Jina Lusifa (lucifer), tunalisoma wapi kwenye biblia? 

Jina Lusifa (lucifer), tunalisoma wapi kwenye biblia? 

JIBU: Hakuna Mahali popote katika biblia ya Toleo letu la Swahili Union version (SUV) au matoleo mengine kadha wa kadha ya kiswahili, utapishana na hili Neno Lusifa. Lakini swali, kama ni hivyo Kwanini tunalitumia kumwakilisha shetani. Je! Limetokea wapi?

Neno hili ni la kilatini, ambalo linamaanisha NYOTA YA ALFAJIRI. Hivyo tukirudi katika maandiko upo unabii katika kitabu Cha Isaya unaomwelezea shetani, na unamtaja yeye kama ndio  Ile “Nyota ya alfajiri”

Isaya 14:12

[12]Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!  Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

Hivyo watakatifu wa zamani, walipokuwa wanatafsiri biblia kutoka katika lugha ya kiyahudi kwenda kilatini (vulgate), kwenye Karne ya 4  Ndipo Neno hili nyota ya alfajiri ambalo linalosomeka kama “Helel” Kwa lugha ya kiebrania likaandikwa kama “lusifa” Kwa kilatini.

Na baadaye Neno hili lilikuja kupata umaarufu, zaidi katika biblia ya Toleo la kiingereza inayojulikana  kama King James version (KJV), kwani waliendelea kuliacha Neno hili la kilatini, Mahali palepale  panaposema nyota ya alfajiri. 

Hivyo umaarufu wa Neno hilo ukasambaa sio tu Kwa waongeaji wa lugha ya kilatini, Bali mpaka Kwa wale wa kiingereza. Na ndio maana mpaka sasa wewe unalifahamu.

Lakini matoleo mengine mengi, Ikiwemo letu hili la kiswahili (SUV), haikutoa katika hiyo lugha ya kilatino, Bali imeacha vilevile kama nyota ya alfajiri.

Hivyo Kwa kuhitimisha ni kuwa shetani ndio huyo huyo Lusifa. Ikiwa utapenda kufahamu majina yake mengine kama yanavyotajwa kwenye biblia basi fungua hapa >>> APOLIONI.

Je! Unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Kumbuka shetani anatambua kuwa muda wake umeisha(Ufunuo 12:12), iweje wewe usitambue. Ni nini unachokisubiria usimkaribishe Yesu katika maisha Yako?  Huu ulimwengu hauna muda mrefu unaisha, itakufaidia nini upate kila kitu, kisha upate hasara ya nafsi yako? Jifikirie  usisubiri kukumbushwa kumbushwa, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi, kisha uchukue hatua

, ikiwa upo tayari Kumpa Bwana Yesu maisha yako, basi fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

 Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Shetani ni nani?

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Moses Simiyu
Moses Simiyu
8 months ago

My name is Moses Tom Simiyu being blessed with your lesson. But recently i lost my phone. But i was very much interested with that topic of ALAMA YA YESU. PLEASE can you resent me that topic. Thank you.