Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa kwanza..

Matendo 23:1 “Paulo akawakazia macho watu; wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.

2 Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.

3 Ndipo Paulo akamwambia, Mungu atakupiga wewe, UKUTA ULIOPAKWA CHOKAA. Wewe umeketi kunihukumu sawasawa na sheria, nawe unaamuru nipigwe kinyume cha sheria?”

Makaburi ya zamani sio kama ya zama hizi.. Haya ya wakati yanachimbwa kuelekea chini, na mtu anawekwa kwenye jeneza na kisha kufukiwa chini, lakini makaburi ya zamani hayakuwa hivyo.. Bali yalikuwa katika mfumo wa pango, ambayo linafunguliwa na watu wanawekwa ndani ya hayo mapango, na kisha kwa nje yanarembwa kwa kupakwa chokaa au rangi nyingine ya kuvutia.

Sasa Bwana Yesu alitumia mfano wa makaburi hayo yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje yanaonekana ni mazuri na kuvutia kana kwamba kuna kitu cha thamani ndani, kumbe ndani yake ni mifupa tu imejaa. Alitumia mfano huo kuwalinganisha na watu ambao kwa mwonekano wa nje wanaonekana wanafaa, wanaonekana na wacha Mungu, wanaonekana ni Watumishi wazuri, wanaonekana ni waimbaji wazuri, ni wakristo wa zuri, kumbe ndani yao ni MIFUPA TU!.. Ni wanafiki.. Bwana alisema Ole wa hao!!.

Mathayo 23;27 ‘Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na MAKABURI YALIYOPAKWA CHOKAA, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa MIFUPA YA WAFU, na uchafu wote.

28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani MMEJAA UNAFIKI NA MAASI’.

Hizo ndizo tabia walizokuwa nazo makuhani na mafarisayo wa wakati huo, walikuwa wamejaa unafiki ndani yao, na wana maasi mengi ingawa kwa nje wanasifiwa na watu wote!!.

Na katika siku hizi zetu tunazoishi, mambo haya haya yanajirudia katikati ya watu wa Mungu.. tunaonekana kwa nje ni wakristo wazuri, ni wahubiri wazuri, ni waimbaji wazuri…lakini ndani tuna unafiki uliopitiliza.. Ndani tumejaa viburi, uongo, kutokusamehe, vinyongo, visasi na kila aina ya uchafu!

Bwana Yesu atusaidie tusiwe kuta zilizopakwa chokaa, bali tuwe wakamilifu nje na ndani..

1Wathesalonike 5:22 “jitengeni na ubaya wa kila namna.

23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

TIMAZI NI NINI

Na ulimi laini huvunja mfupa (Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Awey
Awey
1 year ago

Ubarikiwe sana mtumishi wa Bwana Kwa masomo mema