Category Archive Home

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

Wimbo Ulio Bora 8:6-7

[6]Nitie kama muhuri moyoni mwako,  Kama muhuri juu ya mkono wako;  Kwa maana upendo una nguvu kama mauti,  Na wivu ni mkali kama ahera.  Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu.

[7]Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.

Habari hiyo inamzungumzia Bwana arusi ambaye anataka kuingia katika mahusiano ya ndani na bibi arusi wake, hivyo anaanza kwa kumwomba amkubali Kama “Muhuri” .

muhuri huwa unawakilisha umiliki halali wa kitu hicho..

Hivyo huyu Bwana arusi anamtaka bibi arusi akubali muhuri wake, katika  moyo wake na katika mkono wake…pande mbili…moyoni ikiwakilisha ndani yake na mkononi nje, yaani upendo wa ndani na ule upendo wa nje…kumilikiwa kwa ndani lakini pia kumilikiwa kwa nje..

Na matokeo Ya kufanya hivyo ndio hapo anaendelea kueleza sifa za huo upendo akisema upendo una nguvu kama mauti…yaani Kama vile mauti isivyo pingika juu ya mtu, kwamba kufa atakufa tu, vivyo hivyo upendo wa kweli ukimnasa mtu haupingiki..atamlinda tu.

lakini pia anasema wivu wake ni mkali kama Ahera,  ni mfano huo huo, maana yake hauvumilii maovu, pale unaponajisiwa…ni lazima utatoa tu matokeo..unakula Kama moto moyoni…ndio Uliomla Bwana Yesu alipoona nyumba ya Baba yake imegeuzwa kuwa pango la wanyang’anyi akatengeneza kikoto na kuanza kuharibu kwa makusudi kazi zote za kipepo zilizokuwa zinaendelea pale hekaluni…wivu wa upendo huharibu lakini vile vilivyo viovu.

Bado anasema ‘maji mengi na mito Haviwezi kuuzima, Kama mtu angetoa badala ya upendo  Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa’

yaani hata mtu akijaribu kuuzimisha kwa hongo za kifedha anafanya kazi bure…

Ni kufunua nini rohoni?

Nguvu ya upendo wa Kristo kwetu pale tunapoupokea vizuri..tunakuwa salama milele ndani Yake..

Lakini Hatua ya kwanza Kristo anataka kututia muhuri wake moyoni na mkononi…na muhuri huo ni Roho Mtakatifu (Waefeso 4:30), anataka udhihirisho wa Roho uonekane mioyoni mwetu, lakini pia mwilini (kwa matendo yetu).

Utakatifu wa ndani na nje.

Kuna Watu wanampokea Yesu moyoni tu, lakini badiliko la nje hawana habari nalo, wanamkiri kwa vinywa vyao lakini kwa matendo yao wanamkana..

Tito 1:16

[16]Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.

Hapo bado upendo wa kweli haujafunuliwa…lakini pale tunapodhamiria kumpokea Kristo Kwelikweli, basi nguvu ya upendo wake inatunasa na matokeo yake yanakuwa hata tufani ya namna gani ije, yeye mwenyewe anatushika, hata dunia nzima itutenge bado hatuwezi tikiswa, hata tuahidiwe utajiri na mali zote duniani, bado upendo wetu hauwezi kupungua kwa Kristo, kwasababu ni yeye mwenyewe aliyetunasa kwa agano la muhuri rohoni na mwilini.

Yesu alisema…

Warumi 8:35-39

[35]Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

Bwana akubariki.

Je upo tayari leo kuokoka? Kama ni ndio basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii kwa msaada huo bure.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO

Maombi Maalumu ya Kuombea Ndoa.

Print this post

USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO


Wimbo Ulio Bora 5:2-6

[2]Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! 

Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, 

Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku. 

[3]Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje? 

[4]Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake. 

[5]Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane,  Penye vipini vya komeo. 

[6]Nalimfungulia mpendwa wangu,  Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; 

(Nimezimia nafsi yangu aliponena), 

Nikamtafuta, nisimpate,  Nikamwita, asiniitikie. 

Habari hii inaeleza kisa cha mtu na mpenzi wake, ambayo inafunua mahusiano ya mtu na Kristo, na jinsi mwitikio Wake unavyopaswa uwe.

Hapa anaonyesha mwanamke mmoja akiwa ndani usiku amelala peke yake na mara akasikia mpenzi wake anabisha Mlango amfungulie, 

Lakini  alijawa na uzito, akaanza kukawia-kawia, pengine huwenda kwasababu ya starehe ya kitanda, au kuna mambo yake mengine ya siri alikuwa anayafanya

Lakini bado mpenzi wake aliendelea kugonga, bila mafanikio ya kufunguliwa…na safari hii akatoa mpaka maneno ya upendo yamkini yatamshawishi ili aje kufungua kwa haraka. Lakini bado hakufua dafu.

Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, 

Mpaka dakika ya mwisho, alipogonga, na mbisho ule kuingia moyoni mwa yule mwanamke, ukamchoma ndipo akatoka haraka na kwenda kumfungulia..

Lakini kwa bahati mbaya hakumkuta, kumbe tayari alishaondoka…akaanza kutoka kumtafuta bila mafanikio..na matokeo yake huko nje kukutana na madhara mengine.

Ni nini Kristo analifundisha kanisa lake?

Hili ni jambo ambalo watu wengi humfanyia Kristo rohoni sasa…Anasema..anasema..

Ufunuo wa Yohana 3:20

[20]Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 

Lakini watu hukawia-kawia kwasababu ya udanganyifu wa mambo Ya duniani, mwingine atasema ngoja kwanza nimalize ujana, ndio nitaokoka, mwingine ngoja nipate kazi mwingine ngoja niolewe, mwingine ngoja ifike mwakani, mwingine ngoja nikimaliza masomo ndio nitampokea Yesu..n.k

Ndugu Saa ya wokovu ni sasa Kristo anakuita, wakati ndio huu, usipoufungua moyo wako sasa, utafika Wakati utamtafuta Kristo na hutampata…

Luka 13:24

[24]Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze. 

Luka 12:36-40

[36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 

[37]Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 

[38]Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 

[39]Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 

[40]Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu. 

Okoka leo ndugu, neema ya wokovu ipo sasa lakini haitadumu milele..hiyo sauti inayoita moyoni mwako itii, haraka, starehe za duniani zinapita, maisha yanapita,  ikiwa upo tayari kumkabidhi Bwana maisha yako, basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure kwa msaada huo..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mshulami ni msichana gani?

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).

Print this post

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

Wimbo Ulio Bora 3:1-4

[1]Usiku kitandani nalimtafuta mpendwa wa nafsi yangu, Nalimtafuta, nisimpate.

[2]Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,  Katika njia zake na viwanjani,

Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu. Nikamtafuta, nisimpate.

[3]Walinzi wazungukao mjini waliniona; Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?

[4]Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea, Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu; Nikamshika, nisimwache tena,  Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,  Chumbani mwake aliyenizaa.

Kitabu cha wimbo ulio-bora, ni kitabu ambacho huchukiliwa kimwili na watu wengi kana kwamba kiliandikwa mahususi kwa wana-ndoa.. Jambo ambalo sio kweli, Ikumbukwe kuwa dhumuni kuu la biblia ni kutueleza WAZO la Mungu, juu yetu ambalo hilo alilikamilisha kifasaha kupitia Yesu Kristo. Hivyo popote pale unapopasoma kwa namna moja au nyingine inaeleza kusudi la Mungu kwetu, katika kuyatimiza mapenzi yake..

Na ni kawaida yake tangu zamani  kutumia mifano halisi ya namna mbalimbali ili kudhihirisha kusudi lake kamilifu kwetu.

Kwamfano ameweka familia, tujue sifa za wazazi ili tunapomwita Mungu Baba, tujue tabia za ubaba hasaa zipoje…Ameweka mabwana na watumwa ili tunapomwita yeye Bwana tujue sisi tunapaswa tuweje kwake kama watumwa..

Vivyo hivyo ameweka ndoa, na akajifunua kwetu kama mume, na sisi kanisa ni mke wake…Hivyo anataka tujue kama vile upendo wa mke na mume ulivyo ndivyo alivyo yeye kwetu sisi.

Sasa Katika habari hii, tunaona sifa ya upendo ambao Mungu anataka sisi tuuonyeshe kwake, Upendo usio ule wa upande mmoja, bali na upande wa pili, yaani sio  tu yeye kututafuta sisi wakati wote hapana bali Na sisi tumtafute yeye..

Anaeleza kwa mfano wa igizo picha ya  mwanamke ambaye yupo sikuzote na mpenzi Wake kitandani, lakini ikatokea siku moja alipoamka usiku hakumwona kitandani Mwake…

Hivyo hakuweza kuendelea kulala angali mumewe hayupo, ikambidi atoke aanze Kumtafuta usiku ule ule, sio kwa siri Bali hadharani tena sehemu zenye hatari ambazo walinzi tu usiku hupita kufanya doria..Na alipokutana Nao akawauliza juu ya mpenzi wake kama wamemwona, lakini Baadaye kidogo alimwona..akamkumbatia na kurudi naye mpaka mahali pao maalumu.

Ufunuo wake ni upi.

Yapo majira wewe kama mwana wa Mungu utapitia pengine hali fulani ya kushuka viwango kiroho, (ukame wa kiroho)

Lakini ukiwa na upendo wa kweli kwa Mungu wako, ni wazi kuwa hutakaa tu na kusema Mungu nisaidie…Hapana Utachukua tu hatua kama za huyu mwanamke ya kuamka na kuanza kutafuta namna ya kumtafuta mpenzi wako (Kristo) yaani kurejesha viwango vyako vya mwanzoni, hata kwa kugharimika raha, au vitu n.k..

Ndio hapo mtu hutenga muda mwingi wa maombi, mikesha, mifungo n.k.

Na kama vile yule Mwanamke alipowafuata walinzi usiku, kuwauliza habari za mumewe…Ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye kiu na pendo na Mungu hataridhika kutembea yeye kama yeye tu, ataulizia msaada mpaka kwa viongozi wake wa kiroho apate mwongozo..(ambayo hufunua wale walinzi). Na hatimaye kufikia kilele cha mahusiano na Mungu wake tena.

Ndugu, kumbuka kuwa furaha, na amani, uzuri wa Kristo sio tu wa kuletewa sikuzote, bali pia wa kutafuta…Ni kweli siku za kwanza za wokovu uliona Kristo akijifunua Kwako kwa namna za ajabu, hata kama hukufanya lolote lakini sasahivi ni kama huoni moto ule ule uliokuwa nao…jua tu si kwamba umetenda dhambi au umemkosea Mungu…hapana ni kwamba Mungu anataka amke sasa mtafuta mpenzi wako..kudhihirisha upendo wa kweli..

Ndicho Yesu alichowaambia wale waandishi na mafarisayo juu ya wanafunzi wake..

Marko 2:18 Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile

Ongeza mikesha, mifungo, kusoma Neno sana…Na hatimaye utavipata na furaha yako itazidi ile ya kwanza…

Kwasababu upendo wa kweli hutafuta…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Naomba kujua maana ya haya maneno katika biblia..“Siti Msharifu”, “Mitalawanda” na “kulalama”

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Print this post

Maombi Maalumu ya Kuombea Ndoa.

Ikiwa wewe ni mwanandoa, ni busara kuwa na maombi yako maalumu kwa ajili ya ndoa yako.

Waweza kutenga siku kadhaa katika wiki, au mara mbili katika wiki, kuwa na maombi maaalimu marefu kwa ajili ya ndoa yako. 

Maombi ni nyenzo muhimu katika kuendesha na kufanikisha sehemu zote zamaisha yetu,  huduma inahitaji maombi, kanisa linahitaji maombi, taifa linahitaji maombi, wewe unahitaji maombi, vivyo hivyo na ndoa yako pia inahitaji maombi ili iwe na ustawi Bora katika nyanja zote..hata kama huoni tatizo lolote ndani ya ndoa ..bado unahitaji maombi sana.

 

Kwanini maombi? Ni kwasababu njia pekee ambayo Mungu huweza kuyaingilia maisha yetu ili ayatengeneze vema basi ni kwa njia ya maombi.

 

Ndoa inaweza ikadumu lakini isiwe na amani, ndoa inaweza ikawa na amani lakini isiwe na mafanikio, ndoa inaweza ikawa na mafanikio lakini imekosa Mungu, vilevile inaweza ikawa na umoja lakini imejaa wivu, inaweza ikawa haina shida lakini watoto wanaokuja wakawa na matatizo, inaweza pia ikawa sawa leo, lakini kesho shetani akaishambulia….Hivyo suala la kuombea ndoa ni jambo la muhimu sana.

 

Huu ni mwongozo wa maeneo muhimu ya  kuombea kila uingiapo katika maombi ya namna hii. (Kila kipengele tumia dakika 30)

1) Umoja na Mshikamano.

Mungu alipomuumba mwanaume na mwanamke na kuwaleta katika ndoa aliwafanya mwili mmoja tena..Maana yake aliweka Muunganiko usiowezekana kibinadamu Wa umoja..

Mathayo 19:5

[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? 

 

Hivyo hakikisha unaombea ndoa yako Bwana adumishe umoja wenu, uwe umoja kwelikweli, na kamwe pasiwepo matengano. Maana huo ndio mwanzo wa ndoa thabiti

Omba kwa nguvu, huku ukivunja roho za matengano, ukiangalia zaidi maeneo ambayo unaona kabisa yanahatarisha umoja wenu, yenye dalili ya kutaka kuwaachanisha hayo ndio uyaombee zaidi, ikiwa ni kazi, au watu, au magonjwa, mwambie Bwana apatengeneze hapo..tumia si Chini ya dk. 30 kuombea eneo hilo moja tu.

2) Upendo na utii

Hivi viwili navyo ni nyenzo kubwa sana katika ndoa thabiti. Bwana aliagiza mwanamume ampende mke wake kama mtu apendavyo mwili wake mwenyewe.. vivyo hivyo aliagiza mke amtii mumewe Kama mtumwa kwa Bwana wake.

 

Waefeso 5:22-25

[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 

[23]Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 

[24]Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 

[25]Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 

Hivyo ikiwa wewe ni mke, mwombee sana mumeo Bwana alidumishe pendo lake kwako, lakini pia ikiwa wewe ni mume mwombee mkeo Bwana amjengee utii kwako.

Lakini pia jiombee wewe sawasawa na jinsia yako Bwana akuzidishie upendo na utii..kwasababu vyote hivi ni nyenzo kwa wote, vizidi bila kupungua nguvu kwa jinsi siku zinavyokwenda.

 

3) Maelewano na Amani.

Ndoa ikikosa maelewano hupoteza dira yake.

 

i)  Omba Mungu ajenge usemi mmoja yaani lugha ya maelewano kwanza katika eneo lenu la kiroho.. Maana yake wote msisimame katika Bwana (muokoke), ikiwa mmojawapo hajaokoka mwombee neema Ya wokovu, injili imchome abadilike na kumpokea Kristo, na huku ukimhubiria pia.

ii) Omba pia Mungu awape Maelewano Katika majukumu yenu ya kiroho(utumishi). Mfano ratiba za ibadaza nyumbani,  maombi,  mikesha, mifungo, ushuhudiaji, na utoajik.

Ikitokea mmoja wenu haafiki majukumu hayo, si rahisi mwingine kutekeleza na matokeo yake inakuwa ni kushindwa kutimiza lengo kuu la kindoa. Kumbuka mmewekwa katika ndoa ili mumtumikie Mungu pamoja..hivyo jambo hilo ni lazima Lipewe nafasi ya kwanza na kubwa katika ndoa.

iii) Lakini pia omba maelewano katika mambo Yote ya kimaisha.

Mfano mikakati ya kimaendeleo, matumizi ya kifedha, n.k. huku ukigusia Maeneo yako yote ambayo unaona mikwaruzano inatokea, Au dalili hizo kutokea..ukiharibu hivyo vyanzo kwa maombi yako.

iv) Lakini pia Bwana awajengee mioyo ya kusamehe na kuachilia.

Ndoa nyingi zimeingia dosari, kupoa hata kufikia hatua ya kuvunjika kabisa kutokana na kuwa zimepoteza mioyo wa kusamehe na kuachilia Kwasababu ya majeraha au makosa yaliyofanyika nyuma..

Wakolosai 3:13

[13]mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

Mwambie Bwana sikuzote, wote mpewe mioyo ya kusamehe na kuachilia.

4) Uaminifu

Hapa pia ni mahali pa kupaombea sana.. Wengi wanadhani wanaweza linda ndoa zao kwa kuweka sheria kali, kwa kufuatilia nyendo zao, kwa kuwavisha mavazi ya kuficha mpaka nyuso, Lakini uhalisia ni kwamba ikiwa mtu amekosa uaminifu, huyo kamwe halindiki, atakuzunguka tu, Hivyo omba kwa Bwana juu ya mwenzi wako, na kwako pia Bwana awaumbie moyo wa uaminifu. Hilo linatosha kuwa ulinzi mkubwa kwa ndoa yako.

5) Uvumilivu.

Nyuma ya mafanikio ya kitu chochote chema, ni lazima utaona uvumilivu ulipewa nafasi, hata  huduma ya  kufanikiwa hutegemea uvumilivu. Ndoa haimaanishi kila siku itakuwa ni furaha tu, zipo nyakati za kupishana kibinadamu, za kusemwa vibaya, za kuudhiwa zipo nyakati za kupungukiwa, yapo madhaifu pia.. Hivyo omba moyo wa uvumilivu thabiti uwe juu ya kila mwanandoa.. kuanzia wewe mwenyewe.Ili nyakati ngumu zitakapopita pasiwe na wepesi wa kuiacha ndoa au kuchukua Hatua za madhara.

6) Maongozi ya Mungu

Ndoa ikikosa mwelekeo wa ki-Mungu huishia pagumu. Omba Mungu awape dira sahihi isiyo na majuto katika mikakati yenu yote ya kimaisha.

Omba Bwana ayanyoshe mapito yenu, awafanikishe, awaepushe na njia ya majuto na upotevu wa yule mwovu.. kwasababu maandiko yanatuonyesha ndoa ya kwanza ilivamiwa na uharibifu kwasababu ya udanganyifu wa ibilisi, kwa kitendo cha Hawa kusikiliza na kuifuata njia nyingine ambayo hakuagizwa na Mungu, na matokeo yake alipokula tu lile tunda ikasababisha matatizo makubwa ambayo mpaka sasa tunayaona ..

7) Kibali na maelewano kwa ndugu na wakwe 

Mafanikio Ya ndoa hutegemea pia mahusiano mema kwa ndugu na wakwe..Musa alifanikiwa kuiongoza huduma vizuri kwasababu alikuwa na mahusiano mazuri na mkwe wake Yethro. Ruthu alifanikiwa kuolewa na Boazi mtu mkuu na mwenye uwezo kwasababu alikuwa na ukaribu na mama mkwe wake Naomi hata baada ya kufiwa na mumewe.

Vivyo hivyo na wewe pia uhusiano wako ukiwa mzuri na watu wa upande wa mwenzi wako unaharakisha baraka na neema nyingi za Mungu.

Lakini pia ikiwa mahusiano ni mabovu, basi ndio utumie fursa hii kuombea utapatanisho haraka, sana. Eneo hili ni muhimu sana kuliombea, ijapokuwa wengi hulipuuzia.

8) Watoto

Ikiwa ni ndoa ambayo tayari inayo watoto ni muhimu kuwaombea watoto wako daima, wasiwe chanzo cha nyinyi kufarakana, lakini kuwa mwiba na uchungu kwenye ndoa yenu.

Lakini ikiwa bado hamjawa na watoto, ombea uzao wako ujao ukawe faraja na neema kwenu. Watoto wakiwa wabovu wanaweza kuihatarisha ndoa yako, au kuifanya isiwe na amani. Hivyo waombee sana wokovu, ulinzi, afya, adabu.

Shalom.

Ukizingatia kuviombea vipengele hivyo, kila kipengele si chini ya nusu saa. (dakika 30), utaona neema kubwa sana ya Mungu ikifanya kazi katika maisha yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

NDOA NA TALAKA:

Print this post

Kudhihaki ni nini kibiblia?

Kudhihaki kibiblia ni kitendo cha kumbeza au kumkejeli mtu, shetani au Mungu, (maana yake kumfanya yule mtu aonekane hana heshima, au hana maana), dhihaka pia anaambatana na dharau, utani na hata matusi.

Katika Biblia tunaona kuna watu waliwadhihaki wanadamu wenzao, na wengine walimdhihaki ibilisi na ufalme wake, na wako waliojaribu kumdhihaki Mungu wa mbingu na nchi,..kwa ufupi tuitazame mifano hiyo.

    1. DHIHAKA KWA MWANADAMU.

     Dhihaka ya Ishmaeli kwa Sara.

Tunasoma kipindi Hajiri amempata Ishmaeli kwa Abrahamu, mtoto Ishmaeli alianza kumfanyia dhihaka mamaye mkubwa Sara, na matokeo yako ni kufukuzwa yeye pamoja na mama yake..

Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka”.

Utasoma pia dhihaka za watu kwa watumishi wa Mungu katika 2Nyakati 36:16, Nehemia 4:1, Na pia sehemu nyingine utaona Mungu anawafanyia dhihaka wanadamu wanaoenda kinyume na shauri lake (Soma Zab 2:4 na Zab 59:8).

    2. DHIHAKA KWA SHETANI NA UFALME WAKE.

Kuna wakati Nabii Eliya alimdhihaki mungu-baali pamoja na makuhani wake.

1Wafalme 18:27 “Ikawa, wakati wa adhuhuri, Eliya akawafanyia dhihaka, akasema, Mwiteni kwa sauti kuu; maana ni mungu huyo; labda anazungumza, au ana shughuli, au anasafiri, au labda amelala, sharti aamshwe.

28 Wakapiga kelele, wakajikata-kata kwa visu na vyembe kama ilivyo desturi yao, hata damu ikawachuruzika”.

   3. DHIHAKA YA WANADAMU KWA MUNGU.

Hakuna mahali popote mwanadamu amefanikiwa kumdhihaki Mungu, kwasababu Mungu hadhihakiwi..

Wagalatia 6:7 “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

8 Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele”.

Wapo waliojaribu kumdhihaki Mungu katika biblia lakini walikuja kujua baadaye kuwa Mungu hadhihakiwi.. Mfano wa hao, ni wale watumwa wa mfalme wa Shamu waliomdhihaki Mungu kwa kusema ana uwezo wa kuokoa tu milimani na si nchi tambarare, na matokeo yake waliziona kazi zake.

1Wafalme 20:23 “Basi watumwa wake mfalme wa Shamu wakamwambia, Mungu wao ni mungu wa milima; ndiyo sababu ya kutushinda sisi; lakini na tupigane nao katika nchi tambarare, na hakika tutawashinda wao.

24 Ufanye neno hili; uwaondoe hao wafalme, kila mtu atoke mahali pake, ukaweke majemadari mahali pao.

25 Kisha ujihesabie jeshi, kama jeshi lililokupotea, farasi kwa farasi na gari kwa gari; nasi tutapigana nao katika nchi tambarare, na bila shaka tutawashinda. Akaisikiliza sauti yao, akafanya kama hivyo.

26 Basi ikawa mwakani, Ben-hadadi akawahesabu Washami, akakwea mpaka Afeki ili apigane na Israeli.

27 Wana wa Israeli nao wakahesabiwa, wakapewa vyakula, wakaenda kupigana nao; wakatua wana wa Israeli mbele yao kama vikundi viwili vya wana-mbuzi; bali Washami wakaijaza nchi.

28 Akaja yule mtu wa Mungu, akamwambia mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Kwa sababu Washami wamesema, Bwana ni Mungu wa milima wala si Mungu wa nchi tambarare; basi nitawatia makutano haya yote walio wengi mkononi mwako, nanyi mtajua ya kuwa ndimi Bwana.

29 Wakatua kuelekeana muda wa siku saba. Ikawa siku ya saba vikapangwa vita; wana wa Israeli wakawapiga miongoni mwa Washami siku moja watu mia elfu waendao kwa miguu.

30 Lakini waliosalia wakakimbia mpaka Afeki, mjini; na ukuta ukaanguka juu ya watu ishirini na saba elfu waliosalia. Ben-hadadi naye akakimbia, akaingia mjini, katika chumba cha ndani”.

Kwahiyo Mungu hadhihakiwi wala hajaribiwi wala hapimwi, wana wa Israeli jangwani walijaribu kumpima na maandiko yanasema wakayaona matendo yake..

Zaburi 95:8 “Msifanye migumu mioyo yenu; Kama vile huko Meriba Kama siku ya Masa jangwani.

9 Hapo waliponijaribu baba zenu, Wakanipima, wakayaona matendo yangu.

10 Miaka arobaini nalihuzunika na kizazi kile, Nikasema, Hao ni watu waliopotoka mioyo, Hawakuzijua njia zangu.

11 Nikaapa kwa hasira yangu Wasiingie rahani mwangu”.

Kwa hitimisho hatupaswi kudhihakiana sisi kwa sisi, wala kuwadhihaki watumishi wa Mungu, wala tusijaribu kumdhihaki MUNGU wa mbingu na nchi kwani yeye hadhihakiwi, lakini tunaweza kudhubutu kumdhihaki shetani na majeshi yake, kwa lengo la kumpa Mungu utukufu, na si kujiinua sisi, ikiwa tumesimama vyema na MUNGU, lakini  kama hatujasimama vyema na Mungu, kumdhihaki shetani ni hatari, na kuleta matokeo kama yale yaliyowateka wana wa Skewa (Soma Matendo 19:13-17).

Pia kama umeokoka Biblia imesema tutapitia vipindi vya dhihaka tu (soma) kama Bwana wetu YESU KRISTO pamoja na wanafunzi wake  alidhihakiwa sisi ni akina nani? (soma Luka 22:63, Matendo 2:13 na Waebrania 11:36) lakini yote katika yote tunafundishwa kusamehe, na kuvumilia, kwasababu siku za mwisho ilishatabiriwa kuwa watakuja watu wa kudhihaki wengi (Soma 2Petro 3:3 na Yuda 1:18)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HASIRA YA MUNGU KUKUWAKIA, KWA KUTOMZUNGUZIA TU MUNGU IPASAVYO.

Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. 

NI NANI ALIYEWAONYA KUIKIMBIA HASIRA ITAKAYOKUJA?

Je Daudi aliwachukia viwete na vipofu? (2Samweli 5:6-9)

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Print this post

Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)

SWALI: Silaha za Nuru ni zipi?

Warumi 13:12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru


JIBU: Ni lazima tufahamu ulimwengu wa roho upo katika pande mbili,

  1. Upande wa nuru
  2. na upande wa giza..

Upande wa Nuru ni wa Kristo (Yohana 1:4-5), na upande wa giza ni wa ibilisi.

Na pande hizi hazijawahi kupatana hata kidogo, na kama hazijawahi kupatana maana yake zipo vitani na kama zipo vitani basi zote zina silaha zake, kuhakikisha zinajilinda, lakini pia kushambulia, ili kuua utawala mwingine. Ndio hapo kwanini tunaambiwa tuzivae silaha za nuru. Maana yake mtu anaweza akawa ni wa nuru lakini akawa hana/hajui kuzitumia silaha za Nuru.

Vifungu vifuatavyo ni kututhibitishia kuwa Nuru na giza vipo katika mapambano;

2Wakorintho 6:14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

 

Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru.
13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake

 

Sasa silaha za Nuru ambazo mtu akiwa nazo ataweza kujilinda na mashambulizi ya giza, lakini pia ataweza kuushinda ufalme wa giza ni hizi;

  1. Neno la Mungu.
  2. Haki (Ya Mungu katika Kristo Yesu)
  3. Kweli (Usahihi wa kimaandiko)
  4. Utakatifu
  5. Imani
  6. Injili
  7. Maombi

Silaha hizi, ndio zile zinazotajwa pia kwenye Waefeso 6:10-18, kama silaha za haki.

  • Kweli Kiunoni
  • Dirii ya Haki kifuani
  • Ngao ya Imani
  • Upanga wa Roho
  • Utayari wa injili ya Amani
  • Sala na Maombi
  • Chapeo ya wokovu

Kwa maelezo marefu juu ya silaha hizi, fungua hapa usome >>>  Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Mtu akiwa na mambo haya, ataweza kulishinda Giza, kotekote.. Ambalo, silaha zake ni kama zifuatazo;

  1. Uongo: Ambao huzaa Mafundisho ya uongo,
  2. Uasherati: Uzinzi, tamaa ya macho,
  3. Majivuno :  Ambayo hupelekea uasi,
  4. Chuki : Huzaa Kutokusamehe, unafki, migawanyo
  5. Hofu : mashaka, kupoteza imani na Mungu
  6. Uchawi na uganga: Huzaa ibada za sanamu, miungu, na uvamizi wa mapepo

Swali ni Je! Umejivika silaha Nuru ?

Ikiwa upo nje ya Kristo, huwezi kusimama, unahitaji wokovu kwanza, ikiwa upo tayari kufanya hivyo wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO

Print this post

HEKIMA ILIYO SAHIHI, KATIKA HIMIZO LA UTOAJI SADAKA.

Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Yoashi aliingiwa na wazo la kutaka kuikarabati nyumba ya Mungu (Hekalu), na kuamsha tena shughuli za kiibada zilizokuwa zimeharibiwa Na watawala wabovu waliotangulia..

Hivyo kwa kuwa alijua ukarabati unahitaji fedha, alichukua hatua ya kuwatoza watu kodi ya nyumba ya Mungu..Ambayo iliagizwa katika torati na Musa..(2Nyakati 24:9)

Hivyo akawateuwa  Walawi, walisimamie jambo hilo tangu mwanzo hadi mwisho, lakini likawa kama linacheleweshwa…

Mpaka baadaye akawauliza tena, kwanini kazi inacheleweshwa, kwa kuona hakuna chochote kilichofanyika..

Lakini mfalme akaja na mkakati mwingine, ili shughuli hiyo ifanyike kwa haraka na wakati, akaona kuliko Kuwalazimisha watu kulipa kodi ngoja aweke sanduku kubwa katika lango la hekalu na kupiga panda kwa watu wote wa Yuda waje kumtolea Mungu wao kwa hiari, bila shuruti..

Na wazo lile likapendwa na watu wengi, na hatma yake makusanyo yakawa mengi, kila siku mpaka wakapata fedha za kuwaajiri wajenzi ili kulikarabati hekalu, na kutengeneza vyombo vya nyumba ya Mungu.

2 Mambo ya Nyakati 24:6-14

[6]Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa BWANA, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?

[7]Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya BWANA wamewapatia mabaali.

[8]Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya BWANA.

[9]Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea BWANA kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.

[10]Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.

[11]Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.

[12]Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya BWANA; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya BWANA, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya BWANA.

[13]Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.

[14]Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya BWANA, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya BWANA, daima, siku zote za Yehoyada.

Ni nini tunafundishwa Na Roho Mtakatifu..

Utoaji wenye baraka na anaouhitaji Mungu ni ule wa hiyari na sio wa kulazimishwa…kama kanisa la Kristo Lazima tufikie hatua hii, kwamba viongozi hawawashurutishi watu kutoa mchango, mfano Zaka, Kama vile himizo la kodi, kwamba usipotoa unachukuliwa sheria ya kinidhamu …lakini pia watu nao wanawajibika wenyewe kumtolea Mungu kwa uaminifu na moyo..kanisa lifikiapo hatua hii ya kiroho, Mungu huliongezea baraka sana.

Usikubali kukumbushwa-kumbushwa, au kuhimizwa-himizwa kumtolea Mungu, Bali mtolee Mungu zaka zako, sadaka zako, kwa moyo wa furaha, Bwana atakubariki.

2 Wakorintho 9:6-8

[6]Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

[7]Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Bwana awabariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?

SWALI: Katika sehemu nyingi kwenye maandiko tunaona, Mungu akiwaagiza watu wake Wamsifu au wamwabudu katika uzuri wa utakatifu, nini maana ya uzuri wa utakatifu?

1 Mambo ya Nyakati 16:29

[29]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;  Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu; 

Zaburi 29:2

[2]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;  Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utautakatifu.

Soma pia..

Zaburi 96:9, 2Nyakati 20:21


JIBU: Kuna mambo mawili hapo.

Jambo la kwanza ni “Uzuri” na jambo la pili ni “utakatifu”

Hasemi tumwabudu Bwana katika utakatifu…hapana bali anasema tumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu..

Kwa namna nyingine anamaanisha hivi; tuuone uzuri ulio katika utakatifu ndio tumwabudu yeye Katika huo.

 

Tunaweza tukaujua utakatifu…ambao mfano wake ni kama vile maisha ya upendo, haki, usafi, adabu, amani, utu wema. n.k. Lakini tusione uzuri wa mambo kama hayo mioyoni mwetu au maishani mwetu…wengine wanaona kama utakatifu wa Mungu ni kitu cha kutisha, lakini kumbe Sio..

 

Siku tukiona uzuri wake ndio hatutakuwa na unafki pale tunapoambiwa tufanye jambo lolote katika utakatifu.. 

 

Kwasababu tusipoona hilo, hatma yake huwa ni kutimiza ibada kama tu agizo fulani au utaratibu wa kidini au nidhamu fulani lakini sio katika furaha na faida tuipatayo katika huo utakatifu.

 

Kwamfano Ibada tu yenyewe ni tendo takatifu lakini je tunaifurahia ibada na kujiona tunanufaika sana mioyoni mwetu katika hizo au tunamtimizia Mungu tu haki yake ya kuabudiwa, lakini hakuna chochote kitufurahishacho ndani yake?

Ibada ifanywayo katika uzuri wa utakatifu ni lazima itaambatana na sifa hizi; 

 

Itakuwa Katika Roho na kweli (Yohana 4:24)

 

Itafanywa Katika Moyo mweupe( Zaburi 24:3-4). Mfano kusamehe, na amani moyoni.

Itajaa shukrani na kumfurahia Mungu: 

Zaburi 139:14

[14]Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa 

Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.  Matendo yako ni ya ajabu, 

 

Itamwadhimisha Mungu na kumfurahia sana, kwa maajabu yake na matendo yake makuu, kwa viwango visivyo vya kawaida

Itaambatana na maisha ya utakatifu:

Warumi 12:1

[1]Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 

Maisha yetu ni ibada tosha, mwonekano wako, uvaaji wako, usemi wako, tabia yako, vitaakisi utakatifu wa Kristo.

Je umeuona uzuri wa Mungu, uzuri wa ibada, uzuri wa kukusanyika, uzuri wa uumbaji wake, ambavyo ndio uzuri wa utakatifu? Kama ni ndio basi utamsifu na kumwabudu pia katika tabia zake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

Print this post

Nini maana ya ‘kupelekea mkono’ (Esta 2:21)

SWALI: Nini maana ya “kupelekea mkono” kama ilivyotumika kwenye maandiko. Esta 2:21

Esta 2:21

[21]Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero.

JIBU:

Kupeleka Mkono, ni neno linalomaanisha “kutaka kudhuru”. Kwamfano katika hiyo habari tunaona Mordekai kama msimamizi wa malangoni pa mfalme aligundua njama za watumishi wenzake wengine ambao walitaka kwenda kumuua mfalme..hatujua aidha kwa kumwekea sumu, au kumchoma upanga, au hatua nyingine yoyote ilitayo madhara.

Kitendo hicho kibiblia, huitwa “kupeleka mkono”

Tunaweza kuona jambo lingine kama hilo, wakati fulani Daudi alimkaribia sana mfalme kwa kiwango ambacho angeweza kumuangamiza kama angetaka..lakini akasema nisinyoshe mkono wangu kwa masihi wa Bwana. Maana yake nisimuue.

1 Samweli 24:4-7

[4]Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia BWANA, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri.

[5]Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.

[6]Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. 

[7]Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake.

Bwana akubariki..

Je umempokea Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yako?

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo.. basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.. Pia kufahamu tafsiri ya maneno mengine ya kibiblia tazama chini.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 1 & 2

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Print this post

Mapokeo ni nini?

Mapokeo ni mafundisho, mifumo au taratibu zisizokuwepo ndani ya Biblia zilizotengenezwa na watu na kurithishwa kutoka kizazi hata kizazi.

Yapo mapokeo yaliyo mema na yaliyo hatari kwa Imani.. Mfano ya mapokeo mazuri yasiyo na madhara katika imani kama endapo yakifanyika kwa ufunuo ni pokeo ya kuadhimisha siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu.. katika Biblia hakuna agizo la kuadhimisha siku ya kufufuka kwa Bwana, hivyo mtu asiyeadhimisha hafanyi makosa, lakini pia anayeadhimisha kwa ufunuo wa kutafakari ufufuko wake, pia hakosei, hivyo huu ni mfano wa pokeo lisilo la hatari.

Na mfano wa mapokeo ambayo ni hatari na yapo kinyume kabisa na Biblia, ni yale yanayofanyika ndani ya  ukatoliki, kama kuadhimisha Ekaristi pamoja na ibada za watakatifu (Hizo hazipo kabisa ndani  ya Biblia), na ni hatari kiroho, kwani kuabudu sanamu au kuitumikia Biblia imekataza jambo hilo katika Kutoka 20:4-5.

Pia mfano wa pokeo lingine lililo baya na hatari kiroho ni ubatizo wa watoto.. Pokeo hili ni maarufu sana lakini ni hatari sana, Kwasababu kwenye Biblia hamna mahali popote watoto wadogo walibatizwa, bali tunaona tu waliwekewa mikono na Bwana Yesu.

Sumu ya mapokeo mabaya  ni ile Bwana Yesu aliyoionyesha katika Marko 7:7-13, kuhusu “Heshima kwa mzazi”

Marko 7:7 “Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu,

8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika MAPOKEO YA WANADAMU.

9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.

10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.

11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, Ni Korbani, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;

12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;

13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa MAPOKEO YENU mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba tunaweza kuishi bila mapokeo na bado tukamwona Mungu na ni vizuri zaidi kuishi bila mapokeo kwani mapokeo mengi yanawafanya watu kuwa mateka wa elimu za uongo, ndivyo Biblia inavyosema..

Wakolosai 2:8 “Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.

9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! taratibu za kufunga ndoa yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?

TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?

KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

Je ni Wokovu gani Simeoni aliouona? (Luka 2:30)

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Print this post