Fumo ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Hesabu 25:7)

Fumo ni nini kama tunavyosoma katika biblia? (Hesabu 25:7)

Fumo ni mkuki, lakini katika biblia Neno mkuki linatumika kwa namna mbili, upo mkuki wa kuchomea, na pia upo mkuki wa kurusha.

Ule mkuki wa kuchomea ndio unaoitwa Fumo, ambao askari wanaubeba, na kuchoma maadui zao pale wanapowakaribia,  na kwa kawaida unakuwa ni mizito kidogo na mrefu na wenye ncha kali. Lakini ule mwingine wa kurusha wenyewe kibiblia unajulikana kama mkuki tu hivyo hivyo, isipokuwa wenyewe ni mwepesi kidogo na umetengenezwa hivyo ili utakaporushwa uweze kufika mbali zaidi adui alipo. Zote hizi ni silaha za kivita.

Hivyo unaweza kukutana na haya maneno mawili kwenye biblia yakakuchanganya.. kwa mfano baadhi ya vifungu vinayatajwa maneno yote mawili ni kama vifuatavyo.

1Samweli 17:45 “Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana”.

Ayubu 41:26 “Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha”.

Vifungu vingine ambavyo utakutana na hili neno “Fumo” Ni kama vifuatavyo;

Hesabu 25:7 “Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;

8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli”.

1Samweli 17:7 “Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia”.

1Samweli 26:12 “Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile gudulia la maji, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Soma pia 2Samweli 1:6, Ayubu 39:23,

Halikadhalika na sisi  kama wakristo rohoni ni lazima tuwe na FUMO zetu na MIKUKI yetu mikononi mwetu, ili tuitwe askari kamili wa  Kristo, hizo ndio zile silaha za mkono wa kuume zinazozungumziwa katika 2Wakorintho 6:7… Kwa hizo, ndivyo tutakavyoweza kumpiga shetani, tukizikosa, tujue kuwa shetani hatoweza kutuogopa, na silaha yenyewe ni ufahamu wa kuyatambua mamlaka tuliyopewa katika jina la YESU na DAMU yake. Na kuyatumia..

Yeye mwenyewe alisema..

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Kila mmoja wetu ambaye anasema ameokoka anapaswa ajue kuwa mamlaka hayo amepewa, Hivyo simama kama shujaa, hubiri, haribu kazi za shetani, wafungue watu, mwaribu shetani na kazi zake zote katika maombi. Kwasababu Fumo zetu na mikuki yetu ipo  mikononi mwetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

NYAYO TUNAZOPASWA KUZIFUATA.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments