Jibu: Turejee..
Matendo 15:40 “Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana. 41 Akapita katika Shamu na Kilikia AKIYATHIBITISHA MAKANISA”.
Matendo 15:40 “Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana.
41 Akapita katika Shamu na Kilikia AKIYATHIBITISHA MAKANISA”.
Tunasoma pia akiwathibitisha Wanafunzi katika Matendo 18:23
Sasa maana ya “kuyathibitisha Makanisa na Wanafunzi” ni Ziara za kuwatembelea wanafunzi/waamini ambao tayari wameshapokea Injili, na kuwatia Nguvu katika Imani, kwa njia ya kuwafundisha na kuwakumbusha kanuni za Imani ya kikristo na kudumu katika misingi huo.
Vile vile katika kutatua changamoto zilizokuwa ngumu kutatulika na pia na kuwateua Maaskofu na Mashemasi katikati ya waamini hao, watakaowachunga na kuliangalia kundi..
Kwa mfano tunasoma katika Matendo 14:21-22, Mtume Paulo na wenzake wakirejea Listra, Ikonio na Antiokia kufanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani..
Matendo 14:21 “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, 22 wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi. 23 Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini”
Matendo 14:21 “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia,
22 wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.
23 Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini”
Utasoma pia katika Matendo Tito 1:5, akiagiza uteuzi wa viongozi watakaoliangalia kundi.
Tito 1:5 “Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru”
Mambo kama hayo pia tunapaswa kuyafanya sasahivi, Katika siku hizi za mwisho ambapo shetani anafanya kazi kwa nguvu kuyaharibu makanisa, hatuna budi kusimama kwa nguvu na kuyathibitisha makanisa yetu kwa msaada wa MUNGU.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Roho Mtakatifu amzuie Paulo kuipeleka injili Asia? (Matendo 16:6-7).
Je Paulo, alihimiza kusikiliza nyimbo za kidunia kulingana na Matendo 17:28
Paulo aliwapaje watu karama ya rohoni?
Uchambuzi wa kitabu cha pili cha Paulo kwa Timotheo (2Timotheo).
Print this post
Isaya 1:8 “Na binti Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama KIPENU katika shamba la matango, kama mji uliohusuriwa”.
“Kipenu” ni kijumba kidogo kinachojengwa katikati ya Shamba, kinachomsitiri mlinzi wakati wa kulinda mazao shambani..
Ili kuzuia wezi wa mazao, na wanyama kama nyani, ngedere na wengineo pamoja na ndege inawalazimu wakulima kuweka walinzi mashambani, ili kuyaangalia mazao hayo, sasa kile kijumba cha walinzi, ambacho kinajengwa kwa ubora wa chini kwa kusudi hilo, ndicho kinachoitwa “Kipenu”.
Mara nyingi kijumba hiki, pale ambapo uvunaji umemalizika, huwa kinabaki chenyewe shambani wala hakuna mtu anakithamini tena, wanyama wanaweza kufanya makao huko na hakina thamani tena…… hali hii ya kipenu kusalia chenyewe shambani, na kupoteza uthamani wake ndio Bwana MUNGU anafananisha na jinsi Mji wa Yerusalemu (yaani binti Sayuni) ulivyoachwa..
Kutokana na maovu kuwa mengi Yerusalemu, na Bwana aliwaacha, na mji wao kubaki mpweke kama kipenu, na hivyo hatari yoyote inaweza kuukabili, na ndicho kilichotekea wakati ulipofika Yerusalemu uliachwa kama Kipenu na Nebukadreza, mfalme wa Babeli aliuhusuru na kuuharibu na kuwachukua wenyeji mateka.
Hata sasa tunapomwacha MUNGU, tunakuwa kama Kipenu katikati ya shamba lililokwisha kuvunwa. Nyumba zetu zitakuwa kipenu, roho zetu zitakuwa kama kipenu, biashara zetu zitakuwa kama kipenu na mambo yetu mengine yote yatafananishwa na vipenu.
Hautaweza kuilinda roho yako, wala nyumba yako kama utakuwa nje ya Kristo, ni lazima tu uharibifu wako utafika ghafla siku moja, Mwanadamu ameumbwa kumtegemea MUNGU siku zote, kamwe hawezi kuishi kwa kujitegemea mwenyewe, ni jambo ambalo haliwezekani na gumu sana. Bwana tu ndiye tegemeo letu na ngao yetu.
Zaburi 144:2“Mhisani wangu na boma langu, Ngome yangu na mwokozi wangu, Ngao yangu niliyemkimbilia, Huwatiisha watu wangu chini yangu”.
Bwana atubariki.
AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE
MAVUNO YAMESHAKWISHA SHAMBANI.
USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
Karama kibiblia humaanisha uwezo utokao kwa Mungu wa kufanya/ kutenda mambo yaliyo juu ya uwezo wa kibinadamu katika kutimiza kusudi la ki-Mungu. Karama kwa jina lingine huitwa neema za Mungu.
Kwamfano mmoja huwepa uwezo wa kuponya magonjwa, mwingine unabii, mwingine lugha, mwingine kufundisha, mwingine kukirimu, mwingine uinjilisti N.k.
Sasa neema/karama hizi, zipo za aina kuu tatu.
1) Karama zitokazo moja kwa moja kwa Mungu mwenyewe.
Hii ni aina ya karama(neema) ambayo mtu hupewa sio kwa kuomba, au kupanga au kuchagua…hapana bali Mungu humwita mtu mwenyewe na kuweka wito ndani yake, kwamfano kwenye biblia watu kama Yeremia, Isaya, Mitume na Paulo, walichaguliwa na kupewa neema hizi kwa kusudi maalumu na uwezo maalimu ndani yako, wa kufanya kazi.
2) Karama tuzipatazo ndani ya Kristo.
Hizi hupewa kila mwamini, pindi tu anapoamini na kupokea Roho Mtakatifu. Neema hizi, Roho Mtakatifu Humgawia kila mtu kwa jinsi apendavyo yeye. Ndio hizo tuzisomazo katika (1Kor 12:8-10).
3) Karama tuzipatazo kwa msaada wa watu wengi.
Hii ni aina nyingine ya neema ambayo mtu haipokei kwa jinsi ya kivyake, bali huipokea kwa jinsi anavyohudumiwa na watu wengi ndani ya kanisa la Kristo.
Ndio hii tunaisoma katika;
2 Wakorintho 1:11
[11]ninyi nanyi mkisaidiana nasi kwa ajili yetu katika kuomba, ili, kwa sababu ya ile karama tupewayo sisi kwa msaada wa watu wengi, watu wengi watoe shukrani kwa ajili yetu.
Karama hii huja kwa maombi ya watu wengi.
Na hapa ndipo wengi hupapuuzia kwa viongozi wao. Kwasababu maendeleo ya kanisa, huduma, au madhabahu hutegemea sana uimara wa wale wabeba maono/viongozi…ikiwa wabeba maono hawaombewi kuna viwango hawatavuka hata kama watakuwa na juhudi kiasi gani, watakuwa waombaji kiasi gani, watakuwa waaminifu kiasi gani..kama hawataombewa, watabakia kwenye ngazi fulani sikuzote, lakini viwango vya juu hawatafika.
Kufanikiwa kwa Paulo, hakukutegemea tu wito wake, au utendaji kazi wa Roho Mtakatifu Peke yake, bali pamoja na watu wengi waliokuwa wanamwombea.
Kwamfano huduma hii (nuru ya upendo), inategemea maombi mengi ili iinuke. Ikiwa utaguswa kuchukua muda wako kuiombea maana yake ni kuwa unaitia nguvu viongozi na hatimaye injili inahubiriwa kwa uvumilivu na ujasiri zaidi, na watu wanamwamini Mungu na kumshukuru, matokeo yake yanakuwa kupokea thawabu kwa Mungu kwa zile shukrani.
Sisi (wana nuru ya upendo), na watumishi wengine wa Mungu tunahitaji maombi yenu sana, ili tuihubiri injili kwa ujasiri, kama alivyoomba Paulo.
Waefeso 6:18-19
[18]kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote; [19]pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;
[18]kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
[19]pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;
Mungu awabariki
Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu.
PALE MAOMBI YANAPOGEUKA KUWA MAPAMBANO.
ENYI WAJINGA, ACHENI UJINGA, MKAISHI
Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu
Wimbo ulio bora 2:15
15 : Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.
Kitabu cha wimbo ulio Bora ni kitabu kinachoeleza asili ya upendo wa Kristo kwetu na jinsi tunavyopaswa kuuitikia.
Kuwa urefu wa masomo yaliyo nyuma ya kitabu hiki fungua hapa >>> NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
Lakini kwenye mstari huu, tunaona ni kama vile mtu kwa lugha ya picha anaona mbweha “ Wadogo” wamevamia shamba lake la mizabibu inayochanua na hivyo hawapuuzii kwasababu ya udogo wao, bali anatoa tamko la kukamatwa na kuondolewa…ili shamba lake linalochanua liwe salama.
Kimsingi mbweha si mnyama anayekula nyama tu, bali hula pia mizazibu, na mingine kuiharibu.
Hii ni kufunua nini katika hali zetu za rohoni..
Adui akishaona mahusiano Yetu na Kristo yanazaa matunda, huinua vitu Vidogo vidogo ili kuharibu mahusiano wakati mwingine unaweza usione kama vina madhara sana au vina nguvu sana, lakini katika eneo la kiroho kitu kidogo kina nguvu sawa na kitu kikubwa…
Hivi ndio vinavyoitwa mbweha wadogo..
Mambo Kama haya ni kama vile kuendekeza vishawishi vya dhambi kwenye maisha yako.
Kwa mfano wewe ni binti halafu kila siku unaona wanaume wanazungumza na wewe maneno ya mizaha, sasa kama usipokemea tabia hiyo, ukaona ni kawaida, tabia hizo ndogo ndogo ndizo zinazopelekea mtu baadaye kuanguka kwenye dhambi za uzinzi.
Samsoni, alipoona ushawishi wa delila unaendelea, badala aukatishe yeye akapuuzia mwisho wa siku akatekwa..
Hao ni mbweha wadogo wanaoharibu shamba lako, kila kichocheo na kishawishi kiwe kidogo kiasi gani usikipuuzie.
Wakati mwingine kuendekeza uvivu wa kiroho, yaani kupuuzia maombi, kupuuzia ibada, kidogo kidogo hupelekea kupoa kiroho, na hatimaye unajikuta kabisa umerudi duniani..mpaka unajiuliza nimefikaje hapa? Ni kwasababu uliendekeza uvivu wa kiroho..ulisema. nitaomba kesho, nikesha kesho, nitamtumikia Mungu mwezi ujao..mwishowe ukawa hivyo ulivyo leo…
Angalia ni eneo lipi la maisha yako limevamiwa na hawa mbweha wadogo, kisha chukua hatua za haraka kurekebisha.
Shalom
Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.
Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Kuba ni kitu chenye umbo la duara kinachofunika kwa juu, ni kama paa lililopinda. Lenye mwonekano unaofanana na nusu ya mpira au bakuli lililogeuzwa juu chini.
Mifano ya kuba:
unaweza kuona kwenye ujenzi wa Misikiti mingi na baadhi ya Makanisa na majengo ya kale
Tukirudi kwenye biblia Enzi za kale, ilidhaniwa kuwa dunia ina kuba kwa juu, yaani kifuniko. Ambao ndani yake jua, mwezi na nyota hutembea..
Neno hilo utalisoma katikq vifungu hivi;
Ayubu 22:14
[14]Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione;
Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu.
Amosi 9:6
[6]Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA ndilo jina lake.
Kumbuka, ujumbe unaowasilishwa hapo ni kueleza ukuu uliozidi wa Mungu, katika uumbaji wake na mamlaka yake.
Shalom.
Nini maana ya Israeli?
Binti za Yerusalemu wanaotajwa katika kitabu cha Wimbo ulio Bora 1:5 ni akina nani?
Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)
UNAJISIKIAJE, KUTEMBEA NA SANDA?
JIBU: Maana yake ni “yeye ashindanaye na Bwana”
Siku ile Yakobo alipotokwa na Mungu, kisha akashindana naye usiku kucha bila kumwacha, ndipo yule mtu akamuuliza jina lako nani, akasema Yakobo, akaambiwa hutaitwa tena hilo jina Yakobo, bali Israeli.
Mwanzo 32:28
[28]Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.
Au kwa namna nyingine tafsiri yake ni
“mtu anayeng’ang’ana na Mungu mpaka kuona matokeo”
Ndio jina ambalo kabila zake zote ziliitwa. Leo hii tunaposema taifa la Israeli, tunamaanisha taifa la washindanaji.
Lakini Israeli kwa agano jipya si hii ya mwilini tu.. bali ile ya rohoni ambayo imeundwa na Yesu Kristo mwenyewe..
Warumi 2:28-29
[28]Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili; [29]bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.
[28]Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;
[29]bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.
Maana yake ikiwa umempokea Kristo, wewe tayari ni mwisraeli/myahudi.
Na kama ni mwisraeli, jua asili ya jina lako..kuwa wewe ni mtu wa kung’ng’ana na Mungu…sio mtu mwepesi mwepesi…
Usimrajie Mungu katika vitu virahisi rahisi, huyo ndio sababu kwanini tunakuwa na mifungo na mikesha, kudumu uweponi mwa Bwana wakati mwingi, kumtafuta Bwana, sio kwamba yeye ni mgumu kupatikana hapana, bali kwa asili hataki wana walioitwa kwa jina hilo wawe walegevu,
Wengi hulalamika, mbona sioni uwepo wa Mungu, mbona sioni amani ya kutosha ndani, siono furaha ya wokovu, ukiwauliza vipi juhudi yako rohoni…mmoja atasema ratiba yangu huwa ni maombi ya dk 10 kwa siku, kusoma Neno dk 10.. Sasa mtu kama huyu hawezi kuhudumiwa vema na Mungu ikiwa ameokoka…
Ndugu jitambue wewe ni nani! Ikiwa ni mwisraeli, simama kama mtu shupavu kung’ang’ana na Mungu wako, nje ya hapo, tafuta jina lingine na mungu mwingine mwenye vigezo vyake vya kukuhudumia, lakini kama ni waisraeli wa Kristo, basi ni watu wa kuliitia jina la Bwana bila kukoma (Luka 18)
NINI MAANA YA UKOMBOZI?
Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?
Swali: Mtakatifu wa Israeli anayetajwa katika Isaya 30:9-12 ni nani hasa? Na anakomeshwaje?
Isaya 30:9 “Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana; 10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo; 11 tokeni katika njia, geukeni mtoke katika mapito; MKOMESHENI MTAKATIFU WA ISRAELI MBELE YETU”.
Isaya 30:9 “Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana;
10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;
11 tokeni katika njia, geukeni mtoke katika mapito; MKOMESHENI MTAKATIFU WA ISRAELI MBELE YETU”.
“Mtakatifu wa Israeli” anayezungumziwa katika maandiko hayo na mengine mengi, si mwingine zaidi ya MUNGU MWENYEZI, ALIYEUMBA MBINGU NA NCHI, Huyo ndiye aliye Mtakatifu ambaye alifanya Agano na Israeli, Tunalithibitisha hilo zaidi katika maandiko yafuatayo..
Sasa tukirejea hayo maandiko hapo anaposema “…MKOMESHENI MTAKATIFU WA ISRAELI MBELE YETU”.. kukomesha kunakozungumziwa hapo sio “kule kutoa adhabu” tunakokuelewa, bali ni kitendo cha “Kuzuia jambo lisiendelee kufanyika(kufikisha jambo kikomo)”.. Hivyo andiko hilo lilihusu watu waasi ambao hawapendi sheria za MUNGU, na hivyo wanataka kuambiwa tu maneno laini na manabii, maneno ya faraja si ya kukemewa makosa yao, na lengo la kutaka kusikia hivyo ni ili WAKOME (Yaani wasiendelee) kumwangalia MUNGU, na MUNGU pia aache kuwaangalia.
Kwahiyo Mtakatifu wa Israeli ni MUNGU MWENYEZI, na ndiye pekee anayestahili kuabudiwa na kutukuzwa, na mtu anayejitenga naye ni kwa hasara yake mwenyewe.
Isaya 48: 17 “Bwana, mkombozi wako, MTAKATIFU WA ISRAELI, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata”.
Mistari mingine inayomtaja Mungu kama Mtakatifu wa Israeli ni pamoja na Isaya 12:6, Isaya 47:4, Isaya 17:7, Isaya 30:12, Isaya 47:4, Isaya 48:2 na mingine mingi..
Je umemwamini YESU?.. Fahamu ya kuwa hakuna njia nyingine yoyote ya kumfikia MUNGU isipokuwa kwa kupitia yeye.
VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE
HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?
WhatsApp
Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
14 ambaye katika yeye TUNA UKOMBOZI yaani, MSAMAHA WA DHAMBI”.
Tusome tena Waefeso 1:7..
Waefeso 1:7 “Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao UKOMBOZI WETU, MASAMAHA YA DHAMBI, sawasawa na wingi wa neema yake”.
Kumbe! Maana ya “Ukombozi” ni “MSAMAHA WA DHAMBI”.
Kwamba Tunapopata Msamaha wa dhambi zetu, tunakuwa tumekombolewa na tena tumeokolewa na Nguvu za giza, na kuingizwa katika ufalme wa Mwana wa Pendo lake?.
Hivyo maombi makuu ya Ukombozi ni maombi ya Toba!, kwasababu tunapoomba Toba na kusamehewa katika roho tumepata ukombozi, jambo ambalo ni kuu sana.
Je umemwamini Bwana YESU na kutubu dhambi zako ili upate msamaha wa dhambi??..
Fahamu kuwa hakuna maombi yoyote ya ukombozi zaidi ya yale ya KUTUBU DHAMBI kwa kumaanisha kuziacha kwasababu adui wa kwanza wa mtu ni dhambi ikaayo ndani yake.
Hiyo ndio inayomfunga mtu, na kumharibia njia yake duniani, na njia pekee ya mtu kukombolewa na laana, vifungo, mikosi na kila aina ya vifungo ni kwa njia ya kutubu dhambi.
Ukitaka ndoa yako ikombolewe, tubu na acha uzinzi unaoufanya nje ya ndoa, kama unafanya hayo, hapo ukombozi wa ndoa utazalika wenyewe.
Ukitaka ukombozi wa kazi yako, watoto wako, na mambo yako yote suluhisho ni kutubu na kupata msamaha wa dhambi!.
Lakini tukiikwepa toba na kujitumainisha katika maombi ya kuombewa na kuvunjiwa laana, hakuna ukombozi wowote tutakaopata na hiyo ni Biblia sio theolojia wala mapokeo..
Tubu dhambi leo upate ukombozi, na ufurahie wema wa MUNGU.
Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa URUJUANI, Gari lake limenakishiwa njumu, Hiba ya binti za Yerusalemu”.
“Urujuani” ni neno lingine la rangi ya “Zambarau”..
Neno hilo pia tunalisoma katika kile kitabu cha 2Nyakati 2:7..
2Nyakati 2:7 “Unipelekee basi mtu mstadi wa kazi ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, NA YA URUJUANI, na nyekundu, na samawi, mwenye kujua kuchora machoro, pamoja na wastadi walioko Yuda na Yerusalemu pamoja nami, aliowaweka baba yangu Daudi”.
Rangi ya Urujuani/Zambarau kibiblia iliwakilisha Enzi/Ufalme… Hivyo mtu aliyevaa Mavazi yenye rangi hiyo ya Urujuani/zambarau alifahamika kama mtu mkuu, aidha mfalme, Malkia au jemedari.
Ufunuo 7:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi. 4 Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.
Ufunuo 7:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.
Utasoma tena juu ya rangi hiyo katika.. Mithali 31:22, Yeremia 10:9, Ezekieli 27:7, na Ezekieli 27:16.
Mafundisho Mengine
Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).
Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)
Namna sahihi ya kusoma Neno (biblia).
Tunasahau sana maisha yetu ya sirini, na kuweka nguvu kubwa, katika kuonekana kwetu kwa nje mbele za watu, hatujui kuwa Darasa kubwa la Mungu kwa mwanadamu lipo katika maisha yake ya sirini. Na Mungu humlipa mtu kwa hayo na si mengine.
Mathayo 6:4….na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Kujazi maana yake ni kulipa.
Ikiwa na maana, unayoyatenda sasa iwe ni mema au mabaya kwa siri, malipo yake utayaona baadaye kwa wazi.
Yusufu, kabla ya kuwekwa kuwa msimamizi wa mali yote ya Farao, alitumika kama wakili mwaminifu katika nyumba ya potifa, kwa muda mrefu. Baadaye Mungu akamlipa kwa kumpa Misri yote.
Yuda mpaka kuingiwa na shetani, hadi kumuuza Bwana wake, ni matokeo ya wizi aliokuwa anaufanya kwa siri kwa muda mrefu.
Daudi kabla ya kujazwa mafuta ya kumwangusha Goliathi, ni maisha ya sirini ya Imani aliyokuwa anayadhihirisha kule maporini kwa Mungu wake, mbele ya simba na dubu walipokuwa wanakuja kulishambulia Kundi. 1 Samweli 17:34-37)
Vilevile, kwa mtu yeyote yule, kupata kibali, kutumiwa na Mungu, kuinuliwa viwango vya kiroho..hutegemea sana hali zetu za sirini zinazoendelea sasa, Kwamfano utakuta labda huyu ni mwanakwaya, au mtumishi wa Mungu, lakini katika maisha yake ya sirini, anajichua, ni mzinzi, anakunywa pombe, Lakini kwa nje, anajionyesha kuwa ni mwema, anautunza ushuhuda wake, anavaa mavazi ya kujisitiri, anaongea kwa staha, ana juhudi katika utumishi, akidhani kuwa hilo ndio litamshawishi Mungu kumwongezea neema.
Ukweli ni kwamba hapo anapoteza nguvu, kwasababu tusipokuwa waaminifu katika madogo ya sirini, Bwana Yesu hawezi kutuaminisha katika makubwa.. Tabia mbaya za sirini, zinaharibu huduma zetu, utumishi wetu wa baadaye.
Mtu anataka apandishwe labda cheo kazini, lakini katika nafasi hiyo hiyo ya chini, anaiba, mwingine anataka apewe cheo lakini pale pale alipo hawajali watu walio chini yake, ni mwenye wivu, . Unategemea vipi Mungu amlipe mtu kama huyu?
Kabla hujalipwa na Mungu, unakuguliwa kwanza na Mungu.
Shughulika na maisha yako ya binafsi ya sirini, kwasababu hayo ndiyo yanayokueleza utakuwa nani mbele za watu baadaye.
Nini cha kufanya..
Mwalike Bwana, akuchunguze, sirini mwako, Mawazo yako, tabia zako, matendo yako. Kisha mwombe akuponye, na baada ya hapo anza kutendea kazi uliyoyaomba.
Simamia andiko hili;
Zaburi 139:23-24
23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; 24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele
Mungu akubariki.
USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.
NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.
HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE