Title namna ya kuomba

Fahamu Namna ya Kuomba.

Wengi wa wanaompa Yesu Kristo maisha yao kwa mara ya kwanza, ndio maswali ya kwanza kwanza kujiuliza…nitaombaje! namna gani ya kuomba ili Mungu anisikie!

Kiuhalisia hakuna fomula fulani maalumu ya kuomba wala chuo fulani maalumu cha kujifunzia kuomba, Kwasababu Mungu wetu si mwanadamu wala hana udhaifu wa kutuelewa…Sehemu nyingine katika maandiko inasema “Baba yetu wa mbinguni anajua tujayohitaji hata kabla sisi hatujamwomba”

Unaona? kwa sentensi tu hiyo inaonesha kuwa Mungu si dhaifu wa kutuelewa sisi, kiasi kwamba tunahitaji course fulani tukasome ndipo atuelewe au kutusikia. Kitendo cha Kuwa mwanadamu tu! tayari Mungu anakuelewa kuliko unavyojielewa.

Hivyo mbele za Mungu, hatuendi na mpangilio mzuri wa Maneno kama tunavyoandaa hotuba kwenda kuisoma mbele za Mkuu wa Nchi…Isipokuwa tunakwenda na hoja zenye nguvu...Na hoja hizo ndio zile Bwana alizotufundisha wakati wa kuomba..katika Mathayo 6

“9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

11 Utupe leo riziki yetu.

12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina”.

Kwamba tuombapo tuhakikishe tunaomba toba, na pia tuhakikishe nawasamehe wengine ili na sisi pia tusamehewe…Kadhalika tunapoomba tuhakikishe tunalitukuza jina la Yesu, na pia tunaomba ufalme wake uje…Na pia tusisahau kusema mapenzi yake yatimizwe…kwasababu sio kila kitu tunachokiomba ni mapenzi ya Mungu…Pia tunapaswa tumwombe Mungu atupe riziki zetu za kila siku, kama chakula, mavazi, malazi pamoja na fursa.

Kadhalika tunamwomba asitutie majaribuni hiyo inahusisha kumwomba Bwana atuepushe na yule mwovu katika maisha yetu, imani yetu, familia zetu, kazi zetu, huduma zetu za kila siku za kuwaleta watu kwa Kristo, tunazungukwa na nguvu za yule adui kila mahali, hivyo ni muhimu kumwomba Bwana atuepushe na mitego yake yote.

Na bila kusahau kurudisha utukufu, na kutambua kuwa uweza, nguvu na mamlaka vina yeye milele na milele…Hivyo hakuna kama yeye, na yeye ndiye mwanzo na mwisho.

Hizo ndio hoja zenye nguvu…usitazame ni maneno kiasi gani umekosea kuongea, wala ni lugha gani umezungumza wakati wa kuomba, hakikisha tu maombi yako yanahusisha hivyo vipengele.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

FAIDA ZA MAOMBI.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Maandiko yanasema Eliya aliomba kwa bidii hadi akasimamisha mvua kunyesha kwa MUDA wa miaka 3 na nusu.(Yakobo5:17) Je! kuomba kwa bidii ni kuomba kwa namna gani?

JIBU: Tusome:

Yakobo 5:17 “Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.” 

Kwakuwa habari hii inamzungumzia Eliya hivyo ili kuelewa vizuri hiyo bidii aliyokuwa nayo ni vizuri tukarejea kwenye tukio halisi lenyewe ili tuone ni jinsi gani aliomba. Sasa ukiangalia vizuri utaona biblia haijatoa maelezo mengi juu ya maombi aliyoyaomba siku ile alipozuia mvua. Inaonyesha tu Eliya akitokea kwenye tukio na kuzungumza maneno yale na kuondoka,

 1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.

2 Neno la Bwana likamjia, kusema,

3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.

 Lakini siku ile anarudi, ili kuifungua tena mbingu kwa Neno la Mungu, tunaona halikuwa ni jambo la kutamka na kuondoka tu kuna vitu viliendelea pale embu Tusome:

1Wafalme 18:41 “Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele.

42 Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.

43 Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akanena, Enenda tena mara saba.

44 Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie.

45 Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli.” 

Hapo unaweza ukajifunza mambo kadhaa, cha kwanza Eliya kabla hata hajamwomba Mungu, alishaamini kuwa mvua inakwenda kunyesha siku hiyo katika nchi, na ndio maana alikuwa na ujasiri wa kumwambia Mfalme Ahabu inuka unywe kwani pana sauti ya mvua tele.

Pili alipoonenda magotini sasa ili kumwomba Mungu jibu lake halikuja ndani ya wakati alioutazamia pengine aliomba lisaa la kwanza, akitazamia kabla hata hajamaliza juu kutakuwa kumeshafunga, lakini Yule mtumishi wake alipoenda alirudisha repoti kuwa juu hakuna dalili yoyote ya mvua kunyesha, lakini aliendelea kukaa uweponi mwa Bwana akimshukuru kwa matendo yake makuu, lisaa lingine likapita akamwambia mtumishi wake haya nenda katazame tena, akarudi akasema hakuna kitu, ikaendelea hivyo hivyo lisaa la tatu, la nne, mpaka lisaa la 7 pengine, akamwambia nenda katazame usichoke, ndipo Yule mtumishi wake akarudi akasema ninaona kawingu kadogo kama cha mkono wa mtoto mchanga, Ndipo Eliya alipoacha kuomba akijua kuwa tayari imekwisha kuwa..

Na kama ingetokea hakuna kitu chochote kilichotokea ni wazi kuwa angeendelea hivyo hivyo hata mara 20 au 50, au 100 kwa nguvu ile ile akijua kuwa Mungu ameshamsikia..Huko ndiko kuomba kwa BIDII ambapo hata sisi tunapashwa tuwe nako, Ni rahisi kumwamini Mungu tunapompelekea mahitaji yetu lakini kudumu uweponi Mwake hatuwezi pale tunapoona majibu yanachelewa kidogo, hayajaja ndani ya wakati tuliotuzamia..Tunaanza kumtilia Mungu mashaka pengine hajatusikia. Lakini tukiendelea kushikilia na kumwamini Mungu kuwa ameshatenda, hata kama itapita siku, wiki, mwezi, miaka, ukizidi kushikilia nakwambia milango yote itafunguka mbele yetu. Hivyo kwa ufupi kuomba kwa bidii kunakozungumziwa hapo ni Kukaza kumwamini Mungu mpaka majibu yanapotokea. 

Ubarikiwe sana.


Mada Nyinginezo:

ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?

UFUNUO: MLANGO WA 11

KUNA TOFAUTI GANI KATI YA SALA NA DUA?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

VITA DHIDI YA MAADUI

TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;


Rudi Nyumbani:

Print this post

FAHAMU KURUDI KWA YESU KUKO KWA NAMNA NGAPI?

Wengi, tumeshasikia kuwa Yesu atarudi, lakini mpaka mtu anasema atarudi, maana yake ni kuwa alishawahi kuja hapo nyuma. Na kama tunavyojua Bwana wetu Yesu Kristo alikuja mara moja tu, miaka karibu elfu mbili iliyopita, akaishi, akafa,akazikwa, akafufuka, akapaa mbinguni. Lakini wakati wote alipokuwa hapa duniani aliwaahidi wanafunzi wake kuwa atarudi tena.

Hivyo somo hili, ni muhimu kufahamu,  namna ambazo Yesu alisema atarudi, ili usikose maarifa, kwasababu wengi hapa wanakosa shabaha katika kutambua kauli za Yesu. Naomba Soma kwa utulivu somo hili mpaka mwisho.

Sasa kuhusu kurudi kwake duniani, alizungumza katika nyakati tofuati tofauti kurudi kwa namna mbili.

  1. Namna ya kwanza, ni kama Roho
  2. Namna ya pili ni kama Mwizi

Tuangalie kwa undani, namna hizi mbili. Husasani tutailenga hiyo ya pili.

Je! ni kwa namna gani, alirudi kama Roho,Aliwaambia hivi mitume wake;

Yohana 14:18  “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19  Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.

20  Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.

Soma pia, katika Yohana 16:16, amerudia maneno hayo hayo,

Unaona? Mitume walidhani hawatamwona tena, lakini siku ile aliyopaa mbinguni,siku kumi baadaye, biblia inasema walikuwa wamekusanyika wote mahali pamoja, akawajilia Roho Mtakatifu akawakalia wote, wakajazwa Roho Mtakatifu. Na kama tunavyojua tangu huo wakati na kuendelea, kila mmoja alijua anaye Yesu moyoni mwake, hakuna mtu aliyeuliza Yesu yupo wapi.

Uyatima uliondoka kabisa, kabisa, ndipo wakatambua maana ya yale maneno. Hivyo tumeshaona kurudi kwake kwa kwanza duniani, kulikuja kwa namna hiyo ya Roho Mtakatifu, na mpaka sasa Kristo yupo ndani ya mioyo ya waliomwamini, na kupokea Roho Mtakatifu.

Lakini pia katika maneno yake mengine, alisema atarudi kama mwizi.

Soma,

Mathayo 24:43  Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44  Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

Unaona tena?, Hajasema, atarudi kama askari, au mfanya biashara, bali kama mwizi. Sasa ni vema tujue sifa za mwizi, ni zipi kibiblia, ndipo tuelewe jinsi kurudi kwake kwa namna hiyo kutakavyokuwa.

Ukisoma Yohana 10:10  Yesu anasema hivi;  Mwivi haji ila AIBE na KUCHINJA na KUHARIBU; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”.

Kumbe mwizi hasaa, anayezungumziwa ni mfano wa jambazi, na sio wale wadokozi, ni wale wanaobeba silaha, ili kuharibu na kuua wanaowaona, wachukue mali yao waondoke.

Na Yesu ndivyo atakavyokuja katika siku za mwisho hizi, atatimiza sifa hizo zote tatu.

1.) Jambo la kwanza Atakuja saa tusiyodhani, Kisha ATAIBA kitu chake cha thamani duniani. Ni hicho si kingine zaidi ya watakatifu wake. Hapo ndio suala la unyakuo linapoibukia.

Mathayo 24:40  Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; 41  wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

2) Lakini pamoja na hilo, kuja kwake kutaambatana na KUCHINJA.

Maana yake ni kwamba, kama unyakuo utakupita, dunia itakuwa inajiandaa kuingia katika siku ile ya mapigo ya ghadhabu ya Mungu, ambayo mwisho wake utaishia na Kristo kuonekana katika umbile la kibinadamu kabisa, kuwaua mataifa yote ambayo yatakusanyika kupigana naye katika ile vita kuu ya Harmagedoni.

Ufunuo 19:11  Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12  Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13  Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14  Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15  NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16  Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.

Huu ni wakati ambao Yesu, atauangamiza  ulimwengu, mfano wa mwizi, asiyekuwa na huruma. Usitamani uwepo wakati huo ndugu, ni majuto vilio na kusaga meno.

3) Lakini mwisho kabisa, ATAHARIBU.

Tunafahamu kuwa mwizi, huvunja, mahali ili aingie, huvuruga kila kitu anachokiona, vivyo hivyo na hii dunia itafumuliwa yote, mifumo yote itaangushwa, itafinyangwa upya, yote hayo yatatokea katika siku hiyo hiyo ya Bwana, ambayo itaharibu kila kitu.

2Petro 3:10  Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11  Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12  mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?

Soma pia,(Ufunuo 16:17-21), kuongeza maarifa..

Hivyo ndugu, wakati huu wa Yesu kurudi kama mwizi umekaribia sana, ambao utaanza  Kwanza kwa tukio la unyakuo. Bwana anatutaka sisi tukeshe(rohoni), asitukute tumelala. Ili Siku hiyo isitujilie ghafla, tukabaki hapa duniani.

1Wathesalonike 5:1  Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

4  Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

5  Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

6  Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

7  Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8  Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

Bwana atupe macho ya kuona haya.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako, Je! Ameziondoa dhambi zako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Hujui kesho kama utakuwepo, hujui kama leo atarudi. Hivyo tubu sasa, mwamini Yeye upate ondoleo la dhambi zako, kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Ikiwa utapenda kupokea wokovu basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure. Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.

Kuna tofauti gani kati ya “Mwivi” na “Mwizi”?

Fahamu Namna ya Kuomba.

Rudi Nyumbani

Print this post

Roho ya Malipizi/ roho za malipizi ni nini?

Swali: roho za Malipizi ni nini na mtu anawezaje kuzifunga?


Jibu: roho ya Malipizi au roho za malipizi ni roho zinazojilipiza kisasi baada ya kushindwa vita.

Maandiko yanasema vita vyetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka za giza katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.

Sasa hizi roho za mapepo na za wakuu wa giza, zinaposhindwa vita dhidi ya mtu, au watu, au kanisa basi, huwa zina tabia ya kukimbilia kutafuta sehemu nyingine iliyo dhaifu ya huyo mtu, au watu au kanisa na kushambulia ili kumwumiza yule aliyekuwa anashindana nazo.

Tuchukue mfano, mtu mmoja aliyeokoka ameomba kwaajili ya familia yake (Labda kwajili ya Mke wake au Mume au watoto), na katika kuomba kwake, ameomba ulinzi, na neema ya kumjua Mungu, na Zaidi sana amezikemea roho zote zinazopambana na familia yake, (roho za kurudi nyuma, roho za magonjwa na matatizo mengine) na amezishinda kwa maombi na kuziadhibu sawasawa na 2Wakorintho 10:6.

Sasa roho hizo (za mapepo na wakuu wa giza) zinapoanguka na kushindwa namna hiyo, huwa zina tabia ya kulipiza kisasi…kwa wakati huo zinaondoka na kwenda kutafuta sehemu nyingine ya maisha ya huyo mtu zilizo dhaifu na kuzivamia au kufanya nazo vita kutokana na uchungu na hasira za kushindwa..

Ndio hapo zitaacha kushughulika na familia ya huyo mtu kwa muda, na kwenda kupiga marafiki wa karibu wa huyo mtu, au wazazi, au watu wengine wowote walio wa muhimu katika maisha ya huyo mtu, lengo ni ili kumwumiza huyo mtu au kumsumbua na zinaweza kwenda kupiga kwa magonjwa, hasara au hata mauti kabisa..

Hivyo ni muhimu sana kumalizia maombi kwa kuomba ulinzi kwa watu wote walio karibu nawe ili wazidhurike na ghadhabu za hizo roho.

Hiyo siku zote ndio tabia ya shetani na majeshi yake, “kujilipiza kisasi”

Sasa  pengine utauliza ni wapi katika biblia jambo kama hilo limetokea?..tusome maandiko yafuatayo..

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8  nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9  Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

11  Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

12  Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! KWA MAANA YULE IBILISI AMESHUKA KWENU MWENYE GHADHABU NYINGI, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”.

Umeona hapo mstari wa 12, maandiko yanasema yule ibilisi aliposhindwa alitupwa chini mwenye ghadhabu nyingi, na anashuka kujilipiza kisasi kwa kufanya vita na hao wakaao juu ya nchi na bahari kutokana na kushindwa kwake vita mbinguni. Na hapa tumeshapata jibu kwanini shetani anafanya vita na sisi wanadamu?.. sababu si nyingine Zaidi ya kisasi alichonacho, lakini ashukuriwe Kristo YESU Bwana wetu yupo katika mkono wa kuume akituombea (Warumi 8:34) .

Lakini tukizidi kusoma maandiko hayo mpaka ule mstari wa 17  bado tunaendelea kuona kisasi cha shetani baada ya kushidwa tena vita dhidi ya yule ya yule mtoto (YESU KRISTO) na dhidi ya yule mwanamke (Israeli).

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14  Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15  Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16  Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17  Joka akamkasirikia yule mwanamke, AKAENDA ZAKE AFANYE VITA JUU YA WAZAO WAKE WALIOSALIA, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Umeona tena hapo?.. baada ya Ibilisi kumshindwa “mtoto na yule mwanamke” anapanga tena malipizi juu ya uzao wake, hiyo yote ni kuonyesha roho mbaya ya kisasi aliyonayo adui.

Vivyo hivyo, mpaka leo hiyo roho anayo pamoja na mapepo yake, yakishindwa vita yanaenda kutafuta wengine kumalizia hasira zao, kwahiyo ni muhimu sana pia kuomba maombi ya kufunga na kuzuia hizo roho zisiende kuleta madhara sehemu nyingine ya maisha ya watu unaohusiana nao!.

Na huu ndio umuhimu wa kuwaombea wengine, na pia ndio umuhimu wa kuomba.. Usipokuwa mwombaji na kusubiri kuombewa tu mara kwa mara, upo katika hatari ya kuvamiwa na maroho ya malipizi kutoka katika kila kona (kutokana na maombi ya wengine) endapo hawatafunga hizo roho. Kwahiyo ni muhimu sana kuomba na kuwaombea wengine.

2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

USILIPIZE KISASI.

UFUNUO: Mlango wa 12

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Rudi nyumbani

Print this post

Roho ya Umasikini ni nini na inatendaje kazi?

Swali: Roho ya umasikini ipoje na inatenda kazi kwa namna gani, na inawezaje kumtoka mtu?


“Roho ya umasikini” ni roho inayomshusha mtu kiuchumi, hata kumfanya asifike kule anakotaka kufika kimaendeleo.

Roho hii inapomvaa mtu inamfanya wakati mwingine awe katika hali ya mahitaji kupindukia na hata kuwa katika hali ya madeni mazito.

Kibiblia watu wa Mungu umasikini si sehemu yao.. Ingawa kuna vipindi ambavyo Mungu anaweza kumpitisha mtoto wake kuonja umasikini kwa muda ili kumfundisha baadhi ya mambo, ambayo yatamfaa baadaye atakapobarikiwa.

Na urefu wa kipindi hicho cha madarasa ya Mungu kinategemea mtu na mtu. Wapo ambao watadumu katika hiko kipindi kwa muda mrefu kidogo lakini baadaye watatoka huko, na wapo ambao watadumu katika kipindi kifupi na baadaye watatoka huko na kupewa pumziko la faraja ya Bwana.

Lakini kwa ujumla Mkristo hajapewa umasikini wa kudumu kama sehemu maisha yake…au labda mtu huyo atake mwenyewe kujifanya maskini kwa nafsi yake au kwaajili ya Bwana.

Mtu anayejifanya maskini kwa ajili ya Bwana ni yule ambaye Mungu anamfungulia milango ya kupata vingi lakini kila anachokipata anakitoa na hivyo muda wote anakuwa katika hali ya kutokuwa na vingi…(Mtu wa namna hii ni maskini ingawa ni tajiri).

Mtu huyu anakuwa hawezi kuona furaha au Amani akiwa na viwili wakati mwingine hana hata kimoja. Mtu wa namna hii anakuwa anajifanya mwenyewe maskini kwaajili ya Bwana na kwa taji yake mbinguni, ikiwa anafanya hivyo kwa dhamiri njema na si kama sheria.

Mfano wa watu waliojifanya wenyewe kuwa maskini ingawa wangeweza kuwa matajiri ni Yohana Mbatizaji na BWANA WETU YESU KRISTO.

2Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Na pia wapo ambao walikuwa matajiri na wakadumu na utajiri wao, mfano wa hao ni Ibrahimu na Ayubu..

Sasa hakuna agizo lolote maalumu katika biblia kuwa ni sheria tujifanye kuwa maskini, kama alivyokuwa Bwana au Yohana Mbatizaji,  mtu akijifanya hivyo basi iwe kwa nafsi yake na Mungu wake, na si amri wala agizo.

Lakini pamoja na hayo, upo umaskini mwingine ambao hauletwi na Mungu bali unaletwa na adui shetani. Mara nyingi umasikini huu ni ule unaompata mtu anapokuwa nje ya KRISTO (Maana yake hajaokoka).. au aliyeokoka lakini amepungukiwa na baadhi ya Maarifa ambayo yangemsaidia kusogea kimaisha.

Sasa ni njia gani za kushughulika na roho ya umaskini unaoletwa na adui shetani?

     1. KUOKOKA

Unapookoka kikweli kweli kwa kumaanisha, basi roho zote za adui zinazochochoe na kutengeneza umaskini maishani mwako zinaondoka, na hivyo maisha yako kutengenezeka upya kama yalikuwa yameshaharibiwa na pepo la umasikini.

     2. KUOMBA

Maombi ni silaha tosha kwa kila mwamini, na maombi ni ULINZI, Kama umeshuhudiwa kuwa hali unayopitia sio ya kawaida na wala haitokani na MUNGU, basi ni wakati wa kuingia vitani katika maombi, kuvunja na kukemea kila roho yote inayotaka kujiinua kinyume na maendeleo yako.

    3. PATA MAARIFA.

Kama umeshaokoka na tena ni mwombaji sana lakini bado unaona hali hiyo ya umasikini inadumu muda mrefu, basi huenda Mungu kashakufungulia milango mbele yako ili upige hatua, lakini milango hiyo huioni aidha kutokana na kupungukiwa na MAARIFA, sawasawa na Hosea 4:6.

Hivyo tia bidii katika kutafuta maarifa ya jinsi ya kujiendeleza mbele kupitia kanuni za kibiblia. (Soma sana biblia, na pia sikiliza mafundisho mbalimbali kutoka kwa watumishi wa kweli wa Mungu yahusuyo namna ya kujiendeleza, vile vile ongeza ujuzi katika kile ukifanyacho).

Kupitia njia hizo tatu basi utaweza kujifungua kutoka katika kifungo cha umasikini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

UKITAKA KUMFUATA YESU NI SHARTI UACHE VYOTE!

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Kuota unakabwa, mara kwa mara ni ishara ya nini?

SWALI: Mimi kila nikilala, huwa kuna kitu kinanikaba koo, nakosa pumzi, kinanikandamiza naona kama nakwenda kufa au wakati mwingine ninaganda muda mrefu siwezi kusogea. Hata nikijaribu kukemea, natumia kushindana sana, baadaye kinaniachia, Je hili ni jinamizi?. Jambo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kufunga na kuomba zinaweza pita tu  siku kadhaa halafu kikajirudia tena. Naomba msaada nifanye nini?


JIBU: Hayo ni mashambulizi ya adui ndotoni. Tufahamu kuwa adui hashambulii tu katika mwili, lakini wakati mwingine pia katika ndoto. Wapo watu wanaosumbuliwa na shetani husasani katika maeneo ya ndoto.

Utakuta kila anapolala, ni mfululizo tu wa ndoto za kipepo, labda anafukuzwa-fukuzwa, au anazini-zini na mapepo hayo, au yupo makaburini, anafanya mambo ya kichawi, zaidi wengine zinakuwa ni mwendelezo, yaani pale alipoishia jana, leo anaendelea nazo sehemu ya pili, kila anapolala hana raha, kwasababu anajua vitisho ni vilevile anakwenda kukutana navyo. Wengine mpaka inazidi wanasikia sauti kabisa za mapepo, zikiwasemesha, au wanaona vitu vya ajabu vikipita mbele yao, na hiyo yote hutokea pindi tu wanapopitiwa na usingizi kidogo, haijalishi mchana au usiku. Kundi lingine ndio hili ambalo wanaona kama wananaswa, na kitu Fulani pumzi haitoki, wanaishia kutaabika. N.k.

Sasa, unapokutana na mojawapo ya shida, hizo au mashambulizi hayo ndotoni. Jambo la kwanza ‘hupaswi kuogopa’ Fahamu suluhisho ni moja tu nalo ni YESU KRISTO. Lakini wengi hawajui ni kwa namna gani.

Mambo haya matatu (3), yaelewe yatakusaidia..

1) Tumia jina la Yesu.

Unapojikuta kwenye mashambulizi hayo, usiwe tu bubu. Hakikisha unalitumia jina la YESU kukemea. Kuyadhibiti hayo mapepo na kazi zao. Kwasababu mamlaka hiyo umepewa.

Mathayo 10:19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Lakini ukiona unasumbuliwa na hizo ndoto, halafu unapambana mwenyewe mwenyewe, huna silaha yoyote mkononi mwako, jiandae kukugeuza wewe  kuwa ndio kijiwe chao. Vaa silaha za vita. Jina la Yesu ndio silaha yetu kuu, kutiisha nguvu zote za Yule mwovu.

2) Jiweke vema nafsini, kabla hujalala.

Penda kuwa mwombaji kabla hujalala, usilale tu bila kumkabidhi Bwana usiku wako. Lakini pia hakikisha moyoni mwako, huna makunyanzi ambayo shetani atapata sababu ya kukushitaki. Unajua ni kwanini biblia inasema maneno haya?

Waefeso 4:26  Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27  wala msimpe Ibilisi nafasi

Ni kwasababu shetani hupenda mipenyo kama hiyo, kwamfano moyoni mwako una vinyongo na wenzako, una hasira na jirani zao, mambo kama hayo, husababisha adui kukushambulia kwa njia yoyote nyakati za usiku. Hivyo ukabidhi moyo wako kwa Bwana.

3) Zidisha Imani.

Ikiwa mambo hayo mawili unayafanya, lakini bado unaona mashambulizi, yanaendelea. Basi tatizo kubwa kwako lipo kwenye IMANI.  Imani yako ni chache. Upo wakati mitume walipambana na mapepo wakashindwa kuyatoa. Baadaye wakamuuliza Bwana mbona sisi tulishindwa? Yesu akawaambia ni kwasababu ya upungufu wa imani yenu. Hata leo hii ukiona mkristo unasumbuliwa sana na vibwengo, na vipepo. Ujue pia imani yake bado haijawa imara.

Kwa namna gani?

Bado hujaamini vya kutosha nguvu iliyopo ndani ya JINA LA YESU. Na ushindi ulipoupata kupitia Kristo Yesu moyoni mwako. Unachopaswa kufanya ni kumwamini Yesu asilimia mia alimaliza yote msalabani, uwe jasiri, ondoa hofu, vipepo ni vinyago tu, havina chochote cha kukubabaisha wewe. Ukiona hiyo hali inakuja wewe kuwa  ujasiri na Imani yote, usiope kitu. Kemea. “Sema wewe pepo, mimi nimekombolewa na Yesu, huna uwezo wa kushindana na Roho Mtakatifu aliye ndani. Na sasa nisikilize, kuanzia sasa hili sio hekalu lako. Kwa mamlaka ya kifalme iliyo ndani ya jina la Yesu Kristo mwokozi wangu, nakuamuru toka na kwamwe usirudi hapa tena”.

Ukiwa na ujasiri unaotokana na imani ya Bwana unayemtumikia. Nakuambia pepo hilo litabadili uelekeo mara moja, hata likija kujaribu mara nyingine likakukuta na msimamo wako huo huo, hakuna hofu ndani yako. Ndio bye! bye! Halitakaa lirudi tena itakuwa ni historia.

Kumbuka Samsoni alipokutana na Yule Simba, yeye alimwona kama ni “mzinga” tu uliomletea asali. Hivyo akalirarua, na ndio maana baadaye akaja akakuta asali ndani yake akala akaondoka. Kwasababu alijua nguvu zilizo ndani yake, zinatuliza pepo na bahari, na milima  simbuse hichi kisimba-mbarara kinachonguruma hapa mbele yangu.

Na wewe vivyo hivyo, usiishi kinyonge-nyonge tu, unakubali kunyanyaswa nyanyaswa na hivyo vipepo ambavyo havina kitu kwako kama vile huna mtetezi hapa duniani.. KEMEA! KWA IMANI, na Ujasiri. KAZI ITAKUWA IMEISHA!. Wala usitafute maombezi.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

IMANI “MAMA” NI IPI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

KUOTA UPO MAKABURINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini tunafunga na kuomba?

Kanuni ya kufunga na kuomba inafananishwa na kanuni ya Kuku kuyaatamia mayai yake mpaka kufikia hatua ya kutotoa vifaranga.

Ili mayai yaweze kuanguliwa na vifaranga kutokea ni lazima Kuku ayaatamie mayai kwa siku 21, na ili aweze kuyaatamia kwa mafanikio, basi hana budi kujizuia kula kwa kipindi kirefu ili asipoteze joto la mayai yale. Ndio hapo utaona itampasa atoke mara chache chache kwenda kutafuta chakula kisha kuyarudia mayai yake, na atafanya hivyo kwa siku zote 21.

Maana yake kama kuku hatajiingiza katika hiyo adhabu ya kuutesa mwili wake na kujizuia na milo kwa siku 21, hawezi kupata vifaranga!.

Vile vile kuna mambo ambayo yanahitaji “Joto la kiroho” kwa siku kadhaa za MIFUNGO na MAOMBI na KUJITESA. Ili tuweze kuyapata…Vinginevyo hayatatokea kabisa haijalishi tutayatamani kiasi gani!.

Bwana YESU alisema mambo mengine hayatoki pasipo Maombi na Mifungo..

Mathayo 17:21  “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”

> Ukiona umejaribu kutafuta kitu na hujakipata, ingia kwenye mfungo!

> Ikiwa umeomba na bado hujapata, ongezea na mfungo juu yake!.

> Ikiwa umetafuta na hujapata ongezea na mfungo wa maombi juu yake!.

> Ikiwa unataka Amani, Furaha, au Nguvu za kuendelea mbele, usikwepe mfungo! N.k

Ukiwa ni mtu wa kuomba pamoja na kufunga, utakuwa ni mtu wa mafanikio kiroho na kimwili. Utaangua vingi kwa wakati.. Lakini ukiwa ni mtu wa kukwepa mifungo basi utatumia nguvu nyingi sana kupata baadhi ya mambo.

Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka KWA MAOMBI, na dua, PAMOJA NA KUFUNGA, na kuvaa nguo za magunia na majivu.……………………….

21 naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni.

22 Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danielii, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu.

23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya”.

Na kuna Toba nyingine zinahitaji Mfungo kabisa ili mtu aweze kufunguliwa.

Yoeli 2:12 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya”.

Usikwepe mifungo!

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

IJUE FAIDA YA KUFUNGA PAMOJA NA WANYAMA WAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia

AGANO LA KALE

Vitabu vya Agano la Kale vimegawanyika katika makundi makuu manne (4)

      1. VITABU VYA SHERIA. (Tazama jedwali chini).

JINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGO/SURAMAJIRA YA UANDISHI
1.MWANZOMUSA50Jangwani
2.KUTOKAMUSA40Jangwani
3.MAMBO YA WALAWIMUSA27Jangwani
4.HESABUMUSA36Jangwani
5.KUMBUKUMBU LA TORATIMUSA34Jangwani

     2. VITABU VYA HISTORIA (Tazama Jedwali chini).

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.YOSHUAYoshua24Kaanani
2.WAAMUZINabii Samweli21Israeli
3.RUTHUNabii Samweli4Israeli
4.1SAMWELINabii Samweli31Israeli
5.2SAMWELIEzra (Mwandishi)24Israeli
6.1WAFALMEYeremia (Nabii)22Israeli
7.2WAFALMEYeremia (Nabii)25Israeli
8.1NYAKATIEzra (Mwandishi)29Uajemi
9.2NYAKATIEzra (Mwandishi)36Uajemi
10.EZRAEzra (Mwandishi)10Israeli
11.NEHEMIANehemia13Israeli
12.ESTAMordekari10Shushani Ngomeni(Uajemi)

     3. VITABU VYA MASHAIRI (Tazama Jedwali chini).

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.AYUBUMusa42Jangawani
2.ZABURI Daudi, Sulemani, Wana wa Asafu,Ethani, Hemani, Musa, wana wa Kora na wengine wasiotambulika.150Israeli
3.MITHALISulemani31Yerusalemu (Israeli)
4.MHUBIRISulemani12Yerusalemu (Israeli)
5.WIMBO ULIO BORASulemani8Yerusalemu (Israeli)

    4. VITABU VYA MANABII WAKUBWA (Tazama Jedwali chini).

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.ISAYAIsaya (Nabii)66Israeli
2.YEREMIAYeremia (Nabii)52Israelil (Yerusalemu)
3.MAOMBOLEZOYeremia (Nabii)5Misri
4.EZEKIELIEzekieli (Nabii)48Babeli
5.DANIELIDanieli (Nabii)12Babeli

     5. VITABU VYA MANABII WADOGO (Tazama jedwali chini).

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.HOSEAHosea (Nabii)14israeli
2.YOELIYoeli (Nabii)3israeli
3.AMOSIAmosi (Nabii)9israeli
4.OBADIAObadia (Nabii)1israeli
5.YONA Yona (Nabii)4israeli
6.MIKAMika (Nabii)7israeli
7.NAHUMUNahumu (Nabii)3israeli
8.HABAKUKIHabakuki (Nabii)3israeli
9.SEFANIASefania (Nabii)3israeli
10.HAGAIHagai (Nabii)2israeli
11.ZEKARIAZekaria (Nabii)14israeli
12.MALAKIMalaki (Nabii)4israeli


         AGANO JIPYA

Vitabu vya Agano jipya vimegawanyika katika makundi makuu matano (5)

    1. VITABU VYA INJILI (Tazama jedwali chini)

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.MATHAYOMathayo (Mtume)28Antiokia (Siria)
2.MARKOMarko (Mwanafunzi)16Rumi au Siria
3.LUKA Luka (Mwanafunzi na, Tabibu)24Antiokia (Siria)
4.YOHANAYohana(Mtume, mwana wa Zebedayo)21Efeso (Uturuki)

   2. KITABU CHA HISTORIA (Tazama jedwali chini)

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.Matendo ya MitumeLuka (Mwanafunzi na Tabibu)28Rumi

   3. VITABU VYA NYARAKA ZA PAULO MTUME (Tazama jedwali chini)

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA SURAMAHALI KILIPOANDIKWA
1.WARUMIPaulo (Mtume)16Korintho (Ugiriki)
2.1WAKORINTHOPaulo (Mtume)16Efeso (Uturuki)
3.2WAKORINTHOPaulo (Mtume)13Makedonia (Ugiriki)
4.WAGALATIAPaulo (Mtume)6Efeso (Uturuki)
5.WAEFESOPaulo (Mtume)6Gereza
6.WAFILIPIPaulo (Mtume)4Gereza
7.WAKOLOSAIPaulo (Mtume)4Gereza
8.1WATHESALONIKEPaulo (Mtume)5Korintho (Ugiriki)
9.2WATHESALONIKEPaulo (Mtume)3Korintho (Ugiriki)
10.1TIMOTHEOPaulo (Mtume)6Makedonia (Ugiriki)
11.2TIMOTHEOPaulo (Mtume)4Rumi (Kifungoni)
12.TITOPaulo (Mtume)3Ugiriki
13.FILEMONIPaulo (Mtume)1Rumi (kufungoni)
14.WAEBRANIAinaaminika kuwa ni Paulo (Mtume)13Rumi

   4. VITABU VYA NYARAKA KWA WATU WOTE (Tazama jedwali chini)

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKWA
1.YAKOBOYakobo (Ndugu yake Bwana YESU)5Haijulikani
2.1PETROPetro (Mtume)5Babeli
3.2PETROPetro (Mtume)3Haijulikani
4.1YOHANAYohana (Mtume)5Inaaminika Efeso
5.2YOHANAYohana (Mtume)1Efeso
6.3YOHANAYohana (Mtume)1Haijulikani lakini inasadikika Efeso
7.YUDAYuda (Ndugu yake Bwana YESU)1Haijulikani

   5. KITABU CHA UNABII (Tazama jedwali chini)

N/AJINA LA KITABUMWANDISHIIDADI YA MILANGOMAHALI KILIPOANDIKIWA
1.UFUNUO WA YOHANAYohana (Mtume, mwana wa Zebedayo)22Patmo (kisiwani)

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAJINA YA MANABII WANAWAKE

MANABII WA BIBLIA (Wanaume)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU

Rudi nyumbani

Print this post

MAJINA YA MANABII WANAWAKE

Orodha ya Manabii wa kike katika biblia.


Jumla ya Manabii wa kike (wanawake) waliotajwa katika biblia ni 11, Kati ya hao manabii Tisa (9) walikuwa wa KWELI na Wawili (2) walikuwa wa UONGO.

LIFUATALO NI JEDWALI LA UFUPISHO..

Kulitazama jedwali zima, basi ‘SLIDE’ kuelekea kushoto.

N/AJINAURAIAHALI ZA KIMWILIHALI YA KIROHOMAREJEO
1.MIRIAMUISRAELIDada wa Musa na HaruniWA KWELIKutoka 15:20
2.DEBORAISRAELIHaijatajwa katika BibliaWA KWELIWaamuzi 4:4
3.HULDAISRAELIMke wa ShalumuWA KWELI2Wafalme 22:14,
2Nyakati 34:22
4.MKE WA ISAYAISRAELIMke wa IsayaWA KWELIIsaya 8:3
5.ANAISRAELIMjaneWA KWELILuka 2:36
6.BINTI WA FILIPOISRAELIBinti wa FilipoWA KWELIMatendo 21:8-9
7.BINTI WA FILIPOISRAELIBinti wa FilipoWA KWELIMatendo 21:8-9
8.BINTI WA FILIPOISRAELIBinti wa FilipoWA KWELIMatendo 21:8-9
9.BINTI WA FILIPOISRAELIBinti wa FilipoWA KWELIMatendo 21:8-9
10.NOADIAISRAELI (Mlawi)HaijatajwaWA UONGONehemia 6:14, Ezra 8:33
11.YEZEBELITIRO (LEBANONI)Mke wa Mfalme AhabuWA UONGO (Mchawi)Ufunuo 2:20

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake

Nini maana ya Mithali 11:17 inaposema;

Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake; Aliye mkali hujisumbua mwili wake.


JIBU: Mwenye rehema ni mtu wa huruma, mwenye kusamehe, mwenye kuachilia hata kama tendo alilofanyiwa linastahili adhabu kwa yule mwingine.

Biblia inasema mtu kama huyo huipa faida nafsi yake. Huitendea mema nafsi yake. Ambayo huipata kwanza hapa hapa duniani, kwasababu Bwana alisema kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa na watu.

Marko 4:24 Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, na tena mtazidishiwa.

Maana yake ni anajijengea wigo mpana wa yeye naye kukutana na rehema nyingi mbeleni.

Vilevile anapata faida katika ulimwengu ujao, Bwana  alisema..

Mathayo 5:7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.

Lakini anasema pia, mtu mkali hujisumbua mwili wake. Mtu mkali ni kinyume cha mtu mwenye rehema, ni mtu asiye na huruma, mwenye visasi, asiyejali, mkorofi, akiudhiwa anarudisha Maudhi, akikosewa kidogo, analipiza mara mbili, maneno yake hayana staha, kugombeza wengine kwake ni jambo la kawaida n.k.

Sasa matokeo ya mtu wa namna hii ni kuadhibiwa na Mungu, aidha hapa hapa duniani, au kule aendapo.

Bwana alisema…auaye kwa upanga, atauwa kwa upanga, ukimtendea mtu kwa ukali na wewe ukali utakurudia, ukimpiga mwingine kwasababu kakuudhi kidogo, na wewe utapigwa mahali fulani kwasababu ulimuudhi mwingine.. (hicho huitwa kisasi cha Mungu).

Hivyo tendea mema nafsi yako,lakini pia mwili wako, kwa kumpenda Bwana.Na kuwa mwema.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.(Opens in a new browser tab)

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

(Opens in a new browser tab)NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.(Opens in a new browser tab)

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post