Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?

Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?

SWALI: Mstari huu una maana gani? 1Wakorintho 2:15 “Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”?


JIBU: Ukianza kusoma kuanzia ile mstari wa kwanza utaona mtume Paulo, akieleza vizuri maana halisi ya kuwa mtu wa rohoni.. mtu wa rohoni sio mtu anayeona wachawi, au anayeota ndoto, au anayeona maono, mtu anaweza akawa na vipawa hivyo vyote lakini bado asiwe ni mtu wa rohoni.

Kulingana na mistari hiyo mtu wa rohoni ni mtu aliye na ufahamu wa kuzitambua siri za Mungu kwa Roho Mtakatifu. Na siri kuu ya Mungu ipo katika kumjua Yesu Kristo, ambayo biblia inasema kama watawala wa dunia hii wangeijua , wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu;(1Wakorintho 2:8)..

Unaona, wangejua kuwa suluhisho la mambo yote lipo kwa Yule, maarifa yote na siri zote walizokuwa wanazitafuta kwa miaka na miaka zipo kwa Yule, wasingemsulibisha…biblia inaeleza kabisa..Lakini walifumbwa macho yasione, hivyo wakabakia kuyatambua mambo ya mwilini tu.

Yohana 12:37 “Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;

38 ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema, Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu; Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

39 Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena,

40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.

41 Maneno hayo aliyasema Isaya, kwa kuwa aliuona utukufu wake, akataja habari zake”.

Hivyo ukiona wewe kila siku unamjua Kristo katika viwango vingine, basi ujue kuwa wewe ni mtu wa rohoni mwenye viwango vya hali ya juu..Ukiona kila usomapo Biblia unaziona habari za Yesu, kila ukitazama vitu vya asili unaiona injili ya Yesu, kila Ukitazama Maisha ni kama unayasikia maneno ya Yesu yanazungumza na wewe masikioni yanakuonya kila unalotaka kulifanya unatamani liwe linalompendeza Yesu… hapo wewe ni mtu wa rohoni…Na sio ukisoma biblia unaona wachawi, au ukisali unaona wachawi hapo bado hujawa mtu wa rohoni.

Na ndipo hapo biblia inasema.. mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.. Utakuwa na uwezo wa kuyatambua mambo yote, na siri zote za Mungu wanadamu wasizozijua…hakuna jambo lolote litakuwa ni jipya machoni pako na zaidi ya yote bado utakuwa hautambuliwi na yeyote.. Yaana maana yake, hakuna mwanadamu yeyote mwenye tabia ya asili atakayeweza kukutambua, akikuangalia ataishia tu kuona vya nje, watasema umerukwa na akili kama vile Paulo alivyoambiwa, wengine watasema una mapepo, kama vile Yohana Mbatizaji alivyoambiwa..Wengine watakauambia umelogwa..

Ni kwasababu ufahamu wao umeishia hapo kwenye mambo ya nje, hawawezi kuona zaidi ya hapo..furaha na tumaini lililopo ndani yako..Hawajui kuwa ndani yako ni Roho Mtakatifu anakufundisha, lakini wewe utakuwa na ufahamu wa kuelewa yao yote. Utagundua kuwa wanavyokufikiria wewe sivyo ulivyo.

Hivyo upo umuhimu wa kumpa Kristo maisha yako, kama hujampa au kama ulishampa hapo kabla na ukapoa ni wakati wa kuweka mambo yako sawa..Ili Roho wa Mungu awe na nafasi ya kukufunulia yale usiyoyajua kuhusu Bwana Yesu Kristo.

Ubarikiwe.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618

  Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments