Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 24:67 “Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake”.

Andiko hilo halimaanishi kuwa Isaya alipendezwa na kifo cha mamaye Sara, na hivyo akapata faraja kwa kufa kwake, bali linamaanisha kinyume chake.

Ikumbukwe kuwa Isaka alikuwa ni mwana pekee wa Sara, na Isaka alimpenda sana mama yake, na siku mama yake alipokufa ni wazi kuwa alihuzunika kwa kipindi kirefu,  lakini sasa kipindi anampata Rebeka kama mke wake, ile huzuni ikapungua kwa kiasi kikubwa na akajihisi faraja kama tu ile aliyokuwa anaipata kutoka kwa mama yake.

Ni nini tunajifunza kutoka katika habari hiyo?.

Hapa tunajifunza jinsi mwanamke wa kiMungu anavyopaswa awe!..

Rebeka alikuwa ni mwanamke wa mfano wa kuigwa, kwani aliweza kuwa faraja kwa mume wake kiasi kwamba mume wake akasahau uchungu wote wa kufiwa na mamaye (Maana yake Rebeka alikuwa ni mke kwa Isaka na hapo hapo mama kwa Isaka, kumlea na kumtia moyo). Lakini leo hii wanawake wengi wanafanyika mishale kwa waume zao, na si faraja.

 Mama, dada, binti, msichana kabla ya kwenda kujifunza kwa akina Musa, Eliya, na Danieli, hebu kwanza tenga muda wa kujifunza juu ya wanawake hawa.. Kwasababu tabia ya Musa haitakusaidia sana katika uanawake wako zaidi ya akina Rebeka, au Sara au Mariamu au Ruthu..

Ukitaka kuwa mke bora na mama bora kajifunze kwa akina Hana, Debora, na Tabitha..ukitaka kuwa binti bora nenda kajifunze kwa mashujaa wote wa kike katika biblia kabla ya kuwakimbilia wanaume.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

CHUKI ULIZO NAZO KWA MAADUI ZAKO, SIZO ALIZONAZO MUNGU JUU YAO.

KWANINI KRISTO AFE?

Nilikuwa naomba kujua utofauti kati ya DHAMBI, UOVU na KOSA kibiblia.asante!!

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments