Kwanini Ibrahimu analitaja jina la YEHOVA wakati Musa anasema hakujifunua kwa jina hilo kwao?

Kwanini Ibrahimu analitaja jina la YEHOVA wakati Musa anasema hakujifunua kwa jina hilo kwao?

SWALI: Hujambo mpendwa,naomba nieleweshwe hili tafadhali katika mwanzo 22:14 utaona Ibrahimu alipaita mahali pale YEHOVA-YIRE ambapo alimtoa yule kondoo kuwa sadaka, badala ya Isaka, lakini ukisoma tena katika Kutoka 6:2-3 Mungu anamwambia Musa kwamba hakuwai kujidhihirisha kama YEHOVA kwa Ibrahimu ,Isaka, na Yakobo, bali Mungu mwenyezi. Je! Biblia inajipinga? Asante sana.


JIBU: Kumbuka vitabu vitano vya mwanzo vimeandika na mtu mmoja ambaye ni MUSA (Ambavyo ni Mwanzo, kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na kumbukumbu la Torati ).. Na kama tunavyojua Musa aliviandika vitabu hivi alipokuwa jangwani (yaani akiwa njiani kuelekea nchi ya Ahadi).. Na katika kitabu cha Mwanzo ambacho ndicho tunapata huko habari za Ibrahimu…wakati anaziandika habari hizo akiwa jangwani tayari alikuwa ameshafunuliwa jina hilo jipya la Mungu yaana YEHOVA. Hivyo mahali popote ambapo alisoma habari za Ibrahimu, akimtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa ni lazima angeliandika kwa jina YEHOVA, kadhalika mahali popote ambapo Nuhu angemtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa angesahihisha katika maandishi yake na kuandika jina YEHOVA badala yake..na hivyo hivyo kwa Lutu, Yakobo, Isaka, Yusufu na wengineo.

Sasa utauliza mbona kila mahali katika vitabu hivyo vitano vya kwanza vya Musa kila mahali Mungu katajwa kama BWANA, na si hilo YEHOVA ??

Kumbuka Katika biblia yetu ya Kiswahili na ya kiingereza na ya lugha nyingine zote…kila mahali ambapo leo hii tunapasoma pameandikwa neno BWANA, Kwa asili hapakupaswa paandikwe hivyo…Sehemu nyingi katika agano la lake unapopaona pameandikwa neno BWANA, kwa asili pangepaswa paandikwe neno YEHOVA. Musa nyingi alizitafsiri kama Yehova..kwa mfano katika

Mwanzo 2:7 biblia inasema

“ Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”…Mstari huu Musa aliuandika hivi “Yehova Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai ”

Lakini sasa watafsiri wa kwanza biblia waliona ili kuliheshimu zaidi hilo jina la Mungu si vyema kuandika jina hilo Tukufu na kuu kama lilivyo…Hivyo kwa hekima ya Roho ndipo likawekwa jina BWANA badala ya YEHOVA..Kitu ambacho ni kizuri!..kama tu vile isivyo hekima wala heshima kumwita mzazi wako jina lake halisi na badala yake unamwita jina lake la cheo “BABA”..huwezi kusema shikamoo Joseph badala yake utasema shikamoo Baba. Hivyo si dhambi kumwita Mungu BWANA kama inavyochukuliwa leo na ndugu zetu mashahidi wa Yehova wakidhani kuwa kumuita Mungu BWANA ni kumvunjia heshima..

Biblia zote, pale kwenye utangulizi, zimechapishwa na angalizo hilo pale mwanzoni kabisa.. Kuwa BWANA lilimaanisha YEHOVA.

Kwahiyo kitabu cha Mwanzo kimetaja Yehova na kitabu cha Kutoka kwasababu mwandishi ni huyo huyo mmoja, na aliviandika vitabu hivyo akiwa tayari ameshalijua jina la Mungu kamilifu yaani Yehova.

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?


Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

KWANINI BWANA YESU ALISULUBIWA NA WEZI WAWILI?

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments