Usiyarudie mambo ya kale uliyoyaacha, usiyatamani mambo ya kale uliyoyakimbia, usiirudie njia ya kale uliyoikataa…
Ulikuwa upo mbali na anasa mwaka jana, basi huu si mwaka wa kuzirudia tena, usirudie ulevi uliouacha miaka ya nyuma, usirudie uzinzi ulioushinda miaka ya nyuma, usirudie kujichua ulikokuacha miaka ya nyuma,
Usirudie mavazi yasiyo na staha uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie wala kuitamani mitindo ya kidunia uliyoiacha mwaka jana.
Usirudie starehe za kidunia, mwanzo huu wa mwaka ni wakati ambao shetani anafanya kazi kubwa sana kuwarudisha watu nyuma kiroho, na atashambulia mambo yafuatayo ili kuhakikisha mwamini anarudi nyuma kiroho.
1. Afya.
Atajaribu kukuletea mashambulizi katika eneo la afya, kwa kuitikisa afya yako au ya watu wako wa karibu, ikiwemo pia afya ya uzazi.. Simama endelea mbele usirudi nyuma!.
2. Uchumi.
Atajaribu kutikisa uchumi wako lakini, hawezi kuondoa baraka zako za mwaka, hivyo usitishwe na vimitikisiko vya uchumi vya ibilisi vya hapa na pale, ni vya muda tu wewe endelea mbele usirudie biashara haramu wala tamaa za mali ulizoziacha huko nyuma endelea mbele kwani Bwana anakujua.
3. Ndoa.
Atakuletea vimitikisiko vya kifamilia vya hapa na pale, pia visikutishe kwani ni kawaida yake kutishia, lakini wewe endelea mbele na imani usirudie magomvi uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie anasa za kupunguza mawazo ulizoziacha huko nyuma…yapo mambo mazuri mbele yako kwaajili ya huu mwaka.
Pia ondoa hofu ya kesho…kwamba itakuwaje kesho, itakuwaje disemba…ndio usijizuie kutafakari yajayo, lakini usiufanye moyo wako kuwa mzito kwaajili ya hayo, kwani huo pia ni mlango mwingine wa ibilisi kumrudisha mtu nyuma.
Ukiwa ndani ya Kristo fahamu kuwa mambo yote yatakuwa sawa, haijalishi itachukua muda gani au mambo yanaanzaje…kushinda ni lazima! na ni AMRI.
Usirudi nyuma Baba, usirudi nyuma Mama, usirudi nyuma kaka, usirudi nyuma dada, usirudi nyuma mtoto…kwani matokeo ya kurudi nyuma ni kumfadhaisha Bwana.
1 Samweli 15:11”Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha”.
Utakapofika mwisho wa mwaka tena uwe na sababu ya kumshukuru Bwana kama amekulinda hujarudi nyuma.
Ayubu 23:12 “Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”.
Lakini kama ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, bado hujachelewa hebu kataa hiyo njia na leo mwombe Bwana rehema na kuziacha hizo njia utaona maajabu ya Bwana, kwani atakutia nguvu na utaendelea mbele kwa mbio kubwa, Bwana atakurehemu na utamfurahia.
Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.
Isaya 50:5 “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma
Lakini usipojali na kuendelea katika njia hiyo ya kurudi nyuma, ipo hatari mbele yako..
Mithali 1:32 “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,
Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”
USIRUDI NYUMA! USIRUDI NYUMA!…USIRUDI NYUMA!.
Ukiwa utahitaji msaada wa maombezi ili uzidi kusimama, basi piga namba hizi 0789001312.
Bwana anakupenda, na Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.
SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.
USIIGE TABIA YA NAAMANI
Rudi Nyumbani
Print this post
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza
Kitabu hichi ni moja ya nyaraka zilizondikwa na mtume Paulo katika agano jipya,
Waraka huu amegusia mambo mengi, hasahasa katika eneo la marekebisho na maonyo. Unagusia nidhani na taratibu za kikristo zinazopaswa zifuatwe ndani ya kanisa, unazungumzia pia eneo la uhalisia wa ufufuo wa wafu katika siku ya mwisho pamoja eneo la upendo.
Na huu ndio uchambuzi wake katika maeneo mama;
Paulo anatoa onyo juu ya migawanyo ambayo ilianza kutokea ndani ya kanisa iliyozaa wivu na fitina, ambayo ilisababishwa kwa baadhi ya watu kujiwekea matabaka kwa kujivunia viongozi kwa kusema mimi ni wa Paulo, mimi ni wa Apolo, mimi ni wa Kefa. Akiwatahadharisha na kuwasihi kwa kuwaeleza kwamba wao ni wahudumu tu katika nafasi mbalimbali, bali mkuzaji ni Kristo. Na hivyo hawapaswi kujivunia wao, bali Kristo
Kristo ni hekima ya Mungu na nguvu ya Mungu.(1:18- 2:16)
Eneo la pili Paulo anatoa ufahamu hasaa juu ya hekima anayoitambua Mungu, akionyesha kuwa hekima ya ulimwengu huu, kwa Mungu ni upuzi, bali hekima ya Mungu ameificha ndani ya Kristo Yesu, na hivyo amewachagua watu wadhaifu na wanyonge kuwadhihirishia hiyo. Akionyesha kuwa mtu asitegemee sana kumwona Mungu katika mambo yanayodhaniwa kuwa ni makuu, bali katika Kristo Yesu.
1 Wakorintho 1:24
[24]bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
Katika eneo hili Paulo anastaajabishwa kwa kuzuka kwa zinaa mbaya ambayo haionekani hata kwa mataifa yaani mtu na mzazi wake kuzini,. Akiwaagiza kutoa hukumu juu ya watu kama hao, hata kwa kuwakabidhi shetani (lengo ni waponyeke)
Kwasababu wakiachwa mwisho wao huwa ni kulichafua kanisa, (kulitia unajisi),
Vilevile tunaona Paulo akitoa agizo kuwa kanisa halipaswi kuchangamana na wazinzi.
Akisisitiza kuwa mtakatifu sio tu awe amehesabiwa haki bali pia awe ameoshwa na kutakaswa na udhalimu wote.
Anawaagiza pia watakatifu hawapaswi kupeleka mashtaka yao kwa watu wa kimataifa, bali kanisa ni zaidi ya mahakama ambayo watakatifu wanapaswa watatulie migogoro yao hapo.
Paulo anaeleza kwa upana, taratibu ya kindoa, katika eneo la haki zao za ndani na kuachana, na wito wa utowashi(useja). Katika eneo la haki, anasisitiza kuwa kila mwanandoa anapaswa atambue kuwa hana haki juu ya mwili wake mwenyewe, bali mwenzake, lakini pia katika kuachana, anaeleza ikiwa mwanandoa mmoja haamini, Yule aliyeamini hapaswi kumwachwa mwenzake, ikiwa bado anataka kuendelea kuishi naye. Lakini pia anatoa pendekezo lake Mtu akitaka kumtumikia Mungu kwa wepesi zaidi bila kuvutwa na mambo ya mwilini na dhiki za kiulimwengu. Basi akikaa bila kuoa/kuolewa afanya vema zaidi.
Anaeleza jinsi gani mkristo anapaswa kukabiliana na dhamiri yake na ile ya wengine,katika maamuzi ayafanyayo kwa ujuzi wake, akigusia eneo la vyakula (hususani vile vilivyotolewa sadaka kwa sanamu), kwamba hivyo havituhudhurishi mbele za Mungu, lakini tukila pia tuangalie wengine wanaathirikaje. Tusije tukawakwaza kwa ujuzi wetu. Paulo anaeleza ili tuweze kufikia hapo yatupaswa kuyafanya yote katika upendo.
1 Wakorintho 8:11-13
[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake. [12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo. [13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.
[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.
[12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo.
[13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.
Lakini pia anaeleza haki waliyonayo mitume, kwamba wanaouwezo wa kula katika fungu la kanisa, lakini hawakutumia ujuzi wao wote, ili waweze kuifikisha injili kiwepesi kwa watu bila kuwazuilia na wengine.
Paulo anatoa utaratibu wa ki-Mungu wa namna ya kuhudumu, kufuatana na hali ya kijinsia. Kwamba kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha mwanamume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Hivyo mwanawake anapaswa wafunikwe vichwa awapo ibadani, ili kuonyesha kichwa chake(mumewe) kinamilikiwa na Kristo. Na kwamba wanawake wanapaswa watii uongozi (1Wakorintho 14:34-40)
Paulo anaeleza pia nidhani katika kushiriki meza ya Bwana, kwamba inapaswa ifanywe katika ufahamu na utaratibu sahihi wa rohoni, vinginevyo itapelekea hukumu badala ya baraka
Paulo anazungumzia kwa undani karama mbalimbali ambazo Mungu ameziweka katika kanisa na kwamba zinapaswa ziwe kwa lengo la kufaidiana na kujengana. Lakini anaeleza kipawa kilicho bora zaidi ya karama zote, nacho ni upendo, ambacho anakieleza kwa urefu katika sura inayofuata ya 13, kwamba hichi kimezidi vyote.
1 Wakorintho 13:1-8
[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. [2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. [3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. [4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; [5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; [6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; [7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. [8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
[2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
[3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
[4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
[5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
[6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
[7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
[8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Katika eneo hili Paulo anahimiza fundisho la kufufuliwa kwa wafu, akionyesha jinsi lilivyo umuhimu katika imani ya kikristo, na hiyo ni kutokana na baadhi ya watu waliozuka ndani ya kanisa kufundisha fundisho la kisadukayo kwamba hakuna ufufuo wa wafu.
Akieleza jinsi Bwana atakavyokuja kwamba siku ya kurudi kwake parapanda italia na wote kwa pamoja (tulio hai na waliokufa) tutaipokea miili mipya ya utukufu itokayo mbinguni.
Katika sehemu hii ya mwisho Paulo anawaagiza juu ya utaratibu wa changizo kwa ajili ya watakatifu, kwamba vifanyike kila siku ya kwanza ya juma wakutanikapo, anawaagiza pia wakeshe, wawe hodari, na mambo yao yote yatendeke katika upendo.
Kwa hitimisho ni kuwa waraka huu unalenga hasa marekebisho, juu ya mambo mengi yaliyokuwa yanatendeka kwasababu ya ujinga, upumbavu, na dhambi ndani ya kanisa la Kristo. Na Ukweli ni kwamba mambo kama haya haya ni rahisi kuonekana hata katika kanisa la leo. Waraka huu tuusomapo yatupasa tuutazame kwa jicho la kikakanisa je! makosa kama ya wakorintho yapo katikati yetu, kama ni ndio basi tujirekebishe haraka sana.
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
Kichwa cha waraka huu kinasema. “ Waraka wa pili wa Paulo mtume kwa Wathesalonike”
Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu, kwa kanisa hili la Thesalonike.
Lakini pamoja na hilo tunaona Waraka huu wa pili kama ulivyo ule wa kwanza anawataja pia Timotheo na silwano(Sila), kama waandishi wenza.
Aliundika akiwa Korintho, sawasawa na taarifa tunazozipata katika kitabu cha Matendo 18,.
Maudhui makuu ya waraka huu yalikuwa ni matatu(3), nayo ni;
Kwa maelezo mafupi tuyaangazie maeneo hayo matatu.
> Paulo anawatia moyo watakatifu kwa uthabiti wa imani yao ambayo imesimama sikuzote hata ilipopitia kwenye dhiki nyingi na adha.
2 Wathesalonike 1:4
[4]Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.
> Lakini pia anawaeleza hatma ya watu wanaowaletea adha, kwamba Mungu ni wa haki, na atawalipiza kisasi hao wanaowatesa. Kwa kuwaadhibu kwa maangamizi ya milele.(1:8-9)
2 Wathesalonike 1:6
[6]Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi;
> Lakini anaeleza ahadi ya raha ambayo Mungu amewawekea waamini huko mbeleni watesekao kwa ajili yake.
2 Wathesalonike 1:7
[7]na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake
Anarekebisha upotofu uliozuka juu ya siku ya Bwana,kama kweli tayari imeshakuwapo au la, hivyo katika sura hii ya pili, anawaonya kwa kuwaambia siku hiyo haiji kabla ya ule ukengeufu kwanza kuja, na yule mwana wa kuasi, mwana wa uharibifu (mpinga-kristo) kufunuliwa.
2 Wathesalonike 2:1-3
[1]Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake, [2]kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo. [3]Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
[1]Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
[2]kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
[3]Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
Akiwa na maana kuwa kabla ya Kristo kurudi mara ya pili, ukengeufu wa kiroho mkubwa sana utatokea, na yule mpiga-kristo kujidhihirisha na kujulikana kwa kazi zake.
Ambazo zitakuwa ni kama ifuatavyo;
> Kujiinua juu ya kila kitu kiitwacho Mungu, akijifanya yeye ndio kama Mungu.
2 Wathesalonike 2:4
[4]yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
> Atakuwa na utendaji kazi wa shetani ndani yake, kwa kufanya maajabu ya uongo ili kuwadanganya wote waliomkataa Mungu katika fahamu zao.(2:9-12)
> Lakini mwisho wake utakuwa ni kuangamizwa na Yesu.(2:8)
Paulo anaendelea kusema kwasasa hawezi kutenda kazi kwasababu yupo azuiaye, mpaka atakapoondolewa.
2 Wathesalonike 2:6-7
[6]Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. [7]Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
[6]Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
[7]Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
Na huyo si mwingine zaidi ya Roho Mtakatifu. Lakini kumbuka Sio kwamba ataondolewa lakini mifumo yake inayozuia utendaji kazi wa mpinga-Kristo itafikia mwisho..Kwamfano kanisa kunyakuliwa, na mifumo ya kiutawala iliyoruhusiwa na Mungu maalumu kudhibiti kazi zake, kuachwa kutumiwa na Mungu, na malaika wanaohuduma duniani kwa ajili ya usalama wa watakatifu, kuondolewa..
Vitu kama hivi vitakapoondolewa basi mpinga-Kristo atapata uhuru wote kutendakazi kwa jinsi apendavyo.
Paulo anawasisitiza watakatifu juu ya kuiombea huduma, ili injili ya Kristo itukuzwe, lakini pia aweze kuepushwa na watu wabaya.
Pamoja na hilo anatoa tahadhari kuhusu uvivu, akiwasisitiza wafanye kazi kwa mikono yao, pengine kwasababu ya ufahamu usio sahihi waliokuwa nao hapo mwanzo, kwamba mwisho tayari umekwisha fika.
Pia anawatia moyo watakatifu wasikate tamaa katika kutenda mema. Huku akiwahiza wadumu katika mapokeo yao tu waliyowaachia, na si mengineyo.
mwisho anamaliza na salamu pamoja na baraka kwa kanisa.
Kwa ufupi tuusomapo waraka huu Bwana anataka tuendelee kuthibiti katika imani,.haijalishi ni dhiki za namna gani tutazipitia.
Lakini pia tuwe na ufahamu sahihi juu ya siku za mwisho. Kwasababu tatizo hili lipo hata sasa, baadhi ya watu wakiamini kuwa siku ya Bwana imeshakuja. Lakini kama tulivyojuzwa hapo, haiwezi fika kabla, mpinga-Kristo kudhihirishwa na hilo litakuwa wazi kabisa duniani kote.
Na mwisho ni wajibu wetu kuombea huduma, na wanaojitaabisha kuhubiri injili ili walindwe na watu wabaya. Je unamwombea mchungaji wako?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Maandiko yanasema Makwazo hayana budi kuja (Luka 17:1)
Unapofanyiwa jambo baya na Mtu wako wa karibu au wa Mbali, huwa ni ngumu kusahau…
Kama umeshaokoka na ni mtu uliye mwepesi kusamehe na kusahau, basi Bwana amekutengeneza kwelikweli na umetengenezekeka, Lakini kama ndani yako kuna UGUMU wa kusamehe, fahamu kuwa hilo ni tatizo ambalo unapaswa ulitafutie ufumbuzi haraka sana, mwanzoni mwa mwaka.
Umeumizwa na Ndugu, umeumizwa na Mpendwa mwenzako, umeumizwa na Rafiki, umeumizwa na Mke, Umeumizwa na Mume, umeumizwa na watoto, mchungaji, mshirika wako, mkufunzuki wako au mtu mwingine yeyote, leo itoe hiyo sumu..
Fanya jambo hili moja ili ushinde hali hiyo ya kutokusamehe na hatimaye uachilie msamaha.
UTAFAKARI MSAMAHA WA YESU.
Tafakari ni mambo mangapi mabaya uliyoyafanya au unayoyafanya kwa MUNGU, unaweza ukawa hujawahi kumfanyia mtu ubaya, lakini vipi MUNGU?.. Je hujawahi kumfanyia ubaya kabisa?..huna dhambi kabisa??, huna kasoro kabisa??.. Hilo ni jambo lisilowezekana. (2Nyakati 6:36)
Tafakari tu mawazo yako kwa siku yanavyo vuka na kuwa machafu, na MUNGU anakutazama tu!, tafakari ni vipindi vingapi umewaka hasira moyoni na Mungu anakutazama tu, tafakari ni mangapi amekusamehe, na ni mangapi unayohitaji ukusamehe.
Hayo yote uliyoyafanya na unayoyafanya Mungu anayatazama tu, na yupo tayari kukusamehe, au huenda ameshakusamehe, sasa kama wewe umesamehewa mengi hivyo bure kabisa, vipi na wewe kwanini usimsamehe yule aliyekokosea mwaka jana, au mwezi jana, au siku ya jana??.
Wakati mwingine si lazima yeye akuombe msamaha, Wewe samehe tu hata kama hajaja kukuomba msamaha, maana hata BWANA aliwasamehe wale wasiomwomba msamaha..
Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura. 35 Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.”
Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
35 Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.”
Wengine watakukosea na daima wataendelea kujiona wapo sawa, na wengine wataendelea kukukosea tu!.. Lakini kanuni ni ile ile KUSAMEHE..
Hivyo kwa kuutafakari mambo ya maisha yako, na kasoro zako mbele za MUNGU, Huwezi kukosa sababu za wewe kutosamehe.
Kwa kumalizia hebu tafakari kwa undani maandiko yafuatayo…
Mathayo 18:21 “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? 22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini. 23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. 24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi. 25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni. 26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. 27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. 28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho. 29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. 30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni. 31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka”.
Mathayo 18:21 “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?
22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.
24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.
25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.
26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.
28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.
29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.
30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.
31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka”.
Kumbe tusipokuwa na TAFAKARI ya kutosha kwa msamaha BWANA aliotupa, yaweza kuwa sababu ya sisi pia kutosamehewa!. Lakini kama tukifakari kwamba na sisi tumeshafanya mengi mabaya, ambayo hayakustahili msamaha basi na sisi pia tutasamehe.
Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi. 21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana. 22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.
Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.
21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.
22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.
Mwombe Bwana katika mwanzo wa mwaka huu akuumbie “Moyo wa kusamehe”.. Ni yeye ndiye anayetoa huo moyo, ikiwa tutamwomba, kwa kumaanisha kabisa, Hivyo jifungie chumbani kwako, au tafuta sehemu yoyote yenye utulivu na mwambie Bwana.
TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.
NI KWASABABU YA YESU KRISTO.
Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.
Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?
BWANA ANASAMEHE.
Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha katika mwanzo wake ‘Waraka wa kwanza wa Paulo mtume kwa Wathesalonike’.
Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu. Aliuandika akiwa Korintho. Tumelijua hilo kufuatana na ujio wa Timotheo kutoka Makedonia na kumpa ripoti nzuri ya maendeleo yao ya kiroho, kuanzia eneo la imani, upendo na tumaini, ambazo tunazisoma katika kitabu cha Matendo ya mitume sura ya 18.
Kwasababu ya ugumu wa kuwafikia uliochangiwa na shetani, Akasukumwa kuandika nyaraka hizi mbili kwa watakatifu hawa, kuwajenga katika maeneo kadha wa kadha, ambazo zilipishana kwa miezi kadhaa tu.
Kitabu hichi kina sura tano (5)
Maudhui kuu ya waraka huu ni matatu(3)
Tuyaangalie hayo maeneo matatu kwa ufupisho;
Paulo anaanza kwa kuwashuhudia kwa maneno mengi dhiki alizozipata katika kuieneza injili kwao, na jinsi alivyoweza kustahimili, Na kwamba wao pia wanapopitia dhiki za namna mbalimbali kutoka kwa watu wa taifa lao, wasivunjike moyo na kuiacha imani. Wajue kuwa dhiki pia wamewekewa watakatifu.
1 Wathesalonike 2:14
[14]Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu; kwa kuwa mlipata mateso yale yale kwa watu wa taifa lenu wenyewe, waliyoyapata na hao kwa Wayahudi; [15]ambao walimwua Bwana Yesu, na hao manabii, na kutuudhi sisi; wala hawampendezi Mungu, wala hawapatani na watu wo wote;
[14]Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu; kwa kuwa mlipata mateso yale yale kwa watu wa taifa lenu wenyewe, waliyoyapata na hao kwa Wayahudi;
[15]ambao walimwua Bwana Yesu, na hao manabii, na kutuudhi sisi; wala hawampendezi Mungu, wala hawapatani na watu wo wote;
1 Wathesalonike 3:3
[3]mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
Paulo anagusia maeneo mengi kuanzia upendo hadi utakatifu kwamba wana wajibu wa kuongezeka katika hivyo ili wasionekane katika lawama katika siku ile ya kuja Bwana wetu Yesu Kristo kutoka mbinguni.
1 Wathesalonike 3:12-13
[12]Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu; [13]apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.
[12]Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
[13]apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.
> Anagusia pia katika eneo la kudhibiti miili yetu katika utakatifu na heshima na sio katika tamaa mbaya(4:1-5),
> Halikadhalika wakristo kuonyesha mwenendo wa adabu kwa walio nje, kwa kutenda shughuli zetu wenyewe ili tusiwe na uhitaji wa vitu vyao (4:11-12)
> Pia kama watakatifu ni mwiko kulipana baya kwa baya (5:15),
> Tunapaswa sikuzote tudumu katika kuomba, kufurahi, kushukuru kwa kila jambo, tusimzimishe Roho, tusipuuzie unabii, tujitenge na ubaya wa kila namna.(5:16-23)
> Lakini Paulo anahimiza mwenendo wetu unapaswa uende mpaka kwa wale wanaotusimamia na kutuchunga kwamba tuwastahi.
1 Wathesalonike 5:12-13
[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; [13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;
[13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.
> Na katika yote ni wajibu wetu sote kufarijiana na kuonyana na kuvumiliana na kutiana nguvu(5:14-15)
Paulo anawafiriji kwa kuwaambia wafu waliolala katika Kristo, siku ya mwisho wataamshwa wote..wasidhani kuwa hawatawaona wapendwa wao waliotangulia.
1 Wathesalonike 4:13-16
[13]Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. [14]Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. [15]Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. [16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
[13]Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
[14]Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
[15]Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
Sambamba na hilo, anawafumbua macho juu ya nyakati na majira ya kurudi kwa Yesu kwamba hakutakuwa na taarifa zozote au viashiria vyovyote kwa watu wa dunia. Bali itawajilia kwa ghafla tena katika nyakati ambazo wanasema kuna amani na shwari.
Hivyo anawatahadharisha watakatifu nao kuwa macho wakati wote.
1 Wathesalonike 5:1-11
[1]Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. [2]Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. [3]Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. [4]Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. [5]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza. [6]Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. [7]Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. [8]Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. [9]Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; [10]ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala. [11]Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.
[1]Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
[2]Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
[3]Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.
[4]Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.
[5]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.
[6]Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.
[7]Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
[8]Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.
[9]Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
[10]ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.
[11]Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.
Hivyo kwa ufupi ni kuwa waraka huu. Unawataka wakristo kuthibitika katika imani, haijalishi ni changamoto gani za kimaisha au ugumu gani watakutana nao kwa wapinga-kristo, Wanapaswa waendelee kusimama hivyo hivyo mpaka mwisho katika Kristo Yesu.
Lakini pia wajue Bwana anarudi, na atakuja ghafla, Hivyo yawapasa wawe watu wa mchana sikuzote wasilale usingizi kwa kuhakikisha wanaishi maisha ya utakatifu, na adabu, ili atakaporudi Bwana wasiwe na lawama yoyote.
Je! Umeokoka? Kama ni la, fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya wokovu. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.
VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Yakobo.
Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.
Ni kitu gani umekichagua kwenye nyumba ya MUNGU katika mwaka huu?..Je nafasi fulani, au cheo, au umaarufu, au nini?.
Kumbuka Nyumba ya MUNGU ni zaidi ya jengo la Ibada, bali pia Miili yetu ni nyumba ya MUNGU.
Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu? 21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.
Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?
21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.
1 Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?”
Soma pia 1Wakorintho 6:19, utazidi kuelewa vyema.
Sasa kama Miili yetu ni HEKALU LA MUNGU, yaani NYUMBA YA MUNGU ni kipi umekiamua juu ya Mwili wako katika mwaka huu mpya?, kwamaana Neno linasema Utakatifu ndio ufaao nyumba ya MUNGU, na tena haufai siku moja tu, bali milele…..
Chagua utakatifu wa mwilini na rohoni huu Mwaka, usiishi tena kwa kuuchafua mwili wako kama ilivyouchafua mwaka jana, au miaka iliyopita, anza mwaka na mambo mapya.
Anza kujenga ushuhuda mpya, badilika kimwonekano, watu watakapokutazama waone waseme hakika yule ni mkristo, na watakapokuuliza usema “UMECHAGUA UTAKATIFU KWA MAANA NDIO UFAAO NYUMBA YA MUNGU”.
Sema mwaka huu sio mwaka wa Kushindana na mtu kimavazi ndani ya nyumba ya MUNGU, sema mwaka huu ni wakati wa kuipamba nyumba ya MUNGU kwa utakatifu.
Sema mwaka huu ni mwaka wa kuhubiri UTAKATIFU kila mahali, kwamaana pasipo huo hakuna mtu atakayemwona Mungu (Waebrania 12:14).
2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.
Hili ni neno fupi la mwaka kwako.
Bwana atusaidie sana..
Shalom.
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi
Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.
Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.
Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.
Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:
Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).
Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.
Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.
> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)
> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..
Wafilipi 2:17-18
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote. [18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.
Wafilipi 1:29
[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,
Wafilipi 3:1
[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.
Wafilipi 4:4
[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Sehemu ya Pili:
Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.
Wafilipi 1:27
[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;
Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..
Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)
Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)
Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)
Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)
Wafilipi 4:8
[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)
Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).
Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.
Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.
Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Watu wa nyumbani mwa Kaisari ni watu gani? (Wafilipi 4:22).
Epafrodito ni nani kwenye biblia?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai
Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.
Kama kitabu kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo Mtume kwa Waefeso”. Paulo ndiye aliyeuandika waraka huu.
Aliuandika akiwa kama mfungwa kule Rumi.
Waraka huu una sura sita(6), ambazo tunaweza kuzigawanya katika makundi mama mawili.
1) kundi la kwanza ni Sura ya 1-3,
Sura hizi zinaeleza asili ya Imani yetu iliyo katika Kristo Yesu jinsi ilivyo ya kipekee kwa nguvu na mamlaka, na ubora, na uweza na ukuu, na utajiri, na utukufu usiopimika, kwa akili za kibinadamu.(1:20-23).
2) Lakini kundi la pili ni Sura 4-6
Inaeleza juu ya mwenendo wetu, jinsi unavyopaswa uwe katika imani tuliyoipokea. Kwasababu ni vitu vinavyokwenda sambamba, haviwezi kutenganishwa, katika fundisho la ukristo.
Kwa ufupi; Katika Kundi la kwanza Yafuatayo ni mambo mama ambayo mwandishi ameyazungumzia juu ya mambo tunayoyapata ndani ya mwokozi wetu Yesu Kristo.
Haya ni mambo ya muhimu sana, ambayo tunapaswa tuyafahamu juu ya Kristo tuliyempokea ndani yetu. Kulingana na mwandishi tukiyajua hayo itatufanya tusiwe watoto wachanga, wa kuchukuliwa na kila upepo wa elimu ya uongo, kwa hila za watu, na ujanja, na njia za udanganyifu (4:14).
Lakini katika kundi la pili ambalo ni sura ya 4-6;
Tunaelezwa wajibu wetu kimwenendo, baada ya kumwamini Kristo, jinsi unavyopaswa uwe, kwamba hatupaswi kuenenda kama mataifa waenendavyo, bali kinyume chake tukue mpaka kuufikia utimilifu wake.
Ambayo hiyo huja Kwa njia ya kuhudumiana kwa karama mbalimbali sisi kwa sisi katika kifungo cha umoja, kama kanisa la Kristo. (4:16)
Anaeleza pia yampasa kila mmoja binafsi auvue ule utu wa kale wa dhambi, na kuuvaa mpya mpya wa utakatifu na haki (4:20-24),
kwa kuuvua uongo, pia tusiruhusu hasira zitutawale, tusiwe wezi, vinywa vyetu visitoe maneno mabaya na matusi, tuwe wafadhili sisi kwa sisi, tusimzimishe Roho, upendo wetu udumu, uasherati usitajwe, wala aibu, wala ubishi.
Kwasababu watendao kama haya kulingana na Mungu hawana urithi katika ufalme wa Mungu.
Waefeso 5:5
[5]Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.
Halikadhalika Mwandishi anatoa pia agizo juu ya matendo ya giza kwamba tuyaonapo tuyakemee, vilevile tujiepushe walevi, bali tujazwe Roho wakati wote, kwa kumfanyia Mungu ibada.
Waefeso 5:18-20
[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; [19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; [20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
[19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
[20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Mwandishi anazidi kugusia mienendo yetu mpaka katika ngazi za kifamilia na kikazi.
kwamba wake wanapaswa wawatii waume zao, vilevile waume wawapende wake zao. Watoto wawaheshimu wazazi wao, na wazazi wasiwachokoze watoto wao, Watumwa wawatii bwana zao, na mabwana wasiwatishe watumwa wao.(5:22-6:9)
Anagusia pia eneo la vita vyetu. Kwamba rohoni tupo vitani dhidi ya adui yetu shetani na mapepo yake, yenye kazi ya kuwapofusha watu macho, lakini pia kurusha mishale ya moto kutuangamiza. Hivyo tunapashwa tuvae silaha zote za Mungu, ili tuweze kusimama. (6:10-20). Anaorodhesha silaha hizo. ambazo zinakamilishwa kwa sala na maombi ya daima.
Na mwisho anatoa salamu zake kwa watakatifu, akiwaambia pia habari zake nyingine watakazisikia kwa Tikiko, aliyempeleka kwao.
Kwa ufupisho.
Kitabu hichi kinatupa ufahamu kuhusu ubora wa imani tuliyoipokea lakini pia wajibu wetu baada ya hapo, kwasababu tusipothamini na kulegea adui yetu shetani na majeshi yake yatashambulia imani yetu na hatimaye, tukayakosa tuliyohakikishiwa.
Ukishaamini tembea katika utakatifu. Ukiwa unapiga hatua kila siku kwenda mbali na dhambi, basi fahamu kuwa ukombozi wako ni hakika. Kwasababu msalaba una nguvu ya kukusaidia madhaifu yako.
Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)
Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?
Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.
Jina la Mwokozi Mkuu, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Kosa moja maarufu Mfalme Daudi alilolifanya katika maisha yake, (ingawa baadaye alikuja kusamehewa na Bwana), lilikuwa ni kumuua Uria na kumchukua Mke wake aliyeitwa Bathsheba.
Lakini tukifuatilia chanzo cha kosa, tunaona lilianzia katika MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati ambao Wafalme wanatoka kwenda vitani, ila yeye Daudi hakutoka kwenda vitani pamoja na wenzake badala yake akakaa nyumbani, na matokeo yake ni shetani kupata nafasi ya kumjaribu.
2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU. 2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. 3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti? 4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake. 5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.
2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU.
2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.
3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?
4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.
Laiti Mfalme Daudi angalisimama na kwenda vitani pamoja na wenzake, asingeingia kwenye jaribu kubwa kama lile, ambalo liliuharibu mwaka wake wote na kumchafulia heshima yake kwa vizazi vyote.
Yote hayo ni makosa aliyoyafanya MWANZO WA MWAKA, kumbe kuna kitu katika Mwanzo wa Mwaka, vile vile na katika Mwisho wa Mwaka,..Mwanzo wa Mwaka ni wakati wa kuanza mapambano, si wakati wakulala tena, ni wakati wa kukusanya nguvu ya pamoja na kuingia katika mapambano, ni wakati wa kukusanyika katika nyumba ya MUNGU kupambana kiroho na kuangusha ngome, ni wakati wa kuomba sana.
Bwana atusaidie tuwe na mipango mema katika mwanzo wa Mwaka.
MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)
Kama kinavyoanza kwa utambulisho wake, ‘Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai’.
Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu.
Madhumuni makuu ya waraka huu ulikuwa ni kuwasisitiza Wakolosai jinsi Yesu alivyo UTOSHELEVU WOTE, ambaye kwa kupitia yeye Uumbaji wote umekamilishwa ndani yake, lakini si hilo tu bali na utimilifu wote wa ki-Mungu unapatikana ndani yake, pamoja na hazina zote za hekima na maarifa.
Akiwa na maana kuwa mtu akimpata Kristo, hahitaji kitu kingine cha pembeni kumkamilisha yeye, Utoshelevu wote upo kwake.
Hivi ni vifungu mama,
1:15-17
“15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.
2:3
ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
2:9
“Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.
Anaeleza kwa undani katika sura ile ya pili, kwamba ni kutokana na uwepo wa watu waliolivamia kanisa na kuwadanganya kwa maneno ya ushawishi, nia zao ni kuwafanya mateka kwa elimu isiyo na matunda, ya mapokeo ya kibinadamu, yasiyo ya Kristo (2:8). Kwamba mtu akishika hayo, ndio utimilifu wote unapatikana.
Vilevile kuonekana kwa baadhi ya desturi za kiyahudi ndani ya kanisa, kama vile kushika sikukuu, tohara, sabato, na mwandamo wa mwezi. Vikidhaniwa kuwa vitu hivyo vinaweza kuleta ukamilifu wote pamoja na Kristo (2:11-23)
Na pia kuzuka kwa ibada bandia za kuabudu viumbe vya rohoni (malaika), kwa mawazo kuwa mtu ataupokea ukamilifu.(2:18)
Paulo anaeleza yote hayo hayana wokovu, isipokuwa kwa njia ya haki tuliyoipokea kwa msalaba wake uliofuta hati ya mashtaka yetu, kwa mateso yake pale msalabani ambayo kwa kupitia njia hiyo tumepokea msamaha wa dhambi, pale tu tunapoamini na kubatizwa (2:12-17)
Sehemu ya tatu Paulo anaeleza kwamba kuamini ni pamoja na kuuvaa utu upya wa Kristo. Hivyo huyu mtu hatarajiwi kuendelea kuishi hivi hivi tu, kisa Kristo amemkamilisha kwa kila kitu, bali anapaswa aenende kwa Kristo mwenyewe, ayafikiri yaliyo juu, (3:1-17),
Kwa namna gani?
Kwa kuzifisha tabia za mwilini, kama uasherati, uchafu, kutamani, mawazo mabaya, ghadhabu, matusi. Lakini pia kujivika utu wema, moyo wa rehema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, kusameheana, upendo, ibada. Vilevile si tu katika mambo ya rohoni , bali mpaka kwenye ngazi za kifamilia, kwamba wake kuwatii waume zao, na waume kuwapenda wake zao, na watoto kuwatii wazazi. Hizo ndio tabia za utu mpya.
Katika sura ya 4.
Bado Paulo aendelea kueleza huo mwenendo ndani ya Kristo, unapaswa uonekane mpaka kwa mabwana, kwa watumwa wao. Kwamba mabwana wawape watumwa haki zao, Lakini pia watakatifu wote, wanapaswa kudumu katika maombi, na kuenenda kwa hekima kwa watu wasioamini, katika usemi bora, na kujifunza kuukomboa wakati.
Na mwisho.
Paulo anawasilisha salamu za washirika wenzake wa injili, kwa Wakolosai ikiwemo, Epafra, Luka, Dema, marko, Aristarko, Yusto.
Hitimisho.
Kwa ufupi waraka huu, hueleza kwamba utoshelevu wote upo ndani ya Kristo tu na sio zaidi ya hapo, hatuhitaji kitu kingine cha pembeni kutukamilisha sisi, Lakini ni wajibu wa huyu mkristo kutembea katika maisha mapya ndani yake. Kwasababu mambo yote mawili yanakwenda sambamba hayatengani. Kristo huokoa na kutakasa wakati huo huo. Unapookolewa, saa hiyo hiyo umevikwa utu upya. Huwezi kuendelea katika dhambi.
Ni kipi cha ziada tunachoweza kujifunza katika waraka huu?.
Maombi ya Paulo na Eprafa yasiyokoma kwa kanisa hili(1:3, 9, 4:12):
Hatuna budi kujijengea desturi ya sikuzote kuliombea kanisa la Bwana, hususani mahali tulipo, pamoja na watakatifu wengine tuwajuao. Kwasababu kusimama kwa kanisa hutegemea sana maombi yasiyokoma.
Bwana akubariki. ||kiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii. Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,
Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)
Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia