Nchi iligawanyikaje kama tunavyosoma katika Mwanzo 10:25?

Nchi iligawanyikaje kama tunavyosoma katika Mwanzo 10:25?

Swali: Je katika Mwanzo 10:25 tunasoma kuwa nchi/dunia iligawanyika? Swali ni Je! Iliwaganyikaje? Na je ule ndio ulikuwa mwanzo wa mabara saba (7) tuliyonayo leo?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 10:25 “ Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi maana KATIKA SIKU ZAKE NCHI ILIGAWANYIKA; na jina la nduguye ni Yoktani”.

Kama ukiendelea mbele kidogo kusoma Mlango wa 11 wa kitabu hiko cha Mwanzo utaona kuna tukio lilitokea ambalo ndio lile la kujengwa kwa Mnara wa Babeli, ambapo watu wale walipokuwa katika hatua za awali za kuujenga Mungu alishuka na kuchafua lugha zao na Semi zao, ili wasisikilizane. Na hiyo ikawafanya waache kuujenga ule mnara na kila mmoja kutawanyika na njia yake.

Mwanzo 11:1 “Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja. 

2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko. 

3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.

4 Wakasema, Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.

5 Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokuwa wakiujenga wanadamu.

6 Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 

7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.

 8 BASI BWANA AKAWATAWANYA KUTOKA HUKO WAENDE USONI PA NCHI YOTE; wakaacha kuujenga ule mji.

 9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote”.

Hapo Mstari wa 8  unasema “BWANA AKAWATAWANYA KUTOKA HUKO WAENDE USONI PA NCHI YOTE”.

Sasa huo Mtawanyiko waliotawanywa wanadamu ndio “mgawanyiko wa nchi” unaozungumziwa katika Mwanzo 10:25 na unarudiwa tena katika 1Nyakati 1:19, Na ulitokea katika nyakati za mtu mashuhuri aliyeitwa “Pelegi” aliyekuwa mwana wa Eberi.

Hivyo mgawanyiko wa nchi haukuwa wa kiografia bali wa watu!.. na wala mabara 7 hayakuzaliwa hapo!, na Zaidi sana biblia haijataja mahali  popote kuwa dunia iligawanyika na kuwa mabara 7, huenda yalikuwa hivi hivi saba tangu uumbaji, au huenda yalizalika kipindi Fulani baada ya uumbaji, tusichokijua sisi lakini  si hiko kilichotajwa katika Mwanzo 10:25. Mgawanyiko huo wa Mwanzo 10:25 unahusu watu na si mabara.

Kujua ufunuo uliopo nyuma ya mnara wa Babeli basi fungua hapa >>TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

MNARA WA BABELI

Babeli ni nchi gani kwasasa?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Shokoa ni nini katika biblia?

YESU KATIKA USINGIZI WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments