Na mbinu nyingine shetani anayopenda kuitumia pasipo watu wengi kujua, ni mapepo, anapenda kutumia mapepo kuwapandikizia watu wengi kiburi, kwamfano inatokea mtu kaenda kumuombea mtu mwingine na yule mtu akalipuka mapepo, na yale mapepo, yakaanza kumsifia, “wewe ni mtu hatari sana, tunakuogopa, yaaani unatuunguza na unatutesa sana tangu siku nyingi, yataendelea kumwambia sisi tumetoka jupita tumewajaribu, wachungaji wengi tumewashinda ni wewe peke yako ndio unayetutesa”..na yataendelea kumwambia hadithi nyingi za uongo ambazo zote maudhui yake ni kumnyanyua yule mtumishi, na yule mtumishi pasipo kujua kwamba zile roho ni kongwe tangu Edeni na zinajua namna ya kumwangusha mwanadamu, atadhani kuwa zinamwambia ukweli, atadhani kuwa yeye kweli ndiye wa kipekee kuliko watu wote duniani, pasipo kujua kwamba “shetani ni mwongo tangu zamani na yeye ni baba wa uongo” maandiko yanasema hivyo. Sasa yule mtumishi atatoka pale na kuamini kuwa hakuna kama yeye na pasipo kujua kuwa amepandikiziwa roho ya kiburi tayari, atakwenda huku na huko kujisifu kuwa hakuna kama yeye.