Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)

JIBU: Shalom, utaona katika mstari huo anatumia neno “Tupa” na sio hifadhi au weka, ikiwa na maana ya kupoteza kitu chako cha thamani, chakula chako, na hapo anaendelea kusema kitupe usoni pa maji, ukisoma tafsiri nyingine utaona anasema kwenye habari, au maji mengi, na tunafahamu sikuzote ukitupa kitu mtoni au ziwani au baharini hapo ni kuhesabu kuwa umekipoteza hutakipata tena, sembuse chakula, ambacho kinayenyuka na kuoza haraka..

Lakini kinyume chake mhubiri anatuambia, “maana utakipata baada ya siku nyingi”..Ili kuelewa vizuri huo mstari tusome mistari inayofuata baada ya hiyo, 1 Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi.

(Mhubiri 11: 2 Uwagawie sehemu watu saba, hata wanane; Maana hujui baa gani litakalokuwa juu ya nchi.

Maji mengi kwenye biblia yanawakilisha “watu wengi au mataifa, au makutano (soma Ufun.17:15)”….Unaona, kumbe alimaanisha uwagawie watu sehemu ya fungu lako, bila kujali malipo au watakurudishia nini, unafanya kama unapoteza, Kwamfano unaweza ukawa unavi hazina kidogo kwenye mfuko wako na pengine anatokea mtoto wa ndugu yako anaomba msaada wa ada ya shule, huku mwingine anakuomba chakula, mwingine anakuomba nguo, mwingine anakuomba hifadhi, maadamu vipo ndani ya uwezo wako fanya kuwapa tu kama vile huna matumizi na hiyo fedha, kwasababu biblia inasema hujui mbeleni kutakuwaje, pengine huyo mtu unayemsaidia sasa anaweza akawa msaada mkubwa sana kwako au kwa watoto wako, au kwa ndugu zako.  

Tajiri mmoja wa kidunia ambaye leo hii anajulikana duniani kote anayeitwa Bill Gates, zamani alipokuwa kijana mdogo, alipenda kwenda kusoma magazeti, lakini kwa bahati mbaya alikuwa hana pesa ya kununa gazeti lakini mahali hapo kulikuwa na mzee mmoja mwafrika mweusi, alimnunuliza magazeti, hilo lilimwingia sana moyoni, miaka mingi ikapita akaanza kufanikiwa na kuwa tajiri sana kwa ugunduzi wake wa Microsoft, akakumbuka wema aliofanyiwa na huyo mzee, alingarimika kumtafuta popote alipo, alipomwona alimpatia kiasi cha dolla milioni moja, ambayo kwa pesa yetu ni zaidi ya sh. Bilioni 2,.Unaona gazeti la sh.1000, linakuja kumzaliwa Bilioni 2. Miaka mingi baadaye.  

Hivyo Mhubiri anatufundisha hekima ya maisha ya kawaida, kuna usemi unaosema “kinachokwenda nje ndicho kinachokurudia”, leo hii mtu ukiwa mbinafsi na kuwadharau wengine kwa mafanikio yako kidogo uliyopewa na Bwana, ziangalie pia siku za mbeleni kwa jinsi ya kibinadamu. Na ndio maana hapo anasema sehemu, uwagawie watu 7 hata nane,.Hii Ikimaanisha usichague aina Fulani tu ya watu, tupa kokote,poteza kokote utakuja kupata hicho ulichokipoteza baada muda Fulani, haijalishi itachukua miaka mingi, lakini mwisho wa siku utakipata tu. Hata chakula vyenye asili ya mbegu kama maharage au mahindi, ukivitupa mahali penye ardhi yenye asili ya maji maji baada ya muda Fulani vitakuja kukuwa na kuzaa, na hivyo kukipata kile ulichokipoteza na Zaidi.  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

JIRANI YAKO NI NANI?

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

WATU WASIOJIZUIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments