Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu,

SWALI: Kwanini Nuhu alimlaani Kaanani badala ya mtoto wake Hamu, ambaye ndiye aliyekuwa na makosa?


JIBU: Ni kweli kama tunavyosoma katika maandiko, pindi ambapo Nuhu amelima shamba lake la mizazibu akaaanda divai nyingi akanywa akalewa mpaka akalala uchi hadharani, tunaona mtoto wake mmoja aliyeitwa Hamu alipomuona hakuchukua hatua stahiki kumsitiri Baba yake

Lakini wale watoto wake wawili (yaani Yafethi na Shemu) walipomwona baada ya kuambiwa na Hamu, hawakutaka kutazama bali walichukua mavazi yao mabegani Kisha wakaenda kinyume nyume wakamfunika Baba Yao. 

Nuhu alipopata taaarifa, aliyoyafanya mwanawe wa mwisho alimlaani, lakini laana yake haikuwa Kwa Hamu Moja Kwa Moja Bali Kwa mtoto wake aliyeitwa Kaanani..Sasa swali ni je Kwanini afanye hivyo Kwa Kaanani mjukuu wake, angali kitendo kimetendwa na Hamu.

Mwanzo 9:20-25

[20]Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; [21]akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. [22]Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. [23]Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. [24]Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. [25]Akasema, Na alaaniwe Kanaani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

Ipo mitazamo mingi katika jambo hilo, wapo wengine wanaomini kuwa Shemu alikuwepo na mwanaye huyo mkubwa Kaanani, na huwenda yeye naye alipuuzia kumsitiri Babu yake, au alifanya jambo baya kwake,  wengine wanasema Hamu tayari alikuwa amebarikiwa na Mungu hivyo Baba yake asingeweza Tena kumlaani mtu ambaye amebarikiwa (Mwanzo 9:1),ndio maana laana akaisogeza kwa mjukuu wake.

Wengine wanaaanimi aliposema alaaniwe Kaanani, ni lugha tu iliyomaanisha pia “Baba wa kaanani”

Lakini ni vema tukaona muktadha wa uandishi wote, ikumbukwe kuwa aliyekiandika kitabu hicho ni Musa, na tunafahamu hatma ya taifa la Israeli, ilikuwa si katika mataifa yote duniani, bali pale Kaanani. Hivyo, ulikuwa ni unabii, wa Nuhu, kuonyesha moja wa uzao Shemu uitwao kaanani utalaaniwa. Hivyo tunapokuja kusoma juu ya anguko la wenyewe wa taifa lile, walivyoangamizwa na kuteketezwa na taifa la Israeli, ni kutukumbusha kuwa tayari Kaanani ilikuwa imeshalaaniwa tangu zamani, kuangamizwa kwao na maovu yao ni matokeo ya laana iliyotajwa zamani.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).

Wakaanani walikuwa ni watu gani?

saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments