Category Archive maswali na majibu

Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

SWALI: Je udhaifu ni jambo la kulikubali? Kama tunavyoona mtume Paulo akiusifia katika;

2 Wakorintho 12:9-10
[9]Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juuyangu.

[10]Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Paulo Hajisifii udhaifu, kana kwamba ni mzuri wa kuvutia, hapana hakuna udhaifu ulio mzuri umfanyao mtu ajiivunie huo……lakini linapokuja eneo la Mungu, udhaifu humnyenyekesha mtu, na hivyo humfanya mtu huyo kutegemea zaidi nguvu za Mungu, kuliko uweza wake mwenyewe ndicho kilichokuwa kwa Paulo.

Anasema hakuwa mtu mwenye ujuzi wa maneno, au utashi mwingi wa kitume kama wanavyodhaniwa watumishi wa Mungu wote kuwa nao.

2 Wakorintho 10:10

[10]Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

Lakini katika udhaifu huo wa kunena, maelfu ya watu walikuja kwa Kristo, katika udhaifu huo wa kimwili miujiza mikubwa ilifanyika kwa mikono yake. Hivyo akamshukuru Mungu kwa hilo, ili watu wasidhani ni kwa uwezo wake au kipawa chake fulani maalumu aliweza kuyafanikisha hayo.

Ndivyo tunavyojifunza hata kwa Musa, Mungu kumtumia kwa viwango vile haikuwa katika uweza wake wowote, kwasababu alikiri mbele za Mungu yeye sio mnenaji.(Kutoka 4:10), lakini pia Mungu alimshuhudia kuwa ni mpole kuliko watu wote waliokuwa duniani kipindi kile. Tofauti labda na makuhani wengine au manabii waliokuja au kuwepo kabla yake.(Hesabu 12:3)

hata leo, pale tunapojiona ni wadhaifu fulani mbele za Mungu kimaumbile au kiusemi, au kihali, hapo ndipo mahali pazuri pa kutumiwa na yeye. Usifadhaike wala usife moyo ukasema mimi siwezi, amini tu, kwasababu yeye hategemei ulichonacho, bali Neno lake moyoni mwako, ukiliweka yote yawezekana kwako. Amini tu.

1 Wakorintho 1:26-29

[26]Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

[27]bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

[28]tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; [29]mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. 

fuatilia ushuhuda hizi zitakujenga..

USHUHUDA WA RICKY:

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

Lakini hilo halimaanishi kwamba udhaifu wowote ni mzuri, kwamba tujivunie katika hayo, hapana hakuna raha katika ulemavu, au katika ububu, au katika upofu..Lakini tujapo kwa Kristo ni mtaji mzuri wa Mungu kututumia. Hiyo ni kutudhihirishia kuwa kwa Mungu hakuna kiungo hata kimoja ambacho hakiwezi kumtumikia yeye. Sote kwa pamoja tuwe na elimu tusiwe na elimu, tuwe na afya tusiwe na afya, tuwe vijijini tuwe mijini, tunajukumu la kumtumikia Mungu, na kufanya vema kabisa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.


Mafundisho mengine:

MUNGU ALIVICHAGUA VITU AMBAVYO HAVIKO.

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Ipi tofuati ya “Kutakabari” na “kutakabali”?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Swali: Katika Mhubiri 9:16, neno la Mungu linasema kuwa hekima ya maskini haisikilizwi, je na sisi tunapaswa tusizisikilize hekima/mashauri ya watu wasio na kitu, ili kujinusuru..au andiko lina maana gani?


Jibu: Turejee..

Mhubiri 9:16 “Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; WALAKINI HEKIMA YA MASKINI HUDHARAULIWA, WALA MANENO YAKE HAYASIKILIZWI”.

Tukiusoma huo mstari peke yake ni rahisi kuona au kujifunza kuwa “hatupaswi kusikiliza watu maskini” hususani wanapopendekeza mambo.. (na watu maskini ni pamoja na kundi la watu wasio na elimu kabisa).. Lakini hebu tuanzie ule mstari wa 13, tuone kama hiyo ndio maana yake.

Mhubiri 9:13 “Pia nimeona hekima chini ya jua, nayo ni kama hivi, tena kwangu mimi ilionekana kuwa ni neno kubwa.

14 Palikuwa na mji mdogo, na watu ndani yake walikuwa wachache; akaja mfalme mkuu juu yake, akauhusuru, akajenga ngome kubwa ili kuupiga.

15 BASI, KULIONEKANA HUMO MTU MASKINI MWENYE HEKIMA, naye kwa hekima yake akauokoa mji ule lakini hata hivyo hapakuwa na mtu ye yote aliyemkumbuka yule mtu maskini.

16 Ndipo niliposema, BORA HEKIMA KULIKO NGUVU; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi”.

Huyu Maskini alikuwa na Hekima ya kuuokoa mji, ijapokuwa hakuwa na elimu, wala ujuzi mwingi, pengine wala hakuwa katika siasa ya nchi, lakini alitoa wazo bora, na kufanya nchi isiingie katika vita. Lakini baada ya mji kuokoka na kuwa na Amani, hawakumkumbuka yule maskini kwa kumpa thawabu.

Hilo halikumshangaza sana Sulemani, lililomshangaza Zaidi ni kuona  kuwa “KWANINI HEKIMA ZA MASKINI HAZISIKILIZWI”.. na wakati hao wanazo hekima za kuweza hata kuunusuru mji usiangamie!!!, kama mfano wa huyo tuliyemsoma hapo juu.

Hilo likamshangaza sana Sulemani, na ushauri wake ni kwamba tuwatafute hao (maskini) na kujaribu kusikiliza mashauri yao na tusiwadharau kwani baadhi yao wamebeba vitu vikubwa…

Na ndipo akasema Bora kuwa na hekima kama huyu kijana maskini kuliko kuwa na nguvu (za kimwili na kifedha na kielimu) na kukosa hekima.

Mhubiri 9:16 “Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; WALAKINI HEKIMA YA MASKINI HUDHARAULIWA, WALA MANENO YAKE HAYASIKILIZWI”.

Hivyo kwa tafakari hiyo tutakuwa tumeshapata jibu kuwa sio kwamba Biblia inatufundisha kutowasikiliza maskini au kuwadharau…bali kinyume chake inatufundisha “tusiwe na dharau nao, kwani kwa sehemu moja, wapo baadhi wenye hekima hata za kuweza kuokoa Taifa, mfano wa huyo tuliyemsoma hapo juu”.

Hivyo ndugu usimdharau mtu ambaye unaona ni mnyonge kuliko wewe, ambaye unaona pengine hana mali kama ulizonazo wewe, au hana uwezo kama ulionao wewe, au hana elimu kama uliyo nayo wewe… Watu hao unaowadharau wewe baadhi yao wamebeba vitu vikubwa sana kwaajili yako, ambavyo vinaweza kukusaidia wewe au watu wako!.

Hivyo sikiliza watu wote, na chuja mambo yote. Si wote walio maskini ni wajinga, na pia si maskini wote wana hekima… vile vile si wote walio matajiri wanazo akili, wengi hawana akili wala hekima ingawa mbele za watu wanaweza kusifika..

Biblia inasema heri kijana maskini mwenye hekima, kuliko mfalme mzee halafu mpumbavu (Soma Mhubiri 4:13).

Hivyo hatuna budi kuwa watu wanyenyekevu daima na wenye kusikiliza.

Bwana atusidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwa namna gani Bwana YESU atagawiwa sehemu pamoja na wakuu? (Isaya 53:12)

Swali: Katika Isaya 53:13 tunausoma unabii wa Masihi (yaani YESU), Kwamba atakuja kugawiwa sehemu pamoja na wakuu…je! hawa wakuu ni akina nani atakaokuja kugawiwa nao sehemu?…na nini kinagawiwa hapo?


Jibu: Turejee…

Isaya 53:12 “Kwa hiyo nitamgawia sehemu PAMOJA NA WAKUU, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini ALICHUKUA DHAMBI ZA WATU WENGI, Na kuwaombea wakosaji”.

Mstari huo ni kweli unamhusu BWANA YESU (Aliye Masihi) na ni  rahisi kutafsirika hivi “kwamba kuna wakuu wanaoishi ambao Bwana YESU naye atakuja kupewa sehemu pamoja nao”.

Tafakari hii sio sahihi, na wala sio maana ya maandiko hayo…kwani hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kulinganishwa na YESU wakati huu wa sasa na hata baada ya maisha.

Sasa maana halisi ya mstari huo ni ipi?.

Maana ya mstari huo ni hii… “Mungu atamgawia sehemu Bwana YESU na pia atawagawia sehemu WAKUU”…Maana yake Bwana ana sehemu yake na hao wakuu wana sehemu yao..lakini wote watakuwa na sehemu.

Ndio tukiunganisha maneno hayo mawili tunapata sentensi hiyo “ Mungu atamgawia  sehemu pamoja na WAKUU”...

Sasa hiyo sehemu ni ipi na hao wakuu ni akina nani?

“Sehemu” inayozungumziwa hapo ni “Mji wa kimbuinguni, Yerusalemu Mpya” (Soma Ufunuo 22:19).

Na “Wakuu” wanaozungumziwa hapo ni watakatifu watakaoshinda siku ile,  hao ndio wanaoitwa “wakuu”. (Wale watu wote walioishi maisha ya kujinyenyekeza kama watoto walipokuwa duniani) sawasawa na Mathayo 18:2-3.

Mathayo 18:2 “Ni nani basi aliye MKUU katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”

Soma pia Luka 7:28 utaliona jambo hilo hilo.

Kwahiyo sehemu ya BWANA YESU ni KITI CHA ENZI CHA DAIMA… na sehemu ya watakatifu watakaoshinda, ambao wataitwa wakuu ni YERUSALEMU MPYA.

Na wanadamu wengine ambao hawatakuwepo katika hilo kundi la ‘wakuu’, basi hawana sehemu yoyote katika mji mtakatifu, bali biblia inasema sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti.

Ufunuo wa Yohana 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, SEHEMU YAO NI KATIKA LILE ZIWA LIWAKALO MOTO NA KIBERITI. HII NDIYO MAUTI YA PILI”.

Tujitahidi tukapate sehemu pamoja na Bwana WETU.

Tujinyenyekeze kama watoto, tukatae udunia na kumwamini YESU, tuache dhambi na tuichukie, tutafute haki na kusimama imara.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MKUU WA ANGA.

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Mbari ni nini kibiblia?

Mbinguni ni sehemu gani?

Fahamu Namna ya Kuomba.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

SWALI: Je, mstari huu tunaousoma kwenye Mhubiri 10:15 una maana gani?

Mhubiri 10:15

[15]Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.


JIBU: Kwa namna ya kawaida ya kibinadamu tunajua watu wengi hutamani kuishi mijini kuliko mashambani. Kwasababu mijini huduma zote hupatikana, na ni mahali pa raha. Hata kazi, mtu anazozifanya mashambani, wengi wao ni ili matunda yake wakayafurahie mjini, Au wakaziuze bidhaa zao huko wawe matajiri.

lakini tengeneza picha mtu, ambaye anajitaabiisha kufanya kazi kwa lengo la kuzifurahia mjini, halafu hajui njia ya kufika huko, kinyume chake ndio anakwenda mbali zaidi na mji, anaelekea majangwani au mabondeni?  ni wazi kuwa mtu kama huyo  hawezi kuwa na raha katika kazi yake, kwasababu taabu yake haina faida, alikosa malengo au hakuwa na maarifa sahihi.

Ni ufunuo gani upo nyuma yake?

Na sisi pia tuliomwamini Kristo. Tuna mji ambao tunatarajia kuungia, ndio ule Yerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni kwa Baba..

Ufunuo  21:2-3

[2]Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 

 [3]Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 

Anaendelea kusema…

Ufunuo  22:14-15

[14]Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

[15]Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Huo ndio ule mji halisi ambao hata Ibrahimu aliona, ikamfanya aishi maisha kama ya mpitaji hapa duniani.

Waebrania 11:8-10

[8]Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 

 [9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 

 [10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 

Umeona na sisi ili tuweze kuonekana tumestahili kuuingia katika mji huo wa mbinguni hatuna budi tuwe tumeokolewa na YESU KRISTO. Kwasababu yeye ndio NJIA ya kuuingia mji.

Ukiwa nje ya Kristo tafsiri yake wewe ni mpumbavu, kwasababu taabu yako yote ya hapa duniani, haikufikishi popote haikuepeki mjini mwa Mungu, itakuchosha tu, utakuwa na magorofa, utaijaza akaunti fedha, utakuwa ni miradi mikubwa lakini mwisho utakufa, na kwenda kaburini. Lakini ukiiona njia na kuifuata Yerusalemu basi hufanyi kazi ya bure, unapojiwekea hazina kule hufanya kazi ya kushosha, ni uzima baada ya kifo. Utafaidi matunda yake

Je umeokoka?

Ikiwa bado na unatamani kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. (Opens in a new browser tab)

MJI WENYE MISINGI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Naliazimu nisijue neno lolote kwenu?” (1Wakorintho 2:2).

Jibu: Turejee..

1Wakorintho 2:2 “Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa”

Haya ni maneno ya Mtume Paulo aliyowaambia watu wa kanisa la Korintho… sasa tunaweza kuyaweka katika lugha rahisi namna hii…. “Nilipokuja kwenu (ninyi Watu wa Korintho) nilikusudia kufahamu yale mnayoyajua kumhusu YESU KRISTO, ambaye amesulubiwa na si jambo lingine lolote”.

Maana yake Paulo alitaka kuelewa ni nini Wakorintho wanaelewa kumhusu YESU aliyesulubiwa, hicho tu ndicho alicholenga kujua, na hakutaka kujua mambo mengine..

Kwanini alitaka kujua ufahamu wao kuhusu YESU?…

Ni kwasababu alijua kama wakimfahamu YESU kama inavyopaswa kufahamika, basi Imani yao itakuwa katika msingi thabiti.. Lakini kama wakimfahamu Yesu kwa ushawishi wa Maneno, basi Imani yao itakuwa katika hekima za kibinadamu.

1Wakorintho 2:1 “Basi, ndugu zangu, mimi nilipokuja kwenu, sikuja niwahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa maneno, wala kwa hekima.

2  Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa.”

Vile vile kama watamfahamu YESU wa ishara na miujiza tu, basi Imani yao itakuwa katika miujiza  na ishara kama wale Wasamaria (Yohana 6:26) na si katika Imani thabiti ya YESU ALIYESULIBIWA

Lakini kama wakimfahamu YESU kama Mwokozi aliyesulibiwa kwaajili ya makosa yao na dhambi zao, basi Imani yao itakuwa thabiti, na yenye uhakika.. Itakayowapelekea kuungama dhambi, na kutafuta kuyafanya mapenzi ya Mungu, jambo ambalo ni msingi sana, na ambalo ndio tiketi ya kumwona Mungu (Mathayo 7:21-23)

Hivyo na sisi kilicho kikubwa na cha Msingi ni kuishikilia ile Imani ya Msingi (ambayo ndio Imani mama), ambayo inatupeleka/kutusukuma kujitakasa na kujiepusha na uchafu(dhambi).

Bwana atusaidie, na Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU.

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Malaika wanazaliana?

Wapo wanaodhani kuwa malaika wanao uwezo wa kuzaliana sawasawa na habari ya wana wa Mungu na binti za wanadamu inayozungumzwa  katika kitabu cha Mwanzo.

Mwanzo 6:1-3,  Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Kwa habari hiyo wengi hufikiri, hao wana wa Mungu walikuwa ni malaika, ukweli ni kwamba hawakuwa malaika bali wanadamu. Yesu alisema, tutakapofika mbinguni, hatutaoa wala kuolewa, tutafanana na malaika, Kuonyesha kuwa malaika hawazaliani. (Mathayo 22:30)

Vilevile katika habari hiyo hatuoni kwamba malaika wakiadhibiwa, bali wanadamu, kuonyesha kuwa ni jambo la kibinadamu. Kwa urefu wa fundisho hilo, fungua hapa >>> WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Viungo vya uzazi viliumbwa mahususi kwa viumbe wa ulimwenguni, kwa lengo la kuijaza nchi. Lakini vya mbinguni havikuumbwa kwa utaratibu kama huu wa kwetu.

Hivyo kwa hitimishi ni kuwa malaika watakatifu hawazaliani. Kwasababu wao ni viumbe vya rohoni, waishio milele. Hivyo hawahitaji kuzaliana.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Je malaika wote wana wabawa?

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je malaika wote wana wabawa?

Katika maandiko tunaona, Malaika wakionekana kwa mifano ya viumbe mbalimbali vya duniani, ikiwemo wanadamu. Kwamfano wale wenye uhai wanne, wapo waliokuwa na uso kama wa tai, wengine simba, wengine ndama na wengine wanadamu(Ufunuo 4:7). Maserafi na Makerubi walionekana kuwa ni malaika wenye mabawa. (Kutoka 25:20, Isaya 6, Ezekieli 10).

Lakini wapo pia walionekana kwa mfano wa wanadamu kabisa, mfano wa hawa ni wale waliomtembelea Ibrahimu wakala naye, kisha wakaenda Sodoma. (Mwanzo 18 &19)

Kwahiyo si malaika wote waliokuwa na mwonekano wa mabawa. Lakini ni vema kufahamu kuwa mabawa au mionekano si vitu ambavyo vinawafanya watembee au wawe na uwezo ule, wale ni viumbe vya rohoni hivyo hawategemei kanuni za kidunia kutembea, ijapokuwa wataonekana kama wanadamu bado sio wanadamu, hawawezi kuzaliana, wataonekana na mifano ya ndege sio ndege wala akili zao hazipo vile.

Kwahiyo kujua kama malaika wote wana mabawa au hawana, si muhimu. Muhimu ni kufahamu ni kwamba wamewekwa kutuhudumia sisi tutakaourithi wokovu. Hivyo tumtiipo Kristo maana yake ni tunaruhusu huduma yao kutenda kazi katikati yetu, hapa ulimwenguni.

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Lakini kinyume chake ni kweli umtiipo shetani, tafsiri yake ni kuwa unayaruhusu mapepo kufanya kazi hapa duniani.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MALAIKA NI WALIMU WA SIFA KWETU, TUJIFUNZE KWAO!

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

(Opens in a new browser tab)HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

SWALI: Maana ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.


JIBU: Mstari huo una vipengele viwili cha kwanza ni Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake

Na cha pili ni naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

Tukianzana na hicho cha kwanza. Tufahamu kuwa Mungu ameiandika injili yake sio tu kwenye kitabu chake, bali pia kwenye vitu vya asili, ndio maana Yesu alitumia mifano mingi ya namna hiyo, kuzungumza nao habari zake mwenyewe. Kuanzia wakulima, mimea, wanyama, wafanya biashara, wafalme n.k.

Sasa hapa anasema yeye atunzaye mtini atakula matunda yake. Kumbe kula matunda ni “kutunza”. Usipotunza huwezi pata chochote. Ili uone kazi yako, utaiwekea mbolea, utaipalilia, utaipiga dawa n.k. Na mwisho utakuwa mvumilivu aidha miaka mitatu/ minne ukisubiri  mazao.

Halidhalika rohoni. Sisi kama watoto wa Mungu (tuliookolewa), kila mmoja wetu anao “mtini” moyoni mwake, na huo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo. Wengi wasichojua ni kwamba Kristo huanza kama kichanga, kisha huwa kijana mdogo, baadaye huwa mtu mzima, na mwisho huanza kutenda kazi zake. Kama tu alivyokuwa hapa duniani alivyoishi na Mariamu na Yusufu, hakuanza kufanya chochote pindi anazaliwa.

Hivyo usipomlea ipasavyo hutafaidi matunda yake vema. Ndio mfano wa mpanzi ambao Yesu mwenyewe aliutoa, akasema zile mbegu ziliporushwa nyingine zikaishia njiani, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba, na nyingine kwenye udongo mzuri, moja ikazaa thelathini, nyingine sitini, nyingine mia. Akatoa ufafanuzi wake, kwamba zile zilizofanikiwa kuzaa, ni kwamba zilichangiwa na KUVUMILIA (Luka 8:15). Sasa kuvumilia nini? Kuvumilia  hatua zote tatu za mwanzo, yaani dhiki kwa ajili ya Kristo, kujiepusha na anasa, udanganyifu wa mali, na uvivu wa kulitendea kazi Neno.

Ukuaji wa kiroho tafsiri yake ni ‘Kristo kukua ndani yako’. Ukiona upo  ndani ya wokovu kwa miaka mingi, halafu huoni matunda yoyote ya wokovu wako, katika ufalme wa Mungu, tatizo linakuwa hapo, hukuwa na nafasi ya kuutunza mtini wako.

Ukiokoka, ni lazima bidii ya kusoma Neno iwe ndani yako kila siku, usiwe mvivu wa maombi, vilevile epuka maisha ya kidunia, na ubize uliopitiliza, ambao unakufanya hata nafasi ya Mungu wako unakosa. Ukizingatia hayo, baada ya kipindi Fulani utaona Kristo anavyojengeka nafsini mwako , na kukutumia.

Lakini pia sehemu ya pili inasema naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa,. Ni hekima ya kawaida, ukiwa mfanyakazi mwema kwa bwana wako, hawezi kukuchikia kinyume chake atakupa heshima yako, lakini pia na watu wengine wote wa nyumbani kwake watafanya hivyo.

Si zaidi Mungu?

Heshima hasaa kwa Mungu wako, sio kumwambia “Shikamoo” au kuomba kwa sauti ya unyenyekevu, au kuinamisha kichwa uwapo ibadani. Heshima yake hasaa ni pale unapomtumikia, unapotii agizo lake la kuwaeleza wengine habari za injili, na pale naposimama katika nafasi yako kwenye mwili wa Kristo.

Tutafute kuheshimiwa na Bwana kwa kuwashuhudia wengine injili.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTINI, WENYE MAJANI.

Biblia imemaanisha nini kusema Nyoka atakula mavumbi?(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Je ile habari ya mtini kunyauka inajichanganya?(Opens in a new browser tab)

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo.

SWALI: Nini maana ya mstari huu Yohana 12:35

Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

JIBU:  Yesu alipokuwa duniani, alijilinganisha na Nuru ya uimwengu huu (jua), Yohana 11:9-10…Na hivyo mara kwa mara katika mafundisho yake aliwasisitiza wayahudi juu ya jambo hilo, lakini hawakulielewa.

kwa kawaida jua huwa halizimi, lakini pia huwa halitulii mahali pamoja(kwa jinsi ya kawaida). Litachomoza, litazama,.litaendelea hivyo hivyo katika mzunguko wake. Wakati linaangaza upande mmoja, upande mwingine wa dunia ni giza.

Sasa wayahudi walipomwona Kristo, wengine walimpokea, wengine walimpinga, wengine walimwonea wivu, wengine walimwita mchawi.

Lakini wote hawa, Neema bado ilikuwa juu yao. Bado Kristo alikuwa anawakusanya kama vile kuku akusanyaye vifaranga vyake chini ya mbawa zake (Luka 13:34). Yesu hakudhubutu kwenda kuhubiri kwenye mataifa mengine ambayo yalihitaji hata kumfanya mfalme, ijapokuwa walikuwa wanampinga vikali.

Sasa ndio hapa akawaambia..kwambo hili halitaendelea sana…kuna wakati pia nuru hii  mnayoiona sasa itawafikie na wengine..

ndio hapo akawaambia..

“Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako”.

Maana yake ni kuwa anawaambia aminini mapema, kwasababu nguvu hii inayowalilia mioyoni mwenu itaondoka … Mkikataa neema, mkikataa kujazwa Roho,  Kamwe hamtaweza kulishinda giza kwa nguvu zenu.

Na tunaona ni kweli, jambo hilo liliendelea kwa kipindii kifupi, baada ya Kristo kufufuka, na kupaa, injili kidogo kidogo ikaanza kutoka kwa wahayudi.ikaenda kwa watu wa mataifa yaani mimi na wewe..

Tangu ule wakati, wa mitume, mpaka leo hii inakaribia sasa miaka 2000, wayahudi bado hawajafumbuliwa macho, kwasababu wokovu ni neema kuamini. Sio utashi wa mtu.

Sasa leo hii sisi watu wa mataifa tunayo injili, lakini kanuni ya Nuru ni ileile, huzunguka. Na kwetu pia haitadumu milele. Mungu aliahidi ule mwisho unapokaribia kufika (ambao ndio huu) atawarudia tena Israeli kwa kipindi kifupi. na hivyo kwa upande wetu, hakutakuwa na neema tena ya wokovu itakayokuwa imesalia..

Warumi 11:25-26

[25]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

[26]Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa,

Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;

Atamtenga Yakobo na maasia yake.

Hii ni kutufunisha pia Bwana hasemi na wayahudi tu, bali na anasema sisi pia…

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

Je unaenda katika nuru hiyo? Kama bado wasubiri nini. Geuka leo uoshwe dhambi zako upokee uzima wa milele, usipofanya hivyo kamwe huwezi kulishinda giza.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

(Opens in a new browser tab)Mistari ya biblia kuhusu maombi.(Opens in a new browser tab)

AGIZO LA UTUME.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

TUJIHADHARI NA KUKANWA!.

Mathayo 10:33 “Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni”

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Hebu tulitafakari kwa upana kidogo  hili neno “kukanwa”.

Kukanwa ni ile hali ya kukataliwa na mtu unayemjua, unayetembea naye daima, uliyeweka matumaini yako kwake, mnayekubaliana  au uliye na mahusiano naye ya karibu”

Na ipo tofauti ya “kukana na kusaliti”…kwa urefu juu ya tofauti ya maneno haya mawili fungua hapa 》》Tofauti kati ya kukana na kusaliti ni ipi?

Sasa Bwana YESU anasema kuwa tukimkana mbele ya watu naye atatukana mbele ya Baba yake kule mbinguni.

Hebu tengeneza unafika kule, halafu unakanwa na yule ambaye ulikuwa unaona anatembea na wewe kila siku, anakuponya, anakulinda, ukiliita jina lake maajabu yanatokea, pepo zinatoka na miujiza mingi inafanyika.

Halafu huyu huyu ambaye ulipokuwa duniani alikuwa haonyeshi dalili ya kukukataa lakini unafika kule anakukana anasema hakujui!..ni jambo gumu sana kuamini!.

Lakini ndivyo itakavyokuwa siku ile..

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”

Hatuna budi kukaza mwendo daima na kila siku tukihakiki ni lipi limpendezalo Bwana (Waefeso 5:10).

Mtume Paulo ijapokuwa alikuwa na wingi wa mafunuo lakini alisema maneno haya..

1 Wakorintho 9:26 “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Na pia alisema…

Wafilipi 3:12 “Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu.

13 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;

14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MFALME ANAKUJA.

JINA LAKO NI LA NANI?

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

Rudi Nyumbani

Print this post