Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa,

Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa,

SWALI: Nini maana ya maandiko haya?

Mithali 25:28 “Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta”.

JIBU: Mstari huu unatupa picha jinsi mtu asiyeweza kuitawala roho yake anavyoonekana rohoni.Hapo anasema, roho yake imefanana na mji uliobomolewa usio na kuta..

Zamani, miji mikubwa ilipojengwa ilikuwa ni lazima izungushiwe kuta kubwa na ndefu.. Yerusalemu ulizungushiwa kuta, Babeli ulizungushiwa kuta, Yeriko ulizungushiwa kutwa n.k.  Na lengo la kufanya vile ilikuwa ni kuulinda mji dhidi ya wavamizi, na wapepelezi, wasiingie kokote tu watakako na kuushambulia mji.

Ni vijiji na vimiji vidogo tu ndivyo vilikuwa havina kuta zinazozunguka..lakini miji yote ilikuwa ni lazima iwe na sifa hiyo.

Sasa na rohoni ndivyo ilivyo, ikiwa na maana, kama wewe si mtu wa kuitawala roho yako, ni sawa na ule mji usio na kuta..Na matokeo yake ni kuwa upo hatarini kuvamiwa na kila aina ya maadui zako wa rohoni.

Ukishindwa kuizuia roho yako na tamaa za huu ulimwengu..Kwamba kila kitu unachojisikia kukifanya, wewe unafanya, kijisikia kuzini unakwenda kuzini, ukijisikia kunywa pombe unakunywa.. ukijisikia kuvaa vimini unavaa, ukijisikia kuvaa suruali unavaa, ukijisikia kutumia mkorogo unatumia, fahamu kuwa, utakuwa ni makao ya mapepo yote mabaya duniani.

Kwasababu roho yako haina ulinzi. Ndugu si kila kitu unachokiona, ukifanye, au ukiangalie, au ukisikilize, unapokesha muda wote kwenye tamthilia,  kwenye simu unachati, lakini muda wa kuomba huna, muda wa kujifunza Neno huna.. Wewe ni mji usiokuwa na ukuta..

Utaombewa leo, mapepo yatatoka, lakini kesho yatarudi tena mengine mengi tu, tatizo ni hilo, umefungua malango kwa kila roho inayojisikia kukuingia ..kwasababu umeshindwa kuitawala roho yako. Leo rafiki yako anakuja kukwambia tukabeti, na wewe bila kufikiri unakimbilia huko, unatazama picha za ngono, unasikiliza miziki ya kidunia, ni lazima uvamiwe na mapepo.

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”.

Hivyo ni lazima tujifunze kuzitawala roho zetu, sawasawa na maandiko yanavyotasa.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

Ufisadi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Iman
Iman
1 year ago

Naomba uniunge na group hili Kwa njia ya whatsupp