Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

SWALI: mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.(Mathayo 23:15)

Mathayo 23:15

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.


JIBU: Bwana Yesu anaanza Kwa kueleza bidii ya mafarisayo, kwamba ni hodari wa kuieneza dini zao kiasi cha kufanya umisheni wa kuzunguka hata sehemu za mbali nje ya taifa lao ili kuwafundisha watu mapokeo Yao. Lakini Bwana hawakemei Kwa bidii Yao hiyo ya kuzunguka huku na huko, Bali anawakemea Kwa Imani yanayoisambaza Kwa watu, ambayo ni potofu.

Imani ya kinafki, inayoacha kufundisha mambo ya adili kama (Imani katika Mungu, Upendo, kuja Kwa mwokozi duniani), Bali katika zaka na michango kama ndio tiketi ya kukubaliwa na Mungu (Mathayo 23:23)..

Na matokeo yake ni kwamba wale wanaogeuzwa Huwa wanakuwa na kiu ya dhati ya kusimama. Hivyo Kwa kuwa wanafundishwa uongo, basi wanafanyika kuwa Wana wa udanganyifu mara mbili zaidi ya Hao wenyewe.

Ndio hapo utamwona mtu kama Paulo, alipogeuzwa akawa chini ya elimu ya mafarisayo, lakini matokeo yake yalizidi hata wakufunzi wake wakina Gamalieli, alianza kuwauwa na kuwaburuta wakristo, na ndio ulivyokuwa Kwa watoto wao wote..walikuwa wabaya zaidi Yao, Wana wa jehanamu mara mbili zaidi ya wao.

Hata Leo angalia matokeo ya dini, madhehebu na Imani za uongo. Utagundua kuwa wale wafuasi wao ndio wanaokuwa wabaya zaidi ya wale viongozi, 

Na ndio maana akawaambia hukumu Yao itakuwa kubwa zaidi ya wengine (Mathayo 23:14)

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Kuzimu kuna nini?

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Jehanamu ni nini?

MJUE SANA YESU KRISTO.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments