Title 2019

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.

Ipo dhambi ya Mauti, Hiyo mtu aliye mkristo akiitenda kama Bado Neema ya Mungu ipo juu yake, atakufa lakini ataokolewa siku ya kiyama. Mfano Musa!, alimkosea Mungu, akasamehewa kosa lile lakini adhabu ya kifo haikuondolewa juu yake, Bwana alimwambia kwa kosa lile hataiona nchi ya ahadi na kufa atakufa…lakini baada ya kufa, alikwenda mahali pa watakatifu.Ndio maana utamwona akitokea tena na kuzungumza na Bwana Yesu, yeye pamoja na Eliya katika ule mlima Mrefu.

(Mathayo 17:1-9), Sasa hiyo ni dhambi ya mauti ambayo, unaadhibiwa mwili ili roho ipone (1 Wakoritho 5:5)..Kwa maelezo marefu juu ya dhambi hii ya Mauti, utaipata mwisho kabisa wa somo hili.

Lakini ipo dhambi ya isiyo na msamaha kabisa hapa duniani wala huko katika dunia inayokuja…Hiyo ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Dhambi hii watu wanaitenda na kadhalika mtu asipoielewa dhambi hii ni rahisi kupelekeshwa na shetani sana…Kwasababu shetani anamjua mwanadamu sana kwa miaka mingi, tangu Edeni, hivyo mojawapo ya njia anazotumia kumkandamiza mwanadamu asiye na ufahamu wa kutosha ni kumletea mawazo kwamba ana dhambi isiyosameheka mbele za Mungu, Tutakuja kuona hapo mbeleni kidogo, namna ya kukabiliana na hilo jaribu Kongwe la shetani!

Lakini sasa hebu tujifunze ni namna gani mtu anamkufuru Roho Mtakatifu.

Biblia inasema katika 

Mathayo 12:31 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa.

32 Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao”.

Hapo Neno limewekwa moja kwa moja kuwa yeye atakayenena Neno juu ya Roho Mtakatifu na wala si mwana wa Adamu, haimaanishi kuwa Kuna Miungu watatu, hapana! Mungu ni mmoja tu…Ila Roho Mtakatifu ni Utendaji kazi wa Bwana Yesu Kristo mwenyewe katika mfumo wa Roho, kwasababu Roho Mtakatifu ndiye roho wa Yesu mwenyewe (Matendo 16:7) ndio maana ilimpasa yeye aondoke kwanza katika mwili ili arudi tena katika roho ( soma Yohana 16:16), kwasababu mtu anayefanya kazi katika roho, anakuwa na matunda Zaidi kuliko anayefanya kazi katika mwili, mchawi anayekwenda mahali katika roho anauwezo wa kuathiri kikundi kikubwa cha watu kuliko angekuwa mahali pale katika mwili…Kwahiyo utendaji kazi wa Roho Mtakatifu ndio utendaji kazi wa Mungu, ulio karibu Zaidi na wenye matunda Zaidi kuliko Mungu alivyokuwa katika mwili…ndio maana kuna hatari kubwa sana ukimkufuru….kwasababu nguvu ya kumshawishi mtu kuja kwa Mungu inatokana na Roho Mtakatifu.

Sasa endapo mtu ambaye hajawa mkristo kabisa, na ndani ya moyo wake anasikia kabisa kuna kitu kinamshuhudia kuwa Yesu ndiye njia, na kinampa uthibitisho wa kila aina kuwa hakuna njia nyingine nje ya Yesu Kristo, huyo ni Roho Mtakatifu ndani ya huyo mtu anayemlilia ageuke atubu na kumwamini Yesu, lakini mtu huyo pamoja na msukumo wote huo wa kiMungu ndani yake, na wenye kila aina ya uthibitisho, akaamua kwa idhini yake mwenyewe kuikataa na kutamka maneno ya kufuru wazi kwa kinywa chake dhidi ya ule ushawishi au dhidi ya mtu anayemletea injili ile, Roho Mtakatifu ndani yake anaondoka milele, kamwe mtu huyo hataisikia tena ile sauti ikimshawishi kuwa Yesu ni njia. Kamwe hatasikia tena kitu kikimvuta kutubu, atabakia kupinga injili Maisha yake yote…Hapo Mtu huyo anakuwa na dhambi ya Milele (amemkufuru Roho Mtakatifu)…haiwezekani tena yeye kutubu!…Kumbuka sio kwamba itafika kipindi atatamani kutubu na Mungu amkatae! Hapana! Hatasikia sababu wala hamu ya kutubu mpaka anakufa!..kwasababu anayeleta moyo wa Toba ndani ya mtu ni Roho Mtakatifu mwenyewe, kama mtu anahukumiwa dhambi zake na kutamani kutubu ina maana bado Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yake, lakini asiyetaka kabisa kutubu ni wazi kuwa Roho Mtakatibu hayupo kabisa juu ya Maisha yake.

Kadhalika kama mtu tayari ni Mkristo, na ameshawishika kabisa kumfuata Kristo, na kuonja mema yote na vipawa vyote vya kiMungu na kutambua kabisa ya kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zake na ameshajua utendaji kazi wa Roho Mtakatifu upoje, na kuamua kugeuka kuacha wokovu, na kugeukia shetani moja kwa moja, na kunena maneno ya kufuru dhidi ya Roho Mtakatifu au dhidi ya mtu anayehubiria wengine Injili ya wokovu kwa uweza wa Roho, hapo mtu huyo Roho Mtakatifu anaondoka moja kwa moja juu yake, na harudi tena! Kamwe moyoni ile sauti iliyokuwa inamhukumu atendapo mabaya au iliyokuwa inamwongoza inakuwa haipo tena, huko alikokwenda ndio anakuwa wa huko huko moja kwa moja….hawezi wala hatakuwa na hana hamu ya kutubu tena, wala hatasikia kuupenda wokovu tena, kwasababu anayetupa sisi hamu ya kuendelea kuupenda wokovu ni Roho Mtakatifu.

Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7 Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;

8 bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.”

Sasa kuna kitu kinaitwa kurudi nyuma, au kupoa! Hii inatokea pale, mkristo alikuwa moto sana, alikuwa anaomba na kusali lakini kapunguza kufanya hivyo, alikuwa anafanya kitu Fulani cha kiMungu lakini kakipunguza, alikuwa anahubiria wengine lakini kapunguza, …Kumbuka anakuwana anapoa sio anakuwa baridi!, Mtu anayekuwa baridi maana yake ametoka kwenye wokovu kabisa! Hivyo ni ngumu kurudi tena, yupo hatiani kupata dhambi ya mauti au dhambi isiyosameheka..Lakini aliyerudi nyuma, maana yake anaweza kurudi pale alipokuwepo akitubu na ndani yake, bado kuna kitu kinachomshuhudia kuwa anahitaji kumgeukia Mungu, na hofu ya kwenda kwenye ziwa la moto sasa huyo ni Roho Mtakatifu bado anafanya kazi ndani yake.

Lakini sasa, shetani akishajua kuwa mtu karudi nyuma, jambo la kwanza analokwenda kulifanya ni kwenda kumwekea ukingo asirudi alipokuwepo, na hiyo anaifanya kwa kumletea sauti inayomwambia UNA DHAMBI ISIYOSAMEHEKA! Au UMEMKUFURU TAYARI ROHO MTAKATIFU.

Mwamini yule akisikia sauti ile ndani yake ikimwambia vile basi anavunjika moyo, na kuingia kwenye dimbwi kubwa la mawazo yasiyoisha. Hata hamu ya kuendelea mbele yote inaisha!..Sasa mtu wa namna hiyo hajamkufuru Roho Mtakatifu kwasababu bado anahitaji kurudi kwa Mungu, bado anataka kutubu, hiyo hamu au hitaji la kutubu linaletwa na Roho Mtakatifu, hivyo Roho Mtakatifu bado hajaondoka juu yake, ingawa shetani atamletea mawazo ya kwamba ana dhambi ya milele. 

Kwamfano kuna mtu mmoja mwenye tatizo kama hilo alinitumia ujumbe inbox, akiwa na mashaka hayo na hajui afanyaje…Hebu fuatilia kidogo mazungumzo haya…

Shalom! swali langu ni kwamba je mtu akiokoka halafu akakengeuka ila akarudi tena kuomba toba madhabahuni, je mtu huyu anakuwa kasamehewa au atakuwa hajasamehewa? na jina lake litaendelea kuwepo kwenye kitabu cha uzima?

Nikamjibu swali hilo, nikamtumia na somo linalohusu swali hilo…na kisha akaendelea kuniambia…

“Asante sana Mtumishi wa Mungu…Yani mimi nimeokoka sasa kuna kipindi nikaanguka nikazaa kabla ya ndoa halafu pindi naishi na mwanaume wangu nlikuwa nashika mimba mwenzangu ananiambia nitoe nami nilikuwa nikifanya hivyo lakini badae nikaona amani ikawa inaisha kila kukicha kwa kitendo nlichofanya nikaamua kwenda kwa mchungaji nikamwelezea akanikemea na akanitenga kihuduma kwa muda na akanambia nisirudie tena kutenda dhambi Mungu ataniacha vibaya sana sasa wakati nahudhuria ibada kanisani kuna mpendwa akauliza nililokuuliza mchungaji akajibu akasema mtu huyu hasamehewi tena basi tu tunaendelea kufarijiana ila hakuna msamaha tena hapo basi toka siku hiyo mimi linaniumiza sana neno hilo sijui nifanyeje ili niweze kurudisha amani yangu katika kumwabudu Mungu”.

Baada ya kunitumia ujumbe huo, nikamwambia ni sahihi kabisa alichofanya mchungaji wako kukutenga kwasababu umestahili kutengwa kulingana na maandiko kwa kitendo ulichokifanya, (1 Wakorintho 5:9-13)..Na alikujibu pia sawa, kwamba usirudie tena kufanya hivyo akimaanisha ukatubu!…lakini siku nyingine alipojibu swali kama hilo kwa mwingine akasema mtu kama huyo hana msamaha,….Nikamwambia mchungaji wako sijui Ni kwanini alimjibu vile huyo mtu wa pili lakini naamini hakumjibu huyo mtu wa pili kwa kulinganisha na tatizo ulilonalo wewe, yeye alimjibu yule pengine akimaanisha mtu aliyeacha kabisa wokovu na kukengeuka na kuiacha njia ya msalaba, na kukufuru huyo ndiye mtu ambaye Roho Mtakatifu anaondoka ndani yake kabisa kabisa!…na hatuwezi kumfariji kwasababu hata hatatamani kufarijiwa wala kutamani kanisa..ataendelea kudanganyika na kutamani mambo maovu…

2 Timotheo 3: 13 “lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika”..

lakini sio wewe! Wewe bado kuna nguvu ya kutaka kutubu ipo ndani yako, kitu fulani kinachokusukuma kumrudia Mungu, ambacho ni Roho Mtakatifu…

Sasa hicho kitu cha kumsukuma kutubu endapo kisingekuwepo ndani ya huyu dada, na akawa anafurahia kuendelea na tabia hiyo, hapo ndio angekuwa pengine na hiyo dhambi isiyosameheka…kwasababu Roho Mtakatifu anayehusika katika kumvuta kutubu hayupo…(Yohana 6:44).

Tatizo hili limekuwa ni la watu wengi, hususani waliofanya dhambi za mauaji, ubakaji na utoaji mimba, mizaha iliyopitiliza katika madhabahu za Mungu…Unakuta mtu aliitenda dhambi hii sasa kasikia sauti ndani ikimshawishi kutubu lakini akikumbuka kwamba alishaua kuna kitu kinamwambia huwezi kusamehewa, hivyo anavunjika moyo moja kwa moja, mwingine alitoa mimba kadhaa, mwingine alifanya kitendo kibaya kiasi kwamba hawezi kukisema hata mbele za watu…Sasa mawazo kama hayo yanapokujia, wakati unapotaka kumgeukia Mungu, unapaswa UYAKATAE! Kwa nguvu na kuendelea kusonga mbele, kwasababu ni mawazo ya shetani!

Na pia jiepushe na kutenda dhambi hizo kwasababu madhara yake ndio kama hayo ya kuletewa mawazo ya mkandamizo kutoka kwa shetani!, usipotenda mambo hayo, shetani hawezi kukupata kwa mawazo yake. Na pia dhambi hizo ukizitenda baada ya kuamini, na kumkataa kabisa Roho Mtakatifu. kuna uwezekano mkubwa wa Roho Mtakatifu kuondoka kabisa ndani yake..usisikie tena hamu ya kumpenda Mungu na hivyo kuishia kuipinga injili na wokovu milele.

Bwana akubariki.

Maran atha!. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


DHAMBI YA MAUTI

DHAMBI ZINAZOTANGULIA HUKUMUNI NA ZINAZOFUATA

DHAMBI YA ULIMWENGU

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI?


Nyumbani

Print this post

MIISHO YA ZAMANI.


1Wakorintho10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.”

Shalom ndugu, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe milele. Nakukaribisha tuyatafakari kwa pamoja maneno ya uzima, maadamu rehema zake ni mpya kila siku asubuhi(Maombolezo 3:22-23). Leo tutajifunza hii miisho ya zamani inayozungumziwa kwenye mistari hiyo ni ipi na tutaitambuaje kama tumeifikia au kuikaribia..

Kama ukisoma mistari kadhaa ya juu kabla ya huo, utaona kuwa biblia imeandika mambo maovu na makosa waliyoyafanya wana wa Israeli walipokuwa kule jangwani mpaka ikawapelekea wengi wao wa waliotoka Misri kutokuiona nchi ya Ahadi Mungu aliyowaahidia, kama tunavyofahamu ni watu 2 tu kati ya mamilioni waliotoka Misri ndio walioiona nchi ya ahadi, na mambo yaliyotajwa hapo kuwa yaliwakosesha ni pamoja na ibada za sanamu, uasherati, manung’uniko, na kumjaribu Mungu.

Lakini mfano Mungu angeyaacha tu hivyo hivyo bila kuyaandika kwa ajili ya vizazi vya mbeleni, ni wazi kuwa na sisi pia tungeyarudia yale yale na hiyo ingetupelekea watu wachache sana kuirithi mbingu mfano wa Yoshua na Kalebu.. Lakini Mungu aliyaandika sio tu kwa vizazi vya mbeleni bali pia kwa vile vya mbali zaidi vitakavyofikiwa na miisho ya zamani.

Neno “Miisho ya zamani”, kwa lugha rahisi ni sawa na kusema mwishoni wa nyakati, au majira,..Au ni sawa na kusema pia utimilifu wa nyakati…..au kilele/ukingoni mwa nyakati….Sasa ukisikia mahali popote katika biblia inasema tunaishi katika siku za mwisho,/wakati mwa mwisho , Huo wakati kibiblia haujaanza leo wala jana bali ulianza rasmi takribani miaka 2000 iliyopita,..

1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho.”

Na Mambo hayo kwa mara ya kwanza yalianza kuhubiriwa na Yohana Mbatizaji pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo wakisema, TUBUNI kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia…Kwasababu walijua tayari wameshaingia katika majira ya siku za mwisho.

Lakini swali unaweza ukajiuliza kama ni hivyo, kwanini basi Bwana Yesu akiwa katika mlima wa Mizeituni alianza kuwaeleza tena dalili za siku za mwisho ikiwa tayari anafahamu kuwa yupo katika siku za mwisho, dalili nyingine za nini tena?

Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa Bwana Yesu alikuwa hazungumzii habari za SIKU za mwisho kwani tayari wakati ule ilishajulikana kuwa zile ni siku za mwisho…Bali alikuwa anazungumzia habari ya SIKU ya mwisho jinsi itakavyokuwa…dalili zitakazoonesha kuwa ule mwisho wa yote utavyokuja ..

Ni sawa tu na kusema mwaka 2020 ni mwaka wa uchaguzi, lakini uchaguzi wenyewe utafanyika mwezi wa 10, hivyo kwa namna ya kawaida mwaka wa uchaguzi unapoanza, kunakuwa na vuguvugu la kampeni, vyama vinajiweka tayari, vinaanza kufanya kampeni za nyuma ya mgongo, dalili ndogo ndogo zitaonekana kwa tabia zao, sera zao n.k. lakini kampeni rasmi hazijafunguliwa bado.. hivyo ule wakati ukifika miezi 2 kabla ya uchaguzi wenyewe kufika, ndipo Kampeni rasmi zinafunguliwa na hapo ndipo utaona mambo yanavyofanyika kwa kasi na kwa nguvu ambazo hujawahi kuziona ni kwasababu wanajua muda waliopewa na waliobakiwa nao ni mchache sana kabla ya siku yenyewe kufika..

Na ndivyo Bwana Yesu alivyokuwa anafanya, ni kueleza dalili rasmi za kukaribia kwa “siku” ile ya mwisho na sio kukaribia kwa “siku za mwisho”…akasema mtakapoona wimbi kubwa na manabii wa uongo limejitokeza, wanafanya kampeni ili kukusanya magugu matita matita basi mjue ule mwisho ule umekaribia….hayo mambo hayakuwahi kuonekana katika wakati wowote katika historia tangu kipindi cha mitume hadi kizazi hichi cha karne ya 21, kutokea kwa wimbi kubwa la manabii wa uongo namna hii, yaani kuanzia mwaka 2005 kupanda juu mambo haya ndio yameanza kujitokeza kwa kasi….hii inaonyesha kuwa tunaishi ukiongoni kabisa mwa wakati,.. kipindi cha utimilifu wa wakati.

Alisema watakuja wengi kwa jina langu wakisema mimi ni Kristo,.yote hayo tunayaona kila kukicha.. Hizi ni dalili za kukaribia kwa siku ile kuu ya kuitisha,

Alisema kutaongeza maasi, na upendo wa wengi kupoa,..Leo hii tunaona jinsi teknolojia ya simu na mitandao jinsi ilivyoleta maovu karibu na watu kuliko kipindi chochote cha nyuma, ndani ya simu ndogo tu mtu anaweza akapata mambo yote maovu yanayoendelea ulimwenguni kote, mpaka watoto wadogo sasa hauna jambo lolote la siri kwao. Mambo hayo yameanza kukolea kuanzia kipindi cha mwaka 2005 kupanda juu wala hata sio siku nyingi….Ulimwengu umeshajua kuwa siku zake zimebaki chache hivyo unafanya kampeni kwa nguvu kuielekea ile siku yake kuu ya kuangamizwa.

Na dalili nyingine kubwa Bwana Yesu aliyoizungumzia katika (Mathayo 24:32)ni kuchipuka kwa “mtini” ambao huo unawakilisha taifa la Israeli..Alisema jambo hilo likishaanza kuonekana basi tujue kuwa kizazi hicho hakitapita mpaka hayo yote yatakapotimia…

Kwa upana wa somo hili bofya link hili la kuchipuka kwa Israeli bofya hapa ⏩ Amin! Amin! nawaambia.

Hivyo unaweza kuona hapo kuwa sisi ndio watu tuliofikiliwa na miisho ya zamani.. ndio watu ambao sio tu tunaishi katika siku za mwisho, bali pia ni watu tunaoishi katika ukingo kabisa wa siku hizo…

Je! Bado mambo ya ulimwengu yanakusonga?. Bado upo njia panda? Bado unazini na mke ambaye si wako au mume ambaye si wako?, bado ni mlevi, bado ni mfanyaji mustarbation, bado ni mtazamaji pornography? Bado ni mfanyaji anasa?,bado ni mtoaji mimba, bado mla rushwa? bado tu upo buzy huna muda na injili za wokovu?… Hizi ni nyakati mbaya..Kama bado upo nje ya Kristo jitahidi uingie kabla mlango haujafungwa.

Anasema..

“20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.”(Ufunuo 3:20-22)

Shalomsana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE


Rudi Nyumbani

Print this post

MATUMIZI YA DIVAI.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu

Kama inavyojulikana na wote kuwa Divai ina kilevi…Lakini swali linakuja kama ina kilevi kwanini Bwana Yesu aligeuza maji kuwa Divai, na kwanini Divai ilitumika katika kushiriki?..hata wakati wa kanisa la kwanza, ilitumika katika kushiriki meza ya Bwana?..Na je! Mpaka leo ni sahihi kuitumia kwa kushiriki?

Divai ni kinywaji ambacho kilikuwa na matumizi mengi zamani, Kwamfano Divai iliweza kutumika kama dawa…Ndio maana Mtume Paulo, alimwambia Timotheo asitumie maji peke yake bali atumie mvinyo…

1 Timotheo 5:23 “Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara”..

Unaona hapo? Aliambiwa atumie kwa ajili ya magonjwa yanayompata mara kwa mara, kumbuka Wakati ule, Mitume walisafiri umbali mrefu wakati mwingine wakiwa wamefunga kwenda kuhubiri injili, hivyo ile hali ya kukaa na njaa muda mrefu, utumbo ulikuwa unajisokota, kwahiyo suluhisho la hayo, ilikuwa mtu anakunywa kiasi kidogo cha Divai na ndipo ale chakula kingine…Zingatia hilo Neno ‘kidogo’…biblia inasema hapo kidogo sio sana!..ikiwa na maana kuwa ni kiwango ambacho hakiwezi kuleta madhara ya nje kama kulewa. Ingesema kunywa mvinyo wa kutosha kwa ajili ya tumbo, tungeelewa kuwa maandiko yamehalalisha ulevi. Na pia zingatia dhumuni la kunywa divai hapo sio kulewa, au kujiburudisha, au hamu…hapana! Bali kwaajili ya tumbo, ikiwa na maana kuwa kama afya yake itakuwa vizuri hana sababu ya kuinywa hata kidogo!!

Kadhalika Divai hiyo hiyo haikutumika tu kwa ajili ya matibabu ya magonjwa au madhaifu ya Tumbo, bali pia ilitumika kwa matibabu ya nje! Kama kutibu vidonda n.k..Tunaona jambo hilo katika ule mfano Bwana Yesu alioutuoa wa Msamaria mwema…

Luka 10:30 “Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia MAFUTA NA DIVAI; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.

Umeona hapo?..alimpaka Mafuta na kutia Divai katika majeraha ya yule mtu. Ikionesha kuwa Divai ilikuwa na kazi pia ya kutibu vidonda!..

Sasa tukirudi katika nyakati zetu, tuna dawa zinazotibu vidonda, hatuwezi kutumia tena divai…ingawa sio dhambi wala kosa kuitumia, lakini zipo dawa zinazofanya kazi nzuri Zaidi ya divai, kwamfano kuna dawa inayoitwa SPIRIT wengi wetu tunaijua, dawa hii ni maalumu kwa kusafishia vidonda na kuua vijidudu visivyoonekana kwa macho, dawa hii inakiwango kikubwa sana cha KILEVI kuliko hata DIVAI….kilevi kilichopo ndani ya dawa hiyo ambayo wengi wetu tunaitumia pasipo kufahamu, ni kiwango kikubwa kiasi kwamba mtu akiinywa kwa bahati mbaya anayo hatari ya kuwa kipofu…Hakuna pombe yoyote duniani inayonywewa na mwanadamu yenye kiwango cha kilevi kikubwa kama hicho kilichopo kwenye Spirit.

Kadhalika, zipo pia dawa zinazotumika na wengi zenye kiwango cha kilevi ndani yake, Kwamfano kuna dawa ya kuongeza vitamin kwa kwa Watoto na watu wazima, inayoitwa SSS TONIC Dawa hii ina kiwango cha kilevi asilimia 12, kiasi kwamba mtu anayeitumia akinywa nyingi pamoja na madhara mengine atakayopata lakini pia atalewa!..ndio maana inatumika kwa kiwango kidogo sana kilichothibitishwa na madaktari kwamba hakitaweza kuleta madhara, wala kumlewesha mtu, kijiko kimoja au viwili vya chai, inatosha….sasa kwa njia hiyo iyo ndio Mtume Paulo alimshauri Timotheo atumie Mvinyo (Divai) kidogo kwa ajili ya tumbo..

Pia zipo dawa nyingi za kutuliza maumivu zimetengenezwa na kiwango fulani cha kilevi, ambazo mtu akinywa analewa… na kuna dawa za kuoshea midomo zenye kiwango cha kilevi ndani yake…

Kadhalika dawa nyingi za maji maji zinazotumika kutibu matatizo ya kifua na kukohoa, zimetengenezwa kwa kiwango Fulani cha kilevi ndani yake, kwamfano dawa kama expectorant, Chlorintmeton n.k hizi ni dawa za kifua za chupa zina kiwango cha kilevi ndani yake… kilevi hicho kimewekwa ndani yake kusaidia kuihifadhi dawa hiyo ikae kwa muda mrefu…Hivyo kwa namna moja au nyingine, watu wote wameshakunywa au kutumia kilevi pasipo kujijua kwa malengo mbali mbali kama tiba ya ndani au ya nje…lakini si kwa lengo la kulewa, wala kujiburudisha..

Sasa Divai hiyo zamani ilitumika katika kushiriki meza ya Bwana, na si kwa kulewa.. ambayo inawakilisha damu ya Yesu Kristo, na wakristo wa kanisa la kwanza walikuwa wanaitumia kwa kiasi kidogo sana katika kushiriki meza ya Bwana, na si kwa kulewa…kama tu vile mtu anayetumia mojawapo ya dawa hizo hapo juu kwa kiwango kidogo sana cha tiba, na kisiwe na madhara ya kumlewesha…Kadhalika na katika meza ya Bwana Divai ilikuwa inatumika kwa kiwango kidogo sana, kisichoweza kumfanya mtu alewe kabisa, mtu alikuwa anakunywa kiwango kidogo sana hata robo glasi inaweza isifike, kama ishara tu ya kushiriki DAMU YA YESU…Ingawa walikuwepo watu wachache waliokuwa wanakunywa kwa kiwango kikubwa mpaka kulewa! Hao ni wale ambao walikuwa ni walafi na walevi ambao… hawawezi kuupambanua vyema Mwili wa Kristo na Damu yake, na Mtume Paulo aliwakeme vikali na kuwaonya….kasome (1Wakorintho 11:21-34).

Kwahiyo Divai kama wakristo wa kanisa la kwanza walivyoitumia kwa lengo la kushiriki, na sisi tutafanya kama wao, kwa lengo hilo hilo,tunaitumia katika kushiriki meza ya Bwana katika kiwango kidogo sana kitakachotufanya tusilewe kama wao walivyofanya…na hatunywi divai hiyo kwa hamu, wala kwa kiu, wala kwa kujiburudisha, wala hatuitumii kwa matumizi mengine yoyote ya tamaa wala ulafi..tunatumia kama ishara ya Damu ya Yesu isiyoharibika, kama Damu ya Yesu yenye matumizi mengi, kutibu mambo yote ya rohoni na mwilini, ndivyo ilivyo divai.

Kinachotokea kwenye baadhi ya makanisa yasiyokuwa ya kiroho yanatumia mistari hii ya Biblia kuhalalisha unywaji wa pombe, hivyo mtu yeyote akijisikia tu hamu, au haja ana kwenda kunywa pasipo sababu yoyote, na kulewa kwasababu Mtume Paulo kasema..’usitumie maji peke yake bali mvinyo pia’…Ndugu hiyo sio kazi ya divai kwa Mkristo, na pia pombe nyingine zozote hazijatengenezwa kwa lengo la matibabu, pombe kama hizi zinazouzwa madukani, zimetengenezwa kwa lengo la mtu kulewa, na ulafi, na kujifurahisha, hazijashauriwa hata na daktari yoyote zitumike, na wala hakuna daktari yoyote anayemshauri mtu akanywe pombe…kwahiyo ulevi wa aina yoyote ule ni dhambi…Hakuna mkristo yeyote katika agano jipya aliyelewa kwa pombe hakuna! Na wala maandiko hayajahalalisha ulevi..(Kwa maelezo marefu juu ya ULEVI, Tutumie ujumbe inbox tutakutumia somo hilo).

Vile vile kuna watu wanaotumia juisi ya mzabibu katika kushiriki, lakini ukweli ni kwamba hakuna maandiko yoyote yanayoonyesha kilichokuwa kinatumika ni pombe, bali ni Divai kama divai yenye kilevi ndio iliyokuwa inatumika.

Bwana akubariki sana.

Maran atha! .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JE! ULEVI NI DHAMBI?

MABALASI VILIKUWA NI VYOMBO VYA KUWEKEA NINI?

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU


Rudi Nyumbani

Print this post

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.

Mathayo 26:39 “Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.

40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?

41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU”.

Sentensi hiyo … ‘Roho ipo tayari lakini Mwili ni dhaifu’… inamaanisha kuwa Tunapotaka kufanya kitu chochote cha KiMungu…roho zetu zipo tayari kufanya jambo hilo, lakini miili yetu haipo tayari…

Katika habari hiyo hapo juu tunasoma, Baada ya Bwana Yesu kuzunguka mchana kutwa pamoja na wanafunzi wake kuifanya kazi, jioni ilipofika hawakupata muda wa kupumzika badala yake walikwenda moja kwa moja kwenye nyumba moja ambayo waliandaliwa wakae, wakiwa humo Bwana aliendelea kuzungumza na wanafunzi wake mambo mengi, pamoja na kuwaaga, maana huo ndio ulikuwa usiku wa mwisho kukaa nao, hivyo walikaa masaa mengi kwenye hiyo nyumba, wakiwa wanaimba, na kuonywa katika safari yao, na kutiwa moyo na Bwana..zaidi ya hayo katika usiku huo huo ndio Bwana aliwaosha miguu wanafunzi wake kuwapa kielelezo, pamoja na kushiriki meza ya Bwana…hivyo walichelewa sana muda wa kulala…Ukifuatilia kwa makini utakuja kugundua kuwa sio chini ya saa nane usiku ndio waliacha kuzungumza…Kwahiyo ni wazi kuwa walikuwa wamechoka mno.. Lakini cha kipekee ni kwamba, baada ya mazungumzo hayo ya muda mrefu hivyo, bado Bwana aliwaambia wakasali pamoja naye wasilale…

Hebu tafakari mchana kutwa mmetembea huku na huko, na bado mpaka muda wa usiku mmechelewa kulala, badala mpumzike ndio kwanza mnaambiwa mkasali, kwa hali ya kawaida ni ngumu kidogo lakini Bwana alijua hilo linawezekana…Na ndio maana akawaambia ya kuwa ‘siku zote roho ipo radhi, lakini mwili ndio dhaifu’…Hivyo hapo ni vita vya kupambana na mwili..Ikiwa na maana kuwa tukiweza kuushinda mwili basi tutafaidika sana katika roho.

Sasa ni namna gani ya kuushinda mwili?

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa, sisi kuwa na mwili sio dhambi! Kusudi la Mungu kututengenezea mwili pamoja na tamaa zake halikuwa baya tangu mwanzo, wala halikuwa mtego! Bwana alitutengenezea hii miili, pamoja na tamaa zake ili tuweze kuishi katika hii dunia kwa raha na furaha pasipo kuboreka, ndio kusudi la mwili, kwamba ili tusikwazike kipindi mwili unataka kupumzika, akauumbia kitu kinaitwa usingizi, hivyo wakati mwili ukitaka kupumzika, unazama kwenye usingizi mzito, ambao unampa mtu raha sana anapolala…hebu tafakari kusingekuwa na usingizi, na miili yetu inajizima ghafla tu inapochoka halafu tunaisubiria masaa labda 7 au 8 ndio ijiwashe tena, tuweze kuendelea na shughuli zetu, tungeichoka hii miili kiasi gani??

kadhalika ili mtu asiboreke katika kula, Mungu akauwekea mwili hamu ya kula kiasi kwamba mtu atatamani kula hata kama wakati mwingine hana njaa…lakini kusudi kuu la kula si kutupa sisi raha, bali kuupa mwili nguvu…tafakari endapo kungekuwa hakuna raha yoyote katika kula, lakini tunalazimika kula hivyo hivyo tungeichoka hii miili kiasi gani?..na tungeilisha hata vitu visivyofaa..n.k

Vivyo hivyo ili tuufurahie ulimwengu huu, tusije tukajihisi tumewekwa sehemu isiyo na maana Mungu katuumbia tamaa nyingi tofauti tofauti, ambazo hizo ni kama zinaongeza ladha za kuishi katika huu ulimwengu, tamaa ya kukusanyika pamoja, kucheza pamoja, kufurahi pamoja, na nyingine nyingi….Ndilo lilikuwa ni kusudi la Mungu tuishi katika ulimwengu huu pasipo kuboreka wala kuona ni mahali pabaya….

Lakini baada ya Adamu na Hawa kuasi, dunia yote ikaingiliwa na uovu, hivyo sio kila kitu kikawa kinafaa tena kutamani katika ulimwengu…Adamu akampa shetani milki ya ulimwengu huu, shetani akavumbua na kuwekeza mambo yapotezayo mengi, hivyo kwa yeyote atakayeangukia kwa tamaa moja wapo ya mambo yake aliyoyavumbua yeye, atakuwa amepotea, hivyo ndio maana biblia inatuambia tutoke katika ulimwengu, wala tusiutamani ulimwengu, kwasababu ulimwengu umeshaharibika.

Sasa tukirudi kutafakari ni namna gani tutaushinda mwili.

Mwili hatutaushinda kwa kuukemea, kwasababu tamaa hizi ziliumbwa na Mungu mwenyewe,wala hazikuwekwa na shetani…. huwezi kukemea njaa, wala usingizi, wala huwezi kukemea pua zako zisisikie harufu nzuri, wala huwezi kukemea mwili wako usisimke unapopitia hali Fulani ya kuusisimua.

Njia pekee ya kuushinda mwili, ni kujitenga mbali na vishawishi vinavyosababisha tamaa, kwamfano ukitaka mate yasikutoke, dawa ni moja tu! Kukaa mbali na sehemu wanazotengeneza vyakula unavyovipenda, huwezi kujizuia usitamani chakula mbele ya chakula, ni vita ngumu ambayo hutaiweza, kadhalika unapotaka kujizuia usiwake tamaa za mwili, dawa ni kukaa mbali na vichochezi vyote kama utazamaji wa picha chafu( pornography) pamoja na kampani za kidunia, ambazo kutwa kuchwa ni kuzungumzia hayo mambo, miziki ya kidunia, na pia kutakaa kuwa katika mahusiano na mtu yeyote kabla ya ndoa,Hilo tu! Utasikia mtu anakumbia niombee nishinde tamaa, tamaa zinanisumbua!!! Hakuna maombi yoyote ya kushinda hayo mambo ndugu yangu! Usidanganyike!! Dawa ni kukaa mbali na hivyo vitu.

Kadhalika ukitaka kushinda usingizi dawa ni kukaa mbali na kitanda na kuwa bize!..Unatoa mawazo yako katika kulala na kuyapeleka katika kitu kilichopo mbele yako.. Hakuna maombi yoyote ya kuuzuia usingizi…Bwana Yesu hakuwaambia wakina Petro waamke waanze kukemea pepo la usingizi!! Hapana…aliwaambia waamke wasali!…ikiwa na maana kuwa hakuna cha pepo hapo..Ni jambo la kuamua tu!.

Nimekutana na mtu akiniambia kila nikiingia kwenye ibada, au nikiwa katika kusali au kusoma Neno usingizi unanijia? Lakini nikitazama movie Fulani usingizi haunijii…kwahiyo hilo litakuwa ni Pepo Fulani linalonizuia kusoma Neno!…Ndugu hilo sio pepo! Ni wewe mwili wako umeupa nafasi ya kulala unapotaka kusoma Neno..Utauliza kivipi?…Hebu tafakari kama ni shetani ndiye anayekupa usingizi wakati wa kusoma biblia, jiulize ni movie ngapi za kidunia ambazo pia ulipozifungua kuziangalia tu haijapita dakika tano umelala?..utagundua kuwa hata hizo za kidunia kama umeboreka nazo unalala pia! Sasa kama ni shetani ndiye anayekuletea usingizi unaposoma Neno, vipi unaposinzia wakati unaangalia hizo za kidunia zinazokuboa?..je! na hapo ni shetani? Kwamba anakuletea usingizi usiangalie movie za kidunia?…Hivyo utaona usingizi unakuja wenyewe popote pale unapofanya jambo lisilokunufaisha au lisilokusisimua sana…

Kwahiyo dawa ya kushinda usingizi unaposali ni kwenda kujifunza kwa kina umuhimu wa maombi, ukishajua umuhimu wa maombi, na ukijifunza kutotoa udhuru kuwa ni shetani kakupitia kamwe hutalala!..usingizi utakapokuja utauzima tu!..Wengine wasiolala wala hakuna chochote cha kipekee ndani yao kinachowafanya wasilale wala wasikudanganye kuwa ni pepo lipo juu yako! Hakuna pepo hapo ni wewe mwenyewe hujaamua kuwa makini tu!…Mimi sijawahi kulala ibadani, na wala hakuna chochote cha kipekee kinachoendelea ndani yangu, wala hakuna pepo lolote ninaloshindana nalo ndani, wala hakuna maono ninayoona kujizuia kufanya jambo hilo…Nikujizuia tu! Na kuelewa umuhimu wa hicho kitu! Basi!..Na wote wasiolala wasikudanganye kuwa wao ni wa kiroho sana!…hapana! ni wameelewa tu umuhimu wa kinachoendelea pale na wamejifunza kuuzuia usingizi! Wengine wametambua kuwa kila wakiingia kwenye ibada wakiwa wamekula ni rahisi kulala, hivyo wanajifunza kula baada ya kutoka kwenye ibada n.k….ndicho kinachowafanya wao wasilale, hakuna cha ziada!, wala wasikudanganye kuwa unahitaji kufanyiwa maombi ya deliverance!..hakuna !Ni wewe kubadilika tabia tu!.

Biblia inasema Roho I radhi lakini Mwili ni dhaifu….Roho zetu zipo tayari kutenda mapenzi ya Mungu, vita kubwa ni sisi kuishinda kwa kuelewa ufunuo wa maombi, na kusoma Neno..Kadhalika, tutaishinda kwa kukaa mbali na vitu vinavyonyanyua tamaa ya mambo hayo. Pia nenda kasali mbali na kitanda chako, kama upo mwenyewe, lakini ni vizuri zaidi ukisali na mwenzako au wenzako, kwasababu mtatiana nguvu.

Kwa kumalizia Kumbuka kuwa! Ulimwengu huu, sio ule Bwana alioukusudia tuuishi kwa tamaa za miili yetu, ulimwengu huu shetani amekabidhiwa hivyo, matendo yote ya mwili na tamaa zake zote mwisho wake ni ziwa la moto..Biblia inasema…

Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.


Rudi Nyumbani

Print this post

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu ambalo ni mwanga wa njia yetu, na taa iongozayo miguu yetu..

Biblia inatuambia katikaAyubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia”….Ikiwa na maana kuwa Mema hayawezi kuja wala Amani tusipomjua Mungu vizuri, hivyo moja ya tatizo kubwa linalotukabili sisi wanadamu hususani wakristo ni kutokumjua Mungu vizuri, Hatumjui Mungu anafanyaje kazi, na anawapatiaje watu mema.

Ni Dhahiri kuwa mema mengi tunayoyatafuta ni mema ya hapa duniani, kama vile kuwa na mali, kufanikiwa katika kazi, kupata mume mzuri au mke mzuri wa Maisha, kupata kibali na vingine vingi..Lakini Mema ya ufalme wa Mbinguni ni bora Zaidi na yenye faida mara dufu!

Kwa ufupi leo tujifunze ni kwa namna gani Mungu anawapatia mema watu wake (mema ya hapa duniani).

Biblia inasema Mungu ni Mungu mwenye haki (Zaburi 7:9-11, Zab.11:7, Isaya 45:21), ikiwa na maana kuwa huwapa haki wale wanaostahili haki. Mungu kamwe hawezi kumpa mtu kitu asichokistahili.

Hebu tujifunze kwa mifano kidogo. Inatokea mtu ana biashara yake ya kawaida tu!, na ni Mkristo ambaye ni mwombaji mzuri, na kila siku anaiombea kazi yake, na anatumia mpaka Mafuta, na maji kuiweka wakfu, na pia anayo mpaka picha ya Bwana Yesu nyuma ya ukuta WA jengo la biashara yake, na kila siku kabla ya kuanza kazi anaiombea hata lisaa limoja, lakini bado unakuta pamoja na jitihada zote hizo mambo bado hayaendi vizuri anapata hasara au anaishia kupata mapato kidogo…Sasa yapo mambo mengi yanaweza kusababisha hilo lakini leo tutaangalia jambo kubwa sana linalosababisha matokeo hayo!… Na hilo si lingine Zaidi ya KUTOKUTOA HUDUMA INAVYOSTAHILI.

Unaweza kuwa mkristo mwombaji kweli na mwaminifu katika kuisogeza kazi yako mbele za Mungu, lakini kama hutajifunza kutenda mapenzi ya Mungu katika kazi yako, maombi yako au ya mwingine juu yako hayatasaidia kitu, yatakuwa ni kazi bure, kama ndani ya kazi yako hutatoa huduma nzuri inayovutia, inayostahili wewe kupata faida, kama hutatoa huduma itakayomvutia yule anayetaka kununua kutoka kwako aweze kurudi tena, kama hutakuwa mnyenyekevu, na mtu wa kujishusha katika kazi hiyo, kama hutakuwa mtu wa kupokea ushauri na kuuchuja katika Neno na kuufanyia kazi, kamwe maombi hayatakusaidia chochote, kadhalika kama hutakuwa msafi katika kazi yako, kama hutakuwa ni mpole kwa wateja wako hata ukibandika picha 20 zenye sura zinazofanana na Bwana Yesu nyuma ya ukuta wa jengo hilo, na kuweka stika za Mistari ya biblia 100, hazitasaidia chochote..

Sasa kwanini Vitu hivyo havisaidii chochote katika kukuletea faida?

Ni kwasababu hujajua kuwa Mungu ni Mungu mwenye haki. Na Watumishi wa Mungu wote wanatumika katika kuwapelekea watu huduma njema sharti walifahamu hilo, Mungu hawezi kumtumia mtu kuwapikia uchafu au sumu watu wake!..hivyo kama wewe ni mchafu katika mahali ulipo kwenye kazi yako labda ya Mgahawa, hiyo ndio sababu Mungu hawezi kuinyanyua izidi kusitawi, hapo ili utumike na Mungu kuwalisha watu wake chakula bora ni sharti uwe msafi sana, kwasababu kuna watu wameamka asubuhi kutoka majumbani mwao na huku wamemwomba Mungu awaepushe na hatari zote ikiwemo sumu na uchafu kuingia katika miili yao, sasa Mungu hawezi kuwajibu hao maombi yao kwa kuwaleta kwenye mgahawa wako ambao unapika uchafu na vyakula visivyo na ubora! Kwa kujidanganya kuwa Mungu ameifunika biashara yako..hapana Mungu ni Mungu mwenye haki! Hawezi mtu kumwomba Mkate akampa jiwe!..Mungu hayupo duniani kuwapatia watu mabaya bali mema…

Hivyo ukitaka kazi yako ya mgahawa isitawi usitegemee maombi tu peke yake…Kuwa Msafi wa viwango vya juu sana,kupita wengine..pika chakula freshi na chenye viwango… ndipo Mungu atakufanya kuwa mtumishi wake kuwapatia chakula safi wanadamu wake na utaona wateja ambao hujawahi kuwaona wakimiminika kwenye hiyo kazi yako.

Na kitu kimoja kisichojulikana na wengi, ni kwamba Mungu hatendi kazi kama shetani atendavyo, shetani ndio ana kitu kinaitwa chuma ulete, au mazingaumbwe anatumia kiini macho,kwamba mtu anaweza kupata chochote katika hali hiyo hiyo aliyopo, hata akiwa mchafu, anaweza kutumia nguvu za giza, kuleta wateja..Mungu hana hicho kitu chuma ulete, wala hatumii kiini macho kuwaletea watu wake fedha!..vinginevyo sifa yake ya kuwa Mungu mwenye haki haitakuwepo!.

Kadhalika kama ni duka, Mungu hawezi kukutumia wewe kuwalisha watu vitu vilivyoisha muda wake wa matumizi (vilivyo-expire), hata kama unakesha kwa wiki mara mbili kuiombea, hata kama unaitolea sadaka nyingi kiasi gani, haiwezekani Mungu kukunyanyua.…kwanini hawezi kufanya hivyo kwasababu, yeye sio Mungu wa kuwapa watu sumu..kama tu asivyokuwa Mungu wa watumishi wa uongo (manabii wa Uongo)..Na kadhalika wafanya biashara wa uongo Mungu hawezi kuwa nao, hata wawe waombaji kiasi gani…atawaepusha watu wake na duka lako….

Pia unapokuwa katika kazi yako unapaswa uwe mnyenyekevu, hupaswi kuwa mtu wa hasira na mtukanaji, au mkorofi. Mungu hawezi kukutumia kuwahudumia watu wake uende ukawatukane na kuwazalilisha..Pia unapaswa kuhakikisha unafanya juhudi kufikisha huduma yako mpaka mlangoni mwa wateja wako au wanaohitaji!..Kwasababu hata watumishi wa Mungu wa kweli anaowatumia hutuletea Neno la Mungu mpaka ndani ya mageti yetu kwa unyenyekevu wote, na ndivyo injili ilivyofanikiwa duniani kote…Kadhalika katika kazi yako, kama unauza mkate mfikishie mteja wako mpaka mlangoni, Mungu anapendezwa na watu wanaotua huduma njema, watu wake wahudumiwe mpaka mahali walipo, na mtu anapohudumiwa kwa njia hiyo, moyoni atafurahi na hivyo atamtukuza Mungu na kumshukuru, na akishafurahi na Mungu atafurahiwa na wewe na hivyo kuibarikia hiyo kazi yako izidi kusonga mbele Zaidi..Hapo ndipo atakapomshawishi Yule mtu kuja tena, na Yule mtu kumwambia mtu mwingine, hivyo hivyo mpaka wanakuwa wengi.

Kadhalika Kama ni mjenzi Mungu hawezi kukutumia wewe kuwajengea watu nyumba ambazo zipo chini ya viwango, kwasababu kuna watu wamemwomba Mungu awapatie nyumba zilizobora na fundi aliyemwaminifu na mwenye ujuzi wa kutosha, hivyo ili Ukidhi hiyo nafasi ya kuwa Mtumishi wa Mungu katika eneo hilo, ni sharti ujitahidi kuielewa vyema hiyo kazi kwa kwenda kutafiti mbinu mpya za ujenzi, kuongeza ujuzi wako na kuongeza ustadi…ili Mungu achague kukutumia wewe na si mwingine katika nafasi hiyo, hapo ndipo utakapoona mafanikio makubwa, usikimbilie kutafuta faida ya haraka haraka, …lakini kama hutataka kutafuta kutoa huduma bora yenye viwango, Bwana Mungu atatafuta mtu mwingine hata kama asiye mkristo aliyekidhi hivyo viwango, kuifanya kazi hiyo…..kwahiyo maombi peke yake hayatoshi!. Matendo ndio yenye nguvu zaidi..Inakupasa ujitahidi uwe bora Zaidi ya wengine ili ukawafanyie watu kilicho bora wamtukuze yeye…

Kadhalika na mambo mengine yote yaliyosalia…jambo ni lile lile…. “JITAHIDI KUTOA HUDUMA ILIYO YA VIWANGO VYA KIMBINGUNI ”

Hata unapotafuta kuoa au kuolewa!! Formula ni hiyo hiyo, NI lazima uwe mtakatifu, usipofanya hivyo na kutegemea maombi peke yake, nakuhakikishia hutaolewa wala hutaoa!…au kama utaoa au kuolewa basi utaoa mtu asiyesahihi au kuolewa na mtu asiyesahihi.

Kwanini?

Kwasababu wewe ni mwenye kiburi na mwasherati halafu unamwomba Mungu akupe mume mwenye hofu ya Mungu, mpole, mnyenyekevu, atakayekujali na kukupenda na kukuheshimu, na asiyekuwa mwasherati….Hujui kwamba huyo mume unayemwomba aliye na vigezo hivyo vya hofu ya Mungu, naye pia anamwomba Mungu ampe mke aliye kama yeye alivyo, mwenye hofu ya Mungu kama yeye, msikivu kama yeye alivyo, asiye mwasherati kama yeye, asiye mwenye kiburi na aliye mnyenyekevu…. Sasa Mungu hawezi kumpa mtoto wake nyoka aliyemwomba samaki!…Kwahiyo Mungu atahakikisha anamtafutia Mke mwema yule mwanamume mwenye hofu ya Mungu kama yeye…Na huyo mke atakuwa sio wewe kwasababu wewe huna vigezo hivyo…..Wewe utaishia kupata mwenye vigezo kama vya kwako vya uasherati, kiburi, na kahaba..Lakini ukiwa mtakatifu Mungu atakupatia Mtakatifu mwenzako na wala haitachukua Muda!…Na pia utakatifu ni wajibu!..hatuwi watakatifu tu kwasababu tunatafuta wachumba!..Ni wajibu wetu kuwa watakatifu maadamu tunaitwa wakristo!

Ndio maana Kuna umuhimu wa kumjua sana Mungu, ili mema yakujie…Mungu anataka tufanye kazi ya haki, tupate haki, anataka tuwe watakatifu tuwapate watakatifu, anataka tuwe wakujitoa ndipo na wengine wajitoe kwa ajili yetu…anataka tuwe watu wa kutoa huduma njema ndipo atubariki. Anataka tumjue kwa mapana hayo….Maombi yanafaa sana endapo tutaomba na kutenda!

Zaburi 18:25 “Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

26 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.”

Bwana akubariki sana!. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

MJUE SANA YESU KRISTO.

ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU


Rudi Nyumbani

Print this post

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

Waebrania 6:11 “Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho;

12 ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.

13 Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,

14 akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.

15 Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi”.

Neno uvumilivu siku zote limekuwa sehemu ya Mungu, na sisi vivyo hivyo tunapaswa liwe sehemu ya maisha yetu, Kama Mungu asingekuwa mvumilivu ni wazi kuwa mimi na wewe tungekuwa tumeshapotea siku nyingi, kwani wakati tu tuliposikia injili kwa mara ya kwanza, siku hiyo hiyo Mungu alitazamia tubadilike lakini wengi wetu tulikuwa wakaidi, ndio tukazidi kuwa watenda dhambi hata zaidi ya hapo mwanzo miezi ikapita, miaka ikapita, japo tulikuwa tunasikia kila siku mahubiri yanahubiriwa lakini hatukuzingatia, Sasa kama ingekuwa Mungu ni mtu wa kukataa tamaa mapema, sio mvumilivu, sidhani kama mpaka leo hii tungekuwa tunaishi,.. 

Lakini uvumilivu wake, umekuwa neema kwetu na umemzalia matunda si yeye tu, bali sisi pia. Mimi binafsi ninayo kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuwa mvumilivu kwangu, kwa maana maovu mengi niliyoyafanya huko nyuma nilidhani nilishamkufuru Mungu siku nyingi. Na ni kwanini Mungu anakuwa mvumilivu kwetu?..Jibu ni ili kutuvuta tufikie TOBA halisi.

Warumi 2:4 “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?”

Zaburi 86: 15 “Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli”

Vivyo hivyo na sisi tulio katika imani, Uvumilivu ni moja ya nguzo muhimu sana. Katika mbio hizi zilizo mbele yetu, japo tumewekewa thawabu kubwa huko mwisho mwa safari lakini ukweli ni kwamba milima na mabonde ya ibilisi hayakwepeki, majaribu na masumbufu, na wakati mwingine dhiki tutakutana nazo hapa duniani, na Bwana Yesu alishatueleza kabisa kuwa mambo hayo tutakuwatana yao wala hakutuficha,(Yohana 16:33)..Hivyo ni safari inayohitaji uvumilivu.

Lakini Swali ni Je! uvumilivu wa aina gani huo unaohitajika kwetu?

Kuna mwingine anaweza akawa labda anapitia matatizo yake binafsi, labda uchumi wake umeyumba, au amekumbana na matatizo ya kifamilia, au magonjwa n.k..na huku nyuma hata hana habari na Mungu, sasa mtu wa namna hii, anaweza akatiwa moyo kibinadamu awe mvumilivu katika hali ngumu anayoipitia kwa huo muda..Lakini huo sio uvumilivu unaozungumziwa katika maandiko.

Uvumilivu unaozungumziwa ni uvumilivu unaolenga Imani. Yaani kutokukatishwa tamaa na hali unayopitia sasa hivi ambayo inaweza kukusababishia kupoteza thawabu yako uliyoandaliwa mwisho wa safari..kwamfano wakati mwingine unaweza ukaona unapitia katika hali Fulani ngumu ambayo sababu yake tu ni uliamua kutokukifanya hicho kitu ambacho ni kinyume na mapenzi ya Mungu, unaweza ukawa unatengwa au unachukiwa kwasababu tu umeacha kufanya dhambi, mwanzoni ulikuwa unakunywa pombe na marafiki zako lakini sasa hunywi tena, mwanzoni ulikuwa unakwenda disco lakini sasa huendi tena, mwanzoni ulikuwa msengenyaji lakini sasa husengenyi tena, na matokeo yake kumetokea kundi la watu wanakutengenezea visa tu, wanakuwekea vikwazo,wanakusema vibaya..wakati mwingine ndugu, hata kazini kwako n.k.

Hapo ndipo unapopaswa uvumilie, biblia inasema katika Mhubiri 7: 8 “Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake, Na mvumilivu rohoni kuliko mwenye roho ya kiburi. 
9 Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu”…… 

Pasipo uvumilivu hatuwezi kumzaliwa Mungu matunda..Kama vile Bwana alivyotoa ule mfano wa mpanzi, akasema mbegu nyingine ziliangukia pembezoni mwa barabara nyingine zikaangukia kwenye miamba nyingine zikaangukia kwenye miiba,..nyingine kwenye udongo mzuri, hapo Bwana alikuwa anafunua aina tatu ya vipingamizi mtu atakavyokutana navyo kabla ya kuufikia mwisho mzuri wa safari yake, awali ya yote shetani atataka kumpokonya kile alichokisikia, itafika tena wakati ataudhiwa kwa ajili ya hilo Neno aliloendelea kulishika, baadaye tena baadhi ya mambo yatataka kumsonga asizae, na shughuli za ulimwengu huu na anasa, na tamaa ya mambo mengi …

Lakini Yule ambaye atazaa 30, mwingine 60 mwingine 100 Biblia inasema, hakuifikia hiyo hatua hivi hivi tu, bali aliifikia kwa KUVUMILIA vipingamizi vyote.

Luka 8:11 “Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.

12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.

13 Na wale penye mwamba ndio wale ambao wasikiapo hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa kujaribiwa hujitenga.

14 Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote.

15 Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda KWA KUVUMILIA.’’

Hivyo ndugu, tunapaswa tuilinde Imani Mungu aliyotupa mara moja tu, Na hiyo tutailinda kwa kuvumilia mabaya yote shetani atakayojaribu kutulea mbele yetu yatakayotufanya tuuache wokovu au turudi nyuma….Iwe ni magonjwa, iwe shida ya fedha, iwe ni kukosa mavazi, iwe ni kuwa yatima, iwe ni kuwa mjane, iwe ni kuwa tasa, iwe ni kupigwa au kutengwa au wakati mwingine kufungwa, vyovyote vile yasitufanye sisi kukosa uvumilivu wa kuyaongojea tuliyoandaliwa mbele. Tuige mfano wa Ibrahimu. 

Ufunuo 2:3 “tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka.”

Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

MNGOJEE BWANA

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?


Rudi Nyumbani


Print this post

WALIOITWA NI WENGI, ILA WATEULE NI WACHACHE.

Kama Ukijifunza Biblia kwa undani utagundua kuwa Bwana Yesu hakuwa na wanafunzi 12 tu! Bali alikuwa na wanafunzi wengine wengi sana Zaidi ya 70 biblia inasema hivyo katika (Luka 10:1-2)…Lakini baadaye alikuja kuteua wanafunzi 12 tu miongoni mwao wakutembea naye kila mahali alikokwenda ambao aliwaita Mitume. 

Sasa kama ukizidi kufuatilia kwa makini, utagundua kuwa Bwana Yesu alianza kwanza kuchagua wanafunzi wake wengi katika hatua ya Kwanza, ikiwemo wale 12, kwahiyo tuseme lilikuwepo jopo la watu kama 80 hivi waliochaguliwa na Bwana, na ni wazi kuwa wote Bwana aliowaita aliwaambia kuwa watakuwa na shughuli ya uvuvi wa watu…alipita huko na huko kuwaita kutoka katika ulimwengu, katika njia ile alikutana na mvuvi Petro akamwita, katika njia nyingine akakutana pengine na fundi wa nyumba akamwita, sehemu nyingine akakutana na Mathayo mtoza ushuru akamwita…wengine pengine walikuwa hawana shughuli yoyote wapo mtaani akawaita, likawa kundi moja la watu kama 80 hivi walioitwa….Na wote walioitwa walikuwa sawa machoni pa Bwana Yesu, hakuna aliyekuwa mkubwa zaidi ya mwingine, na wote aliwaambia waache vyote wamfuate, na walimtii..Sasa hiyo ilikuwa ni hatua ya kwanza ya wito..kundi kubwa la wanafunzi liliitwa…. (Kwa somo refu jinsi gani Bwana aliwachagua wanafunzi wake na jinsi anavyowachagua sasa unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia hilo somo).

Hatua ya pili ilifuata kipindi kifupi baadaye, pengine baada ya miezi kadhaa, ambapo Bwana akaanza tena kuwatenga wanafunzi 12, miongoni mwa lile kundi kubwa la wanafunzi wake…kumbuka hawa 12, hawakuteuliwa moja kwa moja kutoka kwenye ulimwengu, hapana! bali kutoka katika lile kundi la wanafunzi wengine aliokuwa nao…Huo ndio ulikuwa mchujo wa pili, Ndio siku ile Bwana Yesu alipokwenda kukesha kwenye maombi na Mungu akamfunulia mitume 12 miongoni mwa lile kundi…

Luka 6:12 “ Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. 13 Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; AKACHAGUA KUMI NA WAWILI MIONGONI MWAO, ambao aliwaita Mitume; 14 Simoni, aliyemwita jina la pili Petro, na Andrea nduguye, na Yakobo na Yohana, na Filipo na Bartolomayo, 

15 na Mathayo na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Simoni aitwaye Zelote, 

16 na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote, ndiye aliyekuwa msaliti. 

17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali tambarare, pamoja na wanafunzi wake wengi, na makutano makubwa ya watu waliotoka Uyahudi wote na Yerusalemu, na pwani ya Tiro na Sidoni; waliokuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao; 18 na wale waliosumbuliwa na pepo wachafu; waliponywa”

Unaona?..Mitume 12 walichaguliwa miongoni mwa kundi la wanafunzi wengi…sasa hawa 12 hawakuchaguliwa kwasababu ya jitihada yao yoyote waliyokuwa nayo, au kwasababu ya utakatifu wao, au kwasababu walikuwa wanajuhudi kuliko wengine, au kwasababu mbele za Mungu wenyewe ndio walikuwa wanaonekana wanaunafuu…Hapana, walichaguliwa kwa Neema tu… Neno ‘neema’ linakaribiana sana kufanana na neno ‘bahati’….lakini sio bahati…Neema ni Zaidi ya bahati, bahati mara nyingine inamwangukia mtu ambaye amestahili, lakini Neema siku zote ni kwa mtu ambaye hajastahili…Hivyo hawa 12 waliochaguliwa katika mchujo wa Pili walipata NEEMA na sio BAHATI. Walikuwa hawastahili kuchaguliwa lakini walichaguliwa…Na hata hao wengine pia sio kwamba hawakuchaguliwa kwasababu walikuwa waovu au kwasababu walikuwa watakatifu sana, hapana! ni uchaguzi tu wa Mungu! Ndivyo ilivyompendeza awachague wale na hao wengine awaache, hatuwezi kuelezea kibinadamu, na wala hatuwezi kumwuliza Mungu kwanini kafanya hivyo! (soma Warumi 9:13-25).

Sasa katika hatua hii ya Pili ndipo linapotimia Neno hili “walioitwa ni wengi ila wateule ni wachache”…Hapo liliitwa kundi kubwa pengine la watu Zaidi ya 80, lakini walioteuliwa kwa Neema kuwa mitume ni 12 tu!.

Lakini bado mchujo unaendelea kwasababu hata miongoni mwa hao walioteuliwa 12, bado kuna uwezekano wa kupotea…Sio kwasababu tu! Umeitwa Mteule basi ndio tiketi ya kusema nimeokolewa…

Biblia inatuambia kuwa hata “wateule wanaweza kudanganyika”.

Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. 

24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; WAPATE KUWAPOTEZA, KAMA YAMKINI, HATA WALIO WATEULE.

25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

 26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki.

 27 Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu”.

Yuda alikuwa miongoni mwa wateule 12, lakini alidanganyika na kupotea!…na hapo biblia inatuonya kuwa katika siku za mwisho watatokea makristo wa Uongo, watatoa ishara na maajabu wapate kuwapoteza kama yamkini hata walio wateule…

Wakati huo tunaoishi ni sasa, wateule wanaozungumziwa hapo ni wale wote ambao Bwana ameshawaita watoke katika ulimwengu, na kuwateua miongoni mwa watu wake, na kuwapa neema ya kuzijua siri za ufalme wa mbinguni kama wewe unayesoma hapa…Kumbuka sio mambo yote Bwana Yesu alikuwa anawaambia makutano, ni machache sana ndio alikuwa anawaambia makutano, siri zake nyingi alikuwa anawafunulia wale mitume 12 tu aliowachagua…wengine wote alikuwa anawafundisha kwa mifano…

Mathayo 13:10 “Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini wasema nao kwa mifano? 

11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali wao hawakujaliwa”.

Unapopata Neema ya kusikia injili popote pale, tena unapata kuzijua siri za ufalme wa mbinguni ambazo wengine hawazioni wala kuzipata, na kuna kitu ndani kinakushuhudia kuwa ni kweli… fahamu kuwa wewe ni mteule, lakini katika hizi siku za mwisho wateule wengi watadanganyika kama tu vile Yuda alivyodanganyika na kuishia kumsaliti Bwana Yesu… Yuda alishawishika kabisa ndani ya moyo wake kumwamini Bwana Yesu katika hatua za kwanza za wito wake, alipata ufunuo kabisa kuwa Yesu ndiye masihi aliyetabiriwa, na hivyo akaingia gharama ya kuacha kila kitu na kumfuata Yesu, kwasababu hakuna mtu yeyote ambaye angemfuata Yesu bila kuacha kila kitu na kujikana nafsi yake, Yuda alifanya vyote hivyo, aliitikia wito inavyopaswa….lakini ilifika wakati akaanza kulizoelea Neno, akaanza kuingiwa na tamaa ya vitu vya ulimwengu, akaanza wizi kidogo kidogo, akaanza kuipenda dunia kidogo kidogo, Bwana hakumfukuza asiambatane naye, alimwacha mpaka mwisho, wala upako wake haukukatika aliendelea nao alitoa pepo na kuombea watu kama kawaida na kupokea uponyaji, lakini mwisho wake ulikuwa mbaya, alipasuka matumbo (Matendo 1:16-20).

Na hata leo, ulianza vyema kusikia injili na kuamua kumfuata Yesu kwa moyo, hapo ni Bwana alikuita kweli na akakuteua kuwa karibu naye Zaidi ya wengine, uliacha vyote na kumfuata…lakini imefika kipindi sasa umelizoelea Neno, umeoza ndani, unamwibia Bwana, umekuwa ni mwana wa ulimwengu huku, huku bado unatembea na Yesu, kumbuka Bwana hatakufukuza wala hatakutenga, ataendelea kutembea nawe kama alivyotembea na Yuda, wala hataonesha dalili ya kukudharau wala kukuvunjia heshima, na wala nguvu ya kufanya miujiza hatakupokonya, lakini mwisho wako utakuwa kama wa Yuda!…ili maandiko yatimie , Yuda alikuwa ni mteule lakini Bwana alisema ni kheri asingezaliwa mtu kama huyo kuliko mambo mabaya ambayo yatakwenda kumpata!…Hebu fikiria Mtu aliyeteuliwa na Mungu mwenyewe anaambiwa maneno hayo?.

Ndugu hizi ni siku za mwisho sana, Hayo ya akina Yuda yalitokea ili kutufundisha sisi watu wa siku hizi za mwisho, kuwa tufanye IMARA WITO wetu na UTEULE WETU. Kama maandiko yanavyotuambia..

2 Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi KUFANYA IMARA KUITWA KWENU NA UTEULE WENU; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.


Imarisha wito wako ewe Mteule. Ni wakati wa kumrudia Bwana pasipo mguu mmoja nje wala mguu mmoja ndani, kabla wakati wa kupasuka matumbo haujafika, kabla wakati wa kujutia kama Yuda haujafika, kabla wakati wa kula tonge la mwisho la Bwana, na shetani kukuingia haujafika, siku hiyo mlango utakuwa umefungwa, Yuda baada ya kulila lile tonge shetani alimwingia, ikawa ndio mwisho wake pale. Tengeneza wakati wako, linda wito wako na utendee kazi uteule wako.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UMEITIKIA WITO INAVYOPASWA?

JE! UMECHAGULIWA KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU?

JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?


Rudi Nyumbani


Maran atha!

Print this post

TUKAZE MWENDO ILI TUUFIKILIE UTIMILIFU.

Mambo ya dunia hii yanatupa picha halisi ya mambo yanayoendelea rohoni, Kwamfano tukiangalia mataifa yaliyoendelea kama ya Ulaya, tukiyalinganisha na mataifa ambayo hayajaendelea kama vile ya Afrika, utagundua kitu kimoja cha tofauti, utaona watu wa huku wanapambana maisha yao yote ili kupata yale mahitaji ya msingi (Basic needs) kama vile Chakula, malazi na mavazi,.Na mtu aliyefanikiwa kuwa na hivyo vitu basi anaonekana tayari ametoka kimaisha ndio maana tunajulikana kama mataifa machanga..Lakini ukitazama yale mataifa yaliyoendelea utagundua kuwa vitu kama hivyo sio kipaumbele chao kwani karibu kila raia anao uhakika wa kupata mahitaji hayo ya msingi wengine tangu wanazaliwa tayari wanayo, kwani serikali tayari ilishaandaa mazingira mazuri kwa raia wao..

Wao kipaumbele chao kikubwa kipo katika mambo ya utafiti, utakuta jopo kubwa la watu limejikita katika mambo ya utafiti maisha yao yote, na matokeo yake ndio tunayoyaona sasa kwa teknolojia wanazozianzisha duniani, uwezo wa kusafiri katika anga za mbali na mambo ya mawasiliano n.k…Na hiyo ndio inayowafanya waonekane kuwa ni mataifa makubwa na watu wake waonekane kama ni watu bora kuliko wengine tukizungumza kibinadamu.

Vivyo hivyo katika mambo ya rohoni, Mtume Paulo aliona baadhi ya makanisa yapo katika hali ya Uchanga, kipindi kirefu kinapita hata wakati mwingine maisha yao yote lakini bado wanahangaika na mambo yale yale ya msingi ya awali, hawaonyeshi dalili ya kuendelea mbele, Watu wanataka kila siku wapigiwe kelele juu ya mafundisho yale yale ya awali,.wanyweshwe maziwa tu na sio vyakula vigumu vya rohoni, Sio kana kwamba Mtume Paulo alikuwa hawezi kuwafundisha mengine, hapana lakini alikuwa anaona kama tu yale ya msingi wanapata shida kuyatii haya mengi watawezaje?..

Na mafundisho yenyewe aliyoyoataja pale ni kama haya: Mafundisho ya TOBA, mafundisho ya kumwamini Mungu, Mafundisho ya Ubatizo, mafundisho ya ufufuo unaokuja, mafundisho ya Hukumu za Mungu zinazokuja, na mafundisho ya ukombozi(kuwekea watu mikono).

Ambayo kimsingi haya yote ni mafundisho ambayo kila siku tunajifunza na tunafundishwa, makanisani, mitandaoni, mikutanoni n.k..

Hapo Je! sisi si, watoto wachanga?, sisi si maskini wa kiroho?.

Waebrania 5:10 “kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.

11 Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia.

12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.

14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya”.

Waebrania 6 :1 “Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu,

2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele.

3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia”.

Hivyo kabla ya kumwomba Mungu atupeleke katika hatua nyingine ya kujifunza siri za ndani za Yesu Kristo, kama hizo ambazo mtume Paulo alizidokeza alipomfananisha na Melkizedeki, kwa jinsi Melkizedeki alivyokuwa hana baba, wala mama, wala mwanzo wa siku wala mwisho, na ndivyo Bwana wetu Yesu alivyokuwa, mfano wa Melkizedeki kuhani wa milele, kuna siri nyingine nyingi sana zimuhusuzo Bwana wetu Yesu Kristo hatuzijui bado , ambazo tukizijua hizo, hatutaishi kama tulivyo..

Kwasababu ni wazi kuwa bado Kristo anajifunua kwetu kila siku, mpaka Yule malaika wa 7 atakapokuwa tayari kupiga baragumu lake, hapo ndipo Siri yote ya Mungu itakapotimizwa.. Na itakapotilimilika SIRI hiyo (Ambayo inamuhusu Yesu Kristo mwenyewe), Mwisho wa kila kitu utakuwa umefika..

Ufunuo 10:5 “Na yule malaika niliyemwona, akisimama juu ya bahari na juu ya nchi, akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni,

6 akaapa kwa yeye aliye hai hata milele na milele, yeye aliyeziumba mbingu na vitu vilivyomo, na nchi na vitu vilivyomo, na bahari na vitu vilivyomo, ya kwamba hapatakuwa na wakati baada ya haya;

7 isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari kupiga baragumu; hapo ndipo siri ya Mungu itakapotimizwa, kama alivyowahubiri watumishi wake hao manabii”.

Hivyo tumwombe Mungu atusaidie tuvute katika hii hatua ya uchanga tuliyopo sasa, Tusifurahie tu wakati wote kuhubiriwa habari za kutubu dhambi, na kubatizwa,..hayo ni maziwa ndugu, bado hatujaanza kula chakula, Tukiweza kuvuka hayo ndipo Mungu atakapotupeleka katika hatua nyingine..Toba na Ubatizo ni mafundisho ya awali ya msingi, lakini jengo lenyewe bado halijasimama…Lengo ni kupandisha jengo sio msingi, ndio maana tunahitaji kukua kila siku…

TUKAZE MWENDO ILI TUUFIKILIE UTIMILIFU.

Shalom. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

SAUTI AU NGURUMO?


Rudi Nyumbani

 

Print this post

YAKUMBUKE YA NYUMA.

Nguvu ya kuendelea mbele tunaipata kwa kutazama tulipotokea…Usipokuwa na jicho la kutazama ulipotokea, usipokuwa na jicho la kukumbuka ni wapi ulipitia, utaishia kuwa mtu wa kunung’unika na kulalamika …

Ili tuweze kuishi Maisha ya ushindi siku zote katika haya Maisha ya hapa duniani, ni lazima tuishi Maisha ya kutafakari ni mambo gani ya nyuma Mungu aliyotutendea….unatazama kama Mungu wakati fulani alikupigania kwa kile, wakati huu atanipigania pia kwa hichi, Imani ndio inapokuja hapo..Ukishindwa kukumbuka ya nyuma kamwe hutaweza kuyashinda yanayokuja.

Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana, wakati mwingine kuandika chini, mambo yote makubwa na madogo Mungu anayokutendea ili usisahau, hiyo itakusaidia pindi utakapokutana na tatizo kama hilo basi utakumbuka kirahisi uweza wa Mungu aliokupigania huko nyuma na utapata nguvu mpya.

Uweza wa Mungu unadhihirika mahali palipo na Imani, na Imani haiwezi kuja kama utayasahau matendo makuu ya Mungu aliyokutendea nyuma…Ndicho kilichowatokea wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, ilikuwa kila mara wanasahau mambo makuu Mungu aliyowatendea nyuma na hivyo kuishia kumdharau Mungu kwa mambo madogo yanayotokea mbele yao, Walipotuma wapelelezi kuipeleleza nchi ya Kaanani na kukuta wenyeji wa kule ni majitu makubwa, badala wakumbuke kuwa Mungu alishawapigania huko nyuma kumwangusha Farao ambaye alikuwa na nguvu kuliko hayo majitu, wao wakasahau na kuanza kujiona nafsi zao kama mapanzi, hivyo ikawa dhambi kubwa mbele za Mungu,

Hayo yamewapata ili kutuonya sisi watu wa zamani hizi, tunapaswa tukumbuke uweza wa Mungu..aliotutendea huko nyuma pindi tunapokutana na jaribu fulani mbele yetu..Hata mwanafunzi ili aweze kulipata swali kisahihi, ni lazima awe na uwezo wa kukumbuka ni wapi alishafanya swali kama hilo, na wapi mtego wa swali hilo upo..asipokuwa na uwezo huo kila kitu kwake kitakuwa ni kipya.

Na ndio maana katika agano la kale Wanyama ambao walikuwa hawacheui walijulikana kama najisi, Mnyama anayecheua ni ambaye anao uwezo wa kula chakula na kukihifadhi tumboni baadaye anakirudisha na kikitafuna tena na kukimeza kama vile ng’ombe,..Inafunua kuwa sisi kama wanyama wa Kristo tusio najisi, tunapaswa tuwe na uwezo wa kukumbuka mambo yote makuu Mungu aliyotutendea nyuma, huko ndio kutafuna tena kile tulichokula, lakini tukiwa wasahauji, ndio yatatukuta kama yale ya wana wa Israeli.

1 Wakorintho 10:9 “Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke

Unapopitia kupungukiwa kidogo, kumbuka kuna kipindi ulipitia hali ngumu kuliko hiyo na Mungu alikufungulia mlango, hivyo tumia huo ushuhuda kukabili tatizo lililopo sasa, useme kama Mungu alinipigania kipindi kile cha taabu atanipigania na sasahivi, kwasababu Mungu ni yule yule habadiliki!…Kama unapitia ugonjwa fulani sasa, kumbuka kipindi fulani nyuma ulipitia ugonjwa wa hatari na Bwana akafungua mlango wa wewe kupona…tumia huo ushuhuda kukataa mawazo ya kukata tamaa sasa..

Kama umezungukwa na hatari, au unakabiliana na hatari, au tatizo mbele yako, sio wakati wa kupaniki, ni wakati wa kurudisha kumbukumbu zako nyuma na kukumbuka Bwana alivyokuokoa kwenye mikono ya waovu, na alivyokuepusha na hatari kimiujiza miujiza.n.k n.k, na kusema kama alifanyia vile, atanifanyia na hata sasa vile vile kama aliwafanyia wale, atakufanyia na wewe,…Mungu aliwaambia wana wa Israeli maneno haya wakati wanakwenda kukabiliana na maadui zao katika nchi ya Kaanani..

Kumbukumbu 7:17 “Nawe kama ukisema moyoni mwako, Mataifa haya ni mengi kunipita mimi; nitawatoaje katika milki yao?

18 Usiwaogope; KUMBUKA SANA Bwana, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote;

19 uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.

20 Tena Bwana, Mungu wako, atampeleka mavu kati yao, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.

21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho.”

Bwana akubariki!, kama utapenda kujifunza Zaidi na kwa urefu juu ya “kukumbuka wema wa Mungu, aliokufanyia nyuma” unaweza kufungua ujumbe huu >>> MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

Maran atha! . jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Katika agano la kale, wayahudi walivyochanganyikiwa sana juu ujio wa masihi mpaka kupelekea kugawanyika makundi mengi, ndivyo ilivyo hata katika agano jipya watu wengi wanavyochanganyikiwa katika habari ya Roho Mtakatifu jinsi anavyokuja juu ya mtu, hadi sasa imepelekea kutokea makundi mengi tofauti tofauti ambalo kila moja linaamini katika uthibitisho wake.

Kama tunavyofahamu katika agano la kale biblia ilishatabiri kuwa Masihi (YESU KRISTO) atakuja, lakini kwa bahati nzuri au mbaya haikueleza katika mtitiriko unaoeleweka sana, bali sisi wa agano jipya kwa Kutazama maisha ya Kristo ndio tunaoelewa jinsi maandiko yalivyotimia ,..Lakini katika agano la kale ilikuwa ni ngumu sana kuelewa, na saa nyingine maandiko yaliyonekana kama yanajichanganya..Kwamfano unabii alioutoa Isaya kuhusu Kristo katika (Isaya 53), inaonyesha kuwa Masihi atakuja kuteswa na kuuliwa kwa ajili ya dhambi za watu wengi..Lakini sehemu nyingine katika kitabu hicho hicho cha Isaya inasema Masihi atakuwa mfalme, naye ataketi katika kiti cha enzi cha Daudi, naye atadumu milele.

Unaona sehemu moja inasema atakufa lakini sehemu nyingine inasema atadumu milele,..Lakini je! Wale walioshikilia tu unabii mmoja labda tuseme wale walioamini kuwa Masihi atasulibiwa, au wale walioamini tu Masihi ataishi milele, je! wote Hawapo sawa? Jibu ni La!..Sisi tunaoishi katika agano jipya ndio tunaojua kuwa Wote wapo sawa kabisa, lakini wote walioweza kuamini nabii zote mbili ndio wapo sawa zaidi kuliko wale wengine, kwani ni Kweli kuna wakati Kristo atasulibiwa atakufa lakini atafufuka na atarudi tena, na atakaporudi atakuja kama Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho kama nabii zote mbili zilivyotabiri.

Yohana 2:33 “Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa.

34 Basi mkutano wakamjibu, Sisi tumesikia katika torati ya kwamba Kristo adumu hata milele; nawe wasemaje ya kwamba imempasa Mwana wa Adamu kuinuliwa? Huyu Mwana wa Adamu ni nani?

35 Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako”.

Sasa tukirudi katika habari za Roho Mtakatifu, kama tusipoweza kuyavunja maandiko na kufahamu utendaji kazi wake, tutaishia kuchanganyikiwa sana, na mwisho wa siku kila mmoja ataamini anachokiamini…

Leo hii kuna watu wanaomini kuwa uthibitisho pekee wa mtu kuwa na Roho Mtakatifu ni kudhihirisha karama Fulani ndani yake, kama vile kunena kwa lugha, kutoa unabii, kufundisha, kuhubiri n.k…na mtu yeyote asipodhihirisha mojawapo ya karama yoyote basi huyo bado hajapokea Roho Mtakatifu na maandiko wanayoyasimamia ni haya …

Matendo 2:17 “Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri”

Na ….

1Wakoritho 12:4 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule”:

Vile vile wapo wengine wanaoamini kuwa uthibitisho wa Roho Mtakatifu, ni kuwa atakuongoza na kukutia katika kweli yote sawasawa na Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.” ….

na hivyo uthibitisho mwingine wowote mbali na huo ni uongo..

Halikadhalika wapo wanaoamini kuwa uthibitisho pekee wa Roho Mtakatifu ni pale anapokushuhudia ndani yako kuwa wewe ni mwana wa Mungu, …sawasawa na Warumi 8:16 “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;”

Wapo wengine wanaoamini uthitisho wa Roho Mtakatifu peke yake ni kukufanya uwe mtakatifu kama vile jina lake lilivyo.…

Na makundi mengine mengi…

Lakini swali ni kama lile lile tu la watu wa agano la kale, je! Wote hawa ni waongo?…Jibu ni hapana wote wapo sawa kabisa!!, isipokuwa tu wanashindwa kutofuatisha utendaji kazi wa Roho Mtakatifu juu ya mtu kulingana na wakati na majira. Kama tu vile wale wa agano la kale walivyoshindwa kufahamu kuwa kuna kuja kwa kwanza kwa Kristo na kuja kwa pili.

Ifahamike kuwa Bwana Yesu aliposema hakuna mtu anaweza kuja kwake kama hakuvutwa na Baba yake aliyempeleka, alimaanisha kusema vile, Leo hii “huwezi hata kuchomwa moyo na maneno ya Mungu kama siyo matunda ya Roho Mtakatifu yanayofanya kazi ndani yako”, ukiona tu unaamini kuna Mungu, ukiona unatamani kumfahamu Mungu hata kama hujaokoka, ukiona unahukumiwa ndani yako kwa ajili ya dhambi zako, ukiona una hofu ya Mungu, basi ufahamu kuwa huyo ni Roho Mtakatifu anatenda kazi ya kukuvuta kwake,..Jambo ambalo si watu wote wanalo, usidhani kuwa injili unayoisikia na kukuchoma moyo inamchoma kila mtu duniani, dhambi uzifanyazo na kusikia kuhukumiwa zinamuhukumu kila mtu duniani, kama ingekuwa hivyo kusingekuwa na vitendo vya kinyama unavyoviona kila mahali..Si wote wapo hivyo, na ndio maana hupaswi kuichezea hiyo neema kwasababu kuna wakati utafika Roho Mtakatifu hatakuvuta tena kwa Mungu, ukishafika huo wakati ndugu, hata Bwana Yesu mwenyewe akutokee hapo, na malaika wote mbinguni, hutakaa ugeuke, kwasababu Roho wa kukuvuta hayupo.

Sasa, ikitokea mfano Yule mtu akautii ule wito na kuamua kutubu dhambi zake, na kufuata vigezo vyote alivyoambiwa na Bwana Yesu vya kwenda kubatizwa, katika maji mengi na kwa Jina la BWANA YESU, hapo ndipo Yule Roho aliyekuwa anamvuta anapata kibali cha kuingia ndani yake, na kufanya maskani humo, na akishaingia anakuwepo huko milele, mtu huyo ndio anakuwa amezaliwa mara ya pili..Sasa kwa kuwa Yule mtu bado ni mchanga kiroho, Roho Mtakatifu anaanza kazi kadha wa kadha ndani yake..mojawapo ni kumsafisha na kuua baadhi ya vitu ambavyo alikuwa hawezi kuviacha, Roho Mtakatifu anamfanya upya tena..

Tito 3:5 “si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;’’

Anaanza kumfanya aupende utakatifu kuliko kitu kingine chochote, hapo ndipo hamu ya baadhi ya mambo ya kidunia inakufa kabisa…hizo ni dalili za awali kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako..Kwa nje unaweza usione chochote, wala usisikie msisimko wowote lakini ndani kunawaka moto wa kutaka kuwa kama Mungu..

Pili anatenda kazi ya kumwongoza na kumtia katika kweli yote: Hapa Anaanza kumwongoza katika vyanzo sahihi vya Neno lake, anaanza kumpa kiu ya kujifunza Neno la Mungu, faraja yake mtu huyo inakuwa kwenye Neno la Mungu tu, na si mahali pengine, anaanza kuona Mungu kwake ndio kila kitu..Uthibitisho ni kuwa hapo kabla hayo mambo alikuwa hayaoni…Ile kiu inaongezeka siku baada ya siku.

Jambo lingine analolifanya Roho Mtakatifu ni kumshuhudia huyo mtu kuwa yeye ni mwana wa Mungu, kushuhudiwa huku sio kusikia sauti inakuambia wewe ni mwana wa Mungu, hapana, bali ni kuona maisha yako unayopitia yanafanana na wana wote wa Mungu waliopita huko nyuma,…..yaliyowapata watakatifu wa nyuma na wewe yanakupata yawe ni mema yawe ni mabaya..Biblia ndio itakuwa uthibitisho wako..Mungu kwako anajidhihirisha kama Baba.

1Petro 5:9 “….mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.”

Jambo lingine ni anakuwa kwako kama mfariji, na mshauri(1Thesalonike 1:16, 2Wakoritho 13:14)): Utaona tu, jinsi atakavyokuwa anakutia nguvu wakati baada ya wakati, unapoishiwa nguvu, utashangaa anaachilia jambo Fulani kubwa ambalo linakupa nguvu ya kuendelea mbele kwa muda mrefu sana…Na ndio maana tunasema mtu yeyote aliye na Roho Mtakatifu kweli hawezi kuishia njiani katika safari yake ya wokovu..(Isaya 40:27-31)

Na ndio maana katika hicho kipindi chote Roho wa Mungu anachokutengeneza, hupaswi kumzimisha,..Wengi wanamzimisha kwa kuanza kuyarudia yale machafu waliyoyaacha huko nyuma, tayari Mungu alishawafanya kuwa huru, lakini bado wanaurudia utumwa..Hapo ndipo mtu hakui wala hasongi mbele kiroho, anabakia kuwa katika hali ile ile, miaka nenda miaka rudi..yeye ni mchanga tu.

Lakini ikiwa mtu huyu atatembea na Roho Mtakatifu kwa uaminifu wote, Roho anakuwa anajaa ndani yake kidogo kidogo, mpaka anafikia ujazo kamili wa Roho Mtakatifu, na ujazo huo ni uhitimu. Hapo ndipo Roho Mtakatifu anakuvika nguvu za kuweza kuwa shahidi wake, kama vile Bwana Yesu alivyoaambia mitume wake..

Matendo 1:8 “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi”.

Hichi ndio kile kilichomkuta Bwana Yesu wakati ule anakwenda kubatizwa, sio kana kwamba ile ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kumpokea Roho hapana bali Roho alikuwa naye tangu kuzaliwa kwake, lakini kwasababu ya kazi ilimpasa Mungu amwongezee nguvu kwa Roho Yule aliyekuwa ndani yake ili kushuhudia habari za ufalme wa mbinguni. Na ndicho kilichokuwa juu ya Mitume sio kwamba kipindi walichokuwa wanatembea na Bwana walikuwa hawana Roho Mtakatifu, walikuwa naye, ndio yule aliyemfunulia Petro kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu n.k isipokuwa walikuwa naye si katika kile kiwango kile Mungu alichokikusudia kwa kazi yake waliyokuwa wanakwenda kuifanya hapo mbele.

Ndivyo ilivyo hata sasa, wengi tunatamani tupokee Roho Mtakatifu katika hatua ya mwisho, lakini sio kuanzia katika hatua ya kwanza.. siku hiyo hiyo tumempa Kristo maisha yake, bado siku hiyo hiyo wanataka Roho Mtakatifu atupe nguvu ya kuwa mashahidi wake kwa mfano wa mitume,..Ni kweli Roho anaweza kufanya yote kwa pamoja, lakini fahamu kuwa ndani yake, bado utakaa chini tu akufundishe,atembee na wewe, akuandae na akuthibitishe.

Hivyo kaka/dada, fahamu kuwa Roho Mtakatifu ni zaidi ya kunena kwa lugha, au kuona maono..Usifurahie kusema tu nilipokea Roho Mtakatifu siku ile nilipoamini,,jiulize je! Hadi sasa Roho Mtakatifu anatembea na wewe, au ulishamzimisha siku nyingi..Je! anakurudisha katika utakatifu?, Je! Anakushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu. Je! Anakuongoza katika kweli yote..Je! anakupasha bahari ya mambo yanayokuja?..Ikiwa hivi vitu vimekufa ndani yako, tubu upesi umgeukie Mungu, mwambie Bwana nataka nianze na wewe upya.

Na ikiwa bado Roho Mtakatifu yupo mbali na wewe nikimaanisha kuwa hujamkabidhi bado Bwana maisha yako, fahamu kuwa biblia ipo wazi inasema, Warumi 8:9… “Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Pasipo huyo, usidhani kuwa utaiona mbingu, au utamfahamu Mungu..Tubu leo kwa kumaanisha kumfuata Kristo itii injili, kisha nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la Bwana Yesu Kristo, Roho Mtakatifu aingie ndani yako na aanze kufanya kazi kwako.

Bwana akubariki sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazondana:

Je! Umepokea kweli Roho Mtakatifu?

Hatua za Roho Mtakatifu katika kutuongoza.

Je! karama ni uthibitisho pekee wa kuwa na Mungu?

HOME

Print this post