KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

Je biblia inatufundisha wakristo kuwa na desturi?.

Jibu ni Ndio!, Biblia inatufundisha kuwa na desturi, ikiwa na maana kuwa desturi ina nyongeza kubwa sana katika Imani ya mkristo.

Sasa desturi ni nini?

Desturi ni kitu chochote mtu anachokifanya kwa kurudia rudia.(Ni Kanuni ya daima ya mtu)

Sasa si kila desturi ni nzuri lakini zipo chache zilizo nzuri, na leo tutaenda kutazama moja ambayo kila mkristo lazima awe nayo.

  1. KUKUSANYIKA

Hii ni desturi ya kwanza na ya msingi  tunayopaswa kuwa nayo, ambayo biblia imeihakiki!

Kukusanyika katika ibada, semina, na mikutano ni jambo ambalo linapaswa liwe desturi ya kila mkristo (maana yake mtu akilala akiamka anapaswa ajue kuwa kukusanyika ni sehemu ya maisha yake) na si jambo la kuamua leo kukusanyika na kesho kutokukusanyika. Biblia inatufundisha kuwa ni lazima liwe desturi kwetu,…sasa utauliza hilo tunalisoma wapi katika biblia..

Waebrania 10:25 “WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA, kama ilivyo DESTURI YA WENGINE; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”.

Umeona?

Kumbe kukusanyika ilikuwa ni desturi ya kundi Fulani la watu wa Mungu, na hapa biblia inatufundisha hayo hayo, kwamba na sisi tusiache kukusanyika KAMA ILIVYO DESTURI YA WENGINE. Maana yake inapaswa iwe desturi yetu na sisi, liwe jambo endelevu.

Kukusanyika ibadani hakupaswi kuwa tendo la leo kuamua na kesho kutoamua, bali linapaswa liwe desturi, iwe unajisikia au hujisikii, kukusanyika ni lazima iwe desturi yako, shetani amewafumba watu macho wasione kama kukusanyika ni desturi badala yake waone kama ni tendo kujisikia au kutojisikia, na hivyo kuwanyonyea Baraka zao!

Hivyo atakachokifanya ni kuwatengenezea udhuru  na vijisababu kwenye vichwa vyao ili awawafanye wasikusanyike na wengine.

Zifuatazo ni sababu kuu nne (4) za kuzikataa na kuzikimbia ambazo zitaharibu desturi yako njema ya kukusanyika na wengine.. kwasababu zinatoka kwa shetani.

1.Nimechoka:

Hii ni sababu ya kwanza ya kuikataa kwasababu hata siku nyingine za wiki unakuwa umechoka lakini huachi kwenda kwenye majukumu yako. Kwahiyo kama ilivyo desturi yako kwenda kazini, basi na kwenda kanisani kufanye kuwa desturi yako.

2.Naumwa:

Hii ni sababu ya pili yenye nguvu inayotoka kwa shetani, hata kama unasikia kuumwa kiasi gani usiache kukusanyika ibadani, kwasababu huko huendi kuongeza ugonjwa bali kuuondoa, kwasababu ugonjwa uliopata umetoka kwa shetani na kanisani shetani hayupo!.

Kama utakuwa na uwezo wa kuamka na kwenda hospitali pamoja na kwamba ni mgonjwa, kwanini usiamke na kwenda kanisani mahali penye uponyaji wa kiungu?

3.Mvua:

Hii ni sababu ya tatu ya shetani, ambayo inaharibu desturi ya wengi ya kwenda ibadani. Mvua isikuzuie kwenda ibadani.. bali nunua mwavuli na makoti ya mvua, na dhamiria kuwa iwe jua au mvua ni lazima ufike ibadani, kama mvua haiwezi kukuzuia kwenda kutafuta riziki za kimwili kwanini ikuzuie kwenda kutafuta riziki za kiroho?

4.Dharura

Dharura ni kitu chochote kinachonyanyuka wakati wa wewe kwenda ibadani, na hizo zinaweza kuwa ni za kikazi, familia, na nyinginezo..  Utakuta mtu anapigiwa simu na kuombwa ahudhurie mahali Fulani, na pasipo aibu ya uso anakubali na ilihali anajua kabisa siku hiyo ni maalumu kwa Mungu wake kukusanyika na wengine, lakini mtu huyo huyo akipokea simu siku za kazi yupo radhi kukataa kuvunjiwa ratiba zake za kazini na kuiheshimu kazi yake, lakini Nyumbani kwa Mungu kwake si kitu, Ukatae huo udhuru utaharibu desturi yako iliyo njema.

Na zipo sababu nyingine nyingi, hizi ni chacche tu, lakini katika hizo zote kataa visababu lakini jenga Desturi.. Huenda Desturi yako leo imeharibiwa na shetani, lakini Bwana Yupo kukusaidia ndio maana unayasikia haya leo.

Unachopaswa kufanya kuanzia leo ni kuomba rehema na kisha kutendea kazi hiki unachokisikia kuanzia leo, weka ratiba ambayo haibadiliki. Kwasababu desturi ya kwenda kanisani imehakikiwa na Roho Mtakatifu kuwa ni desturi njema. Hatuhitaji kuongozwa na Roho Mtakatifu au kupokea maono ya kwenda kanisani au la! Biblia tayari imeshatuelekeza kuwa inapaswa iwe desturi yetu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

EPUKA KUCHELEWA IBADA.

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments