Title unakimbizwa

Kuota unakimbizwa.

Moja kwa moja ndoto kama hii inatoka kwa Yule mwovu, kukimbizwa kwa namna yoyote ile maadamu ni kukimbizwa basi ni kutoka kwa yule mwovu, iwe ni kuota unakimbizwa na watu au kuota unakimbizwa na nyoka au kuota unakimbizwa na ng’ombe, au kuota unakimbizwa na simba, au kuota unakimbizwa na tembo au kuota unakimbizwa na nyuki, au kuota unakimbizwa na kichaa, ni ndoto kutoka kwa mwovu…Sikuzote kitu kinachokimbizwa ni kitu kilicho dhaifu, cha kuwindwa ili kiliwe, swala anakimbizwa na simba, ni kwasababu yeye ni dhaifu, lakini kitu chenye ujasiri kamwe hakikimbizwi.

Ukijiona unakimbizwa fahamu kabisa moja kwa moja kuwa wewe ni dhaifu rohoni, na hiyo  ni kutokana na kuwa upo nje ya Kristo au kama upo basi hauijatambua mamlaka uliyonayo ndani ya Kristo kwa uchanga wako wa kiroho au kwa uzembe wako wa kutokujishughulisha na mambo ya Mungu..

Mithali 28:1 Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.

Hivyo mrudie Mungu wako kama bado haujaokoka, Tubu ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe kwa Jina la Yesu Kristo, ili upate ondoleo la dhambi zake. Au kama tayari ulikuwa ndani ya Kristo na ulikuwa unayumba yumba huu ni wakati wako sasa kusimama imara.

Kisha anza kujifunza biblia kwa bidii, na pia tafuta kanisa la kiroho la kwenda kujifunzia Neno la Mungu, ili likae kwa wingi ndani yako, upate kujua nafasi uliyonayo katika Kristo. Mpaka siku moja na wewe uote unamkimbiza shetani.

2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)”

Usipuuzie ndoto hizo, kwasababu shetani kweli anakuwinda akumeze…Fanya uamuzi wa busara kumgeukia Mungu.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota mbwa kunamaanisha nini?

Mbwa ni mnyama anayeweza kuwakilisha vitu vitatu:

1) Mlinzi

2) Adui

3)Kitu najisi/Mchafu.

Inategemea hiyo ndoto imekuja katika mazingira gani..na pia kama imekuja katika mazingira ya kujirudia rudia au katika hali ya uzito wa kitofauti basi haipaswi kupuuzwa, inayo maana rohoni.

  1. Tukianzana namaana ya kwanza kama mlinzi:

Kama tunavyojua mbwa ni mlinzi. Na katika biblia watumishi wa Mungu pia wanafananishwa na mbwa walinzi.

 Vilevile watumishi  ambao hawasimami katika  nafasi zao kikamilifu za kuwalinda kondoo wa Mungu  wanafanishwa na mbwa walinzi wasioweza kubweka wala kung’ata.

Isaya 56:9-11

[9]Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni.
[10]Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.[11]Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.

Kwahiyo unapoota..mbwa mara kwa mara..pengine amesimama getini tu..au anafukuza kitu  au anafanya kitu fulani kwa ujasiri lakini hana shida na wewe.. hana mpango wa kukudhuru wewe..basi ni Mungu anakukumbusha kuwa uzidi kusisima vema katika nafasi yako kama mlinzi.

Lakini kama unaona mbwa huyo ni mwoga..anakimbizwa kimbizwa tu..anajificha ficha ujue huna nguvu rohoni..hivyo tengeneza mambo yako na Mungu ikiwa wewe ni mtumishi wa Mungu. Kwasababu Mungu anakuona kama mlinzi lakini bado hujakamilika katika kazi yako.

2) Maana ya pili ni kama Adui.

Kibiblia mbwa pia anawakilisha Adui.
Zaburi 22:16

“[16]Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu”.

Zaburi 22:20 “Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa”.

Ukiota unakimbizwa na mbwa..au unashambuliwa nao. Au wanakutisha.au wanakuvizia kuchukua kitu chako..Ujue kuwa upo katika vita rohoni.
Ibilisi anataka kuiba kilicho chako.au kukuangamiza kabisa.. Hapo kama umeokoka huna budi kuwa mwombaji sana..mwambie Bwana akulinde na kukuhifadhli mbali na mashbulizi yote ya adui..pia zidisha kiwango chako cha kumtumikia Bwana ni ulinzi mkubwa sana.

Wafilipi 3:2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao.
Lakini kama hujaokoka..fanya hima mapema sana umrudie Mungu wako. Vinginevyo upo hatarini kuangamia kabisa.

3) Maana ya tatu ni kitu najisi.

Kibiblia mbwa pia anawakilisha kitu najisi” au kichafu .Mbwa huwa hajali ni nini anakula anaweza rudia hata matapishi yake biblia inasema hivyo katika.. Mithali 26:11..

Ni wanyama wasiostahili heshima yoyote..

Mathayo 15:26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

Mbwa hajali ni yupi anakutana naye katika kupata watoto..anaweza kutanana hata na mama yake.
Hivyo kwa ujumla ni kwamba mbwa anawakilisha pia watu waovu..waliodhambini ambao hawajali maisha yao ya kiroho hata kidogo.

Kwahiyo kama unaota mara kwa mara mbwa ambao huelewi wapo kwa lengo gani..leo unamwona hivi kesho vile…ujue kuwa ndivyo Mungu akuonavyo.

Tubu dhambi zako mgeukie Mungu wako kama wewe ni mwenye dhambi..kumbuka katika hali kama hiyo uliyopo sasa ukifa ujue ni moja kwa moja kuzimu..biblia inasema hivyo kwa watu walio hivyo rohoni..

Ufunuo 22:15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Ikiwa upo tayari leo kumkaribisha Kristo ndani ya maisha yako akubadilishe basi fungua hapa kwa ajili ya kupokea mwongozo wa sala ya Toba..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

KUOTA UNAFANYA TENDO LA NDOA.

Kuota unafanya tendo la ndoa au kuota unafanya mapenzi na mtu usiyemjua maana yake ni nini?


Awali ya yote tunapaswa kufahamu kuwa Ndoto yoyote ya zinaa, haitokani na Mungu..Ni aidha inatokana na mtu mwenyewe au shetani. Leo tutaangazia makundi mawili ya watu wanaoota ndoto za namna hii:

Kundi la kwanza ni: Kwa mtu ambaye hajaokoka:

Biblia inasema..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…”

Hii ikiwa na maana kuwa, yale mambo au vile vitu tulivyokuwa tunavifanya au kuvifikiria mchana kutwa mara nyingi huwa ndio hivyo hivyo tunaviota tukiwa tumelala..

Hata kama hatutaviota vilevile kama vilivyo lakini tutaota mambo yanayoendana na matukio tuliyokuwa tunayafanya katika mazingira yanayotuzunguka..Kwamfano kama wewe wiki nzima ulikuwa unashinda mashambani tu kulima na kupalilia shamba lako..Uwezekano wa wewe kuota upo shambani unafanya shughuli kama hizo ni mkubwa sana..Kama wewe ulikuwa shuleni mwaka mzima bwenini uwezekano wa kuendelea kuota ndoto upo shuleni ni mkubwa..

Vivyo hivyo kama wewe ni mlevi unayeshinda bar kila siku usiku uwezekano wa kuota ndoto za upo bar unakunywa pombe na marafiki zako ni mkubwa..Haiwezekani mtu ambaye hajawahi kuenda bar au kunywa pombe Maisha yake yote akaota anakunywa pombe bar na akalewa. Vivyo hivyo hata katika zinaa, kama Maisha yako yote, na wakati wako wote unawaza uzinzi kichwani, unatazama picha chafu mitandaoni, na video za pornography, unafanya mustarbation, unaangalia muvi za mapenzi, unasiliza nyimbo za kidunia za kizinzi, maneno unayozungumza kila mara ni ya usherati tu, jinsi ya kumpata binti yule au kaka yule..Nataka nikuambie kila siku usiku kuota unafanya tendo la ndoa au unafanya mapenzi na mtu usiyemjua au unayemjua itakuwa ni jambo la kawaida kwako.

Kwasababu Maisha yako yote yapo katika uzinzi..Shughuli kubwa iliyo katika ubongo wako ni zinaa..

Vilevile yapo mapepo ya namna hii mahususi kutoka kuzimu yanawavaa watu ambao hawajaokoka ili kuchochea hii hali ndani yao. Ndio hapo utamwona mtu ndoto kama hizi zinakuwa ni sehemu ya Maisha yake, anajikuta mara kwa mara anafanya mapenzi na mtu asiyemjua, leo,Kesho, anapumzika wiki moja hali ile ile inajirudia tena na tena, ukiona hivyo ujue lipo pepo limeshakuvaa.

Unahitaji kugeuzwa Maisha yako.

Kundi la Pili: Kwa mtu aliyeokoka.

Lakini kama wewe upo ndani ya Kristo.

Mambo mawili yanaweza yakawa yanahusika.

La Kwanza. Ni ishara ya kuwa kuna mahali unapoa,.Umepunguza kiwango chako cha nguvu za rohoni, kuna mahali unapadokoa au baadhi ya mambo kidunia yanakuchukua..Hivyo hapo unapaswa uongeze bidii yako kwa Mungu, ongoza kiwango chako cha maombi, tumia muda mrefu kusoma biblia kuliko kufuatilia mambo yasiyokuwa na maana. Simama imara katika Imani yako. Kabla hujalala jijengee utaratibu kwa kuomba. Na hiyo hali haitajirudia tena.

Lakini kama wewe umeokoka na bado unauhakika umesimama imara katika Imani, na ndoto kama hiyo imekujia bila kutazamia, na ishara kuwa ulikuwa hufurahii ni kwamba hata katika hiyo ndoto ulikuwa unaonyesha upinzani,kukataa hicho kitendo, au kujiuliza inakuaje kuaje nipo katika hali hii na mimi nimeokoka.. basi hali kama hiyo ikikujia Ikimee mara moja kwa jina la YESU, kisha mwambie shetani huwezi kunijaribu kwa kishawishi chochote..Na ndoto kama hizo hutaziota tena..

Jambo ambalo watu wengi hawafahamu ni kuwa zinaa, kuiondoa ndani ya mtu inahitaji muujiza, na anayeweza kuikata kiu hiyo ni YESU KRISTO peke yake, haijalishi wewe ni mkristo au wewe ni muislamu au hauna dini ..Ni Yesu pekee ndio anayeweza kukubadilisha na kukufanya uishi Maisha yaliyo  mbali na zinaa.

Dhambi hii, inawashinda wengi, na ndio dhambi inayoongoza kuwapeleka watu kuzimu.  Isitoshe biblia inasema, Kama vile ilivyokuwa katika siku za Sodoma na Gomora ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu. Kumbuka siku za Sodoma na Gomora, kulikuwa na uzinzi wa kiwango vya hali ya juu kama vilivyopo sasa, kulikuwa kuna mashoga na wasagaji waliokuwa wanajidhirisha waziwazi kama ilivyo sasa.. Na hiyo ndio ikiwa sababu ya miji ile kuteketezwa..Lakini cha kuogopesha Zaidi ni kwamba, kati ya maelfu kama sio mamilioni ya watu waliokuwa katika miji ile, ni watu watatu tu ndio walionusurika..wengine wote waliteketea kwa moto..

Luka 17:28  “Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;

29  lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.

30  Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu”

Soma tena kwa makini mstari huu:

Yuda1:7  “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.

8  Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu”.

Unaona? Vivyo hivyo na jambo kubwa Zaidi litakalofanya ulimwengu huu uteketezwe siku ambazo si nyingi, ni dhambi ya zinaa, vilevile watakaonusurika watakuwa ni wachache sana. Mungu huwa hana wengi wape,.Leo hii unaweza kusema mbona kila mtu yupo hivi au yupo vile..Lakini nataka nikuambie  hata kama dunia nzima imeamua kuasi Mungu akimuona mtu mmoja tu, inatosha yeye kuangamiza..

Hivyo ikiwa wewe ni mwenye dhambi, haijalishi dini yako, au dhehebu lako.Yesu anawaokoa watu wote, na bado anaendelea kuokoa ikiwa mtu atakuwa tayari kutaka kuokolewa naye, kwasababu neema yake kaiachia kwa watu wote. Ikiwa leo hii unataka kusema Maisha ya uzinzi basi, nataka YESU anasaidie niishinde dhambi hii na nyingine zote…Ukiwa unamaanisha kweli kufanya hivyo..Basi leo hii hapo ulipo anaweza kukuokoa na kukugeuza na kukufanya kuwa mtoto wake.

Ikiwa upo tayari kubadilishwa leo Maisha yako na Yesu..Basi fahamu kuwa yeye yupo hapo pembeni yako kukusaidia, unachopaswa kufanya ni kufungua tu moyo wako..Uhitaji unione mimi, au usikie sauti yangu..Suala la wokovu ni Zaidi ya upeo wa fikra za kibinadamu. Leo hii YESU atayageuza Maisha yako, na atafanya muujiza mkubwa ndani yako kwa namna ambayo hujawahi kuidhania.

Hata na yale mengine mbali na uzinzi, labda ulevi, matusi, wizi yote atayaua ndani yako ikiwa tu utakuwa tayari kumpokea Leo. Yesu yupo hai, yupo tayari kwa mtu yeyote kumsaidia wakati wowote bure.. hivyo bila kukawia kawia hapo ulipo chukua muda jitenge eneo la utulivu. Kama upo ndani tafuta chumba ujitenge peke yako, kisha piga magoti..Ukiwa hapo chini umepiga magoti sema sala hii kwa sauti..

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU WA KUSHINDA DHAMBI, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA, NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KWA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani Mungu amekusikia ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa matendo, hapo ulipo ikiwa ulikuwa na picha chafu katika siku yako, anza kwa kuzifuta, ikiwa ulikuwa unayafanya  mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Kuanzia leo hii utaanza kuona badiliko kubwa ndani yako. Jambo lingine unalohitaji kufanya ni kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na katika kujifunza biblia ili uukulie wokovu.

Hata kama wewe ulikuwa ni muislamu, tafuta kanisa lililokaribu na wewe la kiroho, waeleze uamuzi wako uliouchukua, kisha wao watakuelekeza hatua inayofuata au kama utahitaji msaada wa kanisa kwa eneo lako basi wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312.. Ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Yazingatie hayo. Na Bwana atakuwa pamoja na wewe katika kila hatua ya Maisha yako. Na ndoto zote hizo za Kuota unafanya tendo la ndoa au kuota unafanya mapenzi na mtu usiyemjua, zitaisha.

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Pia zidi kutembelea website yetu hii, kwa mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

Kuota unafanya Mtihani.

Kuota unakimbizwa.

MKUU WA ANGA.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post