuwa hana mpango wa kuipata hiyo, hapo hapaswi kuutoa huo ujauzito, au kapata ujauzito kwa njia ya ukahaba, hapo hapaswi kuitoa hiyo mimba, atabaki nao mpaka hatua ya kujifungua.
SWALI 04: Ni nani mtu sahihi wa kumpelekea matatizo ya ndoa? Endapo kukitokea kutokuelewana?
Jibu: Endapo kukitokea kutoelewana, ni vizuri kuomba kwa Bwana suluhisho na kurejea biblia kujua ni nini biblia inasema kuhusu hali hiyo, lakini kama bado mwanandoa anahisi anahitaji msaada zaidi basi anapaswa ayafuate makundi yafuatayo.
1: MCHUNGAJI WA KWELI WA BWANA:
Si wachungaji wote ni waaminifu, lakini pia wapo walio wa kweli na waaminifu, watu hao ni kituo bora cha kupata ushauri wa kiMungu na maombezi.
2. MZAZI:
Kama unaye mzazi aliyeokoka basi hicho pia ni kituo bora sana cha kupokea mashauri bora..na yenye msingi mkubwa.
Kamwe usitafute ushauri kwa marafiki, majirani, ndugu wa mbali, au watu usiowajua kuhusiana na mambo ya kindoa.
SWALI 05: Endapo nikagundua baada ya kufunga ndoa Mwenzangu ana matatizo katika uzazi wake (hana uwezo wa kuzaa au kuzalisha)..Je naweza kwenda kupata mtoto nje na kuendelea kuwa naye?
Jibu: Kama mwanandoa mmoja anamatatizo ya uzazi yanayomfanya asiweze kuwa na mtoto, hapo mwanandoa mwingine asiyekuwa na matatizo hayo hapaswi kumwacha Yule mwenye matatizo, wala kuondoka na kwenda kupata mtoto wa kando, atabaki naye huyo huyo siku zote za maisha yake, huku wakimwomba Bwana awafungue!.
Na kama ni mapenzi ya Bwana wao kuwa na watoto, basi Bwana atawapa mtoto haijalishi ni miaka mingapi itapita (Ibrahimu na Sara walipata watoto katika uzee), na Mungu ni Yule Yule hajabadilika.
Lakini pia kama wanaona ahadi za Mungu bado zipo mbali wanaweza ku-adopt mtoto/watoto na kuwalea kama watoto wao.. Vipo vichanga vingi visivyo na wazazi, na mtu akiwalea hao mbele za Mungu ni zaidi hata ya Yule mwenye watoto 100 waliotoka katika uzazi wake.
SWALI 06: Je mkristo anaruhusiwa kupanga uzazi?
Jibu: Ndio wakristo wanaweza kupanga idadi ya watoto wanaotaka kuwa nao!. Biblia haijatoa amri ya kuzaa idadi ya watoto 10 au 50, ni kila mtu atakavyotaka yeye. Lakini imetoa tu angalizo kuwa tuwe watu wenye uwezo wa kuwatunza wakwetu (1Timotheo 5:8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.)
Kwahiyo ni lazima Mkristo awe na uwezo wa kuwatunza watoto wake, hivyo ni lazima awe na uzazi wa mpango.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA-1
MAFUNDISHO YA NDOA.
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?
Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue? Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI 01: Je wakristo tunaruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja?
Jibu: Kwa mujibu wa biblia, Ndoa ya kikristo ni ya mke mmoja na mume mmoja.
Marko 10:6 “Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja”.
SWALI 02: Je kama mtu alifunga ndoa ya kiserikali, au kimila ndoa hiyo inatambulika mbinguni?..Yaani Mungu anawatambua kama ni mume na mke kihalali?.
Jibu: Ndio! Mbinguni watu hao wanatambulika kama ni mke na mume, ingawa ndoa yao haitakuwa ndoa takatifu ya kikristo..maana yake kuna mambo hawataweza kuyafanya wakiwa katika hiyo hali, mfano wa mambo hayo ni Uchungaji wa kundi, au Uaskofu au Ushemasi. Kwasababu nafasi hizo ni za kuhubiria wengine njia sahihi, hivyo haiwezekani mtu awahubirie wengine wafunge ndoa takatifu ya kikristo wakati yeye mwenyewe hayupo katika ndoa kama hiyo. (Atakuwa mnafiki).(Tito 1:6-7).
Hivyo ni sharti aibariki ndoa yake hiyo na kuwa ndoa takatifu ya kikristo ili asifungwe na baadhi ya mambo.
Mfano wa ndio hizi ambazo ni za kipagani lakini Mungu alikuwa anazitazama ni kama ile ya Herode ambayo Yohana mbatizaji aliikemea.
Marko 6:17 “Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;
18 kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo”.
Herode hakuwa mkristo lakini alipomwacha tu mke wake na kwenda kumchukua wa ndugu yake ikawa ni chukizo mbele za Bwana, na vivyo hivyo ndio zote zilizofungwa ambazo zimehusisha mahari pamoja na makubaliano pande zote, basi ndio hizo Mungu anazitazama na zinapaswa pia ziheshimiwe.
SWALI 03: Je Wakristo tunaruhusiwa kutoa talaka?
Jibu: Wakristo hawaruhusiwi kuachana baada ya kuoana. Kwahiyo talaka hairuhusiwi katika ndoa ya kikristo wala mwanaume haruhusiwi kumwacha mke wake katika hali yoyote ile ya udhaifu wa kimwili.
Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”
SWALI 04: Je! Kama Mwanamke alikuwa ameolewa na mwanaume ambaye tayari alikuwa na Mke, je anapookoka anapaswa amwache huyo mume wake au aendelee naye?.
Jibu: Kulingana na maandiko anapaswa amwache kwasababu tayari huyo alikuwa ni mume wa mtu, hivyo ili maisha yake yawe na ushuhuda na aishi kulingana na Neno ni lazima amwache huyo na akaolewe na mwanaume mwingine ambaye hajaoa (lakini katika Bwana tu), au akae kama alivyo.
SWALI 05: Kama mwanaume alikuwa ameoa wanawake wawili na kashaishi nao muda mrefu na kuzaa nao watoto, lakini ukafika wakati akaokoka je anapaswa amwache mmoja na kuendelea na mwingine au?
Jibu: Kama mwanaume alikuwa amemwoa mwanamke wa kwanza katika ndoa ya kikristo (yaani iliyofungishwa kanisani), na baada ya ndoa hiyo akaongeza mwingine wa pili…Na baadaye akatubu na kuokoka upya!. Hapo hana budi kumwacha huyo wa pili kwasababu alikuwa anafanya uzinzi kulingana na biblia, haijalishi ameishi na huyo mwanamke kwa miaka mingapi, na amepata naye watoto wangapi..anapaswa amwache na kubaki na mke wake wa kwanza.
Lakini kama alimwoa mke wa kwanza kipagani na kulingana na sheria za kipagani akaongeza wa pili, na akaishi nao muda mrefu na wanawake hao wote wawili bado wanahitaji kukaa naye, hapaswi kuwaacha labda mmoja wapo wa wanawake hao aridhie mwenyewe kumwacha kwa hiari yake..
Lakini kama ataendelea kubaki nao mtu huyo ndoa yake hiyo ya wake wawili haitawezi kubarikiwa kanisani, na pia yeye mwenyewe hataweza kuwa Mchungaji, askofu au Mwinjilisti au shemasi bali atakuwa muumini wa kawaida tu, kwasababu biblia inasema ni lazima Askofu awe mume wa mke mmoja..
Tito 1:6 “ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu; asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu”.
SWALI 06: Je?.Kujifungua kwa operation au kuzalishwa na wakunga wakiume ni halali kwa mwanandoa wa kikristo?.
Jibu: Operesheni ni njia mbadala ya kukiondoa kiumbe tumboni ili kusalimisha maisha ya mama na mtoto..Hivyo kibibla sio dhambi, kwasababu lengo lake ni kuokoa maisha na si lengo lingine.
Vile vile kuzalishwa na mkunga wa jinsia ya kiume si dhambi, kwasababu lengo ni lile lile kusaidia kuokoa maisha,..Katika eneo la uokozi ni eneo ambalo haliangalii jinsia..
Kwasababu pia zipo operesheni kubwa zaidi hata za kuzalisha ambazo zinahusisha kuondoa au kurekebusha viungo vya ndani kabisa vya uzazi wa mwanamke au mwanaume, ambazo operesheni hizo madaktari wake bingwa wanakuwa ni wa jinsia tofauti na wanaofanyiwa, hivyo hapo kama mtu anataka kupona kwa njia hiyo ya matibabu basi hana uchaguzi, wa atakayemfanyia hiyo operesheni.
Kwahiyo katika mazingira kama hayo, jinsia yoyote itakayotumika kumfanyia matibabu huyo mgonjwa wa kikristo, itakuwa si dhambi kwa mkristo huyo anauefanyiwa hiyo operesheni wala kwa yule anayemfanyia.
Shalom.
Usikose sehemu ya pili…
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
Maswali ya hivi karibuni ni ya kwanza katika orodha, ili kusoma bofya somo husika uingie.Pia ukiwa na maswali/ unahitaji maombezi/ piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312
Unaweza pia kuyapata mafundisho yetu ya kila siku Whatsapp. Jiunge kwa kubofya hapa chini>
Utapata Majibu ya Maswali mengi kupitia page hii. Karibu sana!
1. Kuota Mtu aliyekufa maana yake nini
2. Je apandacho mtu ndicho atakachovuna?
3. Je Kuota unakimbizwa ina maana gani?
4. Je Kuota unafanya mtihani kuna maanisha nini?
5. Kuota Nyoka maana yake nini?
6. Kuota Unasafiri maana yake nini?
7. Kuona una mimba maana yake nini?
8. Nini maana ya Asiyefanya kazi na asile?
9. Namna bora ya kuomba ni ipi?
10. Mtakatifu ni nani?
11. Mtume Paulo alioa?
12. Je Wakatoliki wanaabudu sanamu?
13. Kwanini Wakristo wengi ni maskini?
14. Kuota unapewa Pesa maana yake ni nini?
15. Je! Mungu anaweza kumsahau mtu?
16. Kuota Umebeba Mtoto maana yake nini?
[faqs]
DOWNLOAD PDF
WhatsApp
Swali 1: Ni nani aliyemshawishi Daudi kuwahesabu Israeli ni Mungu au shetani?..Maana 2Samweli 24:1 inasema ni Mungu lakini 1Nyakati 21:1 inasema ni shetani.
Jibu: Ni shetani ndiye aliyemshawishi Daudi kwa ruhusa ya Mungu. Ayubu alijaribiwa na shetani kwa ruksa maalumu kutoka kwa Mungu. Hivyo ni sawa na kusema Mungu ndiye alimjaribu Ayubu..ni hivyo hivyo kwa Daudi pia.
Swali 02: Mungu anadanganya?maana Ezekieli 14:9 inasema anadanganya.
Jibu: Mungu hadanganyi shetani ndiye anayedanganya, mtu mwovu anapoikataa njia ya haki, Mungu anaweza kuruhusu shetani amwingie na kumdanganya, hivyo inaweza kutafsirika kwamba kadanganywa na Mungu lakini si Mungu bali ni shetani (Soma 1Wafalme 22:20-23).
Swali 03: Nabii aliyetabiriwa na Musa kuwa atatokea si Yesu bali ni nabii mwingine kutoka Arabia, Mohamedi (Kumbukumbu 18:15).
Jibu:
Kumbukumbu la Torati 18:15 “BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”
Musa alikuwa mwisraeli na si Mwarabu kutoka Saudi Arabia, na ndugu zake hawakuwa waarabu bali wayahudi..Na Mohamedi hakuwa Mwisraeli bali Mwarabu.
Lakini Bwana Yesu alikuwa Myahudi na alizaliwa Israeli. Na zaidi ya yote alifanya miujiza zaidi haya ya Musa. Kwahiyo Bwana Yesu ndiye aliyetabiriwa pale na yeye ndiye Mwanzo na Mwisho hakuna mwingine. (Matendo 7:37).
Swali 04: Biblia inasema tukifika peponi tutapewa wake mara 100 ya tulionao sasa, mabikira.(Marko 10:30). Kwanini mnasema hakuna kuoa peponi?
Marko 10:28 “Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe. 29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili, 30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”
Marko 10:28 “Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”
Ndugu wake na ndugu waume, sio wake au waume au wachumba, bali ni ndugu wenye jinsia za kiume na za kike, na zaidi ya yote thawabu hizo ni katika ulimwengu huu huu, na sio peponi. Mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa.(Marko 12:25)
Swali 05: Yesu alisema “kila mtu atabeba msalaba wake” iweje yeye achukue dhambi za wengine?
Jibu: Alisema “Mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake anifuate”. Marko 8:34.
Kinyozi akikwambia “ukitaka kuja kwangu kunyoa beba viwembe vyako unifuate na pia uwe tayari kupata maumivu endapo ikitokea hitilafu”.. Je! Kwa kusema hivyo atakuwa amekataa kuchukua mzigo wako wa kukunyoa?.
Na wokovu wa Yesu ni hivyo hivyo, ukitaka kupona, sharti ukubali gharama za wokovu. Ukikwepa gharama utakufa na dhambi zako.(Yohana 8:24).
Swali 06: Paulo kamtabiri Mohamed kupaa mpaka mbingu ya tatu 2Wakorintho 12:2, Mohamed ndiye pekee aliyefika mbingu ya tatu, Yesu hakufika huko.
Jibu: Si Mohamed aliyenyakuliwa mpaka mbingu ya tatu bali ni Paulo mwenyewe. Na Paulo aliishia hiyo mbingu ya tatu tu! Na si zaidi, lakini Bwana Yesu alifika mpaka mbingu za mbingu..ambazo hakuna aliyefika hata mmoja.
Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.
Waefeso 1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa…”
Waefeso 1:20 “aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa…”
Swali 07: Je Bwana Yesu alikuwa ni Mungu au Mwanadamu? Maana biblia inasema alikuwa ni mtu! (Matendo 2:23)
Jibu: Bwana Yesu alikuwa ni Mungu kamili katika mwili wa kibinadamu, kutimiza kusudi Fulani maalumu,
Ukivaa vazi la kiaskari na kwenda kutimiza majukumu yako ya kiaskari, utaitwa askari na vile vile utafungwa na sheria za kiaskari, lakini hiyo haikufanyi wewe usiendelee kuwa mkurugenzi katika kampuni lako uliloliacha huko nyumbani, Au haikufanyi wewe usiendelee kuwa kiongozi katika Mtaa wako au mji wako.
Na Mungu alipouvaa mwili wa kibinadamu ulioitwa Yesu, ilikuwa ni lazima aitwe mtu! kwa kitambo lakini hiyo bado bado haimfanyi asiendelee kuwa Mungu.
Tito 2:13 ”tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”
FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.
KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?
Ni yupi aliyekuwa mkwe wa Musa kati ya Reueli na Yethro?
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?
Rudi Nyumbani
Manabii Wanaume katika biblia walikuwa wengi kiidadi kuliko manabii wanawake.
UFUATAO NI UFUPISHO KWA NJIA YA JEDWALI:
Kutazama Jadwali zima, basi Slide kuelekea upande wa kushoto.
Mbali na hawa walioorodheshwa katika Jedwali hilo hapo juu, walikuwepo pia Manabii wengine ambao hawakuonekana wakitajwa katika kutoa Nabii za Nchi au Taifa.. Mfano wa hao tunawaona katika Jedwali lifuatalo.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
MAJINA YA MANABII WANAWAKE
MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU
WAFALME NA MALKIA WALIOTAWALA YUDA
WAFALME WALIOTAWALA ISRAELI.
Orodha ya Manabii wa kike katika biblia.
Jumla ya Manabii wa kike (wanawake) waliotajwa katika biblia ni 11, Kati ya hao manabii Tisa (9) walikuwa wa KWELI na Wawili (2) walikuwa wa UONGO.
LIFUATALO NI JEDWALI LA UFUPISHO..
Kulitazama jedwali zima, basi ‘SLIDE’ kuelekea kushoto.
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Mitume wa BWANA YESU walikuwa 12, ambapo baadaye walisalia 11 baada ya YUDA ISKARIOTE, aliyemsaliti BWANA kufa kwa kujinyonga!.. Nafasi yake ilichukuliwa na MATHIYA, na hivyo kukamilisha idadi ya Mitume 12
IFUATAZO NI TAKWIMU YA MITUME WA BWANA.
Kutazama column za ziada slide jedwali lifuatalo kuelekea upande wa kushoto.
Swali: Je wale waliowekewa tayari ni akina nani na kwanini Bwana Yesu aseme maneno yale?
Jibu: Tuanzie kusoma mstari wa 20..
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno. 21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako. 22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza. 23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, SINA AMRI KUWAPA, BALI WATAPEWA WALIOWEKEWA TAYARI NA BABA YANGU”.
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, SINA AMRI KUWAPA, BALI WATAPEWA WALIOWEKEWA TAYARI NA BABA YANGU”.
Ili tuelewe vizuri, hebu tafakari mfano huu.. “wanafunzi wawili wamemfuata mwalimu wao wa darasa na kumwomba washike nafasi ya kwanza kitaifa na mwingine ashike ya pili kitaifa katika mitihani yao ya mwisho wa kuhitimu”.. Unadhani jibu la mwalimu litakuwa ni lipi?..
Bila shaka mwalimu atawauliza.. je! Mtaweza kusoma kwa bidii??.. Na kama wale wanafunzi watajibu NDIO!.. Bado Mwalimu hataweza kuwapa hizo nafasi, bali atawaambia mimi sina mamlaka ya kuwapa bali “Wasahishaji watakaosahisha mitihani ya wote ndio watakaotoa majibu ya mitihani yenu na kuwapanga kama mmestahili hizo nafasi au la”..
Ndicho Bwana YESU alichowaambia hawa wana wa Zebedayo!.. ambao walienda kumwomba nafasi ya kuketi pamoja naye katika kiti chake.. na jibu la Bwana YESU likawa, ni “kukinywea kikombe”.. maana yake kukubali mateso kwaajili yake!.. Na wao wakajibu “wataweza”.. Lakini jibu la Bwana likawa “Nafasi hizo watapewa waliowekewa tayari”..maana yake waliostahili.
Na hao waliostahili ni akina nani?
Ni wale watakaofanya vizuri Zaidi ya wengine wote katika mambo yafuatayo.
1. KUKINYWEA KIKOMBE.
Kikombe alichokinywea Bwana Yesu ni kile cha Mateso ya msalabani (Soma Mathayo 26:39), kutemewa mate, kupigwa Makonde, kuvikwa taji ya miiba, na kugongomelewa misumari mikononi..
Na yeyote ambaye atakubali kuteswa kwaajili ya Kristo, na si kwaajili ya mtu au kitu kingine chochote, basi yupo katika daraja zuri la kumkaribia Kristo katika siku ile kuu.
2. KUBATIZWA UBATIZO WA BWANA YESU.
Marko 10:38 “Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au KUBATIZWA UBATIZO NIBATIZWAO MIMI?”
Swali Ubatizo aliobatizwa Bwana YESU KRISTO ni upi?…. si mwingine Zaidi ya ule wa kufa, kuzikwa na siku ya tatu kufufuka, na kupaa juu (soma Luka 12:50), Na ubatizo huu mpaka sasa hakuna rekodi ya wazi ya yoyote aliyeupitia..
Ubatizo tubatizwao sasa ni ule wa maji mengi, ambao ni ishara ya kufa na kufufuka na Kristo (Wakolosai 2:12), kwamba tunapozamishwa katika maji mengi na kuibuka juu, ni ishara ya kufa pamoja na Kristo na kufufuka pamoja naye… Lakini Ule hasa wa kufa na kufufuka na kupaa, hakuna rekodi ya wazi ya aliyeupitia.
Isipokuwa unawezekana ndio maana tunasoma katika Ufunuo 11, kuwa wale washahidi wawili, ni miongoni mwa watakaoupitia..
Ufunuo 11:10 “….Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi. 11 NA BAADA YA SIKU HIZO TATU U NUSU, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama. 12 WAKASIKIA SAUTI KUU KUTOKA MBINGUNI IKIWAAMBIA, PANDENI HATA HUKU. WAKAPANDA MBINGUNI KATIKA WINGU, ADUI ZAO WAKIWATAZAMA”.
Ufunuo 11:10 “….Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi.
11 NA BAADA YA SIKU HIZO TATU U NUSU, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama.
12 WAKASIKIA SAUTI KUU KUTOKA MBINGUNI IKIWAAMBIA, PANDENI HATA HUKU. WAKAPANDA MBINGUNI KATIKA WINGU, ADUI ZAO WAKIWATAZAMA”.
Je umempokea YESU?, Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni.
Maran atha!
USIWE ADUI WA BWANA
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?
UWE KIKOMBE SAFI
Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?
Mtakatifu Rita, ambaye kwa kanisa katoliki anajulikana pia kama ‘mwombezi wa mambo yasiyowezekana’, na ‘mfanya miujiza’.
Ni mama aliyezaliwa mwaka 1381, katika mji unaitwa Kashia, taifa la Italy. Aliolewa akiwa na umri mdogo lakini baada ya mume wake na watoto wake wawili kufa aliamua kujiunga na utawa, ijapokuwa alipitia changamoto, kujiunga na jamii hiyo kwasababu tayari alikuwa ameshaolewa(sio bikira), lakini mwishoni alifanikiwa.
kulingana na kanisa katoliki maombi ya Rita yaliwaletea wengi majibu, lakini pia alitambulika kwa jeraha dogo kwenye kipaji cha uso wake, wakiamini kuwa ni alama ya ukristo, kufuatana na mateso ya Yesu msalabani, mahali alipowekewa taji ya miiba. Alikufa kati ya umri wa miaka 75-76.
Na ilipofika tarehe 24 May 1900, papa Leo XIII, Alimtangaza kuwa mtakatifu. Yaani ukitangazwa kuwa mtakatifu, unakidhi vigezo vya kuwa mwombezi wa walio hai.
Tangu huo wakati wakatoliki wengi dunia wamekuwa wakimfanyia novena, na litania. Na wengi wakishuhudia kuwa matatizo yao sugu, yakitatuliwa, hivyo imemfanya kuwa maarufu sana.
Lakini Je! Jambo hili ni kweli? Ni vema kufahamu kuwa katika maandiko matakatifu (BIBLIA), Hakuna mahali popote, tunafundishwa kuwa watakatifu waliokufa zamani au sasa wanaweza kutuombea. Zaidi sana wanakuwa hawaelewi neno lolote linaloendelea duniani, biblia inasema hivyo katika;
Mhubiri 9:5 kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.
Umeona? Kwahiyo desturi hii, ya kupeleka maombi yetu kwa watakatifu watuombee, ni ya kipagani, Ni ibada za sanamu, ambayo asili yake ilianzia kwenye dini zinazoamini mizimu inaweza kuwasiliana nasi. Kusema hivi haimaanishi tunawapinga wakatoliki, au tunatangaza chuki hapana, bali tunasemezana ukweli ili tupone, kwasababu safari yetu ni moja sote tuurithi uzima wa milele, sisi tunasema ni wakristo.
Haijalishi utakuwa ulifanya novena ya Rita ikakuletea majibu kiasi gani, bado ni ibada ya sanamu, kumbuka pia shetani analeta majibu, si ajabu mambo hayo kutendeka, ili watu wapumbazike katika hayo.
2Wakorintho 11:14 Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
Mwombezi wetu ni mmoja tu naye ndiye YESU KRISTO (1Yohana 2:1). Lakini sio pamoja na Petro, au Paulo, au Eliya, au Mariamu, au Yusufu. Hao wote ni watakatifu ambao walihitaji ukombozi tu kama sisi, na wenyewe walituelekeza kumtazama Yesu Kristo, na sio wao.
Mtume Paulo alisema maneno haya;
1Wakorintho 1:13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Hivyo hakuna haja ya kupeleka maombi yako kwa mtakatifu yoyote, na vilevile wale walio kule hawawezi kutuombea sisi pia. Halikadhalika wewe huwezi kumwombea mwenye dhambi aliyekufa, kwamba Bwana amtoe matesoni. Imani hiyo haipo pia katika biblia. Soma (Waebrania 9:27). Mafundisho ya watu kupitia toharani hayapo katika biblia.
Tujifunze kusoma biblia tutafunguka kwa mengi, mapokeo ya kidini sio Neno la Mungu. Hao wanaoabudu miti na mawe twaweza kuwacheka, lakini tukawa kama wale tu isipokuwa katika mfumo mwingine, tusipopenda kusoma biblia. Tukikataa kuwa wafuasi tu wa kidini tukapenda Neno la Mungu, Roho Mtakatifu atatusaidia kufunguka kwa mengi.
Hivyo ikiwa wewe ulikuwa ni mmojawapo wa wanaopeleka maombi kwa Rita wa kashia, au kwa mtakatifu mwingine yoyote acha sasa kufanya hivyo. Tubu dhambi ukabatizwe, upokee Roho Mtatakatifu ambaye atakuongoza na kukutia katika kweli yake yote(Yohana 16:13).
Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi waweza fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?
Roho Mtakatifu ni nani?.
LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?
KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
SISI TU MANUKATO YA KRISTO.
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.