Silwano ni matamshi mengine ya jina la Sila. Kwa kiyunani ni Sila, lakini kwa kilatino ni silwano. Hivyo Silwano ndio Sila yule tunayemsoma kwenye maandiko.
Habari ya Silwano/Sila hasaa tunaipata katika kitabu cha matendo ya mitume, huyu ni mmoja wa manabii wawili walioteuliwa na wazee wa kanisa la Yerusalemu kuambatana na Paulo na Barnaba katika kupeleka waraka wa makubaliano kwa makanisa ya mataifa.(Matendo 15:22).
Tunaona Sila na Yuda walipofika Antiokia, na kumaliza huduma yao, Yuda alirejea Yerusalemu, lakini Sila aliamua kuungana na Paulo katika ziara zake za kupeleka injili kwa mataifa.
> Sila alipigwa na kufungwa pamoja na Paulo kule Filipi (Matendo 16:19-25).
> Sila anatajwa kama mwandishi mwenza wa kitabu cha Wathesalonike pamoja na Paulo(1&2 Wathesalonike 1:1).
“Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na
katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.”
> Sila alihudumu Beroya.
Matendo ya Mitume 17:10
[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.
> Alihudumu pia Makedonia, na Korintho pamoja na Paulo na wakati mwingine Timotheo (Matendo 15-18)
> Silwano anatajwa kama mjumbe wa mtume Petro, kama mwandishi wa ile barua yake ya kwanza,
> Lakini pia anatajwa kama mtu mwaminifu.
1 Petro 5:12
[12]Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo.
Uaminifu aliokuwa nao ambao ulionekana na kutajwa mpaka kwa mitume, ni uaminifu wa kuwa tayari kujitoa maisha yake kwa ajili ya kuitetea injili bila kujali gharama yoyote.
Sila tunamfananisha na Ruthu, ambaye alipoambiwa arejee nyumbani kwake akakataa , akajilazimisha kwenda na Naomi katika hali ya ajane, katika nchi ya ugenini.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Sila alikuwa na uwezo wa kurudi Yerusalemu pamoja na Yuda, kuhudumu kule lakini akakubali kwenda kwenda katika dhiki na Paulo mataifani. Lakini taabu yake haikuwa bure, bali kazi yake inatambulika mpaka leo.
Sila amekuwa kama kiungo wa kanisa la kwanza pamoja na mitume , tangu wazee wa kanisa Yerusalemu, mpaka Petro hadi Paulo anaonekana akihudumu nao tofauti na washirika wengine wa mitume, walikuwa wakiambatana na mtume Fulani maalumu, mfano tukimwona Timotheo hatuoni popote akihudumu pamoja na Petro, lakini Sila alikuwa kiungo kotekote.
Bwana atupe moyo kama wa Sila. Tupelekwapo, tunajitoa kikamilifu kabisa kwa kufanya zaidi ya tunavyoagizwa..
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?
Rudi Nyumbani
About the author