SWALI: Nini maana ya 2 Wakorintho 8:9
isemayo alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
JIBU: Katika sura hii mtume Paulo anawaandikia wakorintho juu ya huduma ya utoaji kwa watakatifu walio maskini katika makanisa mengine, ya mbali
Na hapa anawasisitiza kukubali kutoa kwa kufuata kielelezo cha Kristo katika eneo la neema yake..Jinsi alivyokubali kuwa maskini, kwa kuacha enzi na utukufu na mamlaka juu mbinguni, na kuja duniani, katika hali ya chini sana (ijapokuwa hakuwa duni), ili tu atukomboe sisi tulio katika hali ya ufukara wa roho.
Kwasababu kama asingeweza kujishusha vile, na kukubali kuhesabiwa si kitu (ijapokuwa alikuwa na nguvu), matokeo yake ni kwamba asingekwenda msalabani kusulubiwa kwa ajili yetu tena uchi, na mwisho wake kusingekuwa na msamaha wa dhambi.
Isaya 53:3
[3]Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Lakini sasa tumepokea neema na utajiri wote wa rohoni kupitia yeye kujishusha kwake.
Waefeso 1:3
[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;
Vivyo hivyo Mtume Paulo anawahimiza Wakorintho waige mfano huo huo, katika eneo la kuwahudumia watakatifu wengine. Akitumia mfano wa Wamakedonia ambao walikuwa ni maskini, na wenye dhiki lakini walikuwa tayari kutoa kwa moyo na furaha kwa watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu.
2 Wakorintho 8:1-3
[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; [2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao. [3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Halikadhalika Bwana anataka na sisi tuhudumiane katika ufahamu wa Kristo, yaani kuwa tayari kuwasaidia watakatifu wengine hata katika hali zetu za dhiki.
Lakini mtazamo ambao si sahihi kuhusiana na vifungu hivi ni kudhani kwamba andiko hilo moja kwa moja linamaanisha lengo la Bwana Yesu kuwa maskini duniani ni ili sisi tuwe matajiri kifedha. Ni kweli kupitia Yesu, tunabarikiwa mwilini, lakini hicho sio kinachozungumziwa hapo. Bwana Yesu kuwa maskini ni kutupa utajiri wa roho zetu, pamoja na ule wa ulimwengu ujao.
Bwana akubariki.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)
Kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi ( 1 Wakorintho 7:14)
Nini maana ya waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? (Matendo 11:23)
Rudi Nyumbani
Print this post
SWALI: Je! kulingana na mstari huu, watoto wa wapagani hawataokolewa?
1 Wakorintho 7:14
[14]Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.
JIBU: Ukianzia juu utaona andiko hilo linazungumzia juu ya wandoa wanaoishi pamoja lakini mmojawapo hajaamini. Bwana anatoa agizo kwamba ikiwa bado huyo ambaye hajaamini anaona sawa kuendelea kuishi naye, basi yule aliyeamini asimwache.
Kwasababu kwa kupitia njia hiyo, yule asiyeamini hutakaswa na yule aliyeamini Pamoja na watoto wake pia.
Lakini je mstari huo unamaanisha kuwa mwanandoa mmoja katika familia akiokoka, basi ameiponya familia yote mpaka watoto wake?
Jibu ni la! andiko hilo halikumaanisha hivyo.
Bali linamaanisha kuwa, kwa kupitia yeye, ni rahisi wao kuambukizwa imani na hatimaye kufanya uamuzi wa kuokoka.
Wokovu hauji kwa kurithishana au kwa ‘niaba-ya’ bali kwa mtu mwenyewe kufanya maamuzi binafsi mara baada ya kushawishwa na injili.
Hata sasa tumeona shuhuda nyingi watu wakiwavuta ndugu zao kwa Kristo, aidha kwa injili au mienendo yao, na hatimaye wote kugeuka.
1 Petro 3:1-2
[1]Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; [2]wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
[1]Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
[2]wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
Hivyo kwa hitimisho, watu wote, haijalishi wakubwa au wadogo, aidha wa waamini au wapagani, wote wanahitaji kumwamini Yesu ndipo waokolewe dhambi zao. Lakini hiyo huja kwa ushawishi wetu, kwa jinsi tunavyosema nao, tunavyoenenda katika mwenendo wetu mzuri, tunapozifanya nyumba zetu kuwa makao ya ibada, ni njia rahisi ya kuwashawishi.
Washirikishena akubariki.
je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?
UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?
Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)
Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.
Ni kitu gani umekichagua kwenye nyumba ya MUNGU katika mwaka huu?..Je nafasi fulani, au cheo, au umaarufu, au nini?.
Kumbuka Nyumba ya MUNGU ni zaidi ya jengo la Ibada, bali pia Miili yetu ni nyumba ya MUNGU.
Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu? 21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.
Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?
21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.
1 Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?”
Soma pia 1Wakorintho 6:19, utazidi kuelewa vyema.
Sasa kama Miili yetu ni HEKALU LA MUNGU, yaani NYUMBA YA MUNGU ni kipi umekiamua juu ya Mwili wako katika mwaka huu mpya?, kwamaana Neno linasema Utakatifu ndio ufaao nyumba ya MUNGU, na tena haufai siku moja tu, bali milele…..
Chagua utakatifu wa mwilini na rohoni huu Mwaka, usiishi tena kwa kuuchafua mwili wako kama ilivyouchafua mwaka jana, au miaka iliyopita, anza mwaka na mambo mapya.
Anza kujenga ushuhuda mpya, badilika kimwonekano, watu watakapokutazama waone waseme hakika yule ni mkristo, na watakapokuuliza usema “UMECHAGUA UTAKATIFU KWA MAANA NDIO UFAAO NYUMBA YA MUNGU”.
Sema mwaka huu sio mwaka wa Kushindana na mtu kimavazi ndani ya nyumba ya MUNGU, sema mwaka huu ni wakati wa kuipamba nyumba ya MUNGU kwa utakatifu.
Sema mwaka huu ni mwaka wa kuhubiri UTAKATIFU kila mahali, kwamaana pasipo huo hakuna mtu atakayemwona Mungu (Waebrania 12:14).
2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.
Hili ni neno fupi la mwaka kwako.
Bwana atusaidie sana..
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
SWALI: Ni kipawa kipi hicho tusichoweza kukisifu jinsi ipasavyo?
2 Wakorintho 9:15
[15]Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.
JIBU: Mungu alitupa mwana wake (Yesu Kristo), kama zawadi kwetu, ambaye anakaa ndani yetu kwa Roho wake Mtakatifu.
Warumi 5:17
[17]Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo.
Yesu (kupitia Roho Mtakatifu), ni kipawa kikubwa ambacho hatuwezi kukielezea uzuri wakev(kukisifu), jinsi ipasavyo.
Ndani ya Yesu ni hakika tunapata vitu vyote (vya rohoni na mwilini)
Hivyo kulingana na vifungu hivyo ukianzia tokea juu katika sura hiyo ya tisa (9), anaegemea hasaa katika eneo la kubarikiwa na Mungu katika baraka za mwilini. ambazo huja ndani ya kipawa hichi cha Mungu.
2 Wakorintho 9:11
[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.
Ni kweli hatuwezi kueleza kwa maneno haya jinsi gani Yesu alivyoleta ukombozi katika maeneo mengi zaidi ya yale tunayoyadhani, si tu katika roho zetu, bali mpaka miili yetu, dunia yetu, uchumi wetu, familia zetu, magonjwa yetu, wanyama wetu, jamii yetu, ardhi zetu, n.k. kipawa hichi kila mahali kinatibu.
Hivyo si rahisi kukisifu kwa jinsi ipasavyo. Ndio maana kwa Yesu tumetia nanga, yeye ndio utoshelevu wetu wote, hatuna haja kwa mtu mwingine yeyote zaidi yake, na ndivyo ilivyo. Hekima ya Mungu iliona hilo ndio maana hakutupa sisi wanadamu kitu kingine zaidi ya Yesu Kristo tu.
Ashukuriwe Mungu kwa zawadi hii. Utukufu heshima na shukrani vimrudie yeye milele na milele. Amina.
Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote
Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)
SWALI: Nini tafsiri ya 2 Wakorintho 9:11-12
JIBU: Katika sura hii mtume Paulo analisisitiza kanisa la Wakorintho, uthamani wa huduma ya utoaji kama njia mojawapo ya utiifu katika kuikiri injili (9:13).
Na hapa anaongezea kuwa Mungu hutoa utajiri katika vitu vyote (si tu vya rohoni tu, bali pia vya mwilini). Na kwamba yeye ndiye huwapa watu mbegu za kupanda na chakula.
Hivyo atutajirishapo lengo lake ni tutumie utajiri huo kwa kutenda mema (9:8), (yaani kuwapa maskini hususani watakatifu), kwasababu ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo(9:9). Na si tutumie katika anasa na ufahari, na ubinafsi.
Ndio hapo anasema “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote”. Na kama tukifanya hivyo, mitume wanasema shukrani zinamfikia Mungu kwa kutii kazi yao hiyo ya kutuhimiza sisi kutoa.
2 Wakorintho 9:11-12
[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. [12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
Hivyo Bwana anatutaka kila atufanikishapo tujue amekusudia tuwasidie wengine walio maskini hususani watakatifu, kwasababu kwa njia hiyo shukrani nyingi humfikia Mungu.
Zaidi vifungu hivi vinasisitiza pia jinsi Mungu anavyoongeza baraka pale tunapotoa sana, akisema atoaye haba hatavuna haba,(9:6). kile tupandacho ndicho tutakachovuna kwake.
Bwana atusaidie tuwe watoaji katika hali zote.
ubarikiwe.
FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.
USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.
Mistari ya biblia kuhusu shukrani.
Swali: Ni kwanini siku/saa ya kuja kwa Bwana YESU anaijua Baba peke yake na mwana haijui?, na ilihali pia YESU ni Mungu?
Jibu: Turejee..
Mathayo 24:36 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.”
Kipindi Bwana YESU yupo duniani, alikuwa hana budi kuwa kama wanadamu wengine, ingawa alikuwa na uungu ndani yake, Hivyo alikuwa anahisi maumivu kama watu wengine,… alikuwa anasikia huzuni kama tu watu wengine, na pia ilimpasa amtafute Mungu kama tu wanadamu wengine wanavyomtafuta, ndio maana alifunga na kukesha milimani kuomba kwa machozi, ili aweze kupokea mafunuo kutoka kwa Baba, kwaajili ya huduma yake na watu wake.
Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.
Hivyo Bwana YESU hakuzaliwa anajua vyote, ilimpasa ajifunze vitu.. alizaliwa hajui kutembea na hivyo ikampasa ajifunze kutembea kama watoto wengine, vile vile alizaliwa hajui kusoma na hivyo ilimpasa ajifunze kusoma na pia ajifunze torati.
Luka 2:46 “na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.”
Luka 2:46 “na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.
46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.”
Hivyo kwa tabia hiyo ya kuendelea kujifunza, ni wazi kuwa si vyote alikuwa anavijua kipindi yupo duniani, ndio maana akasema “ile siku hata yeye haijui”
Lakini alipokufa na kufufuka, mambo yakageuka… ALIJUA YOTE!!, kwani baada ya kufufuka alisema, amepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani.
Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. 17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka. 18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.
Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.
17 Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.
18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.
Sasa hawezi kupewa mamlaka yote mbinguni, halafu asijue saa ya kuja kwake, ni jambo lisilowezekana…
Kiashiria kingine kinachoonesha kuwa Bwana YESU aliijua saa ya kurudi kwake, baada ya kufufuka ni lile neno alilomwambia Petro kumhusu Yohana kwamba “ikiwa anataka akae hata ajapo” soma Yohana 21:22.
Soma pia Ufunuo 3:3, Ufunuo 16:15, Ufunuo 22:12, na Ufunuo 22:20.. Utaona mamlaka ya YESU kuhusiana na kurudi kwake.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana YESU KRISTO sasahivi anajua kila kitu, ikiwemo siku ya kurudi kwake mara ya pili, na mwisho wa dunia (Si wa kawaida kabisa!!)
MCHE MWORORO.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
TUNAPASWA TUWEJE WAKATI WA KUJA KWAKE BWANA YESU?.
Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,
Kwanini Mungu anajifanya kama hajui mambo?
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi
Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.
Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.
Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.
Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:
Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).
Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.
Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.
> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)
> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..
Wafilipi 2:17-18
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote. [18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.
Wafilipi 1:29
[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,
Wafilipi 3:1
[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.
Wafilipi 4:4
[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Sehemu ya Pili:
Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.
Wafilipi 1:27
[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;
Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..
Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)
Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)
Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)
Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)
Wafilipi 4:8
[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)
Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).
Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.
Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.
Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.
Watu wa nyumbani mwa Kaisari ni watu gani? (Wafilipi 4:22).
Epafrodito ni nani kwenye biblia?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai
Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.
WhatsApp
Kama kitabu kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo Mtume kwa Waefeso”. Paulo ndiye aliyeuandika waraka huu.
Aliuandika akiwa kama mfungwa kule Rumi.
Waraka huu una sura sita(6), ambazo tunaweza kuzigawanya katika makundi mama mawili.
1) kundi la kwanza ni Sura ya 1-3,
Sura hizi zinaeleza asili ya Imani yetu iliyo katika Kristo Yesu jinsi ilivyo ya kipekee kwa nguvu na mamlaka, na ubora, na uweza na ukuu, na utajiri, na utukufu usiopimika, kwa akili za kibinadamu.(1:20-23).
2) Lakini kundi la pili ni Sura 4-6
Inaeleza juu ya mwenendo wetu, jinsi unavyopaswa uwe katika imani tuliyoipokea. Kwasababu ni vitu vinavyokwenda sambamba, haviwezi kutenganishwa, katika fundisho la ukristo.
Kwa ufupi; Katika Kundi la kwanza Yafuatayo ni mambo mama ambayo mwandishi ameyazungumzia juu ya mambo tunayoyapata ndani ya mwokozi wetu Yesu Kristo.
Haya ni mambo ya muhimu sana, ambayo tunapaswa tuyafahamu juu ya Kristo tuliyempokea ndani yetu. Kulingana na mwandishi tukiyajua hayo itatufanya tusiwe watoto wachanga, wa kuchukuliwa na kila upepo wa elimu ya uongo, kwa hila za watu, na ujanja, na njia za udanganyifu (4:14).
Lakini katika kundi la pili ambalo ni sura ya 4-6;
Tunaelezwa wajibu wetu kimwenendo, baada ya kumwamini Kristo, jinsi unavyopaswa uwe, kwamba hatupaswi kuenenda kama mataifa waenendavyo, bali kinyume chake tukue mpaka kuufikia utimilifu wake.
Ambayo hiyo huja Kwa njia ya kuhudumiana kwa karama mbalimbali sisi kwa sisi katika kifungo cha umoja, kama kanisa la Kristo. (4:16)
Anaeleza pia yampasa kila mmoja binafsi auvue ule utu wa kale wa dhambi, na kuuvaa mpya mpya wa utakatifu na haki (4:20-24),
kwa kuuvua uongo, pia tusiruhusu hasira zitutawale, tusiwe wezi, vinywa vyetu visitoe maneno mabaya na matusi, tuwe wafadhili sisi kwa sisi, tusimzimishe Roho, upendo wetu udumu, uasherati usitajwe, wala aibu, wala ubishi.
Kwasababu watendao kama haya kulingana na Mungu hawana urithi katika ufalme wa Mungu.
Waefeso 5:5
[5]Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.
Halikadhalika Mwandishi anatoa pia agizo juu ya matendo ya giza kwamba tuyaonapo tuyakemee, vilevile tujiepushe walevi, bali tujazwe Roho wakati wote, kwa kumfanyia Mungu ibada.
Waefeso 5:18-20
[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; [19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; [20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
[19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
[20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Mwandishi anazidi kugusia mienendo yetu mpaka katika ngazi za kifamilia na kikazi.
kwamba wake wanapaswa wawatii waume zao, vilevile waume wawapende wake zao. Watoto wawaheshimu wazazi wao, na wazazi wasiwachokoze watoto wao, Watumwa wawatii bwana zao, na mabwana wasiwatishe watumwa wao.(5:22-6:9)
Anagusia pia eneo la vita vyetu. Kwamba rohoni tupo vitani dhidi ya adui yetu shetani na mapepo yake, yenye kazi ya kuwapofusha watu macho, lakini pia kurusha mishale ya moto kutuangamiza. Hivyo tunapashwa tuvae silaha zote za Mungu, ili tuweze kusimama. (6:10-20). Anaorodhesha silaha hizo. ambazo zinakamilishwa kwa sala na maombi ya daima.
Na mwisho anatoa salamu zake kwa watakatifu, akiwaambia pia habari zake nyingine watakazisikia kwa Tikiko, aliyempeleka kwao.
Kwa ufupisho.
Kitabu hichi kinatupa ufahamu kuhusu ubora wa imani tuliyoipokea lakini pia wajibu wetu baada ya hapo, kwasababu tusipothamini na kulegea adui yetu shetani na majeshi yake yatashambulia imani yetu na hatimaye, tukayakosa tuliyohakikishiwa.
Ukishaamini tembea katika utakatifu. Ukiwa unapiga hatua kila siku kwenda mbali na dhambi, basi fahamu kuwa ukombozi wako ni hakika. Kwasababu msalaba una nguvu ya kukusaidia madhaifu yako.
Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.
Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?
Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.
Jina la Mwokozi Mkuu, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.
Kosa moja maarufu Mfalme Daudi alilolifanya katika maisha yake, (ingawa baadaye alikuja kusamehewa na Bwana), lilikuwa ni kumuua Uria na kumchukua Mke wake aliyeitwa Bathsheba.
Lakini tukifuatilia chanzo cha kosa, tunaona lilianzia katika MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati ambao Wafalme wanatoka kwenda vitani, ila yeye Daudi hakutoka kwenda vitani pamoja na wenzake badala yake akakaa nyumbani, na matokeo yake ni shetani kupata nafasi ya kumjaribu.
2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU. 2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. 3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti? 4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake. 5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.
2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU.
2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.
3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?
4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.
Laiti Mfalme Daudi angalisimama na kwenda vitani pamoja na wenzake, asingeingia kwenye jaribu kubwa kama lile, ambalo liliuharibu mwaka wake wote na kumchafulia heshima yake kwa vizazi vyote.
Yote hayo ni makosa aliyoyafanya MWANZO WA MWAKA, kumbe kuna kitu katika Mwanzo wa Mwaka, vile vile na katika Mwisho wa Mwaka,..Mwanzo wa Mwaka ni wakati wa kuanza mapambano, si wakati wakulala tena, ni wakati wa kukusanya nguvu ya pamoja na kuingia katika mapambano, ni wakati wa kukusanyika katika nyumba ya MUNGU kupambana kiroho na kuangusha ngome, ni wakati wa kuomba sana.
Bwana atusaidie tuwe na mipango mema katika mwanzo wa Mwaka.
NI KWASABABU YA YESU KRISTO.
MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)
Swali: Kwanini pale Edeni pawekwe MITI, isimamie uzima au Mauti na si kiti kingine kama JIWE?.
Jibu: Ijapokuwa zipo sifa nyingi za MITI zinazoipa vigezo vya kuweza kuwakilisha UZIMA au MAUTI…Lakini sifa kuu inayoweza kusimamia nafasi hiyo ni UREFU wa MAISHA.
Mti ndio kiumbe hai pekee kilichoumbwa na MWENYEZI MUNGU kinachoishi muda mrefu kuliko vyote.
Tembo ni kiumbe hai lakini miaka yake ya kuishi ni 80 tu, Kasuku ni miaka 90, kunguru ni miaka 90, kobe ni miaka 200 lakini MITI inafika mpaka miaka 2,000..
Ipo miti yenye miaka zaidi ya elfu chini ya Jua, na bado inaendelea kuzaa matunda yenye ubora ule ule, na zaidi ya yote MITI haisogei ipo palepale, lakini unaishi muda mrefu.
Tofauti na Jiwe, lenyewe Lipo kwa muda mrefu (hata miaka elfu) lakini haliishi (halina uhai), halizai wala haliongezeki liko vile vile siku zote…kama tu mifupa ya mfu iliyopo kaburini kwa mamia ya miaka.
Sasa kwa sifa hiyo ya MTI kuishi muda mrefu, ikiwa bado inaendelea kuzaa matunda yale yale na ikiwa bado ipo eneo lile lile moja..ndio inayoifanya ichukue sifa ya kusimamia UZIMA wa Daima au MAUTI ya daima.
Kwamba tunapotafakari maisha ya MTI (jinsi yalivyo marefu na usivyosogea). Hali kadhalika Mauti ya mtu aliye katika dhambi ni ya DAIMA, na hukumu yake ni ya Daima, vile vile UZIMA wa MTU aliye ndani ya MUNGU ni wa daima na usio badilika.
Sasa huu MTI wa uzima ni nini? Au upo wapi?..
MTI wa uzima ni YESU KRISTO, leo lifahamu hili, Nitakuhakikishia hilo kimaandiko.
Maandiko yanasema Kristo ndiye hekima ya MUNGU.
1 Wakorintho 1:23 “bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi; 24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni KRISTO, nguvu ya Mungu, na HEKIMA YA MUNGU”.
1 Wakorintho 1:23 “bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;
24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni KRISTO, nguvu ya Mungu, na HEKIMA YA MUNGU”.
Umeona hapo?..KRISTO ni HEKIMA ya MUNGU na kama Kristo ni Hekima ya MUNGU, basi yeye ni MTI wa UZIMA kama maandiko yasemavyo katika Mithali 3:18.
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye HEKIMA, Na mtu yule apataye ufahamu…… 18 Yeye ni MTI WA UZIMA kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye HEKIMA, Na mtu yule apataye ufahamu……
18 Yeye ni MTI WA UZIMA kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”
Kumbe YESU KRISTO ni MTI wa UZIMA, na ana heri kila amshikaye!!!… naam si ajabu tuonapo anatajwa kama Mkuu wa Uzima (Matendo 3:15).
Si ajabu tusomapo kuwa hakuna mwingine mwenye Uzima zaidi yake yeye (Yohana 10:10) na yeye lpekee ndiye njia na Uzima (Yohana 14:6).
Si ajabu kusikia kuwa kila anayemkimbilia anapata uzima wa milele (Yohana 3:16, Yohana 6:47).
Kwaufupi hakuna UZIMA nje ya YESU KRISTO, aliyekufa na kufufuka na kupaa mbinguni, yeye ndiye MTI uishio Milele, na kwake yeye kuna Uzima.
Je unao uzima wa milele?…je umeupata huu Mti?..kama bado mkaribishe YESU maishani mwako na akufanye kiumbe kipya na ukabatizwe kwa maji tele na kwa jjina lake YESU.
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.
JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA?
Uzima wa milele ni nini?
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
CHAGUA UPANDE WA UZIMA.