Hiana ni nini?

Hiana ni nini?

Neno “hiana” maana yake ni “usaliti” ule wa mapenzi. Endapo mtu mmoja akimwacha mke wake/mume wake na kwenda kufanya uzinzi , mtu huyo amefanya mambo ya hiana kwa mwenzake. Na Bwana anauchukia usaliti.

Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, ULIYEMTENDA MAMBO YA HIANA, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.

 15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake MAMBO YA HIANA.

  16 Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; BASI JIHADHARINI ROHO ZENU, MSIJE MKATENDA KWA HIANA”.

Lakini mbali na hilo, Watu wote waliokoka mbele za Kristo tunahesabika katika roho kama BIBI ARUSI.. na Kristo ndiye Bwana wetu (2Wakorintho 11:2).

Maana yake tunapoacha kufanya maagizo yake, kama  utakatifu, kuwa na upendo, kuwa watu wa msamaha, wasiolipiza visasi, wasio wazinzi, wezi, walevi, watukanaji, waabudu sanamu  n.k katika roho ni tumemsaliti (Yaani tumefanya mambo ya HIANA). Maana yake tunamtia wivu. Na siku zote kumbuka, Mungu aliposema yeye ni mwenye wivu, hakumaanisha wivu huu wa kawaida, labda mtu anapoona mwenzake kapata kitu Fulani ambacho yeye hanapa! Hakumaanisha huo..kwasababu ni heri ungekuwa huo!… bali wivu alioumaanisha ni a ule wivu wa mtu anapochukuliwa mke wake kipenzi!..Wivu ambao ni mbaya sana, ambao kwetu sisi wanadamu wengi unaishia aidha upande mmoja ufe, au pande zote zife!!..Ndio hapo utasikia aidha mtu kajinyonga..au kaua na yeye mwenyewe kajimaliza!..

Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”

Hiyo ndio maana Bwana Mungu alisema katika…

Kutoka 20: 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; KWA KUWA MIMI, BWANA, MUNGU WAKO, NI MUNGU MWENYE WIVU; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

Wakati Fulani Yuda, na Israeli walimwacha Bwana, na kufanya mambo maovu yasiyofaa ikiwemo kwenda kuabudu miungu mingine, na  Bwana akasema maneno haya juu yao…

Yeremia 3:6 “Tena, Bwana akaniambia siku za mfalme Yosia, Je! Umeyaona aliyotenda Israeli mwenye kuasi? Amepanda juu ya kila mlima mrefu, akafanya huko mambo ya ukahaba, tena, chini ya kila mti wenye majani mabichi.

7 Nami nalisema baada ya yeye kuyatenda hayo yote, Atanirudia mimi, lakini hakurudi; na dada yake, Yuda MWENYE HIANA, akayaona hayo.

8 Nami nikaona, wakati nilipokuwa nimemwacha Israeli mwenye kuasi, nikampa hati ya talaka kwa sababu hiyo ya kuzini, dada yake, Yuda mwenye hiana, hakufanya hofu; bali yeye naye akaenda akafanya MAMBO YA UKAHABA.

9 Hata ikawa, kwa sababu alikuwa mwepesi wa kufanya ukahaba, nchi ikatiwa unajisi, naye akazini na mawe na miti.

10 Na pamoja na hayo yote dada yake, Yuda mwenye hiana, hajanirudia mimi kwa moyo wake wote, bali kwa unafiki, asema Bwana.

 11 Bwana, akaniambia, Israeli mwenye kuasi amejionyesha kuwa mwenye haki kuliko Yuda mwenye hiana.

 12 Enenda, ukatangaze maneno haya kuelekea upande wa kaskazini, ukaseme, Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi, asema Bwana; sitakutazama kwa hasira; maana mimi ni mwenye rehema, asema Bwana, sitashika hasira hata milele.

13 Ungama uovu wako tu; ya kwamba umemwasi Bwana, Mungu wako, na njia zako zimekuwa nyingi kuwaendea wageni chini ya kila mti wenye majani mabichi, wala hamkuitii sauti yangu, asema Bwana.

14 Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; MAANA MIMI NI MUME WENU; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni”.

Je na wewe leo unafanya mambo ya Hiana kwa kuvaa mavazi yasiyofaa??, unavaa suruali, unapaka wanja, unapaka lipstick, unavaa hereni na kuweka wigi kichwani?..je unafanya mambo hayo ya hiana mbele za Mungu wako kwa kulewa na kufanya uasherati na anasa, je unafanya mambo ya hiana kwa kutazama picha za ngono mitandaoni, na kujichua?.. je umefanya mpira kuwa ndio Mungu wako na kuwa mshabiki wa mambo hayo?…Fahamu kuwa kwa matendo yako unamtia Mungu wivu. Na kuzivuta hasira za Mungu karibu nawe. Kumbuka mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu. Hivyo huwezi kuufanya kama unavyotaka wewe, na pia kumbuka tulinunuliwa kwa thamani kubwa, hivyo hatuwezi kuishi tu kama tunavyotaka sisi.

Soma mistari hii uone ni jinsi gani, mambo ya Hiana yanavyomchukiza Mungu wetu >>Yeremia 9:2, Yeremia 5:11, Hosea 6:7, 1Samweli 14:33.

Rudi leo! Kwa Bwana na kutubu!..choma hizo nguo zisizo za kiMungu unazozivaa, wala usimpe mtu!. Na mwombe Bwana akupe badiliko la kweli maishani mwako. Vunja hizo chupa za bia, na vikao vya ulevi na anasa, achana na huyo mvulana/au msichana mnayefanya uasherati sasa, achana na huyo mke/mume wa mtu unayeishi naye, au kutembea naye. Futa hiyo miziki yote ya kidunia katika simu yako. Ukifanya hivyo hiyo ndio TOBA!.. Kisha Bwana mwenyewe atakuongezea nguvu ya kuweza kushinda dhambi!..Lakini usipofanya hayo kwa vitendo, hakuna nguvu yoyote itakayoshuka juu yako.

Na pia kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na Bwana Yesu alisema itatufaidia nini tukiupata ulimwengu mzima halafu tupate hasara za nafsi zetu. Hivyo tafakari hilo siku zote, na ujue kuwa vitu vya ulimwengu huu havina umuhimu sana kama vinavyotukuzwa na watu.. Bwana Yesu anarudi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments