Kujikinai/kukinai ni nini?

Kujikinai/kukinai ni nini?

Neno hilo kama linavyotumika kwenye biblia..linamaanisha aidha mojawapo ya mambo haya matatu:

  1. Kushiba Hadi kufikia hatua ya kutokipenda Tena kile ulichokipokea Mwanzo.
  2. Kuwadharau wengine Kwa kufanya mambo ambayo huruhusiwi kuyafanya
  3. Kujigamba/kujiona wewe unajitosheleza Kwa HAKI yako.

1. Kwamfano katika vifungu hivi limetumika kwa tafsiri ya kushiba,..

Mithali 27:7

[7]Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali;  Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.

Mithali 25:17

[17]Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi;  Asije akakukinai na kukuchukia.

Mhubiri 1:8

[8]Mambo yote yamejaa uchovu usioneneka, jicho halishibi kuona, wala sikio halikinai kusikia.

2). Lakini pia vifungu hivi, vinaeleza kukinai kama kuonyesha kudharau wengine, kwa kukaidi maagizo kwa makusudi.

Kumbukumbu la Torati 17:12

[12]Na mtu afanyaye kwa kujikinai, kwa kutomsikiza kuhani asimamaye hapo kwa kumtumikia BWANA, Mungu wako, au mwamuzi, na afe mtu huyo; nawe utauondoa uovu katika Israeli.

Soma pia.. Kutoka 21:14

3) Halikadhalika mahali ambapo kunaonesha kujikinai kama kujihesabia haki mwenyewe ni hapa

Luka 18:9-14

[9]Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

[10]Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

[11]Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

[12]Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

[13]Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.

[14]Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Soma pia 2Petro 2:11, 

Hivyo na sisi hatupaswi kuwa na sifa hizo mioyoni mwetu. Uendapo mbele za Bwana, Acha kujihesabia haki, Bali jinyenyekeze penda kuomba rehema Kwa Bwana, zaidi ya kueleza sifa zako..na hatimaye Mungu atakuridhia, kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi na kuwapa neema.wanyenyekevu.

Amen

Je! Umeokoka? Ikiwa bado na unapenda Kristo akusamehe dhambi zako zote, na akupe uzima wa milele. Basi fungua hapa ili uweze kupata mwongozo sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Mawaa ni nini? Kama tunavyosoma katika biblia?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

UUNGU NI NINI? (1Petro 1:3-4)

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments