Title May 2025

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

Jibu: Turejee..

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na MAMLAKA, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.

Hapa kuna vitu vinne, vilivyogawanyika katika sehemu mbili.. Kundi la kwanza ni “FALME na MAMLAKA” na kundi la pili ni “WAKUU WA GIZA na JESHI LA MAPEPO” jumla mambo manne (4)

Sasa hebu tuanze na kundi la kwanza la FALME na MAMLAKA.

Mwandishi (ambaye ni Paulo, Mtume wa Bwana YESU) alitumia mfumo wa Tawala za dunia, kutoa picha ya tawala za ufalme wa giza.

Katika Dunia tunajua kunakuwa na Falme za wanadamu… Kwamfano kuna Falme za kiafrika, falme za kiarabu, Falme za kiasia n.k,

Sasa kwa vizazi vyetu nyakati hizi mfano wa Falme ni hizi SERIKALI tulizonazo (ambapo kila nchi inayo serikali yake), lakini zamani za kale Falme zilibaki kuitwa falme..Kwamfano kwenye Biblia utaona kulikuwa na Ufalme wa Umedi na Uajemi, Ufalme wa Babeli, Ufalme wa Uyunani, Ufalme wa Rumi n.k.. Hizi zote zilikuwa ni falme na ziliongozwa na Wafalme.. kwahiyo katika ulimwengu kulikuwepo na Falme Nyingi, zenye wafalme wengi, lakini dunia ni moja.

Tusogee mbele zaidi..

Chini ya kila Falme (au serikali) kunakuwa na Mamlaka, kwamfano katika Serikali ya nchi ya Tanzania, kuna Mamlaka mbalimbali, kuna Mamlaka ya mapato (TRA), Mamlaka ya Maji safi na maji taka, Mamlaka ya mawasiliano, Mamlala ya Hali ya hewa, Mamlaka ya Elimu, Mamlaka ya bandari n.k, hivi vyote ni viungo vya Serikali kwaajili ya kuwahudumu walio chini ya Serikali/Ufalme.

Kwahiyo tunaweza kurahisisha kwa kusema mfano huu, “Vyanzo vya maji vyote vilivyopo katika UFALME wa Tanzania vipo chini ya MAMLAKA ya maji ya maji ya nchi hiyo”… au Ukusanyaji wa kodi za wananchi katika Ufalme/serikali ya Tanzania upo chini ya MAMLAKA ya Ukusanyaji mapato (TRA)….Au jukumu la Ulinzi wa raia na mali zao la Ufalme wa Tanzania lipo chini ya Mamlaka ya ulinzi na usalama kupitia chombo chake maalumu kiitwacho Polisi….Umeona huo muunganiko wa Ufalme na Mamlaka?.

Na kawaida kila Mamlaka inayo Wakuu wake na jeshi.. Ndio hapo utasikia “Mkuu wa mamlaka ya mapato” au Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano,  na jeshi zima la mamlaka hiyo ni wafanya kazi wote waliopo chini ya mamlaka hiyo..

Na katika ULIMWENGU wa giza ni hivyo hivyo, kuna FALME na pia kuna MAMLAKA mbalimbali… Zipo mamlaka za uuaji na utekaji (mfano wa hizo ni zile zilizoruhusiwa kumkamata Bwana YESU (Soma Luka 22:53),

zipo mamlaka za uharibifu wa ndoa, zipo mamlaka za uharibifu wa huduma, zipo mamlaka za uharibifu wa familia, kazi n.k n.k,

Na kila mamlaka ya giza inayo Mkuu wake/Kiongozi ambaye ni Pepo (hao Ndio wanaoitwa wakuu wa giza)..  Hapa ndipo tunapofika katika kundi la Pili la WAKUU WA GIZA na MAJESHI YA MAPEPO.

Sasa kama kuna kiongozi au mkuu, ni wazi kuwa kuna Jeshi chini yake, (hakuna kiongozi/mkuu asiye  na jeshi la watu chini yake la kuliongoza)

hivyo mapepo yote yaliyosalia yanayofanya kazi chini ya Wakuu wa giza ndio wanatengeneza kundi la majeshi ya mapepo wabaya.

Kwahiyo Biblia inaposema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya FALME NA MAMLAKA NA WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, imemaanisha kuwa tunapambana na wakuu wa giza (Wakuu wa mapepo) na majeshi yao ambayo yanatumia Mamlaka na Ufalme wa giza kupambana nasi.

Kwahiyo ufalme wa giza, imesimama katika ngazi zake, kuonyesha kuwa vita vyetu si virahisi kama tunavyovichukulia, kupambana na falme si kazi ndogo! Inahitaji msuli wa kutosha wa kiroho, maana yake ni lazima mtu uwe umesimama kwelikweli, umezama kweli kweli kwenye ufalme wenye nguvu kuliko huo wa giza.

Na hakuna ufalme mwingine wenye nguvu kuuzidi ufalme wa giza, zaidi ya UFALME WA MBINGUNI, ambao Mkuu wa Ufalme huo ni YESU KRISTO (Mwamba Mgumu). Huyo ndiye mwenye nguvu za kuuvunja nguvu zote za falme za giza, na hana namba mbili yake!..

Je unaye YESU moyoni na maishani?.. Kama hujaokoka fahamu kuwa upo chini ya ufalme wa giza na mamlaka za giza hata kama ni tajiri, au una afya au una mafanikio mengine yote, bado upo chini ya utawala wa giza, wanaweza kukufanya chochote kwa wakati wowote, na wanaweza kukutumia vyovyote watakavyo, Mgeukie YESU leo na uhame kutoka katika huo ufalme wa giza.

Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.

17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

Print this post

Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?

Swali: “Halafu ile tama ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti, (Yakobo 1:15).. je kutamani sio dhambi?”


Jibu: Kwa asili kutamani sio dhambi! Bali kunaweza kuwa ni mwanzo wa dhambi.. ni sawa na “kuongea”..kuongea si dhambi lakini kunaweza kuwa chanzo cha dhambi, kutegemea ni nini unaongea..

Na vile vile “tamaa” kwaasili ..imeumbwa ndani ya Mtu, na hata ndani ya viumbe vyote, ambayo lengo lake ni kuhamasisha jambo fulani jema au baya lifanyike katika mwili wa mtu au maisha ya mtu.

Kwamfano hatuwezi kumtafuta MUNGU kama yeye mwenyewe hajaiweka hiyo tamaa ndani yetu..hatuwezi kuomba kama yeye hatatuwekea hiyo tamaa ndani yetu n.k

Vile vile katika masuala ya mwilini,  tusingependa kula wala kuhamasika kula chakula kama tusingewekewa ndani yetu tamaa ya chakula, ile tamaa iliyowekwa ndani inatuhamasisha kula chakula, na tunapokula miili yetu inapata faida, na kutimiza lengo la kuendelea kuishi.. Lakini tamaa hiyo inapozidi mipaka inazaa ulafi na ulevi ambao ni dhambi (Soma Luka 21:34, Warumi 13:13, Wagalatia 5:21, na 1Petro 4:3).

Vile vile pia mtu kawekewa tamaa ndani yake ya kimwili kwa jinsia tofauti na yake, tamaa hiyo Mungu kaiweka ndani ya mtu kwa kusudi maalumu na wakati maalumu, kwamba wakati utakapofika mtu aweze kukutana na mke/mume wake na kuzaa watoto, kutimiza Baraka  alizozisema katika Mwanzo 1:28

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi:”.

Lakini tamaa hiyo inapozidi na kuvuka mipaka kiasi kwamba inampelekea mtu kushindwa kujitawala ndipo anapoanguka katika zinaa na hata zinaaa ya jinsia moja na yake.

Kwahiyo tamaa yoyote ile iwe ya chakula, au ya mwili  kwaasili sio mbaya, ila inapozaa matunda mabaya ndipo inageuka kuwa dhambi..Na ndicho Biblia ilichokimaanisha hapo katika  Yakobo 1:15 kuwa “tamaa ikiisha kuchukua mimba inazaa dhambi”..maana yake katika uasili wake sio dhambi!.. ila inapochochewa kwa njia isiyopaswa ndipo inapozaa dhambi.

Unatazama picha chafu mitandaoni, au unaposoma makala zenye maudhui ya zinaa, au unaposhiriki mijadala yenye maudhui ya zinaa  hapo unaizalia matunda ile tamaa ya mwili ndani yako, na hiyo ni dhambi, kwasababu mwisho wa siku itakupelekea kufanya zinaa au kujichua, au mawazo yako muda wote kutawaliwa na zinaa jambo ambalo biblia imesema kuwa ni machukizo kwa Bwana, moyo uwazayo mabaya (Mithali 6:18).

Biblia inatufundisha kutoyachochea mapenzi..

Wimbo 2: 7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Na tamaa nyingine zote ni hivyo hivyo, hatuna budi kuzitawala ili zisizae dhambi, maana mshahara wa dhambi ni Mauti… na tamaa zinazozaa dhambi zote zinatokana na dunia na si MUNGU..

1Yohana 2:16 kuwa tamaa  ya macho na tamaa ya mwili inatokana na dunia na si Mungu

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Roho ya kukata tamaa ni nini na inatendaje kazi?

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?

Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini.  Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.

Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani  Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)

Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine  mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.

Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea  nguvu zetu tu wenyewe.

Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.

7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na  mwili,

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Hitimisho:

Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.

Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.

Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Print this post

Kwanini Nyaraka za Paulo kwa makanisa tuzifanye kuwa nyaraka zetu leo?

Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?


Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,

Alikuwepo mwanasayansi mmoja  wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).

Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).

Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.

Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,

Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.

Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..

Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.

Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.

Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.

Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.

Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.

Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.

Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.

Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Print this post

SADAKA INAONDOA MADHARA YA MAUTI

Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.

Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..

Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..

Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.

Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.

Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…

1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.

3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”

Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.

Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..

Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.

Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.

Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.

Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..

Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Kibiblia, hekima, ni uwezo wa  kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.

Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)

Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,

Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.

Lakini inapatikanaje?

Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.

Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.

Yesu anapatikana wapi?

Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.

Anapazaje sauti?

Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.

Hivyo, hilo andiko linalosema,

Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.

Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.

Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Kati ya Exegesis na Eisegesis. Ni ipi namna  bora ya kutafsiri maandiko?

JIBU: Haya ni maneno ya kiyunani, yanayoeleza namna tofauti ya kutafsiri maandishi.

1) Eksejesisi (exegesis).

Ni namna ya kutafsiri maandiko kwa kuzingatia mtazamo wa awali uliokusudiwa na mwandishi, kwa kuzingatia muktadha, hali ya kihistoria, matamshi na matumizi ya lugha.

2) Eisojesisi ( Eisegesis).

Ni namna ya kutafsiri Maandiko kwa namna ya mtazamo wa mtu mwenyewe, kwa kulileta andiko liendane Na wazo lake binafsi,. Namna hii haitilii maanani sana kusudio La kwanza la mwandishi, bali lile aliaminilio kuwa ni sahihi Kwake. (Mfano wa hii ni ile namna ya kusema nimefunuliwa)

Kwa ufupi eksejesisi ni Kuliruhusu andiko lijitafsiri lenyewe huku Eisojesisi ni lilete andiko litafsiri ninachokitaka au kiamini.

Je ipi inakubaliwa na Mungu?

Ijapokuwa Eksejesisi,(tafsiri ya awali) ndio msingi hasaa wa kusimamia katika kuyaelewa maandiko lakini eisojesisi pia Mungu huitumia kusema na sisi katika nyakati Fulani.

La kuzingatia ni kwamba kabla hujaipokea namna nyingine.. Ifahamu kwanza asili ya kwanza ya andiko hilo, ilikuwa ni nini.

Kwamfano Bwana Yesu aliposema.

Mathayo 11:28

[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

Katika Eksejesisi hiyo mizigo inayozungumziwa hapo na Bwana Yesu sio umaskini, Mateso, madeni, familia, majukumu,n.k. hapana, bali mizigo ya dhambi. Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha na kusudi la kwanza lililomfanya kuja duniani lilikuwa ni hilo kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi zake.

Lakini pia Bwana anaweza tumia andiko hilo kulenga na mizigo mingine, kwasababu ni ukweli usiopingika alisema pia tumtwike yeye fadhaa zetu zote.

1 Petro 5:7

[7]huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Hivyo namna zote Mungu anaweza kutumia kutujenga. Kwasababu Neno lake ni pana na njia zake hazichunguziki, katika kuwajenga, kuwafariji na kuwaponya watu. Isipokuwa hatari inakuja mtu kukosa kulipambanua vizuri Neno na matokeo yake kutegemea zaidi mtazamo (alioupokea), na kuacha biblia yenyewe kujieleza.

Hii ndio Imekuwa chumbuko la mafundisho mengi ya uongo, na potofu, kwamfano mtu atasema chapa ya mnyama (ufunuo 13) Ni ugonjwa wa Korona (covid-19). Wakati si kweli.

Au mtu atasema Yesu alitengeneza matope kwa mate yake akampaka mtu machoni akaona,(Yohana 9:6-7) hivyo na sisi kufanya kwa namna hiyo si kosa. Kumbe lile lilikuwa ni “ingilio la Mungu” la wakati husika lakini sio agizo la kudumu. Kwani agizo la daima ni kutumia jina la Yesu kutenda/kuamuru jambo lolote.(Kol 3:17)

Hivyo ili kubaki katika upande sahihi ni vema ukajifunza eksejesisi, (kufahamu muktadha wa kimaandiko), na ndio pale esiojesisi inapokuja Basi unaeweza Kuligawanya vema Neno la Mungu. Bila kuleta uharibifu/ madhara yoyote, katika imani au kwa kile unachowafundisha wengine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

MUNGU WETU HUONDOA CHANZO PAMOJA NA MKONDO WAKE.

Jina la Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu, lilio taa na mwanga wa njia yetu.

Unapofika wakati MUNGU wetu wa UPENDO, anapotaka kututoa sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa kuondoa matatizo makuu yanayotishia maisha yetu, basi huo haondoi tu chanzo cha tatizo bali pia na mkondo wake wote anauondoa.

Ili tuende pamoja, hebu turejee wakati Bwana YESU anazaliwa, maandiko yanasema Herode alitafuta kumwua mtoto YESU, lakini Yusufu na Mariamu kupitia onyo la Malaika wa Bwana waliambiwa wakimbilie Misri ili Herode asimwue mtoto.

Lakini jambo la ajabu ni kwamba baada ya Herode kufa, biblia inatuambia hakufa peke yake bali na wengine waliokuwa na nia kama ya kwake ya kumwangamiza mtoto, ambao biblia haijawataja majina yao.

Mathayo 2:19 “Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,

20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana WAMEKUFA WALIOITAFUTA ROHO YA MTOTO”.

Hapo anasema “WAMEKUFA”..na si “AMEKUFA”  Maana yake hakuwa mmoja bali wengi, maana yake si Herode peke yake, walikuwepo na wengine waliokuwa na nia kama ya Herode…huenda wakuu wa majimbo waliofanya kazi na Herode, au makuhani au raia wa kawaida.

Kwahiyo waliokuwa wanaitafuta roho ya mtoto, hawakuwa wachache, bali wengi (ulikuwa ni mkondo) na wote walikufa..Herode alikuwa tu ni kichwa cha pweza, lakini mikia ilikuwa mingi!.

Endapo Yusufu na mtoto wangeendelea kubaki Bethlehemu walikuwepo wapelelezi wengi hivyo taarifa kuhusu mtoto zingemfikia Herode haraka, hata baada ya yale maangamizi kupita bado hatari ilikuwepo, kwahiyo suluhisho ni wote wafe kwanza ndipo usalama uwepo wa Bwana YESU kurudi Israeli.

Sio hilo tu, utakumbuka pia ile habari ya Malkia Esta, wakati Hamani, adui wa wayahudi alipoandika waraka wa wayahudi wote kuuawa, katika siku moja!.. kama ni mwanafunzi wa Biblia utagundua kuwa si Hamani peke yake aliyekuwa adui wa waisraeli kwa wakati ule!, bali walikuwepo wengine wengi katika kila jimbo la mfalme Ahasuero,  Hamani yeye alikuwa ni kichwa tu cha pweza kama alivyokuwa Herode!.

Ndio maana mambo yalivyoharibika kwa Hamani, hakufa peke yake bali na maadui wote wa wayahudi katika ufalme wote.

Esta 9:1 “Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile ADUI ZA WAYAHUDI walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia;

2 siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. …….

5 Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.

6 Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza…………

16 Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, WATU SABINI NA TANO ELFU; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono”.

Watu zaidi ya Elfu 75 walikufa pamoja na HAMANI, ingawa kwa haraka tunaweza kuona kama aliyekuwa adui wa wayahudi alikuwa ni Hamani peke yake, kumbe hakuwa peke yake bali ulikuwa ni mkondo mkubwa ibilisi alioutengeneza kwa muda mrefu!.

Hivyo ukiona mtu mmoja mashuhuri anafanya vita na wewe katika vitu vilivyo sahihi unavyovifanya basi fahamu kuwa hayupo peke yake bali upo mkondo wa ibilisi nyuma yake!, na wakati wa MUNGU ukifika huwa anakiondoa chanzo na mkondo wake, ili amani irejee..

Na MUNGU anapokiondoa chanzo na mkondo wake si lazima awaue maadui zako kama inavyodhaniwa  na wengi, La! Kifo chaweza kuwa njia ya mwisho kwa MUNGU wetu dhidi ya tunaowaona kama maadui zetu,

Lakini badala yake MUNGU anaweza kuwahamisha na kuwapeleka mbali au kukuhamisha wewe ukae mbali nao sehemu salama, au  anaweza kuwabadilisha na kuwafanya watu wazuri (wakamrudia MUNGU)..na lile tatizo likawa limeondoka, na hambadilishi yule chanzo tu peke yake, bali na mkondo mzima, Ndio hapo unashangaa watu waliokuwa wanakuchukia na kukupiga vita sasa wanakupenda, waliokuwa maadui zako sasa mnaishi kwa amani n.k

Swali: Niombe maombi gani ili Mungu aondoe chanzo cha matatizo na mkondo wake?

Badala ya kufikiri namna ya kuomba, fikiri kuzitengeneza njia zako mbele za MUNGU, njia zako zinaponyooka mbele za MUNGU (kwa kuishi maisha ya kumpendeza MUNGU), basi MUNGU anashughulika na vyanzo vyote na mikondo yake, kwa kukurejeshea amani..

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Lakini usiponyoosha njia zako kwa MUNGU, na ukategemea maombi tu peke yake, bado safari itakuwa ndefu, Maisha yetu yanajalisha sana katika kuelezea vyanzo vya matatizo tuliyonayo, yakizidi kuwa safi mbele za MUNGU ndivyo matatizo yatakavyozidi kuwekwa mbali.

Je umempokea YESU?.

Unao uhakika Bwana YESU akirudi leo unakwenda naye?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.

Print this post

What Are the Different Types of Psalms?

If you’ve ever spent time reading the Psalms, you’ve probably noticed how wide-ranging they are—some feel like joyful songs, others like raw cries for help. That’s because the Psalms were written in different styles and for different purposes. Over time, scholars and readers have grouped them into a few main types to help us better understand them. Here’s a more down-to-earth look at each one:

🌟 1. Psalms of Praise

These are the joyful, uplifting psalms that focus entirely on God—who He is, what He’s done, and why He deserves our worship. They usually invite people (or even all of creation) to praise God and then give reasons for doing so.

  • Think: Big-picture awe and wonder.
  • Examples: Psalm 100, Psalm 148
  • Typical line: “Make a joyful noise to the Lord!”

😔 2. Psalms of Lament

These are some of the most emotional psalms. The writer is usually going through something really hard—feeling abandoned, attacked, or just overwhelmed—and cries out to God for help. What’s beautiful is that most of these still end with hope or a promise to trust God no matter what.

  • Think: Honest prayers from a hurting heart.
  • Examples: Psalm 13, Psalm 22
  • Typical line: “How long, O Lord? Will You forget me forever?”

🙏 3. Psalms of Thanksgiving

These are the “thank you” psalms. They usually reflect on a time when the writer was in trouble, called out to God, and then experienced His rescue or provision. It’s a look back at God’s faithfulness.

  • Think: Testimony in song form.
  • Examples: Psalm 30, Psalm 107
  • Typical line: “You turned my mourning into dancing.”

📖 4. Wisdom Psalms

These psalms feel more like life advice than a song. They talk about right and wrong, wise and foolish choices, and what it looks like to live in a way that honors God. Some sound like they could come straight from Proverbs.

  • Think: Spiritual guidance, usually contrasting good vs. evil.
  • Examples: Psalm 1, Psalm 119
  • Typical line: “Blessed is the one who does not walk in the counsel of the wicked.”

👑 5. Royal Psalms

These focus on kingship—sometimes about the earthly king of Israel (like David), and sometimes pointing ahead to the Messiah. They remind us that God is King over everything and that He works through leaders to bring justice.

  • Think: Big picture of God’s rule and promises.
  • Examples: Psalm 2, Psalm 72
  • Typical line: “You are my Son; today I have begotten You.”

💢 6. Imprecatory Psalms

These are the tough ones. In these psalms, the writer asks God to deal harshly with enemies or bring justice to evildoers. They come from a place of deep pain or injustice—not out of personal revenge, but a plea for God to act righteously.

  • Think: “God, this isn’t fair—do something!”
  • Examples: Psalm 69, Psalm 137
  • Typical line: “Let their names be blotted out of the book of life.”

These categories aren’t rigid—many psalms overlap. A lament might turn into praise. A royal psalm might include thanksgiving. That’s part of what makes the Psalms so real and relatable: they reflect the full range of human emotion and experience in our relationship with God.

Print this post

PEPETO LA BWANA LINAPITA.

Shalom,

Je unajua Pepeto ni nini na kazi yake ni ipi?

Turejee Mathayo 3:11-12.

Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

12 Ambaye PEPETO LAKE li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya NGANO yake ghalani, bali MAKAPI atayateketeza kwa moto usiozimika”.

Pepeto ni kifaa maalumu chenye umbile kama la “UMA” ambacho wakulima wa nafaka kama ngano, wanakitumia kupuria/kupepetea ngano.. sasa jamii zetu zinatumia NYUNGO kupepetea nafaka kama mchele na ngano, ambapo ungo ule unazurusha juu nafaka kisha upepo unatenga ile nafaka na makapi.

Lakini zamani wakulima wa ngano hawakutumia nyungo, kwani kulikuwa na matita mengi ya ngano, hivyo UNGO usingetosha kuimaliza kazi yote, hivyo walitumia kifaa hiko kinachoitwa Pepeto, ambacho kinafanana sana na UMA. (Tazama picha chini).

pepeto ni nini

Sasa kiroho Ngano ni “NENO LA MUNGU”, na makapi ni “NDOTO NA MAONO YA UONGO” katika siku za mwisho Bwana atatenga Neno lake na maono ya uongo, na watu wanaolifuata Neno lake na wanaofuata manabii wa uongo.

Yeremia 23:25 “Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto.

26 Je! Mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe?

27 Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu jirani yake, kama vile baba zao walivyolisahau jina langu, kwa ajili ya Baali.

28 Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye ALIYE NA NENO LANGU, na aseme neno langu kwa uaminifu. MAKAPI NI KITU GANI KULIKO NGANO? Asema Bwana”.

Mstari wa mwisho hapo anasema, “Makapi ni kitu gani kuliko Ngano” ikimaanisha kuwa makapi ni unabii/ndoto za uongo zinazotolewa na manabii wa uongo si kitu mbele ya Neno la MUNGU linalofananishwa na Ngano.

Kwahiyo katika siku za mwisho, YESU KRISTO ambaye ndiye pepeto lenyewe, atatenga makapi na ngano, na wanaotumainia makapi na wale wanalotumainia Neno lake.

Hizi si siku za kupelekwa huku na kule na manabii wa uongo, wanaoshinda kutwa kuchwa kutabiri maono ya uongo, wakiwaaminisha na kuwatumainisha watu katika vitu vya ulimwengu huu, kwamba kuwa na hivyo ndio kielelezo cha kwanza cha kukubaliwa na MUNGU.

Bwana YESU alisema, itamfaidia nini mtu apate ulimwengu mzima na kisha apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:36)?..maana yake utabiriwe na nabii au mchungaji au mtume kwamba utapata hiki na kile cha ulimwengu huu, na wakati huo huo haioni dhambi maishani mwako, je hayo aliyokutabiria yatakufaidia nini ikiwa utapoteza uzima wa milele?

Hizi ni siku za mwisho na pepeto hili limeshaanza kupita, na Roho Mtakatifu anawatenga walio wa kwake, hatua hizo zikimalizika kinachofuata ni unyakuo wa kanisa, ambapo walioishi na kulifuata Neno la MUNGU watakusanywa ghalani (mbinguni).. lakini waliofuata makapi watatupwa katika lile ziwa la moto, ndivyo maandiko yanavyosema..

Mathayo 13:29 “Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu…

40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.

41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)

Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?

“Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

Print this post