Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

Jibu; Tusome,

2 Wakorintho 6:3 “Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe”

Leo hii ukizungumzia neno “kukwaza” moja kwa moja akili za wengi zinalenga katika “kuudhi au kumuudhi mtu”.

Hivyo andiko hilo ni rahisi kulitafsiri, kuwa tusiwakwaze watu (yaani tusiwaudhi) kwa namna yoyote ile.

Lakini kiuhalisia andiko hilo halimaanishi hivyo.

Tafsiri ya neno kikwazo/kwazo ni kitu chochote ambacho kinaweza kumzui mtu asisonge mbele, kwamfano mtu anayesafiri kwa gari na akakuta jiwe kubwa katikati ya barabara, limezuia barabara jiwe lile ni kikwazo kikwazo kwake kwa safar yake.

Sasa kibiblia KWAZO ni kitu chochote kinachomzuia mtu kuingia katika Imani au kusonga mbele katika imani..

Hivyo hapo biblia inaposema kwamba tusiwe KWAZO la namna yoyote..imemaanisha kuwa TUSIWE KIKWAZO KWA MTU YEYOTE KUINGIA KATIKA IMANI.

Vipo vitu vingi ambavyo vinaweza kuwa kikwazo kwa watu wengine kuvutiwa na imani ya kikristo. Na mfano wa vitu hivyo ni maisha ya kianasa na kiulimwengu watu wanayoishi.

Kwamfano uvaaji wako unaweza kuwa kwazo kwa mwingine kumpokea Yesu, huwezi kwenda kumhubiria mtu ampokee Yesu na huku akikuangalia wewe unavaa vimini, Unatembea nusu uchi, au unajiuza, au ni mtukanaji, au mlevi.. Hapo ni lazima utakuwa KWAZO tu la yeye kuingia katika Imani na hata wakati mwingine kusababisha jina la Mungu kutukanwa.

Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?

22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?

23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?

24 Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu, kama ilivyoandikwa”.

Katika hali kama hiyo biblia ndio inatuonya tusiwe Kwazo la namna yoyote ile kwa watu, ili utumishi wetu pia usilaumiwe.
Lakini haimaanishi kuwa tusiwaudhi watu kwa namna yoyote ile!.

Katika haya maisha haiwezekani kuishi maisha ambayo hutawaudhi watu kabisa..kwasababu hata ukitenda mema yote bado utawaudhi tu baadhi ya watu..hivyo hilo ni jambo lisiloepukika.

Lakini kuishi maisha ambayo hatutakuwa KWAZO la mtu kuingia katika ufalme inawezekana kwa asilimia zote, endapo tukijikana nafsi kweli kweli, na tukimtegemea Roho Mtakatifu.

Bwana azidi kutusaidia katika hilo ili tusiwe kwazo kwa yeyote!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

 

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

 

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Friedrich the son of JESUS%
Friedrich the son of JESUS%
2 years ago

Barikiwa mtumishi!
Kwa somo zuri BWANA azidi kukupatia ufunuo ili mwili wa KRISTO ujengwe! Maran atha!