Title mtakatifu ni

Roho Mtakatifu ni nani?.

Watu wengi wanajiuliza Roho Mtakatifu ni nani? Jibu  rahisi ni kuwa Roho Mtakatifu ni Roho ya Mungu, Mungu anayo Roho kama vile mwanadamu alivyo na roho, hakuna mwanadamu yeyote asiye na roho.

Na Biblia inasema katika Mwanzo 1:26 kwamba Mwanadamu aliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Ikiwa na maana kuwa kama mwanadamu ana nafsi halikadhalika Mungu naye anayo nafsi, na kama mwanadamu anayo roho vilevile na Mungu naye anayo Roho. Kwasababu tumeumbwa kwa sura yake na kwa mfano wake. Na kama vile mwanadamu anao mwili halikadhalika Mungu naye anao mwili.

Na Mwili wa Mungu si mwingine zaidi ya ule uliodhihirishwa pale Kalvari miaka 2000 iliyopita. Nao ni mwili wa Bwana Yesu Kristo, hivyo Yesu Kristo ndiye Mungu mwenyewe aliyedhihirishwa katika Mwili. Hivyo aliyemwona Yesu amemwona Mungu (Yohana 14:8-10)

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Huyo ni Yesu anayezungumziwa hapo.

Na kadhalika roho iliyokuwepo ndani ya Mwili wa Bwana Yesu Kristo ndio Roho ya Mungu na ndiye ROHO MTAKATIFU MWENYEWE. Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha.

Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.

7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,

8 wakapita Misia wakatelemkia Troa”.

Sasa utauliza kama Roho wa Yesu ndiye Roho Mtakatifu iweje mahali pengine Bwana Yesu anaonekana amejaa Roho Mtakatifu?. Na mahali pengine anaonekana Roho Mtakatifu akishuka juu yake?

Jibu ni kwamba, Roho wa Mungu hana mipaka kama roho zetu sisi wanadamu zilivyo na mipaka, sisi wanadamu Mungu alivyotuumba roho zetu mipaka yake ni katika miili yetu.

Haziwezi kutenda kazi nje ya fahamu zetu au miili yetu.Haiwezekani niongee na wewe hapa na wakati huo huo roho yangu ipo China. Hilo haliwezekani kwetu sisi wanadamu, isipokuwa kwa Mungu linawezekana. Roho wake anauwezo wa kuwa kila mahali, ndio maana wewe uliopo Tanzania utasali muda huu na mwingine aliyepo China atasali na mwingine aliyeko Amerika atakuwa anamwabudu Mungu muda huo huo na wote Roho Mtakatifu akawasikia na kuwahudumia kila mtu kivyake. Huyo huyo anao uwezo wa kuwepo mbinguni, na duniani ndani ya Mwili wa Bwana Yesu na wakati huo huo kuzimu, hakuna mahali asipofika.

Ndio maana utaona alikuwa ndani ya Kristo, na bado akashuka juu ya Kristo, na akaachiliwa juu yetu siku ile ya Pentekoste.

Hiyo ndiyo tofauti ya Roho wa Mungu na roho ya mwanadamu. Roho zetu zina mipaka lakini Roho wa Yesu hana mipaka.

Na ni kwanini Roho wa Yesu anajulikana kama Roho Mtakatifu?

Ni kwasababu yeye ni Roho Takatifu, hiyo ndio sifa kubwa na ya kipekee Roho wa Yesu aliyoibeba..Yeye ni mtakatifu na hachangamani na uchafu.

Na ndio maana uthibitisho wa Kwanza kabisa wa Mtu aliyempokea Roho Mtakatifu ni kuwa Mtakatifu. Umepokea uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu, unakuwa kama YESU. Naamini mpaka hapo utakuwa umeshafahamu Roho Mtakatifu ni nani?

Je! Umepokea moyoni mwako? kama bado ni kwanini? Biblia imesema ahadi hiyo ni ya bure na tunapewa bila malipo, kwa yeyote atakayemwamini.

Matendo 2:39 “Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Gharama za kumpata huyo Roho si fedha bali ni Uamuzi tu! Ukimtafuta Mungu kwa bidii utampata Neno lake linasema hivyo..

Hivyo kanuni rahisi sana ya kumpata ni KUTUBU kwanza: Yaani unamaanisha kuacha dhambi kwa vitendo, kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kwaajili ya ondoleo la dhambi kulingana na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako. Na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako, atakayekupa uwezo wa kuwa kama yeye alivyo yaani Mtakatifu. Vilevile atakushushia na karama zake za Roho kwa jinsi apendavyo yeye juu yako. Hapo ndipo utakapopokea uwezo wa kuwa shahidi wake

Kumbuka biblia inasema wote wasio na Roho Mtakatifu hao sio wake (Soma Warumi 8:9), Hivyo ni wajibu wetu sote kumtafuta Roho Mtakatifu kwa bidii sana. Kwasababu hutaweza kumjua Mungu, wala kupokea uwezo wa kuishinda dhambi kama huna Roho Mtakatifu ndani yako.

Bwana akubariki.

Maran Atha !jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtakatifu ni Nani?

 JIBU: Tafsiri ya kibiblia ya MTU MTAKATIFU ni tofauti na tafsiri ya kiulimwengu.
 
Ulimwengu unatafsiri Mtu mtakatifu ni mtu yeyote anayetenda matendo mema! mtu asiyetenda dhambi!..mtu anayekubalika na asiye na mawaa,
 
Lakini Biblia haitafsiri hivyo, kwasababu hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa Matendo yake, na kujigamba mbele zake, wanadamu wote tunatenda dhambi kwa namna moja au nyingine aidha kwa kujua au kwa kutokujua. Na hivyo wakati unapojiona upo sawa, kumbe haupo sawa..wakati unajiona ni msafi kumbe ni mchafu n.k
 
Sasa Biblia inamtaja mmoja tu ambaye hakuwa na dhambi hata moja na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO peke yake! huyo ndiye biblia imemtaja kuwa mtakatifu, kwasababu alizaliwa bila dhambi na aliondoka duniani bila dhambi hata moja. Huyo peke yake ndiye anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa matendo yake. Na ndiye pekee Mungu anayemwangalia kuwa ni Mtakatifu. Wengine wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
 
Warumi 3: 23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu”
 
Sasa Kwa kupitia huyo sisi wengine tutakaomwamini yeye ndio tutahesabiwa kuwa ni watakatifu,. Kama mtu yeyote hatakuwa ndani ya YESU hawezi kuonekana mtakatifu mbele za Mungu, hata kama anajiona ni mkamilifu kiasi gani, hata kama atatenda matendo ya haki kiasi gani…mbele za Mungu ni kama Uchafu tu!
 
Yesu ni kama vazi letu la nje sisi tulio wachafu! Ukimvaa Yesu mbele za Mungu hakuoni wewe, bali anamwona Yesu mwanawe ambaye ni Mtakatifu, hivyo na wewe unaonekana mtakatifu kwa ajili yake. Hiyo ndio maana ya NEEMA, Tunahesabiwa HAKI (yaani tunahesabiwa kuwa watakatifu) bure kwa njia tu ya kumwamini YESU KRISTO. Hapo ndipo mtu unaouna umuhimu wa YESU kuja duniani, Kwahiyo watakatifu ni wale walio ndani ya YESU tu!.
 
Hivyo wale wanaosema duniani hakuna watakatifu, ni kweli kwa mtazamo wa kibinadamu, lakini kwa mtazamo wa Mungu duniani wapo watakatifu maandiko yanatumabia hivyo katika:
 
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
 
Na hawa ndio wale wale wote walio ndani ya YESU KRISTO.
Sasa utauliza! Ina maana tukiwa ndani ya Yesu hata kama tukitenda dhambi za makusudi, tutazidi kuonekana NI watakatifu mbele za Mungu? jibu ni la! hakuna mtu yeyote aliye ndani ya Kristo, akawaza tena kutenda dhambi za makusudi, hakuna mtu aliye ndani ya Kristo akafanya uasherati, au akalawiti au akaua..ukiona mtu anatenda dhambi za Makusudi huyo bado hajawa ndani ya YESU, bado ni wa Ulimwengu. (Soma 1Yohana 3:9 na Warumi 6:1-2 )..
 
Kwasababu mtu yeyote aliyempokea YESU huwa anapokea hapo hapo kipawa cha Roho Mtakatifu, ambaye huyo kazi yake ni kumwongoza, kumfundisha na kumpasha habari ya mambo yote..kwahiyo mtu wa namna hiyo moja kwa moja atajikuta anatamani kupiga hatua mbele kila siku kuelekea ukamilifu na sio nyuma…Hata ile tamaa ya kufanya dhambi huwa inakufa yenyewe ndani yake, na hivyo hawezi kutenda dhambi mwenyewe za makusudi.
 
Ubarikiwe.

 


Mada Nyinginezo:

JEHANAMU NI NINI?

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

NJAA ILIYOPO SASA.

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

6# SWALI : Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?

JIBU: Tukisoma;

Mathayo 12:25-32 ” Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.

25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?

27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu.

28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia.

29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.

30 Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.

31 Kwa sababu hiyo nawaambia, KILA DHAMBI, NA KILA NENO LA KUFURU, watasamehewa wanadamu, ILA KWA KUMKUFURU ROHO HAWATASAMEHEWA.

32 Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao. “

Tunavyosoma mistari hiyo tunaona kabisa wale Mafarisayo walikuwa wanajua Bwana Yesu ni kweli alikuwa anatoa pepo, na kutenda mambo yote kwa uweza wa Roho wa Mungu, lakini wao kwa ajili ya wivu, na kwa tamaa zao wenyewe,ili tu wawavutie watu kwao, wakakusudia kwa makusudi kabisa, wawageuze watu mioyo ili watu wasimuamini Bwana Yesu,wawaamini wao, na ndipo wakaanza kutoa maneno ya makufuru wanawaambia watu kuwa BWANA anatoa pepo kwa uwezo wa belzebuli mkuu wa Pepo angali ndani ya mioyo yao walikuwa wanajua kabisa anachofanya ni kwa uweza wa Roho wa Mungu.

Ukweli wa jambo hilo unajidhihirisha kwa Nikodemo ambaye naye alikuwa ni mmoja wa wale mafarisayo alipomwendea Yesu usiku na kumwambia

Yohana 3:1-2″Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, RABI, “TWAJUA” YA KUWA U MWALIMU, UMETOKA KWA MUNGU; KWA MAANA HAKUNA MTU AWEZAYE KUZIFANYA ISHARA HIZI UZIFANYAZO WEWE, ISIPOKUWA MUNGU YU PAMOJA NAYE. “

kwahiyo unaona walikuwa wanajua kabisa lakini kwa ajili ya wivu wakaanza kuzusha maneno ya uongo juu ya kazi ya Roho wa Mungu, sasa huko ndiko kumkufuru Roho Mtakatifu. hivyo basi Bwana Yesu alitoa angalizo tunapozitazama kazi za Mungu, pale mtu mwenye Roho wa Mungu anatenda kazi za Mungu kweli huku tunajua ni Mungu ndiye anayefanya kazi ndani yake, na kuanza kusema yule ni mchawi, au anatumia uchawi, au mshirikina, au tapeli, au mwizi, ili tu watu wasiziamini kazi za Mungu au vinginevyo, au unaanza kuzusha propaganda za uongo juu yake, pengine kwa kusudi la kumkomoa! hapo ndugu utakuwa unajimaliza mwenyewe. (Ni kweli si watumishi wote ni wa Mungu,hao ni sawa kuufunua uovu wao). Lakini Hapa tunamzungumzia yule unayemfahamu kabisa ni mtumishi wa BWANA,..wewe hujui umewakosesha wangapi, ambao kwa kupitia yeye, watu wengi wangeokolewa? kufanya hivyo ni hatari sana tuwe makini.

Hivyo hii dhambi unawahusu wale wanaozipinga kazi za Mungu kwa makusudi kabisa (Mfano wa mafarisayo). Hao kwao hakuna msamaha, hawawezi tena kutubu hata iweje wanachongojea ni ziwa la moto.

Lakini shetani naye anapenda kulitumia hili neno kuwafunga watu wajione kuwa wamemkufuru Roho Mtakatifu na kwamba dhambi zao hazisameheki hata wafanyeje,
Hii inakuja sana sana kwa watu waliowachanga ki-imani, kuna shuhuda nyingi za watu waliofungwa na shetani kwa namna hiyo wakidhani kuwa dhambi zao hazisameheki, kuna watu wamekata tamaa wanajiona kwa wingi wa dhambi zao, Mungu hawezi kuwasemehe tena, pengine wameua, wametoa mimba sana, n.k, Sasa jambo la namna hii likija katika mawazo yako likatae linatoka kwa yule mwovu kukufanya wewe ujione kuwa Mungu hawezi kukusamehe umemkufuru, hivyo usijisumbue kutubu kwasababu Mungu hatakusikiliza.

Kumbuka kama tulivyosema Dhambi hii inakaa kwa wale watu ambao ndani yao mioyo ya toba imekufa, au hofu ya Mungu haipo tena kwao, watu waliojikinai, wanaompinga Mungu katika fikra zao japo kuwa walimjua Mungu na uweza wake wote, wanazipotosha kazi za Mungu kwa makusudi kwa faida zao wenyewe,ili wawavute watu kwao, au wawe washirika wao na sio kwa Mungu. Hivyo basi kitendo tu cha wewe kuwa na hii hofu ya kumwogopa Mungu ujue Roho wa Mungu anatenda kazi ndani yako na hayo mawazo ya kwamba umemkufuru Roho Mtakatifu yapinge huyo ni adui ndio moja ya njia zake hizo ili usiufikie wokovu na anapenda kuwatesa watu wengi katika andiko hili.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

DHAMBI YA MAUTI

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI.

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni sawa kuomba novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia?

Mtakatifu Rita, ambaye kwa kanisa katoliki anajulikana pia kama ‘mwombezi wa mambo yasiyowezekana’, na ‘mfanya miujiza’.

Ni mama aliyezaliwa mwaka 1381, katika mji unaitwa Kashia, taifa la Italy. Aliolewa akiwa na umri mdogo lakini baada ya mume wake na watoto wake wawili  kufa aliamua kujiunga na utawa, ijapokuwa alipitia changamoto, kujiunga na jamii hiyo kwasababu tayari alikuwa ameshaolewa(sio bikira), lakini mwishoni alifanikiwa.

kulingana na kanisa katoliki maombi ya Rita yaliwaletea wengi majibu, lakini pia alitambulika kwa jeraha dogo kwenye kipaji cha uso wake, wakiamini kuwa ni alama ya ukristo, kufuatana na mateso ya Yesu msalabani, mahali alipowekewa taji ya miiba. Alikufa kati ya umri wa miaka  75-76.

Na ilipofika tarehe 24 May 1900, papa Leo XIII, Alimtangaza kuwa mtakatifu. Yaani ukitangazwa kuwa mtakatifu, unakidhi vigezo vya kuwa mwombezi wa walio hai.

Tangu huo wakati wakatoliki wengi dunia wamekuwa wakimfanyia novena, na litania. Na wengi wakishuhudia kuwa matatizo yao sugu, yakitatuliwa, hivyo imemfanya kuwa maarufu sana.

Lakini Je! Jambo hili ni kweli? Ni vema kufahamu kuwa katika maandiko matakatifu (BIBLIA), Hakuna mahali popote, tunafundishwa kuwa watakatifu waliokufa zamani au sasa wanaweza kutuombea. Zaidi sana wanakuwa hawaelewi neno lolote linaloendelea duniani, biblia inasema hivyo katika;

Mhubiri 9:5 kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.

Umeona? Kwahiyo desturi hii, ya kupeleka maombi yetu kwa watakatifu watuombee, ni ya kipagani, Ni ibada za sanamu,  ambayo asili yake ilianzia kwenye dini zinazoamini mizimu inaweza kuwasiliana nasi. Kusema hivi haimaanishi tunawapinga wakatoliki, au tunatangaza chuki hapana, bali tunasemezana ukweli ili tupone, kwasababu safari yetu ni moja sote tuurithi uzima wa milele, sisi tunasema ni wakristo.

Haijalishi utakuwa ulifanya novena ya Rita ikakuletea majibu kiasi gani, bado ni ibada ya sanamu, kumbuka pia shetani analeta majibu, si ajabu mambo hayo kutendeka, ili watu wapumbazike katika hayo.

2Wakorintho 11:14  Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

Mwombezi wetu ni mmoja tu naye ndiye YESU KRISTO (1Yohana 2:1). Lakini sio pamoja na Petro, au Paulo, au Eliya, au Mariamu, au Yusufu. Hao wote ni watakatifu ambao walihitaji ukombozi tu kama sisi, na wenyewe walituelekeza kumtazama Yesu Kristo, na sio wao.

Mtume Paulo alisema maneno haya;

1Wakorintho 1:13  Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?

Hivyo hakuna haja ya kupeleka maombi yako kwa mtakatifu yoyote, na vilevile wale walio kule hawawezi kutuombea sisi pia. Halikadhalika wewe huwezi kumwombea mwenye dhambi aliyekufa, kwamba Bwana amtoe matesoni. Imani hiyo haipo pia katika biblia. Soma (Waebrania 9:27). Mafundisho ya watu kupitia toharani hayapo katika biblia.

Tujifunze kusoma biblia tutafunguka kwa mengi, mapokeo ya kidini sio Neno la Mungu. Hao wanaoabudu miti na mawe twaweza kuwacheka, lakini tukawa kama wale tu isipokuwa katika mfumo mwingine, tusipopenda kusoma biblia. Tukikataa kuwa wafuasi tu wa kidini tukapenda Neno la Mungu, Roho Mtakatifu atatusaidia kufunguka kwa mengi.

Hivyo ikiwa wewe ulikuwa ni mmojawapo wa wanaopeleka maombi kwa Rita wa kashia, au  kwa mtakatifu mwingine yoyote acha sasa kufanya hivyo. Tubu dhambi ukabatizwe, upokee Roho Mtatakatifu ambaye atakuongoza na kukutia katika kweli yake yote(Yohana 16:13).

Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi waweza fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Novena ni nini? Na je ipo kibiblia?

Roho Mtakatifu ni nani?.

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

Moja ya maeneo ambayo yamekuwa na uelewa mchanga katika ukristo, ni pamoja na eneo la Roho Mtakatifu. Wengi tunachofahamu kuhusiana na huduma ya Roho Mtakatifu ni kunena kwa lugha tu! Basi. Lakini hilo ni tone moja kati ya bahari kubwa, tunahitaji kumwelewa kwa mapana na marefu ili tujue utendaji kazi wake ulivyo kwa wanadamu na ulimwengu.

Kipo kitabu cha Roho Mtakatifu, ikiwa utapenda kukipata wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya chapisho hili/ au tutumie ujumbe whatsapp.

Leo  tutaona sehemu mojawapo ambayo inahusiana na mafuta ya Roho Mtakatifu.  Unaweza ukajiuliza, kwanini kila mara watu waliposhukiwa na Roho Mtakatifu, maandiko yanatumia neno “wakajazwa”, na sio neno kama ‘wakavikwa’  au labda ‘wakalishwa’. Kwasababu tukisema wakavishwa maana yake tunamfanya yeye kuwa kama nguo, au tukisema wakalishwa tunamfanya yeye kuwa kama chakula. Lakini tukisema wakajazwa tunamfanya yeye kuwa kama kimiminika, na hicho si kingine zaidi ya MAFUTA. Roho Mtakatifu anakuja kwetu kama MAFUTA. Ni vema kulitambua hilo!

Sasa si watu wote wanayo mafuta yote ya Roho Mtakatifu kama Bwana Yesu alivyokuwa,. Leo tutaona aina mbalimbali za mafuta hayo, kisha tujitahidi tuyapokee yote kwa msaada wa Roho.

1.Mafuta ya nguvu

Haya yanapatikana katika UMOJA.

Zaburi 133:1 Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.  2 Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake.

Maana yake ni kuwa jinsi watakatifu wanavyoshirikiana  pamoja kwa umoja, rohoni, yanaonekana ni mafuta mengi yanashuka katikati yao, mengi kiasi cha kufika hata katika upindo wa mavazi. Wanatiwa mafuta, na hayo ni ya nguvu. Kwasababu palipo na umoja ndipo penye nguvu.

Na ndio maana siku ile ya pentekoste, Mungu aliwakutanisha kwanza mahali pamoja wakawa wapo orofani pale sio katika kupiga zoga, hapana, bali katika kusali na kuomba, na kutafakari maneno ya Bwana(Matendo 1:12-14). Na ghafla, wakashangaa, katika siku ya kumi, Roho Mtakatifu amewashukia wote wakajazwa nguvu. Wakawa mashahidi wa Bwana tangu siku ile  na kuendelea (Matendo 2).

Jambo kama hilo utalithibitisha tena katika Matendo 12:14, walipokuwa wamekaa pamoja kumwomba Mungu, mahali pale pakatikiswa, wajazwa Roho Mtakatifu wakanena Neno la Mungu kwa ujasiri. Hivyo hivyo na sisi  tupenda ushirika na wengine, hususani katika kuomba na kufunga. Tukiwa watu wa namna hii tutajazwa mafuta haya na tutapokea ujasiri mwingi sana katika wokovu wetu.

Soma (Mhubiri 4:12)

2. Mafuta ya shangwe

Haya yanapatikana katika usafi na utakatifu.

Waebrania 1:8  Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9  Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio

Shangwe ni ile furaha iliyopitiliza, inayodhihirika hata mpaka kwa nje. Halikadhalika Roho Mtakatifu naye anayo shangwe yake, ambayo hiyo inazidi hata hii ya kidunia, kwasababu ya kwake inakufanya ufurahi sio tu katika raha bali mpaka katika majaribu. (Luka 10:21)

Kwamfano utaona Bwana Yesu alikuwa nayo hata pale msalabani.

Wakolosai 2:15  akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

Tukiwa watu wa kupenda haki(utakatifu), mafuta haya Roho anayaminina, mioyoni mwetu. Maisha yetu yanakuwa ni ya furaha tu, daima, vipindi vyote. Haijalishi mauvimu, kero, udhia, yataonekana kwa nje, lakini rohoni ni shangwe nyingi za Roho Mtakatifu, ndivyo Mungu alichokiweka ndani ya Kristo na kwa wakatifu wa kale ( Matendo 13:52, Waebrania 11:13, , Mathayo 5:12).

Hivyo Tuchague kupenda maisha ya haki ili tuyapate mafuta haya. Ni muhimu sana, ukipoteza furaha ya wokovu, huwezi kusonga mbele.

3. Mafuta ya upambanuzi

Haya yanaachiliwa katika kulitunza Neno la Mungu ndani yako.

1Yohana 2:26  Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27  Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.

Kumbuka biblia ni sauti ya Mungu katika maandishi, hivyo unavyoiweka moyoni mwako, ndivyo inavyoumbika  na kuwa sauti kamili ya Mungu. Na hiyo ndio itakayokufudisha, na kukusaidia kupambanua, ikiwa wewe ni mkristo na una miaka  mingi katika wokovu halafu hujawahi kuisoma BIBLIA yote, bado kuna viwango Bwana hawezi kusema na wewe.  Lakini Unavyozidi kujifunza Neno ndivyo mafuta haya yanavyoachiliwa ndani yako kukufundisha. “Huna Neno, huna sauti ya Mungu”

4. Mafuta ya kuhudumu

Haya huachiliwa katika kuwekewa mikono na wakufunzi wako, au kuombewa na kanisa (wazee wa kanisa).

Huu ni utaratibu mwingine Mungu ameuachilia, katika kanisa, vipo vitu ambavyo huwezi kuvipokea wewe tu mwenyewe. Bali kutoka kwa waliokutangulia kiimani.

Elisha alitiwa mafuta na Eliya, akasimama mahali pake kihuduma (1Wafalme 19:15-16)

Musa aliwatia mafuta wale wazee 70, sehemu ya roho yake ikawaingia (Hesabu 11:16-25)

Daudi na Sauli wote walitiwa mafuta ya Samweli, ndipo wakapokea nguvu kutoka kwa Mungu, kutumika. (1Samweli 15:1, 16:12,)

Vilevile Timotheo, aliwekewa mikono na mtume Paulo  (2Timotheo 1:6), akapokea neema ya kuyasimamia makanisa ya Kristo, mahali pa Paulo.

Vivyo hivyo na wewe usikwepe, wala usimdharau kiongozi wako wa kiroho, hata kama atakuwa ana madhaifu. Anayo sehemu yake aliyopewa na Mungu kwa ajili yako. Jinyenyekeze omba akuwekee mikono neema ya Mungu ijae ndani yako ya kuhudumu, ili Bwana akunyanyue katika viwango vya juu zaidi.

Hivyo kwa kuzingatia aina hizo 4, tukazipokea basi tutamsogelea Bwana katika mafuta mengi sana ya juu. Mfano wa Bwana wetu Yesu Kristo. Roho Mtakatifu atajifunua zaidi ndani yetu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Nini maana ya’Shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo’Ayubu 20:4

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

Masihi ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

USINIONDOLEE ROHO WAKO MTAKATIFU.

Swali: Je! Roho Mtakatifu anaweza kuondoka juu ya Mtu?.Kulingana na Zaburi 51:11?

Tusome,

Zaburi 51:11 “Usinitenge na uso wako, Wala Roho yako mtakatifu usiniondolee“.

Jibu rahisi la swali hili ni ndio!, anaweza kuondoka juu ya mtu, na mtu akabaki kama alivyo…

Mfano wa mtu katika biblia ambaye aliondokewa na Roho Mtakatifu juu yake ni Mfalme Sauli.

1Samweli 16: 14 “Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.

15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua”

Na sababu pekee iliyosababisha Roho wa Mungu kuondoka juu ya Sauli ni tabia ya Sauli ya kutokujali na vile vile kutoyatii maagizo ya Mungu, na kumdharau.

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu”.

23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Na madhara ya mtu aliyempoteza Roho Mtakatifu, ni KUONDOKEWA NA FADHILI ZA MUNGU JUU YA MAISHA YAKE.

Sauli aliondokewa na Fadhili za Mungu, baada tu ya Roho wa Mungu kuondoka juu yake..

2Samweli 7:14 “Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa mapigo ya wanadamu;

15 LAKINI FADHILI ZANGU HAZITAMWONDOKA, KAMA VILE NILIVYOMWONDOLEA SAULI, niliyemwondoa mbele yako”.

Mtu aliyeondokewa na Fadhili za Mungu, anakuwa anaipoteza ile Amani ya KiMungu kipindi amempokea Roho, hali kadhalika ile furaha ambayo ilikuwa ndani yake inapotea!..ile raha aliyokuwa anaipata alipokuwa ndani ya wokovu, inapotea!…Ule utulivu aliokuwa anaupata kipindi Roho yupo juu yake, unapotea….kile kibali alichokuwa nacho kipindi cha mwanzo kinaondoka..anakuwa ni mtu wa kuhangaika, na kusumbuliwa na roho chafu za wivu, hasira, uchungu, na nyinginezo, kama ilivyokuwa kwa Sauli.

Maandiko yanasema Roho wa Mungu alipomwacha tu Sauli, pale pale roho mbaya ikaanza kumsumbua…akaanza kumwonea wivu Daudi, akaanza kuwa mkatili kwa kuwaua makuhani wa Mungu..

1Samweli 22:11 “Ndipo mfalme akatuma watu waende kumwita Ahimeleki, kuhani, mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, hao makuhani, waliokuwako huko Nobu; nao wakaenda kwa mfalme wote pia”.

Hizo ndizo hasara za kumpoteza Roho Mtakatifu.. Mfalme Sauli alipoasi, Fadhli za Mungu zilimwondoka, na akawa mtu wa kukosa amani, furaha, kujiamini, na wivu…

Lakini kumbuka pia, kuondokewa na Roho Mtakatifu si kuacha kunena kwa lugha, au kufanya miujiza, au kutoa pepo. Mtu aliyeondokewa na Roho Mtakatifu bado anaweza kutoa pepo, bado anaweza hata kunena au kwa lugha..

Kwasababu matunda ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu sio Kunena kwa lugha, au kutabiri, au kuona maono, bali ni yale yanayotajwa katika kitabu cha Wagalatia 5:22 “ Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,”.. Mambo hayo ndio yanayopotea ndani ya mtu, pindi Roho Mtakatifu anapoondoka ndani yake.. Na si kunena kwa lugha, au kuona maono, au kutabiri.. Mtu anaweza kunena na kutabiri lakini Roho Mtakatifu akawa hayupo ndani yake..

Utauliza hilo tunalithibitisha vipi?.. Maandiko yanaonyesha Sauli hata baada ya Roho wa Mungu kuondoka ndani yake, bado aliendelea kutabiri..

1Samweli 18:10 “Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, NAYE AKATABIRI NDANI YA NYUMBA. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake”.

Umeona?.. Matunda ya Roho ni tofauti kabisa na kazi za Roho.. Kazi za Roho kama miujiza, unabii, ishara, zinaweza kufanyika kupitia yeyote yule. Bwana alimtumia Punda kuona maono ya malaika mbele ya Balaamu, atashindwaje kumpa maono mwenye dhambi?..

Kwahiyo maono au kunena kwa lugha, sio uthibitisho wa kwanza wa mtu aliye na Roho Mtakatifu, uthibitisho wa kwanza wa mtu mwenye Roho Mtakatifu ndani yake ni hayo matunda tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22, ambayo ni Upendo, amani, furaha, Fadhili, kiasi..yaani kwaufupi ni utakatifu (Waebrania 12:24). Ndio maana Bwana Yesu alisema wengi watakuja siku ile na kusema Bwana Bwana hatukutoa pepo kwa jina lako, na kufanya unabii, lakini Bwana atawafukuza kutoka mbele zake.

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Hata sasa Roho Mtakatifu anaweza kuondoka juu ya Maisha yetu!.. na tukazipoteza Fadhili za Mungu. Na ataondoka endapo TUTAMHUZUNISHA, au KUMZIMISHA.

TUNAMHUZUNISHAJE?

Maandiko yanasema katika Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.

Tabia za kutokujali Neno la Mungu, kama alivyokuwa Sauli ndizo za kwanza zitakazoweza kusababisha Roho Mtakatifu kuondoka juu yetu..Tunapolisikia Neno halafu hatulitii.. badala yake tunaendelea na mambo yale yale mabaya, hapo tunamhuzunisha Roho mtakatifu aliye ndani yetu…

Tunapoendelea kufanya mambo machafu, ambayo tunajua kabisa ni kinyume na Neno la Mungu, hapo tunamhuzunisha na hivyo ni rahisi kutuacha na tukaingiliwa na maroho mengine.

TUNAMZIMISHAJE?

Maandiko yanasema katika kitabu cha 1Wathesalonike 5:19 kuwa “Msimzimishe Roho”.. Maana yake Roho Mtakatifu anaweza kuzimika ndani yetu. 

Na tunamzimisha Roho kwa sisi kuacha kuomba, kuacha kufunga, kuacha kufanya ibada, kuacha kuifanya kazi ya Mungu, kuacha kumtolea, kuacha kumtukuza na kumsifu na kuifanya kazi yake na kuacha kuishi Maisha matakatifu. Mambo haya yanamfanya Roho Mtakatifu kuzimika ndani yetu, na hata kuondoka kabisa na kutuacha.

Bwana Yesu atusaidie tuzidi kudumu katika Neema yake na kuitunza zawadi nzuri ya Roho aliyotupatia (Matendo 2:39).

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

Mtakatifu ni Nani?

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi nyumbani

Print this post

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe,

Leo tutajifunza jinsi ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Yapo mambo makuu matatu yanayovuta uwepo wa Mungu karibu nasi.

  1. MAOMBI

Hili ni jambo la kwanza linalohifadhi uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu. Tunapoingia kwenye maombi Roho Mtakatifu anazidi kusogea karibu nasi,  anasogea kuomba pamoja na sisi (Warumi 8:26) na vile vile anasogea kuzungumza na sisi.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka kipindi, Bwana Yesu anabatizwa katika mto Yordani na Yohana, utaona Roho Mtakatifu alishuka juu ya Bwana kwa mithili ya HUA (Yaani Njiwa).

Lakini katika tukio hilo kuna siri moja imejificha pale, ambayo ukisoma kwa haraka haraka unaweza usiigundue. Na siri yenyewe ni MAOMBI!. Utaona baada ya Bwana kutoka majini, na kusogea pembeni utaona alianza KUOMBA!, na wakati akiwa katika maombi, ndipo Mbingu zilipofunguka na Roho Mtakatifu kushuka juu yake.

Luka 3:21 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, NAYE ANAOMBA, mbingu zilifunuka;

22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe”.

Umeona? Ni wakati alipokuwa anaomba ndipo Roho Mtakatifu alishuka juu yake, na sio wakati anabatizwa tu peke yake.

Vile vile utaona kipindi cha Pentekoste, Mitume na wanafunzi wengine wapolikuwa wamekusanyika mahali Pamoja katika ghorofa wakidumu katika kusali, na kule kule ndipo Roho Mtakatifu akashuka juu yao na kuwajaza nguvu (Soma Matendo 1:13-14, Matendo 2:1-2).

Na sehemu nyingine nyingi, utona kuwa Roho Mtakatifu alishuka wakati watu wakiwa kwenye maombi..

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”.

Vile vile na sisi tukitaka kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu hata tumuhisi ndani yetu, au katikati yetu basi hatupaswi kuyakwepa MAOMBI, kadhalika tukitaka tumsikie anataka nini kwetu au anasema nini, njia pekee ni Maombi!

Sasa inawezekana hujui namna ya kuomba, ni rahisi sana.. Kama utatamani kupata mwongozo wa namna ya kuomba basi tutumie ujumbe inbox, ili tuweze kukutumia somo linalohusu “Njia bora ya kuomba”

  1. KUSOMA NENO.

Hii ni njia nyingine ya Muhimu ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kutuongoza na kututia katika Kweli yote (Yohana 6:13-14), na Kweli ni Neno la Mungu (Yohana 17:17). Hivyo tunapotenga muda wa kuishika biblia na kuisoma kwa lengo la kujifunza, basi Roho Mtakatifu anasogea karibu nasi sana. Ni lazima atusogelee kwasababu ndio kazi yake yeye kutufundisha na kutufunulia maandiko.

Tunaweza kujifunza kwa yule Mkushi aliyekuwa anarudi nchini kwao, ambapo njiani alijikuta anafungua kitabu cha Isaya 53, kilichokuwa kinazungumzia Habari za Masihi, Yesu lakini hakuwa na ufunuo wowote juu ya hilo, Ndipo Roho Mtakatifu akaingia kazini kujisogeza karibu naye ili amtie katika kweli yote!!..

Roho Mtakatifu akaanzaa kuzungumza kwanza na Filipo siku kadhaa kabla hata ya Mkushi huyo kufikiria kusoma hilo andiko, Roho Mtakatifu akaanza kutengeneza njia ya kumkaribia Mkushi huyo, akamwambie Filipo ashuke njia ya jangwa, na alipokutana na yule Mkushi yupo matatani haelewi maandiko, ndipo Roho Mtakatifu akaanza kuzungumza kupitia kinywa cha Filipo. Na hatimaye kumfunua macho yake na kumtia katika kweli yote.

Matendo 8:29 “Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi”.

Roho wa Yesu ni yule yule na tabia zake ni zile zile, tukitaka atukaribie, tumsikie, au tumwone basi ni lazima pia tuwe wasomaji wa Neno.

  1. KUHUBIRI/KUSHUHUDIA.

Agizo kuu ambalo Bwana alilotupatia ni kupeleka injili ulimwenguni kote.

Marko 16:15 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Kwanini kuhubiri/kumshuhudia Yesu kunamsogeza Roho Mtakatifu karibu nasi?. Kwasababu kila tunapofika mahali na kushuhudia tunafanyika vyombo vya Roho Mtakatifu, Hivyo Roho Mtakatifu hana budi kila wakati kuwa nasi kwasababu wakati wote tunatumika kama vyombo vyake, hakuna wakati uwepo wake utakaa mbali na sisi!..

Mathayo 10:18 “nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 KWA KUWA SI NINYI MSEMAO, BALI NI ROHO WA BABA YENU ASEMAYE NDANI YENU”.

Kwahiyo kama wakati wote tutakuwa katika hayo mazingira ya kumshuhudia Kristo, maana yake wakati wote, kinywa kitakachokuwa kinasema ndani yetu ni kinywa cha Roho Mtakatifu, hivyo uwepo wake utakuwa nasi muda wote!, lakini kama hatutakuwa katika mazingira yoyote ya kumshuhudia Kristo ni ngumu Roho Mtakatifu kuwa na sisi, kuzungumza kupitia vinywa vyetu, au kusema nasi!.

Je! Na wewe leo Umempokea Yesu?

Na kama ndio je! Wewe ni MWOMBAJI?..wewe ni MSOMAJI WA NENO?…wewe ni MSHUHUDIAJI?. Kama hufanyi hayo basi, uwepo wa Roho Mtakatifu utawezaje kuusikia?, vile vile sauti yake utaweza kuisikia?!.

Leo shetani kawafanya wakristo wengi wasiwe Waombaji?..utakuta mkristo mara ya mwisho kutenga angalau lisaa limoja kuomba yeye binafsi hata hakumbuki!, (yeye atakuwa anapenda kusikiliza na kusoma mahubiri tu!, na kuombewa lakini kuomba mwenyewe hataki/hawezi), Utakuta mkristo mara ya mwisho kusoma Neno binafsi ni muda mrefu sana, leo hata ukimuuliza mkristo biblia ina vitabu vingapi hajui, ukimpa biblia afungue kitabu cha Yeremia atapepesuka nusu saa hajui kilipo mpaka akaangalie kwenye index, hiyo ni kuonesha ni jinsi gani biblia ni kitabu-baki tu kwake!, na si kila kitu kwake!.

Leo hii ukimwuliza mkristo mara ya mwisho kuzungumza na mtu mwingine Habari za wokovu, au kumshuhudia Kristo, hana hiyo kumbukumbu!, lakini shuhuda za mipira, na za Maisha ya watu wengine zimejaa katika kinywa chake!..

Kumbuka Bwana anatamani yeye kuwa karibu na sisi kuliko sisi tunavyotamani yeye awe karibu nasi, hivyo ni wajibu wetu kuongeza bidii katika kuomba, kusoma Neno, kushuhudia Pamoja na kuishi Maisha matakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Tusome,

Warumi 3:22 “ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;

23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;”

Hapo maandiko yanasema “Wote wamefanya dhambi” na sio “Wote wanafanya dhambi”. Ikiwa na maana kuwa kuna dhambi ambayo imeshafanyika huko nyuma ambayo imewafanya wote wawe katika dhambi.

Na dhambi hiyo si nyingine Zaidi ya ile ya Adamu na Hawa. Maandiko yanasema kwa kukosa kwake mtu mmoja Adamu, sisi wote tumeingia katika hali ya kukosa.

Warumi 5:19 “Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.

Umeona?..Kwa dhambi ya Adamu na sisi tunaonekana tumefanya dhambi, kwasababu tulikuwa katika viuno vya Adamu, wakati Adamu anafanya makosa hayo..Hivyo kwa dhambi yake ikafanya vizazi vyake vyote kuwa katika dhambi. Ndio maana wanadamu wote tunazaliwa na dhambi ya asili bila hata ya sisi kutaka, tunazaliwa tayari tukiwa tumepungukiwa na utukufu wa Mungu.

Ndio maana utaona mtoto anazaliwa na hasira, uchoyo, kiburi n.k.. Hiyo ni kutoka na dhambi ya asili aliyoirithi kutoka kwa Adamu. Na ndio maana maandiko yanasema “wote tumetenda dhambi” na sio tunatenda dhambi.

1 Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.

9 tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.

10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.

Na hiyo ndio sababu pia tunamhitaji Bwana Yesu, atuondolee hiyo dhambi ya asili.

Kwasababu Kristo anafananishwa na Adamu wa pili. Maana yake kama Adamu wa Kwanza alivyotuingiza matatizoni sisi wanawe katika vizazi vyote, kadhalika Adamu wa pili (yaani Yesu Kristo), atatuingiza katika hali ya kuwa watakatifu, endapo tukimwamini na kumpokea..

Warumi 5:18 “Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima.

19 Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.

Pale tunapompokea na tunapotubu dhambi zetu na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, tunakuwa tumezaliwa mara ya pili, na hivyo ile dhambi ya asili tuliyozaliwa nayo inaondoka. Tunakuwa watakatifu, kwasababu Kristo anashusha nguvu ya kipekee juu yetu ya kutusaidia kushinda dhambi…Hivyo tunajikuta tunaishi maisha ya utakatifu na usafi bila sheria.

1Yohana 3:9 “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu”

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, wote walio ndani ya Kristo, dhambi haiwatawali, kwasababu wameuvua utu wa kale na kuvaa utu upya.

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Na ndio maana maandiko pia yanatuonyesha kuwa watakatifu waliopo duniani ndio wanaompendeza Mungu..ikimaanisha kuwa duniani kuna watakatifu.

Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.

Je! Na wewe ni Mtakatifu?.. Umempokea Yesu na kutubu na kubatizwa ubatizo sahihi?. Kama bado kumbuka Kristo yupo mlangoni, na atakaporudi atawachukua tu wale wateule wake na kwenda nao mbinguni, yaani wale wote waliozaliwa mara ya pili, na kuishi maisha ya utakatifu. Lakini wengine waliosalia ambao hawamtaki yeye watatupwa katika lile ziwa la moto.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

1Wakorintho 12:3 “Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.”

Katika hali ya kawaida kila mtu anaweza kusema “Yesu ni Bwana”, hata watu wa kidunia, wanaweza kulitamka hilo neno, lakini wasiwe wamemaanisha, au wamejua uzito wake, wakawa wamelitaja tu.. Lakini kwa mtu ambaye amempokea Roho Mtakatifu, na kufunuliwa kwa Roho kuwa Yesu ni nani, kwanini amekuja duniani, kwanini  amwage damu yake, afe na kufufuka, na yupo wapi sasahivi?..Mtu wa namna hiyo kama akitamka “Yesu ni Bwana”,… kutamka kwake kunakuwa na maana sana na nguvu kubwa. Kwasababu amekutamka katika Roho.

Hivyo Mtu anayetaja “Yesu ni Bwana” katika Roho Mtakatifu ni lazima atakuwa ni mtakatifu, kwasababu amemjua Mungu, kadhalika atakuwa anamheshimu Mungu na kumwogopa, kutokana na ufunuo mzito alioupata kumhusu Yeye (Yesu).

Lakini Yule anayesema  tu “Yesu ni Bwana” bila Roho, maana yake hamjui Yesu, hana mpango na maneno yake, hana  ufunuo wowote alioupata unaomfanya  yeye aseme hivyo, mtu wa namna hiyo kutamka kwake hakuna manufaa yoyote, ndio maana hapo biblia inasema.. “mtu hawezi kusema Yesu ni Bwana isipokuwa katika Roho Mtakatifu”..maana yake atakuwa anasema tu kimdomo, na si kwa kuelewa na kumaanisha.

Bwana Yesu alisema maneno haya…

Mathayo 7:21 “SI KILA MTU ANIAMBIAYE, BWANA, BWANA, ATAKAYEINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22  Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23  Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona?.. Kusema tu “Yesu ni Bwana” bila ya kuwa na badiliko halisi la ndani, ambalo hilo linaletwa na Roho Mtakatifu mwenyewe, ni kazi bure!.. Vile vile huwezi kuwa na Roho Mtakatifu halafu useme Bwana Yesu kalaaniwa.. hilo haliwezekani.

Hivyo ili tuyafanye mapenzi ya Mungu, na maneno ya midomo yetu pamoja na sala zetu zikubalike mbele za Mungu, hatuna budi kuzaliwa mara ya pili, na kuzaliwa mara ya pili kunakuja kwa kutubu dhambi, kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi pamoja na kupokea Roho Mtakatifu.

Baada ya hapo, lolote tunalolitamka la kumwadhimisha Mungu, kumsifu, kumwomba, na kumkiri linakuwa katika Roho, na hivyo linaleta matokeo makubwa sana. Lakini kama hatutatubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, hata sala zetu zinakuwa ni bure, hata sifa zetu kwake zinakuwa ni bure…

2Timotheo 2: 19  “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti kati ya Roho Mtakatifu na Roho Takatifu?

JIBU: Roho Mtakatifu na Roho Takatifu ni kitu kimoja, inategemea neno hilo limetumika wapi

Roho wa Mungu anapozungumza ndani yetu, au kutuongoza, au kutufundisha..anakuwa kama ni mtu yupo ndani yetu akifanya hizo kazi..anakuwa kama ni mtu mwingine mpole ndani yetu anazungumza nasi, anatufundisha, anatushauri, anatufariji, anatutia moyo, anatuongoza n.k..Hivyo hiyo tabia ya kuwa kama mtu wa pili ndani yetu, ndiyo inayofanya biblia sehemu zote iitaje Roho ya Mungu, kwa cheo cha uutu. (yaani Roho M-takatifu).

Hali kadhalika, linapokuja suala la tabia ya Roho ya Mungu, ni sahihi kabisa kusema Roho ya Mungu ni Roho Takatifu, ni Roho Nyenyekevu, ni Roho Tulivu, Ni roho Njema (Danieli 5:12) n.k Hapo hatujaivisha uutu lakini tumeielezea sifa yake.

Yapo madhehebu yanayofanya mambo haya yawe magumu kwa maneno hayo mawili, na hata mengine yamebadilisha biblia zao, kila mahali palipoandikwa kwenye biblia neno Roho Mtakatifu, yamebadilisha na kuweka Roho Takatifu..Hivyo kwao ni kosa kutumia neno Roho Mtakatifu mahali popote. Vile vile yapo mengine ni kosa kutumia neno Roho Takatifu. Pasipo kujua kwamba maneno yote mawili ni sahihi, inategemea ni wapi yametumika.

Kumbuka pia ni wajibu wa kila mmoja aliyeokoka kuwa na Roho Mtakatifu.

Mungu atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE WAJUA?

MAKEDONIA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post