SWALI: Sulemani ana maana gani kusema..Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.?
Wimbo Ulio Bora 2:7
[7]Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.
[7]Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini,
Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.
JIBU: Mwandishi anaeleza hekima ya kweli juu ya mapenzi halisi yanavyoundwa.. na hivyo anawaasa wale wote wanayoyatafuta…wajue kanuni hizo ili wasiingie katika hasara kama sio majuto.
Andiko hilo linalenga nyanja zote mbili;
Anaposema nawasihi enyi binti za Yerusalemu..
Anawakilisha kanisa, au watu wote wanaotaka kuingia katika mahusiano ya kindoa..
Anasema;
Kwa paa na kwa Ayala wa porini… Anaapa Kwa wanyama hawa, lakini tunajua mara nyingi kwenye agano la kale watu walikuwa wanaapa kwa jina la Mungu…lakini hapa anatumia wanyama hawa ambapo ni Paa na Ayala.
Ni aina ya swala, ambao kwa eneo la Mashariki ya kati ilikuwa ni kawaida sana kuwaona kwenye mapori tulivu..
Wanyama hawa wana sifa ya:
Hivyo mwandishi anawasihi watu wanapotaka kuingia katika mapenzi wayaone Kama ni kuwawinda Ayala na Paa… Ambao hawahitaji pupa…
Ndio maana anasema;
“Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.”
Akiwa na maana kuwa unapochochea mapenzi kwa haraka utayapoteza…mfano tu unapomvamia Ayala kwa pupa, hutampata atapotelea mbali…
Bali unapokuwa mtulivu na kumsogelea kidogo kidogo, ni rahisi kumnasa…
Hivyo Katika mahusiano ya mwilini anatuasa kuwa mahusiano ya kweli, yanajengwa katika muda…sio kwa kuyapaparikia…vijana wengi, wanang’ang’ania kuingia katika mahusiano kabla ya umri sahihi, au nyakati sahihi au wengine wakikutana hata wiki haijakwisha, ndani ya muda mfupi sana, utaona wameshaahidiana kuoana, na hatimaye kujikuta, wapo kwenye mahusiano hayo, kipindi kinapopita na kugundua uhalisia wao, na kasoro nyingi wanaanza kujuta kulitokea nini? Ni kwasababu walikurupukia mapenzi wala hawakuruhusu yaamke yenyewe katika wakati wake.
Lakini katika Roho, Bwana anaeleza mahusiano kati ya yeye na mtakatifu wake..Upendo kwa Kristo thabiti, hujengwa kwa jinsi tunavyokaa na kudumu ndani yake, na kujua sifa zake, tabia zake, na uweza wake, Na hiyo inakuja kwa kusoma Neno, maombi, na ibada…watu wanaotembea katika mambo hayo kwa kipindi kirefu ndio wanaozama katika mapenzi ya kweli na Kristo.
Lakini mtu anayempenda Yesu kwasababu kaponywa ugonjwa, au kwasababu kasaidiwa Biashara yake kustawi, au Bwana amemwonekani mahali fulani kipekee, mwingine anamtumikia Mungu kwasababu ya shinikizo fulani la watu…Hapo ni sawa na kumrukia Ayala kwa pupa…hatimaye utamkosa..
Watu hawa wanakuwa ni upendo wa kitambo tu, mambo yakishabadilika waanza kusema mioyoni mwao, kama Yesu mwenyewe ndio huyu ni heri nirudie tu maisha yangu ya nyuma…
Hiyo yote ni kwasababu alikurupuka…bila kujua sifa na tabia za ampendaye.
Usikubali upendo wako kwa Kristo ujengwe kwa matukio ya ghafla…ujenge upendo katika mahusiano ya muda.. ndipo yatakapokuwa thabiti.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.
USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO
Maombi Maalumu ya Kuombea Ndoa.
Print this post
lakini leo nitaka tuone maana ya ndani ya “kukaa ndani ya Yesu”.
Awali ya yote hebu kwanza turejee maandiko.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.
Je umeshawahi kumweka mtu moyoni kwa tendo zuri alilokufanyia?..
Au je umeshawahi kumtoa mtu moyoni kwa tendo baya alilokufanyia?.
Kama umeshawahi kupitia mojawapo ya hizo hali basi utakuwa umeshaanza kuelewa maana ya maneno hayo Bwana YESU aliyoyasema kwamba “kaeni ndani yangu nami ndani yenu…(Yohana 15:4).
Maana yake kuna mambo unaweza kuyafanya ukawa umeingia moyoni mwa Kristo, akavutiwa nawe zaidi, ukawa upo moyoni mwake..
Wapo watu ambao Yesu yupo mioyoni mwao (ndani yao) lakini wenyewe hawapo ndani ya YESU.
Hebu tujifunze zaidi kwa mifano…
Unaweza kuwa na marafiki wawili mmoja yupo moyoni mwako sana (aidha kutokana na jambo zuri alilowahi kufanya kwako) na mwingine ni rafiki tu wa kawaida kwako hayupo ndani yako,
Na kuna watu yawekana ukawa mioyoni mwao, lakini wewe usiwe mioyoni mwao..
Na ni hivyo kwa Bwana, kuna watu wapo ndani ya Yesu na kuna ambao hawapo ndani ya Yesu ingawa wamemwamini Yesu.
Sasa swali la msingi, ni kitu gani tunachoweza kufanya kikatuingiza ndani ya moyo wa Bwana YESU, (yaani tukamvutia sana hata kutuingiza ndani yake?).
Majibu ameyatoa yeye mwenyewe Bwana Yesu.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Meza ya Bwana ni tendo moja linalougusa moyo wa Bwana Yesu kuliko tunavyodhani kamwe usipuuzie ushirika mtakatifu.
Jambo la pili linalotuingiza ndani ya YESU, ni Kuzishika amri zake..
1 Yohana 3:24 “Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa”
Na amri kuu ni Upendo..
2 Yohana 1:5 “Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane. 6 Na huu ndio upendo tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo”.
2 Yohana 1:5 “Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
6 Na huu ndio upendo tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo”.
Kwahiyo kwa kufanya mambo mawili makuu, yaani Ushirika wa meza ya Bwana na tukipendana sisi kwa sisi, tutaugusa pakubwa sana moyo wa Kristo.
Na matokeo ya kuwa ndani ya Yesu kwa kufanya mambo hayo mawili, na kupewa chochote tunachokiomba..
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.
Mwisho: hatua za kukaa ndani ya Yesu kwanza zinaanza kwa wewe kumpokea Yesu, na ndipo mambo hayo mawili yanafuata.
Je umempokea Yesu kweli kweli?, kama bado unasubiri nini?…mpokee Yesu leo, ufanyike kiumbe kipya na kuoshwa dhambi zako.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
WhatsApp
Jibu: Turejee maandiko hayo..
2Nyakati 9:21 “Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu zilizokwenda Tarshishi pamoja na watumishi wa Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na NYANI, na tausi. 22 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima”.
2Nyakati 9:21 “Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu zilizokwenda Tarshishi pamoja na watumishi wa Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na NYANI, na tausi.
22 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima”.
Sasa swali, je Sulemani alifuga NYANI?..
Jibu ni ndio alikuwa anao NYANI, lakini hakuwa anawatumia kwa kitoweo, kwani kulingana na sheria za torati, Nyani alikuwa miongoni mwa wanyama najisi (wasiofaa kuliwa M/Walawi 11:27).
Lakini kama hakuwa anawatumia kama kitoweo alikuwa na anawatumia kwa shughuli gani?.. Jibu ni wazi kuwa kwa MAONESHO au michezo! (Ingawa Biblia haijaweka wazi kuwa ni kwa michezo).. lakini asilimia kubwa ni wazi kuwa Nyani na Tausi walitumika kwa kazi hizo katika majumba ya wafalme.
Hata sasa si ajabu ukiingia Ikulu utakuta nyani na Tausi na wanyama wengine, sasa uwepo wa wanyama wale Ikulu, si kwaajili ya kitoweo kwa Raisi, bali kwa maonyesho tu. Na Sulemani ni hivyo hivyo alikuwa ni mtu anayepokea zawadi nyingi kutoka mataifa mengi, na zawadi hizo ni za kila aina, hivyo si ajabu kuona akipewa zawadi za wanyama, au akifanya biashara za wanyama.
Je na sisi wakristo tunaruhusiwa kufuga wanyama pori hao katika nyumba zetu au wanyama hao wamebeba roho?..
Jibu ni Ndio tunaruhusiwa ikiwa sheria juu ya wanyama hao hazijavunjwa.. kama mtu ana kibali cha serikali kumiliki wanyama hao wa pori, basi kibiblia si kosa kuwamiliki pia, lakini iwe tu kwa dhamira kama hizo za maonyesho, lakini ikiwa kwa shughuli nyingine kama za kiibada au kijangili, ni kosa kibiblia.
Je umempokea YESU?.. Je unajua kuwa tunaishi majira ya kurudi kwa pili kwa YESU?, na parapanda imekaribia sana kulia?..Mwamini Yesu, na tubu.
Je wanyama wote waliwezaje kuenea kwenye safina ya Nuhu?
Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)
LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.
Swali: Je Kula nyama mbichi ni dhambi?.
Kwanini MUNGU aangamize watoto kwenye gharika ya Nuhu?
SWALI: Naomba kufahamu Tafsiri vifungu hivi Mhubiri 4:13-16, isemayo ‘Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki’ Nini maana ya habari ile?
Mhubiri 4:13 Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu. ambaye hajui tena kupokea maonyo. 14 Kwa maana kutoka gerezani alikuja kumiliki; naam, hata katika ufalme wake alizaliwa hali ya umaskini. 15 Nikawaona wote walio hai waendao chini ya jua, ya kwamba walishikamana na huyo kijana, huyo wa pili aliyesimama badala ya yule. 16 Hawakuwa na kikomo hao watu wote, hao wote ambao alikuwa juu yao; lakini hata hivyo wale wafuatao baada yake hawatamfurahia. Hakika hayo pia ni ubatili, na kujilisha upepo.
JIBU:
Mstari wa 13. Unazungumzia jinsi hekima, ilivyo bora kuliko cheo, au umri wa mtu. Yawezekana mtu akawa na vyote, lakini akipungukiwa na hekima, ni hatari kubwa sana, Na dalili moja wapo ya kupungukiwa hekima kama anavyofafanua mhubiri ni kukataa kupokea maonyo.
Mfano wa viongozi wa namna hii kwenye biblia ni Rehoboamu(mtoto wa Sulemani), Nebukadreza (nyakati za mwanzoni), Belshaza, Ahabu, Herode. Unaweza kuona jinsi utawala wao ulivyokuwa mwiba mkubwa kwa taifa, na wengine hata kwa vizazi vya mbeleni, kwasababu hawakukubali maonyo ya ki-Mungu..
Ni lazima tukubali kufundishika, kwasababu huo ndio msingi wa hekima (Mithali 13:1, 13:18, 15:5)
Lakini mstari wa 14
Anaeleza, jambo lingine, linalohusiana na ubatili… anazungumzia habari ya kijana aliyetoka katika umaskini, mpaka kuwa mfalme, aliyetoka vifungoni mpaka kuwa mfalme..
Kufunua kuwa mafanikio ya mwanadamu hayatabiriki, sio tu walio na cheo, au waliozaliwa katika familia ya kifalme, ndio wanaofanikiwa, Bwana anaweza kumwinua maskini, mtu asife faa, na kumfanya mtawala na mkuu, mfano wa Yusufu, na Daudi.
Pia Mstari 15,
Unaeleza kuinuka kwa mtawala mwingine, baada ya huyo kijana. Halafu watu wakashikamana naye huyo..Kuonyesha kuwa sifa za kibinadamu, huwa hauzidumu, maana yake kuwa hata uweje shujaa, ufanye mambo mazuri kiasi gani, utafurahiwa kwa kitambo tu, baadaye utachokwa, siku atakaponyanyuka mwingine, atapendwa, na kufuatawa..na wewe utasahaulika..
Mstari 16
Unaendelea kusema, bado watu waliendelea kumfauta huyo mfalme mpya, yaani walimfurahia pia sawa tu na walivyofurahiwa wafalme wengine nyuma waliopita, lakini ghafla baada ya muda wakamchoka naye pia..Mzunguko ukawa ni huo huo..
Ndipo mhubiri anahitimisha kwa kusema ni ubatili mtupu..Maana yake heshima, sifa, na mapokeo ya kibinadamu hayana umilele nyuma nyake, ni sawa tu na kufuata, upepo, ambapo unaweza kukupa matumaini ya muda, kukupelekea mbali, lakini katikati ya safari, ukayeyukia mbali na usijue unapokupeleka.
Haya ndio mambo tunayoyaona hata sasa katika ulimwengu, ni rahisi sana kuona watu wakimfurahia kiongozi mpya, tena yule mpambanaji, lakini baada ya muda wanaanza kupoteza furaha naye, na hatimaye kumpinga, wakitaka mwingine, na yule mwingine ajapo, huwa vivyo hivyo, wanamfurahia kwa muda, baadaye wanamchoka, mzunguko huo umekuwepo ulimwenguni wakati wote..
Lengo lao ni wakitumainia, kumpata kiongozi bora, lakini hajawahi kutokea..
Hawajui kuwa yupo kiongozi bora, mwema, asiyechokwa, asiye na hila, asitafuta vya kwake, aliyejitoa nafsi yake yeye mwenyewe, anayedumu milele, ambaye huyo mwanadamu akimkubali basi matarajio yake yanafikiwa, kwasababu ankuwa naye wakati wote moyoni mwake.. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.
Amwaminiye, anapokea uzima wa milele. Wengine wote unafuata upepo..
Je! Upo tayari kumpokea leo, Kama ni ndio, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;
Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)
Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.
Wimbo Ulio Bora 2:10-13
[10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako, [11]Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake; [12]Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu. [13]Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.
[10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,
[11]Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake;
[12]Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.
[13]Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.
Mahusiano yoyote yale hukumbwa na vipindi tofauti tofauti.ni sawa na dunia na misimu yake, kuna vipindi Vya kiangazi, vipindi vya masika, vipindi vya joto, na vipindi vya baridi…
Vivyo hivyo pia mahusiano yoyote hukumbwa na nyakati kama Hizi..
Watu wa agano la kale walikuwa katika nyakati ngumu za upendo na Mungu, nyakati zao zilijawa na misuko-suko, ukame na kutaabika, nyakati za jasho na damu…Kwasababu shetani alikuwa na nafasi kubwa katika maisha ya wanadamu, lakini walikuwa hawajamjua bado Mungu vizuri.
Lakini mwokozi alipokuja, alituliza dhoruba zote, mawimbi yote, jua lote, mizigo yote, na taabu zote ..alilitimiza hilo kwa kujitoa kwake pale msalabani. Ndio maana akasema yeye ni Bwana wa sabato, ( pumziko). Kwasababu Alikuja kuleta pumziko haswaa la pendo lake, ili mtu asikae katika masumbufu ya aina yoyote rohoni.
Hivyo leo hii anasema nasi kama mtu amwambiaye mpenzi wake habari za faraja..
10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako, [11]Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake; [12]Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika,
10]Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,
[11]Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake; [12]Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika,
Huu ni wakati wa kuitikia wito wake mkuu wa upendo usio na usumbufu.. mpokee sasa ukuburudishe maishani. Akupe uzima wa milele, akupe faraja na tumaini uone maana ya maisha. Nyakati hizi ni za hatari, ulimwengu hauwezi kukupeleka popote, kinyume chake utaishia jehanamu tu ukiufuata, lakini ukimgeukia mwokozi na kumfuata utapata uzima wa milele.
SHALOM.
MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe sana.. Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu mkuu lililo Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).
Upo ufunuo mkubwa Musa alioupata uliomfanya awe mpole kuliko watu wote duniani kwa wakati ule, kama maandiko yanavyosema..
Hesabu 12:3 “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”.
Na ufunuo huo ni “KUELEWA ZAIDI YA WENGINE WANAVYOKUWA WANAELEWA”
Sasa kabla ya kwenda kwa Musa hebu tujifunze kwanza kwa Bwana wetu YESU KRISTO (Mwamba Mgumu).. Bwana wetu maandiko yanasema alikuwa mpole sana (soma Mathayo 11:29 na Mathayo 21:5), kiasi kwamba alitemewa mate hakurudisha, alitukanwa hakujibu, alipigwa hakurudisha mapigo (soma 1Petro 1:23).
Sasa ni kitu gani kilichomfanya awe mpole kiasi kile?, upole ambao ni ngumu kwetu sisi kuwa nao?.. Jibu tunalipata pale kwenye Luka 23:34 aliposema Baba wasamehe kwakuwa hawajui watendalo!.
Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, KWA KUWA HAWAJUI WATENDALO. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura”.
Nataka uone hilo Neno “KWA KUWA HAWAJUI WATENDALO”… Maana yake YESU alikuwa anajua zaidi ya watu walivyokuwa wanajua, alijua wale watu wanafanya mambo wasiyoyajua.. ni kama tu mtoto anayesaidia haya ndani ya nguo yake, anafanya jambo asilolijua ambalo si sahihi, lakini kwasababu wewe unajua zaidi ya yeye ajuavyo, huishii kumkasirikia bali kumsaidia.
Lakini kama usingejua zaidi ya hapo, ungeishia kuona mtoto anafanya makusudi na ni mjinga, na Bwana YESU ndicho alichokiona, aliona wanaomsulubisha si akili zao zinafanya vile, bali wanafanya mambo wasiyoyajua kwamaana kama wangejua ni nani wanayemsulibisha hakika wasingefanya vile, ndivyo maandiko yanavyosema..
1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; 8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu”.
1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu”.
Ni hivyo hivyo kwa Yuda, wakati wengine wana huzuni ya Bwana kusalitiwa, tayari Bwana alijua sababu za Yuda kumsaliti kuwa hazikuwa akili zake bali ni ili maandiko yatimie, hivyo hiyo haikumfanya Bwana amchukie Yuda au aache ukarimu wake kwake.
Sasa turejee kwa Musa… naye pia siri ya upole wake ni hiyo hiyo!, alikuwa ANAELEWA ZAIDI YA WENGINE WALIVYOKUWA WANAELEWA.
Wakati wana wa Israeli wanamlalamikia na kumnung’unikia Farao na kumwona ni mkatili, Musa alielewa zaidi ya wanavyoelewa wao..
Wakati wengine wanamwona Farao ni Mgumu, lakini Musa alielewa kuwa ule ugumu wa moyo wa Farao ni Mungu ndiye aliyeuweka ndani yake, hivyo Farao alikuwa hafanyi yale kwa akili zake.. kwahiyo Musa hakuchanganywa na kiburi cha Farao, kwasababu alikuwa anaelewa zaidi ya wengine wanavyoelewa..
Kutoka 4:1 “Bwana akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; LAKINI NITAUFANYA MGUMU MOYO WAKE, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao”.
Na hiyo ikamfanya Musa awe mpole kuliko wengine wote kwasababu alijua kila kitu kipo chini ya uongozo wa Mungu.
Vivyo hivyo na wewe na mimi, ni lazima tuelewe zaidi ya wengine wanavyoelewa ili tupate utulivu, wakati mwingine huwezi kupata utulivu usipojua sababu ya mambo, si kila tukio baya linalotokea mbele yako ni shetani, mengine Mungu anayaleta kwasababu maalumu, kinachohitajika ni utulivu na kumngoja Bwana.
Si kila mtu anayekukataa kapewa huo moyo na shetani, wengine ni Mungu kaifanya mioyo yao hivyo, ili Mungu baadae aonyeshe uweza wake wote kwako, na umtukuze!..unaweza ukajaribu kufanya kila kitu kizuri na hata ukaonyesha wema wote bado usipate kibali, hiyo haina tafsiri kwamba kuna shida kwako, hata Musa alitoa ishara tisa mbele ya Farao lakini hazikuzaa matunda..ila mwisho wake ulikuwa mkubwa.
Vile vile nawe pia kabla hujafikiria kupaniki kwa hali yoyote unayokutana nayo mbele yako, hebu tuliza kwanza akili kumwomba Mungu akufunulie sababu.. Hali nyingine za misukosuko hazitoki kwa shetani, bali ni Mungu anayezileta kwa makusudi yake Mema, kwasababu kamwe Mungu hapendi kuwatesa wanadamu, lakini anayaruhusu mengine ili yalete ushuhuda mkubwa hapo mbeleni.
Tafakari vipi kama Farao angetii tu kwa lile pigo la kwanza, leo tusingemjua Mungu katika uweza ule wote, vipi kama Ayubu asingepitia yale yote, leo tusingemjua Mungu kama ni mwokozi anayerudisha vyote ambavyo vimepotea kabisa..kwahiyo ni kutulia tu na kumwomba Mungu uelewa wa kina wa yanayoendelea!.
Na ukipata uelewa wa kutosha wa yanayoendelea, au yaliyotokea zaidi ya ulivyokuwa unaelewa, au watu wanavyoelewa, utakuwa mpole kuliko watu wote, utakuwa na ujasiri kuliko watu wote, utakuwa mwenye nguvu kuliko watu wote, pasipo kujali hali zinazoendelea.
Bwana atusaidie tupate kuelewa ziaid ya tunavyoelewa sasa.
Maran atha!
Je! Petro na wenzie walitambuaje kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya?
Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)
Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?
Wimbo Ulio Bora 8:6-7
[6]Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu. [7]Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.
[6]Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.
[7]Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.
Habari hiyo inamzungumzia Bwana arusi ambaye anataka kuingia katika mahusiano ya ndani na bibi arusi wake, hivyo anaanza kwa kumwomba amkubali Kama “Muhuri” .
muhuri huwa unawakilisha umiliki halali wa kitu hicho..
Hivyo huyu Bwana arusi anamtaka bibi arusi akubali muhuri wake, katika moyo wake na katika mkono wake…pande mbili…moyoni ikiwakilisha ndani yake ni mkononi nje, yaani upendo wa ndani na ule upendo wa nje…kumilikiwa kwa ndani lakini pia kumilikuwa kwa nje..
Na matokeo Ya kufanya hivyo ndio hapo anaendelea kueleza sifa za huo upendo akisema upendo una nguvu kama mauti…yaani Kama vile mauti isivyo pingika juu ya mtu, kwamba kufa atakufa tu, vivyo hivyo upendo wa kweli ukimnasa mtu haupingiki..atamlinda tu.
lakini pia anasema wivu wake ni mkali kama Ahera, ni mfano huo huo, maana yake hauvumilii maovu, pale unaponajisiwa…ni lazima utatoa tu matokeo..unakula Kama moto moyoni…ndio Uliomla Bwana Yesu alipoona nyumba ya Baba yake imegeuzwa kuwa pango la wanyang’anyi akatengeneza kikoto na kuanza kuharibu kwa makusudi kazi zote za kipepo zilizokuwa zinaendelea pale hekaluni…wivu wa upendo huharibu lakini vile vilivyo viovu.
Bado anasema ‘maji mengi na mito Haviwezi kuuzima, Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa’
yaani hata mtu akijaribu kuuzimisha kwa hongo za kifedha anafanya kazi bure…
Nguvu ya upendo wa Kristo kwetu pale tunapoupokea vizuri..tunakuwa salama milele ndani Yake..
Lakini Hatua ya kwanza Kristo anataka kututia muhuri wake moyoni na mkononi…na muhuri huo ni Roho Mtakatifu(Waefeso 4:30), anataka udhihirisho wa Roho uonekane mioyoni mwetu, lakini pia mwilini (kwa matendo yetu).
Utakatifu wa ndani na nje.
Kuna Watu wanampokea Yesu moyoni tu, lakini lakini badiliko la nje hawana habari nalo, wanamkiri kwa vinywa vyao lakini kwa matendo yao wanamkana..
Tito 1:16
[16]Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.
Hapo bado upendo wa kweli haijafunuliwa…lakini pale tunapodhamiria kumpokea Kristo Kwelikweli, basi nguvu ya upendo wake inatunasa na matokeo yake yanakuwa hata tufani ya namna gani ije, yeye mwenyewe anatushika, hata dunia nzima itutenge bado hatuwezi tikiswa, hata tuahidiwe utajiri na mali zote duniani, bado upendo wetu hauwezi kupungua kwa Kristo, kwasababu ni wewe mwenyewe aliyetunasa kwa agano la muhuri rohoni na mwilini.
Yesu alisema…
Warumi 8:35-39
[35]Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Je upo tayari leo kuokoka? Kama ni ndio basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii kwa msaada huo bure.
Wimbo Ulio Bora 5:2-6
[2]Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku. [3]Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje? [4]Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake. [5]Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo. [6]Nalimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.
[2]Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha!
Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu,
Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku.
[3]Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje?
[4]Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.
[5]Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo.
[6]Nalimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita;
(Nimezimia nafsi yangu aliponena),
Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.
Habari hii inaeleza kisa cha mtu na mpenzi wake, ambayo inafunua mahusiano ya mtu na Kristo, na jinsi mwitikio Wake unavyopaswa uwe.
Hapa anaonyesha mwanamke mmoja akiwa ndani usiku amelala peke yake na mara akasikia mpenzi wake anabisha Mlango amfungulie,
Lakini alijawa na uzito, akaanza kukawia-kawia, pengine huwenda kwasababu ya starehe ya kitanda, au kuna mambo yake mengine ya siri alikuwa anayafanya
Lakini bado mpenzi wake aliendelea kugonga, bila mfanikio ya kufunguliwa…na safari hii akatoa mpaka maneno ya upendo yamkini yatamshawishi ili aje kufungua kwa haraka. Lakini bado hakufua dafu.
Mpaka dakika ya mwisho, alipogonga, na mbisho ule kuingia moyoni mwa yule mwanamke, ukamchoma ndipo akatoka haraka na kwenda kumfungulia..
Lakini kwa bahati mbaya hakumkuta, kumbe tayari alishaondoka…akaanza kutoka kumtafuta bila mafanikio..na matokeo yake huko nje kukutana na madhara mengine.
Hili ni jambo ambalo watu wengi humfanyia Kristo rohoni sasa…Anasema..anasema..
Ufunuo wa Yohana 3:20
[20]Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Lakini watu hukawia-kawia kwasababu ya udanganyifu wa mambo Ya duniani, mwingine atasema ngoja kwanza nimalize ujana, ndio nitaokoka, mwingine ngoja nipate kazi mwingine ngoja niolewe, mwingine ngoja ifike mwakani, mwingine ngoja nikimaliza masomo ndio nitampokea Yesu..n.k
Ndugu Saa ya wokovu ni sasa Kristo anakuita, wakati ndio huu, usipoufungua moyo wako sasa, utafika Wakati utamtafuta Kristo na hutampata…
Luka 13:24
[24]Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
Luka 12:36-40
[36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. [37]Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. [38]Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. [39]Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. [40]Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.
[36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.
[37]Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.
[38]Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.
[39]Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa.
[40]Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.
Okoka leo ndugu, neema ya wokovu ipo sasa lakini haitadumu milele..hiyo sauti inayoita moyoni mwako itii, haraka, starehe za duniani zinapita, maisha yanapita, ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana maisha yako, basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure kwa msaada huo..
Mshulami ni msichana gani?
Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).
Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).
Ikiwa wewe ni mwanandoa, ni busara kuwa na maombi yako maalumu kwa ajili ya ndoa yako.
Waweza kutenga siku kadhaa katika wiki, au mara mbili katika wiki, kuwa na maombi maaalimu marefu kwa ajili ya ndoa yako.
Maombi ni nyenzo muhimu katika kuendesha na kufanikisha sehemu zote zamaisha yetu, huduma inahitaji maombi, kanisa linahitaji maombi, taifa linahitaji maombi, wewe unahitaji maombi, vivyo hivyo na ndoa yako pia inahitaji maombi ili iwe na ustawi Bora katika nyanja zote..hata kama huoni tatizo lolote ndani ya ndoa ..bado unahitaji maombi sana.
Kwanini maombi? Ni kwasababu njia pekee ambayo Mungu huweza kuyaingilia maisha yetu ili ayatengeneze vema basi ni kwa njia ya maombi.
Ndoa inaweza ikadumu lakini isiwe na amani, ndoa inaweza ikawa na amani lakini isiwe na mafanikio, ndoa inaweza ikawa na mafanikio lakini imekosa Mungu, vilevile inaweza ikawa na umoja lakini imejaa wivu, inaweza ikawa haina shida lakini watoto wanaokuja wakawa na matatizo, inaweza pia ikawa sawa leo, lakini kesho shetani akaishambulia….Hivyo suala la kuombea ndoa ni jambo la muhimu sana.
Huu ni mwongozo wa maeneo muhimu ya kuombea kila uingiapo katika maombi ya namna hii. (Kila kipengele tumia dakika 30)
Mungu alipomuumba mwanaume na mwanamke na kuwaleta katika ndoa aliwafanya mwili mmoja tena..Maana yake aliweka Muunganiko usiowezekana kibinadamu Wa umoja..
Mathayo 19:5
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
Hivyo hakikisha unaombea ndoa yako Bwana adumishe umoja wenu, uwe umoja kwelikweli, na kamwe pasiwepo matengano. Maana huo ndio mwanzo wa ndoa thabiti
Omba kwa nguvu, huku ukivunja roho za matengano, ukiangalia zaidi maeneo ambayo unaona kabisa yanahatarisha umoja wenu, yenye dalili ya kutaka kuwaachanisha hayo ndio uyaombee zaidi, ikiwa ni kazi, au watu, au magonjwa, mwambie Bwana apatengeneze hapo..tumia si Chini ya dk. 30 kuombea eneo hilo moja tu.
Hivi viwili navyo ni nyenzo kubwa sana katika ndoa thabiti. Bwana aliagiza mwanamume ampende mke wake kama mtu apendavyo mwili wake mwenyewe.. vivyo hivyo aliagiza mke amtii mumewe Kama mtumwa kwa Bwana wake.
Waefeso 5:22-25
[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. [23]Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. [24]Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. [25]Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.
[23]Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
[24]Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
[25]Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
Hivyo ikiwa wewe ni mke, mwombee sana mumeo Bwana alidumishe pendo lake kwako, lakini pia ikiwa wewe ni mume mwombee mkeo Bwana amjengee utii kwako.
Lakini pia jiombee wewe sawasawa na jinsia yako Bwana akuzidishie upendo na utii..kwasababu vyote hivi ni nyenzo kwa wote, vizidi bila kupungua nguvu kwa jinsi siku zinavyokwenda.
Ndoa ikikosa maelewano hupoteza dira yake.
i) Omba Mungu ajenge usemi mmoja yaani lugha ya maelewano kwanza katika eneo lenu la kiroho.. Maana yake wote msisimame katika Bwana (muokoke), ikiwa mmojawapo hajaokoka mwombee neema Ya wokovu, injili imchome abadilike na kumpokea Kristo, na huku ukimhubiria pia.
ii) Omba pia Mungu awape Maelewano Katika majukumu yenu ya kiroho(utumishi). Mfano ratiba za ibadaza nyumbani, maombi, mikesha, mifungo, ushuhudiaji, na utoajik.
Ikitokea mmoja wenu haafiki majukumu hayo, si rahisi mwingine kutekeleza na matokeo yake inakuwa ni kushindwa kutimiza lengo kuu la kindoa. Kumbuka mmewekwa katika ndoa ili mumtumikie Mungu pamoja..hivyo jambo hilo ni lazima Lipewe nafasi ya kwanza na kubwa katika ndoa.
iii) Lakini pia omba maelewano katika mambo Yote ya kimaisha.
Mfano mikakati ya kimaendeleo, matumizi ya kifedha, n.k. huku ukigusia Maeneo yako yote ambayo unaona mikwaruzano inatokea, Au dalili hizo kutokea..ukiharibu hivyo vyanzo kwa maombi yako.
iv) Lakini pia Bwana awajengee mioyo ya kusamehe na kuachilia.
Ndoa nyingi zimeingia dosari, kupoa hata kufikia hatua ya kuvunjika kabisa kutokana na kuwa zimepoteza mioyo wa kusamehe na kuachilia Kwasababu ya majeraha au makosa yaliyofanyika nyuma..
Wakolosai 3:13
[13]mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
Mwambie Bwana sikuzote, wote mpewe mioyo ya kusamehe na kuachilia.
Hapa pia ni mahali pa kupaombea sana.. Wengi wanadhani wanaweza linda ndoa zao kwa kuweka sheria kali, kwa kufuatilia nyendo zao, kwa kuwavisha mavazi ya kuficha mpaka nyuso, Lakini uhalisia ni kwamba ikiwa mtu amekosa uaminifu, huyo kamwe halindiki, atakuzunguka tu, Hivyo omba kwa Bwana juu ya mwenzi wako, na kwako pia Bwana awaumbie moyo wa uaminifu. Hilo linatosha kuwa ulinzi mkubwa kwa ndoa yako.
Nyuma ya mafanikio ya kitu chochote chema, ni lazima utaona uvumilivu ulipewa nafasi, hata huduma ya kufanikiwa hutegemea uvumilivu. Ndoa haimaanishi kila siku itakuwa ni furaha tu, zipo nyakati za kupishana kibinadamu, za kusemwa vibaya, za kuudhiwa zipo nyakati za kupungukiwa, yapo madhaifu pia.. Hivyo omba moyo wa uvumilivu thabiti uwe juu ya kila mwanandoa.. kuanzia wewe mwenyewe.Ili nyakati ngumu zitakapopita pasiwe na wepesi wa kuiacha ndoa au kuchukua Hatua za madhara.
Ndoa ikikosa mwelekeo wa ki-Mungu huishia pagumu. Omba Mungu awape dira sahihi isiyo na majuto katika mikakati yenu yote ya kimaisha.
Omba Bwana ayanyoshe mapito yenu, awafanikishe, awaepushe na njia ya majuto na upotevu wa yule mwovu.. kwasababu maandiko yanatuonyesha ndoa ya kwanza ilivamiwa na uharibifu kwasababu ya udanganyifu wa ibilisi, kwa kitendo cha Hawa kusikiliza na kuifuata njia nyingine ambayo hakuagizwa na Mungu, na matokeo yake alipokula tu lile tunda ikasababisha matatizo makubwa ambayo mpaka sasa tunayaona ..
Mafanikio Ya ndoa hutegemea pia mahusiano mema kwa ndugu na wakwe..Musa alifanikiwa kuiongoza huduma vizuri kwasababu alikuwa na mahusiano mazuri na mkwe wake Yethro. Ruthu alifanikiwa kuolewa na Boazi mtu mkuu na mwenye uwezo kwasababu alikuwa na ukaribu na mama mkwe wake Naomi hata baada ya kufiwa na mumewe.
Vivyo hivyo na wewe pia uhusiano wako ukiwa mzuri na watu wa upande wa mwenzi wako unaharakisha baraka na neema nyingi za Mungu.
Lakini pia ikiwa mahusiano ni mabovu, basi ndio utumie fursa hii kuombea utapatanisho haraka, sana. Eneo hili ni muhimu sana kuliombea, ijapokuwa wengi hulipuuzia.
Ikiwa ni ndoa ambayo tayari inayo watoto ni muhimu kuwaombea watoto wako daima, wasiwe chanzo cha nyinyi kufarakana, lakini kuwa mwiba na uchungu kwenye ndoa yenu.
Lakini ikiwa bado hamjawa na watoto, ombea uzao wako ujao ukawe faraja na neema kwenu. Watoto wakiwa wabovu wanaweza kuihatarisha ndoa yako, au kuifanya isiwe na amani. Hivyo waombee sana wokovu, ulinzi, afya, adabu.
Shalom.
Ukizingatia kuviombea vipengele hivyo, kila kipengele si chini ya nusu saa. (dakika 30), utaona neema kubwa sana ya Mungu ikifanya kazi katika maisha yako.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
NDOA NA TALAKA:
SWALI: Silaha za Nuru ni zipi?
Warumi 13:12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru
JIBU: Ni lazima tufahamu ulimwengu wa roho upo katika pande mbili,
Upande wa Nuru ni wa Kristo (Yohana 1:4-5), na upande wa giza ni wa ibilisi.
Na pande hizi hazijawahi kupatana hata kidogo, na kama hazijawahi kupatana maana yake zipo vitani na kama zipo vitani basi zote zina silaha zake, kuhakikisha zinajilinda, lakini pia kushambulia, ili kuua utawala mwingine. Ndio hapo kwanini tunaambiwa tuzivae silaha za nuru. Maana yake mtu anaweza akawa ni wa nuru lakini akawa hana/hajui kuzitumia silaha za Nuru.
Vifungu vifuatavyo ni kututhibitishia kuwa Nuru na giza vipo katika mapambano;
2Wakorintho 6:14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. 13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake
Sasa silaha za Nuru ambazo mtu akiwa nazo ataweza kujilinda na mashambulizi ya giza, lakini pia ataweza kuushinda ufalme wa giza ni hizi;
Silaha hizi, ndio zile zinazotajwa pia kwenye Waefeso 6:10-18, kama silaha za haki.
Kwa maelezo marefu juu ya silaha hizi, fungua hapa usome >>> Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Mtu akiwa na mambo haya, ataweza kulishinda Giza, kotekote.. Ambalo, silaha zake ni kama zifuatazo;
Swali ni Je! Umejivika silaha Nuru ?
Ikiwa upo nje ya Kristo, huwezi kusimama, unahitaji wokovu kwanza, ikiwa upo tayari kufanya hivyo wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?
NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO