Title kuota una mimba

KUOTA UNA MIMBA.

Usipokuwa na uelewa wa kutosha  juu ya ndoto, unaweza ukajikuta unatoka nje ya kusudi la Mungu ambalo amekukusudia wewe uishi kwalo hapa duniani..

Na hiyo imewafanya watu wengi wazunguke huko na huko, kutafuta tafsiri ya ndoto zao..Lakini jambo la kwanza na la msingi sana kufahamu ni kuwa, tunapaswa kujua kuwa ndoto yoyote ni lazima iwepo katika mojawapo ya  makundi haya matatu:

> Kundi la kwanza ni ndoto zinazotokana na Mungu,

> Kundi la Pili ni ndoto zinazotokana na shetani,

> na kundi la tatu ni ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe.

Sasa ndoto hizi zinazotokana na mtu mwenyewe huwa zinaathiriwa sana na mambo mbalimbali aidha kutokana na mazingira ya mtu yanayomzunguka au shughuli anazozifanya mara kwa mara,  au mambo anayoyawaza kila wakati..Na aina hii ya ndoto ndiyo inayochukua asilimia kubwa sana ya ndoto watu tunazoziota kila siku, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto tunazoziota kila siku na hizi huwa hazina maana sana, lakini watu kwa kukosa ufahamu imefanya wahangaike kutwa kuchwa kutafuta tafsiri ya kila ndoto yanazoziota mpaka inawafanya kuwa watumwa wa ndoto…Kumbe kiuhalisia sio kila ndoto ina ujumbe wa kutufaa..

Hivyo mtu akishakuwa na uelewa wa namna ya kuzigawanya ndoto hizi katika makundi haya hatapata shida kuitafsiri ndoto yake..Hivyo nakuashuri pitia kwanza somo hili kisha ndio tuendelee.  >> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI? 

Sasa ukiota una mimba: Ikiwa ndoto hiyo haitokani na shughuli zako mwenyewe au mazingira yanayokuzunguka, au mawazo unayoyawaza kila mara, kwasababu kumbuka ndoto kama hizi huwa zinawatokea mara nyingi wanawake, kwahiyo uwezekano wa kuangukia katika  kundi hilo la tatu la ndoto ni mkubwa kwasababu wanawake maisha yao tangu wakiwa watoto wanawaza siku moja ni kuwa na mtoto kwahiyo kuota wamebeba mimba si jambo la kushangaza, au utakuta mwingine maisha yake yote anatamani sana kuwa na mtoto, hana watoto, moja kwa moja mtu kama huyo ni rahisi kuota ni mjamzito au mwingine utakuta anaishi na mwanamke mjamzito  karibu na mazingira yake au jana amemwona mwanamke mmoja barabarani akipita akiwa mjamzito akajikuta usiku anaota kabeba mimba akadhani kuwa ndoto hiyo inamaana sana kwake..,

Ikiwa ni hivyo, basi zipuuzie tu, ni ndoto zinazokuja kutokana na mawazo yako. Hizo hazibebi ujumbe wowote kwako.

Lakini hapa tunadhania kuwa ndoto hiyo haijatoka katika vyanzo vya namna hiyo, 

Sasa fahamu kuwa tendo lolote kuchukua mimba liwe ni jema au liwe ni baya, liwe limekuja kwa  njia ya uzinzi au kwa njia ya haki ni lazima tu kiumbe kipya kije duniani mwisho wa siku hakuna namna!..Na kabla hakijaja lazima dalili Fulani zionekane…Hivyo kama ndoto yako  imekuwa ni ya kujirudia rudia basi itilie maanani zaidi kwasababu inaweza kuwa imebeba ujumbe kutoka kwa Mungu,..

Utakumbuka Farao alipoota ndoto ile ihusuyo miaka saba na njaa na miaka saba ya neema, ilikuja mara mbili, hata kama ilichukua taswira nyingine lakini ujumbe ulikuwa ni mmoja..ndipo akawa na uhakika wa kuwa ndoto ile ni ya kuizingatia..Vivyo hivyo na wewe ikiwa unaota mara kwa mara una mimba, ni mjamzito izingatie sana ndoto hiyo.

Kwahiyo jambo unalopaswa kufanya hapo kwa kuwa wewe ndiye unayeyafahamu maisha yako zaidi kuliko mtu mwingine yeyote , kaa chini kwa utulivu mwingi utafakari maisha yako na njia yako unayoiendea sasa hivi..iwe ni katika huduma yako, iwe ni katika familia yako, iwe ni katika shughuli yako unayoifanya sasa, kuna uamuzi uliuchua, au kuna jambo ulilifanya  ambalo hivi karibuni utakwenda kuona matokeo yake..

Hivyo kama ulimwomba Mungu juu ya kitu Fulani, kwa muda mrefu akupatie basi kaa katika matarijio ya kukipata, au kama ulijitaabisha katika kitu ambacho kwasasa faida yake haionekana kaa katika matarajio ya kukipata muda si mrefu..

Sara alikuwa katika matarajio ya kupata mtoto kwa muda mrefu, lakini wakati ulipofika malaika alimjia na kumwambia panapo wakati kama huu mwakani utalea mtoto..VIvyo hivyo na wewe kama upo katika mstari ulionyooka na Mungu wako basi tarajia Mungu kukupa kile ulichokuwa unakitafuta. Kwasababu mimba sikuzote ni matokeo ya ile mbegu iliyoingia ndani yako..Kama ni mbegu njema uliipanda basi utavuna kilicho chema.

Vile vile kama ulikuwa ni mwovu unafanya mambo yasiyompendeza Mungu nawe pia kaa katika matarajio ya kukipata hicho ulichokuwa unakifanya, ikiwa ulikuwa mchawi jiandae kuvuna matunda ya uchawi wako, ikiwa ulikuwa ni tapeli au mla rushwa jiandae kukumbana na ulichokihangaikia, kama ulikuwa ni mrushi vile vile jiandae kukutana na malipo yake hivi karibuni…

Usishangae kukutana na mabaya, kwasababu biblia inasema dhambi nayo huwa inapitia hatua hizo hizo mpaka kufikia mauti.

Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”

Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.”

Isaya 59:3 “Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.

4 Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.”

Hivyo kama unatenda maovu sasa, acha mara moja, Tubu dhambi zako, umegukie muumba wako YESU KRISTO kabla huo wakati wa mabaya haujafika, lakini kama unajijua upo katika njia iliyonyooka na umekuwa katika dua ya kumwomba Mungu kwa ajili ya kitu Fulani chema..Basi kuwa katika matarajio ya kukipata siku za hivi karibuni.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

USHUHUDA WA RICKY:

MTETEZI WAKO NI NANI?

KUOTA UNAPEWA PESA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAJIFUNGUA.

Kuota unajifungua kuna maanisha nini?


Ndoto hii inaweza ikawa na maana mbili, maana ya kwanza ambayo ninaweza  kusema inawapata wengi, ni ile inayotokana na shughuli nyingi au mambo tuliyowahi kuyapitia, au kuyawaza, au kuyatenda mara kwa mara huko nyuma.

Biblia inasema.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…….”.

Hivyo sishangai kama ndoto hii atakuwa anaotwa na mwanamke, kwasababu yeye kwa sehemu kubwa katika maisha yake, amekuwa akiwaza pengine siku moja atajifungua, au hivi karibuni anakwenda kujifungua au mwengine tayari huko nyuma alishawahi kujifungua,..

Hivyo matukio kama hayo kujirudia rudia katika ndoto zake litakuwa ni jambo la kawaida sana. Kwahiyo kama wewe ni mmojawapo wa wanaoyapitia hayo, basi ipuuzie tu ndoto ya namna hiyo, kwasababu haina maana yoyote rohoni.

Lakini maana ya pili, ambayo ni ya rohoni, ni kwamba ikiwa ndoto hii umekujia kwa namna ambayo sio ya kawaida, yaani kwa uzito mkubwa sana, na unahisi kuna uzito Fulani ndani ya moyo wako, basi ujue ndoto hiyo imebeba ujumbe. Na tafsiri yake ni kuwa lipo jambo zuri au baya linakwenda kukujia, kulingana na ulichokuwa unakifanya katika maisha yako.

Tunajua sikuzote mpaka mtu anafikia hatua ya kuzaa ni wazi kuwa tayari huko nyuma alishabeba mimba kwa muda mrefu, hivyo angalia katika maisha yako ni nini umekuwa ukikibeba, na ukikisubiria, basi ujue hivi karibuni utakwenda kukiona kikijidhihirisha (kukuletea matokeo fulani). Kama umekuwa ukifanya jambo jema basi tazamia kuona matunda ya wema wako hivi karibuni.

Luka 1:30 “Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

Lakini kama wewe ni mwenye dhambi (yaani haupo ndani ya Kristo) basi jiandae hivi karibuni kukutana na matunda ya mambo maovu uliyokuwa unayafanya katika maisha yako,

biblia inasema..

Ayubu 15:35 “Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu”.

Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo”

Yakobo 114 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”.

Unaona wanachozaa sikuzote watu waovu ? Na ndio maana sehemu nyingine inasema..

Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.

Hivyo jiangalie wewe katika maisha yako yote, na mambo yako yote unayoyatenda Je, ni jambo gani unakwenda kulizaa hivi karibuni? Je! ni uzima, au mauti?

Lakini habari njema ni kuwa Yesu leo anaweza kukuokoa, na kukufanya umzalie matunda mazuri, na akabatilisha mabaya yote ambayo yamepangwa mbele yako, ikiwa tu utakubali kumruhusu ayageuze maisha yako, Yeye yupo tayari kukusamehe ikiwa utakuwa tayari kutubu kwa moyo wako wote, Hivyo ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi uamuzi huo ni wa busara sana. Unachotakiwa kufanya ni kufungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na Mungu peke yake atakigeuza unachokizaa kiwe chema.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Au jiunge kwa kubofya link hii>> 

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Arabuni maana yake ni nini?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

Kuota unaolewa/ unaoa kunamaanisha nini?


Zipo ndoto zenye maana katika Maisha yetu, na pia zipo ndoto zisizo na maana yoyote katika Maisha yetu,.

Hizi zisizo na maana ni ndoto ambazo, ubongo wetu unajiundia wakati tunapokuwa tumelala kutoka katika mazingira yetu yanayotuzunguka, au mambo ambayo tulikuwa tunayawaza au tunayafanya mara kwa mara, Na ndio maana biblia inasema;

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi..”

Hivyo asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, zinaangukia katika hili kundi. Kama wewe ni  mshonaji, basi tarajia asilimia kubwa ya ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitakuwa ni za namna hiyo,..Vilevile ndoto kama Kuota unaolewa/unaoa, wazo hilo pengine si geni katika kichwa chako,kwamba siku moja umekuwa ukifikiria kuwa utakuja kuoa au utaolewa, Hususani pale unapokuwa umefikia umri huo, lakini bado haijawa hivyo kwako.

Au inakuja kutokana na kuwa umekuwa ukihudhuria mazingira ya harusi mara kwa mara, Hivyo ubongo wako ukayachukua hayo matukio na kuyarudia hivyo hivyo au kwa namna nyingine unapokuwa umelala.

Lakini pia ndoto za namna hii zinaweza kuwa ni za rohoni, hivyo kubeba maana Fulani,

Kwa mfano ikiwa ulikuwa katika kumwomba Mungu, akupe mume/mke, ukiota upo katika ndoa, basi ujue jambo hilo lipo mlangoni kwako.

Lakini unachopaswa kufanya ili Mungu akupe sawasawa na chaguo lake.

  • Kwanza unapaswa uwe katika utakatifu,
  • Vilevile unapaswa uwe mwombaji,

Lakini ukiwa ni mzinifu, unatanga tanga na kila mwanaume, au mwanamke,  au unaishi mtu ambaye  hamjaona, sahau Mungu kulitekeleza hilo, na kama likifanikiwa basi ujue huyo utakayempata hujachaguliwa na Mungu.

Ili kufahamu njia sahihi ya kumpa mweza wa Maisha fungua hapa;

>>> NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Lakini hayo yote ni lazima uwe katika wokovu, ukimpata Kristo, umepata vyote, Ukimkosa yeye, umepoteza vyote mpaka uzima wako. Hivyo kama leo hii unahitaji kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, basi uamuzi huo ni mzuri kwako..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua link hii, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia kama utahitaji kujiunga katika magroup yetu ya Whatsapp unaweza ukabofya hapa chini>>

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KUOTA UNA MIMBA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Ayubu 26:6 “Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko”.

Kama tunavyojua mashimo mengi yanayochimbwa huwa yanawekwa mifuniko juu, ili kusudi kwamba ikitokea mtu mgeni akapita kwa njia ile iwe ni mchana au usiku kwa bahati mbaya asitumbukie,

Lakini biblia inatumbia kaburi la mauti lipo wazi sikuzote, na uharibifu hauna kifuniko..

Uharibifu kwa jina lingine ni kuzimu.. Akimaanisha kuwa kuzimu haina mfuniko wowote, mfano ikitokea umepita katika njia hiyo kwa namna yoyote, basi kutelezea humo na kuzama ni mara moja..haijui huyu ni mgeni, au ni mwenyeji au ni mtoto. Ukizama umezama!.

Na ndio maana leo hii mtu akifa katika dhambi, moja kwa moja atajikuta ghafla tu yupo kuzimu, (Ayubu 21:13). atajiuliza amefikaje fikaje huko. Lakini ndio hivyo tayari ameshafika huko mahali ambapo hatatoka tena milele,.atakachokuwa anasema huko ni Laiti ningejua, laiti ningefahamu, nisingefanya hiki au kile..

Biblia inatuambia..

Isaya 5:14 “Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo”.

Unaona? Unashuka kwa ghafla sana, tusitamani tufike huko. Kila inapoitwa leo, tumwombe Mungu vilevile tujitahidi kukaa mbali na dhambi kwa kadiri tuwezavyo.

Watu wote wanaochukuliwa katika maono na kupelekwa kule, na kuonyeshwa sehemu tu ya mambo yanayoendelea humo, huwa hawatamani kuhadithia, kwasababu wote wanaowaona humo, ni vilio vya majuto tu, wanatamani wapewe dakika hata moja warudi watengeneze mambo yao lakini haiwezekani tena..

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, NI VIVYO HUYO ASHUKAYE KUZIMUNI HATAZUKA TENA KABISA.

10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Utatamani urudi duniani siku hiyo itashindikana…Mfano tu wa Lazaro na yule Tajiri…Yule tajiri aliomba akawahubiriwe ndugu zake ili wasifike mahali pale alipo pa mateso lakini ilishindikana..Na Watu wanaoshuka huko ni wengi sana wasiohesabikia. Hivyo mimi na wewe tulio hai, tuikwepe dhambi…

Tusipende kufuata mikumbo ya watu, kisa wanakwenda Disko na sisi tuende, kisa wanavaa nguo za kikahaba na sisi tuvae, kisa wanafanya uasherati na sisi tufanye..kisa wanatumia pombe na sisi tutumie ..Kamwe usiwaige hao..Kwasababu wanaoshuka huko ni wengi sana, na kuzimu haijai watu..(Mithali 27:20, Mithali 30:16)

Kumbuka hizi ni zile siku zilizotabiriwa za maasi kuongezeka. Kwahiyo usishangae kuona wimbi kubwa la watu wanaofanya dhambi hadharani bila hofu.

Zaidi macho yetu yaelekee mbinguni, kwani unyakuo upo karibu, Au hata kama hautakukuta wakati wako, basi tufahamu kuwa kifo nacho hakipo mbali, Hivyo ni wajibu wetu kujiimarisha na kujithibitisha kwamba tupo katika mstari wa Imani.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

SWALI: Mimi Nina MUNGU Wangu ambae Ni ALLAH subhanallah…sasa kwanini nimkabidhi maisha Yesu wakati naye alizaliwa Kama mimi?


JIBU: Mama yako alizaliwa kama wewe…lakini ilifika wakati Mwenyezi Mungu aliyakabidhisha maisha yako kwake. Ili uwe salama, ulindwe, uhifadhiwe, ulishwe na upendwe..na pamoja na hayo ufundishwe kanuni za maisha ambazo peke yako bila wazazi au mlezi usingeweza kujifunza.

Vivyo hivyo ulipaswa ukae chini ya sheria za wazazi wako ndipo uweze kufanikiwa, endapo ungekuika sheria hizo basi maishani usingefanikiwa….Na kama sio Mwenyezi Mungu kuyakabidhisha maisha yako kwa wazazi wako ambao wamezaliwa kama wewe, maisha yako yangukuwa magumu sana hapa duniani au hata pengine usingezaliwa kabisa au kama ungezaliwa ungekufa.

Vivyo hivyo Yesu alizaliwa kama sisi tulivyozaliwa, (Ingawa hakuzaliwa na dhambi ya asili kama sisi, kwasababu mimba yake ilitungishwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu), na katika nyakati hizi za uovu na mateso na dhiki za ulimwengu.

Mungu kwa huruma zake na kwa jinsi anavyotupenda akamtuma huyu Yesu Kristo, ili awe kama mzazi kwetu kwasababu sisi wenyewe hatutaweza kwa nguvu zetu na kwa akili zetu kujiongoza..Ndio maana hatuna budi wote tuyakabidhi maisha yetu kwake ili tuwe salama sasa na ahera.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

17 Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.

18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”

Yesu anapoingia maishani mwetu, anatupa furaha, faraja, amani, upendo na tunapata ulinzi dhidi ya Adui shetani na mapepo yake yote, siku zote za maisha yetu na tumaini la uzima wa milele.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

Ubatizo wa moto ni upi?

YULE JOKA WA ZAMANI.

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAJISAIDIA SEHEMU ZA WAZI.

Kuota Unajisaidia sehemu za wazi. Maana yake ni nini?


Ndoto hii, imekuwa ikiotwa mara kadhaa wa kadha na watu wengi. Kwa mfano mtu mmoja alinisimulia ndoto yake, anasema katika ndoto alijikuta yupo stendi ya basi, na pale palikuwa na watu wengi sana, ghafla akaanza kujisaidia lakini yeye alikuwa anajitahidi kufanya vile asionekana..Na alipomaliza akidhani hajaonekana wakati akiwa anarudi nyumbani mtu mmoja ambaye alikuwa anamjua akamfuata akamwambia mbona nilikuona unajisaidia pale stendi?..Anasema kwa kweli aliposikia hivyo   alijisikia aibu sana.

Na ndivyo ilivyo ndoto za namna hii, ni lazima mwisho wa siku utajisikia aibu tu, wengine wanaota wamejinyea, mavi, wengine wakiwa shuleni, kazini, uwanjani n.k. ..kwasababu kitendo cha kujisaidia huwa sikuzote ni cha aibu na ndio maana kinafanyika kwa siri chooni.. Lakini ikiwa unajisaidia kwa wazi ni Mungu anakuonyesha ni jinsi gani, mambo yako machafu yatakavyokuja kuwa dhairi siku moja mbele za watu wengi..kama hutatubu dhambi zako au hutasimama imara leo hii kwa Mungu wako.

Inaweza isiwe sasa, lakini kumbuka siku ile ya hukumu inafika..ambapo mambo yote yaliyokuwa yanafanyika kwa siri yatawekwa wazi.

2Wakorintho 5:10  “Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya”

1Wakorintho 4:5  “Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye ATAYAMULIKISHA YALIYOSITIRIKA YA GIZA, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.

Unaona? Hivyo ikiwa hujatubu dhambi zako, maisha yako bado ni machafu, YESU KRISTO bado hajaingia ndani yako kukusafisha uwe hai..Ni heri ukaamua kufanya hivyo kabla nyakati hizo mbaya hazijafika..Huu ndio wakati wa wewe, kusema basi..Nahitaji kuanza upya na Kristo..Usiseme mimi ni muislamu, hata wewe Unapaswa umgeukie YESU Kristo kwasababu yeye ndio njia na kweli na Uzima ya kukufikisha wewe mbinguni.

Ukimkaribisha leo maishani mwako, atakupokea na kukufanya upya. Unaona ni hali gani ulijisikia ulipojiona unafanya kitendo cha aibu katikatika ya umati wa watu..Sasa embu fikiria siku ile ya hukumu, Maisha yako yataanza kutazamwa  na Mungu mbinguni, pamoja na majeshi ya malaika zake, pamoja na watakatifu wa Mungu mamilioni kwa mamilioni..wote wanakutazama siku ile ulivyokuwa unazini na mume au mke ambaye si wako, watakutazama ulivyokuwa unajisaga kisirisiri mwenyewe nyumbani mwako..watakutazama ulivyokuwa unafanya mustarbation kwa siri chumbani, watakutazama ulivyokuwa unaangalia picha za uchafu, lakini kwa nje unaonekana wewe ni mwema, watakutazama mimba ulizotoa japo ulikuwa unajulikana kama ni mwanamke mstaarabu, machoni pa watu watu..watakutazama ufiraji uliokuwa unaufanya kwa mkeo, japo kwa nje unaonekana mtu unayejiheshimu….Siku hiyo watakutazama..Ni itakuwa ni AIBU KUU, ambayo utatamani hata usingezaliwa.

Lakini hayo yote ya nini mpaka yakukute wakati Kristo bado anakupenda?..Njoo kwa YESU ayabadilishe maisha yako leo hii..biblia inasema..saa ya wokovu ni sasa..Umeshindwa kuacha pombe, lakini Ukimruhusu Yesu aingie maishani mwako, ataikata hiyo kiu ya pombe, itakwisha kabisa..Umeshindwa kuacha uzinzi lakini ukimfuata Yesu leo hii, atakusaidia na hiyo hali utaishinda..na mambo mengine yote maovu unayoyatenda saa hii, ukimkabisha Yesu maishani mwako atakugeuza..anachohitaji kwako ni moyo wa toba tu basi..Na kumaanisha kweli kweli wala sio kujaribu..

Hivyo ikiwa umemaanisha kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

KUOTA UPO UCHI.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMETUMBUKIA SHIMONI.

Ogopa wadanganyifu, ambao wanakuambia suluhisho la ndoto Fulani uliyoota labda tuseme kuota umetumbukia shimoni, au umekimbizwa na nyoka,au umezama kwenye maji au unafanya uasherati na mtu usiyemjua kwamba ukanunue dawa yao Fulani itakusaidia kutatua hilo tatizo.. Wengi wanaokuambia hivyo kama si washirikina basi uwe na uhakika ni matapeli.. Ndoto, au maono, ni mambo yanayotoka ndani ya mtu, yaani katika utu wake wa ndani, Hivyo hayawezi kutibiwa kwa tiba za nje, kama vile dawa na vidonge, Ni sawa na mtu aliyefiwa, huwezi kumwambia nenda kameze PAIN KILLER, tatizo lako la huzuni litakwishwa, badala yake utatumia njia ya kumfariji, ndipo hapo atakapogangika kwasababu ugonjwa wake ni wa moyoni na si nje..

Hivyo ni vizuri kufahamu, ndoto asili yake ni rohoni, Kwahiyo tiba yake ni lazima iwe ya rohoni na si ya  nje.

Kwa utangulizi:

Zipo ndoto za aina tatu.

  1. Ni zile zinazotokana na Mungu: Ambazo hizi zinachukua sehemu ya wastani ya ndoto anaziziota mtu kila siku.
  2. Ndoto zinazotokana na shetani: Hizi nazo zinachukua sehemu ya wastani wa ndoto mtu anazoziona kila siku.
  3. Ni zile zinazotokana na mtu mwenyewe: Hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa sana ya ndoto mtu anazoziota kila siku.

Sasa kama kuota umetumbukia shimoni: Mara nyingi wengine wanaota wapo ukingoni mwa shimo wanakaribia kuanguka, wengine wapo tayari chini  kabisa kwenye  shimo refu lenye giza, wengine wananing’inia ikingoni mwa shimo na kila wanapojaribu kujivuta juu watoke wanajiona ni wazito sana, wanahitaji msaada..n.k. zote hizo ujumbe wake ni mmoja. Kuwa maisha yako yapo hatarini kama hutachukua uamuzi ulisohihi Mungu anaokuagiza uufanye.

Ikiwa wewe umeokoka (yaani maisha yako yamefichwa ndani ya YESU KRISTO):  Na ndoto kama hii kuota umetumbukia shimoni imekujia kwa uzito sana, au imejirudia rudia mara nyingi, basi ongeza umakini wako kwa MUNGU,kwasababu mahali unaweza kwenda kukwamba usisonge mbele katika imani yako, pili omba sana, hususani katika mazingira uliyopo, na mambo unayoyafanya yote hakikisha unamtanguliza Mungu kwanza..Na Bwana atakuvukisha au kukukwepesha kabisa na majaribu hayo.

Soma  (Yeremia 38:6, Maombolezo 3:52-57).

Lakini kama wewe hujaokoka na unafanya mojawapo ya hivi vitu:

  • Wewe Ni mzinzi: basi ujue Mungu anakupa ujumbe huu..

Mithali 22:14 Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake.

Mithali 23: 27 Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Ukiendelea kuwa na tabia hiyo, mwisho wako utakuwa ni mbaya..Utaingia mahali ambapo utashindwa kutoka milele.

  • Ikiwa hutendi haki: Au unamuundia mwenzako visa, ili asisonge mbele, basi andiko lako ni hili.

Mithali 26: Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.

Zaburi 7: 14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.

15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!

16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.

Hayo yote yanajumuisha watu wote waovu..Kuwa hatma ya maisha yao ni shimo refu la mauti kama hawatatubu.

Hivyo yatengeneza mambo yako kwa Mungu haraka iwezekanavyo..Kumbuka Yesu ndio njia, na kweli na Uzima (Yohana 14:6), anakuonyesha hivyo kwasababu anakupenda ili utubu umgeukie yeye, uache dhambi ayasafishe maisha yako. Ni nani ajuaye kuwa leo kukukutanisha na ujumbe huu ni kwa makusudi yake maalumu UOKOKE LEO?..Hivyo usipuuzie wito huo, mruhusu leo ayaokoe maisha yako akutoe katika shimo hilo refu la mauti ambalo upo sasa, au kama haupo basi siku si nyingi utakuwepo,ukiendelea na tabia yako.

Lakini  Ikiwa unatii na upo tayari kufanya hivyo sasa.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya Hivyo na Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je Kutoa Mimba ni dhambi?

Je Utoaji mimba/ kutoa mimba ni dhambi?..Je kama mtoto aliye tumboni anahatarisha uhai wa mama na madakatari wakamwambia anapaswa atoe hiyo mimba ili aishi vinginevyo atakufa..je endapo akiitoa ili kunusuru uhai wake kwa sababu za kiafya atakuwa amefanya dhambi ni muuaji?

JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu maana ya utoaji mimba..Utoaji mimba ni kitendo cha mzazi wa kike..kuondoa kiumbe ambacho tayari kimeshaanza kuishi katika tumbo lake..Hicho kinaweza kuwa katika wiki ya kwanza au katika mwezi wa mwisho wa 9. Hatua yoyote inayohusisha kukiondoa hicho kiumbe tumboni kwa mwanamke katika kipindi hicho cha muda  ni kitendo cha UTOAJI MIMBA.

Utoaji mimba umegawanyika katika sehemu mbili..1) Utoaji mimba kwa sababu za kiafya 2) Utoaji kwa sababu nyingine zisizo za kiafya.

Tukianza na sababu za kiafya

Hii inahusisha pale mama mjamzito..labda kaugua ghafla na ile mimba ndani ya tumbo lake ikaharibika au mtoto akafa tumboni…Ili kuokoa maisha ya mama analazimika kwenda kuiondoa hiyo mimba hospitalini..Katika hali kama hiyo mama huyo hafanyi dhambi kwasababu tayari mtoto kashakufa..hivyo anapaswa atolewe huko aliko na kuzikwa.

Pia Inaweza kutokea mimba ya mama mjamzito ikatoka yenyewe kabla ya wakati wake…Hali kama hiyo pia hakuna dhambi iliyotendeka..Ingawa sio kawaida mimba kutoka yenyewe…

Lakini pia inaweza kutokea Mama mjamzito kapata tatizo au ugonjwa ambao utamlazimisha aondoe ile mimba iliyopo tumboni mwake ili kunusuru uhai wake. Na asipofanya hivyo kuna hatari ya kufa. Katika hali kama hiyo ambayo imethibitishwa..endapo mimba hiyo akiitoa hafanyi dhambi. Kwasababu amefanya hivyo  ili kunusuru uhai wake…na asipofanya yeye pamoja na hicho kiumbe tumboni watakufa.

Lakini pia ni muhimu kufahamu kuwa..Hata katika hali hiyo ambayo madaktari wamesema kwamba ni ngumu kunusuru uhai  wa mama akiwa na kiumbe tumboni..YESU KRISTO wa Nazareti hashindwi jambo..Mimba inaweza isitolewe na mwanamke huyo akazaa vizuri kabisa bila kufa wala kupata tatizo lolote..wanadamu wanashindwa mambo lakini Yesu Kristo hana rekodi ya kushindwa…Na wapo wanawake wengi wametendewa na Yesu miujiza kama hiyo…wamepewa ripoti na madaktari kwamba aidha waiondoe mimba waishi au waendelee kukaa na hiyo mimba wafe…lakini Bwana amewapigania na wameshinda vitisho vya vifo na wamejifungua salama kabisa bila tatizo lolote…Na waliotendewa hivyo na Yesu wapo wengi sana.

Lakini hiyo inahitaji imani thabiti isiyo na mashaka kwa Yesu Kristo…Lakini kama mtu ataingiwa na mashaka basi ni heri akaenda kuiondoa hospitalini…Kwasababu biblia imesema mtu asiye na imani asitegemee kupokea kitu kutoka kwa Mungu…

Yakobo 1.6 “… Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

8 Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.”

Sababu za PILI za kutoa mimba ni sababu zisizo za kiafya 

Sababu hizi zinahusisha…Pale mwanamke anapopata mimba na wakati hana mpango wa kuwa na mtoto kwa wakati huo…Mwanamke wa namna hiyo akiitoa mimba ambayo tayari kashaipata anafanya dhambi..ni Muuaji.

Mwanamke ambaye amepata mimba kwa kubakwa au kwa mtu asiyempenda na akaenda kuitoa anafanya dhambi tayari, ni muuaji.

Mwanamke ambaye kapata mimba na kalazimishwa na mtu aliyempa mimba kwamba aitoe na yeye akaitoa anafanya dhambi huyo ni muuaji kabisa.

Mwanamke ambaye kapata ujauzito na Baba aliyehusika na ujauzito huo kaikataa hiyo mimba na mwanamke akaenda kuitoa hiyo mimba anafanya dhambi  ni muuaji.

Mwanamke anayetoa mimba kwasababu ya umasikini au hali ngumu ya kimaisha kwa kuhofia malezi ya mtoto yatakuwaje anafanya dhambi ni muuaji.

Na sababu nyingine zote zilizosalia zisizo za kiafya..Ni dhambi kutoa mimba kwa kutumia hizo sababu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNA MIMBA.

Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?

KIELELEZO CHA MWANAMKE KATIKA NYUMBA.

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEPOTEA.

Kuota umepotea mjini, au kuota umepotea shuleni, au kuota umepotea msituni, au kuota umepotea njia panda au kuota umepotea katika riadha au kuota umepotea sehemu usiyoijua, kwa vyovyote vile maadamu ni ndoto ya kupotea basi fahamu kuwa ndoto za namna hii mara nyingi zinatokana na Mungu.

Na huwa zinakuja kwa makundi yote ya watu, (Yaani wale walio ndani ya Kristo na wale walio nje ya Kristo).

Sasa ikiwa kama wewe hujaokoka  Biblia inasema:

Zaburi 37: 18 Bwana anazijua siku za wakamilifu, Na urithi wao utakuwa wa milele. 

19 Hawataaibika wakati wa ubaya, Na siku za njaa watashiba. 

20 Bali WASIO HAKI WATAPOTEA, Nao wamchukiao Bwana watatoweka, Kama uzuri wa mashamba, Kama moshi watatoweka.

Unaona wasio haki sikuzote huwa wanapotea, hivyo  kuota umepotea ni ujumbe ambao Mungu anakuonyesha hali yako ilivyo rohoni, na kama vile huko ndotoni unavyojiona unahangaika huku na kule kutafuta njia sahihi ya kufika mahali unapotaka kufika na unashindwa, unateseka sana huku na kule, unaonyeshwa kuwa kuna wakati utafika utautafuta huo wokovu ulioupoteza na hautauona milele…na kibaya zaidi wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Zaburi 1:6 Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.

Mungu anakupenda na ndio maana anakuonyesha mambo kama hayo mapema ili utengeneze njia zako sasahivi, maadamu upo hai, maadamu imeitwa leo, Kesho inaweza isiwe yako, unaweza ukajiona upo sawa sasa katika Maisha yako, labda umejiendeleza, umefika mbali, una afya nzuri, umefanikiwa, unayo familia nzuri, lakini Mungu anakuambia umepotea, haijalishi upo katika mafanikio gani leo hii, Unachopasw kufanya ni ugeuke uombe msaada kwa Mungu naye atakuonyesha njia…na njia yenyewe ni YESU KRISTO.

Yohana 14:6  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.  

Unaona kama yeye ni njia basi alikuja kukitafuta kilichopotea kama anavyosema katika..

Mathayo 18:10  “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.

11  [Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea”.]

Kwahiyo ikiwa leo utakubali kutii na kumpa Maisha yako, basi atayaokoa na kukusamehe kabisa, ikiwa upo tayari sasa, hapo ulipo piga magoti kisha chukua dakika chache tafakari mambo yote maovu ulioyomfanyia Mungu, kisha kwa Imani, zungumza na Mungu, mwombe rehema,usimfiche chochote mwambie akusamehe maanisha kabisa kwasababu hapo ulipo anakusikia…Kisha ikiwa toba yako imetoka moyoni kwa dhati, na kwamba upo tayari kuacha yote ya nyuma uliyoyafanya basi fahamu kuwa Mungu amekusamehe, hivyo tu,

Sasa hatua inayofuata ni kwenda kutafuta mahali wanapobatiza

Ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO sawasawa na (Matendo 2:38) Ili ukamilishe wokovu wako uwe milki halali ya YESU KRISTO, ndipo Mungu akumwagie kipawa chake cha Roho Mtakatifu. Hivyo zingatia hayo maagizo yote ni muhimu sana kuyafanya, ikiwa hufahamu vizuri ni wapi utapata ubatizo sahihi, basi wasiliana na sisi kwa namba hizi 0789001312 au 0654555788.Tutakusaidia kutafuta maeneo karibu na wewe.

Vile vile ikiwa wewe tayari ulishaokoka, na ndoto kama hizi, kuota umepotea shuleni, au kuota umepotea msituni, au kuota umepotea njia panda au kuota umepotea katika riadha au kuota umepotea sehemu usiyoijua zinakujia, basi fahamu kuwa Mungu anakukumbusha kuwa, unakaribia kuiacha njia ya wokovu, aidha kuna uamuzi unaokwenda kuufanya ambao utakupotezea ramani yako ya wokovu moja kwa moja, au umeshaanza kuifanya..au kuna dhambi unaitenda ambayo haimpendezi Mungu sasahivi,Hivyo kuwa makini sana.. Shika sana ulicho nacho asiye mwovu akalitwaa taji lako.

Ezekieli 44: 9 Bwana MUNGU asema hivi; Hapana mgeni, ambaye moyo wake haukutahiriwa, wala mwili wake haukutahiriwa, atakayeingia patakatifu pangu, miongoni mwa wageni walio kati ya wana wa Israeli. 

10 Lakini Walawi waliofarakana nami, hapo Waisraeli walipopotea, waliopotea na kuvifuata vinyago vyao, watachukua uovu wao wenyewe.

Kwahiyo jitazame, kumbuka Bwana alipokutoa, usimwache yeye..Mungu anakuonya kwa njia hiyo kwasababu anakupenda..Hivyo ukiona unalolijfanya sasahivi linakutenga na Mungu kama linakushinda nguvu ya kulitawala  basi liweke kando mtafute muumba wako kwanza kwa usalama wa roho yako na hayo mengine yawe baadaye kama yatakuwa na umuhimu.

Ubarikiwe sana.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unafanya Mtihani.

KUOTA UNA MIMBA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIRUHUSU INZI WATUE JUU YA ROHO YAKO.

Kibiblia mapepo yanafananishwa na inzi.

Inzi siku zote huvutiwa na mazingira ya aina mbili. Ya kwanza ni uchafu. Mahali palipo na uchafu hapakosi inzi, Na ndio maana Bwana baada ya kuhakikisha taifa la Misri linanuka uvundo, kwa harufu na uchafu wa wale vyura waliokufa, akawaanda na inzi waje juu yao ili wayafurahie mazingira yao. Ndio hapo utaona akawaleta wengi sana juu ya wamisri wakawa kero kubwa sana kwao.

Kutoka 8:24 “Bwana akafanya; wakaja wingi wa mainzi kwa uzito sana, wakaingia nyumbani mwa Farao, na katika nyumba za watumishi wake, tena katika nchi yote ya Misri; nayo nchi iliharibiwa kwa ajili ya wale mainzi”

Lakini sio hilo tu, watu wengi wanapuuzia wakidhani kuweka mazingira tu safi ndio kutawafukuza. Lakini pia inzi wanavutiwa na mazingira ya vidonda. Palipo na vidonda, utaona inzi wengi wanakusanyika kwenye eneo hilo.

Maana yake nini? Rohoni ukiwa na majeraha ambayo hayajafunikwa au kutibiwa, kunaweza kukusababishia kuvuta uwepo wa mapepo juu ya maisha yako, Unaweza kweli ukawa umejitahidi kuwa mbali na uchafu wa rohoni na mwilini, huibi,huzini,  unaishi maisha ya utakatifu, unatumika kanisani n.k.

Lakini kama una majeraha rohoni mwako,ambayo hayajatibiwa, bado mapepo yanaweza kupata nafasi ya kukusumbua. Una kinyongo cha muda mrefu na mwenzako, hujaachilia, hujasemehe, una uchungu, una wivu, una hasira zisizoachilika,. Fahamu kuwa hayo ni mazingira mazuri ya mapepo.

Ndio hapo utaona mkristo, ameokoka halafu analipuka mapepo, au anasumbuliwa na nguvu za uovu. Unajiuliza mbona huyu hana maisha machafu lakini yanamkuta haya? Sababu kubwa ni eneo hili. Ndio maana biblia inatuambia tulinde sana mioyo yetu kuliko vyote tuvilindavyo. Moyo hukaribisha roho za nje kiwepesi.

Tibu moyo wako, jiachie kwa Yesu, kubali kujikana nafsi, kubali kujishusha, kubali kusamehe, kubali hata kupoteza hicho ulichonacho, ili uiponye nafsi yako. Wivu, hasira, chuki, visitawale kabisa maisha yako. Viwe na adui wako.

Unaweza kusema hizi hali nitazishindaje? Jibu ni kuwa yote hayo yanawezekana endapo tu, utaishi maisha ya kumtazama Kristo, zaidi ya nafsi yako. Macho yako yakielekea kwa Yesu tu daima ukajifunza kwake, kidogo kidogo utaona  tabia za mwilini zinaanza kukuachia, unajifunza tabia za Yesu. Na yeye mwenyewe atakusaidia kukuponya kabisa kabisa kwasababu aliahidi hivyo katika Neno lake.

Hosea 6:1 “Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.  2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake”.

Alisema pia..

Yeremia 30:17 Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye.

Jeraha zetu za rohoni ameahidi kuziponya. Na  Neno lake ni kweli halitanguki, limethibitishwa. Hivyo anza sasa kumkaribia Kristo na kujifunza kwake.(Mathayo 11:28-29)

Bwana akubariki.

Maombi yangu:

Ee, Baba tumejifunza jinsi adui yetu ibilisi anavyopata nafasi katika mioyo yetu pale tunaposhindwa kuzitibu jeraha zetu. Lakini leo tumetambua makosa yetu, nasi tunatubu mbele zako. Tunaomba utusamehe Baba yetu, Tumedhamiria kutoka katika mioyo yetu kukufuata wewe, na kujifunza kwako, Tunaomba ututibu majeraha yetu yote, yaliyodumu kwa muda mrefu na mfupi, ondoa hasira, ondoa vinyongo, kutokusamehe, wivu, ndani yetu. Nasi tunaamini tangu siku ya leo unatukamilisha.  Asante        Baba kwa kutusikia. Tunaomba tukishukuru katika jina la Yesu Kristo. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.(Opens in a new browser tab)

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.(Opens in a new browser tab)

KUOTA UNA MIMBA.(Opens in a new browser tab)

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?

Rudi nyumbani

Print this post