Category Archive Uncategorized @sw-tz

HEKIMA ILIYO SAHIHI, KATIKA HIMIZO LA UTOAJI SADAKA.

Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Yoashiliingiwa na wazo la kutaka kuikarabati nyumba ya Mungu (Hekalu), na kuamsha tena shughuli za kiibada zilizokuwa zimeharibiwa Na watawala wabovu waliotangulia..

Hivyo kwa kuwa alijua ukarabati unahitaji fedha, alichukua hatua ya kuwatoza watu kodi ya nyumba ya Mungu..Ambayo iliagizwa katika torati na Musa..(2Nyakati 24:9)

Hivyo akawateuwa  Walawi, walisimamie jambo hilo tangu mwanzo hadi mwisho, lakini likawa kama linacheleweshwa…

Mpaka baadaye akawauliza tena, kwanini kazi inacheleweshwa, kwa kuona hakuna chochote kilichofanyika..

Lakini mfalme akaja na mkakati mwingine, ili shughuli hiyo ifanyike kwa haraka na wakati, akaona kuliko Kuwalazimisha watu kulipa kodi ngoja aweke sanduku kubwa katika lango la hekalu na kupiga panda kwa watu wote wa Yuda waje kumtolea Mungu wao kwa hiari, bila shuruti..

Na wazo lile likapendwa na watu wengi, na hatma yake makusanyo yakawa mengi, kila siku mpaka wakapata fedha za kuwaajiri wajenzi ili kulikarabati hekalu, na kutengeneza vyombo vya nyumba ya Mungu.

2 Mambo ya Nyakati 24:6-14

[6]Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa BWANA, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?

[7]Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya BWANA wamewapatia mabaali.

[8]Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya BWANA.

[9]Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea BWANA kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.

[10]Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.

[11]Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.

[12]Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya BWANA; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya BWANA, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya BWANA.

[13]Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.

[14]Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya BWANA, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya BWANA, daima, siku zote za Yehoyada.

Ni nini tunafundishwa Na Roho Mtakatifu..

Utoaji wenye baraka na anaouhitaji Mungu ni ule wa hiyari na sio wa kulazimishwa…kama kanisa la Kristo Lazima tufikie hatua hii, kwamba viongozi hawawashurutishi watu kutoa mchango,mfano Zaka, Kama vile himizo la kodi, kwamba usipotoa unachukuliwa sheria ya kinidhamu …lakini pia watu nao wanawajibika wenyewe kumtolea Mungu kwa uaminifu na moyo..kanisa lifikiapo hatua hii ya kiroho, Mungu huliongezea baraka sana.

Usikubali kukumbushwa-kumbushwa, au kuhimizwa-himizwa kumtolea Mungu, Bali mtolee Mungu zaka zako, sadaka zako, kwa moyo wa furaha, Bwana atakubariki.

2 Wakorintho 9:6-8

[6]Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

[7]Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Bwana awabariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

SWALI: Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

Yuda 1:3

[3]Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.


JIBU: Mwanzo mwa waraka huu, mtume Yuda anaanza kwa kusema maneno hayo “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote”

Aliowaandikia waraka huu ni watu wote waliomwamini Yesu, (yaani waliookoka) kwamba wokovu huo ni wao Wote.

Anaandika maneno hayo pengine kutokana na dhana iliyokuwepo ya watu kufikiri kuwa wokovu ni wa jamii ya watu fulani tu.. pengine wayahudi, au waliotahiriwa, au mabwana tu..Hapana

Bali Kristo alikivunja kiambazi chote, ili watu wote wastahili kushirikia neema yake sawasawa.

Wagalatia 3:26-28

[26]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.

[27]Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.

[28]Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.

Jambo hilo kwa mwanzoni lilikuwa ni gumu kupokelewa hata na baadhi ya watakatifu wa Yerusalemu. Utakumbuka walipomwona Petro ametumwa na Roho Mtakatifu kwenda nyumbani mwa Kornelio mtu wa mataifa bado ilikuwa ngumu kupokelewa na wao…kwasababu imani na dini zote walizozijua tangu zamani, zote zilikuwa ni za kitabaka, kibaguzi, kitaifa n.k..na sio za kila mtu.

Kitendo cha Yesu kuwaambia kahubirini habari njema za ufalme kwa mataifa yote, bila kujali lugha, cheo au jinsia hawakuelewa vema..ndio maana siku ile ya pentekoste walikuwepo watu wengi wamekusanyika watu wa kila taifa chini ya jua. Na wote wakajazwa Roho Mtakatifu.(Matendo 2)

Hivyo ujumbe huu ni lazima ukae mioyoni mwetu hata sasa ili tusiwe Na ubaguzi katika kuwavuta watu kwa Kristo, au tusionyeshe upendeleo kwa kundi fulani tu la watu, Mungu hapokei uso wa mwanadamu.. linapokuja suala la wokovu na mema yote ndani yake watu wote wamestahili na ni sawasawa machoni pake, kushiriki vipawa vyote vya Mungu.

Mwingine atasema, huwezi kumjua Mungu mpaka uwe chini ya nabii au kuhani fulani, hilo si sawa..

Lakini jambo lingine la kujifunza ni kuwa ijapokuwa ni wetu sote anasema tuishindanie imani.. kwasababu adui naye yupo kazini kutaka kuwang’oa watu wa Mungu kwenye mstari wa imani ya kweli, na kuwafanya waangukie imani danganyifu, zilizoletwa na watu wanaojiingiza Kwa siri ndani ya kanisa..

Hivyo anaeleza mkristo ni wajibu wake, kuilinda imani yake, kwa kuendelea kudumu katika kuomba, upendo, na kujifunza vigezi halisi vya neema ya Mungu, ili asiigeuze kuwa ndio chanzo cha kuishi kwenye dhambi na uovu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

Print this post

Nini maana ya ‘kupelekea mkono’ (Esta 2:21)

SWALI: Nini maana ya “kupelekea mkono” kama ilivyotumika kwenye maandiko. Esta 2:21

Esta 2:21

[21]Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero.

JIBU:

Kupeleka Mkono, ni neno linalomaanisha “kutaka kudhuru”. Kwamfano katika hiyo habari tunaona Mordekai kama msimamizi wa malangoni pa mfalme aligundua njama za watumishi wenzake wengine ambao walitaka kwenda kumuua mfalme..hatujua aidha kwa kumwekea sumu, au kumchoma upanga, au hatua nyingine yoyote ilitayo madhara.

Kitendo hicho kibiblia, huitwa “kupeleka mkono”

Tunaweza kuona jambo lingine kama hilo, wakati fulani Daudi alimkaribia sana mfalme kwa kiwango ambacho angeweza kumuangamiza kama angetaka..lakini akasema nisinyoshe mkono wangu kwa masihi wa Bwana. Maana yake nisimuue.

1 Samweli 24:4-7

[4]Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia BWANA, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri.

[5]Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.

[6]Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. 

[7]Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake.

Bwana akubariki..

Je umempokea Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yako?

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo.. basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.. Pia kufahamu tafsiri ya maneno mengine ya kibiblia tazama chini.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 1 & 2

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Print this post

‘laana ya torati’ maana yake ni nini?

SWALI: Nini maana ya ‘laana ya torati’, ambayo Kristo alikuja kutukomboa kutoka katika hiyo?

Wagalatia 3:13

[13]Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;


JIBU:

Mungu alimpa Musa Torati ambayo ndani yake haikuwa na baraka tu pale Mtu alipoitii, bali pia ilikuwa na laana nyuma yake pale mtu alipoiasi..

Sasa hizo laana ndio ziliitwa “laana ya torati”, yaani adhabu, hukumu na kutengwa na uso wa Mungu.

Ukisoma Kumbukumbu la torati sura ya 27 – 28 inaeleza kwa undani juu ya baraka na laana mtu azipatapo pale anapoitii Au kunapoikataa torati..

Kwamfano

Kumbukumbu la Torati 27:26 inasema;

[26]Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.

Hivyo wanadamu, wote hawakufanikiwa kuzishika amri zile, na sheria Mungu alizowapa, na matokeo yake ikiwa ni laana juu ya kila mtu.

Warumi 3:10-12,23

[10]kama ilivyoandikwa, ya kwamba,  Hakuna mwenye haki hata mmoja. [11]Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. 

[12]Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja…

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

Sasa Kristo alipokuja, alifanywa laana kwa ajili yetu..sawasawa na hiyo Wagalatia 3:13, maana yake aliichukua hukumu yetu ya makosa kwa kupigwa na kufa kwake pale msalabani ili sisi tuponywe..

Warumi 8:1

[1]Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

Ndio maana mtu yeyote ambaye hajamwamini Kristo bado yupo Chini ya hukumu na adhabu, kwasababu atataka kumpendeza Mungu kwa kutegemea tu nguvu zake mwenye, na hatimaye mwisho wa siku atashindwa..kwasababu hakuna mwanadamu aliyewahi kuishika torati yote…

Atasema haibi, hasemi uongolakini wakati huo huo ana mawazo mabaya, yote hayo ni makosa na dhambi…na mshahara wa dhambi sikuzote ni mauti..(Warumi 6:23)

Umeona umuhimu wa Yesu maishani mwetu?

Unasubiri nini usimwamini, akutoe katika laana hiyo, ili uhesabiwe bure kwa neema yake?

Mpokee sasa akuokoe…bofya hapa kwa mwongozo wa sala hiyo…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Neema ni nini?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 21:3 Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:3

[3]Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

JIBU:

Mstari huo unatufundisha mambo ambayo Mungu huvutiwa nayo zaidi…

Mungu hupendezwa zaidi na sisi tunapoishi maisha ya haki, tunatenda mema, tunawajali wengine, tunaishi sawasawa ni viwango vyake vya kiroho hapa duniani..kwake hiyo ni bora zaidi ya sadaka zetu tumtoleazo.

Sadaka huwakilisha mambo yote Ya kidini tunayoweza kumfanyia Mungu, mfano ibada, fedha, mifungo, maombi, kuhubiri, kuimba n.k

Bwana huvutiwa zaidi na mioyo na tabia zetu, na sio zile Ibada za nje tu..

Haimaanishi kuwa hapendezwi na hivyo vitu hapana…bali hivyo vifanywe baada ya kutii kwanza..

Tunaona jambo kama hilo amelisisitiza sehemu nyingi kwenye maandiko; Tukianzia kwa Sauli alimwambia, hivyo;

1 Samweli 15:22

[22]Naye Samweli akasema,  je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu  Sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu,  Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

Mika 6:6-8 inasema;

[6]Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?

[7]Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?

[8]Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Soma pia..

Isaya 1:11-17 – Inasema…Bwana huchukizwa na sadaka za watu wanaishi katika dhambi

Hivyo ni lazima tujiulize Je! tunatenda haki kwa wengine?

Je! Tunatembea kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wetu?

Je! tunamtii Mungu, kuliko vitu vingine vyovyote?

Je tunawahurumia wengine…?

Mambo kama haya ndio yenye uzito zaidi kwa Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

MCHE MWORORO.

Print this post

Je kuna Yohana wangapi katika biblia?

katika agano jipya wapo watu wanne ambao wametajwa kwa jina la Yohana.. Wawili kati ya hao ndio hujulikana sana…ambao ni Yohana mbatizaji na Yohana mtume wa Yesu ..hawa wametajwa Sehemu nyingi katika agano jipya..

1) Yohana Mbatizaji

Mfano vifungu ambavyo utamsoma Yohana mbatizaji ni kama vifuatavyo:

  • (Luka 1) – Kama mwana wa Zekaria na Elisabeti
  • (Mathayo 3:13-17), Kama aliyembatiza Yesu
  • (Marko 6; 14-29)- Kama aliyekatwa Kichwa na Herode.

2) Yohana mtume.

Hivi ni vifungu vinavyomtaja Yohana Mtume;

  • (Mathayo 10:2) – Kama mmoja wa mitume 12 wa Yesu
  • (Marko 1:19) Kama ndugu wa Yakobo, na mwana wa Zebedayo

Na ndiye mwandishi wa injili ya Yohana, pia na nyaraka zote tatu (1,2, 3 Yohana, ) pamoja na kitabu cha Ufunuo.

3) Marko (Msaidizi wa huduma ya Paulo na Barnaba)

Yohana mwingine ni Marko, ndiye mwandishi wa kitabu cha Marko,..anatajwa katika kitabu cha Matendo 12:12, 13:5, Wakolosai 4:10

Na ndiye aliyekuwa Msaidizi wa Paulo na Barnaba katika ziara zao za kupeleka injili kwa mataifa.

4) Yohana babaye Petro

Yohana mwingine ni Baba wa Simoni Petro anatajwa katika;

Yohana 1:42

[42]Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).

Soma pia Yohana 21:15-27

Hivyo jumla Yao ni wanne…

Je ungependa kufahamu Zaidi watu wengine Katika biblia? Kama ni ndio basi jiunge tazama chini kwa makala nyingine..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Filipo ni nani na je! Kuna Filipo wangapi katika biblia?

Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?

Kwanini nguo za waliomwua Stefano ziwekwe miguuni mwa Sauli?.

Print this post

Kuseta ni nini?

Kuseta kama ilivyotumika kwenye maandiko maana yake ni kukiharibu kitu, aidha kwa kukiponda, kukikanyaga, au Kukivunja vipande vipande.

Kwamfano kwenye maandiko kama haya tunaweza kuona neno hilo..

Warumi 16:19-20

[19]Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.

[20]Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]

Hapa Mungu anaonyesha kwamba pale tunapokuwa mbali na mambo mabaya ndivyo anavyomponda shetani chini ya miguu yetu..

Kuonyesha kuwa njia kuu ya kumshinda shetani sio kumkemea bali ni kujitenga na mambo maovu.

Vifungu vingine ni kama hivi..

Zaburi 110:5

[5]Bwana yu mkono wako wa kuume;  Ataseta wafalme,  Siku ya ghadhabu yake.

Hapa Mungu anaonyesha ukali wa ghadhabu yake juu ya watu waovu..hata wale wanaoonekana ni wakuu, hawataikwepa hasira yake atawaharibu kwa kuwaponda- ponda.

kwa hitimisho ni kuwa kuseta ni kuharibu kabisa Kabisa ..Na Mungu amekusudia kufanya hivyo sio kwetu bali kwa shetani… Ni sisi tu kuishi maisha yanayomlingana yeye ikiwa tayari tumeshaokoka…Lakini ikiwa ni kinyume na hapo tutaingia katika mkondo huo huo wa shetani, wa kuharibiwa endapo hatutamwamini Yesu Kristo leo.

Je upo tayari kumpokea Yesu leo? Kama ni ndio basi bofya hapa >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWEKE SHETANI MBALI NA WEWE.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

DANIELI: Mlango wa 2

Print this post

SAFARI YA KUUONA USO WA MUNGU.

Musa (Mgongo)

Kristo (kioo)

Mbinguni (Dhahiri)


Ilikuwa ni shauku ya Musa kutaka Kuuona uso wa Mungu baada ya muda mrefu kukaa bila kumwona Mungu..

Lakini tukirudi kwenye maandiko yanasema, Mungu alizungumza na Musa uso kwa uso kama mtu anavyozungumza na rafiki yake.

Kutoka 33:11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.

Lakini iweje tena, aombe kuuona uso wa Mungu, na Mungu kumwambia huwezi kuuona uso wangu ukaishi?

Kutoka 33:20 Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.

21 Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;

22 kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa

mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;

23 nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana

Ukweli ni kwamba kuuona uso wa Mungu, sio kuona mwonekano Fulani, au umbo Fulani la Mungu. Hapana, bali ni kumjua yeye ndani ni nani.. Tangu zamani Mungu alikuwa akijifunua kwa wanadamu kupitia maumbile mbalimbali, ambayo yanaweza kuchukua taswira ya vitu, wanadamu au malaika(huitwa Theofania),. Hivyo kwa namna yoyote ile Mungu anapomtokea mtu kwa namna mojawapo ya hizo na kuisikia sauti yake kama vile mwanadamu mwenzako anavyozungumza na wewe, ni  sawa na kusema Mungu amesema nawe uso kwa uso. Lakini haimaanishi kuwa umeouna uso wake. Kuuona uso wake ni kumjua yeye ni nani.

Sasa Mungu akamwambia, Musa, huwezi kuniona ukaishi, Kwanini amwambie vile, Je! Mungu ni kifo? Hapana, Mungu ni uzima, lakini Musa alikuwa bado hajakamilika kwasababu ya dhambi, hivyo utukufu wa Mungu asingeweza kuustahimili, kwasababu wakati wa kuustahimili ulikuwa bado, kwani ulihitaji kwanza ondoleo la dhambi kabisa.

Hivyo Mungu akamwonyesha sehemu yake ya nyuma (Mgongo). Lakini Uso hakuuona.. Ndipo akamjua Mungu kwa sehemu yeye ni nani..

Alipomwona alishangaa sana, kwa zile tabia na sifa, Mungu alizokuwa nazo, jinsi zilivyo tofauti na mawazo ya wanadamu.. Pengine alijua ataona mafunuo makubwa ya nguvu na uweza, na mamlaka, ya ukuu, na utukufu usioelezeka kibinadamu, lakini alipomwona Mungu alimwona ni mwenye huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye hukumu za haki.

Kutoka 34:5-7

5 Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana.

6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si

mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;

7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba

zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.

Hata sasa, mtu anayemtambua Mungu kwa namna hii,  basi ameuona mgongo wa Mungu.. Na pale mtu anapoiga tabia hizo basi, amemkaribia Mungu sana.

Lakini safari ya kuuona Uso wa Mungu, ilikuwa bado haijakamilika..

Uso (Katika kioo)

Hivyo wakati ulipofika, Mungu akamtuma mwanawe duniani, (Yesu Kristo), kutuonyesha sasa uso wa Mungu ulivyo..Maandiko yanasema hivyo;

Yohana 1:18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.

Umeona kumbe, hakukuwahi kutokea mtu duniani aliyeuona uso wa Mungu, na moja ya kazi kubwa aliyokuja kuifanya Yesu duniani ni kumfunua Mungu(uso wake) ni nani?

Na kwasababu hakuna mtu mwenye dhambi anayeweza kumwona Mungu akaishi, ilimbidi yeye mwenyewe awe fidia ya dhambi zetu, kwa kufa kwake pale msalabani, ili sisi tuhesabiwe kuwa hatuna dhambi (kwa neema), na ndipo sasa tustahimili kuuona utukufu wa Uso wa Mungu.

Na alipotukamilisha kwa namna hiyo, basi, akatuwezesha pia kumkaribia Mungu tumwone.

Yesu akatufunulia uso wa Mungu, kuwa yeye ni UPENDO. Na upendo wake si ule wa kibinadamu, , kwamba nakupenda kwasababu umenipenda, au umenitendea jambo zuri.. Hapana, bali ni ule usio na sharti wa kuonyesha fadhili hata kwa wanautuchukia..

Musa, aliishia kujua huruma tu za Mungu  juu juu (kibinadamu), lakini hakujua kuwa hata jino kwa jino, ilikuwa ni makosa, kumwonea mwenzako hasira, au hata kumfolea ilikuwa ni makosa, yanayostahili hukumu,  talaka Mungu hapendezwi nazo.. Musa hakujua kuwa Mungu anataka tumwone yeye kama BABA, ambaye ni ‘ABA’ yaani Baba mwenye mahusiano ya karibu na mwanawe, kama ilivyokuwa kwa Yesu na Mungu,yeye alidhani Mungu ni wa kutoa tu amri, sheria na hukumu, Musa hakujua kuwa mwenye dhambi (mfano wa mzinzi, mwanamke mchawi) hapaswi kutupiwa mawe, bali kuhubiriwa injili ili atubu.. Yote hayo Yesu alikuja kutufunulia, kiufasaha kabisa wala hakutuficha chochote..

Kwa jinsi nyingine ni kuwa sisi tumemwona Mungu kupitia Kristo, na kwa kupitia uhalisia wa maisha yake. Tukiyaishi maneno ya Kristo, basi tumemjua Mungu uso wake, kiufasaha kabisa..

Lakini Safari bado inaendelea… Uso wa Mungu katika kilele chake, bado hatujaufikia…

Utauliza kwa namna gani?

Uso dhahiri (mbinguni)

Ni kwamba kwasasa tunaouona kwa njia ya KIOO, bado hatujauona kiuhalisia kabisa kwa macho, japo tunaweza kusema kuona kwenye kioo hakuna tofauti na kuona kabisa kwa macho, lakini ladha huwa zinatofautiana, kumwona Raisi kwenye Tv, ni Yule Yule utakayemwona kwa macho, lakini ladha ni tofauti..

Hivyo Kristo alikuwa kama chapa (kioo) ya Mungu yenyewe, duniani..Yaani sisi tayari tumemwona Mungu kupitia Kristo Yesu..

Waebrania 1:3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;

Ndio maana maandiko bado yanasema, kwasasa tunaona kwa kioo, lakini wakati ule tumjua sana yeye alivyo..

1Wakorintho 13:12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.

Wakati wa kuona dhahiri, wema wote wa Mungu, itakuwa ni mbinguni.

Tutamjua katika eneo gani?

Katika eneo lilelile la upendo, (sawasawa na ile 1Wakorintho 13 ilivyokuwa inaeleza habari hiyo tangu juu)

Hapo ndipo tutaufurahia upendo wa Mungu katika namna ambayo hatujawahi kuijua, kwa vile vitu tulivyoandaliwa na yeye mbinguni, milele…

Hivyo, hatuna budi sasa kutembea katika upendo wa Mungu kwasababu yeye ndio huo..

1Yohana 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Hitimisho:

Hatua za kuuona  Uso wa Mungu, zilianza, na Musa, (kwa mgongo), zikaja kwa Kristo (kwa kioo), na mwisho mbinguni, (dhahiri).

Je! Umempokea Kristo? Ikiwa bado, fahamu kuwa  huwezi kamwe kumwona Mungu, hata iweje, mpokee leo, akuoshe dhambi zako, kwasababu kumbuka pia alimwambia Musa, hatamwesabia mtu mwovu kuwa hana hatia, yaani kila mmoja atapewa anachostahili. Ukifa katika dhambi zako, hakuna upendo huko kuzimu,hutatolewa huko na kuletwa mbinguni.. kwasababu umechagua mwenyewe giza. Yesu alisema Jehanamu ya moto ipo, na mtu asipomwamini yeye, atakufa katika dhambi zake. Hivyo ndugu, Ingia ndani ya Yesu leo upokee neema, hujui ni lini utaondoka duniani, usiishi tu kama mnyama, tubu dhambi mkimbilie Yesu, akuponye.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

UFAHAMU UFUNGUO WA KUMPENDA BWANA ZAIDI

Print this post

Je tunajazwaje maarifa ya mapenzi yake? (Wakolosai 1:9)

Wakolosai 1:9

[9]Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;

JIBU:

Vifungu hivyo vinaonyesha kiu ya mtume Paulo juu ya watakatifu wa kanisa la Kolosai, Kwamba wajawe kuyajua mapenzi ya Mungu katika hekima yote na ufahamu wa rohoni.

Alijua ili kanisa liweze kumpendeza Mungu na kusimama ni lazima lijue mapenzi ya Mungu makamilifu.. Hivyo Ikawa shauku yake tangu zamani lijazwe kujua mapenzi hayo.

Mapenzi ya Mungu ni yapi?

Kuna makundi mawili (2), ya mapenzi ya Mungu.

1)Mapenzi Ya daima

2) Mapenzi Ya wakati

Mapenzi ya daima: Ni yale ambayo yapo wakati wote, na kwa wote kwamba kila mwamini lazima ayatimize..mfano wa haya ni..ni kama utakatifu (1Wathesalonike 4:3), kuhubiri Injili, kuishi kwa upendo, kukusanyika pamoja, kudumu katika maombi, kumwabudu Mungu.

Lakini mapenzi ya wakati: Ni yale ambayo Mungu anakusudia uyafanye katika kipindi fulani tu, ni mapenzi yasiyo na mfanano, au mwendelezo fulani.. Kwamfano Mungu anakutaka leo usihubiri, bali uende kumtembelea yatima mmoja kijijini. Mfano wa kama alivyoambiwa Filipo awaache makutano aende jangwani kwa ajili ya yule mtu mmoja mkushi.(matendo Matendo 8:26)

Au wakati mwingine unapitishwa katika jaribu fulani, halafu pasipo kujua kuwa hilo ni darasa la Mungu ili kutumiza kusudi fulani, unajikuta unakemea na kushindana nayo…Ndio maana Bwana Yesu alipoomba juu ya kuondolewa kikombe cha mateso, alimalizia kwa kusema Baba mapenzi yako yatimizwe.

Sasa yote haya yanahitaji hekima na maarifa kuyatambua na kuyatimiliza. Si rahisi kuyatambua kwa akili za kibinadamu au kuyatimiliza.

Lakini Swali linakuja mtu anawezaje kupata maarifa hayo ya mapenzi ya Mungu?

1) Kwa maombi.

Jambo la kwanza Paulo analitaja ni kuomba, aliwaombea watakatifu Wa Kolosai kwasababu alijua uwezekano wa kupokea Maarifa hayo upo katika maombi.

Yakobo 1:5

[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.

Maombi hufungua mlango wa Mungu kuyaingilia maisha yetu na kututia katika kusudi Lake kamilifu. Mungu anafanya kazi ndani yetu kupitia maombi…Bila uombaji haiwezekani kutembea ndani ya mapenzi yote ya Mungu.

2) Neno la Mungu.

Kwa kusoma Neno ndipo unapojua Tabia za Mungu, nini anataka na nini hataki. Sauti ya Mungu, maagizo ya Mungu ya moja kwa moja yasiyohitaji usaidizi ni biblia takatifu.

Zaburi 119:105

[105]Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Mtu ajijengeaye tabia ya kusoma biblia, si rahisi kuanguka au kutoka nje ya mpango wa Mungu. Kwasababu lile neno linakaa ndani yake kama mafuta kumfundisha.

3) Mashauri Ya kikristo.

Bwana anafunua mapenzi yake tuwapo katika mabaraza yetu kutafakari maneno yake.. alisema wawili watatu kwa jina lake yupo hapo hapo katikati yao…Wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau, tunaona walikuwa zaidi ya mmoja, ndipo wakiwa katika kutafakari habari za Kristo, Aliungana nao bila hata wao kujua akaanza kuwafundisha, na mwisho wote kujua mapenzi makamilifu ya Mungu ni nini..(Luka 24)

Na ndio maana hatupaswi kulikwepa kanisa kwasababu huko tunaungana na viungo vingi katika Mwili wa Kristo, na hivyo kujengana na kuonyana. Hatimaye mapenzi ya Mungu yanafunuliwa kwetu.

Hata wakati ule kulipotokea sintofahamu ndani ya kanisa kuhusu vyakula na sheria..baraza lilikalishwa kule Yerusalemu kisha mahojiana mengi yakaendelea …lakini mwishoni Mungu alitoa maarifa kwa kusema wajiepushe.na damu na uasherati lakini sio mataifa watwikwe tena kongwa la torati lililowashinda wao.(Matendo 15 )

Hivyo ni vema kumshirikisha pia mpendwa mwenzako/ kanisa mpango wako, yapo mashauri ya ki-Mungu ndani yao yaliyojaa hekima yatakusaidia.

4) Upambanuzi wa kiroho

Huu ni uwezo wa Mungu ambao mtu humwingia kutokana na kiwango chake cha juu cha ukuaji wa kiroho (Waebrania 5:14).. Bila kutegemea kuomba au kumuuliza Mungu mtu hutambua lililo la kweli na lililo la uongo.. lililosahihi na lisilosahihi, la rohoni au la mwilini, lenye Mwongozo wa ki- Mungu au kibinadamu. Tunaweza kujua mapenzi ya Mungu kwa ujuzi huu, unaozalika kutokana na ukomavu wetu wa kiroho.

Hitimisho:

Hivyo wewe kama mwana wa Mungu, kumbuka ni sharti kutembea ndani ya mapenzi yake…madhara ya kutembea nje ya hayo ndio kama yale aliyoyasema Bwana kwenye Mathayo Mathayo 7:21..

[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baraka ni nini na kuna aina ngapi za baraka?.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

Print this post

Biblia inaposema upanga wa mmoja ukawa kinyume na mwenzake inamaana gani? (Ezekieli 38:21)

SWALI: Je ni kitu gani hasaa kilikuwa kinatokea mpaka wafikie hatua kama ile, je! Ni utahira ulikuwa unawapata au ni nini hasaa?


JIBU: Silaha mojawapo ambayo tuona Mungu alikuwa akiitumia kuwashindania watu wake mara myingi wawapo vitani, Ni hii ya “machafuko” yaani Ni kuwavuraga maadui washindwe kuelewana na hatimaye kuanza kushambuliana wao kwa wao.

Kwamfano wa matukio kama hayo tunaweza kuyathibitisha katika habari hizi;

Wana wa Israeli Walipoizunguka Yeriko.

Waamuzi 7:22

[22]Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye BWANA akaufanya upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na Tabathi.

Sasa tuone ni njia zipi alikuwa anazitumia Mungu mpaka wauane wao kwa wao, watu ambao walikuwa wamekubaliana kabisa kwenda vitani?

1). Bumbuazi

Hii ni hali ya kutoweza fikiri vema, kuwa kama mtu fulani nusu aliyerukwa na akili.

Kumbukumbu la Torati 28:28

[28]BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;

Hii ni hali yakutokuwa sawa katika ufahamu, unamwona mwenzako kuwa ndiye adui, na hatimaye vita vinaanza kabla hata ya maadui wenyewe kufika..hili ndio yamkini Bwana alilowapiga watu wa Yeriko.

Kama tu vile Mungu alivyowapiga upofu watu wa Sodoma na Gomora wasione mlango wa Lutu, vivyo hivyo hawa wanapigwa katika eneo la fikra wasifiri vema wauane, wao kwa wao.

2) Kutofautiana kauli.

Hii ni namna ambayo mnapisha usemi. Kiasi kwamba hakuna mtu wa kumsikiliza mwenzake, huyu anataka hili, Yule hili, kila mmoja haafikiani na mwenzake hatimaye chuki inatokea, matengano na mwisho kuanza kupigana wao kwa wao.

Watu wa Babeli walipigwa ‘usemi’ isipokuwa tu wao hawakufikia hatua ya kuuana, lakini ni namna tu hii hii .(Mwanzo 10)

3) Shuku na visasi

Hii ni hali ya kuwashuku wenzako kuwa ni wasaliti, hivyo ghafla kupoteza imani nao, na kuanzisha vita ili kujilinda…mfano wa hili tunaliona kwenye ile vita ya Yuda na majeshi ya wamoabu, waamoni na wameuni walipokutanika kupigana na taifa la Mungu..ghafla moabu Na amoni wakaipiga Seiri, halafu baadaye wakarudiana Wao kwa wao.

2 Mambo ya Nyakati 20:22-23

[22]Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.

[23]Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.

Hii ya visasi inatokeaje?

Labda mmoja alikuwa na chuki na mwenzake, hivyo unamlipizia kisasi, na huyu naye kaona ndugu yake kauliwa anaamka kumtetea, mara kabila hili na hili hatimaye taifa zima linaiingia katika kujiharibu.

Hivyo Mungu anapotaka kutupigania, silaha hii huwa anaitumia hata katika agano jipya hususani hapo kwenye kugonganisha ndimi.

Kwamfano mtume Paulo alipokamatwa awekwe barazani ili ahukumiwe…kwa hekima ya Roho alipewa kujua kuwa katikati ya baraza wapo mafarisayo na masadukayo. Hivyo alilolifanya ni kuwachonganisha ndimi, badala ya kumshambulia yeye..wakaanza kushambuliana wao kwa wao…hiyo ni silaha ya Bwana ambayo kwa hekima ya Roho aliitamka..

Matendo ya Mitume 23:6-7

[6]Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.

[7]Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.

Ni vema kufahamu aina hii ya silaha ni mbaya kuliko ile ya kushindana na adui yako.

Lakini ni vema kufahamu kuwa hata shetani hutumia silaha hii, pale tunapotoka nje ya mpango wa Mungu.

Israeli iliingia kwenye vita vya wao kwa wao, na kupelekea mauaji mengi sana…

Ni nini kilitokea?

Baadhi ya wana wa Benyamini waliendekeza dhambi ya uasherati mpaka ikafikia hatua inayokaribia ile ya sodoma Na Gomora na Israeli yote ilipopata taarifa, wakataka wawatoe hao watu wauliwe, lakini wabenyamini wakawaficha kwasababu ni watu wa kabila lao. Machafuko yakaanzia hapo, hatimaye wakauana Sana. (Waamuzi 19-21)

Hata sasa silaha hii shetani hupenda kuirusha kwenye kanisa la Mungu, watu wapoteze upendo na utakatifu ili waanze kulana na kung’atana..kwasababu ya wivu, visasi na vinyongo.

Wagalatia 5:14-15

[14]Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.

[15]Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.

Lazima tuijue hila hii ya shetani na kukataa kuipa nafasi.. Na Bwana atatuhifadhi, na matokeo itakuwa ni yeye kuleta machafuko kwa maadui zetu wanaposimama Kinyume na sisi.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

Print this post