Title kuota nyoka

KUOTA NYOKA.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu YESU KRISTO, Suala la upambanuzi wa ndoto ni moja ya mambo ambayo yanawasumbua wengi, lakini kwa bahati mbaya watu wengi wamekosa kujua tafsiri ya ndoto zao, kulingana na maandiko…

Hivyo kabla ya mtu hukimbilia kupewa au kutafuta tafsiri ya ndoto yake ni vizuri kwanza akafahamu kuwa ndoto zimegawanyika katika makundi makuu matatu, kundi la kwanza ni zile ndoto zinazotokana na Mungu, kundi la pili ni zile zinazotokana na shetani na kundi la tatu ni ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe, na hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya ndoto tunazoziota karibu kila siku, na aina hii ya tatu huwa inakuja kutokana na shughuli zetu tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka kila siku..

Ndoto za namna hii huwa hazibebi ujumbe wowote, hivyo hazihitaji kutafsiriwa, mara nyingi zinapaswa zipuuziwe..ikiwa hujafahamu vizuri namna ya kuitambua ndoto yako kulingana na makundi haya basi bofya somo hii ulipitie kisha ukishamaliza tuendelee…>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza tafsiri ya ndoto hii ya kuota nyoka, sasa ikiwa ni ndoto ambayo inajirudia rudia, basi izingatie sana..kumbuka Nyoka katika maandiko tangu mwanzo anasimama kama ishara mbaya,

Na nyoka amebeba tabia kuu tatu, ya kwanza ni kudanganya kama tunavyomsoma pale Edeni alivyomdanganya Hawa (Mwanzo 3:1-5), tabia ya Pili ni kuuma kama biblia inavyotuambia atakugonga kisigino (Mwanzo 3:15), na ya tatu ni kumeza, kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo 12:4), pale alipotaka kummeza mtoto yule alipotaka kuzaliwa,..Na tabia hizi zote Shetani anazo na ndio maana kila mahali alifananishwa na joka, na sio kiumbe kingine chochote kama vile kondoo au njiwa.

Hivyo ndoto za namna hii nyingi zinatoka kwa shetani, na chache sana zinakuja kutoka kwa Mungu, lakini tukianza kuchambua upande mmoja mmoja hatutamaliza, wengine wanaota wanakimbizwa na nyoka, wengine wanaota wanaumwa na nyoka, wengine wanaota wameviringishwa na nyoka, wengine wanaota wapo karibu na ziwa au bahari na lijoka likubwa linatoka huko, wengine wanaota wanamezwa na joka, wengine wanaongea nayo n.k. n.k. vyovyote vile chamsingi ambacho mtu anapaswa kufahamu hapo ni kuwa ziwe zinatoka upande wa Mungu au upande wa shetani,..Ni kwamba ADUI YUPO MBELE YAKO.

Hapo Shetani yupo karibu na wewe kutimiza kazi hizo tatu au aidha mojawapo,

Jambo la kwanza ni  kukudanganya au tayari ameshakudanganya: Sasa Ikiwa upo nje ya Kristo yaani hujaokoka basi fahamu kuwa upo chini ya udanganyifu wa shetani tayari, hivyo hapo unaonyeshwa hali yako ilivyo rohoni, Jambo unalopaswa kufanya ni kurudi kwa Kristo haraka sana kabla udanganyifu haujawa mkubwa zaidi ukakuzalia matunda ya mauti, hapo ulipo tayari umepofushwa macho pasipo hata wewe kujijua. Hivyo tubu umgeukie Mungu haraka sana, maadamu muda bado upo.

Au kwa namna nyingine shetani anakaribia kukushawishi kuingia katika kosa au dhambi ambayo itakugharimu sana, hata maisha yako, hivyo angalia njia zako, uchukue tahadhari, funga milango yote ambayo unaona itakupeleka mbali na Kristo, acha kufanya vitu ambavyo sasa hivi unavifanya unaona kabisa havimpendezi Mungu, acha haraka sana, upo mtego wa shetani nyuma yake.

Pili shetani anakutegea mtego au anataka kukuletea madhara aidha katika huduma yako, au afya yako,au familia yako au shughuli yako, anataka kukugonga kisigino chako usisonge mbele, hapo unapaswa uongeze kiwango chako cha maombi kama Bwana Yesu alivyosema ombeni msije mkaingia majaribuni..Hivyo ili kumshinda silaha uliyonayo ni kuomba sana.

Tatu shetani anataka kukimeza kile ambacho Mungu amekipanda ndani yako:

Na jambo la kwanza huwa anakimbilia ni NENO LA MUNGU hilo ndilo huwa anafanya bidii sana kupambana nalo kwasababu anajua likishakuwa ndani ya mtu litakwenda kuleta madhara makubwa sana katika ufalme wake hivyo anasimama hapo karibu na wewe ili akimeze kile ulichokisikia.. inafananishwa na zile mbegu ambazo zilingukia njiani ndege wakaja kuzila,

Mathayo 13:18 “Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.

13.19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.”

Hivyo kwa ufupi ikiwa upo nje ya Kristo fanya hima uingie ndani, na ikiwa upo ndani ya Kristo chukua tahadhari uimarishe uhusiano wako na Kristo kwasababu shetani yupo karibu na wewe kushindana nawe kwa kila hali..

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

UZAO WA NYOKA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota unakemea mapepo/ unashindana na nguvu za giza.

Kunaweza maanisha namna tatu, ya kwanza, ni kwamba unapitia kweli vita vya kiroho, lakini ya pili ni unaonyeshwa na Mungu uhalisia wa vita vya kiroho, na tatu unaonyeshwa uwezo wa hali yako ya  kiroho.

Maandiko yanasema

Waefeso 6:12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama

Tukianza na maana ya kwanza,

Mara nyingine adui huanzisha mashambulizi kuanzia ndotoni, wakati mwingine utakuta mtu anaota ameumwa labda na nyoka kidoleni halafu  anapoamka, anashangaa kinauma kweli, na kama haiishii hapo, anaanza kuona kidole kinazidi kutengeneza kidonda, mpaka kuleta madhara mwili mzima, sasa hayo ni mashambulizi ya kipepo. Na hivyo ikiwa ndoto yoyote umeiota ambayo unaona uhalisia wake mpaka nje, unashindana na mapepo halafu linakukaba, unahangaika kitandani. Ujue ni mashambulizi ya adui, hapo unayo mamlaka ya kubatilisha, kwa jina la Yesu.

Lakini mara nyingine, utajikuta unaota tu unakemea mapepo, unashindana nayo. Si kwamba utakuwa unamashambulizi ya adui, lakini unaonyeshwa tu uhalisia wa vita vya kiroho, na hivyo vipo halisi, au vitakuja mbeleni katika safari yako ya maisha, na unapaswa uvishinde, kwa jina la YESU, kwa simama imara ndani yake..

Na mwisho ni Mungu anakuonyesha kiwango cha kiroho, ulichopo au unachopaswa uwe nacho. Mwingine atakuwa ameokoka, lakini anahofu ya kutoa pepo au kuombea watu, Mungu anakuonyesha uwezo wa kushindana na nguvu za giza unao, au unapaswa uanze kazi ya kuwaombea wengine wanaosumbuliwa na nguvu za giza. Lakini pia pale unapojiona umezidiwa nguvu zao, ni kuonyesha uongeze kiwango chako cha kiroho, kwa maombi, utakatifu, na Neno, ili uwe thabiti rohoni kuzipinga hila za adui.

Kwahiyo kwa vyoyote vile kuona unakemea mapepo, au unashindana na wachawi kwa jina la Yesu. Ni kuonyesha kuwa ni wakati wa kusimama  imara na Bwana. Kwasababu shetani ni adui wako, na adui za ndugu zako, na hivyo unapaswa umpinge sikuzote kwa kuwa thabiti rohoni kwa wewe ambaye umeokoka.

Lakini Ikiwa hujaokoka, basi ni vema ukafanya hivyo leo kwa kumkaribisha Yesu moyoni mwako, ukifahamu kuwa kamwe huwezi kumshinda adui kwa nguvu zako unamwita Kristo.

Ikiwa upo tayari  waweza kufungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kuupokea wokovu. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?(Opens in a new browser tab)

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Kuota unakabwa, mara kwa mara ni ishara ya nini?

SWALI: Mimi kila nikilala, huwa kuna kitu kinanikaba koo, nakosa pumzi, kinanikandamiza naona kama nakwenda kufa au wakati mwingine ninaganda muda mrefu siwezi kusogea. Hata nikijaribu kukemea, natumia kushindana sana, baadaye kinaniachia, Je hili ni jinamizi?. Jambo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kufunga na kuomba zinaweza pita tu  siku kadhaa halafu kikajirudia tena. Naomba msaada nifanye nini?


JIBU: Hayo ni mashambulizi ya adui ndotoni. Tufahamu kuwa adui hashambulii tu katika mwili, lakini wakati mwingine pia katika ndoto. Wapo watu wanaosumbuliwa na shetani husasani katika maeneo ya ndoto.

Utakuta kila anapolala, ni mfululizo tu wa ndoto za kipepo, labda anafukuzwa-fukuzwa, au anazini-zini na mapepo hayo, au yupo makaburini, anafanya mambo ya kichawi, zaidi wengine zinakuwa ni mwendelezo, yaani pale alipoishia jana, leo anaendelea nazo sehemu ya pili, kila anapolala hana raha, kwasababu anajua vitisho ni vilevile anakwenda kukutana navyo. Wengine mpaka inazidi wanasikia sauti kabisa za mapepo, zikiwasemesha, au wanaona vitu vya ajabu vikipita mbele yao, na hiyo yote hutokea pindi tu wanapopitiwa na usingizi kidogo, haijalishi mchana au usiku. Kundi lingine ndio hili ambalo wanaona kama wananaswa, na kitu Fulani pumzi haitoki, wanaishia kutaabika. N.k.

Sasa, unapokutana na mojawapo ya shida, hizo au mashambulizi hayo ndotoni. Jambo la kwanza ‘hupaswi kuogopa’ Fahamu suluhisho ni moja tu nalo ni YESU KRISTO. Lakini wengi hawajui ni kwa namna gani.

Mambo haya matatu (3), yaelewe yatakusaidia..

1) Tumia jina la Yesu.

Unapojikuta kwenye mashambulizi hayo, usiwe tu bubu. Hakikisha unalitumia jina la YESU kukemea. Kuyadhibiti hayo mapepo na kazi zao. Kwasababu mamlaka hiyo umepewa.

Mathayo 10:19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Lakini ukiona unasumbuliwa na hizo ndoto, halafu unapambana mwenyewe mwenyewe, huna silaha yoyote mkononi mwako, jiandae kukugeuza wewe  kuwa ndio kijiwe chao. Vaa silaha za vita. Jina la Yesu ndio silaha yetu kuu, kutiisha nguvu zote za Yule mwovu.

2) Jiweke vema nafsini, kabla hujalala.

Penda kuwa mwombaji kabla hujalala, usilale tu bila kumkabidhi Bwana usiku wako. Lakini pia hakikisha moyoni mwako, huna makunyanzi ambayo shetani atapata sababu ya kukushitaki. Unajua ni kwanini biblia inasema maneno haya?

Waefeso 4:26  Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27  wala msimpe Ibilisi nafasi

Ni kwasababu shetani hupenda mipenyo kama hiyo, kwamfano moyoni mwako una vinyongo na wenzako, una hasira na jirani zao, mambo kama hayo, husababisha adui kukushambulia kwa njia yoyote nyakati za usiku. Hivyo ukabidhi moyo wako kwa Bwana.

3) Zidisha Imani.

Ikiwa mambo hayo mawili unayafanya, lakini bado unaona mashambulizi, yanaendelea. Basi tatizo kubwa kwako lipo kwenye IMANI.  Imani yako ni chache. Upo wakati mitume walipambana na mapepo wakashindwa kuyatoa. Baadaye wakamuuliza Bwana mbona sisi tulishindwa? Yesu akawaambia ni kwasababu ya upungufu wa imani yenu. Hata leo hii ukiona mkristo unasumbuliwa sana na vibwengo, na vipepo. Ujue pia imani yake bado haijawa imara.

Kwa namna gani?

Bado hujaamini vya kutosha nguvu iliyopo ndani ya JINA LA YESU. Na ushindi ulipoupata kupitia Kristo Yesu moyoni mwako. Unachopaswa kufanya ni kumwamini Yesu asilimia mia alimaliza yote msalabani, uwe jasiri, ondoa hofu, vipepo ni vinyago tu, havina chochote cha kukubabaisha wewe. Ukiona hiyo hali inakuja wewe kuwa  ujasiri na Imani yote, usiope kitu. Kemea. “Sema wewe pepo, mimi nimekombolewa na Yesu, huna uwezo wa kushindana na Roho Mtakatifu aliye ndani. Na sasa nisikilize, kuanzia sasa hili sio hekalu lako. Kwa mamlaka ya kifalme iliyo ndani ya jina la Yesu Kristo mwokozi wangu, nakuamuru toka na kwamwe usirudi hapa tena”.

Ukiwa na ujasiri unaotokana na imani ya Bwana unayemtumikia. Nakuambia pepo hilo litabadili uelekeo mara moja, hata likija kujaribu mara nyingine likakukuta na msimamo wako huo huo, hakuna hofu ndani yako. Ndio bye! bye! Halitakaa lirudi tena itakuwa ni historia.

Kumbuka Samsoni alipokutana na Yule Simba, yeye alimwona kama ni “mzinga” tu uliomletea asali. Hivyo akalirarua, na ndio maana baadaye akaja akakuta asali ndani yake akala akaondoka. Kwasababu alijua nguvu zilizo ndani yake, zinatuliza pepo na bahari, na milima  simbuse hichi kisimba-mbarara kinachonguruma hapa mbele yangu.

Na wewe vivyo hivyo, usiishi kinyonge-nyonge tu, unakubali kunyanyaswa nyanyaswa na hivyo vipepo ambavyo havina kitu kwako kama vile huna mtetezi hapa duniani.. KEMEA! KWA IMANI, na Ujasiri. KAZI ITAKUWA IMEISHA!. Wala usitafute maombezi.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

IMANI “MAMA” NI IPI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

KUOTA UPO MAKABURINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuota upo uwanjani (uwandani)

Nini maana ya kuota upo uwanjani/uwandani?

Jibu: Kiroho uwanja au uwanda unawakilisha mahali pa mapambano.Wanamichezo wote wanaoshindania tuzo, huwa mashindano hayo yanafanyikia viwandani/uwandani.

Kwahiyo unapoota kuwa upo Uwandani na shughuli zako hazihusiani na viwanja, basi fahamu kuwa upo katika mapambano. Na mapambano hayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya.
Mapambano Mazuri:

Mapambano mazuri ni yale ya imani, hivyo kama umeokoka vizuri na umesimama kisawasawa na ukapata ndoto au ono unashindana na watu wengi au wachache katika uwanja/uwanda basi fahamu kuwa huenda Mungu anakuonyesha, au kukukumbush vita vya kiimani vilivyopo mbele yako. Hivyo huna budi kupiga mbio..sawasawa na kile kitabu cha Waebrania 12:1

Waebrania 12:1”Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”.

Soma pia Wafilipi 1:30, Wafilipi 1:27, na 1Wakorintho 9:24.

Lakini kama umejiona upo uwandani peke yako, basi kuna jambo la lingine Mungu anataka kusema nawe. Na hilo huenda ni jambo la tahadhari.

Na tahadhari yenyewe ni kama ile ya Kaini.

Wakati Kaini alipotaka kumwua Habili, alimtenga na kumpeleka uwandani. Na hiyo ni kanuni ya adui anapotaka kumdhuru mtu, anampeleka kwanza uwandani, mahali ambapo hapana watu, wala msaada wa kitu chochote..

Hivyo unapojiona upo uwandani/uwanjani peke yako, au upo na mtu mmoja, basi fahamu kuwa adui anatafuta kukuharibu au kuharibu mambo yako ya kiroho na kimwili.

Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Kwahiyo uotapo ndoto hiyo, kama hujaokoka zingatia kuokoka, na pia kama una wokovu usio thabiti (maana yake wewe ni vuguvugu) basi zingatia kuwa moto, ili adui asipate nafasi ya kukumaiza.

Lakini kama tayari upo dhani ya wokovu ulio thabiti, basi zingatia Maombi, omba maombi ya kuharibu hila zote na njama za adui, na kutakuwa shwari.
Bwana akubariki.

Tafadhalishea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

Kuota mbwa kunamaanisha nini?

UZAO WA NYOKA.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Wale Nyoka waliowadhuru wana wa Israeli jangwani walikuwa wana maumbile ya moto au?. Maana maandiko yanasema walikuwa ni Nyoka wa moto, Na kama walikuwa wenye maumvile ya moto, waliwaumaje watu na walitokea wapi? Walishushwa au?

Jibu: Tusome,

Hesabu 21:6 “BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa”

Neno “moto” hapo halijatumika kuelezea maumbile (yaani miili) ya hao nyoka, kwamba wana miili iliyoundwa kwa malighafi ya moto, hapana!. Bali limetumika kuelezea “Rangi” ya hao Nyoka, kwamba wana rangi ya moto.

Rangi ya moto, inafananishwa na rangi ya “Shaba”. Mtu anaposema “sahani ile ni ya shaba” na anayesema “sahani ile ni ya moto” Ni kitu kimoja, wote wanamaanisha kitu kimoja.

Ndio maana baada ya pale utaona Musa anaagizwa atengeneze nyoka wa shaba, kuwakilisha rangi ya hao nyoka.

Hesabu 21:8 “Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.

9 Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi”.

Nyoka hao wenye rangi ya moto, ni jamii ya Nyoka maarufu sana wenye sumu kali wanaopatikana jangwani, hadi leo wapo (Ni nyoka wa asili kabisa), maisha yao ni jangwani tu hawawezi kuishi mahali pengine, na huwa wanajificha chini ya mchanga, na kubakisha sehemu ndogo tu ya kichwa juu, hivyo si rahisi kuonekana.
Na endapo mtu akipita na bahati mbaya akakanyaga mchanga mahali ambapo nyoka huyo kajificha, basi aling’atwa na hakukuwa na matibabu.

Hivyo kwa hitimisho, walikuwa ni nyoka wa asili, isipokuwa rangi yao ni ya Moto (au shaba).

Lakini pamoja na hayo kulikuwa na ufunuo mkubwa juu ya tukio hilo lililowatokea wana wa Israeli, na huyo nyoka wa shaba, mpaka akaitwa Nehushtani.

Kwa maelezo marefu juu ya Nehushtani, unaweza kufungua hapa>> NEHUSHTANI.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

Kuota unaolewa/ unaoa kunamaanisha nini?


Zipo ndoto zenye maana katika Maisha yetu, na pia zipo ndoto zisizo na maana yoyote katika Maisha yetu,.

Hizi zisizo na maana ni ndoto ambazo, ubongo wetu unajiundia wakati tunapokuwa tumelala kutoka katika mazingira yetu yanayotuzunguka, au mambo ambayo tulikuwa tunayawaza au tunayafanya mara kwa mara, Na ndio maana biblia inasema;

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi..”

Hivyo asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, zinaangukia katika hili kundi. Kama wewe ni  mshonaji, basi tarajia asilimia kubwa ya ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitakuwa ni za namna hiyo,..Vilevile ndoto kama Kuota unaolewa/unaoa, wazo hilo pengine si geni katika kichwa chako,kwamba siku moja umekuwa ukifikiria kuwa utakuja kuoa au utaolewa, Hususani pale unapokuwa umefikia umri huo, lakini bado haijawa hivyo kwako.

Au inakuja kutokana na kuwa umekuwa ukihudhuria mazingira ya harusi mara kwa mara, Hivyo ubongo wako ukayachukua hayo matukio na kuyarudia hivyo hivyo au kwa namna nyingine unapokuwa umelala.

Lakini pia ndoto za namna hii zinaweza kuwa ni za rohoni, hivyo kubeba maana Fulani,

Kwa mfano ikiwa ulikuwa katika kumwomba Mungu, akupe mume/mke, ukiota upo katika ndoa, basi ujue jambo hilo lipo mlangoni kwako.

Lakini unachopaswa kufanya ili Mungu akupe sawasawa na chaguo lake.

  • Kwanza unapaswa uwe katika utakatifu,
  • Vilevile unapaswa uwe mwombaji,

Lakini ukiwa ni mzinifu, unatanga tanga na kila mwanaume, au mwanamke,  au unaishi mtu ambaye  hamjaona, sahau Mungu kulitekeleza hilo, na kama likifanikiwa basi ujue huyo utakayempata hujachaguliwa na Mungu.

Ili kufahamu njia sahihi ya kumpa mweza wa Maisha fungua hapa;

>>> NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Lakini hayo yote ni lazima uwe katika wokovu, ukimpata Kristo, umepata vyote, Ukimkosa yeye, umepoteza vyote mpaka uzima wako. Hivyo kama leo hii unahitaji kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, basi uamuzi huo ni mzuri kwako..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua link hii, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia kama utahitaji kujiunga katika magroup yetu ya Whatsapp unaweza ukabofya hapa chini>>

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KUOTA UNA MIMBA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNATOKA DAMU YA HEDHI.

kuota unatoka damu ya hedhi inamaanisha nini kibiblia?


Yapo mambo mawili;

Jambo la kwanza unapaswa ujue asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, si zote zina tafsiri ya rohoni kukusaidia, naweza kusema asilimia hata 90 ya unavyoviota kila siku vinatokana na ubongo wako wenyewe.

Ubongo wako Mungu kauumba kwa namna ambayo unaweza kuhifadhi kumbukumbu ya mambo unayofanya karibu kila siku, au mambo ambayo ulishawahi kuyapitia au mazingira ambayo ulishawahi kuyoana au kuwepo..

Kwahiyo katikati ya hayo yote, Ubongo wako utajiundia matukio na kuyachezesha akilini mwako wakati ukiwa umelala.

Biblia inasema hivi..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;….”

Umeona? Kwamfano ikiwa wewe kazi yako ni uvuvi na mara nyingi huwa unakesha baharini kuvua, kuota ndoto unajiona unavua au unatengeneza nyavu, itakuwa ni kitu cha kawaida kwako kujirudia rudia mara kwa mara, halikadhalika kwa  mpishi, au mwalimu, au mjenzi, kuota anafanya mojawapo ya ujuzi wake, litakuwa ni jambo la kawaida sana.

Vilevile katika hizo zipo ndoto ambazo zinaotwa na jinsia husika tu, kwamfano kuota unajifungua, hizi ndoto huwezi sikia zikiotwa na mwanaume, vivyo hivyo na kuota unatoka damu ya hedhi ni ndoto zinazowahusu wanawake peke yao, mwanaume hawezi kuota hivyo kwasababu jambo kama hilo hajawahi kulipitia katika Maisha yake yote,

Kwahiyo ndoto kama hii ikikujia isikusumbue sana. Elewa ni ndoto itokanayo na mazingira unayopitia.

Lakini pia jambo la pili ni kuwa.. Mungu anaweza kuzungumza na sisi, pia kwa njia hizo hizo za ndoto za mazingira yetu ya kila siku.

Kwamfano katika biblia utaona kulikuwa na wafungwa wawili waliokuwa gerezani na Yusufu, mmoja alikuwa anafanya kazi ya kumnywesha mfalme, na wa pili alikuwa ni mpishi. Siku moja wote wawili wakaota ndoto, na ndoto walizoota zililandana na mazingira yao ya kazi.. Lakini zilikuwa zimebeba ujumbe mzito kutoka kwa Mungu.

Mwanzo 40:5 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. 

6 Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika. 

7 Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo? 

8 Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie. 

9 Mnyweshaji mkuu akamhadithia Yusufu ndoto yake; akamwambia, Katika ndoto yangu nimeota, uko mzabibu mbele yangu. 

10 Na katika mzabibu mlikuwa na matawi matatu, nao ulikuwa kana unamea, unachanua maua, vishada vyake vikatoa zabibu zilizoiva. 

11 Na kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, nikampa Farao kikombe mkononi mwake. 

12 Yusufu akamwambia, Tafsiri yake ndiyo hii. Matawi matatu ni siku tatu. 

13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mnyweshaji wake……..

16 Mkuu wa waokaji alipoona ya kwamba hiyo tafsiri ni ya mema, akamwambia Yusufu, Mimi kadhalika nilikuwa katika ndoto yangu, na tazama, ziko nyungo tatu za mikate myeupe juu ya kichwa changu. 

17 Na katika ungo wa juu, mlikuwa na kila namna ya chakula kwa Farao, kazi za mwokaji; ndege wakavila katika ungo juu ya kichwa changu. 

18 Yusufu akajibu, akasema, Tafsiri yake ndiyo hii Nyungo tatu ni siku tatu..

Ukiendelea kusoma pale utaona ni kweli, mambo hayo yaliwakuta vilevile kama Yusufu alivyowatafsiria.

Unaona sasa “point” hapo ni kuwa walichoota kiliendana na kazi zao au mazingira yao ya kila siku, yule wa kwanza alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme akajiona anaweka divai mezani pa mfalme, kutoka katika mzabibu, ..Yule mwingine ni mpishi, aliona mikate kichwani pake.

Vivyo hivyo na wewe kuota unatoka damu ya hedhi, mara mara,  na tena kama ndoto hiyo inakujia kwa uzito Fulani basi ujue upo ujumbe mzito Mungu wa Mungu nyuma yake.. Na ujumbe huo unatoka kwenye biblia.

Sasa ipo Habari moja ambayo pengine ulishawahi kuisikia, lakini leo hii nataka uifuatilie tena kwa ukaribu. Habari yenyewe ni kuhusu yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa muda mrefu wa miaka 12. Tusome;

Luka 8:43  “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,

44  alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

45  Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.

46  Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.

47  Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.

48  Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani”.

Umeona mwanamke huyu, tatizo lililomsumbua kwa muda mrefu, lilimgharimu pesa nyingi, kwa waganga, halikuweza kutatuliwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa YESU TU PEKE YAKE.

Jiulize kwanini liwe ni kutokwa na damu, na si kingine?

Wewe unaota kutokwa na damu, jiweke katika nafasi ya huyo mwanamke, na ujue leo ni mahali gani sahihi pa kukimbilia.

Kama wewe hujaokoka, na unadhani dunia itakuwa ni jibu la Maisha yako, au utatuzi wa matatizo yako, leo hii ujue Mungu anasema na wewe kuwa  UMEMWACHA YESU APITE.

Mungu anakuonyesha YESU tu ndio jibu la Maisha yako, haijalishi wewe ni muislamu, au dini gani,..Ni Yesu tu pekee ndiyo kila kitu kwako. Na anachotaka tu ni ushike pindo la vazi lake, aiponye roho yako.

Maana ya Kushika pindo la vazi lake, ni kuonyesha kuwa unahitaji msaada, hivyo hapo ulipo kama Maisha yako yapo dhambini, basi tubu leo, mpe Bwana Yesu Maisha yako. Na atakupokea na ataiponya roho yako, na hata mwili wako ikiwa una matatizo.

Hivyo ikiwa upo tayari kutubu leo na kutaka akufanye kuwa kiumbe kipya, akuponye misiba yako, akupe tumaini jipya, hata kama wewe ni muislamu,  basi uamuzi huo ni wa busara sana. Hivyo fungua hapa  Kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Jiunge na kundi la whatsapp kwa kubofya chini;

Group la whatsapp  Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama masomo mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA?

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNACHEZA MPIRA.

Kuota unacheza mpira kuna maanisha nini kiroho?


Ndoto za namna hii kuwa zinakuja kutoka katika makundi mawili,

Kundi la kwanza ni kutokana na shughuli za kila siku.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”.

Kwamfano kuota unacheza mpira, asilimia kubwa ya ndoto hii huotwa na wanaume. Na hiyo ni kutokana na kwamba aidha mtu huyo kwa sasa anajishughulisha na mchezo wa mipira, au huko yumba alishawahi kucheza mpira, aisha shuleni au mitaani n.k..

Sasa ukiota ndoto ya namna hii mara kwa mara, basi huna haja ya kuwa na wasiwasi kwani ni ndoto tu, ambayo imekuja kutoka na shughuli za kila siku, Na hiyo inakuwa haina maana yoyote rohoni.

Kundi la Pili, ni kutokana na Mungu.

Lakini pia, ndoto kama hiyo inaweza kuja kwa namna ya kipekee sana, yaani kwa uzito usiokuwa wa kawaida, pengine ulikuwa unashindana sana kucheza, timu yako imezidiwa sana, au mmewazidi wale wengine sana, au wewe unacheza vizuri au vibaya kuliko wengine.. Kiasi kwamba ulipoamka  imekukaa sana akilini tofauti na ndoto ambazo ndoto ambazo unaotaga kila siku.

Basi ukiona hivyo lipo jambo Mungu anakukumbusha.

Kumbuka hapa dunia tupo katika mashindano, Na kila mmoja ni kama mchezaji, Na Lengo la mchezaji sikuzote ni kushinda tu, na sio kushindwa, ili mwisho wa siku akapokee medali ya dhahabu au kombe.

Biblia inasema..

1Wakoritho 9.24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Unaona, wewe kwa upande wako ulijiona unashiriki katika mchezo aina ya mpira, wengine wanaota wakikimbia riadha, wengine wakiogelea n.k.

Hivyo kuota unacheza mpira ni Mungu anakukumbusha kuwa upo kwenye mashindano ndugu. Sijui kwa upande wako maisha yako yapoje, kwasababu watu wengine Mungu anazungumza nao hata mara mbili au mara tatu, ili tu waelewe sauti ya Mungu..Lakini hawasikii. Soma hapa..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao”,

Hivyo kama wewe ni mmojawapo na bado upo nje ya Kristo, ni heri ukajitathamini vizuri tena. Kwasababu Yesu anao mpango mkubwa na wewe katika maisha yako haijalishi wewe ni muislamu na nani. Unachopaswa kufanya ni kumgeukia tu yeye uanze kushindana mashindano ambayo alikukusudia wewe ushindane ya kwenda mbinguni.. Kwasababu lipo taji bora alilokuandalia.

Si bahati mbaya ukutane na ujumbe huu. Hivyo usipuuzie, Mungu anakupenda, na anataka kukuokoa.

Ubarikiwe.

Fuatilia vichwa vingine vya masomo vilivyoainishwa chini ikiwa utahitaji kumjua Kristo zaidi.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEGANDA

SWALI: Shalom, nimekuwa na shida usiku nakuwa kama nimeganda siwezi kusogeza mkono au mguu au kuongea lakini akili nakuwa bado ninayo huwa nakemea inachukua muda kidogo naachiwa nashindwa kujua tatizo ni nini naomba nisaidie.


JIBU: Ndoto yoyote ambayo inakuja, na unajikuta katika mazingira ya kupambana na hali Fulani na huku unatumia jina la Yesu, ambapo mwanzoni inaonekana kuleta upinzani Fulani lakini baadaye inakuja kuachia kwa jinsi unavyozidi kuendelea kukemea ni ndoto yenye ujumbe kutoka kwa Mungu..

Wengine wanaota wanashindana na wachawi, na wale wachawi mwanzoni ni kama wanataka kumshinda lakini baadaye anawashinda kwa jina la YESU, wengine wanaota wamekutana na roho za mapepo, halafu kila alipolitaja jina la Yesu sauti, haitoki, lakini kwa jinsi alivyokuwa anaendelea kulitaja mwisho wa siku sauti inatoka na anayashinda.. Mwingine hata sio mapepo bali hali fulani ya udhaifu, kama hiyo ya kwako, unajikuta umeganda huwezi kusogeza kiungo chako hata kimoja, kila unapojaribu unashindwa, unajikuta unahitaji msaada kwa kulitaja jina la Yesu, na unapofanya hivyo mwanzoni ni kama inashindakana lakini baadaye inaachia hali hiyo  inaisha ghafla..

Zote hizo ni ndoto zenye ujumbe mmoja,..Ambao ni Mungu tu anakuonyesha SILAHA pekee ambayo inayoweza kukupa ushindi dhidi ya adui yako shetani, na silaha hiyo tayari umeshaijua ambayo ni jina la YESU. Hivyo ni kuongeza bidii ili uwe na mamlaka kamili juu ya jina hilo kuu.. (Kumbuka mamlaka hayaji kwa kulitamka tu kama ulivyoona kwenye ndoto, bali yanakuja kwa kumwelewa Yesu Kristo katika Neno lake, ndipo kutamka kwako kuwe na nguvu).

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.

Unaona hakuna lolote litakalokushinda, ikiwa maneno ya Mungu yatakuwa ndani yako kwasababu utakuwa umepewa mamlaka kamili na Kristo mwenyewe ya kushinda mambo yote..

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru’’.

Hivyo jitahidi kumjua Kristo zaidi, au ongeza  bidii, ili upokee mamlaka hayo kamili..Ndio ujumbe mkuu unaopewa hapo.

Vile vile sababu nyingine ya pembeni, ambayo unapaswa ujue katika ndoto kama hizo za kujikuta umeganda kitandani na huwezi kufanya chochote, ambapo wengine zinakuja katika uhalisia kabisa kana kwamba  sio ndoto, bali ni kitu halisi na wanajiona hawawezi kusogeza kiungo chao chochote kitandani, na anatamani hata mtu amsaidie kusogeza mkono wake  lakini hawezi kumwambia, na wengine wanasema amekufa lakini yeye anajiona bado ..Ni kwamba hapo Mungu anakuonyesha, hali halisi ya jinsi watu wanavyokufa, na  Kwamba yapo maisha baada ya kufa, sio kama wengine wanavyodhani, ukifa huelewi chochote, La, ukifa roho yako inaendelea kuishi inaondolewa katika mwili wako na kupelekwa mahali pengine..(Mhubiri 12)..

Hivyo siku ya kufa, kila mtu atajiona jinsi anavyotoka katika mwili wake na kwenda sehemu nyingine, na ataona pia wanaomzunguka jinsi anavyowaacha!.

Hivyo tunapaswa tujiulize , je! tumejiandaaje huko tuendako? Jibu lipo katika maisha ya kila mmoja jinsi anavyoishi.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KUOTA NYOKA.

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

WAKATI WA JIONI KUTAKUWAKO NA NURU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

Kuota mtu amekufa au ndugu amekufa.


Wakati mwingine unaweza ukaota umefiwa na mzazi, au kaka au dada, au mtu wako wa karibu sana. Na ndoto hizi huwa zinakuja kwa uzito sana, kiasi kwamba unaposhtuka huamini kama kweli ilikuwa ni ndoto, kwasababu unaona kama tukio hilo lilikuwa ni halisi kabisa..unabaki kuishia  kumshukuru Mungu na kusema asante  kwa kuwa ilikuwa ni ndoto tu..

Ndoto kama hizi huwa zinawapata watu wengi, na kama haijawahi kukutokea, basi itakuja kukupata siku moja katika maisha.. Lakini fahamu kuwa ni Mungu  hapo anakukumbusha hatma ya maisha yako na ya ndugu zako itakavyokuwa..kwamba siku moja wataondoka duniani, sio lazima wafe kwa njia hiyo hiyo uliyoiona kwenye ndoto hapana bali inaweza ikaja kwa njia yoyote lakini lakini kitendo ni kile kile kifo..

Vilevile inaweza ikawa ni hivi karibuni, au isiwe hivi karibuni pengine baada ya miaka 5 au 10 au hata 50 lakini ujumbe ni ule ule, kifo kinakuja.

Hivyo ni wajibu wako kufanya mambo mawili makuu juu ya maisha ya ndugu zako angali wakiwa bado hai,

  • Kwanza: Ni kwa kuwahubiria habari njema za wokovu, wamrudie Mungu kama hawajaokoka..
  • Na pili: Ni kuwaombea maisha yao hapa duniani yawe ni ya kumcha Mungu na Mungu awaepusha na njama za Yule adui.

1Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka.”

Unaona Nabii Samweli hakuacha kuiombea Israeli japokuwa ilikuwa inamchukiza Mungu kwa sanamu zao, lakini alikuwa akidumu katika kuwaombea..aliwaombea kwa bidii sana, na akahesabu kwamba ni dhambi kuacha kuwaombea ndugu zake,…na pia akawa anawaonya..hata Musa naye kule jangwani ni mara nyingi Mungu alitaka kuwaangamiza wana wa Israeli kwa matendo yao maovu lakini kwa maombi ya Musa Mungu alighahiri mabaya yao.

Hivyo na wewe ikiwa upo ndani ya Kristo ni rahisi Mungu kusikia maombi yako na Mungu akawaweka katika mstari sahihi ikiwa utaendelea kuomba kwa bidii juu yao bila kukata tamaa, na vile vile Mungu atawaepusha na mabaya na njama nyingi za ibilisi ziliyopangwa kinyume chao, ikiwemo vifo ambavyo sio vya wakati.

Lakini kama upo nje ya Kristo, hakuna dua yoyote itakuwa rahisi kwa ndugu zako. Hivyo nakushauri umpe Bwana Yesu maisha yako leo, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha na kuwa tayari kumfuata yeye kwa moyo wako wote ili Bwana akuokoe kwanza wewe, ndipo iwe rahisi kusikia maombi yako kwa wengine.. Yesu sio wa watu wa dini Fulani tu, hata kama wewe ni muislamu, kimbilio lako ni YESU tu, wala hakuna mwingine..Yeye ndiye anayekuahidi uzima wa milele, yeye pekee ndio anayetoa faraja ya kweli ukiwa kwanza hapa duniani, na hata utakapofika kule..

Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi hapo

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa kuukamlisha wokovu wako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Au jiunge Whatsapp hapa

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

https://chat.whatsapp.com/GBX2lWIcoCq8zmlnXJgaWQ

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unafanya Mtihani.

KUOTA UNAPAA.

USIKIMBILIE TARSHISHI.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post