MIRIAMU

MIRIAMU

Miriamu alikuwa ni dada yake Musa na Haruni, wa damu (Hesabu 26:59), Miriamu ndiye aliyekuwa wa mwisho kuzaliwa katika famila ya Yokebedi na Amramu. Biblia inasema naye pia alikuwa ni nabii. Hawa watatu Bwana aliwaita kipekee kuhudumu katika hatua ya kuwaongoza wana wa Israeli. (Mika 6:4)

Huduma ya Miriamu ilikuwa ya kipekee na kielelezo kwa wanawake, kwani baada ya Bwana kulipiga jeshi la Farao kwa kulitosa kwenye Bahari ya Shamu, Miriamu alisimama na jeshi kubwa pamoja na wanawake wenzake, wakamwimbia Bwana kwa MATARI na kucheza! (Kutoka 15:20-21).

Wakiwa jangwani katika safari yao ya kwenda nchi ya Ahadi. Miriamu pamoja na Haruni walianza kumnenea Musa, na kumlaumu, kwasababu ya Mwanamke wa kiKushi aliyemwoa. Jambo hilo likamchukiza sana Bwana na hatimaye Bwana kumpiga Miriamu kwa ukoma. Lakini baadaye alikuja kupona baada ya Musa kumwombea. (Kutoka 12:1-6).

Miriamu alikufa kabla ya kuiona nchi ya Ahadi, alikufa katika Bara la Sini, huko Kadeshi, na huko ndiko alikozikiwa.(Kutoka 20:1).

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1.Musa ni nani?

2. Haruni ni nani?

3. Fimbo ya Haruni ilikuwaje?

HOME

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments